ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 24, 2022

HOFU HUSABABISHWA NA NINI?

 


Mtaalamu wa Saikolojia, Dr. Chris Mauki, amewahi kuandika kuhusu dhana ya hofu au mashaka. Akitoa ufafanuzi alisema na kusisistiza kuwa, “hofu au woga, ndio adui namba moja anayedhoofisha  nishati ya mwili wa mwanadamu kwa haraka pengine kuliko kitu kingine; na kwamba wengi wameshindwa kufikia malengo na ndoto zao katika maisha kwa sababu ya hofu, mashaka na woga.”


Hata hivyo, wapo watu wengine ambao wameelemewa na tabia ya hofu kwa kiwango cha juu sana, kitu ambacho kinawaathiri, na kuwafanya washindwe kufuatilia hata mambo muhimu ya maisha yao.Hofu ni hulka ambayo humpata kila binaadamu, ingawaje kwa viwango vinavyotofautiana. 

Kwa mujibu wa historia, hata makamanda wa vita, walioogopwa sana, walikabiliwa na hofu! Waliogopa kushindwa vita, kuchukuliwa mateka au hata kuuawa. Lakini, tofauti ya hawa na wengine, ni ujasiri na hamasa ya kushinda waliyoijenga ndani yao kila siku.

Tunaambiwa na wataalamu kuwa, kama ulivyo wasiwasi na woga, hofu ni athari ya kisaikolojia ambayo hutokana na hisia au mawazo hasi. 

Ndio maana Mwandishi John F. Paul anatuhimiza tusitawaliwe na mawazo hasi. Anasema: “Akili zetu hazikuumbwa ili kukaa na hasi, kwani unapokuwa mtu wa kuwaza au kusema hasi, kumbukumbu hizo zinasafirishwa na  kuhifadhiwa katika akili (ubongo) ya ndani, na baadaye kudhihirika au kutokea kiuhalisia.”

Kinachowakabili watu wengi, wakashindwa kuanza kufanya biashara ki-vitendo, ni hofu au woga wa kufeli, lakini vilevile wapo wanaoogopa vitu visivyojulikana.

Watu hawa badala ya kufikiria ni kwa namna gani watakabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza, wao wanajenga hofu ya kushindwa na wanaanza kuwaza madhara yatakayowapata watakaposhindwa.

Friday, September 23, 2022

OCODE YAPIGA JEKI UJENZI WA DARASA JIPYA WANAFUNZI WA KILUVYA.

 


Na Victor Masangu,Kiluvya 


Shirika lisilokuwa na kiserikali la Organization for Community Development (OCODE)  katika kuunga mkono juhudi zinazofanya na serikali katika kuboresha sekta ya elimu imejenga darasa la awali kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaosoma katika shule ya msingi Kiluvya.

Hayo yamebainisha na Mkurugenzi wa Shirika hilo la OcodeJoseph Jakson  wakati wa halfa fupi na kukabidhi rasmi darasa hilo jipya ambalo limejengwa kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wa awali ambao wanasoma katika shule hiyo kupata fursa ya kujifunza kusoma kuhesabu na kuandika.

Katika sherehe hizo za makabidhiano zimeweza kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na walimu kutoka shule mbali mbali wakiwemo walezi pamoja na wazazi wa wanafunzi hao.

"Katika kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu tumefanikiwa kujenga vyumba vinne vya madarasa kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wa awali katika manispaa ya ubungo,alisema Mkurugenzi huyo.


Aidha alisema kuwa shirika lao  kwa kipindi cha miaka minne wameweza kujenga madarasa katika shule za msingi.Goba,Kiluvya,Malamba mawili pamoja na Kibwegere na yamegharimu kiasi cha zaidi ya milioni 113.

Katika hatua nyingine alisema lengo lao kubwa ni kuwasaidia wanafunzi kwa kuwajengea miundombinu mizuri ya madarasa kwa ajili ya kuwasaidi kupata elimu ambayo ni Bora.

"Mbali na kukabidhi chumba hiki cha darasa la awali pia tumeweza kukabidhi madawati,viti pamoja na meza kwa ajili ya walimu waweze kufundisha katika mazingira mazuri,"alisema Jakson.

 Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kheri James ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo alilipongeza shirika Hilo la Ocode kwa kujikita na kusaidia kuboresha zaidi sekta ya elimu  hasa kwa wanafunzi wa awali.

