ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 1, 2023

MWANADADA HUYU MLEMAVU ANATAMANI KUKUTANA NA RAIS SAMIA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

"Siri yangu ni Mwenyezi Mungu tu ndiye anayenipa moyo, ingawa mara nyingine nakata tamaa hasa pale bidhaa zangu zinaposhindwa kwenda sokoni kimauzo kwasababu soko ninalolitegemea ni mtandaoni na wateja kupata ni changamoto lakini sikati tamaa naendelea kutengeneza bidhaa nzuri za viwango" anasema mwanadada mjasiliamali Suki's Craft, Mtanzania mwenye asili ya Asia anayeishi jijini Mwanza akishiriki Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki ya TCCIA yanayofanyika katika viwanja vya Furahisha kata ya Kirumba. Kisha akaongeza "Nimejiunga kwenye magroup mengi ya whatsaaap hivyo kila maonesho yakiitishwa naziona fursa za kushiriki" Jeh! nini ombi lake kwa Serikali na vipi siku akikutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan atamwambia nini? #jembefm #samiasuluhuhassan #ikulumawasiliano #tanzania #maoneshoyabiashara

Wednesday, August 30, 2023

WAZALISHAJI NAMBA MOJA WA VIFAA VYA UJENZI TOKA NCHINI UGANDA WASHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA MWANZA

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Tukiwa bado tuko katika maenesho ya wafanyabiashara Afrika Mashariki (EAC) yanayoendelea katika viwanja vya Furahisha Mwanza yakiandaliwa na TCCIA tunakutana na mwekezaji huyu anayetoka nchini Uganda anayejihusisha na zana za ujenzi toka kampuni ya EA ROOFING . Pamoja na wenyeji Tanzania, washiriki wengine ni kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan kusini na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Tuesday, August 29, 2023

YANGA WAENDELEZA PALE WALIPOISHIA WAIKUNG'UTA JKT RUVU 5-0


 "WANANCHI MNARA UNASOMA 5G TU." 

Mechi hii tofauti na ya KMC, JKT Tanzania waliwauliza Yanga Sc swali la utimamu wa mwili na Improvisation kutoka kwa wachezaji nyota wa Yanga.

Nidhamu ya kukaa nyuma na kuweka idadi kubwa ya wachezaji kuutazama mpira ilikuwa sahihi japo maswali makubwa kwao yalikuwa ni namna gani wataweza kushikilia bomba bila mpira kwa kuwa na nidhamu ile ile, concentrations ile ile, organization ile ile na ustahmilivu ule ule.

Bahati mbaya kwao Yanga Sc sio kuwa Bora tu Bali wana tanki la kutosha kucheza kwa spidi na intensity ile ile dakika 90 za mchezo.

Kocha Gamondi ana faida ya kujenga physique ya kutosha kwa idadi kubwa ya wachezaji wake kumnufaisha kutekeleza maelekezo yake kiwanjani.

Huyu Maxi Zengeli ukiachana na ubora wake sio na kificho ila ana Mentality ya kuutamani ushindi muda wote na inaisaidia timu.

5G haziji kwa hamasa ama bahati mbaya. (Maandalizi na ku settle dressing room kupata timu zaidi kuliko just star players )

CHUKUA HII TOKA KWANGU 
Na KochaWaWhatsapp 
Mwokoziwabunju 
Niaminimimi

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SOKO LA CRDB KIZIMKAZI DIMBANI, KUSINI UNGUJA ZANZIBAR

 

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (watatu kushoto) kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya CRDB Bank Foundation, Martin Warioba (kushoto) wakifanya tukio la uzinduzi wa ujenzi wa soko la kisasa la CRDB Kizimkazi Dimbani linalojengwa kwa ufadhili wa Taasisi ya CRDB Bank Foundation, unaonatarajia kugharimu takribani Shilingi Bilioni Mbili hadi kukamilika kwake. hafla hiyo ambayo ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea kilele cha Tamasha la Kizimkazi, imefanyika leo Agosti 29, 2023, Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (watatu kushoto) kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya CRDB Bank Foundation, Martin Warioba (kushoto) wakifanya tukio la uzinduzi wa ujenzi wa soko la kisasa la CRDB Kizimkazi Dimbani linalojengwa kwa ufadhili wa Taasisi ya CRDB Bank Foundation, unaonatarajia kugharimu takribani Shilingi Bilioni Mbili hadi kukamilika kwake. hafla hiyo ambayo ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea kilele cha Tamasha la Kizimkazi, imefanyika leo Agosti 29, 2023, Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) akipata maeleo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mtendaji wa Taasisi ya CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa kuhusu ujenzi wa soko la kisasa la CRDB Kizimkazi Dimbani linalojengwa kwa ufadhili wa Taasisi ya CRDB Bank Foundation, unaonatarajia kugharimu takribani Shilingi Bilioni Mbili hadi kukamilika kwake. hafla hiyo ambayo ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea kilele cha Tamasha la Kizimkazi, imefanyika leo Agosti 29, 2023, Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.
 
