ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 4, 2015

MVUA YASABABISHA KUAHIRISHWA KWA MECHI YA KAGERA Vs SIMBA DIMBA LA CCM KAMBARAGE

 NA ALBERT G SENGO: SHINYANGA

Kufuatia mvua kubwa kunyesha kwa takribani siku mbili mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania bara baina ya Kagera Sugar dhidi ya Simba Sports Club uliokuwa uchezwe kwenye dimba la CCM Kambarage mjini Shinyanga umeahirishwa hadi siku ya jumatatu. BOFYA PLAY KUJUA KILICHOJIRI
Kutuama kwa maji hasa katika maeneo muhimu kwenye magoli ya pande zote mbili ndiyo sababu kuu kwa mwamuzi aliyepangwa kwa mchezo huo Erick Anock kutoka Arusha kusimamisha mchezo huo na kushauriana na kamati husika kisha mchezo kuahirishwa.
Hali katika moja ya lango uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga kufuatia mvua zilizonyesha kwa takriban siku mbili na leo siku iliyopangwa kwa kipute..
Hata mzunguko wa uwanja uko katika hali tete ya tope.
Hata mzunguko wa uwanja uko katika hali tete ya tope.
Kutoka jukwaa kuu na eneo la katikati ya uwanja.
Lango la kaskazini.
Hali halisi dimbani.
Benchi la Simba liko nusu wengine wakitafakari kujumuika.
Kutoka jukwaa kuu muonekano wa uwanja wa Kambarage.
Kufuatia kufariki kwenye ajali ya basi iliyotokea katika eneo la Mkundi nje kidogo ya mji wa Morogoro mnamo April 3 mwaka huu (2015), wanachama saba (7) wa Klabu ya Simba ya Dar es salaam kutoka tawi la Mpira na Maendeleo maarufu kama Simba UKAWA ambalo limewahi kutangazwa kufutwa wakafariki dunia, huu ndiyo ujumbe wa mashabiki wenzao wa Simba tawi la Terminal.
Mashabiki wa Simba tawi la Terminal katika picha ya pamoja ndani ya dimba la CCM Kambarage mara baada ya mchezo kuahirishwa leo.
Mazingira ya nje ya uwanja wa CCM Kambarage hii leo.

NGUMI KUFANYIKA MKWAKWANI TANGA MEI 2

Bondia Alen Kamote wa Tanga atapanda uringoni mei 2 katika uwanja wa mkwakwani tanga kukabiliana na Emilio Norfat katika mpambano wa raundi 12 mbali na mpambano uho siku hiyo pia kutakuwa na mapambano mengine makala moja ya mpambano wenye mvuto zaidi ni kati ya bondia mwenye makazi yake mkoa wa Morogoro Cosmas Cheka atakaekabiliana na Said Mundi kutoa mkoa wa tanga
 
Promota wa mpambano uho Ally Mwazoa aliongeza kwa kusema mbali na mapambano hayo kutakuwa na mapambano mengine yatakayowakutanisha  Jacobo Maganga na Fadhili Kea wakati Juma Mustafa akipamana na Ally Magoma uku Saimon Zabroni akioneshana umwamba na Hamisi Mwakinyo na Jumanne Mohamed na Bakari Shendekwa na Zuber Kitandura na Rajabu Mahoja

Mpambano uho unafanyika mkoa wa tanga baada ya kutopata burudani ya mchezo wa masumbwi kwa kipindi cha mda mrefu kidongo hivyo mpambano uho utafuraiwa na wakati wa Tanga na vitongoji vyake

Siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.
 

WAANDAMANA DHIDI YA AL-SHABAAB GARISSA.

Maandamano Garissa.

Wananchi wa mji wa Garissa nchini Kenya wamefanya maandamano kupinga vitendo vya kundi la Al Shabaab, lililoshambulia chuo kimoja kikuu mjini humo na kuwaua watu 147 wengi wao wakiwa wanafunzi hapo jana.
Waandamanaji pia wameelezea kutoridhika na vyombo vya usalama nchini humo wakisema havikuchukua hatua za kutosha kutoa ulinzi kwa waliouawa na kwa raia wengine kwa jumla.
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu cha Garissa wamekuwa wakiendelea kuwasili katika eneo hilo kuitambua miili ya wapendwa wao.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu .
Garissa.
Serikali ya Kenya imekuwa ikiwasafirisha manusura wa shambulio hilo kwa mabasi kuelekea makwao huku miili ya waliouawa ikisafirishwa mjini Nairobi.
Wakati huo huo rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, amesema Somalia na Kenya zinafaa kuimarisha uhusiano wao katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Tamko hilo linajiri siku moja baada ya shambulio hilo la Alshaabab katika chuo kimoja kikuu mjini Garrisa.CHANZO: BBC SWAHILI

PADRI AUDAX KAASA AONGOZA IBADA KATIKA KANISA LA MTAKATIFU JOSEPH DAR ES SALAAM

 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali  Pengo, akiubusu msalaba, wakati wa Ibada ya Ijumaa Kuu katika   Kanisa la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam,  Katikati aliyeshikilia msalaba huo  ni Padri Audax Kaasa wa kanisa hilo.(PICHA ZOTE  NA KHAMISI MUSSA)
 Mtoto Benedicta Mushi, ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Masaka English Medium  akiubusu msalaba, wakati wa Ibada ya Ijumaa Kuu,  kulia kwa mtoto huyo ni Baba mzazi Philip Mushi
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernad Membe, akikomunika Ekaristi Takatifu  katika Kanisa  Kuu Katoliki  la Mt. Joseph Dar es Salaam
Meneja Miradi Jimbo la Mtama Wilaya ya Lindi, Paul Maokola akibusu mkono wa  Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali  Pengo,  wakati wa Ibada ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam  kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Mtama, mkoani  Lindi  Bernad Membe

