ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 13, 2025

RC TANGA ALIPONGEZA SHIRIKA LA TASAC KWA UTOAJI WA ELIMU JUU YA MADHARA YA UCHAFUZI WA MAZINGIRA YA BAHARI

 




Na Oscar Assenga,TANGA


SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limepongeza kutokana na juhudi zake kubwa za kutoa elimu kwa wananchi wakiwemo wadau mbalimbali juu ya madhara yatokanayo na uchafuzi wa mazingira ya bahari ambayo yanaweza kuelekea athari za kiuchumi kwa mtu moja moja na Taifa kwa ujumla.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt.Batilda Buriani wakati akifungua warsha ya mpango wa Taifa wa kujiandaa na mapambano ya umwagikaji wa mafuta katika bahati na mafuta.

Ambapo alisema licha ya sekta ya uchumi kuathirika kuna uwezekano mkubwa wa kupotea kwa viumbe vya bahari endapo juhudi mbalimbali hazitafanyika.

Aidha alisema kwamba jamii inapaswa kutambua umwagikaji wa mafuta katika bahari na maziwa unaweza ukaathiri vyanzo vya mapato ya wananchi wakiwemo wavuvi na hivy kuathiri uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini Taifa kwa ujumla

"Niseme tu kwamba Semina hii ina umuhimu mkubwa kwani mafuta yatakapo mwagika watu tunategemea mazao ya baharini tutapata hasara Tanga tumeshaanza na kujikita katika zao la Mwani hivyo kukitokea dharura yeyote ni lazima kuwa tayari kukabiliana nayo hivyo ni lazima tujiandae kimafunzo na kivifaa.



“Kwa kweli tunalipongeza shirika la TASAC kwa juhudi mbalimbali inazozifanya ikiwemo kutoa elimu jumuishi pamoja na ugawaji wa vifaa vinavyoweza kutumika wakati wa dharuraniwatake kuendelea kuongeza elimu hiyo kwa wadau wakiwemo wananchi sambamaba na kuwa na vifaa vya kutosha”Alisema



Hata hivyo alitumia wasaa huo kusifu juhudi za shirika hili la kutoa vifaa vya kukabiliana na changamoto hizo huku akitaka lazima wawe na utaribu mzuri wa kuvitumia ili kuweza kufikiwa kwa urahisi ili oparesheni ikitokea iwe rahisi kuvipata.

Alisema mkoa umejipanga kutoa elimu kwa wadau wote wa bahari pamoja na wananchi jinsi ya kutumia vifaa vitakavyotumika wakati wa kupambana na dharura ya umwagikaji wa mafuta hii ikilenga kuongeza zaidi ushirikiano katika kupambana na majanga pale yatakapotokea.


"Bandari ya Tanga hususani eneo la Chongoleani linatarajiwa kuwa lango kuu la kupokea na kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga Chongoleani , ujenzi wa bomba hilo upo katika hatua za mwisho wenzetu tayari wameshaweka matank ya kuhifadhia mafuta, Mkoa una mashamba ya mafuta umeyatenga tumeshatenga vitalu ambapo wenzetu wa makampuni makubwa wana maeneo yao"

"Umuhimu wa hii semini ni mkubwa sana mafuta yatakapo mwagika watu tunategemea mazao ya baharini tutapata hasara Tanga tumeshaanza na kujikita katika zao la Mwani hivyo kukitokea dharura yeyote ni lazima kuwa tayari kukabiliana nayo hivyo ni lazima tujiandae kimafunzo, kivifaa.



Awali akizungumza Mkurugenzi wa Idara ya Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa mazingira kutoka TASAC Leticia Mutaki alisema kuwa katika kuendelea kudhibiti na kupambana na athari za kimazingira katika bahari shirika hilo linaendelea kutekeleza mpango wa kitaifa wa umwagikaji wa mafuta.

