ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 23, 2016

LIGI KUU UINGEREZA LIVERPOOL PASU KWA PASU NA NEWCASTLE, MANCHESTER CITY YAPAA HADI NAFASI YA TATU.


Manchester City imepanda hadi nafasi ya tatu katika jedwali la ligi ya Uingereza baada ya kuicharaza Stoke City 4-0 huku ikitarajiwa kumenyana ana Real Madrid katika kombe la vilabu bingwa Ulaya siku ya Jumanne.









Fernando alifunga kwa kichwa na kuwaweka City kifua mbele kabla ya Sergio Aguerro kufunga kwa njia ya Penalti.
Baadaye Kelechi Ihienacho aliyetangazwa mchezaji bora katika mechi hiyo alifunga mabao mawili.
Eden Hazard alifunga bao lake la kwanza na kuisadia timu yake kuishinda Bournemouth.
Cesc Fabregas alisaidia katika mabao matatu ya Chelsea akitoa pasi nzuri kwa wafungaji Pedro,Hazard na baadaye Willian.
Vilevile Newcastle iliimarisha matumaini yao ya kusalia katika ligi ya Uingereza baada ya kutoka sare ya 2-2 na wenyeji Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Daniel Sturridge na Adam Lalana waliiweka mbele Liverpool kabla ya Newcastle kukomboa kupitia Papis Cisse na Colback .

Liverpool vs Newcastle 2 2 All Goals & Highlights Premier League 23/4/2016

MENEJA WA DIAMOND ATAJA ANAPOKOSEA ALI KIBA, ADAI AKITAKA AMSIMAMIE YUPO TAYARI

Meneja wa Diamond, Sallam Sharaff yupo tayari kumsimamia Alikiba iwapo akitaka iwe hivyo.


Akiongea kwenye mahojiano na gazeti la Champion, Sallam alisema: Sina tatizo kabisa, akitaka tufanye kazi nitamweleza mahitaji yangu akikubali tutafanya kazi. Nilishawahi kukutana na Kiba, Nairobi, alinifuata akaomba tupige picha, sikuwa na kinyongo, tukapiga ikawa safi japokuwa ile picha aliitumia kunitukanisha baadaye.

Akifafanua kuhusu hilo, Sallam alisema: Hakuiweka yeye katika mtandao, aliitoa kwa mashabiki wake ambao wakasema nimeenda Nairobi kumfuata Ne-Yo halafu nikafukuzwa, wakasema mimi ndiyo niliomba kupiga picha na Kiba, ikawa gumzo sehemu nyingi. Ukweli nilikuwa na Ne-Yo na Diamond ambaye alikwenda pale kurekodi, yeye Kiba alikuwa Coke Studio.

Anasema Kiba alimuomba radhi na kudai kuwa aliwatumia wapost lakini wakaweka maneno yao.

Kuhusu anavyomchukulia Kiba kimuziki, Sallam alisema:

Siwezi kusema anakosea wapi, maana kila msanii ana njia zake. Wimbo wake wa Mwana ni mkali na ulifanya vizuri yawezekana anakosea kwenye ‘market’. Kuna vitu lazima ulazimishe, hata Diamond yupo juu lakini hawezi kutoa kitu halafu akatulia tu akaacha watu wapende wenyewe. Kila mtu ana staili yake yawezekana yeye hataki kwenda kwenye staili kama hiyo, ndiyo maana kuna muda huwa nasema huwezi kumfananisha Diamond na Ali kwa sababu wanaimba muziki wa tofauti. Wote ni Bongo Fleva lakini staili zao ni tofauti, kwa mtu anayefuatilia muziki anaweza kugundua hilo.

Kuhusu bifu ya Diamond na Kiba, Sallam alisema:

Hakuna bifu kabisa, mimi nafahamu hilo. Wameshakutana na kusalimiana na hakuna chochote. Nasema kabisa wanapiga stori na wanaongea ‘fresh’ kabisa. Kinachotokea ni kwamba watu wanawauliza kama wana bifu kwa hiyo wenyewe wanasema hawana bifu basi, lakini kwa kuwa hakuna maelezo mengi watu wanachukulia hivyo.

