ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 30, 2022

HATIMAYE BABU OWINO AKUBALI RUTO ALIMRAMBISHA SAKAFU RAILA "NI KAMA NDOTO"


 Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino hatimaye amekubali kwamba kinara wa chama chake Raila Odinga alishindwa katika uchaguzi wa Agosti 9 dhidi ya Rais William Ruto. Babu Owino alisema hatimaye alikubali kwamba Raila alishindwa katika uchaguzi wa Agosti 9. 

Babu anaonekana kukubali matokeo ya uchaguzi huo baada ya kiongozi wa nchi kuhutubia kikao cha pamoja cha bunge mapema Alhamisi, Septemba 29. 

 Akitumia majukwaa yake ya mitandaoni, mbunge huyo mchanga alibainisha kuwa amekiri Raila alipoteze na kuongeza kuwa yuko tayari kuwa katika upinzani. “Leo nimeamini hii kitu ilienda kweli. Ni kama Ndoto.

 Sasa, lazima tupate wadhifa wa mwenyekiti wa PAC na pia tuipige serikali darubini," alisema. 

Haya yanajiri siku chache baada ya Babu kuonya chama cha Orange Democratic Movement dhidi ya mipango ya kumteua mbunge John Mbadi kuchukua wadhifa wa mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu. 

Mbunge huyo mwenye utata aliapa kutomwachia Mbadi, ambaye alikosa nafasi ya kiongozi wa wengi bungeni. "Chama cha ODM, kwa heshima inayostahili, kwa nini John Mbadi ashuke kutoka wadhifa wa kiongozi wa Wengi hadi uenyekiti wa PAC, ambao nilitengewa mimi? 

Hili halitafanyika!!! Sitakubali," Babu alisema kwenye ukurasa wake wa Twitter. 

Babu alisema umefika wakati kwa wabunge vijana kuchukua nafasi za uongozi, akisisitiza kuwa tayari chama kimemzawadia Mbadi na nafasi ya kuteuliwa katika Bunge la Kitaifa. 

Kwa upande wake, Mbadi alipuuzilia mbali madai ya Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino kwamba ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Uhasibu ya Umma (PAC). 

Katika Hotuba Yake ya Kwanza Bungeni Wakati wa mahojiano na NTV mnamo Ijumaa, Septemba 23, Mbadi alisema chama hicho hakina mamlaka ya kuchagua wenyekiti wa kamati. 

TASAC YATOA ELIMU KWA WANANCHI KATIKA MAONESHO YA TANO YA TEKNOLOJIA YA MADINI GEITA

 

 

Afisa Masoko Mwandamizi wa Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC)  Martha Kalvin (wa kwanza kulia) akikabidhi zawadi Kwa  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Bw. Msafiri  Mbibo  alipofanya ziara katika kutembelea Banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya tano  Teknolojia ya madini yanayofanyika mkoani Geita.

 Afisa Masoko Mwandamizi wa TASAC Martha Kalvin akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wengine wa Taasisi hiyo kwenye Banda lao.


SHIRIKA LA Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limebainisha kwamba katika kutekeleza majukumu yake limejikita kwenye kutoa elimu kwa wananchi kufahamu namna linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria

Hayo yalisemwa na Afisa Masoko Mwandamizi wa  Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Martha Kelvin wakati wa mahojiano maalumu na mtandao huu katika Maonesho ya tano ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayofanyika Mkoani Geita.

Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo pia Shirika hilo limeendelea kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho hayo ili kufahamu namna  linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria.

Alisema kwamba wanashiriki maonesho hayo ya teknolojia na uwekezaji kwenye sekta ya madini yanayofanyika mkoani Geita ili kuweza kutoa elimu kwa wananchi juu ya majukumu yanayotekezwa Kisheria. 

“Lakini kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba katika vyombo vya usafiri kwa njia ya maji”

Aidha pia alisema katika maonesho kutoa elimu kwa wananchi wa Geita hususani wadau wa Madini katika jukumu letu la kipekee kwenye biashara ya Meli ambapo kwa sasa wanafanya uondoshaji wa shehena kwa makinikia na mashine zinazotumika katika migodi hivyo wanawakaribisha waweze kupata elimu zaidi itakayowasaidia kujua nini cha kufanya wanapotaka kuagiza mashine zao kuziingiza hapa nchini na kuzitoa pia na usafirishaji wa Makinikia

Kwa mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimmizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.