Ambapo alisema mpango huo unahusisha wadau mbalimbali pamoja na wananchi katika ngazi za wilaya hii ikiwa na lengo la kuongeza uelewa na itayati wa kupambana na majanga yanapotokea.

Aidha Mutaki alisema kuwa TASAC inaendelea kusiamamia usalama wa vyombo vyote vinavyofanya safari katika bahati kuhakikisha vinakuwa na ubora wakati wote hii ikiwa na lengo la kupambana na athari za kimazingira ambazo zinaweza kujitokeza na kuelekea athari kwa viumbe na rasilimali nyingine zinazopatikana baharini.


"Pia tunashughulika na usalama wa vyombo vinavyopita kwenye maji tunaviangalia ili visichafue mazingira yetu sasa hivi tuna suala la uchumi wa buluu ambao sasa hivi Duniani imeelekeza kwamba Kuna maliasili nyingi kwenye maji lazima tuvune kwa namna ambayo itaweza kuwa endelevu TASAC tunawajibu wa kuhakikisha kwamba maliasili zote zilizopo kwenye maji zinabaki salama"



Alisema wamekuja mkoani hapa kujenga timu ili kunatokea bahati mbaya ya umwagikaji wa mafuta ili wawe na watu ambao wanaweza kufanya nao kazi katika kudhibiti athari zianazoweza kujitokeza kutokana na mafuta mabayo yanavuja.

“Tunao mradi wa EACOP ambao unaosafirisha mafuta kutoka kule Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania kama itatokea dharira yeyote ya umwagikaji wa mafuta ili kuweza kupunguza athari za kimazingira" Alisema.

Hata hivyo Mwakilishi kutoka shirika la bandari Zanzibar Abubakar Ally amelipongeze shirika la uwakala wa Meli Tanzania 'TASAC' kutokana na mafunzo hayo ambayo wameendelea kuyatoa kwa wadau wa usafirishaji wa majini pamoja na wananchi ambapo matokeo yake yameonekana na kufanikiwa kwa asilimia kubwa.

Wednesday, March 12, 2025

WAZIRI KIKWETE AKOSHWA NA MAANDALIZI YA UWASHWAJI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA MKOA WA PWANI

 VICTOR MASANGU/KIBAHA/PWANI

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, vijana,ajira na watu wenye ulemavu  Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka vijana wa halaiki ambao  wamechaguliwa kushiriki  katika maandalizi ya uwashwaji wa  Mwenge  wa uhuru Kitaifa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kuwa wazalendo na nchi yao na kutunza na kuzilinda rasilimali za Taifa.

 Ridhiwani ameyasema hayo wakati alipofanya ziara kwa ajili ya kutembelea na kugagua  mwenendo na maandalizi katika eneo la uwanja  wa shirika la elimu Kibaha ambapo utakaotimika kwa ajili ya uwashwaji wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa ikiwa sambamba na kuzungumza na vijana hao na kuwahimiza kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha maandalizi.

Naye  Injinia  kutoka  ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Charles  Kabeho ambaye pia ni msimamizi wa ukarabati wa eneo la uwanja utakaotumika  kuwashiwa Mwenge wa uhuru amebainisha kwamba  kwa sasa ukarabati  kwa sasa umeshafikia  asilimia 75.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge amebainisha kwamba maandalizi yote kwa ajili ya kuelekea katika  tukio  la kuwasha Mwenge wa Uhuru Kitaifa yanaendelea vizuri katika maeneo ya miundombinu ya barabara, nishati ya umeme, maji na kwamba  hadi  sasa hali ya ulinzi na usalama imeimarishwa kwa kiwango kikubwa.

Sherehe za uwashwaji rasmi  wa  Mwenge wa uhuru kitaifa  zinatarajiwa kufanyika rasmi Aprili 2 mwaka huu katika viwanja vya shirika la  Elimu Kibaha vilivyopo Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani ambapo viongozi mbali mbali wa  ndani na nje ya nchi wanatarajia kushiriki katika tukio hilo.