Alisema serikali kuwa serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu hivyo juhudi ambazo zinafanywa na Ocode zinapelekea kuleta matokeo chanya ya kuwasaidia watoto wadogo kupata elimu bora kuanzia ngazi za chini.

Katika hatua nyingine aliwataka wazazi na walezi kuwalinda na kuwatunza watoto wao ili kuachana na vitendo vya wizi na uhalifu na badala yake wahakikishe wanawapatie elimu iliyo Bora.

"Wazazi na walezi mnapaswa kuhakikisha mnawalinda na kuwatunza watoto wenu ili waachane kabisa na vitendo vya uharifu na wizi sio anaiba vitu anakuletea na wewe unafurahia tu hii tabia sitaki kuisikia kabisa kikubwa ni watoto wetu kupata elimu,"

"Rais wetu wa awamu ya sita amekuwa mstari wa mbele katika kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu hivyo katika kuunga juhudi hizi Ocode wameweza kujenga madarasa ya awali  kwa ajili ya kuwasaidi watoto,"alisema Kheri .

Naye mkuu wa shule ya msingi Kiluvya Leah Sanga alisema mafunzo ambayo wamepatiwa na Ocode pamoja na ujenzi wa madarasa kumeweza kuwa mkombozi katika kuwasaidia watoto hao waweze kusoma na kuandika.

WATOTO WASIOCHANGANYIKANA NA WENGINE KWENYE VITUO VYA MALEZI NA MAKUZI WAMEKUWA NA TATIZO LA UDUMAVU

 

 


Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania Shukuru Musabila kulia akimkabidhi vifaa vya Michezo shule ya Msingi Gofu juu aina ya mabembea yenye thamani ya Milioni 13.5Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Perpetua Mhina  kwa ajili ya makuzi ya watoto wanaosoma darasa la awali kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Gofu Juu Monica Joseph

 -

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania Shukuru Musabila kulia akimkabidhi vifaa vya Michezo shule ya Msingi Gofu juu aina ya mabembea yenye thamani ya Milioni 13.5Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Perpetua Mhina  kwa ajili ya makuzi ya watoto wanaosoma darasa la awali kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Gofu Juu Monica Joseph
Sehemu ya wanafunzi wa darsa la awali katika shule ya Msingi Gofu Juu Jijini Tanga wakiwa kwenye mabembea hayo mara baada ya kukabidhiwa -yaliyotolewa na Shirika la Brac Maendeleo Tanzania 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania Shukuru Musabila  akizungumza mara baada ya kumalizika makabidhiano hayo
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Perpetua Mhina  akizungumza ambapo aliishukuru Shirika la Brac Tanzania kwa kuwasaidia msaada huo
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Gofu Juu Monica Joseph akizungumza


Sehemu ya watumishi wa Shirika la BRAC Tanzania wakiuwa wamekalia bembea hilo kabla ya kulikabidhi
Hapa wakiwa kwenye picha za pamoja mara baada ya makabidhiano hayo


Na Oscar Assenga,TANGA.

TAFITI zilizofanywa zinaonyesha  watoto wanaokuwa majumbani wasiochanganyikani na wengine katika vituo vya malezi na makuzi wamekuwa na tatizo la udumavu ambalo limepelekea  utambuzi wao kuwa ni hafifi .

Hayo yalisemwa na   Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania Shukuru Musabila wakati wa halfa ya kukabidhi vifaa vya Michezo shule ya Msingi Gofu juu aina ya mabembea yenye thamani ya Milioni 13.5 kwa ajili ya makuzi ya watoto wanaosoma darasa la awali.

Alisema kwa maana hawawezi kutambua kitu kutokana na umri wao lakini wanapokuwa kwenye vituo wanakuwa na malezi mazuri na makuzi ya utambuzi wa kisaikoloji na kiakili unakuwa mzuri zaidi kumjenga na kuweza kumuandaa kikamilifu.

"Nitoe wito kwa wazazi na malezi kuendelea kuwabaini watoto wote ikiwemo wenye ulemavu kwenda kwenye vituo vya malezi huku akisisitiza kwamba wanakabidhi vifaa hivyo kwa vile  vinapatikaba kwa jamii" Alisema 

Aidha alisema kwamba wataendelea kufanya kazi na Serikali na wadau wengine kuhamasisha hasa kwenye malezi na makuzi ya watoto ili baada ya mradi kwisha ili wazazi na walezi waweza kuchukua nafasi yao ya kuchangia gharama za ukarabati wa vifaa na chakula.

