ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 14, 2015

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014-2015

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani nchini,Dk. Charles Msonde akizungumza na wanahabari jijini dar leo.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Shule za sekondari za binafsi zaongoza 10 bora matokeo ya mtihani wa  kidato cha nne uliofanyika mwaka jana.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam,Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani nchini  (NECTA),Dk.Charles Msonde amesema katika matokeo ya kidato cha nne ya mtihani wa mwaka jana ufaulu umeongezeka  kwa asilimia 12.67 ikilinganishwa na mwaka 2013.

Katika matokeo hayo msichana wa shule ya sekondari ya Baobab ,Nyakaho I. Marungu ndio aliyeongoza mtihani huo na kufatia wavulana.

Shule za Sekondari za St.Fransis ya mkoani Mbeya wanafunzi sita na Feza wanafunzi nane na kufanya shule hizo kuingia katika 10 bora kwa kutoa idadi wanafunzi wengi ikilinganishwa na shule zingine.

Msonde amasema matokeo hayo  yanatokana na mfumo mpya  wa GPA kwa kuangalia masomo saba  hivyo ufaulu umetokana na mfumo huo.



SIMU YASABABISHA AJALI.

 WATU arobaini wamejeruhiwa katika ajali mbaya ya basi la abiria lililoacha njia na kupinduka eneo la kijiji cha Bulalu, kata ya Nyanguge wilayani Magu mkoani Mwanza.

Taarifa za awali zilizotolewa na Diwani wa kata ya Nyanguge wilayani Magu, Hillali Elisha, zilieleza kuwa basi hilo lenye namba za usajili T891DAK liliacha njia na kupinduka likitokea Sirari mkoani Mara likielekea jijini Mwanza.
 "Chanzo cha ajali kimedaiwa kuwa ni mwendo kasi lakini baadhi ya abiria walidai dereva wa gari hilo alikuwa akiongea na simu ya mkononi na mbele kulikuwa na gari dogo la abiria (daladala) ambapo lilipunguza mwendo ambao dereva wa basi hakuustukia kwa kukosa umakini hivyo kwa kasi aliyokuwa nayo ilimlazimu kulikwepa" alisema.

Elisha alisema baada ya kulikwepa daladala hilo, gari hilo lilimshinda na hivyo kuacha njia kisha kupinduka mara mbili na kusababisha majeruhi 40 ambao baadhi wamevunjika miguu, mikono na kuumia sehemu mbalimbali milini, hakuna aliyepoteza maisha. 
Baadhi ya abiria waliopata majereha kwenye ajali hiyo wakiwasiliana na ndugu zao kwa simu.
Wananchi wakiangalia kama kuna abiria wenye kuhitaji msaada waliosalia.
Hali halisi.
Eneo la tukio.
Diwani Elisha amewataka madereva kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani kujiepusha na ajali zinazoepukika ikiwa ni pamoja na kudhibiti mwendo kasi wa vyombo vyao vya usafiri.

Pia amewapongeza wananchi wa eneo la kitongoji cha Bulalu katani Nyanguge kwa kufika eneo la tukio kwa wakati na kutoa msaada kwa abiria huku wakiweka ulinzi wa mizigo ya abiria jambo ambalo limedhihirisha uzalendo mkubwa walionao.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA MISA MAALUM YA KUMUOMBEA MAREHEMU EVODIUS WALINGOZI KANISA LA MTAKATIFU JOSEPH DAR ILIYOONGOZWA NA MWADHAMA POLICARP KADINALI PENGO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaliamia na Askofu Eusebius Nzigilwa, wakati wa Misa maalum ya kumuombea Marehemu Evodius Walingozi, iliyofanyika leo Feb 14 kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na baadhi ya waumini wa dini ya Kikristu wakati wa Misa maalum ya kumuombea Marehemu Evodius Walingozi, iliyofanyika leo Feb 14 kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaliamia na Mwenyekiti wa Bodi ya Madini Wizara ya Fedha Richard Kasesela, wakati walipokutana katika Misa maalum ya kumuombea Marehemu Evodius Walingozi, iliyofanyika leo Feb 14 kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam. Katikati yao ni Mwenyekiti wa Kanisa hilo, Paul Mzuka. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mwenyekiti wa Kanisla la Mtakatifu Joseph, Paul Mzuka, baada ya kuhudhuria Misa maalum ya kumuombea Marehemu Evodius Walingozi, iliyofanyika leo Feb 14 kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam. Picha na OMR 

KITU KIPYA KABISA KUTOKA KWA ISHA MASHAUZI “NIMPE NANI” …NI ZOUK RHUMBA LENYE UTAMU WA MASAUTI

ZAIDI BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
Wala hakosei kusema ‘kujua kazi ni raha’. Isha Mashauzi anashuka tena kivingine na wimbo mpya kabisa uitwao “Nimpe Nani” unaodhihirisha kuwa anaijua vema kazi yake.