Tuesday, March 11, 2025

AL AHLY WAGOMEA MCHEZO DHIDI YA ZAMALEK

 

Klabu ya Al Ahly ya Nchini Misri imegoma kushiriki mechi yao ya dabi dhidi ya Zamalek inayotarajiwa kuchezwa leo ikisisitiza kuwa Shirikisho la Soka la Misri (EFA) linapaswa kuteua Mwamuzi wa kigeni badala ya kutumia Waamuzi wa ndani pia Klabu hiyo imetishia kujiondoa kwenye Ligi Kuu ya Misri endapo ombi lao halitatekelezwa.


Dabi hiyo ilikuwa sehemu ya hatua ya mbio za ubingwa lakini EFA ilitangaza usiku wa kuamkia leo kuwa mchezo huo utasimamiwa na Waamuzi wa ndani kinyume na makubaliano ya awali na kufuatia mkutano wa dharura uongozi wa Ahly ulitoa tamko rasmi ukitaka mchezo huo uahirishwe hadi Mwamuzi wa kigeni apatikane.

Ahly ilisisitiza kuwa iliwasilisha maombi yake mapema ikitaka Waamuzi wa kigeni kwa mechi muhimu ili kuhakikisha haki inatendeka hasa baada ya makosa ya mara kwa mara ya Waamuzi wa ndani kutotenda haki, hata hivyo Shirikisho ilijibu ikidai muda haukutosha kuwapata Waamuzi wa nje na kuitaka Ahly kuunga mkono Waamuzi wa ndani.

Mpaka sasa EFA haijatoa tamko jipya huku hali ya sintofahamu ikiendelea, yanajiri hayo huku Katika msimamo wa ligi ya Misri Pyramids FC inaongoza kwa alama 42 Ahly ikiwa ya pili na 39 huku Zamalek ikishika nafasi ya tatu kwa alama 32.

WAZIRI KIKWETE ATUA PWANI AWAPA MOYO WA UJASIRI WATOTO WA HITIFAKI KUELEKEA UWASHWAJI WA MWENGE WA UHURU APRIL 2

 


VICTOR MASANGU,KIBAHA

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, vijana,ajira na watu wenye ulemavu  Mhe. Ridhiwani Kikwete  leo machi 11 amefanya ziara ya kutembelea na kugagua eneo la uwanja wa shirika la elimu Kibaha ambao utatumiaka katika sherehe za uwashwaji wa Mwenge wa uhuru Kitaifa ambapo baada ya kupita  ameridhishwa  sana  na maandalizi ambayo yanaendelea kufanyika katika uwanja huo.
 Ridhiwani ameyasema hayo wakati alipofanya ziara kwa ajili ya kutembelea na kugagua  mwenendo na maandalizi katika eneo la uwanja  wa shirika la elimu Kibaha ambapo utakaotimika kwa ajili ya uwashwaji wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa ikiwa sambamba na kuzungumza na vijana hao na kuwahimiza kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha maandalizi.

"Nimeridhishwa sana na maandalizi yanayofanyika katika eneo hili la uwanja wa shirika la elimu Kibaha ambapo kutafanyika tukio kubwa la  sherhe za uwashwaji wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa na kwamba nimeweza kuona mwenendo mzima  wa ukarabati wa uwanja huo ikiwa pamoja na kupata fursa ya kuzungumza  vijana wa halaiki,"amesema Ridhiwani Kikwete.

