ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 20, 2024

RAIS SAMIA NA MAPAMBANO YA KUZUIA VIFO VYA MAMA NA MTOTO NCHINI TANZANIA

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA.

Kupitia tafiti mbalimbali zilizofanyika nchini sababu kubwa inayochangia vifo vya mama na mtoto ilionekana kuwa ni kupitia ucheleweshwaji wa aina tatu. Kwanza ni ngazi ya jamii kufanya maamuzi sahihi kwa wakati kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya. Pili ilikuwa ni njia au miundombinu ya kumfikisha katika vituo vya kutolea huduma za afya. Tatu ni kwenye vituo vyenyewe vya utoaji huduma za afya wanakofika, mama anakuta wateja ni wengi wanaohitaji huduma, vitendea kazi kuwa vichache wakiwemo wahudumu wenyewe, vitengo mbalimbali vikiwemo vya kufanyia upasuaji na mazingira mengine. Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba na kutoa wito kwa Redio za jamii kusaidia kuelimisha umma juu ya mfumo wa M-Mama unaotoa fursa ya usafiri wa dharula kwa Mama na Mtoto mchanga kuanzia kwenye ngazi ya jamii hadi kwenye vituo vya kutolea huduma wakati wa dharula.

Thursday, December 19, 2024

DUBE APIGA HAT TRICK YANGA IKISHINDA 3-2 DHIDI YA MASHUJAA.

 


MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam.

Nyota imemng’aria mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube Mpumelelo aliyefunga mabao yote matatu dakika za saba, 21 na 53, wakati mabao ya Mashujaa yamefungwa na David Ulomi dakika ya 45 na Idrisa Stambuli dakika ya 62.

Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 30 na kurejea nafasi ya tatu, ikizidiwa pointi moja na watani, Simba SC baada ya wote kucheza mechi 12 na wote wapo nyuma ya Azam FC yenye pointi 33 za mechi 15.

Kwa upande wao Mashujaa baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 19 za mechi 15 sasa wakibaki nafasi ya saba.

JESHI LA ZIMAMOTO PWANI LATOA ELIMU KWA WANANCHI 600 KUPAMBANA NA MAJANGA YA MOTO

 NA VICTOR MASANGU, PWANI

 
Jeshi la  zimamoto ya uokoaji Mkoa wa Pwani katika kuhakikisha inapambana  na kuzuia  majanga ya moto imeamua kuendesha zoezi la kutoa elimu na mbinu  kwa vitendo katika makundi  mbali mbali ikiwemo wakinamama wajasiriamali kwa lengo la kufahamu jinsi ya namna kukabiliana na  moto  pindi unapotokea.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima wakati wa maonesho ya nne ya viwanda,biashara na uwekezaji amebainisha kwamba kwa kipindi cha siku nne  wameweza kufanikiwa kuwafikia zaidi ya wananchi 600 ambao wamenufaika na elimu mbali mbali inayohusiana na masuala ya kupambana na kuzima moto.

Kamanda huyo amebainisha kwamba lengo kubwa la kutoa elimu hiyo kwa ajili ya kuweza kujifunza namna ya kupambana na majanga la moto  katika maeneo mbali mbali ikiwemo katika maeneo ya makazi ya watu wanayoishi , mashuleni, sambamba na maeneo mengine yenye mkusanyiko wa watu wengi.

"Sisi kama jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani tumeamua kushiriki katika maonesho haya ya viwanda, biashara na uwekezaji na tumetumia fursa hii katika kutoa elimu na mbinu mbali mbali kwa wananchi wetu na tumefanikiwa kuwafikia wananchi zaidi ya 600 kutoka katika makundi mbali mbali wakiwemo mama lishe, wakinababa, vijana, viongozi, wafanyakazi wa hotelini, pamoja na wanafunzi kutoka shule mbali mbali,"alisema Kamanda Jenifa.

Kamanda aliongeza kwamba kwa sasa wameweka mikakati ya programu endelevu ambayo itakuwa ikiendelea katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Pwani katika kutoa hamasa kwa wananchi ya kuweza kutumia nishati  safi na salama ikiwa sambamba kutoa elimu juu ya kupambana na majanga ya moto.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo amempomgeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha matumizi mazuri ya nishati safi na salama na kwamba na wao wataendelea kumuunga mkono katika kuwaelimisha zaidi wananchi umuhimu wa kutumia nishati safi.

