ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 12, 2022

MBUNGE MWENYE TUHUMA YA MAUAJI AJISALIMISHA POLISI KENYA.

Mbunge wa Kimilili DIdmus Barasa amejisalimisha kwa polisi baada ya kuwa mafichoni kwa siku mbili.

Barasa alijipeleka katika kituo cha polisi cha Bungoma Ijumaa Agosti 12 asubuhi kuhusiana na kisa cha mauaji. 

Alhamisi Agosti 11 polisi walitoa makataa ya saa sita kujisalimisha katika kituo chochote cha polisi. Mkurugenzi wa DCI Georhge Kinoti alisema Barasa atahojiwa kuhusiana na kifo cha msaidizi wa mpinzani wake Brian Olunga. 

Kinoti alikuwa ametoa onyo pia kwa yeyote ambaye anamficha Barasa aksiema kuwa atachukuliwa hatua madhubuti. 

"Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mtu yeyote ambaye atapatikana amekuwa akimficha mshukiwa huyo wa mauaji," Kinoti alisema Aidha kikosi maalum kilikuwa kimeundwa kumsaka Barasa tangu aingia mafichoni baada ya kuripotiwa kumpiga risasi Olunga. 


DC MOYO :ZAIDI YA WANANCHI 48, 434 WAMEJITOKEZA KUCHANJA CHANJO YA UVIKO 19

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akishuhudia baaadhi ya wananchi wa wilaya hiyo wakipata chanjo ya UVIKO 19 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kuchanja inayoendelea nchini nzima.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akishuhudia baaadhi ya wananchi wa wilaya hiyo wakipata chanjo ya UVIKO 19 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kuchanja.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na baaadhi ya wananchi wa wilaya hiyo wakati wa kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya UVIKO 19 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kuchanja inayoendelea nchini nzima.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akishuhudia baaadhi ya wananchi wa wilaya hiyo wakipata chanjo ya UVIKO 19 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kuchanja.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akishuhudia baaadhi ya wananchi wa wilaya hiyo wakipata chanjo ya UVIKO 19 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kuchanja.

 

Na Fredy Mgunda,Iringa.

 

ZAIDI ya wananchi 48,434 wa wilaya ya Iringa wamefanikiwa kuchanja chanjo ya UVIKO 19 kwa lengo la kuendelea kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Colona ambao umeshasababisha vifo vingi vya wananchi wa wilaya hiyo.

 

Akizungumza wakati wa kampeni ndogo ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kuchanja chanjo ya UVIKO 19, Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa hadi kufikia tarehe 26/7/2022 walikuwa wamewafikia jumla ya wananchi 48,434 ambao wamepata chanjo ya UVIKO 19 dozi ya pili ya chanjo ya Janssen ambayo ni sawa na asilimia 39.24 ya walengwa 123,418.

 

Moyo alisema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha wananchi waliokuwa na miaka 18 na kuendelea waweze kupata chanjo ya UVIKO 19 katika kipindi cha kampeni ndogo inayoendelea hivi sasa katika wilaya ya Iringa.

 

Alisema kuwa kwa sasa wilaya ya Iringa imetenge jumla ya vituo 79 vinavyotoa huduma za chanjo pamoja na zoezi la uchanjaji katika vituo watoa huduma wanaotumia huduma za mkoba ili kuwafikia wananchi popote walipo.

 

Moyo alisema kuwa viongozi wa serikali, taasisi mbalimbali kama shule,vyuo, viongozi wa bajaji, daladala,bodaboda,saluni,vikoba, viongozi wa dini,siasa wadau wa afya,wazee mashuhuri na wazee wa kimila kuhakikisha wanashirikiana na serikali ya wilaya ya Iringa kuhamasisha jamii ili iweze kupata chanjo ya UVIKO 19.

Alisema kuwa wataalamu wa afya na jamii wanapaswa kupongezwa kwa namna ambavyo wamekuwa wanalishughulikia suala la kitaifa kwa kuwa inaonyesha kwa namna gani wanavyojitoa kutoa elimu kwa wananchi hadi wanachanja kwa hiyari chanjo ya UVIKO 19.

 

Moyo alisema kuwa anatarajia wananchi ambao hawajapata chanjo ya UVIKO-19 watashiriki kupata chanjo hiyo ambayo inaendelea kutolewa na wataalamu wa afya.

 

“Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiwaasa wananchi kushiriki kupata chanjo ya UVIKO-19 kwani maradhi hayo bado yapo nchini hivyo tushiriki kupata chanjo ya UVIKO-19,” amesema.

  

Moyo amesema baada ya maneno ya uongo na dhana potofu kuonekana kuwa ni propaganda zisizo na maana yoyote, wananchi wameamua kushiriki chanjo ya UVIKO-19 kwa manufaa yao.

