ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 31, 2014

WAZIRI KAMANI AWATAKA WANANCHI WA JIMBO LA BUSEGA KUIPA KIPAUMBELE ELIMU YA MSINGI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dr. Titus Kamani akiweka jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya Halmashauri ya kijiji cha Shimanilwe wiayani Busega mkoani Simiyu.








USIKU WA LEO VILLA PARK KUNALIPUKA SHANGWE NI MALAIKABAND LIVE.



 BOFYA PLAY KUSIKIA MPANGO MZIMA.


BENDI ya muziki wa dansi ya Malaika yenye masikani yake jijini Dar es salaam, leo Mei 31 iko jijini Mwanza kwa ajili ya kutoa burudani kwa mashabiki wa jiji hilo.

Mratibu wa ziara hiyo, Meneja wa burudani wa Villa Park Resort Ramadhan Maganga alieleza kuwa, ziara ya Bendi hiyo imeratibiwa kwa pamoja na Villa Park Resort ya jijini Mwanza na Alpha Hoteli ya mkoani Geita, ratiba ya ziara hiyo imeanza jana Mjini Geita Mei 30.

“Wakazi na mashabiki wa Mji huo hakika wameshuhudia sauti yenye mvuto ya mwimbaji mahiri Christian Bela na kundi zima la wanamuziki wa Malaika bendi lakini pia wamepata fursa ya kuzisikia live nyimbo zao na ufundi wa wapigaji vyombo na wacheza show wakali bila kumsahau Rapa mkali Totoo ze Bingwa pale ndani ya Omega Resort,” amezungumza tena meneja huyo.

Maganga amesema leo jumamosi ya Meii 31 2014 ni zamu ya wakazi na mashabiki wa Jiji la Miamba ya Mawe (Rock City) ambapo bendi ya Malaika itatoa burudani ya uhakika ndani ya Villa Park Resort ambapo Bela ambaye hujiita Rais wa Vijana atafanya makubwa.

“Bela atautambulisha live kwa kuimba wimbo wake mpya unaotamba kwa sasa katika Radio, TV na Kumbi za burudani wa “Nani kama Mama” lakini pia atawashukuru kwa kuwaonyesha mashabiki wa muziki wa dansi Tuzo yake aliyoipata hivi karibuni ya Kilimanjaro Music Award (KMA) 2014 lakini wakiwa Villa watasindikizwa na Bendi ya Super Kamanyola ya jijini Mwanza,” alieleza.

Aidha baada ya jijini Mwanza, bendi ya Malaika itahitimisha ziara yake Kanda ya Ziwa kwa burudani ya kufa mtu katika Mji wa kibiashara na Madini wa Kahama katika Ukumbi wa Social Club ambapo itakuwa ni mara ya kwanza kabisa kufanya ziara yake hiyo kwa Mikoa hii.

Wito wangu kwa wananchi na mashabiki wa muziki wa dansi wasikubali kusimuliwa bali wafike kujionea burudani ya uhakika kutoka kwa wanamuziki wa bendi hiyo ambapo katika maeneo yote watakayotoa burudani mashabiki watalazimika kulipia kingilio cha Sh. 10,000/= tu, ulinzi wa mali utaimalishwa kwa asilimia 100 hivyo hakutakuwa na usumbufu wowote na watoto chini ya miaka 18 hawataruhusiwa kuingia kwenye show hizo.

GEORGE TYSON HATUNAYE TENA.

Msiba mwingine umeikumba tasnia ya Filamu nchini (BONGO MOVIE) baada ya Director aliyeleta mapinduzi makubwa kwenye tasnia hiyo George Tyson, kufariki dunia kwenye ajali iliyotokea jana usiku ikitokea mjini Dodoma alikokwenda kwaajili ya kazi ya kutengeneza kipindi cha 'The Mboni Show'.


George Tyson amefikwa na mauti katika ajali mbaya baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kupinduka mara kadhaa kutokana na kupasuka tairi.


Ajali hilo ilitokea majira ya saa moja eneo la gairo mkoani Morogoro.  Watu wengine wanne waliokuwa kwenye gari hilo walikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro kwa matibabu kutokana na kuumia sehemu mbalimbali mwilini.

Tutaendelea kuwapa taarifa kadri zinavyotufikia.

Friday, May 30, 2014

KILI MUSIC TOUR MWANZA YASUBIRIWA KWA HAMU.