"Wananchi  wa Mkoa wa Pwani ninawaomba pindi majanga ya moto yanapojitokeza wanatakiwa kutoa taaarifa mapema kwa mamalaka ambazo zinahusika na wanatakiwa wapige simu namba 114 kwa ajili ya kupata huduma ya haraka kutoka kwa wahusika ili waje kwa aajili ya kuudhibiti moto,"alisema Kamanda.

Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha habari na elimu wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Joyce Kapinga amewahimiza wananchi wa wote wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanazingatia maelekezo yote ambayo wanapatiwa kutoka kwa wataalamu ikiwemo kuwakumbusha kufunga milango yote na madirisha pindi janga la moto linapotokea majumbani mwao.

Nao baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Pwani ambao wamepata fursa ya kupatiwa elimu ya kupambana na majanga ya  moto wamelipongeza jeshi la zimamoto na uokoaji kwa kuweza kuona umuhimu mkubwa kwa kutumia maonesho hayo kwa kutoa elimu na mbinu ambazo zitaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa pindi moto unapotokea.

WALIMU MAKADA WAASWA KUDUMISHA MAHUSIANO MEMA.


Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Lindi Patrick S. Magarinja akitoa elimu ya mahusiano bora baina chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali ili kukuza sekta ya elimu hapa nchini.
Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Lindi Patrick S. Magarinja akitoa elimu ya mahusiano bora baina chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali ili kukuza sekta ya elimu hapa nchini
Baadhi ya walimu Makada wa CCM wakiwa kwenye mafunzo maalumu 

Na Fredy Mgunda, Songwe.

Walimu makada wametakiwa kuwa mstari wa mbele Kwa kuhakikisha wanadumisha mahusiano mema baina yao na kati ya Chama na Serikali ili kukuza sekta ya elimu hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Lindi Patrick S. Magarinja wakati alipokuwa akitoa mada kama Mkufunzi kwenye Kongamano la Jukwaa la Walimu makada wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe.

Magarinja aliwataka Walimu waendelee kudumisha Mahusiano mema kati ya Chama na Serikali Kwa lengo la kuleta ustawi,utulivu ndani ya nchi pamoja na kusimamia Itikadi za Chama Cha Mapinduzi ikiwemo Ujamaa na kujitegemea kwani ndiyo msingi Mkuu unaowafanya wanaCCM kuwa wamoja bila kubaguana.

Magarinja amesema CCM itaendelea kufuata Itikadi zake za Ujamaa na kujitegemea kwa kuwa zimekuwa mhimili mkubwa wa kuwezesha WanaCCM kuwa wamoja katika  na kufanikisha ushindi wa CCM kwenye chaguzi mbalimbali kwani ushindi wa CCM unatokana na namna Makada wake wanavyo kuwa wamoja na kujitoa kupitia rasilimali zao kwa maslahi mapana ya Chama Cha Mapinduzi

NI PROFESA LIPUMBA TENA UWENYEKITI CUF.


 Matumaini na imani ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), yamebaki vile vile kama ilivyokuwa miaka 25 iliyopita, baada ya kumchagua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wao taifa.

Profesa Lipumba anaukwaa wadhifa huo, baada ya kupata kura 216 katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho, akiwashinda wenzake saba waliokuwa wakichuana katika nafasi hiyo.


Hii inampa nafasi mwanasiasa huyo aliyebobea katika masuala ya uchumi ya kukiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo na hivyo kuweka historia ya kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa kwa miaka 30 nchini.


Katika uchaguzi huo, uliofanyika jana Jumatano, Desemba 18, 2024, Profesa Lipumba ameshinda kwa kura 216 kati ya kura 592 halali zilizopigwa.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi wa chama hicho, Mashaka Ngole, anayemfuatia Profesa Lipumba ni Hamad Masoud aliyepata kura 181.


Aliyekuwa Makamu mwenyekiti wa CUF bara, Maftah Nachuma ndiye aliyefuatia akipata kura 102, huku Wilfred Rwakatare akipata 78.

