ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 15, 2019

MAGOLI: YANGA U20 2-1 SIMBA U20 (U20 PREMIER LEAGUE - 14/06/2019)


Timu ya vijana ya Yanga chini ya miaka 20 imewaduwaza vijana wenzao wa Simba kwa kuwachapa mabao 2-1 katika mchezo wa kundi A hatua ya nane bora ya ligi kuu Tanzania Bara kwa vijana inayoendelea kwenye Dimba la Azam Complex Chamazi, jijini Dar es Salaam. Simba ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 27 kupitia kwa Jackson James, lakini Yanga walitumia dakika nne za mwisho kupata pointi tatu muhimu, wakianza kusawazisha dakika ya 90 kupitia kwa Yassin Salah, kabla ya Erick Msagati kupachika goli la ushindi dakika ya 90+4.

MWANZA YAJADILI ONGEZEKO KUBWA LA WAMACHINGA LISILOENDANA NA IDADI YA WATEJA



Serikali imeshauriwa kutunga sera inayotambua wafanyabiashara wadogo al-maarufu MACHINGA ili waweze kutoa mchango wao katika kukuza pato la taifa.

Ushauri huo umetolewa na mhadhiri wa Chuo Cha Elimu ya Biashara - CBE DKT.NASIBU MRAMBA wakati akiwasilisha matokeo ya utafiti kuhusu mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara wadogo (MACHINGA) jijini mwanza.

Utafiti uliofanywa na taasisi ya maendeleo jumuishi (I4ID) pamoja na shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana la KIVULINI umebaini kuwepo kwa ongezeko kubwa la wafanyabiashara wadogo katika jiji la Mwanza lisiloendana na idadi ya wateja.

Mhadhiri wa chuo cha elimu ya biashara (CBE)DKT. NASIBU MRAMBA amewasilisha matokeo ya utafiti huo kwa madiwani pamoja na watendaji wa manispaa ya Ilemela jijini Mwanza. 

Habari njema kwa Watanzania, Sadio Mane kukosa mechi ya ufunguzi dhidi ya Taifa Stars

Mkufunzi wa Senegal Aliou Cisse amethibitisha kuwa nyota wake wa Liverpool Sadio mane amepigwa marufuku ya mechi moja hivyobasi hatoshiriki katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Taifa Stars ya Tanzania nchini Misri.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 atakosa mechi ya kundi C dhidi ya Tanzania tarehe 23 mwezi Juni mjini Cairo baada ya kupewa kadi mbili za njano katika mechi ya kufuzu ya Senegal.

''Kutokuwepo kwake hakutatuathiri kwa njia yoyote'' , kocha Cisse aliambia vyombo vya habari vya Senegal kabla ya kuondoka katika kambi yao ya mazoezi katika eneo la Alicante Uhispania kuelekea Misri.

''Ni kweli kwamba uwepo wake ni muhimu sana kwetu lakini bila yeye tuko dhabiti.Shirikisho la soka CAF limeamua hivyobasi hatuna budi'', Cisse aliongezea.

Mane alipewa kadi ya njano katika mechi ambayo Senegal ilipata ushindi wa 1-0 dhidi ya Equitorial Guinea mnamo tarehe 17 Mwezi Novemba 2018 na pia alipokea kadi nyengine ya njano katika mechi ya ushindi wa 2-0 dhidi Madagascar mnamo tarehe 23 mwezi Machi 2019 ijapokuwa haijathibitishwa katika takwimu za mechi za Caf.

Caf imetakiwa kuthibitisha.

Mchuano huo nchini Misri, unaotarajiwa kuanza tarehe 21 mwezi Juni hadi 19 Julai , utakua wa Mane wa nne wa Afcon na itakuwa mara ya pili kukosa mechi ya ufunguzi ya Senegal.

Alikosa mechi ya ufunguzi ya Simba hao wa Teranga katika fainali za 2015 nchini Equitorial Guinea dhidi ya Ghana kwa kuwa alikuwa anauguza jeraha la kifundo cha mguu alilopata alipokuwa akiichezea klabu yake ya zamani Southampton.