Friday, April 3, 2015

JEMBE FM YAPANIA KUWA SEHEMU YA UCHANGIAJI KATIKA UKUAJI WA MAENDELEO YA JIJI LA MWANZA

Mkurugenzi wa Mtedaji wa Jembe ni Jembe ambaye ni mmiliki wa Jembe FM Radio, Dr. Sebastian Ndege, kwa mara ya kwanza hii leo amezungumza na wakazi wa mkoa wa Mwanza kupitia masafa mapya ya 93.7 Jembe FM kuwakaribisha kuwa sehemu ya familia ya redio hiyo sanjari na kuelezea mipango na mikakati ya kituo hicho. 
Dr. Ndege amesema kuwa Jembe FM imepania kuwa sehemu ya uchangiaji wa ukuaji wa maendeleo ya jiji la Mwanza lenye hazina za kitalii, uvuvi, madini na sekta mbalimbali za uchumi, viwanda biashara kwa kuhakikisha inapenya kihabari na kuainisha changamoto mbalimbali za jamii husika ikiwa ni sambamba na kutoa ushauri kwa nini kifanyike. ZAIDI BOFYA PLAY KUSIKILIZA YALIYOJIRI TANGU AWALI KUPITIA JEMBE FM.

Mkurugenzi wa Mtendaji wa Jembe ni Jembe ambaye ni mmiliki wa Jembe FM Radio, Dr. Sebastian Ndege (kulia) akitambulishwa hewani na moja kati ya watangazaji wa kituo hicho Timoth Ngalula (kushoto). 
Mtangazaji Timoth Ngalula akiendelea kufanya yake at the same time 'Casmir Jembe' akiiba upicture ndani ya 93.7
Kutoka Jembe DjZ ni Dj K-Flip ndiye aliyekuwa akifanya makamuzi. 
Jembe na producer Okeleky.
Kutoka Jembe DjZ ni 
Mikakati mipango na mifano yenye uhalisia.....Dah... watu kwi-kwi-kwi...
Very interesting.....ingawa picha za tukio hili zilipigwa kwa kutumia kamera zisizo na sauti.
Mfano kwa dhati...
Jembe DjZ wamekubali mada.
Wasikilizaji wa kwanza kupiga simukupitia 93.7 Jembe Fm Mwanza ambao walijizawadia zawadi mbalimbali ikiwemo Tshirt za JEMBEKA complimentary za kutinga Jembe Beach katika kusherehekea sikukuu ya Pasaka ambapo msanii wa Bongo Fleva Young Dee sanjari na JJ Band watakisanukisha siku hiyo. Kutoka kushoto ni Alex Richard mkazi wa Kirumba Mwanza, baada ya Dr. Jembe ni Regan Regan Robert mkazi wa Kabuholo Kirumba Mwanza na George Lucas mkazi wa Nyamanolo Mwanza.
Sasa ni wakati wa kula bata @jembenijembe Instagram.
Washkaji wametoka Arusha hadi Mwanza 'KUJEMBEKA' kutoka kushoto ni Fredy Materu, George Albert, Ray, na Bonny wakiwa na rubani wao 'Casmir Jembe' pale kati.
Another one.

MH. LOWASSA KATIKA IBADA YA IJUMAA KUU LEO

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwa ameungana na Waumini wengine katika Ibada ya Ijumaa Kuu ya Pasaka iliyofanyika kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Azania Front la Dar es Salaam leo.
Ibada ikiendelea.
Sehemu ya Waumini wa Kanisa la KKKT Azania Front jijini Dar es Salaam, wakiwa kwenye Ibada ya Ijumaa Kuu leo.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akiongoza Ibada ya Ijumaa Kuu ya Pasaka iliyofanyika leo.

Igizo la Yesu likiongozwa na Bw. Moses Kombe alivyokuwa na wanafunzi wake kabla ya kuteswa hadi kutungikwa msalabani, wakati wa ibada ya Ijumaa Kuu ya Pasaka kwenye Kanisa la KKKT Azania Front jijini Dar es Salaam leo.
Mh. Edward Lowassa akifatilia igizo la mateso ya Yesu, lililoigizwa na Umoja wa Kwaya zote za Usharika wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani.
Igizo likiendelea.
Mmoja wa watoto waliokuwepo Kanisani hapo akiangalia Igizo hilo.
Mmoja wa Waigizaji hao.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akipitia vifungu vya Biblia wakati Igizo la Yesu likiendelea.
Yesu akipelekwa kwa Pilato.
Vijana hao wakiigiza pale Yesu alipofikiswa kwa Pilato kuhukumiwa, wakati wa ibada ya Ijumaa Kuu ya Pasaka kwenye Kanisa la KKKT Azania Front Dar es Salaam
Huzuni ilitawala wakati wa Igizo hilo.
Yesu akiwa amebebeshwa Msalaba katika Igizo hilo.
Muumini wa Kikristo, Moses Kombe akitungikwa msalabani kama Yesu katika igizo lililofanywa na Vijana wa Umoja wa Kwaya zote za Usharika wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Azania Front, Jijini Dar es salaam, wakati wa ibada ya Ijumaa Kuu leo.
Kuna waliomlilia na Wengine kufurahia.