Kisha alifuata Juma Nkumbi aliyepata kura sita, Athumani Kanali kura tano, Chifu Yema na Nkunyuntila Chiwale wakiambulia kura mbili kila mmoja.


Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara, Othman Dunga ameibuka mshindi akipata kura 182 kati ya 533 halali zilizopigwa.

Dunga alifuatiwa na Miraji Mtibwiliko aliyepata kura 159, Magdalena Sakaya kura 140, Juma Nkumbi 34, Mohamed Ngulangwa 29 huku Komein Rwihura akipata kura 18.


Jumla ya kura 542 zilipigwa katika uchaguzi huo, huku 533 zikiwa halali na tisa ziliharibika.


Ngole ametangaza pia matokeo ya uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti Zanzibar uliokuwa na wagombea watano.


Katika nafasi hiyo, Mbarouk Seif Salim aliyepata kura 159 ndiye aliyeibuka mshindi, huku Husna Mohamed Abdallah akifuatia kwa kupata kura 150.


Aliyefuata ni Haroub Mohamed Shamis aliyepata kura 117, kisha Ali Rashid Ali kura 74 na Mohamed Habibu Mnyaa akipata kura 56.

Katika uchaguzi huo, kura saba ziliharibika kati ya 563 zilizopigwa.

Baada ya matokeo hayo, Ngole amesema uchaguzi wa ngazi ya wajumbe wa Baraza la Uongozi utafanyika leo asubuhi.

MBUNGE NEEMA LUGANGIRA ALIVYODHIBITI NJAMA ZA MTUHUMIWA WA UBAKAJI WA MTOTO WA MIAKA 9 KUMTOROSHA MTOTO

 

Na Mwandishi Wetu,BUKOBA.

MBUNGE wa Viti Maalumu kupitia CCM anawakilisha NGOs Tanzania Bara Neema Lugangira amelazimika kuingilia kati tukio la kubakwa mwa mtoto wa miaka 9 wilaya ya Bukoba na kuzuia jaribio la kumtorosha mtoto huyo. 

Akizungumza namna alivyopata taarifa kutoka kwa mwananchu kuhusu tukio hilo baya la ubakaji kwa binti huyo mdogo wa miaka 9, Mbunge Neema alisema kwamba alisema kwamba tukio hilo lililotokea Desemba 8 mwaka huu ambapo alipokea simu Desemba 17 kutoka  kwa mwananchi kutoka kata ya  katika kuongea naye mzee huyo alimueleza kuhusu uwepo wa mtoto wa kike wa miaka 9 aliebakwa na kuharibiwa.

Alisema kwamba mkazi huyo alimueleza tukio hilo lilitokea Desemba 8 mwaka huu na baada ya jitihada za wananchi kwenye mtaa bibi wa mtoto akaenda kutoa taarifa Kituo cha Afya ili mtoto apate huduma na baadae kwenda Polisi.

Mzee huyo alimweleza Mbunge Lugangira kuwa kuna jitihada kwamba mtuhumiwa anaweza kutoka kwa dhamana na mtoto aliyefanyiwa ukatili huo atoroshwe na kimeshaandaliwa kiasi cha fedha.

Kufuatia taarifa hiyo Mbunge Neema aliamua kujiridhisha na taarifa hiyo kisha akawasiliana na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Erasto Sima  naye akafanya mawasiliano na OCS ambaye  alifika Kituo cha Polisi Bukoba lakini kwa bahati mbaya yule mtuhumiwa wa ubakaji alikwisha tolewa mchana huo kwa dhamana ambapo ambapo walifika wanaume  wawili kuomba dhamana lakini waliambatana na kiongozi.

“Kwa hakika niwashukuru Mhe DC, RPC, OCD, OCS, Dawati la Jinsia na Ustawi kwa kuchukua hatua kwanza kuhakikisha usalama wa mtoto husika na mtuhumiwa amerudishwa ndani kutokana na mazingira tatanishi” Alisema Mhe Lugangira 

“Nimshukuru pia Waziri wa Mambo ya Ndani nilipompa taarifa hii aliibeba kwa uzito ukubwa na Waziri wa Jamii Dkt Dorothy Gwajima ambaye nilimpa taarifa hii naye alitoa maelekezo nitakapofika Bukoba  niambatane na na Bi Rebeccah Gwambasa, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa tuende polisi kupata taarifa na tuende kukutana na familia” Alisema  Mbunge Neema 

Alisema walifika Polisi na kwenda kwenye familia kuonana na bibi wa mtoto, mama wa mtoto na familia imerejeshewa imani baada ya mtuhumiwa amerejeshwa na yupo mahabusu.