Kuhusu madai kuwa uongozi wa Diamond unafanya fitna ya kuzuia video za Kiba zisipigwe katika vituo vikubwa vya nje kama MTV na Trace, Sallam alisema:

Siyo kweli. Kiba na ana nguvu kubwa MTV na Trace kuliko Diamond kwa ajili ya Seven (ni mmoja wa wasimamizi wa Ali Kiba). Seven alikuwa mfanyakazi wa MTV, anawajua watu wote wa MTV, hata yule bosi wa Trace wa sasa alikuwa chini ya Seven, ndiyo maana hata video yake ya Chekecha Cheketua ilichezwa wiki nzima mfululizo ikiwa ni ‘Exclusive’.

Wenzetu katika vituo wanaangalia vigezo vyao. Nikupe siri kuwa wakati naanza kazi na Diamond, alikuwa anabaniwa kweli zisipigwe kabisa hata Channel O.

Aliendelea: Siwezi kutaja jina lakini nyimbo zilikuwa zinapelekwa DStv hapo lakini anaambiwa hazina viwango, zinarudi. Aliyekuwa anafanya hivi ni Mtanzania na ni mhusika mkubwa wa muziki wa Tanzania. Nilimfuata nikamchana ‘live’ baadaye tukaamua kazi zetu kuzipitishia Nigeria kisha tukarudi hapa na kila kitu kikawa rahisi. Niwashauri watu kuwa wafanye kazi na watangaze kazi zao dunia ya sasa hakuna kitu kinachoenda chenyewe tu.

sss

SERIKALI YAKIRI KUDAIWA TSH 67.3 BILIONI NA WALIMU.

Serikali imesema bado inadaiwa na walimu deni linalofikia Sh67.3 bilioni, ikiwamo mishahara.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Seleman Jaffo alitoa kauli hiyo mjini Dodoma jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Aida Khenani bungeni.

Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kujua Serikali imechukua hatua gani kumaliza madai ya walimu ya muda mrefu nchini.

Pia, alihoji kuhusu madai ya walimu waliosahihisha mitihani ya kidato cha nne mwaka jana ambao hawajalipwa hadi sasa.

Naibu Waziri huyo alisema Serikali imeendelea kulipa madeni ya walimu kupitia mamlaka zake kila yanapojitokeza.

“Mfano, Oktoba 2015, Serikali ililipa Sh20.1 bilioni na Februari mwaka huu imelipa Sh1.17 bilioni za madeni ya walimu nchi nzima,” alisema Jaffo.

Alitoa mchanganuo kuwa kati ya kiasi kinachodaiwa, alisema Sh17.5 bilioni ni madeni yasiyo ya mishahara wakati madeni ya mishahara yanafikia Sh49.8 bilioni ambayo kwa pamoja yanafanyiwa uhakiki.

Kuhusu malipo ya walimu waliofanya kazi ya kusahihisha mitihani alisema baadhi ya mikoa haijapeleka madai yao hadi sasa licha ya kuwa mwisho wa kupelekwa ilikuwa ni Aprili 15.

Alisema mikoa tisa tu ndiyo ilipeleka na kuitaja kuwa ni Mbeya, Mara, Tanga, Arusha, Kigoma, Lindi, Mtwara, Kilimanjaro na Iringa.

Alisema madeni hayo ya mikoa hiyo yanahakikiwa ili walimu walipwe.

MAGAZETI YA LEO> MOTO WA MAGUFULI WABABUA BUNGENI. MVUA YA KIMBUNGA KIKALI KUANZA KESHO. HATIMAYE MAHAKAMAYA MAFISADI KUANZA JULAI.


 Moto wa Magufuli wababua bungeni, Mvua ya kimbunga kikali kuanza kesho, Hatimaye mahakama ya mafisadi kuanza Julai.  

 Samia ataka juhudi udhibiti wa silaha haramu, Kitwanga haponyoki Infosys, sababu 3 za UKAWA kugomea bajeti ya JPM.   

