Thursday, May 1, 2025
TRAORE ASHUKURU NCHI ZILIZOANDAMANA KUMUUNGA MKONO.
PADRI KITIMA AVAMIWA NA KUJERUHIWA POLISI YAMSHIKILIA MTU MMOJA.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linachunguza tukio la kushambuliwa kwa Padri Charles Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), ambaye alijeruhiwa kichwani usiku wa kuamkia Mei Mosi, 2025 katika eneo la maliwato ya kantini ya TEC, Kurasini.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, tukio hilo lilitokea majira ya saa nne na robo usiku.
Padri Kitima alikuwa ametoka kuhudhuria kikao cha viongozi wa dini kilichodumu kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa moja jioni. Baada ya kikao hicho, aliendelea kubaki katika kantini ya Baraza kwa ajili ya kupata kinywaji, ambapo baadaye alielekea maliwatoni na ndipo alipovamiwa na kushambuliwa na watu wawili waliotumia kitu butu.
Padri Kitima alipelekwa katika Hospitali ya Aga Khan kwa ajili ya matibabu na hali yake inaelezwa kuwa inaendelea vizuri. Kabla ya kuhamishiwa Aga Khan, alipatiwa huduma ya kwanza katika kituo kidogo cha afya kilichopo ndani ya eneo la TEC.
Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja, Rauli Mahabi (maarufu kama Haraja), mkazi wa Kurasini, kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi wa kina ukiendelea ili kuwabaini wote waliohusika na kuhakikisha hatua kali zinachukuliwa mara moja.
Mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio wameripoti kuwa Padri Kitima alionekana akizungumza na watu kadhaa kabla ya kuondoka kuelekea maliwatoni, na muda mfupi baadaye waliona watu wakikimbia eneo hilo, huku yeye akiomba msaada akiwa anatokwa damu.
Padri Charles Kitima mbali na kuwa Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), mbali na nafasi yake ndani ya Kanisa Katoliki, Padri Kitima anajulikana kwa misimamo yae ya kukosoa na kuwa mstari wa mbele katika masuala ya haki za binadamu, utawala wa sheria na uwajibikaji wa kijamii.
RAIS DKT. SAMIA AKISHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI MKOANI SINGIDA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Akishiriki Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani inayoadhimishwa Mkoani Singida kitaifa, leo tarehe 1 May, 2025.
Wednesday, April 30, 2025
NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU AHIMIZA WALIMU KUWALINDA WATOTO ANA WIMBI LA UKATILI
IMEANDIKWA NA. VICTOR MASANGU/PWANI SAUTI NA ALBERT G.SENGO Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Charles Mahera,amewataka walimu, wazazi, pamoja na walezi nchi nzima kuhakikisha kwamba wanaweka mipango madhubuti ambayo itaweza kuwalinda na kuwatunza watoto na wanafunzi kwa lengo ikiwa ni kuweza kupambana na wimbi la vitendo vya unyanyasaji na ukatili ili waweze kusoma katika mazingira ya usalama na amani. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Aprili 29, 2025 wakati wa kufunga rasmi mafunzo ya matumizi bora na salama ya vifaa vya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi, yanayotekelezwa kupitia Mradi wa Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) ambayo yamefanyika katika ukumbi wa shirika la elimu Kibaha Mkoani Pwani na kushirikisha jumla ya walimu wapatao 1,800 kutoka mikoa minne ya Tanzania bara. Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Awali na Msingi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi Suzanne Nusu, amebainisha kwamab kati ya Halmashauri 184 wamejitahidi zimefanikiwa kupata fursa ya kupelekewa vifaa hivyo vya tehama ambapo walimu nao wamenufaika na kupatiwa mafunzo. Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo ya Tehama wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuweza kuona umuhimu wa kuwapa ujuzi wa kuwafundisha teknolojia na kuahidi kwenda kuyafanyia katika kwa weledi katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao katika kuboresha elimu. Mafunzo hayo ya Tehama yameshirikisha walimu wapatao 1800 yamewashirikisha washiriki mbali mbali kutoka Mikoa ya Geita, Tabora,Simiyu pamoja na Kagera ambapo lengo lake ni kuongeza viwango vya sifa za walimu kuanzia elimu ya awali hadi sekondari.
WALIOUA VIJANA BUNGENI KENYA WAFICHULIWA NA VIDEO NA PICHA ZA BBC
Mnamo Juni 25, 2024, damu ilimwagika katika Bunge la Kenya.
Siku hiyo, maelfu ya waandamanaji walielekea bungeni ili kusitisha muswada wa fedha #FinanceBill2024 kupitishwa kuwa sheria.Tuesday, April 29, 2025
KUUNDWA KWA JAB NI HATUA YA KUIMARISHA NA KUBORESHA SEKTA YA HABARI - MAJALIWA
![]() |
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, |
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema Serikali ya Awamu ya Sita imechukua hatua kadhaa katika kuimarisha na kuboresha sekta ya habari nchini ikiwa ni pamoja na kuunda Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.
Waziri Mkuu amesema hayo leo tarehe 29 Aprili, 2025 wakati akifunga Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika jijini Arusha kwa siku mbili.“Kwenye sekta ya habari na utangazaji, falsafa ya “4Rs” za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, alizozibainisha baada ya kuingia madarakani mwezi Machi 2021, imetekelezwa kwa vitendo hususani kwenye eneo la “Reforms” (Mageuzi),” amesema Waziri Mkuu na kuongeza;
“Serikali ya Awamu ya Sita katika kutekeleza falsafa hii imechukuwa hatua mbalimbali kuimarisha sekta ya habari na utangazaji nchini kwa kuunda chombo kipya cha kushughulikia usajili wa taaluma ya waandishi wa habari yaani Bodi ya Ithibati”.