======   ======   =======

 Kizimkazi, Zanzibar, 29 Agosti 2023: Katika juhudi za kuendelea kuwezesha jamii inayoizunguka kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Benki ya CRDB kupitia Tasisi yake ya CRDB Bank Foundation inatarajia kujenga soko la kisasa katika Kijiji cha Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja visiwani Zanzibar. Hafla ya kuweka jiwe la msingi la soko hilo imefanyika katika eneo la Kizimkazi Dimbani kama sehemu ya shamra shamra za tamasha la Kizimkazi na kuhududhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko hilo, Rais Dkt. Samia ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali ombi la Mkoa wa Kusini kujenga soko hilo la kisasa ambalo litachochea maendeleo ya watu wa Kizimkazi na Mkoa wa Kusini Unguja kwa ujumla.
“Mwaka jana kama mnakumbuka mlinipa kilio hiki cha soko la jamii ya Kizimkazi. Sasa mimi nikalitupa Mkoa ambapo na wao wakalipeleka CRDB na leo wako hapa kwenye field tayari kuweka jiwe la msingi na ujenzi unaendelea. Kwa hiyo tuwashukuru sana CRDB kwa kutushika mkono katika hilo na haya ndo maendeleo ya Kusini tuliyoyasema na ndo madhumuni ya tamasha letu hili la Kizimkazi” alisema Rais Dkt. Samia.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kwa kutambua uchumi wa watu wa kusini unatemegea sana uvuvi, Benki chini ya Taasisi yake ya CRDB Bank Foundation imeamua kuwekeza katika ujenzi wa soko la kisasa ambalo litakwenda kuongeza thamani katika biashara kwa wakazi wa eneo la Kizimkazi. Katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa soko, Benki imetenga takribani Shilingi Milioni 157.8 na tayari ujenzi wa sehemu ya kwanza tayari umeanza.

“Kwa muda mrefu Benki ya CRDB imekua mdau mkubwa wa maendeleo ya Kizimkazi kupitia tamasha la Kizimkazi ambapo hadi kufikia tamasha la mwaka huu, Benki ya CRDB imeshafanya uwekezaji wa takribani Shilingi Bilioni 1 na soko hili la kisasa la Samaki litaghrarimu zaidi ya Bilioni 2 hadi kukamilika kwake ambapo sehemu ya kwanza ya ujenzi itakamilika mnamo mwezi Oktoba 2023” amesema Nsekela.
Mbali na utoaji wa huduma za fedha kwa wananchi wa pande zote mbili za Muungano, Benk ya CRDB pia imekua ikitekeleza sera yake ya uwekezaji katika jamii katika pande zote mbili. Sera hiyo ya uwekezaji katika jamii inaelekeza 1% ya faida kurejeshwa katika jamii katika maeneo ya elimu, afya, mazingira na uwezeshaji kwa wanawake na vijana.

“Mbali na ujenzi wa soko hili la kisasa, Benki kupitia taasisi yake ya CRDB Bank Foundation imeendelea na dhamira yake ya kuleta mageuzi katika mchezo wa Resi za Ngalawa ambapo katika tamasha la Kizimkazi la mwaka 2023, Benki imewekeza zaidi ya Milioni 119.5 katika mashindano ya Resi za Ngalawa ambazo ni sehemu ya Tamasha la Kizimkazi” aliongeza Nsekela.
Mwaka 2021, Benki ya CRDB ilikua mdhamini kuu wa Tamasha la Kizimkazi kwa kugharamia tamasha lote asilimia kuanzia mafunzo kwa wajasiriamali, michezo, maonyesho ya wafanyabiashara hadi kilele cha tamasha. Mbali na hilo Benki ilifadhili ujenzi wa nyumba za madaktari na Ofisi ya Sheha.