NEC ifanya tathmini ya uchaguzi asema Majaliwa, Vigogo bima ya afya watumbuliwa, Serikali ya JPM yakaliwa Kooni. 

Friday, April 22, 2016

I LOVE MWANZA KARIBU JIWE KUU SAFARI KUELEKEA JEMBEKA FESTIVAL 2016

Njia kuelekea Jiwe Kuu inachangamoto zake ni barabara inayopitika kimtindo.
Taswira kuelekea Jiwe Kuu Kitangiri Mwanza.
Rock City.
Kutoka moja ya vilele vya Jiwe kuu utakuwa na fursa ya kuona maadhari ya Malaika Beach Resort Mwanza.
Team Yangu ya Utalii ikiwa na wadau Bodi ya Utalii Tanzania..
Moja kati ya mawe ya heshima.
Mabango.
Team #iLoveMwanza #JembekaFestival2016 #Jembeka NaVodacom
Bob White katika moja ya angle za Jiwe Kuu ambako kuna mawe ya historia.
Gsengo at the area.
Vijito juu ya jiwe Kuu.
Kileleni Jiwe Kuu.
Juu kabisa Jump Jump zinahusika....
Wow...
safiii......
The view from the top...!!
Hapa ndipo mahala mmoja wa watemi wa Kabila la wasukuma mwenye historia kubwa Mwanamalundi aliketi panaitwa Matako ya Mwanamalundi.
Jiwe Kuu hili ni jiwe moja lenye ukubwa wa kama hekari mbili hivi ambapo juu yake kuna mawe zaidi ya 4000 yaliyojikita sehemu na sehemu kuleta mvuto wa kipekee katika muonekano.
Kutokana na utulivu unaotawala eneo hili na upekee wa mawimbi ya sauti ukimya umesababisha wahubiri na watumishi wa makanisa kulitumia eneo hili kama sehemu ya ibada.
Kona katikati ya mawe upenuni.
Mungu kweli ameumba dunia Jiwe hili ni kama limejiegesha lakini jinsi lilivyojishikiza ni kwaaina ya kipekee kama limejishikiza hivi,, ukadhani linaweza kuanguka lakini kumbe ahata usukume vipi halianguki,
Let us try.....aaaaah wapi.!!!
Me at ze place.
Getto juu ya mwamba.
Mnyama huyu anaitwa ......
Ma-super stars wa kesho.

MKUU WA WILAYA YA TEMEKE, SOPHIA MJEMA AZINDUA MICHUANO YA UMISETA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema ambaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa Michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA), akipiga dana dana wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam leo.
 Wanafunzi wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto), akikabidhi vifaa vya michezo kwa Shule ya Sekondari ya Azania vilivyotolewa na Kampuni ya Coca Cola. Kulia Ofisa kutoka kampuni ya Coca Cola wadhamini wakubwa wa michuano hiyo kwa mwaka 2016.
 DC Mjema akisalimiana na mwamuzi wa mchezo kati ya timu ya Sekondari ya Tirav ya Yombo na Makongo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Makongo ilishinda mabao 2-1.
 DC Mjema akiwasalimia wachezaji wa timu ya Tirav.
 DC Mjema akisalimiana na wachezaji wa timu ya Makongo Sekondari.
Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema (kulia), akitoa nasaha zake kwa wachezaji hao kabla ya kuanza kucheza.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Tirav na viongozi mbalimbali.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Makongo na viongozi mbalimbali.
Hapa akiwa katika picha ya pamoja na waamuzi wa mchezo huo na viongozi mbalimbali.
Hapa mtanange ukiendelea.
Golikipa wa timu ya Tirav, Abdul Badi akiokoa moja ya hatari katika lango lake.
Wachezaji wa timu ya Makongo wakishangilia baada ya kupata bao lao la kwanza.

Na Dotto Mwaibale

MKUU wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema amezindua michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA) katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam huku akisisitiza kuwa yataendelea kuwaibua wachezaji wengi chipukizi.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mjema aliishukuru kampuni ya Cocacola kwa kudhamini mashindano hayo huku akiyaomba makampuni na wadau wengine kujitokeza kudhamini michezo mbalimbali.