Mane , ambaye alishinda taji la ligi ya mabingwa Ulaya akiichezea Liverpool mwezi huu, alijiunga na Simba wa Teranga katika mazoezi nchini Uhispania siku ya Alhamisi kabla ya yeye na wenzake kuelekea Misri siku ya Ijumaa.

Anatarajiwa kucheza mechi nyengine za Senegal mjini Cairo dhidi ya Algeria tarehe 27 mwezi Juni na Kenya siku nne baadaye.

KOMBORA LAANGUKA KARIBU NA UBALOZI WA MAREKANI.


Kombora limeanguka katika nyumba moja karibu  na ubalozi wa Marekani katika mji wa mkuu wa Baghdad nchini Iraq.

Kwa mujibu wa taarifa iliyoandikwa kutoka kitengo ya Mawasiliano ya Usalama wa Wizara ya Ulinzi ya Iraq, kombora la aina ya Katyusha limeanguka ndani ya nyumba katika eneo la al-Cadiriya katikati mwa Baghdad.

Hata hivyo kombora hilo halikusababisha uharibifu wowote.

Taarifa zaidi kuhusu kombora hilo haijatolewa.

Kwa upande mwingine, kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka chanzo cha usalama, kombora hilo limeangukia nyumba inayoangaliana na Ubalozi wa Marekani mjini Baghdad.

MAKAMPUNI YAUNGANA KUFANYA USAFI UFUKWE WA COCO JIJINI DAR

Baadhi ya wafanyakazi kutoka makampuni mbalimbali ya jijini Dar es Salaam wakishangilia kwa kutiana hamasa mara baada ya kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa usafi Baharini na kuunga mkono Kampeni ya Serikali ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyofanyika leo Coco Beach jijini Dar esSalaam. Makampuni yaliyojitokeza kufanya usafini Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Verge of Africa na Nipe Fagio.
Baadhi ya wafanyakazi kutoka makampuni mbalimbali ya jijini Dar es Salaam wakifanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa usafi Baharini na kuunga mkono Kampeni ya Serikali ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyofanyika leo Coco Beach jijini Dar esSalaam. Makampuni yaliyojitokeza kufanya usafini Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Verge of Africa na Nipe Fagio. 

Baadhi ya wafanyakazi kutoka makampuni mbalimbali ya jijini Dar es Salaam wakiwa na mifuko ya uchafu mara baada ya kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa usafi Baharini na kuunga mkono Kampeni ya Serikali ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyofanyika leo Coco Beach jijini Dar esSalaam. Makampuni yaliyo jitokeza kufanya usafini Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Verge of Africa na Nipe Fagio.

Baadhi ya wafanyakazi kutoka makampuni mbalimbali ya jijini Dar es Salaam wakiwa na mifuko ya uchafu mara baada ya kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa usafi Baharini na kuunga mkono Kampeni ya Serikali ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyofanyika leo Coco Beach jijini Dar esSalaam. Makampuni yaliyo jitokeza kufanya usafini Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Verge of Africa na Nipe Fagio.
Baadhi ya wafanyakazi kutoka makampuni mbalimbali ya jijini Dar es Salaam wakiwa na mifuko ya uchafu mara baada ya kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa usafi Baharini na kuunga mkono Kampeni ya Serikali ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyofanyika leo Coco Beach jijini Dar esSalaam. Makampuni yaliyo jitokeza kufanya usafini Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Verge of Africa na Nipe Fagio.

Friday, June 14, 2019

HIVI NDIVYO EDEN HAZARD ALIVYOTAMBULISHWA KUWA MCHEZAJI RASMI REAL MADRID C.F.


LIVE: Eden Hazard's Real Madrid C.F. presentation! New Real Madrid Player at Estadio Santiago Eden Hazard's Real Madrid Eden Hazard

POLISI TANZANIA ZANZIBAR YABANWA MBAVU NA WABABE KUTOKA ARUSHA


Jembe Mirjam Volleyball Championship 2019 imekamilika katika siku yake ya pili Alhamisi ya tarehe 13 Juni 2019 katika viwanja vya Mirongo jijini Mwanza.

