ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 16, 2022

DAWASA YAJENGA BWAWA KUBWA LA KUHIFADHI MAJI PWANI


Mtendaji mkuu wa Dawasa  Injnia Cyprian Luhemeja akizungumza katika ziara hiyo juu ya mikakati ambayo wamejiwekea katika kukabiliana na chanagamoto ya maji hasa katika kipindi cha miezi ya ukame.

 Na Victor Masangu,Pwani 

Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika kukabiliana na changamoto za ukosefu wa maji  imeaanza kuweka mipango madhubuti na kuchukua hatua stahiki wakati wa  ukame unapotokea  kwa kujenga mabwawa mbali mbali kwa ajili ya kutunzia maji.


 Kauli hiyo imetolewa na mtendaji mkuu wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja ambapo  alisema kwamba Ujenzi wa mabwawa hayo yataweza kusaidia wananchi kuondokana na adha na kero waliyokuwa wakiipata.

Kuhemeja alifafanua kuwa kiwango kilichopo kwa sasa cha upatikanaji wa maji kitaweza kutuvusha katika kipindi kizima cha kiangazi na kwamba wananchi wa Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani wasiwe na shaka yoyote.


Pia Luhemeja katika hatua nyingine amewataka wananchi wote kuhakikisha kwamba wanatunza na kulinda vyanzo vyote vya maji  ili kuwepo na upatikanaji wa maji ya uhakika katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na Mkoa wa Pwani. 


“Itakumbukwa kwamba mnamo mwaka jana maeneo kadhaa ya Jiji la Dar es Salaam yalikumbwa na tatizo la uhaba wa maji nah ii ni kutokana na ukame uliosababishwa na kutokunyesha kwa mvua za vuli na ndio maana wakuu wa mikoa hii miwili wameweza kuungana kwa pamoja na kamati za ulinzi na usalama wakaona ni jambo la busara kuweza kutembelea na kujionea vyanzo vya maji,” alisema Luhemeja.


Kadhalika Luhemeja alisema kwamba mamlaka hiyo kwa sasa imeweka mipango madhubuti kwa ajili ya kuweza kuendelea  kufanyabjitihada za makusudi za kuhakikisha kwamba kiasi cha maji kilichopo kwa sasa kinalindwa ili kuweza kudhibiti hali ya  upotevu wa maji.


Kadhalika aliziomba kamati za ulinzi na usalama za mikoa yote miwili kushirikiana kwa dhati ili kuweza kuwadhibiti baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiyachepusha maji na kwamba ana imani kubwa bwawa ambalo wamelijenga kwa ajili ya kuhifadhia maji litakuwa ni mkombozi hasa katika kipindi chote cha ukame.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amosi Makala ametoa wito kwa wananchi pamoja na viongozi mbali mbali wa dini zote kuhakikisha wanafanya maombi kwa ajili ya kuombea mvua za vuli zinyeshe ili kusiweze kutokea tena majanga ya ukame kama ilivyoweza kutokea katika kipindi cha mwaka jana hali ambayo ilipelekea vyanzo  vya  maji  kupungua na kusababisha  wananchi kupata usumbufu.


Pia  katika ziara hiyo Makala ameridhishwa na kazi amabzo zinafanywa na viongozi wa Dawasa na kuwahakikishia wakazi wa Mkoa huo kuwa hali ya upatikanaji wa huduma ya  maji safi na salama kwa sasa ni nzuri hivyo wasiwe na shaka.


“Ndugu zangu waandishi wa habari mwaka jana kuliweza kutokea hali ya ukame wa maji kutokana na kutonyesha kwa mvua za vuli  lakini nataka niwaambia kitu kikubwa ni kuomba Dua na maombi mvua zinyeshe na sio kuilaumu serikali kwani serikali haileti mvua na kwamba tutazidi kushirikiana na mamlaka husika lengo ikiwa hali ya maji iweze kupatikana katika kipindi chote,”alisema Makala.


 Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wenye tabia ya kuchepusha maji kutoka kwenye vyanzo vya maji na kuahidi kuwachukulia hatua kali kwa wale wote ambao watahusika kwani lengo la serikali ni kuwapelekea huduma ya maji safi na salama  katika maeneo mbali mbali.