 

“Mara nyingi kitu kigeni kikitokea kuna baadhi ya watu wanapotosha na kuzungumza ndivyo sivyo juu ya jambo hilo utadhani wanalitambua kumbe hawafahamu ila hili la UVIKO-19 wengi wao wamelitambua na kulielewa ndiyo sababu wamejitokeza kwa wingi kuchanja,” anasema Moyo

 

Mkazi wa kata ya Magulilwa John mwigane anasema wataalamu wa afya wamekuwa wanafika hadi vijijini na kutoa elimu kwa jamii kIsha kuwapatia chanjo hiyo ya UVIKO-19.


“Hadi hivi sasa elimu inaendelea kutolewa kwa jamii huku vijijini na wanaitikia ushauri wa kupatiwa chanjo ya UVIKO-19 kwani wanatambua kuwa ukipata maradhi hayo bila kuchanja utapata matatizo makubwa kwenye changamoto ya kupumua pindi ukiupata ugonjwa huo,” anasema.

 

Mkazi wa kijiji cha Ndiwili Hamisa Malima anasema kuwa viongozi na wananchi wa Wilaya ya Iringa kwa pamoja wameungana katika kuhakikisha wanapata chanjo ya UVIKO-19 ndiyo sababu ya wananchi kujitokeza kuchanja chanjo ya UVIKO 19.

 

“Mtu anaona atapata maambukizi ya UVIKO-19 yeye mwenyewe na hayo ni maradhi ambayo hayana matibabu hivyo ameona hawezi kupata tatizo kisa kutochanjwa kwa kutosikiliza wataalamu wa afya na kuwasilikiza wazushaji,” anaeleza

 

Hivi karibuni Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza hivi karibuni kwenye tamasha la MZIKI MNENE lililofanyika uwanja wa Nangwanda Mkoani Mtwara amesema imethibitika kuwa njia ambayo ni salama ya kujikinga na ugonjwa wa UVIKO-19 ni kupata chanjo kwani ukichanja utakuwa umejikinga na kuikinga jamii ya watanzania.

 

Waziri Ummy amesema Serikali inaendelea kuwalinda wananchi wake katika maambuzi ya magonjwa mbalimbali kwa kutoa chanjo ikiwemo ya UVIKO-19.

 

“Sisi kama Wizara ya Afya tutatumia mbinu mbalimbali ambazo zitakazowafikia wananchi kama tunavyotumia matamasha haya kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kupata huduma ya chanjo ya UVIKO-19,” anamaliza kwa kusema Waziri Ummy.

Raphael Tuju Asifia Matokeo ya Raila Mlima Kenya "Yuko Tayari Kumrithi Uhuru"


Afisa Mkuu Mtendaji wa Azimio La Umoja, Raphael Tuju amesema kuwa muungano huo ulifurahishwa na matokeo ya kura ya Raila Odinga katika eneo la Mlima Kenya. 

Tuju alishikilia kuwa Raila na mgombea mwenza wake, Martha Karua, walifanya vyema sana katika eneo linalotawaliwa na United Democratic Alliance (UDA).

 Alieleza kuwa matokeo hayo yalionyesha kuwa Raila bado ana uzito katika eneo hilo licha ya muungano wa Kenya Kwanza unaohusishwa na Naibu Rais William Ruto kujinyakulia kura nyingi. 

Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Chama cha Jubilee alionyesha imani kuwa kutokana na matokeo hayo Raila yuko tayari kumrithi Rais Uhuru Kenyatta. 

"Tuna matokeo ya wale waliompigia kura Raila, bora zaidi kuliko ilivyokuwa miezi sita iliyopita au mwaka mmoja uliopita.La muhimu ni kwamba amefanya vyema sana, na tunatarajia habari njema na jukumu langu hapa Bomas kuhakikisha kila kitu kinaendelea vyema," Tuju aliongeza. 

Tuju pia alipongeza vyombo vya habari kwa kuonyesha matokeo tofauti, akibainisha kuwa inasaidia kuweka chombo cha uchaguzi kinachoongozwa na Wafula Chebukati kudhibiti. "Nadhani ni maendeleo chanya kwamba vyombo vya habari vilishiriki katika mchakato huu wa kisiasa wa uchaguzi. Lakini tunapaswa kufahamu kwamba kuna vikwazo," Tuju aliongeza. 

Ruto avuna zaidi Maoni yake yanakujia baada ya matokeo yaliyotolewa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuashiria kuwa kiongozi wa Chama cha Narc Kenya Martha Karua alifedheheshwa nyumbani kwake kaunti ya Kirinyaga baada ya chama cha United Democratic Alliance (UDA), unaoongozwa na mgombea urais wa Kenya Kwanza William Ruto kunyakua viti vyote vya ubunge.