Mchezo ukikamilika Pentagon kutok mkoani Arusha wakifanikiwa kuibuka washindi baada ya kuongoza Set 3 na Polisi Tanzania Zanzibar wakitoka na Set 1

Mgeni rasmi wa mchezo huo wa pili alikuwa Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege ambaye pamoja na kueleza kwa nini aliamua kujitosa kudhamini mashindano hayo pia ametumia mwana huo kueleza wazi mipango ya baadaye kwa Jembe Fm kuingia katika masafa ya redio mikoani mbalimbali hapa nchini.





Thursday, June 13, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA WABUNIFU WADOGO WA MITAMBO YA KUFUA UMEME IKULU DSM


Mhe. Rais Magufuli anakutana na Wabunifu wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kutumia maji ya mito. Ikulu Jijini Dar es salaam. Tukio hili linarushwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya Redio, Televisheni, Mitandao na Youtube channel ya Ikulumawasiliano.

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII AAHIDI MAKUBWA MICHUANO YA VOLLEYBALL MWANZA


NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Constatine Kanyasu ameahidi makubwa katika Jembe Mirjam East Africa Volleyball Championship 2019.

Hii ni Michuano ya Volleyball iliyoanza kwa kasi na kishindo ikihudhuriwa na mashabiki wengi kiasi cha kusisimua Jumatano hii ya Tarehe 12/Juni katika viwanja vya Mirongo wilayani Nyamagana jijini Mwanza na kutarajiwa kudumu hadi tarehe 16 ya Mwezi huu Juni 2019 ambapo mshindi atajulikana na kuchomoka na zawadi ya mtakato..

Tuesday, June 11, 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TOKA JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