“Lakini nimesikitishwa sana nikiwa kama Mbunge wa CCM kwa sababu kiongozi aliyeambatana na wale wanaume wawili kwenda kuhakikisha mtuhumiwa anapata dhamani ni kiongozi aliyechaguliwa na wananchi kutoka kwenye Kata ya Kitendaguro na kitendo hicho ni kinyume na CCM na CCM haitaungana na haita kuwa sehemu ya uhalifu na CCM ipo kwenye kusimamia haki na tunamsikia Rais Dkt Samia Suluhu Hassa. anavyopambana kuhakikisha anaimarisha haki na utawala bora mpaka akaunda tume maalumu ya haki jinai iliyotoa mapendekezo kama taifa kuumarisha haki jinai na yamefanyiwa kazi, Alisema Mhe Neema Lugangira

Alisema hivyo haiwezekani wao kama viongozi kuwa sehemu ya kupindisha mchakato wa kisheria na jambo hilo limemsikitisha akitambua kitendo cha kiongozi huyo na tayari taarifa ameifikisha kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera na anaamini Chama kitachukua hatua stahiki. 

“Viongozi kunapokuwa na matukio ya kihalifi ukiwemo ubakaji na ulawiti hatupaswi kushiriki na kutafuta namna ya kuharibu ushahidi wa kesi hiyo na serikali imejipanga kuhakikisha inaimarisha,viongozi wasiwe sehemu ya kukwamisha jitihada zinazofanywa na Jeshi la Polisi “Alisema  

Hata hivyo aliwaomba wazazi wajitahidi kuongea na watoto wao na kuwahimiza maadili na mienendo na wawe wanaongea nao mara kwa mara ili waweze wapesi kutoa taarifa katika familia yoyote itakayokumbana  na ukati kwa watoto.

“Kwa Jeshi la Polisi na viongozi tuhakikishe haki inatendeka na nitoe rai kwa mamlaka husika kusimamia vema mchakato wa kesi hiyo uweze kukamilika ili mtuhumiwa huyo aliyebaka mtoto wa miaka 9 afikishwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake na kama itathibitika achukuliwa hatua kali” Alihitimish Mhe Neema Lugangira.

WALIMU MAKADA WA CCM WAPIGWA MSASA SONGWE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.

 

 Katibu wa siasa, uenezi na mafunzo kutoka mkoa wa Iringa, MWL Joseph Ryata akitoa elimu kwa walimu Makada wa CCM mkoa wa Songwe kuelekea uchaguzi mkuu mwakani 2025Makatibu wa siasa, uenezi na mafunzo kutoka katika mikoa ya Iringa,Njombe Lindi na Songwe wakiwa tayari kuwapiga msasa walimu Makada wa CCM mkoa wa Songwe 

Baadhi ya viongozi wa CCM mkoa wa Songwe 
Picha ya pamoja viongozi wa CCM na walimu Makada wa CCM mkoa wa Songwe baada ya kupigwa msasa kuelekea uchaguzi mkuu mwakani 
Baadhi ya walimu Makada wa CCM mkoa wa Songwe wakiwa makini kupata elimu kutoka kwa makatibu wa siasa, uenezi na mafunzo kutoka mikoa minne


Na Fredy Mgunda, Songwe.

Zaidi ya walimu 500 Mkoani Songwe wamepewe elimu ya namna ya kutafuta kura za chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani 2025 nchi nzima.


Akizungumza wakati wa kutoa mafunzo hayo katibu wa siasa, uenezi na mafunzo kutoka mkoa wa Iringa, MWL Joseph Ryata aliwataka Makada hao kuhakikisha wanaenda kutoa elimu kwa wananchi wajitokeze kujiandikisha kwenye vitambulisho vya mpiga kura.