Aidha Shirika hilo pia lina wajibu wa kuhimiza ufanisi, uchumi na uaminifu, kuendeleza upanuzi wa sekta ya usafirishaji kwa njia ya maji, kuhimiza ushindani katika biashara ya uwakala wa meli, na kuingia kwenye majukumu ya kimkataba na watu wengine au kikundi cha watu.

Maonesho hayo ya Teknolojia ya Madini ni maonesho ya tano kufanyika Mkoani Geita yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza Teknolojia za kisasa katika sekta hiyo pamoja na Taasisi nyingine ikiwemo TASAC.


Shirika la Viwango Tanzania (TBS) latoa semina kwa wafanyabiashara jijini Mwanza

 

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetoa semina elekezi kwa wafanyabiashara wanaoagiza na kuuza bidhaa mbalimbali za chakula na vipodozi jijini Mwanza ili kuwajengea uwezo kutekeleza shughuli zao kwa kuzingatia Sheria.

Semina hiyo imefanyika Alhamisi Septemba 29, 2022 ikiwashirikisha wafanyabishara mbalimbali wakiwemo waagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi, wamiliki wa maghala ya kuhifadhia bidhaa na wamiliki wa maduka makubwa ya bidhaa za jumla.

Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Wilaya Nyamagana mkoani Mwanza Amina Makilagi aliwataka wafanyabishara kuwa wazalendo kwa kuhakikisha wanaingiza nchini bidhaa zenye ubora zisizo na madhara kwa watumiaji

Alisema Mwanza ni jiji la pili kiuchumi nchini na pia kitovu cha biashara katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki hivyo ni vyema wafanyabishara wakatumia fursa hiyo vizuri kwa kuhakikisha wanaagiza bidhaa zenye viwango na kuzihifadhi katika mazingira salama ili zisiharibike kabla ya kumfikia mtumiaji.

"Serikalini inayoongozwa na Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha miundombi ya usafiri na usafirishaki ikiwemo ujenzi wa meli mpya katika Ziwa Victoria, bandari kavu ya Fela, reli ya kisasa (SGR) hadi jijini Mwanza na uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Mwanza ili kurahisisha shughuli za kibiashara" alisema DC Makilagi. 

Katika hatua nyingine, Makilagi alionya kuwa wafanyabishara wanaouza bidhaa zenye viambata sumu wanaliangamiza taifa na wanaenda kinyume na lengo la Serikali ya kuhakikisha afya ya wananchi iko salama akisema tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika zinaonyesha magonjwa kama kansa yanasabanishwa na ulaji wa vyakula pamoja na utumiaji wa vipodozi vyenye viambata sumu.

Pia Makilagi aliipongeza TBS kwa kuendelea kutoa elimu na semina kwa wadau mbalimbali ili kutambua bidhaa zenye ubora na zile zenye viambata sumu zilizopigwa marufuku akisema kila mdau anapaswa kutimiza wajibu ili jamii iwe salama.

Naye Meneja wa TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja alisema Shirika hilo litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa wafanyabishara wanaoingiza sokoni bidhaa zilizopigwa marufuku ingawa kabla ya kuchukua hatua hizo TBS inawaelimishwa kwanza.

Kwa upande wake mmoja wa wafanyabiashara walioshiriki mafunzo hayo, Mohamed Muhran alisema watazingatia elimu waliyoipata kwenye semina hiyo ikiwemo kuagiza na kuuza bidhaa zilizosajiliwa kusajiliwa kisheria ili kwa pamoja kwa kushirikiana na TBS wafanikishe jitihada za kuondoa sokoni bidhaa zenye viambata sumu.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi akifungua semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa TMDA Buzuruga jijini Mwanza.
Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi (katikati) akifungua semina elekezi ya kuwajengea uelewa wafanyabiashara jijini Mwanza ili kufanya biashara zao kwa kuzingatia sheria hususani kutoingiza sokoni bidhaa zenye viambata sumu. Wengine ni Meneja wa TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja (kulia) na mwakilishi wa wafanyabiashara Mohamed Muhran (kushoto).
Washiriki wakifuatilia ufunguzi wa semina hiyo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi.
Meneja TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja akitoa ufafanuzi kuhusiana na umuhimu wa semina hiyo.
Meneja TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo. Wengine ni Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi (katikati) na mwakilishi wa wafanyabiashara Mohamed Muhran (kushoto).
Meneja TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo. Wengine ni Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi (katikati) na mwakilishi wa wafanyabiashara Mohamed Muhran (kushoto).
Afisa Usalama Mwandamizi wa Chakula TBS, Julius Panga akiwasilisha mada kuhusu sheria ya usajili wa bidhaa wakati wa semina hiyo.
Washiriki wakifuatilia mada wakati wa semina hiyo.
Washiriki wakifuatilia kwa umakini semina hiyo iliyoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ikiwashirikisha wafanyabiashara jijini Mwanza.
Watumishi wa TBS Kanda ya Ziwa wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa semina hiyo.
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya Nyamagana Amina Makilagi (katikati waliokaa).
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya Nyamagana Amina Makilagi (katikati waliokaa).
Watumishi wa TBS Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi (katikati waliokaa).
Semina hiyo ya siku moja inatarajiwa kuleta tisha kwa wafanyabiashara ikiwemo kutoagiza na kuuza bidhaa za chakula na vipodozi zilizopigwa marufuku ambapo hatua hiyo ni mwendelezo wa TBS kutoa semina na mfunzo kwa wadau mbalimbali nchini.