Vyama vinavyohusishwa na muungano wa Azimio ya Raila Odinga, ambao una Martha Karua kama mgombea mwenza, umeshindwa kunyakua kiti hata kimoja cha ubunge Kirinyaga. Daily Nation linaripoti kwamba wagombeaji wa UDA katika Kirinyaga ya Kati, Gichugu, Ndia na Mwea walishinda viti vyao mtawalia, na kuipa Narc Kenya na vyama vingine vya Azimio fedheha. 

BUMBULI OUT YANGA.

Uongozi wa klabu ya Yanga, umemalizana na Afisa Habari wake Hassan Bumbuli baada ya mkataba wake kwisha.


 

Ocode yawapiga jeki vijana 185 manispaa ya Ubungo kupata mafunzo

Mkurugenzi mtendaji wa. Ocode Joseph Jackson mwenye shati la drafti akizungumza na waandishi wa vyombo mbali mbali vya habari hawapo pichani kuhusiana na jinsi walivyojipanga katika miradi ya kuwasaidia vijana
Naibu meya wa Manispaa ya Ubungo Hassan Mwasha mwenye suti nyeusi ambaye alikuwa mgeni rasmi akifafanua Jambo kwa waandishi mara baada ya kumalizika kwa halfa hiyo.
Mjumbe wa bodi ya Ocode Godfrey Boniventura akieleza namna walivyojipanga katika mradi wa bonga katika kuwasaidia vijana wasikae vijiweni.

Na Victor Masangu.

Katika kuwakomboa vijana  ambao wanashindwa kujiendeleza zaidi  pindi wanapomaliza masomo yao ya shule za msingi na sekondari Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya ya Organization for Community Development (OCODE) imekuja na mpango wa mradi wa pili ujulikanao Kama Bongo lengo ikiwa ni kuwawezesha vijana.


Mradi huo ambao kwa Sasa unatekelezwa katika manispaa ya ubungoJijini Dar es Salaam  umeanzishwa maalumu kwa ajili ya kuweza kuwasaidia vijana wenye kuanzia umri wa miaka 13 hadi 19 ambao walishindwa kuendelea na mfumo rasmi wa elimu.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Ocode Joseph Jackson wakati wa halfa ya mahafali kwa vijana wapatao 193 ambao wameweza kuhitimu baada ya kumaliza masomo yao kutoka Veta na kufanikiwa kujifunza katika fani mbali mbali.


Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa lengo la mradi huo ni kuweka mipango madhubuti ambayo itaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa vijana wa manispaa ya ubungo kuweza kupata fursa ya kujiajiri wao wenyewe na hatimaye kujikwamua kiuchumi.


"Katika mradi huu wa bongo tumejikita zaidi kwa vijana na kwamba una malengo makuu matatu ambayo moja wapo ni kuwapatia watoto fursa ya elimu Bora,lakini pili ni kuwapa vijana stadi mbali mbali za maisha na jambo lingine la tatu ni kuwasaidia vijana katika suala zima la kujikwamua kiuchumi ili wasiwe tegemezi,"alisema Jakson.


Aidha alibainisha kwamba mradi huo wa bonga kwa sasa ni awamu ya pili na kwamba vijana hao walioweza kuhitimu wataweza kuleta chachu ya mabadiliko kutokana na ujuzi na fani mbali mbali ambazo wamezisomea katika chuo Cha Veta.


Kwa upande wake mjumbe wa bodi ya Ocode Godfrey  Boniventura ambaye alimwakilisha Mwenyekiti wa bodi hiyo alibainisha kuwa kati ya wahitimu hao 193 waliomaliza wameweza kujifunza kozi tofauti ikiwemo ushonaji wa nguo.kupika.kupamba,fani ya kutengeneza simu,udereva pamoja na fani nyingine.


Aidha mjumbe huyo aliongeza kwamba katika fani hizo kwa kiasi kikubwa vinagusa maisha ya watu hivyo ana Imani kubwa vijana hao watakuwa mabalozi wazuri katika jamii kwa kile ambacho wamefundishwa na kuwasihi wasibweteke na badala yake waongeze ujuzi na ubunifu zaidi katika kutimiza malengo yao.


Katika hatua nyingine aliwataka kuachana na tabia ya kukaa katika makundi ambayo hayana msaada kwao na badala yake waweze kujiunga kwa pamoja kwa kuongeza thamani ya ujuzi wao ili waweze kupata soko kwa urahisi zaidi.