“Kitu kikubwa ninachowaomba wanachi kuhakikisha  kwamba  wanaachana mara moja na tabia ya kuchepusha maji katika  vyanzo  vya  mto ruvu kwani wakifanya hivyo kunapelekea  maji yapungue katika vyanzo vyetu vya maji”alisema Kunenge.       


Ujio wa ziara hiyo ya siku moja ambayo imefanywa na wakuu wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani pamoja na wajumbe wa kamati za ulinzi na usalama wa mikoa miwili imeweza kusaidia kujionea chanzo cha maji Cha mto Ruvu pamoja na mitambo ya Ruvu juu na Ruvu chini.

WAZIRI MCHENGERWA KUUNDA KAMATI MAALUMU YA KUANDAA MDUNDOWA KITANZANIA

 


 
Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema anakwenda kuunda kamati maalum kwa ajili ya kuratibu uzalishaji mdundo  wa muziki wa  kitanzania ambao utaitangaza  Tanzania Duniani.  

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo leo Julai 13, 2022 alipotembelea studio ya kuzalisha kazi za sanaa ya Wanene na kufanya majadiliano na wafanyakazi wa studio hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.


 “Dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuwa na mdundo utakaoitambulisha nchi yetu kimataifa ili kuuza utamaduni wa nchi yetu kwenye mataifa mbalimbali duniani” amesisitiza Mhe. Mchengerwa.

Amesema Kamati hiyo maalum itaundwa na walimu wabobezi   kutoka vyuo vikuu, wazalishaji wa Muziki, wanamuziki pamoja na viongozi wa kimila(machifu).


Amesema Tanzania imebahatika kuwa na utajiri wa utamaduni ambao kama utatumika vizuri kutengeneza midundo  ya miziki kama ilivyo kwa nchi mbalimbali duniani utasaidia  kuitangaza  Tanzania na  kuinua  uchumi wa Tanzania.


Aidha, amewapongeza wazalishaji hao wa muziki ambapo amesema wanafanya kazi nzuri ya  kuandaa kazi bora  ambazo zina ubunifu mkubwa. 


Amesema amefurahishwa kuona wazalishaji wenye ubunifu mkubwa ambapo amesisistiza kuwa kama watashirikiana kwa pamoja na Serikali wataweza Kwa upande wake Meneja wa Studio ya Wanene Humphrey Domboka amemshukuru Waziri Mchengerwa kwa kuwa karibu na wadau wa wa sekta ambazo anazisimamia.

Domboka amesema endapo Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kunakuwa na mapinduzi makubwa ambapo amempongeza Mhe. Rais kwa kazi kubwa anayofanya  kwenye sekta ya Sanaa, Utamaduni na Michezo.

SKOFU NZUMBI-AHIMIZA SUALA LA SENSA AMESEMA HATA WANA ISRAEL WALIHESABIWA

 

ASKOFU na Mwenyekiti wa kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Dogo la Kaskazini Mashariki mwa Tanzania Mussa Nzumbi kulia akiteta jambo na Mchungaji wa Kanisa Waadventista Kana Tanga  Mchungaji wa Kanisa hilo Tanga  Julius Mbwambo kabla ya kuanza vikao vya maandalizi ya kuelekea kusheherekea Jubilee ya miaka zaidi 50 ya Kanisa hilo


Na Oscar Assenga,TANGA.

ASKOFU na Mwenyekiti wa kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Dogo la Kaskazini Mashariki mwa Tanzania Mussa Nzumbi amesema suala la Sensa ya Watu na Makazi ni muhimu kwa maendeleo ya nchi huku akieleza maana hata bibilia inasema wana wa Israel walihesabiwa

Huku akiwahimiza waumini wa kanisa hilo kuhakikisha wanashiriki kwenye zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kikamilifu ili Taifa liweza kujiua idadi ya watu na kuweza kupanga mipango ya kuweza kuwahudumia.

Nzumbi aliyasema hayo wakati wa vikao vya maandalizi ya Jubilee ya miaka 50 ya Kanisa hilo katika kanda ya Tanga ambapo alisema wakati wanaelekea kwenye maadhimisho hayo

Alisema sambamba na hilo wataendelea kuliombea Taifa na viongozi ili kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kuwepo ili wananchi waweze kupata nafasi ya kumuabudu Mungu.

