ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 5, 2025

WAZEE BARÀZA LA CCM KIBAHA MJI WAIBUKA NÀ KUTOA TAMKO LA KUMPAMBANIÀ RAIS DKT.SAMIA ASICHAFULIWE KWA MITANDAO

 


VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Baraza la wazee wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji Mkoa wa Pwani limelaani vikali viendo vya baadhi ya makundi ya vijana kutoka nchini Kenya kutokuwa na busara kwa kuamua kumkosea heshima  Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia kwenye mitandao ya kijamii hali ambayo inaweza kupelekea uchochezi  hali ya sintofamu kwa wananchi.

Wazee  hao wa baraza wametoa maazimioa hayo ya pamoja wakati wa kikao hicho ambacho kimekutana kwa ajili ya kuweza kujadili mambo mbali mbali yakiwemo masuala yanayohusiana na hadhi ya uongozi hasa  kuona Rais wa nchi ya Tanzania Rais Dkt SamiaSulhu Hassan anakosewa heshima na baadhi ya vijana hao wa kenya kitendo ambacho hawawezi kukifumbia macho hata kidogo.

Akisoma maazimio hayo Katibu wa Baraza la wazee wa chama cha  mapinduzi (CCM) ndugu Issack Kalleyya  amebainisha kwamba wameamua kuketi na kutoa maazimio hayo ya pamoja  kutokana na kuwepo kwa mshikamano mkubwa uliopo kati ya nchi ya Tanzania na wenzetu wa nchi za jirani ikiwemo Kenya.

"Kama baraza la wazee wa chama  chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini tumeamua kukutana kwa pamoja na kutoa maazimio yetu juu ya jambo hilo ikiwemo juu ya kuweza kutafakari kwa kina hali ya Amani na utulivu ndani ya Wilaya yetu na nchi kwa ujumla, sambamba na matukio  mbali mbali ambayo yanayoendelea katika nchi jirani ya Kenya ambayo yanafanywa na baadhi ya vijana,"amebainisha Katibu Kalleyya.
 
Aidha katika kikao hicho baraza la wazee limemshukuru kwa dhati  Rais wa  Kenya Mheshimiwa Willian Samoi Ruto kwa maamuzi yake mazuri ambayo ameyatoa ya  kuomba radhi kwa Watanzania na Waganda juu ya matendo ya vijana wao mitandaoni na kwamba  wanathamini sana  hatua yake ya kidiplomasia kama kiongozi wa Kenya katika kutambua umuhimu wa uhusiano mzuri baina ya Taanzania na  nchi  nyingine za jirani.
Kadhalika Katibu wa baraza hilo amesisitiza kuwepo kwa hali ya umoja kwa  Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa mujibu wa tamko la Mheshimiwa Moses Wetang’ula, Spika wa Bunge la Kenya, ambaye aliyesema kuwa Tanzania haina shida na Kenya na kwamba tunapaswa kuendelea na udugu wetu bila taharuki zisizo kuwa  na msingi yoyote.

Pia kikoa hicho cha baraza katika maazimio yao hawakusita kumsifu na kumpongeza kwa dhati  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kuweza kusimamia kwa vitendo utekelezaji wa miradi  mbali mbali ya kimkakati kama vile Reli ya Kisasa (SGR) na Bwawa la Mwalimu Nyerere lililopo Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani , ambapo kutokana na juhudi zake ameiweka Tanzania katika njia ya chachu ya  maendeleo makubwa ya kiuchumi pamoja na  kijamii.

Sambamba na hilo kikao cha baraza hilo kimeweza kutoa  rai kwa Serikali yetu tukufu kulinda heshima ya Taifa letu, kwa kuhakikisha kuwa wageni wote wanaoingia nchini wanazingatia sheria za nchi, ikiwa pamoja na kuwazuia wale wenye nia za kuvuruga  hali ya amani amani ya nchi sambamba na kulaani vikali  matendo ya udhalilishaji dhidi ya Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuweza kuendelea kudumisha hali  ya amani na utulivu nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la wazee wa CCM Wilaya ya Kibaha mjini Mtoro Katele amesisitiza na kuweza kutoa wito  kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukuwa hatua zinazostahili ili kuhakikisha heshima ya Taifa letu na kuona kwamba inahifadhiwa kwa kiwango kikubwa pamoja  na kuimarisha mshikamano wa hali na mali wa kikanda katika nchi za jirani.

Hivi  karibuni kumekuwepo na baadhi ya vijana kutoka nchini kenya kutokuwa na busara kwa kuanza kukosea heshima Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kupitia mitandao mbali mbali ya kijamii hali mmbayo ilimlazimu Rais wao Willian Samoi Ruto   kuomba radhi kwa Watanzania na Waganda kwa kile ambacho kimefanyika.