Naye Naibu Meya wa Manispaa ya Ubungo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo Hassan Mwasha ameipongeza Asasi ya Ocode kwa kuanzisha mradi huo wa kuwasaidia vijana na kuahidi kushirikiana nayo bega kwa bega kwa maslahi ya kuwakomboa vijana.


Pia aliwaasa vijana wote ambao wamebahatika kupata fursa ya mafunzo hayo kutokuwa na vitendo vya kuzagaa vijiweni na badala yake waweze kujiunga katika vikundi lengo ikiwa ni kupatiwa fursa ya mikopo ambayo itaweza kuwasaidia katika kupambana na wimbi la umasikini.


Naibu Meya huyo pia hakusita kuwakumbushia vijana hao kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika zoezi la sensa ya watu na makazi ambalo linatarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu kujitokeza kwa wingi ili serikali iweze kutambua idadi kamili ya wananchi wake.


Asasi ya Ocode imekuwa ikifanya kazi zake mbali mbali katika Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam ambapo imekuwa ikitekeleza miradi ya elimu kwa vijana pamoja na kuboresha maisha ya jamii pamoja na sekta ya michezo.

Thursday, August 11, 2022

NAIBU KATIBU MKUU CCM AMFARIJI MBUNGE WA KWIMBA KIFO CHA MAMAYE

 
Naibu katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara CHRISTINA MNDEME akitia saini kitabu cha maombolezo alipofika nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Kwimba mh.SHANIF MANSOOR  ,ambaye Agosti 6,Mwaka huu alifiwa na Mama yake  MALEKSULTAN MANSOORALI HIRANI,Ambapo Maziko yake yamefanyika Agosti 11,Mwaka huu Jijini Mwanza.
Mbunge wa jimbo la Kwimba mkoani Mwanza mh. SHANIF MANSOOR,(Mwenye suti Nyeusi) Akiwa na familia yake, Akimpokea Naibu katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara,CHRISTINA MNDEME,Alipofika nyumbani kwa Mbunge huyo,Jijini Mwanza Kuhani Msiba wa Mama wa Mbunge huyo,MALEKSULTAN MANSOORALI HIRANI.

RC MGUMBA AWATAKA WAKURUGENZI TANGA KUTOKUTEGEMEA BIASHARA YA VIWANJA

 

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga wakati wa ziara yake aliyoambatana na kujitambulisha kwao  ikiwa ni mara ya kwanza kutembelea wilaya hiyo tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba katika akiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Pili Mnyemaa kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga Kanali Maulid Surumbu wakifuatilia jambo kwa umakini

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za mkoa huo kutotegemea mradi wa uuzaji viwanja kama chanzo cha mapato badala yake waangalie biashara nyingine za kuwekeza.

Aidha, amewataka kuwa na utaratibu wa kuwekeza kwenye miradi ya kiuchumi badala ya kupeleka fedha zote kwenye miradi ya huduma za jamii. 

Mgumba amesema hayo leo Jumatano Agosti 10,  wilayani Mkinga alipokuwa akizungumza na Mkuu wa Wilaya na watendaji wa wilaya hiyo alipokwenda kujitambulisha ikiwa ni mara ya kwanza kutembelea wilaya hiyo tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Akizungumzia suala la viwanja, Mgumba aliwataka wakurugenzi hao kuwa waangalifu katika upimaji wa viwanja kutopima ardhi yenye rutuba kwa mustakabali wa usalama wa chakula.

Pamoja na mambo mengine, Mgumba amepokea taarifa ya mapato na matumizi ya wilaya hiyo na miradi mbalimbali ikiwamo kuanzisha shamba la miche ya mkonge, soko la samaki, eneo la maegesho na mengineyo.

“Mradi wa kuuza viwanja naomba mtoe kwenye orodha ya miradi yenu kwa sababu ni ya muda tu si endelevu na pia muwe makini msipime ardhi yenye rutuba halafu kesho tukikosa chakula tumlaumu Mungu.

“Kama tunataka usalama wa chakula kwa kizazi hiki na kijacho lazima tulinde ardhi yetu. Leo tunataka kuzalisha mkonge tani 300,000 lakini hatuwezi kwa sababu maeneo yaliyokuwa mashamba ndiyo yamekuwa makazi,” amesema Mgumba.

Kuhusu miradi ya kuwekeza ikiwamo masoko, alisema haimaanishi wilaya isifanye huduma za kijamii bali waangalie ni namna gani wanaweza kuwekeza na kuendelea kujiingizia mapato ya ndani.

Katika hatua nyingine, Mgumba amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, kutenga maeneo ya ibada (kanisa na msikiti) katika maeneo ya biashara, viwanja vya wazi na viwanja vya michezo wakati wa upimaji viwanja.