Alisema kuelekea Jubilee hiyo wanamshukuru Mungu amewasaidia kwenye eneo hilo wamekuwa na ongezako kubwa la waumini na huduma za kijamii ikiwemo shule ya Kana Central English Medium na wamekuwa na huduma za kijamii wanazofanya maeneo mbalimbali kama kutoa damu hivyo yote yanawaleta pamoja kutafaraka.

Aidha alisema wanaendelea kuhimiza suala la sensa ya watu na makazi kwa maana suala hilo ni la kibibilia hata wana wa Israel walihisabiwa hivyo ni muhimu kwa sababu ili taifa liweza kujua idadi na serikali iweze kuwahudumia.

“Kwenye Jubilee hii tunaiombea Serikali,wananchi Mungu aendelee kutulinda amani na upendo vikatawale kwenye Taifa letu tunaamini kunapokuwa na utulivu ndio tunapata nafasi ya kwenda kumuambudu mungu kwa uhuru na utulivu zaidi”Alisema Askofu Nzumbi

Hata hivyo alisema kwamba wanaiombea pia Rais ,Serikali ,Mkoa wa Tanga na maeneo mbalimbali yaweze kuwa salama na amani iweze kutawala .

“Tupo hapa Kanda ya Central kwa ajili ya mikutano ya Jubilee ya miaka 50 ya Kanisa hilo Jijini Tanga tunamshukuru Mungu ametusaidia kazi kwenye eneo hilo tumekuwa na ongezako kubwa la waumini na huduma za kijamii kama shule ya Kana Central English Medium na wamekuwa na huduma za kijamii tulizofanya maeneo mbalimbali kama kutoa damu yote hayo yanawaleta pamoja kutafarakani”Alisema

Akofu Nzumbi alisema wana mshukuru Mungu kwa kazi kubwa na Jubilee hiyo inawasaidia wa waumini watafakari mahali walipotoka na mahali wanapokwenda.

“Lakini tuna mikakati kufungua shule ya sekondari Ngomeni itakayosaidia vijana wetu waweze kupata elimu ya dunia sambamba na kufungua kituo vya afya kwenye baadhi ya maeneneo nitoe wito kwa Jamii,kanisa na wananchi tuendelee kushiriki kwa mshikamano tufanye kazi tuendelea kusaidiana”Alisema Askofu Nzumbi

Naye kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa la Wasabato Julius Mbwambo alisema tukio la kusheherekea maiaka zaidi ya 50 katika kanda ya Tanga ni kazi ya mungu imekuwa sana na kwa miaka hiyo wanakiri kumuona mungu akitembea nao.

Alisema wanaendelea kusherehekea miaka ya kazi ya Mungu na wanaamini yule Mungu aliyekuwepo hapo awali waendelea kuwa naye huku akieleza wataendelea kuifanya kazi ya Mungu mpaka atakaporudi kwa mara ya pili

Thursday, July 14, 2022

TANESCO TANGA YAWAONYA WANAOHARIBU MIUNDOMBINU

 



Afisa Usalama wa Shirika la Tanesco Mkoa wa Tanga Emanuel Kimario akizungumza na waandishi wa habari leo .

Na Oscar Assenga, Tanga

SHIRIKA la Umeme nchini Tanesco limewaonya wananchi wenye tabia za kuhujumu miundombinu kuacha mara moja tabia hizo kabla hawajachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani na kifungo.

Onyo hilo lilitolewa na Afisa Usalama wa Shirika la Tanesco Mkoa wa Tanga Emanuel Kimario wakati akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu changamoto zinazosababisha ukosefu wa umeme kutokana na uharibifu na hujuma kwenye miundombinu ya shirika hilo.

Alisema vitendo hivyo vinafanywa na baadhi ya wananchi wasio waaminifu na kusababisha shirika kutumua fedha nyingi kurudisha huduma na shughuli za umeme katika hali ya kawaida na pia kupelekea wateja kukosa huduma hiyo na kuzorotesha shughuli za kiuchumi za kila siku.

“Lakini kutokana na gharama kubwa ambazo zinatumika kurudisha huduma kutokana na uharibifu shirika linaingia gharama kubwa na hivyo kupunguza kasi ya usambazaji wa umeme kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme”alisema

Hata hivyo aliomba wananchi wawape ushirikiano kwa kuwafuchua wananchi ambao wamekuwa wakihujumu miundombinu ya shirika hilo ikiwemo kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili waweze kuchukuliwa hatua na kuhakikisha miundombinu yao inakuwa salama na huduma inapatikana ipasavyo.