JESHI LA POLISI (M) MWANZA 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
11.06.2019.
Tukio la Kwanza
JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAMSHIKILIA KIJANA MMOJA AITWAYE MICHAEL MAYALA, MIAKA  16, MKAZI WA KISHINDA KWA TUHUMA ZA  KUMBAKA BERTHA JOSEPH, MIAKA 13, MWANAFUNZI WA DARASA LA NNE HUKU AKIWA AMEMZIBA MDOMO NA PUA KWA KANGA HADI KUPELEKEA  KUPOTEZA MAISHA, KITENDO AMBACHO NI KINYUME NA SHERIA
TUKIO HILO LIMETOKEA TAREHE 05.06.2016 HUKO KATIKA KIJIJI CHA KISHINDA, WILAYA YA SENGEREMA, HII NI BAADA YA MTUHUMIWA HUYO AKIWA NA BINAMU YAKE (MAREHEMU) NA  NDUGU ZAO WENGINE WAWILI WANAOISHI WOTE HAPO KIJIJINI KWA BIBI YAO WALIKWENDA SHAMBANI KUPALILIA MATUTA AMBAPO KILA MMOJA ALITAKIWA KUPALILIA MATUTA MATANO(5).
AIDHA, WENZAO WAWILI WALIMALIZA NA KUTANGULIA NYUMBANI WAKABAKI MTUHUMIWA NA MAREHEMU WAKIMALIZIA KAZI NDIPO MTUHUMIWA ALIMKAMATA MAREHEMU NA KUMZIBA MDOMO NA PUA KWA KUTUMIA KANGA ALIYOKUWA AMEVAA MAREHEMU KISHA KUMBAKA NA KUPELEKEA MAREHEMU KUPOTEZA MAISHA PAPO HAPO.
BAADA YA TUKIO HILO MTUHUMIWA ALIRUDI NYUMBANI NA ALIPOULIZWA NA WAZAZI KUWA MWENZAKE YUKO WAPI ALIJIBU KATANGULIA KURUDI NYUMBANI, NDUGU WALIANZA KUMTAFUTA MAREHEMU BILA MAFANIKIO NDIPO MTUHUMIWA ALITOROKA NYUMBANI KWENDA KIJIJI CHA KATUNGURU KWA NDUGU ZAO WENGINE, FAMILIA ILIMTILIA MASHAKA NA BADAE WALIMKAMATA NA KUMPELEKA POLISI ALIPOHOJIWA ALIKUBALI KUHUSIKA NA TUKIO HILO NA KUWAPELEKA POLISI HADI SHAMBANI ENEO MWILI WA MAREHEMU ULIPOKUWA.
JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAENDELEA NA MAHOJIANO NA MTUHUMIWA PINDI UCHUNGUZI UKIKAMILIKA ATAFIKISHWA MAHAMANI. MWILI WA MAREHEMU TAYARI UMEFANYIWA UCHUNGUZI NA KUKABIDHIWA KWA NDUGU KWA AJILI YA MAZISHI.
Tukio la Pili;
JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAMSHIKILIA  JOHN SAMWELI, MIAKA 18, MKURYA, MKAZI WA IBANDA, KWA TUHUMA ZA KUMLAWITI MTOTO WA KIUME  JINA TUNALIHIFADHI, MWENYE UMRI WA MIAKA MIWILI NA NUSU NA KUMSABABISHIA MAUMIVU MAKALI SEHEMU ZA SIRI, KITENDO AMBACHO NI KOSA LA JINAI.
TUKIO HILO LIMETOKEA TAREHE 10.06.2019 MAJIRA YA SAA 13:00HRS HUKO MAENEO YA IBANDA KATA YA KIRUMBA WILAYA YA ILEMELA, HII NI BAADA YA MTUHUMIWA KUMCHUKUA MTOTO NA KUMRUBUNI KUWA ANAKWENDA KUMNUNULIA SODA NDIPO WALIPOFIKA VICHAKANI ALIBADILIKA NA KUMTENDEA KITENDO HICHO CHA KIKATILI.
HATA HIVYO, WAKATI MTUHUMIWA ANAENDELEA KUTENDA UNYAMA HUO. MTOTO ALIKUA AKIPIGA KELELE AKIOMBA MSAADA, WATU WALISIKIA NA KWENDA KUMSAIDIA NDIPO WALIMKUTA MTUHUMIWA AKIWA ANAMLAWITI MTOTO. WANANCHI WALITOA TAARIFA POLISI NDIPO ASKARI WALIFIKA KWA HARAKA ENEO LA TUKIO NA KUFANIKIWA KUMKAMATA MTUHUMIWA.
JESHI LA POLISI LINAENDELEA NA MAHOJIANO NA MTUHUMIWA PINDI UCHUNGUZI UKIKAMILIKA ATAFIKISHWA MAHAKAMANI. MTOTO AMEPELEKWA HOSPITALI YA MKOA SEKOU TOURE KUPATIWA MATIBABU NA HALI YAKE INAENDELEA VIZURI.
JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINATOA ONYO KWA BAADHI YA VIJANA WENYE TABIA CHAFU NA YA KIKATILI YA KUBAKA/KULAWITI KUWA WAACHE KWANI NI KINYUME NA SHERIA NA ENDAPO MTU/WATU WATABAINIKA HATUA KALI ZA KISHERIA ZITACHUKULIWA DHIDI YAO.

IMETOLEWA NA;
MULIRO J MULIRO-ACP
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA
11 JUNE, 2019.

CECAFA yYAWAJIBU SIMBA NA YANGA BAADA YA KUSUSIA KAGAME CUP.

Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesema mashindano ya Kagame Cup 2019 yataendelea licha ya kutokuwapo Simba na Yanga. Amesema Yanga ni timu isiyo na msaada, ndio sababu hufungwa 5-0 au 6-0 kwenye mashindano ya kimataifa. Mashindano hayo ya timu 16 yatafanyika Julai 17-21.

Utakumbuka hapo jana Klabu ya Yanga imesema haitoshiriki michuano ya Kagame Cup yatakayofanyika mwezi Julai 2019, jijini Kigali, Rwanda kwa sababu, wachezaji wengi wamemaliza mikataba, wengine wapo na timu ya taifa, na waliobaki wapo mapumziko.
Nicholas Musonye

Wakati hayo yakijiri, tayari Simba SC ilishatangaza kuwa haitoshiriki mashindano hayo, uamuzi huo umetokana na ratiba ya mashindano hayo kuingiliana na ratiba ya maandalizi ya msimu ujao wa Ligi ya Bingwa AFRIA (CAFCL) na Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) 2019/2020.