Amesema viwanja vya wazi lazima viwepo pia halmashauri isiangalie tu viwanja ilimradi iongeze mapato kwamba kuacha aneo la wazi ni kama unapoteza mapato.

“Kwa hiyo maeneo ya wazi yawepo na maeneo ya ibada yawepo, huwezi kujenga soko kisha usitenge kiwanja cha msikiti au kanisa utaonekana mtu wa mpango miji ambaye haelewi. Yaani mtu atoke pale kwenye biashara yake halafu kanisani au msikitini aende zaidi ya Km 30.

“Kwa hiyo katika mipango yenu mnapopanga miji hizo nyumba za ibada nazo ziwepo ili watu wanapofanya biashara pale tusiwaweke mbali na Mwenyezi Mungu,” alisema Mgumba.

Awali akitoa taarifa ya mikakati ya wilaya hiyo kuongeza mapato ya ndani, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Kanali Maulid Surumbu alisema ili kuboresha mapato yake ya  ndani wamejiweka mikakati ya kujenga soko la samaki katika kijiji cha Jasini, ukamilishaji wa soko la mazao Maramba na machinjio ya kisasa Kasera.

“Aidha, tumeandaa michoro ya mipango miji na upimaji wa viwanja katika Mji wa Horohoro, Kasera na ukanda wa bahari (Beach Plots) ambapo Kampuni ya World Map imeandaa michoro ya mipango miji na upimaji wa viwanja takribani 4,583 vya makazi, biashara na viwanda katika Rasi ya Manza (Manzabay).

“Mikakati mingine ni kujenga maegesho ya magari katika eneo la Horohoro mpakani, stendi ya mabasi na maeneo ya huduma za kijamii, kuanzisha shamba la miche ya mkonge lakini pia tayari tumenzisha mnada katika kijiji cha Sokonoi,” alisema.

Aidha, Kanali surumbu alisema tayari uboreshaji wa stendi ya Manza kama stendi ya Wilaya umeshaanza sanjari na ujenzi wa soko la kisasa la mazao Horohoro mpakani (Mradi Mkakati).

MKURUGENZI MPYA UTPC ATUA OFISI ZA WAANDISHI PWANI.

 


Mkurugenzi mtendaji mpya wa UTPC Keneth Simbaya akizungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya (CRPC) hawapo pichani alipotembelea Ofisi zao maili moja Kibaha.


Na Victor Masangu,Pwani 

Mkurugenzi mtendaji mpya wa umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania  (UTPC)  Kenneth Simbaya ameahidi kushirikiana bega kwa bega na klabu zote kwa lengo la kuweza kuleta mapinduzi na mabadiliko chanya katika tasnia hiyo ambayo yatasaidia waandishi kuheshimika na sio vinginevyo.


Kauli hiyo ameitoa leo Agosti 10 wakati alipotembelea Ofisi ya klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Pwani(CRPC) na kupata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji kwa lengo la kuweza kubadilishana mawazo kwa lengo la kuboresha zaidi klabu zao.


Simbaya pia ameweza kugagua ofisi hiyo pamoja na kujionea vitendea kazi mbali mbali ambavyo vinatumiwa na waandishi wa habari wa Mkoa wa Pwani katika kuanda habari zao na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kuijenga tasnia ya habari hapa nchini.


"Kikubwa mm leo tangu nichaguliwe ndio klabu hii ya waandishi Mkoa wa Pwani ndio nimekuja kuwatembelea ingawa nitafanya ziara yangu rasmi ya kuweza kukutana na viongozi wote pamoja na wanachama kwa hivyo nimefarijika kukutana na waandishi wenzangu ambao tumefanya nao kazi kwa kipindi kirefu tangu nikiwa Rais wa UTPC,"alisema Simbaya.


 Pia alisema licha ya kutembelea ofisini pia  lengo lake lingine kubwa ni kuhakikisha kwamba anaweka mikakati ya kuleta mabadiliko chanya katika klabu za waandishi wa habari kwa kuwaongezea ujuzi wa kozi mbali mbali ambazo zitawafanya waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.


Kadhalika aliongeza kuwa kitu kikubwa ni kuwa wavumilivu na kutokukata tamaa katika utekelezaji wa kuhabarisha umma na kwamba inapaswa kujifunza zaidi na kuangalia nini ambacho akistahili kukifanya na nini ambacho kinastahili kuanza nacho ili kutimiza malengo.


Kwa upande wake Katibu wa klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Pwani Gustaphu Haule pamoja na mratibu Charles Kusaga wamesema lengo lao ni kufika mbali zaidi hivyo wanahitaji sapoti kutoka kwa uongozi wa UTPC ikiwemo kuwapatia mafunzo ya aina tofauti ambayo yataweza kuwa mkombozi katika sekta ya habari.