Mashindano hayo yatashirikisha timu zaidi ya 40 katika mchezo wa mpira wa kikapu kwa vijana wa Shule za Sekondari kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini huku ikishirikiana na waandaaji wa michuano ya michezo ya Shule za Sekondari UMISETA katika kuhakikisha wanapata wachezaji wenye elimu kutoka mikoa yote hapa nchini.

Akizungumzia  mashindano hayo  Meneja wa Biashara wa Coca Cola Maurice Njowoka alisema wameamua kuongeza mchezo ili kupanua wigo wa mashindano hayo hapa nchini.

Aidha alisema lengo la kuungana na waandaaji hao, badala ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) pekee ni kutaka kupata wachezaji sahihi, kutoka mikoa yote, na ambao wako katika mashule ya Sekondari.

"Hii itatusaidia kupata wachezaji sahihi wenye elimu na ambao kweli wanasoma shule za sekondari,"alisema Njowoka.
Alisema tofauti na mwaka jana, tuliwatumia TFF pekee jambo ambalo tulipata wachezaji lakini katika mazingira magumu zaidi.

Alisema michuano ya mwaka huu wanaimani watapata wachezaji kiurahisi kwa sababu UMISETA ina rekodi ya wanafuzni wanaosoma katika shule za sekondari.

Njowoka alisema kwa kuanzia jijini Dar es Salaam, wametoa jezi na vifaa kwa shule za Sekondari zilizohudhuria katika mashindano hayo.

Alisema baada ya Dar es Salaam, wanaelekea Mwanza, Mbeya, Arusha na Moshi kwa ajili ya kuzindua rasmi michezo hiyo ambayo shule zinaanza kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa.

Alisema katika udhamini wao watatumia kinywaji cha Coca Cola kwa upande wa soka, wakati Kikapu watatumia Sprite, lengo ni kufanikisha michuano hiyo safari hii kutokana na kuongeza idadi ya mchezo.

GARI LANUSURIKA KUTEKETEA KWA MOTO MCHANA HUU.

 Gari ndogo aina ya Nissan Xtrail  limenusurika kuteketea kwa moto mchana huu katika barabara ya Mwanza - Shinyanga eneo la Maliasili njia kuelekea Nyegezi. 

Mashuhuda wanasema kuwa hitilafu ya umeme ilitokea upande wa injini kwenye betri na motoukazuka. 
 Baada ya kutokea moto huo baadhi ya vijana waishio maeneo ya Igogo na karibu na eneo hilo walikimbilia gari hilo wakijidai kusaidia kuzima moto kwa kutumia mchanga na matawi huku wakingoa baadhi ya spea za gari hilo lililopata ajali.

Milipuko ya baadhi ya parts zilizokuwa zikiungua zilisababisha vijana hao kusambaratika. 
Licha ya Zimamoto kuchelewa kufika eneo la tukio lakini walifanikiwa kuuzima moto huo. PICHA NA ZEPHANIA MANDIA  WA GSENGO BLOG.

WASHIRIKI 10 WAINGIA NDANI YA KUMI BORA YA WIKI YA SHINDANO LA AIRTEL TRACE MUSICSTARS.

Mmoja ya majaji wa shindano la Airtel Trace Music Stars ambaye ni mtangazaji wa TV mahiri, Mwanamuzi, Mwigizaji na mfanya biashara , Jokate Urban Mwegelo (wa kwanza kulia) akiongea na jopo la majaji wenzake wakati wakichagua vijana waliofudhu kuingia kumi bora katika wiki hii. Zoezi hili lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel Tanzania zilizoko Moroco jijini Dar es Saalam Jana
Mmoja ya majaji wa shindano la Airtel Trace Music Stars mtunzi wa nyimbo na mwaimu wa Muziki Anthony Joseph Namata“JOETT (aliyesimama) akisoma na kupigia maoni ya majaji wenzake juu ya washiriki waliofanya vizuri katika shindano la Airtel Trace Music Stars na kuingia katika kumi bora ya wiki hii wakati majaji hao walipokutana kufanya uchaguzi.
Mmoja ya majaji wa shindano la Airtel Trace Music Stars mtunzi wa nyimbo na mwaimu wa Muziki Anthony Joseph Namata“JOETT (kulia) akitoa hoja kwa jopo la majaji wenzake wakati wakichagua vijana waliofudhu kuingia kumi bora katika wiki hii. Zoezi hili lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel Tanzania zilizoko Moroco jijini Dar es Saalam Jana.  Pichani ni  mtengenezaji wa Muziki na mfanyabiashara Luciano Gadie Tsere   (katikati) na  Lucy T. Ngongoseke,  mratibu wa Airtel Trace Music Stars