Kadhalika Ridhiwani Kikwete amewataka vijana wa halaiki ambao  wamechaguliwa kushiriki  katika maandalizi ya uwashwaji wa  Mwenge  wa uhuru Kitaifa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kuwa wazalendo na nchi yao na kutunza na kuzilinda rasilimali za Taifa.
Naye  Injinia  kutoka  ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Charles  Kabeho ambaye pia ni msimamizi wa ukarabati wa eneo la uwanja utakaotumika  kuwashiwa Mwenge wa uhuru amebainisha kwamba  kwa sasa ukarabati  kwa sasa umeshafikia  asilimia 75.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge amebainisha kwamba maandalizi yote kwa ajili ya kuelekea katika  tukio  la kuwasha Mwenge wa Uhuru Kitaifa yanaendelea vizuri katika maeneo ya miundombinu ya barabara, nishati ya umeme, maji na kwamba  hadi  sasa hali ya ulinzi na usalama imeimarishwa kwa kiwango kikubwa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kwamba wamejipanga vizuri na kwamba wanatarajiwa kukabidhiwa rasmi uwanja huo amabo utatumika kwa ajili ya sherehe za uwashwaji wa Mwenge wa uhuru Kitaifa na kuwahimiza wananchi wa Mkoa wa Pwani kujitokeza kwa wingi siku hiyo.
Sherehe za uwashwaji rasmi  wa  Mwenge wa uhuru kitaifa  zinatarajiwa kufanyika rasmi Aprili 2 mwaka huu katika viwanja vya shirika la  Elimu Kibaha vilivyopo Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani ambapo viongozi mbali mbali wa  ndani na nje ya nchi wanatarajia kushiriki katika tukio hilo.

KONGAMANO LA TATHIMINI YA UJENZI WA HOSPITALI YENYE MAADILI YA KIISLAMU LAFANYIKA TANGA

 

 




Na Oscar Assenga, TANGA

KONGAMANO la Tathimini ya Ujenzi wa Hospitali itakayosimamia maadili ya Kiislamu limefanyika Jijini Tanga huku wadau wa maendeleo nchini wakiombwa kuchangia kufanikisha ujenzi huo ambao utakuwa chachu kwa kutoa huduma kwa maadili ya kiislamu.

Akizungumza wakati wa kongamano hilo Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanga Islamic Development Foundation (TIDF) ujenzi wa Hospitali hiyo Shehe Mohamed Jumaa Mzaruba alisema ujenzi ulianzishwa mwaka 2013 lakini umekuwa ukisuasua kutokana na kutokuwa taarifa za ukweli kuwafikia watu badala ya za ukweli ambazo zingeweza kusaidia kufanikisha ujenzi huo.

Alisema kwamba wanawaomba wadau kutoka maeneo mbalimbali kujitokeza kuchangia ujenzi wa Hospitali hiyo ambayo itakuwa ni faraja kubwa kwao kutokana itakuwa ikisaidia kuwezesha kutoa huduma kwa maadili ya kiislamu.

Aidha alisema kwamba hilo jambo ni huduma ya kijamii hivyo wanaomba wadau mbalimbali kutoka dini tofauti tofauti kuchangia ujenzi huo ambao umechukua muda mrefu ili liweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma.

Mwenyekiti huyo alimuomba Rais Dkt Samia Suluhu kuwasaidia katika ujenzi wa Hospitali hiyo itakayojengwa eneo la Tumbirii Kata ya Masiwani Jijini Tanga

Naye kwa upande wae Mlezi wa Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Mkoa wa Tanga Farida Mwakichui alisema wanashukuru mkoa kupata neema kubwa waislamu walioanzisha taasisi hiyo kwa ajili ya hospitali ya kiislamu.

“Tunafurahi tunashukuru na tunamuomba awajalie waweze kufikia malengo waliojiwekea lengo kubwa kumstiri mwanamke na mwanaume wamethubutu kufikiria hilo na wanamuomba mwenyezi mungu aliwezeshe maana watakuwa wamenusurika na aibu ya kufedheheka “Alisema

Aidha alisema ujenzi wa hospitali hiyo utakapokamilika utawawezesha kupata stara zao kwa wakimama ambao wanakwenda hospitali kupata huduma mbalimbali za matibabu.