“Tumekuwa tukifanya operesheni kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha huduma inapatikana na pale ambapo mwananchi anabainika amehujumu miundombinu kunawachukuliwa hatua”Alisema

Aidha alisema hivi karibu kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kulitokea hujuma kwenye maeneo yao na walifanikiwa kuwamata baadhi ya watuhumiwa mashauri yao yapo mahakamani na mmoja wapo alifunguliwa shauri la uhujumu uchumi namba 1 la mwaka 2022 na limemalizika na mtuhumiwa amehukumiwa kwenda Jela miaka 20.
  

Alisema hatua ya kukamatwa mtuhumiwa huyo na wengine ambao mashauri saba  yanaendelea kwenye mahakama za wilaya za Handeni,Lushoto na Tanga mjini  ambapo kati ya hayo mawili yametolewa hukumu ni kutokana na operesheni ambayo wameifanya kushirikiana na vyombo vyengine vya usalama na kufanikiwa kuwakamataa.

Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa Mohamud Hamisi shauri hilo lilimalizika Julai 12 mwaka huu huku akitoa rai kwa wananchi kulinda miundombinu na kuitunza ikiwemo kutambua kwamba ni jukumu la watu wote kuilinda na wale wanaofanya hujuma kuacha kufanya hivyo kwani hawapo tayari kuona watu wachache wanahujumu muindimbiu hiyo .

MVUVI APOTEA ZIWANI WAWILI WAOKOLEWA MKEWE ANAKOROGA UJI ILI APATIKANE

 Taarifa mbaya kutoka Ziwa Victoria, zinamhusu mvuvi aliyejulikana kwa jina la Salehe Haruna (42) anatajwa kuzama maji katika eneo la Sweya wilayani Nyamagana mkoani Mwanza,

Mkewe Salehe aitwaye Helleno Misoji ameonekana kuweka kambi pembezoni mwa eneo la ufukweni mitumbwi inapotia nanga, akikoroga uji kwenye mafiga pasina kuwa na moto akilia na kuliita jina la mumewe.

Wednesday, July 13, 2022

Mike Sonko Kugombea Ugavana Mombasa, Mahakama Yampa Ruhusa

Mahakama ya juu imefutilia mbali uamuzi wa Tume Huru ya Uchaguzi (IEBC) na afisa mkuu wa tume hiyo katika kaunti ya Mombasa wa kumzuia liyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko kuwania nafasi ya ugavana kaunti ya Mombasa.

 UGC Mahakama pia imeagiza afisa wa uchaguzi wa Kaunti na IEBC kukubali karatasi za uteuzi wa Sonko. Mahakama hiyo ya majaji watatu wakiongozwa na Stephen Githinji iliamua kwamba Sonko anastahili kwa mujibu wa katiba kuwania ugavana Mombasa.

MBUNGE SALIM ALMAS AMALIZA CHANGAMOTO YA MAJI NAKAFURU - KATA YA LUPIRO ACHIMBA VISIMA 5 WANANCHI KICHEKO

 



MBUNGE wa Jimbo la Ulanga (CCM) Mhe Salim Alaudi Hasham ametatua  ya changamoto ya miaka mingi ya kukosa maji safi na salama kwa wananchi wa kijiji cha Nakafuru kata ya Lupiro wilayani Ulanga ambapo kwa sasa wakazi wake wananufaika na huduma hiyo

Wananchi hao walimuomba mbunge wa Jimbo hilo awatatulie changamoto hiyo kwani ni adha kubwa jambo linalopelekea kina mama na watoto kuteseka kufuata maji kwa umbali mrefu na wakati mwengine kunywa maji yasiyo salama jambo linalohatarisha maisha yao kwani Afya zao zinakuwa matatani.

Mbunge huyo baada ya kusikia kilio hicho akatoa kiasi cha Shilingi milioni 2.5 kwaajili ya uchimbaji wa visima vitano na utengenezaji wa miundombinu ya bomba ili maji yapatikane kwa uhakika bila changamoto.