Shukuru alisema wamekabidhi vifaa hivyo kwa shule ya awali iliyopo  katika kituo cha  shule ya Msingi Gofu Juu Kata ya Nguvumali ikiwa ni muendelezo wa jitihada zao  za kuwasaidia watoto hapa nchini walioanza mwaka 2006.

Alisema kwamba mradi huo kwa  Tanzania una maeneo makuu matatu mojawapo ikiwa ni kuwasaidia kuwezesha wazazi na walimu  elimu ya makuzi ya watoto ambao wana miaka  kati ya mitatu hadi mitano .

"Tulianza kwa mikoa ya Mbeya,Dar na sasa tumefikisha katika mikoa ya Tanga na Dodoma na maeneo mengi nchini lengo lao ni kuwafikia watoto katika maeneo mbalimbali katika malezi na makuzi ulinzi na mtoto na katika eneo hili tunafanya kazi na  Serikali kupitia wizara ya Maendeo ya Jamii,Wanawake na Makundi Maalumu kuandaa kiongozo cha malezi ya watoto chini ya miaka mitano " Alisema 

"Kwa namna hiyo leo wanakabidhi vifaa vya michezo kwa shule ya Gofu Michezo lakini hiki ni moja ya vituo 20 vilivyopo Tanga na vyengine zipo Korogwe na maeneo mbalimbali hivyo nitoe wito kwa wazazi sisi kama Brac Maendeleo Tanzania tumeweza kuwafikia watoto hao wakiwa kwenye vituo hivyo lakini wazazi tunawaita ili kuweza kuendelea kuwapa ulinzi watoto hao maana wanapokuwa wakiwa kwenye kituo wanakuwa na ulinzi .

Awali akizungumza wakati wa halfa hiyo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Perpetua Mhina alitoa shukrani kwa Shirika la Brac Maendeleo  Tanzania kwa namna wanavyoendelea kusaidia katika sekta ya elimu na kwa makuzi kwa watoto .

Perpetua alisema  mabembea hayo yatasaidia kukuza vipaji vya watoto  kama lengo lao kauli mbiu yao inavyosema kujifunza kwa vitendo hiyo wanaamini kupitia uwepo wake utakuwa kichocheo cha kuwasaidia hata watoto wasiopenda shule  akiyakumbuka atakuwa hawezi kukosa shule na hivyo kupunguza hata utoro

Naye kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Gofu Juu Monica Joseph alisema kwamba wanalishukuru Shirika la Brac Tanzania kwq namna wanavyopeleka miradi ya maendeleo kwenye shule hiyo na kituo hicho kimekuwa ni chachu kwao kwa ajili ya kupata watoto wanaojiunga na darasa la awali kwa ajili ya kujiunga na darasa la kwanza.

Hata hiyo alitoa wito kwa wazazi na Jamii kushirikiana naa kuweza kulinda vifaa vinavyoletwa ili watoto waweze kujifunza zaidi huku akieleza kwamba changamoto kubwa ni kwamba shule hiyo haina uzio hivyo watu mbalimbali wanaweza kupita bila ruhusa.

"Hivyo  tunaomba wadau watusaidie kuweka uzio kwenye shule hii ili vifaa vinavyopelekwa shule hiyo viweze kuwa salama"Alisema

NYUKI WAMVAMIA MLEVI NA KUMUUA SHAMBANI.

 


Mwanamume mwenye umri wa kati kutoka eneo la Gaturi kaunti ya Murang'a ameaga dunia baada ya kuvamiwa na kundi la nyuki. 

 James Wambu anasemekana alikuwa anatembea akitokea sokoni alikokuwa amekwenda kubugia pombe Jumanne, Septemba 20 jioni, wakati alilemewa kutokana na kulewa chakari na kulala katika moja ya shamba jirani.

 Kwa mujibu wa mashahidi, kulikuwa na vijana ambao walikuwa wamekwenda kuvuna asali katika shamba hilo ambako mwendazake alikuwa amelala. 

Katika harakati hiyo, vijana hao walilemewa na nyuki na kukimbia ili kuokoa maisha yao lakini Wambu ambaye alikuwa amelewa chakari, alishindwa kujinusuru.

 "Mahali ambapo wanaume hao walikuwa wakilina asali ni mita chache kutoka ambapo mwathiriwa alikuwa amelala."

 “Wahalifu hao walikimbia na kumwacha Wambu akiwa amelala chini na nyuki wakamvamia na kumwacha mahututi” alisema mmoja wa walioshuhudia. 

Chifu msaidizi wa eneo hilo Peter Gethi alipokea simu kutoka kwa wakazi wakimtaarifu kuhusu kisa hicho na wakati alipofika katika eneo la tukio, Wambu alikuwa tayari ameangamia.

 "Tulifahamisha polisi waliokuja kuchukua mwili huo na kuupeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti walipokuwa wakianza uchunguzi wa tukio hilo," Gethi alisema. 

Familia ya marehemu sasa wanashinikiza haki itendeke kwa jamaa wao wakidai kuwa wanaume waliokwenda kuvuna asali wangeliwazia kumuondoa mahali hapo kabla ya kuendelea na misheni yao. 

KUTOKA Kakamega 

Mnamo Mei 2022, iliripotiwa kuwa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), katika taarifa yake ilifichua kuwa mganga alitumia nguvu zake za kichawi kuwasaka wezi wa mifugo na kuwafikisha polisi. 

Kwa mujibu wa DCI, mmiliki wa mifugo hiyo, Imbiakah, alimtembelea mganga huyo baada ya kukuta mifugo yake haipo. 

Polisi walisema baada ya mganga huyo kufanya uchawi wake, washukiwa waliotajwa kwa majina ya Hillary Momanyi, 22, John Bukhazio, 28 na Winston Mutiele, 20, waliibuka. 

Washukiwa hao walibeba mbuzi na ndama waliodaiwa kuiba huku kundi la nyuki wakiwavamia mikono.

WAPORA UNGA BAADA YA TRELA ILIYOKUWA IKISAFIRISHA KUPATA AJALI

Baadhi ya wananchi waliokuwa karibu na Hoteli ya Ole Sereni kwenye Barabara ya Mombasa siku ya Ijumaa, Septemba 23, waliangukia zare ya kupata unga wa bure wakati huu uchumi unavyowalemea wengi. Trela hiyo iliyokuwa imebeba unga wa mahindi ilipata ajali na kuvutia wapita njia. 

 Bela za unga zilianguka kutoka kwenye trela hiyo na kutapakaa barabarani, na kuvutia wakaazi wa eneo hilo waliowacha shughuli zao na kuanza kupora unga huo wa mahindi. 

Wenye magari walinaswa kwenye video za wanagenzi wakipakia bele hizo kwenye magari yao, huku wengine wakiwakodi wana bodaboda waliyosubiri kusafirisha mali. 

 Inaaminika kwamba trela hiyo ilikuwa imepita uzani unaohitajika kusafirisha mzigo huo, na kuifanya kuwa vigumu kwa dereva huyo kuithibiti kati ya 'interchange' ya Mombasa Road na Southern Bypass. 

Haijabainika ni kampuni ipi iliyokuwa ikisafirisha unga huo. 

Tukio hili linajiri wakati ambapo taifa linashuhudia mfumko wa bei ya unga wa mahindi, unaozwa kwa kati ya shilingi 200 na 250 kwa pakiti ya mbili. 

Maisha yamekuwa magumu kwa wengi wanaotegemea bidhaa hiyo, tangu serikali iondoe ruzuku ya unga hivi majuzi. 

Thursday, September 22, 2022

WAKULIMA ZAIDI YA 1200 WACHANGAMKIA FURSA YA KILIMO CHA VANILLA ZANZIBAR.

 Na Victor Masangu,Zanzibar

Zaidi ya wakulima 1200 wamejitokeza kuwekeza katika kilimo cha zao la vanilla visiwani Zanzibar kwa lengo la kujikwamua kiuchumi na kuondokana na wimbi la umasikini.

Wakulima hao wameamua kuungana na kujikita zaidi katika kilimo hicho ambacho wanaamini kitaweza kuleta mabadiliko chanya ya kuchochea ongezeko katika pato la Taifa pamoja na kuleta maendeleo kwa mkulima mmoja mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Vanilla International Limited Saimon Mkondya ambao walifanya ziara kwa ajili ya kutembelea na kunionea mashamba hayo ya Vanilla alisema lengo kubwa ni kuwasaidia wakulima kujikwamua kiuchumi.