Mwaka 2022, Benki ya CRDB ilijenga maabara ya Shule ya Sekondari ya Kizimkazi pamoja na kununua vifaa vyake vya maabara. Sambamba na hilo Benki ilifadhili michezo yote na zaidi kuleta mapinduzi katika mchezo wa Resi za Ngalawa ambapo uliweza kuvutia watu wengi zaidi na kutoa zawadi kubwa zilizoweza kubadili maisha ya wana Kizimkazi ikiwemo zawadi kubwa ya boti ya kisasa yenye thamani ya Shilingi Milioni 30 kwa mshindi.




SIKU 4 KABLA YA TUKIO TIKETI ZIMEBAKI CHACHE COUPLES MEET SINGLES MWANZA

 𝙅𝙐𝙈𝘼𝙈𝙊𝙎𝙄 ya Tarehe 2 September 2023 chagua uiweke akilini au moyoni?

. 𝗨𝗸𝘂𝗺𝗯𝗶:- Villapark Social Hall Kirumba Mwanza. ‘Couples Meet Singles’ Tutagonga pichaz za kutosha kwa Red carpet. . . 𝗞𝗶𝗶𝗻𝗴𝗶𝗹𝗶𝗼: - Single 70,000 na double 100,000. . Tiketi zinapatikana duka la BJ FASHION iliyopo Furahisha Kirumba pamoja na Ofisi za Jembe Fm Mwanza zilizopo Furahisha Kirumba jijini Mwanza au piga simu namba 0763 74 92 86 au 0759097744.

MBUNGE MAIMUNA PATHANI UTAJIRI WA LINDI UPO KWENYE MADINI

 

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Maimuna Pathan akiongea wakati wa kongamano la madini lililofanyika katika wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi huku akielezea fursa mbalimbali zinazotokana na upatikanaji wa madini katika mkoa huo.


Na Fredy Mgunda, Nachingwea.

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Maimuna Pathan amesema Lindi utakuwa mkoa tajili Tanzania kutokana na uwepo wa madini ya Kila aina katika ardhi ya mkoa huo.


Akizungumza wakati wa kongamano la madini lililofanyika katika wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi,Mbunge Maimuna Pathan alisema kuwa wananchi wa Mkoa wa Lindi wanatakiwa kuzitumia vilivyo fursa za uwepo wa madini katika ardhi ya mkoa huo ambao utakuza uchumi wa taifa zima.


Pathan alisema kuwa baada ya miaka mitano kila mtu anatakuwa anazungumzia utajiri wa madini uliopo katika katika mkoa wa Lindi tofauti na ilivyokuwa awali.


Aliwataka wananchi wa Mkoa wa Lindi kuchangamkia fursa zote zilizopo kwenye sekta ya madini ili kukuza uchumi wao na kupata maendeleo kutokana uwepo wa madini mbalimbali.


Pathan alisema kuwa wananchi wanatakiwa kuwa makini na utunzaji wa mazingira kwenye maeneo ambayo madini yanachimbwa 

Monday, August 28, 2023

BRELA "TUMEJIZATITI KUHAKIKISHA WATEJA WANAOSAJILI MAKAMPUNI MAJINA HAYAGONGANI"

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe leo ametembelea banda la BRELA katika maenesho ya wafanyabiashara Afrika Mashariki (EAC) yanayofanyika katika uwanja uwanja Furahisha Mwanza yakiandaliwa na TCCIA Kutoka viwanja hivyo jijini hapa Jembe Fm inazungumza na wadau wa banda hilo wakati ukaguzi wa bamanda ukiendelea.

MABAKI YA MWILI YALIYOKAA MOCHWARI SIKU 190 YAZIKWA.


Baada ya mabaki ya mwili wa Josephine Mngara (27), mkazi wa Mtemboni, Mji mdogo wa Himo, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro kukaa Mochuari kwa siku 190 sasa familia yake imekabidhiwa mabaki ya mwili huo na kwenda kuyazika katika makaburi ya Mereseni yaliyopo katika Mji mdogo wa Himo.

Mwanamke huyo ambaye aliyekuwa akiishi na mpenzi wake Mtaa wa Mtemboni wilayani hapa inadaiwa kuuawa kikatili na mpenzi wake usiku wa kuamkia Februari 19, mwaka huu kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.Februari 23, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kisare Makori aliiambia Mwananchi kuwa usiku wa kuamkia Februari 19 kuna mwili ulikutwa umechomwa moto na kutelekezwa kwenye pagale ambapo polisi katika kuchunguza walikuta michirizi ya damu kutoka nyumba jirani kuelekea eneo ambalo mwili ulikokutwa umeungulia.