MWENGE WA UHURU KUZINDUA KUWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI 13 YA MAJI MKOANI TANGA YENYE THAMANI YA BILIONI 16.7

 

 



Na Oscar Assenga, TANGA

JUMLA ya Miradi 13 katika Sekta ya Maji yenye thamani ya Sh.Bilioni 16,713,383,870 inatarajiwa kuzinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 mkoani Tanga ambao unatarajiwa kuwasili mkoani hapa kesho na kuzunguka maeneo mbalimbali kwenye mkoa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Omari Lugongo alisema kwamba miradi hiyo itanufaisha wananchi 85,017 ambao wanapata huduma ya maji safi na salama na kuondokana na adha ambazo walikuwa wanazipata awali.

Alisema kila Halmashauri itakuwa na mradi na miradi 6 ya uzinduzi,miradi 5 ya uwekeji mawe ya msingi katika miradi hiyo itakayozinduliwa itajumuisha vijiji 12 lakini kuwahudumia watu 28000 na karibia asilimia 1 ya wakazi wa mkoa wa Tanga.

Alisema kwamba pia kuna miradi ya uzinduzi katika Jiji la Tanga kupitia Tanga Uwasa ambapo kutazinduliwa mita za malipo kabla na ni maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu ya viongozi wa chama na serikali ili kuhakikisha maji yanatumika kwenye viwango lakini yanatumika wananchi waweze kulipia kulingana na uwezo wao.

Aidha alisema kutakuwa na uzinduzi kwenye Jiji la Tanga ya Mita za malipo kabla 4,000 zitazinduliwa na mwenge pamoja na kuwepo na miradi mengine ya uzinduzi kwenye wilaya za Handeni ,Lushoto ,Mkinga na mwengine utakuwa ni mradi wa uwekeji mawe ya msingi.

Alisema katika wilaya ya Pangani kwenye Jimbo la Waziri wa Maji kutakuwa na mradi wa uwekeji jiwe la msingi mradi wa maji Mkwaja ili uweze kukamilika kwa kipindi kifupi kijacho na katika miradi wanayoweka uzinduzi ni Kwedizinga wilaya ya Handeni Vijiji,Mgombezi Korogwe Mjini na hapo wamejenga visima 900 vya Rais Samia Suluhu.

Aidha alisema kati ya visima hivyo ambavyo ni mradi maalumu wa kutatua changamoto ya maji kwenye maeneo yasiyokuwa na maji wilaya ya Korogwe watakuwa na mradi wa uzinduzi na wilaya ya Muheza watakuwa na mradi wa visima 900 watakwenda kuweka jiwe la msingi lakni watu wameshaanza kupata huduma ya maji ikiwemo wilaya ya Mkinga wanazindua mradi wa maji Gombero na wilaya ya Tanga ambazo ni Mita za Luku za Maji na wilaya ya Lushoto ni mradi wa Funta –Wanga

Meneja huyo alisema pia kuna miradi mitano ya uwekaji wa mawe ya msingi kwenye eneo la Kwamaligwa wilaya ya Kilindi ambao utahudumia vijiji saba na mradi wa Maji kwamahizi ambao utahudumia eneo la Handeni Mjini.

Alieleza pia Mwenge huo utatembelea mradi wa ukarabati miundombinu ya maji Lushoto Mjini ambao utaboresha huduma kwa wakazi zaidi 23,000 na uwekeji jiwe la msingi mradi wa maji Mkwaja na Visima 900 wa Rais kwa wilaya ya Muheza ambapo miradi hiyo yote inakwenda kuwahudumia wakazi wa Tanga asilimia 3 hivyo wanategemea miradi hiyo itakapokamilika itasaidia kuboresha asilimia 3.3 ya wakazi wa Tanga wakati ile asilimia 1 ya miradi itakayozindua nayo inakuwa imeshakamilika.

“Nimpongeze Rais Dkt Samia Suluhu kwa utekelezaji wa miradi hii pamoja na Mkuu wa Mkoa kwa kuendelea kutuongoza vema katika mkoa wetu pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa huu Rajab Abdurhaman “Alisema

mwisho

UDSM YAWAITA WADAU WA ELIMU KUSHIRIKI MAADHIMISHO WIKI YA UTAFITI NA UBUNIFU.

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

CHUO  Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeutaarifu umma wa Watanzania na kuwaalika wadau wa elimu na maendeleo, kwa ujumla kushiriki katika Maadhimisho ya kumi ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya UDSM yatakayofanyika kuanzia Juni 9- 11, 2025 katika Viwanja ya Maktaba ya Chuo.