Awali akizungumza mmoja wa viongozi wa Kundi la Sema na Tanga Ahmed Awadhi aliaamrufu Ahmed Mbu alisema jambo hilo ni nzuri kutokana na wakina mama watapata stara kutokana na kwamba wanawake watatibiwa na wanawake na wanaume kwa wanaume na vizuri sana

RC KUNENGE AWAASA WATENDAJI NA WAKUU WA USALAMA KUONGEZA JUHUDI KATIKA KUWAHUDUMIA WANANCHI

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewataka watendaji wa Kata pamoja na wakuu wa usalaam wa Wilaya zote ndani ya Mkoa huo kuongeza juhudi za utendaji kazi hasa kwa kuwahudumia wananchi kwenye maeneo yao  kwani kufanya hivyo ni kutekeleza agizo la Rais wa nchi ambae amekuwa kisisitiza kuwa kipaumbele chake ni kuondoa kero kwa jamii

Kunenge ameyasema hayo  leo Jumatatu Machi 10,2025 wakati wa  mafunzo  ya uraia na utawala bora yaliyofanyika Mjini Kibaha chini ya   Wizara ya katiba na sheria  lengo likiwa ni kuwajengea uwezo watumishi hao juu ya kuimarisha utendaji kazi wao

"Sisi sote tunamwakilisha mheshimiwa Rais wetu na kipaumbele chake ni kuondoa kero kwa wananchi wake hivyo tusipotekelza majukumu yetu sawsawa tutakuwa tuna muangusha jambo ambalo halitakiwi"amesema

Amewataka watendaji hao kuyatumia mafunzo hayo kwa kuboresha utendaji wao  na kuleta mabadiliko chanya katika maeneo yao jambo litakaloleta faida kulingana an malengo ya serikali 


"Mkiyatumia vizuri mafunzo haya italeta maana lakini kama mtayapuuza itakuwa hasara kwa muda uliotumika na hata gharama zilizotumika hivyo ni vema mkayafanyie kazi ili yalete tija" amesema.

Kwa upande wake  Mrakibu msaidizi wa Polisi Nicolaus Mhagama amewataka watendaji wa kata kuzingatia kanuni na sheria zilizopo pindi wanapowahudumia waannchi ili kuepusha migogoro isiyokuwa na ulazima

"Sasa hivi serikali imewaongezea nguvu kwa kuwaletea Polisi Kata hao ni watu muhimu ambao mnaweza kushirikiana nao huko kwa kuimarisha usalama" amesema

Mratibu wa mafunzo hayo  kutoka wizara ya katiba na sheria  wakili Prosper  Kisinini amesema kuwa serikali imeona umuhimu wa kuwapa mafunzo hayo watendaji wa ngazi mbalimbali lengo likiwa ni kuimarisha utoaji wa huduma kwa jamii.
Mwisho .

Monday, March 10, 2025

Sunday, March 9, 2025

MIAKA MINNE YA SAMIA WANAHABARI MWANZA WAJA NA MAFIGA MANNE

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Wanahabari mkoa wa Mwanza wameandaa kongamano la "Mafiga Manne' litakalofanyika Machi 18 mwaka huu, likilenga kutathmini maendeleo yaliyofanyika ndani ya miaka minne ya utawala wa Rais Samia Suluhu. Linatarajia kuhudhuriwa na washiriki kati ya 3,000 hadi 3,500 yakiwemo makundi mbalimbali kama wakulima, wavuvi, waendeshaji wa vyombo vya usafiri wa umma, ikiwemo pikipiki (bodaboda) na wafanyabiasha wasodo,alisema Mratibu wa Kongamano, Aloyce Nyanda, jana. "Tukumbuke kwamba Rais Samia aliingia madarakani Machi 19, sisi tunafanya kongamano siku moja kabla ambapo washiriki watapewa nafasi ya kuuliza maswali na kutoa maoni kuhusu maendeleo aliyofanya, ni wapi pamekamilika na wapi bado kuna pengo," alisema na kufafanua zaidi kwamba: Mwaka jana lilifanyika kongamano kama hilo kwa jina la 'Mafiga Matatu', ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akaulizwa maswali na kuyajibu akielezea hali ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hatua uliyofikiwa. Kwa mfano, alisema Nyanda, Waziri Mkuu aliulizwa kuhusu umeme wa uhakika utapatikana lini, akawahaidi watanzania kwamba changamoto hiyo itatatuliwa muda mfupi. "Na kwa tathmini tuliyofanya sisi waandaaji wa Kongamano tumegundua ahadi ya Waziri Mkuu imetimia, nishati hiyo sasa ni ya uhakika, hasa baada ya bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere kuanza kufanya kazi," alisema. #samiasuluhuhassan