Zoezi la uchimbaji wa visima limekamilika na mapema katibu wa mbunge wa jimbo hilo Ndugu Thomas Justice Daffa amewakabidhi wananchi visima hivyo na kuwataka wavitumie kwa umakini kwa kuvitunza ili viwasaidie kwa muda mrefu.

Visima hivyo vilivyochimbwa na kampuni ya Msabi pia vitakuwa nanutaratibu wa kufanyiwa matengenezo mara kwa mara na kampuni hiyo ili kuhakikisha wananchi wa eneo hilo hawakosi maji safi na salama wakati wote.

Baada ya kukabidhiwa visima hivyo wananchi wa eneo hilo walimshukuru mbunge kwa msaada huo mkubwa kwani kilio hicho kilikuwa cha miaka mingi na walimuomba aendelee na moyo hio wakuwasikiliza wananchi wake na kuwatatulia changamoto zao zinazowakabili.

Penye mafanikio hapakosi changamoto wanachi hao baada ya kupata maji wakaendelea kumuomba mbunge awapambanie kupata umeme wa uhakika katika baadhi ya vitongoji vyao ambavyo havijafikiwa na umeme jambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo kwani wanashindwa hata kufanya biashara ndogo ndogo kwa kukosa huduma hiyo.

Katibu wa Mbunge Ndugu Thomasi Justice Daffa kwaniaba ya mbunge aliwaahidi kulibeba swala hilo na kulisimamia kidete ili nishati hiyo muhimu iwafikie wananchi wote wa nakafuru.

Tuesday, July 12, 2022

MBUNGE DR KABATI NA MNEC MTEWELE WAUNGANA KUPINGA UKATILI KWA WAELEMAVU IRINGA.

 

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa viti kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa viti kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa vifaa kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
 Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele na Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati wakizundua mchezo wa mpira wa kikapu wakati wa kongamano la watu walemavu mkoani Iringa

Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele na Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati wakizundua mchezo wa mpira wa kikapu wakati wa kongamano la watu walemavu mkoani Iringa


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wameungana kwa pamoja kupinga ukatili wa kijinsia hasa kwa watu wenye ulemavu mkoani Iringa na Tanzania kwa ujumla.

Akizungmza wakati wa Kongamano maalum lililolenga kupinga ukatili wa kijinsia pamoja na kutoa elimu ya Sensa ili kuwajengea uelewa na kujitokeza kuhesabiwa katika zoezi la Sensa linalotarajiwa kufanyika Mwezi nane Mwaka huu,MNEC Mtewele alisema kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia mkoa wa Iringa yamekuwa yakitokeza mara kwa mara hivyo ni lazima kuyakomesha matukioa hayo.

MNEC Mtewele alisema kuwa wananchi wa Iringa wanapaswa kutambua madhara yanayotokana na ukatili wa kijinsia kwa jamii husika kwa kuwa kumfanyia mtu ukatili ni jambo ambalo halikubariki katika jamii yoyote ile ya kitanzania.

Alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa Mkoa huo unaongoza kwa ukatili wa kijinsia na kwamba jamii yote hususani wakazi wa Mkoa huo wanapaswa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali katika kutokomeza vitendo hivyo kama anavyofanya Mbunge Kabati.

“Ni aibu sana na fedheha kwa mkoa wetu kuongoza katika vitendo vya ukatili wa kijinsia, tunapaswa kupiga vita kwa nguvu zetu zote na mtu akikutwa na hatia ya kuhusishwa na vitendo hivi anapaswa kuchukuliwa hatua kali hata kufungwa maisha” alisema MNEC Mtewele huku akionesha kukasirishwa na vitendo hivyo.

katika hatua nyingine amezungumzia umuhimu wa watu wenye ulemavu kushiriki katika Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika mwezi wa nane mwaka huu na kuhimiza kuhesabiwa kwa watu wenye ulemavu na kwamba zoezi hilo  litaifanya Serikali kutambua idadi ya watu hao na hivyo kupata huduma kwa urahisi kutokana na mahitaji yao na maeneo walipo.