DC MOYO AMEDHAMILIA KUTOKOMEZA UJANGIRI KATIKA HIFADHI YA RUAHA

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na wananchi wa kijiji cha Kitisi kata ya Idodi juu ya umuhimu wa kutunza na kuwalinda wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha 
Mradi wa Lion landscapes Wiston Mtandamo akiongea na wananchi wa kijiji cha Kitisi kata ya Idodi juu ya umuhimu wa kutunza na kuwalinda wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha 
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kitisi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa kupewa elimu ya kuwatunza na kuwalinda wanyama pori wa Hifahdi ya Taifa ya Ruaha

Na Fredy Mgunda, Iringa.

 

MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ametangaza vita na mwananchi yeyeto anajihusisha na ujangiri wa wanyama pori katika hifadhi ya Taifa Ruaha hiyo imetokana na kuongezeka kwa vitendo vya ujangiri katika Vijiji ambavyo vinaizunguka hifadhi hiyo.

Akizungumza wakati wa utiaji wa saini Mkataba wa makubaliano ya katika uhifadhi na usimamizi, maendeleo ya jamii na kukutunza mali hai zote baina ya wananchi wa Kijiji cha Kitisi na Lion landscapes katika kata ya Idodi wilaya ya Iringa, Moyo alisema kuwa ujangiri umekuwa unaongezeka kila siku.

Moyo alisema kuwa serikali itawafungulia mashitaka viongozi wa Serikali za vijiji wakiwemo wenyeviti watakaozembea katika vita ya kutokomeza ujangili katika maeneo yao huku akiwataka kuunda vikundi maalum vya ulinzi shirikishi. 

Alisema kuwa umeanza kuongezeka kwenye Vijiji ambavyo vinapakana na hifadhi ya Taifa Ruaha kiasi kwamba kunahatarisha uhai wa wanyama pori ambao wamehifadhiwa katika hifadhi hiyo. 

Moyo alisema kuwa serikali ya wilaya ya Iringa haitamfumbia macho mtu yeyeto yule ambaye atakutwa na kesi ya ujangili basi ajue maisha yake yataishia Gerezani. 

Aidha mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo aliwapongeza Lion landscapes kuendelea kuwalinda wanyama pori na kuviwezesha kiuchumi Vijiji ambavyo vipo kwenye mradi huo.


Awali meneja wa Mradi wa Lion landscapes Wiston Mtandamo alisema kuwa bado wananchi wa Kijiji cha Kitisi wanaendelea na ujangili kwa kuuwa wanyama mbalimbali kwa ajili ya kupata kitoeo,kutumisha Milla na wengi kwa ajili ya biashara haramu ya kuuza nyama pori mtaani kinyume na sheria za nchi.

Mtandamo alisema kuwa kwa kipindi cha miezi mitatu wamekamata mitego tisa ambayo ilikuwa imetegwa porini kwa ajili ya kuwanasa wanyama pori Jambo ambalo linasababisha kutoweka kwa baadhi ya wanyama pori.

Kwa upande wake diwani wa kata ya mapogolo Julias Mbuta amewahimiza wananchi wa kijiji hicho na vijiji vyote vinavyounda kata ya Idodi kuhakikisha wanashirikiana Mradi wa Lion landscapes na serikali katika kuendeleza uhifadhi kwa manufaa ya Vijiji vyote vilivyo jirani na vilivyo nje ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Wednesday, September 28, 2022

WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA KUELEKEA UZINDUZI WA KITAIFA WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA VVU TANZANIA.

