ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 5, 2024

SIMBA AU YANGA NANI KULIHESHIMISHA TAIFA HII LEO

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Hizi hapa tambo za mashabiki wa soka toka jijini Mwanza wa timu zilizoishangaza Afrika, Simba na Yanga kwa kuwa timu mbili kutoka taifa moja Tanzana kutinga hatua ya Robo fainali na sasa zikiwa katika safari kuelekea michezo yao ya marudiano kuwania nafasi ya kutinga nusu fainali Klabu Bingwa Barani Afrika. Swali jeh ni nani atakaye liheshimisha Taifa hilo lililopo Afrika Mashariki, ni Simba au Yanga au pengine wababe wote hao? ........................ KWA UPANDE WA UFUNDI. KOCHA Mualgeria wa Simba SC, Abdelhak Benchika amesema kwamba mchezo wa kesho dhidi ya wenyeji, Al Ahly Jijini Cairo utakuwa mgumu, lakini wamejipanga kuwakabili mabingwa wa Afrika. Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari mapema jana Alhamisi Jijini Cairo, Benchika amesema kwamba hawapo Misri kwa ajili ya kufungwa, bali kushindana na hawahofii chochote. Kwa upande wa pili Yanga Africans, kocha wake Muargentina Miguel Angel Gamondi amesema kwamba leo anaweza kumpata mchezaji mmoja tu kati ya wanne aliowakosa kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Waliokosekana kwenye mchezo wa kwanza wa nyumbani ni mabeki Kibwana Shomari, Kouassi Attohoula Yao (Ivory Coast)na viungo Peadoh Pacome Zouazoua (Ivory Coast) na Khalid Aucho (Uganda.