Brand Manager wa Bia ya Kilimanjaro kutoka Kampuni ya Bia nchini (TBL) akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo katika ukumbi wa Gold Crest jijini Mwanza tayari kwa mpango mzima wa burudani kesho Jumamosi uwanja wa CCM Kirumba Mwanza. MSIKILIZE HAPA KWA KUBOFYA PLAY.


Kutoka kushoto ni Joh Makini, Richie Mavoko, Laban Mbibo aka Dabo 'The Energy God',na Young Killer wakiwa meza moja kuzungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Mwanza
Mkali wa muziki wa Africa Mashariki mwanadada Mwasiti Almasi ametoa ahadi kwa mashabiki wake kutoa burudani yenye utofauti 'full kiwango' kwani kila siku sanaa yake amekuwa akiiongezea kitu kipya.
Richie Mavoko.
Nikki wa Pili (L), Mwasiti (R).
Kutoka kushoto ni Mwasiti Almasi, Ommy Dimpoz, Ben Paul, G. Nacko, Young Killer na mkali wa Ragga Dabo. 
Tyme ya Ommy Dimpoz kuzungumza na wanahabari.
Richie Mavoko (L) na Joh Makini (R).
BAADA ya Kilimanjaro Music Tour kuonesha mafanikio makubwa Mjini Moshi ambapo show ya kwanza kabisa ilifanyika Jumamosi iliyopita, sasa masikio yote na macho yanaelekea jijini Mwanza ambapo show ya aina yake itafanyika katika uwanja wa CCM Kirumba Jumamosi ya Tarehe 31 na tayari wakazi wa meonekana kuisubiri kwa hamu show hiyo ambayo ndiyo gumzo sasa nchini.

Tayari joto la show hiyo limeshaanza kwa Promosheni mbalimbali natayari imeanza kuleta msisimko mkubwa kwa wakazi wa Rock City huku waadhamini, Kilimanjaro Premium Lager wakiwaahidi wakazi wa Mwanza mambo makubwa zaidi.

Wasanii watakaoipamba show hiyo tayari wako jijini Mwanza ambaoni pamoja na Ommy Dimpoz, Izzo Biznes, Christian Bella, Fid Q, Weusi (Joh Makini, Niki wa Pili, G. Nako) Mwasiti, Young Killer, Vanessa Mdee na Richie Mavoko.

Meneja wa Bia ya kilimanjaro Premium Lager amesisitiza kuwa hii siyo ziara ya washindi a Tuzo za Mziki za Kilimanjaro (Kili Music Awards), bali ni ziara ya kuwasaidia wasanii kutangaza kazi zao mikoani.

"Huwezi kupeleka kila mtu lakini tumejitahidi kuwachukuwa wasanii mbalimbali ili wapelekeburudani mikoani na waweze kutangaza kazi zao" alisema.

Ameongeza kuwa baada ya wakazi wa Moshi kuipokea vizuri ziara hiyo, ni matarajio ya Kilimanjaro Premium Lager kuwa show ya Mwanza itakuwa kubwa zaidi. "Baada ya kutoka Mwanza,ziara hii itaelekea Kahama Juni 7, Kigoma Juni 14, Iringa Juni 21, Mbeya Agosti 9, Dodoma Agosti 16, Tanga Agosti 23,Mtwara Agosti 30, Dar es Salaa September 6"

Kaulimbiu ya mwaka huu ni 'Zungusha Kikwetukwetu' 

MIKE TEE AJA NA BRAND NEW HIT - MCHEPUKO

Artist  ; Mike Tee
Beat by Hermy B at B Hitz Studioz
Vocal taken by Producer Mbezi at SZKK studioz
Mixed by Producer Mbezi

Distributed Under Kitaa Promotions
Kitaa Radio

BONIFACE ft MIKE TEE - ULISEMA


Artist   : BONIFACE & MIKE TEE
Song   : ULISEMA
Audio Produced By Mike Tee at Mykey Records 
Video By Kitaa Video / Visualized By Mike Tee

Thursday, May 29, 2014

MMILIKI WA TIMU YA MAN UNITED, AFARIKI DUNIA BILA KUKANYAGA DIMBA LA OLD TRAFORD.