Bright Phiri kutoka ICAP akitoa somo kwa wanahabari.

Utafiti wa THIS 2022-2023 utahusisha takriban kaya 20,000 zilizochaguliwa kwa sampuli wakilishi. Hii ina maanisha kaya zote nchini zina fursa sawa ya kuchaguliwa kuwa sehemu ya utafiti huu.

Kwa ujumla inakadiriwa watu 40,000 watashiriki katika Utafiti wa THIS 2022-2023.
Washiriki watakaohusika katika utafiti huu ni wanawake na wanaume wenye umri wa miaka 15 au zaidi, ambao kaya zao zimechaguliwa na wameridhia kushiriki.
Godfrey Obonyo mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo akiwasilisha somo katika darasa hilo.

Utafiti huu utafanyika nchi nzima Tanzania bara na Zanzibar, kwa kutumia dodoso la kukusanyia taarifa na upimaji wa VVU na Homa ya Ini aina B na Homa ya Ini aina C kwa hiari.
Mratibu wa mafunzo Mwanaidi Msangi akifafanua jambo.

Watafiti watakuwa na vitambulisho vitakavyoonesha kuwa wanatambuliwa na mamlama rasmi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vishkwambi vitatumika kukusanya taarifa kupitia mahojiani ya ana kwa ana.
Mzee Mavunde.

Kuna faida gani ya kushiriki katika Utafiti?
THIS 2022-2023 itakupa fursa ya kupima VVU kwa hiari na usiri nyumbani kwako. Ni muhimu kupima na kufahamu hali yako. Ukigundulika una VVU, utaunganishwa na huduma za tiba na matunzo mapema iwezekanavyo ili uweze kuishi maisha yenye afya.

Ushiriki wako utasaidia kuboresha huduma za afya, sera na programu ili kudhibiti janga la ukimwi Tanzania.

Kwa umakini darasani.



SIMBACHAWENE KUZINDUA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI 2022-2023

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,George Simbachawene anatarajia kuzindua utafiti wa pili kitaifa wa Viashiria na Matokeo ya Virusi vya Ukimwi (VVU) Tanzania (TANZANIA HIV IMPACT SURVEY-THIS 2022-2023) 

Simbachawene atazindua utafiti huo jijini Mwanza Septemba,29,2022 kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa,ambapo utahudhuriwa na Naibu Waziri wa Afya,Dk.Godwin Mollel,Balozi wa Marekani nchini,Donald Wrigh,Mtakwimu Mkuu wa Serikali,TAMISEMI,wadau na sekta mbalimbali.

Mkurugenzi Mkazi wa ICAP,Haruka Maruyama akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu utafiti huo amesema kuwa uzinduzi utafanyika katika mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar,ukilenga kuzifikia kaya takribani 20,000 sawa na watu 40,000.

Amesema utafiti huo wa pili utatathmini kushamiri kwa maambukizi mapya ya VVU na matokeo ya huduma za VVU katika jamii na kuangalia malengo ya Umoja wa Mataif ya kudhibiti UKIMWI (UNAIDS) 95-95-95.

Mayaruma amesema THIS 2022-2023 utatumia dodoso la kukusanya taarifa za upimaji wa VVU,Homa ya Ini B na Homa ya Ini C kwa hiari,ukihusisha kaya takribani 20,000 sawa na watu 40,000 wenye umri wa miaka 15 na kuendelea ambao kaya zao zimechaguliwa na kuridhia kushiriki.

Pia fursa ya upimaji wa VVU itatolewa kwa hiari na usiri katika kaya,hivyo ni muhimu wanakaya kupima na kufahamu hali zao za maambukizi ya VVU ikiwemo Homa ya Ini B na C, watakaobaini wataunganishwa na huduma za tiba matunzo,hivyo kuisaidia serikali na wadau wengine kuboresha huduma za afya,sera na mipango ya kudhibiti maambukizi ya VVU nchini.

“THIS 2023-2023 ni utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali (ICAP) lililopo Chuo Kikuu cha Columbia Marekani,kwa usaidizi wa kitaalamu wa kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa kwa ufadhili wa Serikali ya Marekani chini ya Mfuko wa Dharura wa Kupambana na UKIMWI unaolenga kutathmini matokeo ya afua mbalimbali za kinga,tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU' amesema Mayaruma na kuongeza;

“Utafiti huo utatoa mwongozo kwa serikali na wadau wengine kutekeleza malengo ya UNAIDS 95-95-95 ya kudhibiti janga la UKIMWI kufikia 95 asilimia ya watu wote wanaioshi na VVU kufahamu hali zao, 95 ya waliogundulika watapatiwa huduma za matibabu na asilimia 95 wanaoishi na VVU wajue kiwango cha VVU mwilini.”