MICHUANO MIKUBWA YA VOLLEYBALL KUANZA KUSHIKA KASI JUMATANO HII MWANZA


Jumatano ya Tarehe 12 mwezi juni 2019 ni uzinduzi wa Michuano mikubwa ya Volleyball kwa timu mbalimbali ambazo tayari zimetua jijini Mwanza.

Michuano kufanyika wapi?
Itashirikisha timu gani?
Nani mgeni rasmi kwa michuano hiyo?

Mwanafunzi amuua mwenzake kwa kumpiga jiwe kichwani


Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Rashid Said (17) amefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa jiwe lililompata kichwani eneo la kisogoni na mwenzake ambae ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu huko Kibaha mkoani Pwani.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema kuwa tayari jeshi la Polisi linamshikilia mwanafunzi huyo ili kuendelea na taratibu za kisheria.

Alieleza kuwa Juni 7 mwaka huu maeneo ya Pichandege marehemu alijeruhiwa kwa kupigwa jiwe baada ya tukio hilo alipelekwa katika hospital ya rufaa ya Tumbi kwa matibabu ambapo siku iliyofuata alifariki dunia.

Mwili wa marehemu umepelekwa hospital ya taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi. Jeshi la polisi Pwani limetoa wito kwa jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi ili kujiepusha na matatizo ama kujikuta wakichukuliwa hatua za kisheria.

Monday, June 10, 2019

JEH CHELSEA IMEHARIBIWA MIPANGO? EDEN HAZARD KUELEKEA REAL MADRID


ESPN FC’s Gab Marcotti takes on Steve Nicol, Janusz Michallik and Dan Thomas in a lively debate about Chelsea’s outlook in the Premier League next season after the departure of Eden Hazard to Real Madrid. The panel examine how that move, along with manager Maurizio Sarri’s possible departure for Juventus and a looming transfer ban, will impact the Blues in 2019-20. Marcotti says Chelsea will be fine, because they’ve been preparing for Hazard’s departure and the possible transfer ban, but the rest of the panel is not having it, leading to some shouting between Marcotti and Nicol.

HAFLA YA UAPISHO NA KUPOKEA MRABAHA KUTOKA AIRTEL IKULU DSM



Ikulu, Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 10 Juni, 2019 awaapisha viongozi wafuatao aliowateua hivi karibuni - 1.Mhe. Innocent Lugha Bashungwa(Mb) kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara 2.Bw. Charles Edward Kichere kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe 3.Bw. Edwin Mhede Kuwa Kamishna mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Aidha Mhe. Rais Dkt. Magufuli anashuhudia kuanza kupokelewa kwa Fidia za kila mwezi kutoka katika Kampuni ya Bharti Airtel na kupokea Mchango Binafsi wa Mwenyekiti wa Bharti Airtel Bw. Sunil Mittal kwaajili ya Ujenzi wa Hospital ya Uhuru Ihumwa Jijini Dodoma

THE DESK AND CHAIR FOUNDATION YAKABIDHI MIUNDOMBINU YA INTENETI KWA MPC

Mwenyekiti wa Taasisi ya "The Desk & Chair Foundation", Sibtain Meghji (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza, Edwin Soko (kushoto) kifaa cha kusambaza mawasiliano ya mtandao wa Intaneti (Router) pamoja na nyaya za umeme (Cable) ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za chama hicho katika kutimiza vyema majukumu yake ya kihabari katika jamii.

CHANZO/BMG Habari
Taasisi ya “The Desk & Chair Foundaton” ya jijini Mwanza imeunga mkono juhudi za Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa Mwanza (Mwanza Press Club-MPC) kwa kukabidhi miundombinu ya Intaneti.