LUHAGA MPINA ACHUKUA FOMU YA KUWANIA NAFASI YA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA VITI 15 TANZANIA BARA

 

 Mbunge wa Kisesa, Luhaga Joelson Mpina (kushoto) akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kupitia kundi la Viti 15 Tanzania Bara na Ndg. Matilda Mgeni, Karani wa Masijala ya CCM Mkoa wa Dodoma leo Agosti 10, 2022


MBUNGE wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Joelson Mpina amechukua na kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kupitia kundi la Viti 15 Tanzania Bara.

Mpina amechukua na kurejesha fomu hiyo leo Agosti 10, 2022 ikiwa ni siku ya mwisho ya zoezi la kuchukua na kurejesha fomu za kuomba nafasi mbalimbali za uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa chama hicho kwa mwaka 2022.

Mbunge huyo wa Kisesa amechukulia fomu hizo katika Ofisi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Dodoma na kukabidhiwa fomu hizo na Ndugu. Matilda Mgeni, Karani wa Masijala ya CCM Mkoa wa Dodoma.

Mpina amechukua fomu hizo leo Dodoma ikiwa ni siku chache tangu kuhitimu Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Operesheni Venance Mabeyo katika Kambi ya Kikosi cha Jeshi Makutupora Dodoma mafunzo yaliyomalizika Agosti 5, 2022.

MBUNGE ANAYESHUKIWA KUMWUA MLINZI WA MPINZANI WAKE NCHINI KENYA AONGEA KUTOKA MAFICHINI.


 Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa Azungumza Kutoka Mafichoni 

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kudaiwa kumuua mlinzi wa mpinzani wake kwa kumpiga risasi kichwani mnamo Jumanne, Agosti 9. 

Mbunge huyo ambaye ni mshukiwa mkuu katika mauaji ya Brian Olunga ambaye alikuwa mlinzi wa mpinzani wake mkuu Brian Khaemba, alizungumza kupitia kwa mtandao wa kijamii baada ya kutangazwa mshindi wa ubunge wa Kimilili.

Barasa ambaye aligombea kwa tiketi ya chama cha UDA alifanikiwa kutetea kiti chake kwa kura 26,861 dhidi ya kura 9,497 za Khaemba wa DAP-K na kuwashukuru wakaazi wa Kimilili kwa kumpa muhula mwingine wa kuwahudumia kama mbunge wao.

“Asante sana watu wa eneo bunge la Kimilili kwa kunichagua kwa kura nyingi sana kwa muhula mwingine. Nawapenda sana,” Barasa aliandika kwenye mitandao ya Facebook na Twitter.

Barasa atuhumiwa kumuua mlinzi wa mpinzani wake Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, Barasa alimpiga risasi kichwani msaidizi wa mpinzani wake Brian Khaemba katika kituo cha kupigia kura cha Chebukwabi.

Kisa hicho kilitokea majira ya saa kumi na mbili jioni, Barasa na Khaemba walipokutana katika kituo hicho kuangalia zoezi la kuhesabu kura. 

“Didmus Barasa alichomoa bastola yake na kumlenga msaidizi wa Khaemba kwa jina Brian Olunga. Alimpiga risasi upande wa mbele wa kichwa alikobubujika damu nyingi,” taarifa ya polisi inasema. 

Polisi washuku Barasa alitorokea Uganda

Polisi wanashuku kuwa mbunge huyo huenda alitorokea taifa jirani la Uganda ambako anaendelea kujificha huku msako dhidi yake ukiendelea. 

Wednesday, August 10, 2022

MFAHAMU MNYAMA FISI KIUNDANI ZAIDI.

 

Fisi  ni mmoja wa spishi za  wanyama wanaokula mizoga yaani wanyama waliokufa au walioachwa na wanyama wala nyama, kwa mfano simba au chui. Mbali na kula nyama, fisi  pia hula ndege, mijusi na wadudu.

·         Maisha yake ni miaka 20.

·         Uzito:75kg au zaidi.

·         Ujauzito : miezi 3.

·         Urefu: zaidi ya nchi 35

Fisi huishi kifamilia na kwa taarifa fisi  hujenga kabisa sehemu wanazokaa ,huzaa watoto kuanzia wawili mpaka wanne, kichwa chake hufanana na mbwa ila tofauti yao ipo katika muonekano,  ni mnyama ambaye miguu yake ya nyuma ni mifupi zaidi, hivyo unaweza ukamgundua kwa jinsi anavyotembea na matendo yake, huishi popote sehemu kame, vichakani na hata sehemu ambazo zina majani yenye ukijani sana, hivyo ni mnyama ambaye popote kwake ni kambi.