Amesema taarifa za utafiti huo ni muhimu kwa kuwa zitasaidia Tanzania kufikia malengo ya 95-95-95 na kuweza kudhibiti VVU ifikapo 2030,pia utafiti utatumika kupima maambukizi ya homa ya ini B na homa ya ini C kwa hiari.

Mayaruma amesema THIS 2022-2023 ni mwendelezo wa ule wa awali wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi uliofanyika katika ngazi ya kaya Oktoba 2016 hadi Agosti 2017, hivyo utawapa viongozi wa serikali,wafanyakazi wa afya,asasi za kiraia na watafiti,mwongozo wa kipekee wa kufanya maamuzi juu ya sera ya VVU,programu,ufadhili na kuwezesha familia kuwa na afya bora na taifa lenye ustawi.

Imeelezwa kuwa utafiti huo wa kitaifa utahusisha kaya za maeneo mbalimbali ili kufahamu idadi ya maambukizi mpya ya VVU,ushamiri wa VVU/UKIMWI na waliopo katika matibabu ni miongoni mwa washiriki kuanzia umri wa miaka 15 na kuendelea.

Mkurugenzi huyo Mkazi wa ICAP ameleza kuwa ushauri nasaha utatolewa,watafiti watachukua sampuli ya damu kutoka mkononi kwa ajili ya kupima,majibu yatatolewa siku hiyo hiyo na watakaobainika kuwa maambukizi ya VVU watapewa rufaa katika vituo vya afya walivyochagua kwa usimamizi zaidi na usiri utazingatiwa.  

Ameongeza THIS 2022-2023 itatoa mwongozo ngazi ya kitaifa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa taarifa,kuongeza miundombinu ya maabara na uwezo wa rasilimali watu,taarifa za uelewa wa kina kuhusu mwitiko wa kitaifa katika kudhibiti VVU,mgawanyiko wa tabia hatarishi za VVU na utumiaji wa huduma za tiba na matunzo zitatolewa.

Kwa mujibu wa takwimu kiwango cha maambukizi ya VVU kitaifa ni kiwango cha 4.2 Tanzania Bara ambapo mkoa wa Njombe unaongoza kwa kuwa na kiwango cha 11.4,Iringa 11.3,Mbeya 9.3,Mwanza 7.2,Kagera ikiwa na kiwango cha 6.5 ambapo mgonjwa wa kwanza alipatikana hapa nchini 1981.

Takwimu za matumizi ya dawa za kufubaza (ARV’s) mkoa wa Lindi unaongoza kwa kiwango cha zaidi ya 100,Kilimanjaro 66.8,Kagera 66.0,Songwe 64.6,Pwani 63.5,Mara 63.4,Dodoma Njombe 60.5 huku mikoa inayobaki ikiwa chini ya kiwango cha 60 cha matumizi ya dawa hizo.

Kwa upande wa Zanzibar Mkoa wa Kaskazini Unguja, unaongoza kwa matumizi ya dawa za ARV’s ukiwa na kiwango cha 44.5 ikielezwa sababu ni mwingiliano wa watu kibiashara na utalii ambapo Mjini Magharibi una asilimia 21.0.

Maambukizi ya VVU Mkoa wa Kaskazini Unguja una kiwango cha 0.6 sawa na Mjini Magharibiki huku Kusini Pemba ikiwa na kiwango cha 0.3.
 

RC MGUMBA AWATAKA WAHITIMU WA MAFUNZO OPERESHENI MABEYO 2022 KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA TIJA

 

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba kulia  akikagua gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga
 Gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga wakipita mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo
 gwaride la vijana wahitimu wa mafunzo  kwa mujibu wa sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo kikosi cha 835 KJ cha Mgambo JKT wilayani  Handeni  Mkoani Tanga wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo 

Na Oscar Assenga HANDENI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba amewataka vijana waliohitimu wa mafunzo ya Operesheni Mabeyo 2022 wanakwenda kujiunga na vyuo vikuu hapa nchini kuhakikisha wanatumia vizuri mitandao ya kijamii kwa faida ikiwemo kujiepusha  na matumizi mabaya.na sio vyenginevyo.