Thursday, April 4, 2024

PAULMAKONDA AKIAPISHWA IKULU AKIANDIKA HISTORIA MPYA

 MAKONDA AANDIKA HISTORIA MPYA UENEZICCM

- Ni kuwa Mwenezi aliyehudumu muda mfupi kuliko wenezi wote tangu CCM iundwe - licha ya mbwembwe na sarakasi zake amedumu kwa miezi mitano na wiki moja tu kitini, muda mchache kuliko Shaka aliyekaa miaka miwili kasoro na Sofia Mjema aliyekaa miezi kumi kwa awamu ya sita - kuondolewa kwake kwaibua mijadala wengi wakimpongeza Rais Dkt Samia kuendelea kuisuka vyema sektetarieti ya CCM na kuimarisha Serikali - wengine wasema hawakutaraji kama angefika hata miezi miwili kwenye kiti hicho kutokana na kauli na matendo yake - Kibarua kigumu kwa mrithi wake Akitarajiwa kutekeleza hasa shughuli za kikatiba za mwenezi badala ya kujikita kwenye maigizo mfano wa sinema za kihindi kama kwa mtangulizi wake "Idara ya Itikadi na Uenezi ni kitengo nyeti na muhimu ndani ya CCM...Miongoni mwa majukumu ya idara hiyo ni kushughulikia na kueneza masuala ya itikadi na Sera za CCM, kupanga na kusimamia mafunzo na maandalizi ya makada na wanachama na kusimamia vyombo vya habari vya chama, mawasiliano na uhamasishaji wa umma. sio kitengo cha maigizo, majigambo na ngonjera za kupanda mara farasi mara sijui trekta. Itikadi ni maarifa itikadi ni maoni, anahitajika mtu atakaelewa hilo sio ujanjaujanja" Mjumbe wa NEC, jina kapuni Na. Mwandishi wetu, Katika hali isiyo ya kawaida wanachama wa chama cha mapinduzi (CCM) wamejikuta wakishangilia kuenguliwa kwa aliyekuwa katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Paul Christian Makonda na kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha. Makonda ambaye alitangazwa kuwa Mwenezi wa CCM Oktoba 22 mwaka jana 2023 akichukua nafasi ya Sophia mjema aliyekalia kiti hicho tangu Januari mwaka huo ambaye pia alichukua kiti hicho kutoka kwa Shaka Hamdu Shaka aliyepokea kijiti kutoka kwa Polepole alisifika kwa mbwembwe na sarakasi nyingi katika kipindi chake cha miezi mitano na wiki moja ya uenezi wake tofauti na malengo ya uwepo wa nafasi hiyo nyeti ndani ya chama hicho Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwenezi huyo 'aliyerumbuliwa ni kama alipagawa hivi kuona ameteuliwa kuhudumu kiti hicho na kuanza kuropoka ropoka katika kila alipopanda jukwaani bila kujali aina ya hadhira "Miongoni mwa vituko vya ajabu kufanywa na mwenezi wetu huyu kwa kweli ni kutufundisha ujinga watanzania, yaani ametuambia tusiende mahakamani tukipata changamoto sasa tusipoenda mahakamani si tutauana kweli vijijini huko. Kiongozi anayetamba kukagua utekelezaji wa ilani hawezi kuropoka kijinga namna hii". Anasema Salum Kabambe mwanachama wa CCM Alipoulizwa kutoa maoni yake na gazeti hili mmoja wa wajumbe wa halimashauri kuu ya chama hicho (jina kapuni) juu ya uongozi wa makonda na kutolewa kwake alisema kuwa ameshangaa imekuwaje ameweza kufikisha hadi miezi mitano kwa kuwa siku ya kwanza tu alipozungumza na wanachama pale Lumumba alimuona kuwa hawezi kudumu kitini humo akiamini bado ana mawenge "Kwa kweli hata kumthibitisha ni kwa sababu tu tunampenda mheshimiwa Rais na kumheshimu, hivyo isingekuwa vyema kumkatalia pendekezo la huyu bwana kuwa mwenezi, wengi wetu tulijua hawezi hii nafasi". Amesema MNEC huyo "Kwa asili Mwenezi wa CCM anapaswa kuwa mtu mwenye maarifa, anayeweza kuunganisha wenzake, anayeweza kujifunza ili akafundiashe wengine, ndiye mtangazaji mkuu wa itikadi ya chama chetu, kwa hiyo ndio muuzaji hasa wa sura na roho ya CCM lazima mtu huyo asiwe mropokaji kama Makonda. Makonda ni jasiri sana akiambiwa nenda kaseme hili hapo utampenda lakini sio yeye kwenda kuanzisha na kuongoza idara muhimu kama hii". Aliongeza MNEC Alipoulizwa kama ni hivyo aliwezaje kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na sasa anaenda kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha, alisema kuwa ukuu wa mkoa sio sawa na ukatika wa uenezi wa chama. Mtu yeyote anaweza kuwa mkuu wa mkoa lakini si kila mtu anaweza kuwa katibu mwenezi anayefaa na kuongeza kuwa hata huko Arusha akienda na mitazamo yake ile ile hatotoboa. "Idara ya Itikadi na Uenezi ni kitengo nyeti na muhimu ndani ya CCM...Miongoni mwa majukumu ya idara hiyo ni kushughulikia na kueneza masuala ya itikadi na Sera za CCM, kupanga na kusimamia mafunzo na maandalizi ya makada na wanachama na kusimamia vyombo vya habari vya chama, mawasiliano na uhamasishaji wa umma. sio kitengo cha maigizo, majigambo na ngonjera za kupanda mara farasi mara sijui trekta. Itikadi ni maarifa itikadi ni maoni, anahitajika mtu atakaelewa hilo sio ujanjaujanja" aluongeza Mjumbe huyo

YANGA SC KILA GOLI MILIONI 100 ZA KITANZANIA DHIDI YA MAMEMLODI.

 


YANGA SC KILA GOLI MILIONI 100 ZA KITANZANIA DHIDI YA MAMEMLODI.