“Ndugu zangu naomba sana kuhamasisha wazazi na walezi kuhakikisha watu wote wenye ulemavu tulinao majumbani wanahesabiwa, usimfiche mtu mwenye ulemavu kwani kwa kufanya hivyo utaifanya Serikali kukosa idadi yao na hivyo kushindwa kuwafikia kuwapatia huduma zao wanazostahili” amesisitiza MNEC Mtewele

 

MNEC Mtewele alimazia kwa kumpongeza Mbunge Ritta Kabati kwa hatua yake ya kusaidia watu wenye mahitaji maalum na kwamba kwa kufanya hivyo anaunga mkono jitihada za Serkali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia na vitendo vya ukatili hasa kwa watoto na walemavu.


Awali akizungumza wakati wa kongamano hilo mbunge DR Ritta Kabati alisema kuwa  imekuwa ni ndoto na kiu yake ya muda mrefu pia imetokana na kushuhudia changamoto nyingi wanazokumbana nazo watu wa makundi maalum hususani wenye ulemavu, wazee, watoto, yatima na  wanawake ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri a Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan za kupinga ukatili wa Kijinsia.

 

Mgeni Rasmi kutokana na changamoto hizo nilianza
kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha napunguza au kuondoa changamoto hizo kabisa” alisema DR Kabati

Alisema kuwa amekuwa akiuliza mara kwa mara maswali na hoja zinazohusu watu wenye Ulemavu Bungeni ili kutafuta ufumbuzi ikiwemo mabadiliko ya kisheria na sera mbalimbali kuendana na mazingira yao.


Dr Kabati alisema kuwa aliamua kuanzisha kampeni maalum ya kusaidia vifaa saidizi ikiwemo fimbo, basikeli, mafuta na hata kuboresha miundombinu katika baadhi ya maeneo ili wasikutane na changamoto hiyo.

Aidha, ameongeza kuwa baada ya kuona hali ya uhitaji katika jamii ni kubwa, aliamua kuanzisha Taasisi maalum ya kushughulikia changamoto zinazowakabili  watu waliopo kwenye makundi maalum inayoitwa RITTA KABATI TRUST FUND, ambayo itajihusisha moja kwa moja kutafuta ufumbuzi wa changamoto za watu wenye mahitaji maalum kwa kuwafuata kwenye maeneo yao na kuwatambua ili kufanya uratibu wa kuwasaidia.

“Taasisi hii inalenga Kukuza utu na heshima kwa watu wenye ulemavu na kutoa ushauri wa matibabu bila malipo kwa walemavu pamoaja na kusaidia miradi na shughuli nyingine za kiuchumi zinazoendeshwa na watu wenye ulemavu” alisema DR Kabati.

Aidha amebainisha kuwa kazi nyingine ni kuanzisha na kudumisha vituo vya walemavu ili kusaidia
jamii na kujihusisha katika michezo hususani ya watu wenye ulemavu kwa k
uanzisha mashindano mbalimbali ya michezo na burudani katika Mkoa wa Iringa. 

Kazi nyingine ni pamoja na kusaidia programu na mipango inayolenga kuwaelimisha na kwafahamisha wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu kuhusu changamoto mahususi zinazowakabili watoto wenye ulemavu na jinsi ya kuwatunza.

TANGA UWASA YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA AJILI YA MASHINDANO YA UMITASHUMTA

 

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kulia akikabidhi vifaa vya michezo vyenye thamani ya milioni 2 kwa Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kasim Kaonekana kwa ajili ya michezo ya Umitashumta iliyoanza leo kwenye shule ya Sekondari Tanga School
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kulia akikabidhi vifaa vya michezo vyenye thamani ya milioni 2 kwa Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kasim Kaonekana kwa ajili ya michezo ya Umitashumta iliyoanza leo kwenye shule ya Sekondari Tanga School
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly wa tatu kutoka kushoto na Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kasim Kaonekana wa tatu kutoka kushoto wakiwa jezi za traki suti vyenye thamani ya milioni 2 kwa kwa ajili ya michezo ya Umitashumta iliyoanza jana(juzi) kwenye shule ya Sekondari Tanga School

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kulia akikabidhi vifaa vya michezo vyenye thamani ya milioni 2 kwa Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kasim Kaonekana kwa ajili ya michezo ya Umitashumta iliyoanza leo kwenye shule ya Sekondari Tanga School


Na Oscar Assenga,TANGA.