Mwenyekiti  wa taasisi hiyo, Sibtain Meghjee amemkabidhi Mwenyekiti wa MPC, Edwin Soko vifaa hivyo na kuahidi kuendelea kushirikiana bega kwa bega na klabu hiyo katika kuchochea maendeleo ya Mkoa Mwanza.

Baada ya kupokea vifaa hivyo, Soko amesema uwepo wa miundombinu ya Intaneti ya uhakika kwa waandishi wa habari ni nyezo muhimu katika kutekeleza majukumu yao huku akiishukuru taasisi ya “The Desk & Chair Foundation” kwa mchango wake katika kuimarisha shughuli za waandishi wa habari.

Katika hatua nyingine, Edwin Soko ameongeza kuwa MPC itaendelea kufanya kazi na taasisi ya The Desk & chair pamoja na wadau mbalimbali wa Mkoa Mwanza pamoja na Serikali ya awamu ya tano na kuchochea maendeleo ya Mkoa wa Mwanza.

“Uwezo wa miundombinu utasaidia waandishi wa habari kutuma habari zao na kupokea taarifa muhimu na pia kuhudhuria mikutano kwa njia ya mtandao” amesisitiza Soko.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni kipanga njia cha Intaneti kimoja (Router), waya za kuunganishia kifaa hicho, waya za umeme pamoja na vifushi vya intanenti ambapo hatua hii imekuja baada ya MPC kupata uongozi mpya Juni 01, 2019 ambao umeanza kujenga mahusiano mema na wadau wa habari ili kujenga mahusiano mazuri.
Kifaa hicho (Router) kutoka kampuni ya mawasiliano Tanzania (TTCL) kina uwezo wa kuunganisha kompyuta 30 kwa wakati mmoja hivyo kitasaidia wanachama wa MPC kupata huduma ya intaneti kwa uhakika huku pia wasio wanachama wakichangia gharama kidogo za uendeshaji.

TAKUKURU YAWABURUZA MAHAKAMANI WATUHUMIWA SAKATA LA MFANYABIASHARA ALIYEKWAMISHWA MIAKA MI 3


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)leo kuwafikisha mahakamani watuhumiwa watatu waliohusika na uzuiaji wa mzigo wa mfanyabiashara ambaye sakata lake liliibuliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wa kikao cha ya Rais na wafanyabiashara.


POLEPOLE AWAFUNDA MAKATIBU WA ITIKADI NA UENEZI MKOA WA IRINGA


Katibu wa itikadi,siasa na uenezi wa CCM taifa Ndugu Humfrey Polepole akitoa semina kwa makatibu wa idara ya Itikadi na uenezi wa mkoa wa Iringa iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo
Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi Taifa (MNEC) Salim Asas akiwahutubia makatibu wa idara ya Itikadi na uenezi wa mkoa wa Iringa walikuwa wakipewa semina na Katibu wa itikadi,siasa na uenezi wa CCM taifa Ndugu Humfrey Polepole juu ya Idara hiyo,semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo
 Baadhi ya makatibu wa Idara ya Itikadi,siasa na uenezi mkoa wa Iringa wakiwa makini kumsikiza Katibu wa itikadi,siasa na uenezi wa CCM taifa Ndugu Humfrey Polepole alipokuwa anawafunda.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.


Katibu wa itikadi,siasa na uenezi wa CCM taifa Ndugu Humfrey Polepole Amewataka viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia chama hicho kutokuwa chanzo cha migogoro na majungu bali wawe suluhisho kwa kuwa lengo la chama ni kusimamia serikali na kuwaletea watanzania Maendeleo.



ameyasema hayo kwenye semina ya kuwafunda katibu wa Idtikadi na uenzi wa ngazi zote mkoani Iringa, Polepole amesema kuwa kuna baadhi ya viongozi wamekuwa chanzo cha migogoro hata kufanya kurudisha nyuma maendeleo ya chama.



Amesema kuwa chama hicho kimejengwa kwenye misingi bora kwa lengo la kutumikia wananchi na kusikiliza watu pamoja na kujua shida zao lakini kuna baadhi yao wanaleta majungu wao kwa wao jambo linalofanya kutowavumilia.