Akizungumza na Waandishi  wa Habari Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-Utafiti, Prof. Nelson Boniface (Pichani) amesema kuwa Maonesho hayo yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 11, 2025 na mazungumzo ya mashirikiano ya kimkakati, kongamano, maonesho na mawasilisho ya watafiti na wabunifu likiwa ni jukwaa la washiriki kupata fursa ya kubadilishana maarifa na ushirikiano.

Aidha, Prof.  Boniface amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni: "Kutumia teknolojia ya Dijitali ili kukuza utafiti, ubunifu na ubiasharishaji,".

Ameongeza kuwa miradi mingi itakayooneshwa ni ile ya wanafunzi na Wanataaluma huku akitanabaisha kuwa mtoa Mada Mkuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Peter Ulanga na Profesa Lilian Kaale Mkurugenzi katika masuala ya Ubunifu UDSM.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinatumia fursa hiyo kujipambanua kwa jamii kwa kuonesha shughuli zake za utafiti, ubunifu, huduma kwa umma na ubadilishanaji maarifa kwa kuunga mkono Dira ya  Taifa ya  Maendeleo 2050.



Wednesday, June 4, 2025

UBABE WA TWIGA STARS DHIDI YA DRC MUUAJI NI YULE YULE CLARA LUVANGA

 

TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars’ imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ‘Léopards Dames’ katika mchezo wa kirafiki leo Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam.


Mabao ya Twiga Stars leo yamefungwa na wacheza wa FC Juárez ya Mexico, mshambuliaji Opah Clement Tukumbuke dakika ya 26, beki Julitha Aminiel Tamuwai Singano dakika ya 43 na kiungo mshambuliaji wa Al Nassr ya Saudi Arabia, , Clara Cleitus Luvanga dakika ya 47, wakati bao pekee la Chui Jike limefungwa na mshambuliaji wa TP Mazembe ya kwao, Lubumbashi Esther Dikisha Bushiri dakika ya 90.


Ulikuwa mchezo wa pili kuzikutanisha timu hizo ndani ya tano, baada ya Ijumaa pia Twiga Stars kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 hapo hapo Azam Complex, mabao ya Twiga Stars yote yakifungwa na Clara Luvanga dakika ya 28 na 88, wakati bao pekee la Léopards Dames lilifungwa na Esther Dikisha dakika ya 72.


Michezo hiyo ni maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) kwa timu zote ambazo zinatarajiwa kufanyika nchini Morocco kuanza Julai 5 hadi 26, mwaka huu.


Tanzania imepangwa Kundi C pamoja na Afrika Kusini, Ghana na Mali, wakati DRC ipo Kundi A pamoja na wenyeji, Morocco, Zambia na Senegal na Kundi B kuna Nigeria, Tunisia, Algeria na Botswana.

UKEREWE YAWASHUKURU WAFANYAKAZI BENKI ya CRDB UKARABATI MADARASA MAWILI, MADAWATI 200

 


Mkuu wa Wiliya ya Ukerewe, Mheshimiwa Christopher Emily Ngubiagai amewashukuru wafanyakazi wa Benki ya CRDB kwa kukarabati madarasa mawili na madawati 200 kwa ajili ya Shule ya Msingi Hamkoko.

Akipokea msaada huo kutoka kwa Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Godfrey Rutasingwa, mkuu huyo wa wilaya amesea mazingira mabovu ya madarasa yanasababisha utoro kwa watoto wengi jambo ambalo seriklai inashirikiana na wadau kulifanyia kazi ili watoto wote wasome kwa utulivu unaohitajika kufanikisha ndoto zao.

“Hakika leo wafanyakazi wa Benki ya CRDB mmetupa somo kwa kujitoa kwenu kuhakikisha mnaigusa jamii jamii yetu ya wana Ukerewe. Hakika huu ni upendo mkubwa sana kutoka kwa wafanyakazi ambao sio tu inatugusa jamii ya hapa Ukerewe bali Tanzania nzima kwa ujumla. Mmeonyesha kujali na alama hii ya upendo haitosahaulika. Asanteni sana kwa heshima hii kubwa mliyotupa,” amesema Mheshimiwa Ngubiagai.

Amesisitiza kuwa shule zikiwa na miundombinu mizuri huwafanya watoto wapende kusoma kutokana na kuvutiwa na mazingira mazuri na madarasa ya kisasa, madawati bora ya kukalia. Kwa kulitambua hilo, amesema serikali inafanya kila liwezekanalo kuhakikisha inajenga shule mpya popote inapohitajika nchini na kukarabati miundombinu ya hsule za miaka mingi.

Akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi waliokuwepo kwenye hafla ya kukabidhi madarasa na madawati hayo, Mheshimiwa Ngubiagai amesema ni muhimu kwa jamii kujitoa kuchangia kuboresha mazingira ya shule kwa ajili ya watoto wa Kitanzania kujifunza kwa umakini na akaitumia nafasi hiyo kuwapongeza wafanyakazi wa Benki ya CRDB kwa kuonyesha mfano katika kujitoa kwa jamii wanaoyoihudumia na inayowazunguka.

“Hii imekuwa bahati kwetu kwani mngeweza kwenda sehemu nyingine lakini mliona inafaa kuja Ukerewe kusaidia kutatua changamoto za madarasa na kutoa madawati haya 200. Kwa kweli mmetufundisha na kutupa deni kubwa mioyoni mwetu kwani Watanzania wengi huwa wepesi kuchangia harusi na sherehe nyingine ila wazito kujitoa kwenye elimu kama mlivyofanya wafanyakazi wa Benki ya CRDB,” amesema.

Kwa upande wake, Rutasingwa amesema msaada huo umetolewa kupitia Programu ya Employee Volunteering iliyoanzishwa mwaka 2020 ambapo wafanyakazi wa Benki ya CRDB huchanga fedha kutoka kwenye mishahara yao na kuielekeza kutatua kero iliyopo kwenye jamii katika sekta ya elimu, afya, mazingira na watu waishio katika mazingira magumu.

“Moyo huu wa kujitoa kwa wafanyakazi wetu ni mwendelezo wa jitihada zinazofanywa na Benki ya CRDB kurudisha na kuwekeza katika jamii inapotoa huduma. Benki yetu hutenga asilimia moja ya faida yake baada ya kodi kwa ajili ya kuiwezesha jamii. Tunachangia madarasa, madawati, na miundombinu mingine ya shule. tunatoa vifaatiba na kuhamasisha afya ya jamii. Kupitia kampeni ya Pendezesha Tanzania, tunashiriki kutunza mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na tupo mstari wa mbele katika kuwawezesha wanawake na vijana kujitegemea kiuchumi,” amesema Rutasingwa.

Mkurugenzi huyo amefafanua kuwa utekelezaji wa Programu ya Employee Volunterring unaanzia ngazi ya mfanyakazi mmoja mmoja, matawi, ofisi za kanda mpaka idara za makao makuu ya Benki ya CRDB.

“Katika ngazi ya kanda, tayari tumeratibu na kutekeleza miradi katika kanda za Pwani, Dar es Salaam, na Kaskazini. Leo tunafungua ukurasa mpya wa jitihada hizi katika Kanda hii ya Ziwa kwa kukabidhi rasmi madarasa mawili na madawati 200 kwa shule hii ya Hamukoko hapa wilayani Ukerewe,” ameeleza Rutasingwa.

Kwa wazazi, Rutasingwa amewakumbusha umuhimu wa kuandaa mazingira haya ya kiuchumi kugharimia elimu akieleza kwamb benki ya CRDB inayo Akaunti ya Junior Jumbo inayomwezesha mzazi kuweka fedha taratibu kwa ajili y amahitaji ya mwanaye huku ikimwandaa mtoto kuwajibika kiuchumi kwa kuanza kutumia huduma za benki tangu akiwa mdogo.

“Akaunti hii haina makato na inamwezesha mzazi kuweka akiba kidogo kidogo kwa ajili ya masomo ya mtoto wake, kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu. Unachohitaji ni cheti cha kuzaliwa cha mtoto, kitambulisho cha mzazi au mlezi, na shilingi 5,000 ya kuanzia ili kufungua akaunti hii,” amesema.

Tuesday, June 3, 2025

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) MKOA WA MWANZA KATIKA MAANDALIZI YA MAZISHI YA MZEE SILVIN IBENGWE MONGELLA.



Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mwanza Ndg Michael Masanja Lushinge Smart (MNEC) (katikati aliyesimama) Mapema Leo Tarehe 03, juni 2025 Ameongoza kikao Cha Kamati ya maandalizi ya Mazishi ya Mzee  Silvin Ibengwe Mongella Ambaye ni Baba Mzazi wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Ndg John Mongella Ambacho kimefanyika nyumbani Kwa marehemu Kijiji cha Kabusungu Kata Sangabuye Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza

Aidha Mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili Uwanja wa ndege Mwanza siku ya Alhamis 05 juni, 2025 majira ya saa 12 Asubuhi na kuhifadhiwa 
Ijumaa 06, juni Mwili wa marehemu utawasili kijiji cha Kabusungu Kata Sangabuye Wilayani Ilemela Kwa Ibaada ya maombolezo kisha Ibaada ya mazishi itafanyika Tarehe 07, juni 2025 katika Kijiji cha Kabusungu

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake libarikiwe 

Imetolewa na Ofisi ya Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza