ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 15, 2024

RC KUNENGE AMKABIDHI MIKOBA RASMI DC MPYA WA KISARAWE MAGOTI

 NA VICTOR MASANGU, PWANI.

Mkuu mpya wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Mhe.Petro Magoti ameapishwa leo rasmi  na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge na kuahidi hatokuwa kikwazo chochote katika kusikiliza kero na changamoto za  wananchi bila ubaguzi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa halfa fupi ya uapisho wake uliofanyika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani na kusema kwamba  ameteuliwa  na  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan hivyo atatimiza wajibu wake ipasavyo kwa weledi na uadilifu mkubwa kwa kushirikiana na viongozi wenzake.

DC MAGOTI NA WAZIRI JAFO WASHIRIKI MAZISHI YA MWENYEKITI BAMITA TAIFA


 NA VICTOR MASANGU, KISARAWE

 
Mkuu mpya  wa Wilaya ya Kisarawe Mh. Petro Magoti  leo Jumamosi ameungana na mamia ya  wananchi wake wa kutoka sehemu mbali mbali za Kisarawe kwa ajili ya kushiriki mazishi kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA).

Marehemu mzee Salumu Sung'e salumu ambaye pia alikuwa ni Mjumbe wa kamati ya amani ya Wilaya ya Kisarawe  alifariki siku ya  jana Mkoani na mazishi yake yamefanyika kijiji cha Mengwa kata Boga na kuhudhuliwa na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Wilaya ya Kisarawe.

Akitoa salamu za rambi rambi katika msiba huo Mkuu wa Wilaya hiyo petro Magoti ameelezea mambo makubwa na mazuri aliyoyafanya marahemu  Mzee Salumu katika enzi za uhai wake akiwa  katika nafasi ya Mjumbe wa Kamati ya amani katika Wilaya ya Kisarawe na nafasi mbali mbali za uongozi.

Mkuu huyo wa Wilaya  aliwaomba wananchi wa Kisarawe  kuhakikisha kwamba wana muhenzi kwa heshima  mzee huyo na kuwaomba kuweka misingi mizuri kwa ajili ya kudumisha amani na upendo  na kumpa ushirikiano  wa kutosha katika shughuli mbali mbali zinazofanyika katika Wilaya  ya Kisarawe.

Kadhalika alifafanua kwamba kwa  niaba ya Serikali ya  Wiaya ya Kisarawe ametoa pole nakusema Serikali ipo bega kwa bega katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na huzuni kubwa kwa ndugu, jamaa na marafiki pamoja na familia  nzima.

Pia katika mazishi hayo Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Mh. Seleman Jafo ambaye pia ni Waziri wa nchi Ofisi ya Rais muungano na mazingira naye ameshiriki kikamilifu na wananchi wa jimbo lake katika mazishi hayo na kuwafariji wafiwa wote ambao wameondokewa na mzee huyo ambaye alikuwa ni kiongozi wa kuigwa.

Waziri Jafo alisema kwamba marehemu wakati wa uhai  wake alikuwa ni mtu shupavu na imara na alikuwa mwenye kutekeleza majukumu yake ya kazi ipasavyo  na kwamba atamkumbuka kwa yale yote mazuri ambayo ameweza kuyafanya kwa wananchi wa Wilaya ya Kisarawe na maeneo mengine.

"Kwa kweli mzee wetu nimekuwa nae kwa kipindi kirefu sana na tumeweza kufanya naye kazi kwa umoja kwa kipindi chote kwa hivyo natoa pole nyingi sana kwa ndugu jamaa na marafiki kwa kuondokewa na mzee wetu na kitu kikubwa tuendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ampokee na apumzike salama,"alisema Waziri Jafo.

Katika mazishi hayo pia wamehudhulia viongozi mbali mbali wakiwemo wa chama cha mapinduzi wakiongozwa na mwenyekiti wao Halfani Sika, mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kisarawe, viongozi mbali mbali wa madhehebu ya dini, wakuu wa idara pamoja na wananchi kutoka maeneo ya Kisarawe na maeneo mengine ya jirani ya Jiji la Dar es Salaam.

Friday, June 14, 2024

SHINDANO SAMIA CHALLANCE LATINGA MWANZA KAMA KUMSIFIA RAIS UCHAWA BASI HATA WAPINZANI NAO NI MACHAWA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

"Mnasema ninyi siyo CHAWA Jeh ina maana mnawachukia machawa?" Ni swali la mwanahabari G. Sengo wa Jembe Fm Mwanza, katika Mkutano wa taasisi ya Africa Ant-Violence Journalist, ambao wako jijini Mwanza kwaajili ya kusimamia shindano la SAMIA CHALLENGE YOU KNOW, lililojikita katika kushindanisha wananchi rika zote katika kushindana kuainisha na kuelezea shughuli mbalimbali za maendeleo zilizofanywa na zinazofanywa Serikali hapa nchini. Shindano la 'SAMIA CHALLENGE YOU KNOW' kwa jiji la Mwanza litafanyika kwa siku mbili yaani Jumamosi ya Tarehe 15 na Jumapili ya Tarehe 16 ambapo washindi watatu watajinyakulia zawadi za fedha taslimu.

ZAIDI SIKILIZA TAARIAFA HII. #mwanza #samiasuluhuhassan

JUMAPILI HII MWANZA PATACHIMBIKA RC MTANDA USO KWA USO DHIDI YA DC NASSARI

 NA ALBERT G. SENGO/ MWANZA

Ilianza kama utani lakini hivi lakini sasa inakwenda kuwa nayo historia inakwenda kuandikwa, kwa mara ya kwanza wakazi wa jiji la Miamba (Rock City) Mwanza wanakwenda kushuhudia mtanange wa kukata na shoka baina ya timu ya Veterani ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda dhidi ya timu ya Veterani ya Mkuu wa Wilaya ya Magu Joshua Nassari. Kwa mujibu wa wasemaji ambao pia ni wachezaji wa timu zote mbili wanasema ni uhakika kwamba viongozi hao wawili nao watashuka dimbani kuwa sehemu ya 'First Eleven' ya wachezaji ishirini na mbili wa pande mbili zinazoshuka kupepetana Jumapili ya wiki hii yaani tarehe 16 Juni 2024 katika dimba la Nyamagana jijini hapa, ambapo tayari mashabiki toka ofisi za Serikali toka wilaya za karibu wamepanga kuhudhuria mtanange huo wenye 'KAULI MBIU SHIRIKI MICHEZO ILI KAZI IENDELEE' #mwanza #magu #samiasuluhuhassan

NHIF TANGA YAIBUKA MSHINDI WA UTOAJI HUDUMA BORA ZA AFYA KATIKA MAONYESHO YA 10 YA BIASHARA NA UTALII JIJINI TANGA


 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga  Evans Nyangasa  (kulia) akikabidhiwa Cheti cha Ushindi wa utoaji huduma za bima ya afya na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi ,Dkt Batilda Burian (kushoto) kwenye maonyesho ya 10 ya Biashara na Utalii yaliyofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara Jijini Tanga na  yaliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga (kulia) Evans Nyangasa akikabidhiwa Cheti cha Ushindi wa utoaji huduma za bima ya afya na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi ,Dkt Batilda Burian (kushoto) kwenye maonyesho ya 10 ya Biashara na Utalii yaliyofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara Jijini Tanga na  yaliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita





RC PWANI AMUAPISHA RASMI PETRO MAGOTI KUWA MKUU MPYA WA WILAYA YA KISARAWE

 

NA VICTOR MASANGU,PWANI 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge leo amemuapisha rasmi Petro Magoti kuwa mkuu mpya wa Wilaya ya Kisarawe na kumuagiza kwamba anaweka kipaumbele kikubwa katika suala zima la ulinzi na usalama katika maeneo mbali mbali.

 Katika halfa hiyo ya uapisho  imehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali viongozi wa chama,wakurugenzi,wakuuwa Wilaya,wakuu wa idara  pamoja na wageni wengine kutoka sehemu mbali mbali.

Mara baada ya kuapishwa rasmi Mkuu huyo mpya wa Wilaya Petro Magoti alitoa shukrani kwa Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kumuamini na kumchagua katika nafasi hiyo.

Mkuu huyo aliahidi kushirikiana bega kwa bega na viongozi wengine wa Wilaya ya Kisarawe pamoja na Mkoa mzima wa Pwani kwa lengo la kuweza kuleta maendeleo kwa wananchi.


"Nashukuru kwa dhati kwa Rais kuweza kunichagua katika nafasi hii na mm nitakuwa mstari wa mbele katika kusaidia na viongozi wenzangu katika kuwatumikia wananchi wa Wilaya ya Kisarawe ",alisema Magoti.

Aidha Magoti alisema kuwa ataonyesha taswira nzuri katika suala zima la uwajibikaji katika uongozi wake na kwamba atayatekeleza yale yote ambayo ameagizwa na Rais  kuyatekeleza  katika sekta mbali mbali.

"Nchi hii ya Tanzania ina watu wengi sana ambao ni wasomi na wengine wana uwezo mkubwa lakini mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweza kumpendeza na kuamua kunichagua katika nafasi hii na mm namwomba Mungu anijalie niwe mtiifu katika kazi hii,"alifafanua  Magoti.

Kadhalika Mkuu huyo alimwakikishia Mkuu wa Mkoa wa Pwani kumpa ushirikiano wa kutosha yeye pamoja na wasaidizi wake wote.

Magoti aliongeza kuwa katika kutekeleza majukumu yake atahakikisha anafanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia misingi ya kuwa na mshikamano pamoja na utiifu.

Aliwaomba viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) wa ngazi zote pamoja na wananchi kufanya kazi kama timu ya pamoja ili kuweza kumsaidia Rais katika mambo mbali mbali.

"Mimi nimefanya kazi Ikulu na Rais wetu kwa kweli anachapa kazi kweli usiku na mchana maana halali kwa hivyo na sisi viongozi tunapaswa kuiga mfano wake katika kutimiza wajibu wetu,"alisema Magoti.

 Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani mara baada ya kumuapisha Mkuu huyo wa Wilaya alimtaka kusikiliza kero na changamoto mbali mbali za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kunenge alisema kwamba katika Wilaya ya Kisarawe kunatakiwa kuangalia vipaumbele ikiwemo suala la kusimamia hali ya ulinzi na usalama kwa wananchi wake.

Pia alimuimiza kutumia muda wake katika kusimamia mambo mbali mbali ya msingi ikiwemo suala kutekeleza katiba ya nchi pamoja na kutekeleza Ilani ya chama kwa vitendo.

Pia Kunenge hakusita kukumbishia suala la ukusanyaji wa mapato ikiwa sambamba na kutangaza vivutio vya utalii vilivyomo katima Wilaya husika na kuweka mikakati ya kuwa na kilimo chenye tija.

 Rais wa awamu ya sita  Dkt Samia Suluhu Hassan hivi karibuni alimteuwa Petro Magoti kuwa mkuu mpya wa Wilaya ya Kisarawe ambapo leo amepata fursa ya kuapishwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge.

Thursday, June 13, 2024

HAKUNA DAWA YA KUPAKA KIUNGO CHA MWANAUME ILI IINGIZWE KWENYE CHA CHAKIKE KAMA TIBA HUO NI WIZI TU

NA ALBERT G. SENGO/ MWANZA

"Ni wizi mtupu, utaishia kuchezewa na kuambulia maradhi" na Dr Mossi, ni Bingwa wa Tiba asili, Ajali za moto, Vidonda vya tumbo, Utumbo kuoza, Ganzi mwilini, Uzazi kwa kina dada , Chango la kuchoma na Kuhariibu mimba, Uvimbe tumboni na Walio vimba matumbo , Kusafisha Figo ghalama ni nafuu sana kwa atakae hitaji huduma ya kuonana na daktari.

Dr. Mossi atakufuata popote ulipo kwa huduma maalum, pia kwa wale wanaosumbuliwa na Bawasili au Mang'ondi daktari anatibu ndani ya wiki moja tu, Matatizo ya ngozi au Mapele yanayo toa maji maji tiba ipo ambapo ngozi yako itarudi vizuri kama awali. Kwa maelezo na ushauli tembelea TikTok ya Dr. Mossi, au Whatsapp 0764219747 na utahudumiwa popote pale ulipo. Nawatakia afya njema na Mungu awabariki. #samiasuluhuhassan #mwanza #Ukerewe #tibaasili

Tuesday, June 11, 2024

WATANZANIA WAWILI WAPELEKA KITABU CHA UTENGAMANO WA AFRIKA, AFRIKA KUSINI

 

Wanahistoria wawili wadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Maxilian Chuhila na James Zotto katika picha ya pamoja baada ya kukipeleka kitacho chao kuhusu Utengamano wa Africa, mgogoro wa Sahara nchini Africa Kusini.
Dk Maxilian Chuhila akizungumza na wanazuoni kutoka Chuo Kikuu cha Johannesburg kuhusu kitabu cha utangamano wa Afrika  baada ya kukifikisha kitabu hicho nchini Africa Kusini


BAADA ya kuzindua kitabu kinachohusu  Utengamano wa Afrika; Mgogoro wa Sahara  nchini Tanzania na baadae Kenya,  Watanzania wawili kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)  wamefanikiwa kukifikisha kitabu chao nchini Afrika Kusini.


Wanahistoria hao  Dk Maximilian Chuhila na James Zotto wamefanikiwa kukipeleka kitabu chao  nchini  Afrika Kusini wakilenga kitumike kufundishia elimu ya juu katika nchi za Afrika.

Awali, Dk Chuhila na Zotto walifanya uzinduzi wa kitabu hicho kilicho chapishwa na APE Network Chuo Kikuu Katoliki cha Ruaha (Rucu) mkoani Iringa na baadae wakakipeleka Chuo Kikuu cha Kennyata, Nchini Kenya.

Jana Juni 11, 2024 wahadhiri hao walifanikiwa kufikisha maudhui ya kitabu hicho katika Chuo Kikuu cha Johannesburg huku wakipata nafasi ya kuzungumza na  wanahistoria mbalimbali kutoka nchini humo wakiwamo wanafunzi na wahadhiri.

Dk Chuhila ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Historia nchini amesema kitabu hicho ni miongoni mwa vitabu vilivyo onyesha kwa undani masuala ya utengamano wa Afrika hasa kuhusu mgogoro wa Sahara.

Kabla ya kuandika, Wanahistoria hao wawili walifanya utafiti nchini Morroco kisha kuja na kitabu wanacho amini kama kikitumika vyuo vikuu kitaongeza uelewa kuhusu utnganao wa Afrika hasa, mgogoro huo wa Sahara.

Awali, Zotto alisema utengamano wa Afrika ni silaha laini inayoweza kumaliza mzozo wa Sahara uliodumu kwa zaidi ya miongo miwili sasa.
 Morroco na  Chama cha Ukombozi wa Sahara ya Magharibi Polisario zimekuwa  zikilumbana kwa zaidi ya miongo miwili  kuhusiana na udhibiti wa eneo hilo.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Iringa, Jimson Sanga amesema jitihada za wanahistoria hao zinapaswa kuigwa na wahadhiri wengine kwamba, badala ya kuandaa maudhui yanayoishia ndani ya nchi, wanaweza kusambaza duniani kote.

“Binafsi nimeona kumbe inawezekana, kama tunaweza kufanya tafiti za ndani ya nchi basi tunaweza kufanya tafiti nche na maandiko yetu yakatumika katika kutoa elimu vyuo vikuu mbalimbali,” amesema Sanga.

Amesema badala ya kuwa wanapokea maandiko na vitabu kutoka mataifa mengine, wanaweza pia kusambaza maudhuo hayo nje ya nchi.
Mwisho.