Waziri Mkuu Majaliwa amesema Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari iliyozinduliwa mwaka huu ina jukumu la kusimamia viwango vya kitaaluma kwa wanahabari ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa matakwa ya kisheria chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229.
Amesema hatua nyingine zilizochukuliwa na Serikali ni kuhakikisha inawezesha shirika la Habari la utangazaji kuwepo kisheria pamoja na kuimarisha Idara ya Habari Maelezo kwa kununua vitendea kazi vikiwemo Magari na vifaa vya kurushia matangazo mbashara.
Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu inayosema “Uhabarishaji kwenye Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba katika uhuru wa vyombo vya habari” inalenga kujadili athari za teknolojia ya akili mnemba katika uendeshaji wa vyombo vya Habari na uhuru wake.Amesema Serikali katika kuhakikisha Akili Mnemba (AI) inatumika kwa njia inayowezesha badala ya kudhibiti uhuru wa vyombo vya habari, imeanzisha mchakato wa kuandaa sera maalum ya AI na waandishi wanaowajibu wa kuchangia ili kupata sera nzuri.
“Sera hii itatoa mwongozo wa matumizi ya AI katika vyombo vya habari, ili kuhakikisha kwamba teknolojia mpya zinaendana na misingi ya uhuru wa vyombo vya habari, uwazi, na uadilifu wa uandishi wa Habari, hivyo mtumie muda wenu hapa kujadili na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha sera hiyo,” amesema Waziri Mkuu.
WAZIRI MKUU AWASILI ARUSHA AFUNGUA MKUTANO WA 73 WA ACI AFRICA .
Na. Vero Ignatus/Arusha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amewasili Mkoani Arusha na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Paul Christian Makonda pamoja na viongozi wengine wa Serikali na Chama leo tarehe 28 Aprili, 2025.Waziri Mkuu anatarajia kufungua Mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la viwanja vya ndege kwa kanda ya Afrika (ACI Afrika) unaofanyika kwenye Hotel ya Mount Meru.
.jpeg)
Awali akitoa salamu kwa mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda Arusha amemshukuru Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
kwa kuridhia uwanja huo mzuri wa kisasa katika mkoa wa Arusha ambapo unaweza ukawa namba moja basi ama namba mbili katika nchi ya Tanzania .

Vile vile ameshukuru Prof. Godius Walter Kahyarara Katibu Mkuu wa Wizara kwa kuridhiwa uwanja huo kutumika kwa ndege ndogo zinazounganisha Afrika ya Mashariki kwa wageni wanaotaka kutua katika uwanja huo
"Nafahamu hatua zinaendelea vizuri na siyo muda mrefu Mamlaka watatangaza ya kwamba Arusha unaweza kutumia sasa uwanja wa ndege kama point of interest na kuwaruhusu wageni wenye private jet kuja Arusha bila kuhangaika kwenda Kilimanjaro. Alisema Makonda.
SERIKALI ITAFANYIA KAZI HARAKA MAAZIMIO YA KONGAMANO LA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI- MSIGWA.
"TUSIONGELEE AMANI KAMA HATUTAKI KUONGELEA HAKI" PADRI KITIMA
Ni kupitia Channeli ya inayomilikiwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania {TEC} ikiwa ni moja ya chombo cha Uinjilishaji kwa njia ya Sauti na Video, fuatilia yale yaliyojiri.
Monday, April 28, 2025
JK ASHIRIKI KUTOA MAFUNZO CHUO KIKUU CHA HAVARD HUKO BOSTON KWA MAWAZIRI WA NCHI ZINAZOENDELEA
Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete yuko mjini Boston, Marekani, ambako anashiriki katika kutoa mafunzo kwa Mawaziri wa Fedha na Mawaziri wa Mipango kutoka nchi mbalimbali zinazoendelea.
MBUNGE KOKA AFANYA KUFURU YA MAENDELEO UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA KWA VITENDO
NA VICTOR MASANGU,KIBAHA
MNGEZA B BINGWA WA ERASTO CUP MUHEZA,HALMASHAURI KUWAUNGA MKONO MADIWANI WATAKAOANZISHA LIGI KWENYE MAENEO YAO
HALMASHAURI ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga imesema kwamba itaendelea kuwaunga mkono madiwani ambao watakaoanzisha Ligi mbalimbali katika maeneo yao kwa lengo la kuhamasisha michezo na kufungua fursa za ajira kupitia sekta hiyo.
MBIO ZA KILOMITA 5 ZA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI ZAFANA, JIJINI ARUSHA (World Press Freedom Day, 5K Fun Run)
Mbio hizo zilianzia kwenye uwanja wa Ghymkana /Mgambo na kumalizikia hapo hapo Ghymkhana; ambapo zilihudhuriwa na wanahabari mbalimbali , wadau wa habari na wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa.
Maadhimisho ya Vyombo vya habari duniani yanafanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 27 hadi 30 Aprili 2025, ambapo siku ya kwanza yameanza na mbio za kilomita 5 na kesho kutafanyika mikutano mbalimbali katika hoteli ya Gran Melia.
Maadhimisho hayo yanaratibiwa na JamiiAfrica au zamani Jamii Forums, Serikali , shirika la Kimataifa la Elimu , Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na wadau wengine wa Habari nchini na Kimataifa.