RASMI: Muwekezaji wa klabu ya Yanga , Gharib Said Mohamed maarufu kwa jina la GSM ametoa ahadi kwa wachezaji wa klab ya Yanga kuwa atanunua kila goli litakalofungwa dhidi ya klabu ya Mamelodi Sundowns  kwa Tsh 100 Milioni,


πŸ‘‰Gsm 100 Milioni

πŸ‘‰Raisi Samia Suluhu 10

πŸ‘‰01 Milion - Aziz Ki 

πŸ‘‰05 Milion - Mwigulu

πŸ‘‰02 Milion - Mavunde


#SPORTSRIPOTI

Wednesday, April 3, 2024

ANGEL BENARD AOLEWA TENA.

 


Baada ya ndoa yake ya mwanzo kupasukiana, Msanii wa injili Angel Benard aolewa tena na mwanaume mwingine anayeishi nchini Marekani

Angel Benard aliyefahamika kwa nyimbo kadhaa ikiwemo Siteketei, watu walidhani ndoa yake ya mwanzo yeye na mumewe walikuwa na furaha sana kwa jinsi walivyokuwa wakiwaona ikiwemo mitandaoni, hivyo minong'ono imeibuka kuguata kuolewa tena nchini Marekani
Huku taarifa zikidai kuwa miezi mingi iliyopita Angel alikimbilia mahakamani kutaka talaka yake toka kwa mumewe wa mwanzo ili awe huru kuendelea na maisha yake mengine na alipopata talaka yake rasmi hakusubiri ameolewa tena na mwanaume anayeishi Marekani.

Monday, April 1, 2024

WANAOTOROSHA KOROSHO KWENDA NJE YA NCHI WAONYWA, SIKU ZAO ZINAHESABIKA

 

 



Na Oscar Assenga, TANGA.

BODI ya Korosho Tanzania Mkoani Tanga imewaonya wakulima wenye tabia za kutorosha Korosho kwenda kuuza nje ya nchi kuacha mara moja kufanya hivyo kwani siku zao zinahesabika kutokana na vyombo vya dola vinawatambua na watapokamatwa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Moja ya athari za utoroshaji wa Korosho kwenda nje ya nchi ni pamoja na kutokufikia malengo ya uzalishaji ikiwemo nchi mapato ambayo yangeweza kusaidia katika kuchochea maendeleo kwa wananchi wake.

Onyo hilo na Kaimu Meneja wa Bodi ya Korosho Mkoa wa Tanga Atufigwege Mwakyagi wakati akizungumza na waandishi wa habari namna bodi hiyo ilivyojipanga kukabiliana na vitendo hivyo huku wakiwataka wenye tabia hizo kuacha mara moja

Alisema kwani kufanya hivyo maana yake ni kulihujumu zao hilo pamoja na juhudi za Serikali ni kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na bora ili kuweza kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo hicho chenye tija.

“Ndugu zangu mnaotorosha korosho kufanya hivyo ni kosa na vyombo vya dola hivyo tambueni siku zenu zinahesabika sisi kama bodi hatutakubali kuona watu wanahujumu zao hilo kwani zinatakiwa kumnufaisha mkulima na Rais wetu Dkt Samia Suluhu ameweka nguvu kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri na bora”Alisema

Aidha alisema kwamba wale ambao wanafanya hivyo wanataka kufifisha juhudi za Serikali ambazo ni kuona wakulima wa zao hilo wananufaika nalo na hatimaye kuweza kujikwamua kiuchumi na kubadilisha maisha yao hivyo hawatakuwa tayari kuona zinakwamishwa kwa namna yoyote ile.

Kaimu Meneja huyo alisema mauzo ya korosho msimu uliopita yalikuwa ni tani 741 kwenye mnada uliofanyika wilayani Mkinga na kufanikisha kuingiza fedha kiasi cha Sh.Milioni 703 ambazo wakulima wa zao hilo wameweza kunufaika nalo.

Akizungumzia suala la udhibiti ubora wa zao hilo alisema kwamba wa sasa wamekuwa wakitoa mafunzo kwa wakulima ili kuweza kulima kilimo chenye tija ili kudhibiti ubora kuhakikisha unakuwa mzuri kabla ya kwenda sokoni ambapo wamekuwa wakiuza kwenye mfumo rasmi.