RC Mgumba aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya katika kambi ya JKT Kabuku 835 KJ wilayani Handeni wa mujibu wa Sheria Operesheni Jenerali Venance Mabeyo 2022,ambapo alisema kwa sababu vijana wengine waliopo vyuoni wamekuwa na uhuru uliopitiliza na kufanya mambo bila uwepo wa usimamizi.


Alisema lazima wazazi washirikiane katika kuwatembelea watoto wao mara kwa mara kwa maana unaweza kujua mtoto wao anasoma kumbe anasomeshwa jambo ambalo baadae linaweza kuwa na athari kwake na Jamii kwa ujumla.


"Niwasihi wazazi wenzangu muwe mnafanya kuwatembelea watoto wenu wanapokuwa vyuoni lakini wahitumu leo niwaase mkatumie vizuri mitandao ya kijamii kwa ajili ya faida na sio nyenginevyo maana vijana wengine waliopo vyuoni anaweza kudanganywa mwenye mitandao ya kijamii ukashurutishwa jambo ambalo unaweza kufanya kwa tamaa"Alisema


Mkuu huyo wa Mkoa alisema matokeo yake wanadhalilisha wazee wao Jamii na Ndugu na Taifa kwa ujumla hivyo hakikisheni suala la nidhamu wanalishikilia kweli hasa wale wanaoenda kuishi vyuoni.


"Kwa sababu mtakumbana na watu mbalimbali ikiwemo wanasheria wasije kuwapotosha nyie mmeiva na mmefundwa nidhami na uadilifu kaishini maisha hayo"Alisema Mkuu huyo wa Mkoa.


Awali akizungumza wakati wa ufunguji wa mafunzo hayo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT) Meja Jenerali Rajab Mabele aliwataka wahitimu wa mafunzo wasiende kutu mika vibaya katika maeneo mrakayokuwepo wakati wote mkumbuke kiapo mlichoapa.


Alisema kuwa kama wanavyofahamu majukumu ya JKT ni malezi ya vijana na uzalishaji wa mali na kufanya shughuli za ulinzi wa Taifa katika kutekeleza majukumu hayo ya kila siku.


Hata hivyo alisema hivyo kutolewa mafunzo hayo kwa vijana wa mujibu wa sheria na mafunzo ya mujibu wa sheria op Jenarali Mabeyo yamekuchukua muda wa majuma 12 mfululizo.


Mkuu wa Jkt alisema kwamba wahitimu hao wamejifunzamasomo mbalimbi yakiwemo ya uzalishaji mali,nadharia na vitendo kwa ujumla lengo kukuza moyo wa uzalendo kuwajengea nidhamu ,ukakamavu na ujasiri.


Alisema hiyo itawafanya wajitambue kuwa ni sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuilinda,kuijenga na kuitetea nchi yao.



Naye kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha 835 KJ JKT Kabuku Luteni Kanali Raymond Mwanri alisema vijana hao wakiwa kwenye mafunzo hayo wamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa Taifa lao,Uzalendo na utii kwa mamlaka zilizowekwa kwa mujibu wa sheria .


Hata hivyo aliwataka wahitimu hao kuhakikisha wanakiishi kiapo hicho huku akieleza wamefaulu katika viwango mbalimbali vya kuhitimua mafunzo hayo.


Hata hivyo kwa upande Mkuu wa Mafunzo wa JKT Tanzania Kanali Aisha Matanza alisema mafunzo ya vijana ya kujitolea kwa mujibu wa sheria ya Jenero Mabeyo yamekuwa chachu kuweza kuwaimarisha vijana kuwafanya wakakamavu na wazalendo kwa nchi yao.

CWT IRINGA YAWAONYA WALIMU WENYE MAHUSIANO YA KINGONO NA WANAFUNZI

 

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na walimu namna ambavyo ukatilii wa kingono unavyokuwa kwa kasi baina ya walimu na wanafunzi
Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami  akiongea jambo na  Mwenyekiti wa Chama cha waalimu Mkoa wa Iringa Mwalimu Stanslaus Muhongole wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho wilaya ya Iringa Vijijini
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongongozwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami kutoka kwenye mkutano huo mara baada ya kumaliza kuhutubia
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akipokea hotuba ya walimu wa Iringa Vijijini wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho.


Na Fredy Mgunda,Iringa.

CHAMA Cha Walimu Wilaya ya Iringa vijijini (CWT) kimeonya kuwa hakitohusika na utetezi Wa Waalimu watakaojihusisha na vitendo vya utovu Wa nidham ikiwemo mahusiano ya kingono na wanafunzi.