"Kilimo cha zao hili la Vanilla kinasaidia Sana wakulima na kwamba kitaweza kuleta mabadiliko chanya zaidi ya kimaendeleo pamoja na kuchangia katika pato la Taifa kwa hiyo ni zao muhimu sana na linatajwa kuwa zao namba mbili kwa Bei kubwa duniani,"alisema Mkurugenzi huyo.

Aidha mkurugenzi huyo alibainisha kuwa kwa Sasa wamefanikiwa kuwapa ajira vijana wapatao 270 na kuwahimiza vijana wengine kushiriki kwa wingi katika kilimo cha zao Hilo.

Kwa upande wake kijana mmoja anaefahamika kwa Jina la Mohammed Mzee miaka 27 Mkazi wa Zanzibar  ameeleza kuwa ameacha kutumia Dawa za Kulevya aina ya Bangi mara baada ya kushiriki katika Kilimo cha Vanila ambacho kimebadilisha Maisha yake.

Ameeleza kwa takribani miaka 10 amekuwa akitumia bangi pamoja na kuishi maisha ya maskani ambapo hakuwa na muelekeo katika Maisha yake.
 
“Kiukweli sikuwa kwa Miaka mingi nilikuwa naishi maisha ya Maskani na kutumia Bangi ila baada ya kushawishiwa kujiunga na Kilimo cha Vanila nimeacha kutumia na sasa naelewa mustakabali wa Maisha yangu,” ameeleza.


Ameongeza kwamba kilimo hicho kina mfanya anakuwa anakuwa na Shughuli nyingi na kukosa muda wa kukaa Maskani na kutumia bangi na starehe nyingine.

Ameeleza kwa sasa anauhakika wa kuingiza kiasi kisichopungua Laki 350 na kuendelea baada ya kuingia katika kilimo hicho ambapo anashirikia katika shamba la Vanila Internation Limited Zanzibar huko bungi.

Wednesday, September 21, 2022

RAILA NA MARAFIKIZE WALIVYOSAKATA NGOMA USIKU KUCHA WAKISEMA NI YA MWISHO KAMA RAIA.

Tweet

Conversation

Video ya Raila Odinga, na Suleiman Shabhal miongoni mwa viongozi wengine wa kisiasa imezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii.  

 Baadhi ya wale ambao wako na Raila ni katibu wa muungano wa wafanyakazi nchini COTU Francis Atwoli, Peter Kenneth, mbunge wa Jubilee Maina Kamanda na Suleiman Shahbal. 

Kundi hilo liko katika sehemu ambapo inaaminika wanafuatilia matokeo ya uchaguzi wa urais ambayo yanaendelea kutangazwa na vyombo vya habari baada ya kujumuishwa. 

Kwenye video hiyo, Raila anaonekana akiwa amevalia suti licha ya kuwa ni usiku na hivyo kutoa ishara ya mtu aliye tayari kwa shughuli rasmi. 

Aidha mkononi anaonekana na simu ambapo ni kama alikuwa amezungumza na mtu fulani kabla ya kusisimka na kaunza densi. 

Baadhi ya marafiki alio na wao wanasema kuwa watu wanengue mwili vizuri hapo kwa sababu ndiyo ya mwisho akiwa bado raia. "Densi ya mwisho akiwa raia," mmoja alisema kuashiria kuwa alikuwa na imani kwamba kiongozi huyo wa ODM ataibuka mshindi wa urais. 

Video hiyo ilipakiwa mtandaoni na mwanahabari Jamal Gaddafi na nukuu za baadhi ya komenti zinasema: "Nafurahi nikiona Baba ana Furaha pia. Nani anacheka mwisho?" 

Tazama video hapa chini: Kauli za Wakenya 

@nandiThembi aliandika: "Huoni wanafanya sherehe ya mwisho kama Raia! Kesho hatakuwa Raia!" 

@Abdulmoduor aliandika: "Mimi nafurahi pia Baba anapofurahi." 

@elmer__254 aliandika: "Acha Jamaa akalie hio Kiti amesumbukana ya kutosha." 

@IreneKahiga1 aliandika "Furaha sana"