Pamoja na kwamba ni mnyama ambaye jina lake linakuzwa sana kwamba anatabia ya kula mizoga, lakini fisi ni mnyama anayewinda na hula nyama fresh, akikosa mawindo yake hufanya uporaji kwa wanyama kama simba na inapokosekana hata nafasi hiyo, basi akikutana na mfupa, mzoga  hutafuna.

Wakati wanyama wengine wengi wakiwa wanaongozwa na madume, ukifika katika koo za fisi majike ndio viongozi, lakini mbali na uongozi pia fisi jike ana nguvu za mwili kuliko dume, bahati waliyonayo mbaya wanyama hawa hupata tabu sana ya uzazi pindi jike linapozaa, watoto wao wengi hufa wakati huo , hivyo kama jike atazaa wakati dume halipo ana nafasi kubwa ya kuzaa watoto wafu, kwani fisi dume hutoa msaada kwa jike wakati wa kuzaa hasa ulinzi.

Fisi ni mnyama anayeweza kukimbia umbali mrefu kwa taratibu, we tangulia na spidi 120 yeye atakuja na 30 na atakukuta tuu njiani ukiwa umeanguka au umeishiwa nguvu au misuli kukaza na hapo ndio  atakukamata kwa urahisi, Fisi huzaliwa akiwa anaona wakati huohuo.

Fisi jike huwa na maamuzi yote kuanzia mahabani mpaka mgawanyo wa kazi.
Fisi dume tunaweza kusema ni mnyama bwege anatawaliwa na jike lake pamoja ya kwamba huwa kauli hii wadau wengi wa maliasili zetu  hawapendi kuisikia lakini ukweli ndio huo.

Fisi hunguruma, hucheka pia hutoa milio mbali mbali inategemea na alipo, na hiyo huwa ni lugha wanayotumia kuwasiliana akifanya hivyo wenzie wakisikia wanajua tuu kuna jambo gani limemsibu mwenzao.

Fisi jike huwa na muonekano wa jinsia mbili, katika uke wake kwa juu au sehemu ambayo mwanamke hukeketwa, ile sehemu kwa fisi huwa na ukubwa mkubwa sana inaweza fika nchi saba, jambo hilo humfanya aonekane na muonekano wa jinsia mbili.

Fisi wakikosana kwa kuibiana chakula au dume, na kwa bahati mbaya mmoja awe Mdogo, hupigana mpaka Mdogo kufa, na kama wapo sawa mnyonge hukimbia, wakati huo dume hubaki likishangaa tuu na kushindwa lianzie wapi.

Usisubutu kumvizia fisi kwa nyuma, namna pekee ya kujirinda hurusha  kinyesi chake kwa ghafla na atakuacha ukiwa umechanganyikiwa huku yeye akikimbia. Uoga kwake huisha akiwa na njaa Kali, kwa mfano hawezi kumuwinda binadamu mkubwa, lakini litokeapo suala la njaa Kali huwa hajali umri wa mtu.

Watoto wake wanapofikisha umri wa miaka miwili mama yao huwatimua, wakajitegemee. Fisi anapokutana na watoto wa simba huwaua pasina huruma.
Fisi dume halitakagi kusikia habari za watoto, huwa linaamini ni Mali ya jike, hivyo hanaga nao msaada kabisa.

Fisi jike huwa na mwili mkubwa kuliko dume. Adui yao mkubwa ni mbwa mwitu, kwakuwa huwapora nyama ambazo wao wametafuta kwa tabu sana, pengine kwa kuhatarisha maisha yao.

Fisi wanaogopa sana dume la simba, wanaweza kuwasumbua majike wa simba watatu lakini likija dume huwa linahakikisha mmoja kati yao anachechemea, hivyo wanapomuona simba dume hupiga kelele za kupeana habari kuna hatari.

Fisi ana uwezo mkubwa wa kunusa, hivyo ukifukia kitu hata chini anaweza kukitambua endapo tuu kina harufu ya damu damu. Viumbe hawa wakijihakikishia akiba ya chakula katika himaya zao, basi hufanya sherehe na sherehe zao huwa na ufanano na sherehe za binadamu, hucheza, hufurahi, hufanya ngono na ugomvi huzuka pia wakati huo watoto wote hufichwa ndani ya nyumba.

Fisi jike huweza kupiga dume mpaka likahama nyumba, na hutumia sana ujanja huu endapo jike linataka kuishi na mchepuko wake ndani. Fisi huamini pia katika umoja.
Fisi ni mnyama mnyonge sana na ni mnyama ambaye karibia wanyama wote wawindaji ni wababe kwake, kinachowasaidia ni hali ile ya kutembea makundi makundi yaani kifamilia, ndio huwafanya na wao waonekane kidogo wanajiweza.