Mmiliki wa timu ya Manchester United, Malcolm Glazer, amefariki dunia huko nyumbani kwake Marekani akiwa na umri wa miaka 85.
Glazer aliinunua klabu hiyo mwaka 2005 kwa pauni milioni 790 sawa na shilingi trioni 2.2, na akashuhudia timu hiyo ikipata mafanikio kadhaa ikiwemo kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya na ya Ligi Kuu ya England.

Hata hivyo, Chini ya umiliki wake uliosabibisha deni kubwa kwa klabu hiyo ''the Red Devils'' walishinda taji la premia ya Uingereza mara tano na vile vile taji la klabu bingwa mwaka wa 2008 .
Wanawe mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuadhiri umiliki wa United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo .
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenyehisa katika soko la hisa la NY stock Exchange.
Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl .
Bwenyenye huyo ambaye hakuwahi kanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.
Glazer inasemekana alianza kisiriri kuwashawishi wenye hisa wa klabu hicho kumuuzia hisa zao tangu mwaka wa 2003 kabla ya kutwaa umiliki wama wa 2005.
United ambayo msimu uliopita ilitangaza faida kubwa ya asilimia 20 yaani pauni milioni 418 inakabiliwa na deni la zaidi ya pauni milioni 400.
Glazer aliyeugua kiharusi tangu mwaka wa 2006 amewawachia wanawe sita umiliki wa klabu hiyo ya Uingereza.

MWENYEKITI WA CCM GEITA AMTAKA MKURUGENZI WAKE AJITATHIMINI.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Joseph Msukuma.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita kimemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Geita Bi. Irine Mwakalinga kujipima na kuona kama anatosha kuwatumikia wananchi wa mji huo badala ya kutumia maamuzi ya ubabe na kuwaburuza katika utekelezaji wa majukumu yake. MSIKILIZE KWA KUBOFYA PLAY.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa CCM mkoani humo Joseph Msukuma alipozungumza na waandishi wa habari juzi jijini Mwanza, alieleza kuwa, Mkurugenzi Irene Mwakalinga amekuwa mwanzilishi wa kuibua migogoro kwa maamuzi yake ya kibabe bila kuwahusisha wananchi na badala yake amekuwa akitoa maamuzi kwa kisingizio cha utekelezaji wa sheria za Mipango Miji.

Msukuma alieleza kuwa kufatia uamuzi huo kupingwa na wananchi na kuufikisha kwa viongozi wa CCM Mkoa wa Geita na kuchukua hatua ya kuingilia kati kutaka kufahamu ukweli juu ya jambo hilo kulizua mjadala mkali na kupelekea kuibuka mgogoro kwa muda wa siku 25 baina ya viongozi wa Chama hicho na Mkurugenzi huyo pamoja na Mwenyekiti Halmashauri hiyo.
  
“Hivi karibuni wananchi ambao ni wafanyabiashara wa mji wa Geita waliamuliwa kuondolea  katika soko lililopo katikati mjini humo kutokana na eneo hilo kudaiwa kupewa mwekezaji bila kuwahusisha wananchi jambo lililozua mgogoro baina ya wananchi na mzabuni aliyefika kuanza ujenzi wa choo kwenye eneo hilo, hali iliyopelekea wananchi kulalamika kwa viongozi wa CCM Mkoa huo,”alieleza.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Joseph Msukuma akizugumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.

Msukuma alieleza kwamba Mkurugenzi huyo amekuwa na tabia ya kutoa maagizo hayo na kuamuru kuwaondoa wananchi waliokuwa wanafanya shughuli za biashara katika baadhi ya masoko lilikwemo la katikati ya mji huo hali iliyopelekea uongozi wa CCM Mkoa kumuomba Mkuu wa Mgoa wa Geita Said Magalula kuitisha kikao cha pamoja kushirikisha wadau wote.

“Mkuu wa Mkoa Magalula alikubaliana na ombi la Chama na jana aliitisha kikao hicho ambacho kiliwashirikisha viongozi wa Halmashauri, CCM Mkoa na Wilaya, wananchi ambao ni wafanyabiashara wa soko hilo ili kujaribu kubaini ukweli iwapo taratibu zilifuatwa na wananchi kuhusishwa juu ya ujenzi huo ikiwa pia kupewa eneo mbadala la kufanyia shughuli zao,” alisema.