MAMA KOKA AUNGANA NA WANAWAKE WA SF GROUP KUTOA MSAADA KWA VITUO VYA WATOTO YATIMA KIBAHA MJI

 

NA VICTOR MASANGU, KIBAHA


Wafanyakazi wanawake wa kampuni ya Sf Group ya Jijiji Dar es Salaam wameungana kwa pamoja na baadhi ya wanawake  wa CCM katika jimbo  la Kibaha mji na kutoa msaada wa mahitaji mbali mbali katika kituo cha afya Mkoani pamoja na vituo vya watoto yatima na wenye mahitaji maalumu.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wenzake Mkurugenzi wa rasilimali watu  na utawala wa kampuni ya Sf Group Maria Faustine  amebainisha kwamba wameaamua kutumia maadhimisho ya sherehe za siku ya mwanamke duniani kutembelea maeneo mbali mbali na kutoa msaada kwa wa mahitaji mbali mbali kwa ajili ya kuweza kuwasaidia watu na makundi yenye wahitaji.


Mkurugenzi huyo amebainisha kwamba wameweza kuchangia na kutoa msaada wa vitu mbali mbali vikiwemo sukari, sabuni, mchele, mafuta ya kula  , unga, miswaki, dawa ya meno pamoja na mahitaji mengine  muhimu ambapo jumla ya vitu vyote vimegharimu kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 4 .

"Tumeshiriki kikamilifu katka siku ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani na sisi kama wafanyakazi wanawake wa kampuni ya Sf, Group tumeweza kufanya matendo ya huruma na kutembelea katika vituo vya kulelea watoto yatima pamoja na wale wanaoishi katika mazingira magumu na tumetembelea  kituo cha afya mkoani na tumetoa msaada wa mahitaji mbali mbali,"alisema Goreth.

Kwa upande wake Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka amebainisha kwamba wameamua kuungana kwa pamoja kati  ya waafaanyakazi wa Sf Group pamoja na  baaadhi ya wanawake wa wa CCM katika kwenda kuwatembelea watu mbali mbali wenye mahitaji.  

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe.Silvesty Koka amesema kwamba lengo lake kubwa ni kuendelea kuwasaidia watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu na kwamba ataendelea kushirikiana bega kwa bega na wamiliki wa vituo hivyo katika kuendelea kuwasaidia katika mambo mbali mbali.
Naye Diwani wa kata ya Pangani Agustino Mdachi amewashukuru wanawake hao kutoka kampuni ya SF Group pamoja na Mke wa Mbunge kwa kuweza kwenda kutoa msaada katika vituo vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Nao baadhi ya wanawake waliojifungua waliopata fursa ya kutembelewa katika kituo cha afya mkoani na wamemshukuru kwa dhati Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Koka pamoja nawanawake wa Kampuni ya Sf Group kwa kuweza kuwapatia mahitaji na msaada wa vitu mbali mbali.

Wafanyakazi wa SF Group wameweza kutumiamia maadhimisho ya siku ya mwanamke Duniani ambapo imeweza kutembelea kituo cha afya Mkoani  na kutoa  msaada  katika wodi ya wananawake ikiwa sambamba na kutoa msaada  katika vituo vya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu katika kata za Misigugusugu pamoja na kata ya Pangani.