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) imetoa vifaa vya michezo vyenye thamani ya Milioni 2 kwa ajili ya michezo ya Umitashumta kwa wanafunzi wa Jiji la Tanga inayoanza leo kwenye shule ya Sekondari Tanga School ili kuhakikisha michezo hiyo inafanyika kwa tija kubwa.

Halfa ya makabidhiano ya vifaa hivyo ilifanyika leo kwenye ofisi za Mamlaka hiyo ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly alimkabidhi Afisa Elimu Msingi wa Jiji hilo Kasimu Kaoneka kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Tanga.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Hilly alisema wameamua kutoa msaada huo wa vifaa vya michezo ili kuweza kuunga mkono mashindano hayo.

Alisema wao Tanga Uwasa kama wadau wa elimu wanatambua umuhimu wa michezo katika elimu kwa ajili ya wanafunzi ili waweze kupata afya nzuri na kuweze kusoma vizuri  kwa hiyo wamechangia katika kuhakikisha michezo hiyo inafanikiwa na wanafunzi wanafurahi.

Alisema wanatambua kuwa mazingira bora yanasaidia kuwa na elimu bora licha ya kuchangia michezo lakini wanachangia ujenzi wa madarasa na viti vingine ili kutenegenza mazingira mazuri ya elimu.

Awali akizungumza wakati akipokea vifaa hivyo Afisa Elimu Msingi wa Jiji la Tanga Kasimu Kaoneka ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Spora Liana alisema kwamba michezo ni kitu muhimu kwa wanafunzi kwani wanaenda shuleni kupata taaluma lakini sio taalima tu ni pamoja na michezo ambacho ni kivutio kimojawapo kina mfanya mwanafunzi aweze kwenda shuleni.

Alisema  na hivyo kupitia michezo atapata na taaluma yake na hivyo anasisimua ubongo wake hatua inayopelekea kitu anachofundishwa anakipata  kwa sababu mwili unakuwa upo imara na timamu kiakili.

“Tunawashukuru Tanga Uwasa kwa kutupatia vifaa hivi vya michezo na tunahaidia kwamba tutahakikisha tunaleta vikombe vingi na tutawakaribisha wakati wa kukabidhiwa”Alisema

Hata hivyo alisema michezo hiyo ngazi ya Kanda inaanza leo ambapo itahusisha wilaya za Mkinga,Pangani,Muheza na Tanga na yanafanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Tanga School

Naye kwa upande wake Kasimu Issa anayesoma Darasa la saba shule ya Msingi majani mapana alisema wanashukuru kwa msaada huo wa vifaa hivyo kuhakidi kwenda kufanya vizuri kwenye mashindano hayo.

DC KISWAGA ATUMIA MCHEZO WA BAO KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUHESABIWA SIKU YA SENSA.

 


Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akiongea na wananchi kuhusu umuhimu wa SENSA ya watu na makazi kwa wananchi wa Tarafa ya Pawaga
Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akikabidhi zawadi kwa mshindi wa mchezo wa bao na kuongea na  wananchi kuhusu umuhimu wa SENSA ya watu na makazi kwa wananchi wa Tarafa ya Pawaga
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kucheza mchezo wa bao mbele ya 
mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga juu ya umuhimu wa SENSA ya watu na makazi
Baadhi ya wananchi waliojitkeza kumsikiliza mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga juu ya umuhimu wa SENSA ya watu na makazi

 

 Na Fredy Mgunda,Iringa.

 

WANANCHI wa wilaya ya Iringa wametakiwa kujitokeza kuhesabiwa siku ya SENSA ili kutengeneza taswira halisi ya serikali kujua idadi ya wananchi kwa lengo la kutafuta namna bora ya kuwapelekea maendeleo wananchi kulingana na idadi iliyopo kila eneo.

 

Akizungumza wakati wa sikuku za sabasaba mkuu wa wilaya ya Kahama,Festo Kiswaga alisema kuwa wananchi watakiwa kujitokeza siku SENSA ili waweze kuhesabiwa kwa ajili ya maendeleo yao.

 

Kiswaga aliwata viongozi mbalimbali kutumia fursa ya uwepo wa michezo kwenye vijiji,mitaa,kata na tarafa kuhamasisha wananchi wajitokeze kuhesabiwa.

 

Alisema kuwa kwenye kila mchezo kunakuwa nakundi kubwa la wananchi hivyo ni rahisi sana kufikisha ujumbe wa SENSA na ujumbe ukapokelewa vizuri.