MWL Ryata alisema ili CCM ishinde kwa kishindo inahitaji mtaji mkubwa wa wapiga kura na jukumu hilo wanapewa walimu Makada wa CCM mkoa wa Songwe.


Alisema chama cha Mapinduzi (CCM) kina njia na msingi yake ya kupata ushindi hivyo ni vyema Makada hao wakaelewa namna gani ya kuwa tayari kuzitafuta kura za CCM katika uchaguzi ujao.


MWL Ryata alisema walimu wamekuwa wana ushawishi mkubwa katika kila jambo huko wanakoishi na jamii watumie nafasi na nguvu waliyonayo kuhakikisha wananchi wakiandikisha kwa wingi na CCM inashinda kwa kishindo

RC LINDI AZINDUA KITUO CHA POLISI DARAJA “A” WILAYA YA LINDI

 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Polisi wa Mkoa wa Lindi wakati wa  uzindua kituo cha polisi wilaya ya lindi ambacho kitaongeza ufanisi wa kazi wa Jeshi kulinda amani na majukumu mengine
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack alipowasili wakati wa  uzindua kituo cha polisi wilaya ya lindi ambacho kitaongeza ufanisi wa kazi wa Jeshi kulinda amani na majukumu mengine

Na Fredy Mgunda, Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack amezindua kituo cha polisi wilaya ya lindi ambacho kitaongeza ufanisi wa kazi wa Jeshi kulinda amani na majukumu mengine.

Mkuu wa Mkoa amemshukuru Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Samia Suluhu Hassani kwa muda mfupi ambao amekuwepo madarakani kwa kulitazama jeshi la polisi hasa kwenye kuboresha miundombinu ya kufanyia kazi na pia miundombinu ya usafirishaji ndani ya jeshi la polisi.

 Telack Ametumia fursa hiyo kulipongeza jeshi la polisi kwa kazi kubwa ya kusimamia amani na kufanya mkoa wa Lindi kuwa wenye utulivu wakati wote.

Awali katika hotuba yake ya kumkaribisha mgeni rasmi kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi Acp. John Imori alisema ujenzi wa kituo hicho daraja A ulianza Mwaka 2022 nakukamilika 2023 ambapo mkandarasi wa mradi huo alikuwa ni fundi mkuu wa kikosi cha Polisi cha ujenzi . 

Mradi huu umetumia kiasi cha Milioni mia tisa arobaini na nane laki tatu themanini na nne elfu mia tisa hamsini na moja (948,384,951/=)

Sambamba na ujenzi huo, Acp J. Omori alitaja miradi mingine ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya polisi vinayoendelea katika hatua mbalimbali ndani ya mkoa wa lindi. 

miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa kituo cha Polisi daraja c na nyumba mbili za makazi ya askari kwenye kata ya Nandagala wilaya ya Ruangwa Milioni 164, ujenzi wa kituo cha polisi daraja c kwenye kata Kibutuka wilaya ya Liwale wa Milioni 115, ujenzi wa kituo cha polisi daraja c kwenye kata ya Somanga wilaya Kilwa wenye thamani ya sh Milioni 115, Ujenzi wa kituo cha Polisi daraja c kata Tingi wilaya ya kilwa wenye thamani ya sh Milioni115, Ukarabati wa kituo cha Polisi kwenye kata ya Naipanga wilaya ya Nachingwea Milioni 52, ukarabati wa kituo cha Polisi Nanjilinji  kwenye kata ya nanjilinji wilaya ya kilwa Milioni 15. 

Aidha, Mhe. Telack ametumia jukwa hilo kuwaomba viongozi wa dini kuwaombea watoto ambao wapo katika hatari ya matendo ya ukataili wa kijinsia na mmomonyoko wa maadili.

Tuesday, December 17, 2024

DKT. YONAZI AMPONGEZA MHE. BALOZI MUTATEMBWA

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt, Jim Yonazi akiwa katika  picha ya pamoja wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt, Jim Yonazi akiwa katika  picha ya pamoja wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt, Jim Yonazi akiwa katika  picha ya pamoja wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.

Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) wakiwa katika matukio tofauti wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuaga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) wakiwa katika matukio tofauti wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuaga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) wakiwa katika matukio tofauti wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Dkt Henry James Kilabuko na Kumuaga Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa tukio lilofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.