Mwenyekiti Wa CWT Wilaya ya Iringa Vijijini Mwalimu Simoni Mnyawami amesema ni aibu kusikia waalimu wakitajwa kuhusika uhalifu huo huku akisisitiza hatua zaidi za kisheria zichukuliwe ili iwe fundisho Kwa watakaobainika.


Mwenyekiti huyo ameyasema hayo wakati wa mkutano mkuu wa CWT baada ya Mgeni wa Heshima mkuu wa wilaya ya Iringa kuwataka waalimu kuzingatia weledi wa taaluma kwa kuwafifichua wanaojihusisha kingono na  wanafunzi.


Mnyawami alisema kuwa suala la utovu wa nidhamu linapaswa kuheshimuwa kwa kila mwalimu ili kulinda hadhi ya taaluma hiyo Ikiwemo Utoro, ulevi wa kupindukia pampja na baadhi ya waalimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi.


 Mwenyeji wa Mkutano Huu mkuu wa kikatiba Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Iringa vijijini Mwl Simoni Mnyawami alisema ni muhimu waalimu akatambua na kuheshimu taaluma waliyo nayo Kwa kuwa wamepewa dhamana na serikali pamoja na jamii kuwa walezi wa watoto katika kuwajenga kinidham na kitaaluma

 

Kulingana na Changamoto ya utovu wa nidham unaotajwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo aliyekuwa Mgeni wa heshima anasema jambo la walimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi  halipaswi kufumbiwa macho

 

Moyo amewataka walimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wanaowafundisha ili taifa liweze kupata wasomi wengi ambao wanauwezo wa kuja kukisaidia Taifa hapo baadae.


Alisema kuwa Kuna baadhi ya walimu wamekuwa wakiaribu taswira halisi ya kada ya ualimu kwa baadhi ya walimu kufanya mapenzi na wanafunzi na  uwafanyia ukatili wanafunzi kwa makusudi hivyo walimu wanapaswa kutoa taarifa kwa mwalimu yeyeto atakayekutwa anafanya vitendo vya ukatili.


Alisema kuwa kazi kubwa ya mwalimu ni kuwafundisha wanafunzi waweze kufaulu na sio kuwafanyia ukatili wanafunzi..


Aidha Moyo alimazia kwa kusema kuwa walimu wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa wamekuwa wanafanya vizuri kwenye kufundisha wanafunzi ndio maana matokeo yake yamaekuwa mazuri mwaka hadi mwaka.

MNYAMA SIMBA KIVUTIO KIKUBWA KWA WATALII HIFADHI YA RUAHA

 

Mnyama Simba ameelezwa ndiye anayevutia idadi kubwa ya watalii wanaoitembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha inayotajwa kuwa na kiwango kikubwa cha wanyama hao nchini na kwa bara zima la Afrika.Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na watendaji na Maafisa Tarafa wa Wilaya ya Irimga pamoja na kiongozi wa hoteli ya Jabali Asili wakati wa ziara ya kitalii katika Hifadhi ya Taifa ya RuahaMnyama Simba ameelezwa ndiye anayevutia idadi kubwa ya watalii wanaoitembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha inayotajwa kuwa na kiwango kikubwa cha wanyama hao nchini na kwa bara zima la Afrika.Mnyama Simba ameelezwa ndiye anayevutia idadi kubwa ya watalii wanaoitembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha inayotajwa kuwa na kiwango kikubwa cha wanyama hao nchini na kwa bara zima la Afrika.


Na Fredy Mgunda, Iringa

MNYAMA Simba ameelezwa ndiye anayevutia idadi kubwa ya watalii wanaoitembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha inayotajwa kuwa na kiwango kikubwa cha wanyama hao nchini na kwa bara zima la Afrika.

Wakizungumza wakati wa ziara ya Utalii ya maafisa Tarafa na Watendaji kutoka wilaya ya Iringa iliyoratibiwa na mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo, walisema kuwa wamefurahishwa na namna hifadhi hiyo ilivyokuwa na vivutio vingi ambavyo vipo ndani ya hifadhi hiyo kama vile mnyama Simba.

Stella makali na Aunt Mbilinyi ni watendaji wa kata walisema kuwa wamefurahi kufanya utalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha baada ya kuona namna ambavyo mnyama Simba anavyofanya mapenzi jambo ambalo
hawajawahi kuliona toka wanzaliwe hivyo inawafanya watafute muda mwingine wa kwenda kufanya utalii katika hifadhi hiyo.