Kwa mujibu wa Msukuma wakati wa kikao hicho maelezo kutoka pande mbili kati ya Halmashauri na wananchi zilisikilizwa kwa umakini na Mkuu wa Mkoa na wajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo, ambapo wananchi walikubali kuupokea mradi huo lakini unatekelezwa eneo gani ndipo kuliibua hoja ya malalamiko kutoka kwa wananchi.

Alieleza kuwa baada ya kelele za malalamiko ya wananchi huku majibu yaliyotolewa na Mkurugenzi huyo yakionekana kutojitosheleza hali iliyobainika kukiukwa kwa utaratibu mzima ikiwa ni pamoja na utolewaji wa zabuni hiyo jambo ambalo, Mkuu wa mkoa alifikia uamuzi wa kutoa amri ya kusitishwa haraka kwa ujenzi wa mradi huo unataraji kugharimu Sh. Milioni 90.

“Tulikubaliana kwa pamoja kuwa choo hicho sasa kijengwe eneo la awali lilipo jengo la zamani linalo milikiwa na halmashauri, tumeafikiana na wadau wote kwenye kikao hicho, tunataraji maamuzi na maagizo ya serikali ya mkoa yatafuatwa na kuwa mwisho wa mgogoro huo, kwa hili nampongeza sana Magalula na Kamati yake pamoja na wananchi kuwa waelewa,”alisema.

"Hebu pima hili Mkurugenzi mama Mwakalinga alianzisha tozo ambazo hazikuzingatia sheria, tozo ambazo hazikusainiwa na Waziri Mkuu, tozo zilizokuwa za aina yake kwa kuamrisha Misikiti, Makanisa, Shule kulipa tozo na kweli zilitekeleza na ushahidi tunao tulimpa hadi Waziri Mkuu, kama wadau hao wakirudi nyuma na kudai fedha zao hasara kwa nani? sasa ajitathimini kwa hayo kama anatosha basi aendelee na utekelezaji lakini kama hatoshi basi ajiweke kando kupisha wengine"

Aidha Msukuma amedai kuwa mnamo Mwaka 2012 Mkurugenzi huyo alitengeneza mitaro ile hali akijua kuwa barabara husika litakwenda kufanyiwa matengenezo makubwa hivyo itavunjwa, mitaro hiyo iliyogharimu zaidi ya milioni 115 ilipo kamilika tu baada ya mwezi mmoja ilivunjwa na serikali ikaingia hasara.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa mara kadhaa kupitia vikao mbalimbali wamekuwa wakimshauri Mkurugenzi huyo kuwa masuala yote ya maamuzi yanayohusu wananchi lazima akutane na wananchi wachangie maoni yao na wampe ushauri badala ya kukaa tu mezani bila utafiti na kutoa tamko.

"Ninadiriki kumwita mzigo kwa sababu moja, Mweshimiwa Waziri wa TAMISEMI alipokuja wananchi walimuonyesha eneo la Stendi, stendi ile ili chakachuliwa na waziri alitoa siku sitini iwe imerekebishwa lasivyo atakuja kumrekebisha yeye, alichokifanya nikurundika udongo ambao uko mpaka leo, sasa kama yeye hawezi tunaendeleaje sisi wanasiasa kuvumilia kuona Mawaziri wetu wakiitwa mizigo wakati mizigo tunayo huku" alisema Msukuma na kuongeza kwa kusema.  

"Sasa sisi wawakilishi wa chama wasaidizi wa Mawaziri, wasaidizi wa Rais tunasema wale wote watakaojitathimini na kujiona kuwa mizigo kwa halmashauri zetu wajitathimini na kutafuta sehemu nyigine za kwenda"

Juhudi za kumpata Bi. Irene (Mkurugenzi wa Halmashauri ya Geita) kwaajili ya kutoa uamuzi na msimamo wake bado zinaendelea, kwani licha ya kupigiwa simu mara kadhaa simu yake iliita bila  kupokelewa.

BIA YA SAFARI LAGER YASHINDA TUZO LA UBORA KIMATAIFA 2014.

Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu tuzo iliyopata hivi karibuni ya ubora wa kimataifa Dar es Salaam.
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akionyesha moja ya tuzo za dhahabu ilizowahi kupata wakati wa mkutano na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu tuzo iliyopata hivi karibuni ya ubora wa kimataifa Dar es Salaam.
 BIA YA SAFARI LAGER YASHINDA TUZO LA UBORA KIMATAIFA 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Dar es Salaam, Alhamisi 29Mei 2014;Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza ushindi wake wa tuzo la Ubora wa Kimataifa 2014 maarufu kama ‘International High Quality Trophy 2014’ katika mashindano ya Monde Selection. Safari Lager itapokea tuzo hiyo Jumatatu tarehe 2 Juni, mjini Bordeaux, Ufaransa.