NA; Mwandishi Wetu - Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt Jim Yonazi amempongeza Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Anderson Mutatembwa kwa Kuteuliwa kuwa Balozi.

Dkt. Yonazi Ametoa pongezi hizo Tarehe 16 Disemba 2024, wakati akimuaga Mhe. Balozi Mutatembwa na Kumakaribisha Naibu katibu Mkuu mpya Dkt. James Kilabuko.

Dkt. Yonazi amempongeza Balozi Mutatembwa kwa kufanya kazi ya ushauri kwa utulivu aliyotokana hekima aliyojijengea na kujaliwaa na Mwenyezi Mungu kuwa nayo “Na ndiyo maana Mhe. Rais ameweza kukuamini na kukuteuwa katika nafasi ya Ubalozi ili uweze kumuwakilisha yeye pamoja na Nchi katika maeneo ambayo atakayoona inampendeza.” Alifafanua

Aliendelea kusema kuwa, nafasi ya ubalozi ni nafasi nyeti na adhimu sana na ni fursa inayopatikana kwa watu wachache sana, “umepata fursa nyeti sana ya kuitumikia Taifa naamini utaendelea kufanya kazi kama ambavyo umekuwa ukifanya hapa na utakaoenda kufanya nao kazi watafaidika na kufurahia kama tulivyo faidika sisi.” Alibainisha Dkt. Yonazi

Akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu mpya Dkt. James Kilabuko, Katibu Mkuu Dkt. Yonazi alisema Ofisi ya Waziri Mkuu ni Ofisi yenye majukumu mazito yenye watumishi wachapakazi wenye kutizama tija katika utendaji wa majukumu yao ya kila siku.

Naibu Katibu Mkuu, Dkt. James Kilabuko Alimshukuru Mhe. Rais kwa kumteuwa katika nafasi hiyo na kuona kwamba anaweza kumsaidia Katibu Mkuu Kiongozi katika nafasi hiyo, aliendea kusema kuwa anategemea kupata ushirikiano kutoka kwa Watumishi na Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika kumsaidia Katibu Mkuu Dkt. Jonazi kiutendaji na kufikia malengo yanayotegemewa na mamlaka za juu.

Kwa Upande wake Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa , alimshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea Kumuamini na kumteuwa katika nafasi hiyo.

Aidha, Ameishukuru Menejimenet ya Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu pamoja na watumishi wa Ofisi hiyo kwa ushirikiano waliomupatia wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ofisini hapo, aliendelea kusema kuwa ni sehemu ambayo atapakumbuka kwani amefanya kazi kwa amani na Utulivu wa hali ya juu.

TRA PWANI YAKUTANA NA WAFANYABIASHARA,VIONGOZI WA DINI KUPANGA MIKAKATI YA ULIPAJI KODI

 


VICTOR MASANGU, PWANI

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Mkoa wa Pwani imesema kwamba itawahudumia walipakodi wake wote kwa kuzingatia misingi imara ya kuwa na uadilifu, uwajibukaji,, weledi pamoja na suala la kuwa na uaminifu pavmoja na kuweka mikakati endelevu ya kuwatembelea sehemu zao za biashara kutoa ushauri, kusikiliza changamoto zinazowakabili ii kuzitafutia ufumbuzi katika utoaji bora wa huduma.
 
Hayo ameyabainisha  Kamishina wa uchunguzi upande wa Kodi Hashimu Ngoda wakati wa alipokutana  kuzungumza na baadhi ya viongozi  wa jumuiya za wafanyabiashara, viongozi wa dini, pamoja na watendaji wa TRA  kwa lengo  kuweza   kubadilishana mawazo,kusikiliza changamoto, kupeana ushauri  ambao utaweza kusaidia katika kuongeza kasi ya ukusanyaji wa kodi.

Ngoda amebainisha kwamba TRA kwa sasa wapo katika mwezi wa hamasa hivyo wameamua kufanya ziara katika maeneo mbali mbali kwa lengo la kukutana na walipakodi wao ikiwa sambamba na kutoa ushauri,kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati ya pamoja ambayo itaweza kusaidia katika ukusanyaji wa kodi.