Alisema mabaki ya mwili huo, ikiwemo mifupa na sehemu nyingine imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) kwa ajili ya taratibu nyingine za kiuchunguzi ikiwemo vipimo vya vinasaba (DNA) ambavyo vilipelekea kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kujiridhisha na mabaki ya mwili yaliyokutwa eneo la tukio.

Hata hivyo, siku chache baadaye wakati Jeshi la Polisi likimsaka mtuhumiwa huyo,  alituma ujumbe mfupi wa maneno (sms) kwa mama mkwe wake, Theodora Msuya, mama mzazi wa binti huyo  akiomba radhi na kusema roho ya yake inamuuma kwa kujihusisha na mauaji hayo.

"Mama samahani sio kosa langu, nilimkuta ...na mke wangu kwangu nikavunja mlango tukaaza kupigana na ... mimi nikashika panga na yeye akachukuwa mpini wa jembe akawa anarusha nikakwepa ndiyo akampiga mke wangu mpaka chini, akanipa nauli akanambia sepa niachie mimi ataua mtu, mulize (...) mama mimi sijui roho yangu inauma sana mchana mwema," ilisomeka meseji hiyo kwenye simu ya mama mkwe. 


Hata hivyo, Mei 18, mwaka huu baada ya miezi mitatu kupita Jeshi la Polisi Mkoani hapa lilifanikiwa kumtia mbaroni Erasto Gabriel (31) mkazi wa Mtemboni aliyekuwa akiishi na mwanamke huyo (marehemu) kwa madai ya kuhusika na mauaji hayo.

Mama wa marehemu, Theodora Msuya  amesema tukio hilo limewaumiza sana familia na ameacha  pengo kubwa kwa familia na kwamba marehemu amemwachia watoto wanne wadogo na kwamba hajui atawalea vipi kwa kuwa maisha yake ni duni.

"Tunamshukuru Mungu tumezika mabaki ya mwanangu lakini hili tukio limetujeruhi sana maana hata sijui pakuanzia, mwanangu kaniachia watoto wanne wadogo na hata sijui nawaleaje maana sina uwezo hapa nilipo," amesema.

Mama huyo ameiomba serikali kupitia mamlaka zake kuitendea haki familia hiyo ikiwemo kumchukulia hatua za  sheria aliyehusika na mauaji ya mwanaye.

Anna Juma, ambaye ni dada wa marehemu ameziomba mamlaka zinazohusika kumchukulia hatua kijana huyo kwa kukatisha uhai wa ndugu yake ili iwe ni fundisho kwa vijana wengine.

RAIS SAMIA ATEUA BOSI MPYA USALAMA WA TAIFA.

 


Rais Samia Suluhu Hassan akimuapisha Balozi Ali Idi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa leo Agosti 28, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Massoro aliteuliwa kushika nafasi hiyo Januari 3 mwaka huu na kudumu kwenye ofisi hiyo nyeti kwa miezi nane kabla ya kuteuliwa kuwa balozi.

Kabla ya kupewa jukumu hilo Massoro alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu na Mkurugenzi wa Shughuli za Ndani wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa Balozi Siwa ameapishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam tayari kuitumikia nafasi hiyo nyeti na muhimu kwa Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Balozi Siwa alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko

wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) nafasi aliyohudumu tangu Septemba 20, 2018.

Kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda kwa takribani miaka mitatu kuanzia 2015 hadi 2018.

KUTANA NA MASHINE RAHISI YA KUFANYA USAFI NA KUVUTA UCHAFU, NYUMBANI NA KWENYE MAGARI - BEI POA SANA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

JEMBE FM inakutana na Shimomo international Pte LTD ambao wao wamekuja na mashine ya kuvuta uchafu na vumbi kwenye carpet za majumbani, za kwenye magari na madirisha ni moja kati ya wadau wanaoshiriki Maonyesho haya ya 18 ya Biashara ya Afrika Mashariki (MEATF) yanayofanyika katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza kwa wiki moja kuanzia Agosti 25, 2023 hadi Sepetemba 3, 2023. Pamoja na wenyeji Tanzania, washiriki wengine ni kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan kusini na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

RAIS SAMIA AMEKUTANA NA KATIBU MKUU WA UMOJA WA POSTA AFRIKA IKULU DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) Dkt. Sifundo Chief Moyo wakati alipofika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 28 Agosti, 2023.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) Dkt. Sifundo Chief Moyo wakati alipofika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 28 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana  na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) Dkt. Sifundo Chief Moyo wakati alipofika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 28 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) Dkt. Sifundo Chief Moyo mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 28 Agosti, 2023.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) Dkt. Sifundo Chief Moyo (kulia) na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 28 Agosti, 2023.