Kwanza kaa ukijua fisi sio mnyama wa kumchezea, naye ana uwezo wa kukurarua vile vile, usijeanza fikiria zile hadithi za shule ya msingi ukamchukulia pia, sungura mwenyewe akimuona anafungua njia vibaya sana, japokuwa si kiumbe anayevamia moja kwa moja, huuma kwa kuvizia, jihami vya kutosha na uwe na silaha nzuri kama fimbo nzito, mawe yenye ujazo mzito, na usimpe nafasi ya kumuonesha unamuogopa japokuwa kicheko chake chaweza kukutia hofu Mara dufu.

Kumbuka anapotoa sauti hizo, wenzie wanaposikia hujua kuna jambo, hivyo hakikisha haumpi nafasi hiyo, vinginevyo wakiwa zaidi ya wawili ni hatari kwa maisha yako.

Wanyama hawa wapo wa kutosha sehemu kama ngorongoro,Selous, mikumi, Serengeti , katavi, na sehemu zingine za mbuga za hifadhi za wanyamapori.

FIFA KUENDELEA KUISAIDIA TANZANIA, YALIDHISHWA NA UTENDAJI WA RAIS SAMIA

 

Na John Mapepele

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani(FIFA) Gianni Infantino  amesema  FIFA itaendelea kuisaidia Tanzania kutokana na kuridhishwa na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Michezo.

Akizungumza usiku wa kuamkia leo Agosti 10, 2022 mara baada ya kupokelewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Mohamed Mchengerwa katika kiwanja cha ndege cha Kilimanjaro amesisitiza kuwa FIFA itaendelea kuisaidia Tanzania.

Akiongozana na wachezaji mahiri wazamani waliopata kucheza katika makombe ya dunia na mwamuzi  Corina amesema amefurahishwa na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Tanzania.

"Tayari FIFA imekwishatoa msaada wa ujenzi wa viwanja changamani Dar na Tanga lakini wako tayari kwa ajili ya kuongeza vituo katika kanda nyingine" amefafanua Mhe. Mchengerwa

Aidha, Mhe. Mchengerwa amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa kwenye ambayo imesaidia Tanzania kupiga hatua duniani katika michezo.

Mhe. Mchengerwa amepokea viongozi mbalimbali wa juu kwenye mashirikisho ya Soka duniani na kufanya  vikao vya kuendeleza michezo ambao leo wanahudhuria mkutano Mkuu wa 44 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) jijini Arusha.

Aidha, Mhe. Mchengerwa ametumia fursa hiyo kuendelea kuimarisha mahusiano na mashirikiano na nchi mbalimbali ambazo tayari ziliahidi kuendeleza mashirikiano katika sekta za michezo, Sanaa na Utamaduni.

Mkutano huu wa kihistoria unatarajiwa kuhudhuria na zaidi ya watu mia tano na waandishi wa habari zaidi ya mia moja huku ikitarajiwa kuangaliwa na zaidi ya watu bilioni moja.

Tayari viongozi  wakuu wa mashirikisho yote ya Soka kutoka mabara yote wamewasili na Waziri Mkuu, Mhe. Kassimu Majaliwa  anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan.

Tuesday, August 9, 2022

KUTANA NA BOGA KUBWA KAMA MTU NANE NANE MWANZA

 Ndani ya maonesho ya nane nane 2022 yanayofanyika viwanja vya Nyamhongolo, wilayani Ilemela mkoani Mwanza, kutana na boga aina ya Iyoba lenye uzito wa kilo 40 na urefu wa kimo cha mtoto wa umri wa miaka mitatu.

Mzalishaji ni mkulima Martine N. Kaganda kutoka kijiji cha Kibitilwa wilayani Kwimba.

'MBUZI HUYU KIVUTIO CHA MAONESHO NANE NANE MWANZA'

 UFUGAJI wa kisasa wenye tija ndiyo unaohimizwa na Serikali ya Tanzania.

Katika banda la Wilaya ya Misungwi twende tukajifunze namna ya ufugaji wenye tija wa ng'ombe na mbuzi.






TLS YAJITOSA NANE NANE KUTOA MSAADA WA KISHERIA KWA WAKULIMA, WAVUVI NA WAFANYABIASHARA MWANZA.

 0.1 Unaweza kujiuliza Sheria na Maonesho ya Wakulima, Wavuvi na Wafanyabiashara vinaingiliana wapi?

0.2 Wakulima, Wavuvi na Wafanyabiashara wananufaika vipi na wadau wa sheria kutoka TLS?