"Mkoa wa Pwani ni moja kati ya Mkoa muhimu sana katika ukusanyaji wa mapato  kwani katika kipindi cha miezi mitano wameweza kufuka malengo ambayo wamejiwekea katika ukusanyaji na ukizingatia kwa sasa TRA tupo  katika mwezi wa hamasa ndio maana tumeamua kuwatembelea walipa kodi wetu na kuwapongeza kwa kutoa kodi kwa hiari,"alisema Meneja Masawa.

Naye Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Masawa Masatu amewashukuru kwa dhati wafanyabiashara wote wa Mkoa wa Pwani na kuwaomba  wanaendelee kushirikiano  kwa hali na mali katika suala zima la ulipaji wa kodi kwa hiari ili serikali iweze kukusanya mapato yake kwa maendeleo ya wananchi.

 Napendakuchukua fursa hii ya kuwapongeza kwa dhati wafanyabiashara wote wote ndani ya Mkoa wa Pwani na kitu kikubwa ninawashauri kuendelea kutoa ushirikiano mkubwa katika kulipa kodi  na lengo letu ni kukusanya mapato mengine ambayo yatasaidia kupata fedha na serikali kuweza kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo,"alibainisha Meneja Masawa.

Nao baadhi ya viongozi wa dini akiwemo Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Pwani Hamisi Mtupa ameipongeza TRA kwa kuweza kuweka mazingira mazuri kwa wafanyabiasshara tofauti na kipindi cha miaka ya nyuma na kuwahimiza wahakikishe wanaendelea kulipa kodi kwa hiari kwa maslahi ya wananchi.
 

Wafanyabiashara amabao wameshiriki katika kikao hicho wamesema kwamba TRA Mkoa wa Pwani kwa sasa imekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu na mafunzo mbali mbali ambayo yameweza kuwasaidia katika kuendesha shughuli zao za kibiasshara bila kupata usumbufu wa aina yoyote ile.

Ziara ya mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani inaendelea kufanya ziara katika maeneo mbali mbali kwa ajili ya kuwatembelea walipa kodi wao ikiwa ni mwezi wa hamasa wenye lengo la kuweza kutoa elimu,ushauri, pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili ili kuzitafutia ufumbuzi katika suala zima la kulipa kodi kwa hiari kwa maendeleo ya nchi.

Monday, December 16, 2024

TAMASHA KUBWA SAME UTALII FESTIVAL SEASON 2 KUFANYIKA DESEMBA 20 -22 SAME KILIMANJARO

 

 


Na Oscar Assenga, 

TAMASHA Kubwa la Same Utalii Festival Season 2 linatarajiwa kufanyika Desemba 20 hadi 22 mwaka huu  katika wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro ambalo limeidhinishwa kufanyika kila mwaka lengo likiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu kuhamasisha utalii nchini.

Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari Mkuu wa Wilaya ya Same Kasilda Mgeni alisema kwamba maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na  litatanguliwa na lingine Desemba 17 hadi 19 kutakuwa na matukio yatakayotanguliwa tamasha hilo.

Aliyataja matukio ambayo yatatangulia kabla ya kufanyika kwa Tamasha hilo ni Utalii wa Matibabu (Tourisim Clinic) ambapo wananchi watapata matibabu bure ya utalii na kutakuwepo na madaktari ambao watachunguzi wananchi wenye changamoto za magonjwa mbalimbali .

“Hii itafanyika kwa ajili ya wananchi wa Same na hata wale ambao watakuwa wamewahi mapema kwa ajili ya tamasha hili nao watanufaika na huduma hiyo wakati wakisubiri kuanza kwake”alisema

Mkuu huyo wa wilaya alisema kwamba katika kuelekea Tamasha hilo Desema 18 mwaka huu kutakuwa na treni itakuwa inatokea Dar kwenda wilaya ya Same kwa ajili ya utalii itakuwa imebeba watalii wa kitanzania na wengine kutoka nje ambapo itaanza safari zake Desemba 18 jioni na watafika Desemba  19 asubuhi.