 

Walisema kuwa wamefurahia kutembelea hifadhi hiyo kwa namna ambavyo wameona wanyama Simba anavutia kiasi kwamba ukiwa katika hifadhi hiyo utakuwa na furaha muda wote kwa namna ambavyo vivutio
vingi vilivyopo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

 

“Tumerithishwa,Tuwarithishe tuungane kwa pamoja kuokomeza ujangili katika hifadhi yetu ya Ruaha iliyopo mkoa wa Iringa ili hata watoe watu waje waone wanyama na vivutio vilivyomo hifadhini”alisema makali

 

 

Emmanuel Ngabuji ni kaimu Afisa Tarafa Pawaga alisema kuwa hifadhi ya Taifa ya Ruaha imejaliwa kuwa na vivutio vingi ambavyo mtalii akifika katika hifadhi hiyo atafurahia na hatatamani kuongoka kutoka kuwapata furaha awepo kwenye hifadhi hiyo ikiwa na kumuona mnayama Simba ambaye amekuwa kivutio kikubwa.

 

Ngabuji alisema kuwa watendaji wengi imekuwa mara yao ya kwanza kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha na kumshuhudia mnyama Simba akiwa katika fungate jambo ambalo liliwafurahisha watalii wote walikuwepo katika hifadhi hiyo ya taifa.

Simba ni mnyama anayependwa katika historia yake yote, na ni ishara ya ujasiri na nguvu. Wanyama hawa kitabia wana miili yenye nguvu—na miungurumo inayoweza kusikika kutoka umbali wa maili tano,” alisema.

Ngabuji alisema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akiutangaza utalii wa ndani kupitia filamu ya Royal Tour ambayo imeanza kuleta matokeo chanya ya ongezeko la watalii nchi na watalii wa ndani kuongezeka kutembelea vivutio  mbalimbali.

 

Naye Menaja Msaidizi wa Hoteli ya Jabali Asili, Josina Mkundi alisema; “Filamu ya Royal tuwa imewaongezea wageni wengi wa kimataifa wanaotembelea hifadhi hiyo na kujionea vivutio vyake lukuki, akiwemo mnyama Simba. Navyoongea sasa hoteli yetu imejaa.”

“Tuna wageni wengi kutoka Uingereza, Ujerumani na Marekani. Pamoja na kufurahia manzari nzuri ya hifadhi hii, wanyama wakubwa na wadogo na aina mbalimbali za ndege, mnyama wanayetaka kumuona zaidi na bila kuchoka ni Simba.”

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa lengo la kuwapeleka maafisa Tarafa na watendaji kutalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha ni kutambua umuhimu wa utalii na namna ambavyo wanaweza kuwalinda wanyama pori wasitoweke ili kuwaliaisha wananchi wengine. 

Moyo alisema kuwa maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha kunaongeza chachu ya ongezeko la watalii katika ukanda wa nyanda za juu kusini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika kusisimua uchumi kupitia sekta hiyo muhimu nchini. 

Alisema kuwa mnyama Simba amekuwa kivutio kikubwa kwa watalii ndio maana mtalii asipoona Simba anahisi kama hajafanya utalii, “leo maafisa Tarafa na watendaji wamefanikiwa kumuona Mnyama Simba akiwa fungate jambo ambali limefurahisha sana”. 

Mohamed Moyo alisema barabara hiyo itajengwa kupitia sehemu ya mkopo wa masharti nafuu wa Sh Trilioni 1.2 uliotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya kuboresha usalama, ustahimilivu wa tabianchi, uwezo wa barabara za ndani na viwanja vya ndege vya mikoa.

Mmoja wa watalii hao kutoka Ujerumani, Romy Wagner alisema mbali na kushuhudia kwa macho yake aina mbalimbali za wanyama na uoto wa asili hifadhini humo, shauku yao ilikuwa kuwaona Simba kwa macho yaolakini pia waliona chui saba wakiwa katika kundi moja, juu ya mti. 

Naye dereva wa mkuu wa wilaya ya Iringa Ramadhan Sosovele alisema makundi makubwa ya nyati, tembo na simba yalikua kivutio chao kikubwa na akafichua kwamba watendaji na maafisa tarafa wengi wao ni mara yao ya kwanza kuwaona wanyama hao katika maisha yao ya asili hifadhini tofauti na walivyozoea kuwaangalia katika filamu.