Tuzo ya Ubora wa Kimataifa au ‘International High Quality Trophy’ ni tuzo ya heshima linalotolewa kwa bidhaa ambazo zinashinda tuzo za ‘Gold’ au ‘Grand Gold’ kwa zaidi ya miaka 3 mfululizo. Safari Lager inepewa tuzo hiyo ya heshima kwa kuweza kushinda ‘Gold’ na ‘Grand Gold’kwa zaidi ya miaka mitatu mfululizo.

Akizungumuza na waandishi wa Habari, Meneja wa Bia ya Safari Lager, Bw. Oscar Shelukindo,  alisema, “Safari Lager ni bia ambayo siku zote nia yake ni kuridhisha wateja wake na kwa miaka yake yote…Tunaishukuru sana Monde Selection kwa heshima waliyotupa nahii inatupa motisha ya kuendelea kuwapa wateja wetu bia bora zaidi”.

Bw. Fimbo Butullah, Maneja Masoko wa Safari Lager aliongezea kwa kusema, “Tungependa tena kuishukuru Monde Selection kwa heshima waliyotupa, wateja wetu na kwa Watanzania kwa ujumla. Sisi Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager  kwa kufika hapa tulipo sifa hizi si za TBL peke yake ni za Watanzania kwa ujumla na haswa wateja wtu wanaotumia bia ya Safari Lager”.

Fimbo alimaliza kwa  kutoa wito kwa wateja wa Safari Lager kuendelea kutumia bia hiyo kwani ndio bia namba moja kwa ubora na kwa mauzo Tanzania na pia ni bia namba moja Afrika na leo hii tunapozungumza imepata heshima ya pekee ya ubora wa kimataifa.


WAREMBO WANAOSHINDANIA MISS TABATA 2014 WAENDELEA KUJINOA KWENYE UKUMBI WA DAR WEST PARK.


 Warembo wanaoshindania miss Tabata 2014 wakiwa kwenye pozi wakati wa mazoezi ya shindano hilo na fainali itakalofanyika siku ya Ijumaa tarehe 06/06/ 2014. Mashindano haya ya Miss Tabata 2014 yatafanyika kwenye ukumbi wa Dar West Park.
 Mwalimu Pasilida Mandari anayewanoa warembo watakaochuana vikali kwenye shindano la Miss Tabata 2014 akizungumza na warembo hao wakati wa mazoezi.
 Warembo watakaochuana vikali kwenye shindano la Miss Tabata 2014 wakiwa watokelezea kwenye pozi tofautitofauti wakati wa mazoezi yanayoendelea eneo la Tabata Dar West Park.
Warembo watakaochuana vikali kwenye shindano la  Miss Tabata 2014 wakiwa kwenye mazoezi.
  Mwalimu akimwelekeza mmoja wa warembo wakati wa mazoezi
Ilifika kipindi cha kutoa burudani ilikuwa ni noma sanaaaaaa!!!!!!

Wednesday, May 28, 2014

MALAIKA BAND KUFANYA ZIARA KANDA YA ZIWA.

NA PETER FABIAN, MWANZA.


BENDI ya muziki wa dansi ya Malaika yenye masikani yake jijini Dar es salaam, Mei 30 itakuwa ziarani katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa kuwapagaisha kwa burudani mashabiki wake.

Mratibu wa ziara hiyo, Meneja wa burudani wa Villa Park Resort Ramadhan Maganga alieleza kuwa, ziara ya Bendi hiyo imeratibiwa kwa pamoja na Villa Park Resort ya jijini Mwanza na Alpha Hoteli ya mkoani Geita, ratiba ya ziara hiyo itaanzia Mjini Geita Mei 30 siku ya Ijumaa.

“Wakazi na mashabiki wa Mji huo hakika watashuhudia sauti yenye mvuto ya mwimbaji mahiri Christian Bela na kundi zima la wanamuziki wa Malaika bendi lakini pia watapata fursa ya kuzisikia live nyimbo zao na ufundi wa wapigaji vyombo na wacheza show wakali bila kumsahau Rapa mkali Totoo ze Bingwa pale ndani ya Omega Resort,” alisema.