Washiriki 10 waingia  ndani ya kumi bora ya wiki ya shindano la Airtel Trace Music Stars

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Leo imetangaza washiriki kumi bora wa wiki  wa shindano kubwa barani Afika lijulikanallo Airtel Trace Music Stars lililolizinduliwa mwanzoni mwa mwezi wa pili na kuwapatia fursa vijana kuonyesha vipaji vyao.

Kabla ya kutangaza washindi hao Jopo la majaji linaloshirikisha wasanii na wataalamu wa muziki akiwemo mtangazaji wa TV mahiri, Mwanamuzi, Mwigizaji na msanii aliyejikita katika maeneo mengi, Jokate Urban Mwegelo,  mtunzi wa nyimbo na mwaimu wa Muziki Anthony Joseph Namata“JOETT pamoja na mtengenezaji wa Muziki na mfanyabiashara Luciano Gadie Tsere   likikaa mwishoni mwa wiki na kuchagua  waimbaji 10 bora kati ya vijana walioweza kushiriki mpaka sasa.

Akitangaza baadhi ya vijana waliioingia katika kumi bora , Jaji Anthony Joseph Namata“JOETT alisema “moja kati ya vigezo vilivyotumika kuwapata hawa walioingia kumi bora ni pamoja na uwezo wao wa kuimba pamoja na  sauti  lakini pia idadi ya kura anazozipata kutoka kwa wasikilizaji. 

Hivyo basi napenda kuchukua fulsa hii  kutangaza vijana waliofanikiwa kuingia katika kumi bora ambao ni pamoja naTeddy Benedict Code  55210241, Beny Sule Code 55210243, Eddy Zone (Jack) Code 55210245, Anneth Stanley Code 55210248, Sarah Code 55210249,  Nicole Grey Code 55210253, Yvone Masai Code 55210254, Adili Kwezi Code 55210115, Anneth Komba Code 552101256 , David Benson Mahenge Code 55210244”

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando alisema “Tunafurahi kuona vijana wengi wamejitokeza kushiriki  na kuonyesha vipaji vyao kwa mwaka huu, natoa wito kwa vijana kuendelea kushiriki kwani mashindano bado yanaendelea.

Sambamba na hilo tunawaomba watanzania wawapigie kura washiriki wanaowapenda pamoja na vijana hawa ili waweze kuendelea kutetea nafasi zao na hatimae kuingia kwenye tano bora na kisha kupenya kwenye fainali za kitaifa zitakazofanyika hapa jijini Dar es saalam mwishoni mwa mwezi Mei”

‘Ili kupiga kura kwa mshiriki unaempenda unatakiwa kupiga 0901002233 Kisha kuingiza code namba ya mshiriki au tuma SMS yenye code ya namba ya mshiriki kwenda namba 15594”  aliongeza Mmbando

Huu ni msimu wa pili wa  Shindano la Airtel Trace Music Stars ambapo sasa shindano hili lipo katika  hatua kitaifa, fainali za taifa zinategemea kufanyika 20 Mei 2016 ambapo mshindi wa kwanza atajishindia shilingi million 50, pamoja na kupata nafasi ya kwenda kushiriki katika mashindano ya taifa mwezi Juni Lagos nchini Nigeria.  Mshindi wa pili ataondoka na shilingi million 5 na watatu shilingi milioni 2 Ili kushiriki piga namba 0901002233.rekodi wimbo wako sasa