“Sasa hivi hii ni ccm mpya chini ya mwenyekiti Dr John Pombe Magufuli na hana utani anataka kazi tu na wale ambao wanaona wameshindwa watupishe maana unapoacha sumu ndani si ya siku itakudhuru tunapogombana wanaoumia ni watanzania waliotupa dhamana ya kusimamia serikali”Alisema Polepole



Polepole ameongeza kuwa kwasasa mlango uko wazi endapo mtu anaona atashindwa kupelekana na kasi ya CCM mpya chini ya mwenyekiti wao John Pombe Magufuli ni vyema akapisha na kuacha wanaojua kufanya kazi.

 

Hata hivyo Polepole amewataka viongozi kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa huku akimtaka katibu wa itikadi na uenezi mkoa wa Iringa Ramadhani Baraza kuunganishi vizuri na kuendelea kuwatumikia wananchi vizuri kwa kueleza mambo mazuri yanayofanywa na serikalia ya CCM.



Vile vile Polepole amewasifu viongozi katika ngazi zote kwasababu wameibadilisha ccm na wananchi wameelewa dhamira ya Chama katika kuisimamia serikali.



Aidha Polepole alisema kuwa chama cha mapinduzi kikifanya vibaya kwa wananchi ujue kuwa idara ya Itikadi na uenezi haijafanya kazi yake ipasavyo,hivyo ni lazima kila kiongozi awajibike ipasavyo ili kutimiza malengo ya chama.



“Tunatakiwa kushughulikia matatizo ya wananchi kwa kuwapa mafunzo mbalimbali viongozi wa ngazi za chini ili kueneza vilivyo cha hicho ambacho kipo madarakani muda mrefu sasa” alisema Polepole



Polepole aliwaambia viongozi hao kuwa uongozi ni kujitolea na sio kutegemea kupata maslai furani kwenye chama wakati unagombea nafasi mbalimbali lazima uwe unasehemu ya kuingiza kipato kingine na usitegemee kuvuna kutoka kwenye chama.



Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi Taifa (MNEC) Salim Asas alimtaka katibu wa itikadi na uenezi mkoa wa Iringa Ramadhani Baraza kuratibu namna nyingine tena ya kuwawezesha makatibu hao kuanzia ngazi ya chini hadi juu kupata fedha za kufanyia kazi mafunzo walipata kutoka kwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM taifa Ndugu Humfrey Polepole.



“Ramadhani Baraza nakuomba uratibu zoezi hilo ili tuone jinsi ya kuwasaidia makatibu hao ili waweze kukieneza vilivyo cha chetu kwa wananchi wote huko waliko” alisema Asas



Naye katibu wa itikadi na uenezi mkoa wa Iringa Ramadhani Baraza alisema ameyapokea maagizo yote na atayafanyia kazi ili idara hiyo mkoa wa Iringa iwe mfano kwa mikoa mingine hapa nchini.

TBL YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI 2019 KWA VITENDO


Baadhi ya kiwanda cha Konyagi kilichopo chini ya TBL Group wakiwa na mabango yenye ujumbe wa utunzaji wa mazingira baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti na kusafisha mazingira
Wafanyakazi wa TBL kiwanda cha Arusha wakishiriki kupanda miti katika eneo la Themi, Arusha Baadhi ya wafanyakazi wa TBL kiwanda cha Arusha wakiwa na bango lenye ujumbe wa utunzaji wa mazingira baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti zaidi ya 1,000 katika eneo la chanzo cha maji kilichopo Mtaa wa Kambarage,Kata ya Themi katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2019.

Sunday, June 9, 2019

'IMETOSHA' ASEMA MONGELLA - ATOA SIKU 10 KWA KITUO CHA AFYA BWISYA KUKAMILIKA


Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ameagiza ujenzi na upanuzi wa Kituo cha Afya Bwisya kilichopo katika Kisiwa kidogo cha Ukara wilayani Ukereni kukamilika ifikapo Juni 17, 2019.