Maganga alisema kwamba Mei 31 mwaka huu katika ziara hiyo itakuwa zamu ya wakazi na mashabiki wa Jiji la Miamba ya Mawe (Rock City) ambapo bendi ya Malaika itatoa burudani ya uhakika ndani ya Villa Park Resort ambapo Bela ambaye hujiita Rais wa Vijana atafanya makubwa.

“Bela atautambulisha live kwa kuimba wimbo wake mpya unaotamba kwa sasa katika Radio, TV na Kumbi za burudani wa “Nani kama Mama” lakini pia atawashukuru kwa kuwaonyesha mashabiki wa muziki wa dansi Tuzo yake aliyoipata hivi karibuni ya Kilimanjaro Music Award (KMA) 2014 lakini wakiwa Villa watasindikizwa na Bendi ya Super Kamanyola ya jijini Mwanza,” alieleza.

Aidha baada ya jijini Mwanza, bendi ya Malaika itahitimisha ziara yake Kanda ya Ziwa kwa burudani ya kufa mtu katika Mji wa kibiashara na Madini wa Kahama katika Ukumbi wa Social Club ambapo itakuwa ni mara ya kwanza kabisa kufanya ziara yake hiyo kwa Mikoa hii.

Wito wangu kwa wananchi na mashabiki wa muziki wa dansi wasikubali kusimuliwa bali wafike kujionea burudani ya uhakika kutoka kwa wanamuziki wa bendi hiyo ambapo katika maeneo yote watakayotoa burudani mashabiki watalazimika kulipia kingilio cha Sh. 10,000/= tu, ulinzi wa mali utaimalishwa kwa asilimia 100 hivyo hakutakuwa na usumbufu wowote na watoto chini ya miaka 18 hawataruhusiwa kuingia kwenye show hizo.

ULEVI CHANZO CHA KUPOROMOKA KWA MASUMBWI NCHINI

Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akimfua bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi.

BONDIA namba moja nchini katika uzito wa  light welterweight ,  Ibrahimu Class 'King class Mawe' ameibuka na kukemea vikali tabia ya baadhi ya mabondia kwenda kwenye mapambano ya ngumi bila kuwa na nidhamu au kuchukulia kama wanakwenda 'picnic'.

Ameyazungumza hayo katika ukurasa wake wa facebook mapema hivi karibuni akipinga matukio yanayo fanywa na baadhi ya mabondia wakubwa nchini Tanzania kwa kuingia ukumbini huku wakiwa wamelewa au mkononi wakiwa wameshika chupa za vileo.

Bondia huyo alienda mbali zaidi kwa kusema kuwa bondia anapo kwenda kwenye ngumi yupo kazini kwa kuwa ni kazi kama kazi nyingine hivyo anapokwenda haijalishi siku hiyo anacheza au hachezi, hivyo ni lazima awe na nidhamu kwa mashabiki ili apate wapenzi wengi na wapya zaidi.

Wapenzi wa ngumi wanapatikana kwenye ngumi, "Haiwezekani shabiki anayekutambua akutambulishe kwa watu wenye staha zaoau mashabiki wengine wa ukweli, ohoo 'King Class Mawe' yule ameshika bia" hawezi kukubali na hali hiyo akijua fika atakutana na majibu na maswali "Bondia mwenyewe mlevi namna ile?" Hali hiyo inapoteza mwelekeo wa mashabiki wa mchezo wa masumbwi nchini.

Class aliongea hayo hivi karibuni baada ya mabondia Mada Maugo na Thomasi Mashali kuamua kuzipiga kavu kavu kwa kitu kilichotambulika kuwa wao ni walevi tena wakiwa katika ukumbi wa ngumi Frends Corner Manzese

"Kitendo hiki cha kupigana ovyo sikiingi mkono hata siku moja wakati walishapigana uringoni sasa watafute promota ili wapigane tena" "Kitendo chao cha kupigana ovyo kinatukosesha thamani sisi mabondia chipkizi ambapo mchezo huu wa masumbwi tunautegemea na tunaupenda kwa kuwa tuna malengo nao"

"Ushauri wangu kwa mabondia wasifanye kuwa kwenda kwenye ngumi wanaenda kwenye starehe na kama unajiona wewe mlevi bora ubaki nyumbani kwako unywe basi na si vinginevyo kwa kulewa mbele ya mashabiki wa mchezo wa masumbwi nchini tunaonekana mabondia wote walevi, tafadhalini mabondia wenzangu na samahani kama nitakuwa nimewakwaza nawaomba tushilikiane ili mchezo wa masumbwi usonge mbele. Alimaliza.