 

Kiswaga alisema kuwa mchezo wa Bao la solo limekuwa kiunganishi kikubwa kwa wananchi na serikali kama ambavyo hayati mwalimu Nyerere alitumia mchezo huo katika harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika na kufaulu kuupata uhuru huo.

 

Hivyo michezo yote inatakiwa kupewa kipaumbele sawa ili kuiweka jamii ya wanamichezo pamoja na kutumia fursa za michezo kwa maendeleo ya taifa.

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa vijana wilaya ya Iringa vijijini,Makala Mapesa alisema kuwa mchezo wa bao la solo ni mchezo ambao unachezwa na watu wa lika zote kwa ajili ya fursa na kutengeneza fursa za kimaendeleo wakiwa wanacheza mchezo huo.

 

Mapessa alisema kuwa mchezo wa bao la solo umekuwa moja ya michezo ambayo unatakiwa kutumia akiri nyingi na maarifa kuliko kutumia nguvu hivyo ukicheza mara kwa mara mchezo huo akili yako itachangamka kwenye kufikiri.

 

Aliowamba vijana kuucheza na kuenzi mchezo huo wa kitamaduni kwa kuondoa dhana ya kuwa mchezo huo ni wawazee tu na sio mchezo wa vijana.

 

 

 

Monday, July 11, 2022

MSICHANA ANG’ATWA SIKIO NA BABA WA KAMBO AKIMNUSURU MAMA YAKE KATIKA KIPIGO


CHANZOKonzi La Moyo TV Show

Msichana wa Miaka 25 Mkazi wa Buswelu Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza (jina tunalihifadhi) amejikuta akipoteza sikio Katika harakati za kumnusuru Mama yake mzazi aliyekuwa akipigwa na Baba yake wa Kambo. 

Hayo yametokea tarehe 09.07.2022 Siku ya Jumamosi saa Saba usiku  ambapo mwanaume huyo (jina tunalihifadhi) alisadikika kumpiga Mkewe ambaye amejifungua kwa upasuaji Siku sio nyingi kisa kikiwa wivu wa mapenzi.


Msichana huyo akiongea na Konzi la Moyo amesema Katika kuamua ugomvi huo alivamiwa na Baba huyo na kung’atwa siko lake la kulia huku akimtuhumu kuingilia mambo yasiyomhusu. 

Mwanaume huyo amefikishwa kituo cha polisi Kirumba kwa hatua za kisheria. Konzi la Moyo TV Show tutaendelea kukuletea mwendelezo wa taarifa hii. Unaweza ukatoa taarifa ya ukatili kwa namba 116 au piga namba 0736975666 uzungumze na Wataalamu wa elimu nafsi kwa msaada wa UShauri BURE.

WAZIRI MCHENGERWA AMWAKILISHA RAIS SAMIA MSIBA WA BI.HINDU

 

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe,  Mohamed Mchengerwa wa pili kutoka kushoto akiwa msibani na waombolezaji wengine




Na John Mapepele

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia  Suluhu Hassan leo Julai 10, 2022 ametoa salamu za rambirambi kwenye msiba wa  msanii  mkongwe wa Filamu nchini Chuma Seleman maarufu kama Bi. Hindu.

Salamu hizo zimetolewa kwa niaba yake na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe,  Mohamed Mchengerwa Magomeni jijini Dar es Salaam  nyumbani kwa marehemu kabla ya kwenda kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.

Akimzungumzia marehemu, Mhe. Mchengerwa amesema, Mhe. Rais amemwelezea   Bi. Hindu kuwa ni msanii aliyetoa mchango mkubwa katika tasnia ya Sanaa hapa nchini.

"Bi Hindu ametoa  elimu ya sanaa kwa wasanii wengi sana, Serikali inatambua mchango wake. Mhe Rais amepokea msiba huu kwa msiba huu kwa mshituko mkubwa". Amefafanua Mhe, Mchengerwa

Aidha, amesema marehemu Hindu amefariki wakati Serikali inafanya mapinduzi makubwa  katika sekta za Sanaa.

Katika msiba huo Katibu Mwenezi wa CCM komrade Shaka na viongozi mbalimbali wa Serikali, Michezo na Sanaa wamehudhuria.