“Lakini pia kutakuwa na mabehewa manne  kwa watalii wanaokuja ,behewa la nyama choma,vinjwaji na michezo aina mbalimbali kwa watoto ili watoto wasiboreke wawe na eneo lao la michezo na kutakuwa na mabehewa la mziki mpaka watakapofika same Desema 19 tayari kuanzia utalii 20 hadi 22”Alisema

Aidha alisema wameona utalii waubadilishe kidogo na wapo watakaokuja kwa njia ya magari ambapo Desema 20 kutakuwa na uzinduzi rasmi wa tamasha wataenda kutalii kwenye hifadhi ya Mkombazi na jioni watarudi kutakuwa na mkesha kwa ajili ya watalii mbalimbali  kupata burudani kutoka kwa wanamuziki mbalimbali watatumbuiza .

 

Mkuu huyo wa wilaya alisema katika kunogesha Tamasha hilo Desema 21  mwaka huu idadi ya watu wameongezeka kutoka 2000 kipindi kilichopita  na wanatarajiwa kuongezeka kufikia watu 20,000 kwa sababu wameongeza kipengen za marathon.

Alisema katika watu watakimbia kuanzia Kilomita 21,Kilomita 10  na Kilomita 5  na wengine watakwenda kutalii mlima Kidenge ambao ni mlima mzuri unaofanana na ukuta mmoja uliojengwa nchini china upo wilayani humo ambao ulifufuliwa hivi karibuni na wizara wameridhia uwe kivutio cha utalii.

Akizungumzia mlima huo alisema ni mzuri na unakona nzuri na Rais Dkt Samia Suluhu amewajengea barabara nzuri ili kuwezesha watalii kuweza kufika bila kuwepo kwa changamoto huku akitaja kivutio kingine kuwa ni upepo mkali na mlima shengena uliopo kwenye Hifadhi ya Msitu wa Chome una vivutio vingi  vya utalii kuna ndege ambao hawapatikana duniani ilisopokuwa huko shengena.

Alisema pia kuna chura ambaye hapatikana sehemu yoyote duniani na watu wataendelea na burudani ya mziki kutoka kwa wasani mbalimbali ambao watatumbuiza kwenye siku hiyo niwakaribishe watanzania wote kwa ujumla

“lakini pia kutakuwa na mabanda mbalimbali ya maonesho yataaandaliwa kwa ajili ya tamasha hilo litafanyikia same mjini na Marathon zitaanza hapo na kutakuwa na bidhaa mbalimbali zitakazonyeshwa na watalii”Alisema

“Lengo la Tamasha hili ni kumuunga mkono Rais Dkt Samia Suluhu tunavyofahamu aliweza kutangaza vivutio vya utalii nchini na kuweza kuingiza fedha za kigeni kupita Filamu ya The Rayal Tour sisi hapa Same tumebaini vipo vivutio vya utalii ambavyo havijatangazwa na hivyo kutumia nafasi hiyo kuzitangaza”Alisema

Hata hivyo alisema lengo pia ni wananchi wa wilaya ya Same wainuke kuichumi kupitia Same Utalii Festivali na hivyo kuinua kipato cha wajasiriamali,wamiliki wa hoteli,mama ntilie ,bodaboda na kuna bidhaa zinazotokana na utalii uliopo same nao wenyewe watapata fedha na hivyo kuinuka kiuchumi.


“Wananchi wamehamasika sana baada ya kufanyika lile tamasha la kwanza ambalo lilifanyika na hivyo kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa wana nchi na kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta ya utalii kuweka Same kwenye Mahoteli muhimu “Alisema

Akizungumza namna tamasha hilo lilivyoongeza idadi ya utalii alisema kabla wajaanza Same Utalii Festival takwimu zilionyesha katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi idadi ya watalii walikuwa kati ya 3,000 hadi 7,000 kwa mwaka.

Alisema baada ya tamasha kufanyika kwa mujibu wa takwimu za Hifadhi hiyo  watalii wameongezaka kutoka 3,000 hadi 7,000 hadi kufikia elfu 9,000 na wamebaini lazima kuwepo na hotel nyingi za kutosha hivyo kuwahamaisha wawekezaji kuwekeza kwenye wilaya hiyo ili huku akieleza hotel mbili zimejengwa kupitia uhamasishaji huo eneo la Shengena na jengine kwenye lango la hifadhi ya Mkomazi.