WANAJESHI 11 WAUAWA NA BOKO:H NIGERIA

Taarifa kutoka mjini Buni Yadi katika jimbo la Yobe Kaskazini mwa Nigeria, zinasema kuwa watu 24 wakiwemo wanajeshi 11 wameuawa katika shambulizi dhidi ya kambi za wanajeshi.
Inaarifiwa kuwa kundi la Boko Haram ndilo linashukiwa kufanya mashambulizi hayo.

Waliwaambia wanakijiji kutokuwa na hofu kwani nia yao haikuwa kuwadhuru raia bali maafisa wa usalama.Wakaazi wanasema washambuliaji waliwasili katika eneo hilo kwa magari kumi ya kawaida na gari moja la kijeshi.
Wanajeshi 11, polisi 13 akiwemo mwanamke mmoja waliuawa.
Pia waliteketeza majengo na magari ikiwemo makazi ya kiongozi mmoja wa kijadi na kituo kimoja cha polisi.
Taarifa zaidi bado zinajitokeza pole pole hasa kwa kuwa mawasiliano yamekuwa magumu kutokana na miundo mbinu mibovu.
Jimbo la Yobe ni moja ya majimbo matatu ambayo serikali imeweka sheria ya kutotoka nje usiku. Licha ya sheria hiyo mashambulizi ya mara kwa mara yamekuwa yakishuhudiwa mengi yakifanywa na Boko Haram. CHANZO:BBC SWAHILI

Tuesday, May 27, 2014

WASHINDI WA MEI 27.2014.COCA COLA MWANZA WAKABIDHI ZAWADI - JIONEE MWENYEWE KOMBE LA DUNIA

JAFET KISUSI MKUU WA MAUZO KANDA YA ZIWA AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BW.WESTON GERSON CHOKALA. KUTOKA URAMBO TABORA.
KUSHOTO NI JAFET KISUSI .MKUU WA MAUZO KANDA YA ZIWA AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWBUSHIRI NASSOR NKYA KUTOKA NYEGEZI KONA MWANZA.
KUSHOTO NI JAFET KISUSI .MKUU WA MAUZO KANDA YA ZIWA AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWHASSAN ATHUMAN IDD KUTOKA NYAKATO MWANZA.
KUSHOTO NI JAFET KISUSI. MKUU WA MAUZO KANDA YA ZIWA AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWROBERT MABANILA KUTOKA MALAMPAKA
KUSHOTO NI JAPHET M.KUBEBEKA MANAGER TRAINING AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BW.ALPHONCE SHUJA. KUTOKA IGULWA USHIROMBO GEITA
KUSHOTO NI JAPHET M.KUBEBEKA MANAGER TRAINING AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWBAHATI THOMAS KUTOKA LULEMBELA MBOGWE GEITA
KUSHOTO NI JAPHET M.KUBEBEKA MANAGER TRAINING AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWDAVID YOHANA KUTKA KATENTE USHIROMBO GEITA
KUSHOTO NI JAPHET M.KUBEBEKA. MANAGER TRAINING AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWWILLIAM MWITA KUTOKA BUTAMBALA USHIROMBO GEITA
KULIA NI MARCO MASAKA MENEJA MASOKO KANDA YA ZIWA AKIKABIDHI FLAT SCREEN KWAMSHINDI BW. RWEURA JOVIN MUKEBEZI. KUTOKA BUKOBA
KUSHOTO NI JAPHET M.KUBEBEKA MANAGER TRAINING AKIMKABIDHI MSHINDI WA FLAT SCREEN BWHEZRON MANANGWA KUTOKA KAPEL-USHIROMBO
JASMEN NOAH MSHINDI WA TIKETI YA BRAZIL.KATIKATI.KUSHOTO NI MARCO MASAKA AKIMTAMBULISHA KWA WAANDISHI WA HABARI.KULIA NI KEVIN MOJA YA WAFANYAKAZI WA COCA COLA JIJINI MWANZA.
WASHINDI WOTE  PICHA NA [ ZEPHANIA MANDIA ]