Hii ni ‘single’ yake ya pili nje ya taarabu ukiiacha wimbo wake wa  kwanza “Nimlaumu Nani” uliopigwa katika miondoko ya rhumba. 


“Nimpe Nani” ni wimbo unaoelea kwenye miondoko ya zouk rhumba lakini ukikolezwa kwa mbali na vionjo vya mduara.


Wimbo huo wa dakika tatu na nusu ambao umerekodiwa katika studio za C9 Records chiniya producer C9 Kanjenje, Kinanda kimepigwa na Kali Kitimoto na C9, magitaa ya bass na solo yamepigwa na Babu Bomba wa Malaika Band. 


Sauti zote tamu unazozisikia humo ni za Isha Mashauzi kasoro sehemu ndogo sana isiyozidi sekunde 5 iliyo itikiwa na Easy Man.

Friday, February 13, 2015

WANANCHI WA MAENEO YA KATA YA IGOMA WAANZA KULIPWA FIDIA KUPISHA UJENZI WA MAEGESHO YA MAGARI.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Halifa Hida,
NA PETER FABIAN 
GSENGO BLOG 
MWANZA.

HALMASHAURI ya Jiji la Mwanza, litatumia kiasi cha zaidi ya Shilingi milioni 500 kuanza kuwalipa fidia wananchi 47 wa maeneo ya Kata ya Igoma jirani na makaburi ya waliokufa katika ajari ya Meli ya MV  Bukoba ili kupisha eneo hilo kujengwa maaegesho ya magari makubwa na daladala. 

Akizungumza na leo Ofisini kwake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Halifa Hida, alisema kwamba tayari Jiji hilo kuanzia Februari 9 mwaka huu limeanza kuwalipa fidia wananchi wa maeneo hayo waliofanyiwa uthamini kwa mujibu wa taratibu na sheria za ardhi na mipango miji.

“Halmashauri ya Jiji tumeanza kulipa fidia wananchi hao kutokana na kupatikana kwa fedha kiasi cha Sh. 500.84 milioni,  hii inatokana na wananchi wa maeneo hayo kufanyiwa uthamini na kuzuiliwa kuyaendeleza maeneo yao kwa muda murefu jambo ambalo limekuwa likisababisha wananchi kuilaumu Halmashauri,” alisema.

Hida alisema kwamba wananchi wanaolipwa fidia ni wale waliokwenye orodha na waliofanyiwa uthamini Septemba 9 mwaka 2014, watalipwa kulingana na eneo la kila mmoja, Halmashauri ilipofanya zoezi hilo lakini ilishindwa kuwalipa kwa wakati wananchi hao kutokana na kukosa fedha baada ya kumaliza kufanya uthamini.

“Wananchi hawakutuelewa kabisa kila tulipokuwa tukiwaeleza wavute subira, pia tuliwaeleza Serikali haiwezi kukataa kulipa fidia halali kwa wananchi wake zaidi itachelewesha tu, hali hii ilionyesha kuwa kero na kusababisha wananchi kila mara kulalamikia halmashauri,”alisema.

Aidha Mkurugenzi Hida, alisema kwamba wananchi ambao wameanza kuchukua malipo ya fidia zao wanapaswa kuachia maeneo hayo ili kuwezesha kuanza mchakato wa mradi wa ujenzi wa kituo kikubwa cha maengesho ya magari makubwa ya mizigo na daladala ili kuwezesha magari makubwa ya mizigo kutoingia katikati ya mji.

“Jiji letu linakabiliwa na changamoto ya msongamano wa magari hali iliyopelekea kuangalia jinsi ya kupunguza ikiwa ni pamoja na kuanzisha maegesho ya magari makubwa (Teminor Track) ili kuzuia magari hayo ya mizigo kuingia katikati ya Jiji lakini pia tutajenga kituo cha daladala ili zisiegeshe barabarani kama ilivyo sasa,”alisema.

Hida alitoa wito kwa wananchi wa maeneo yote yaliyofanyiwa uthamini kufika na vielelezo ambavyo vitawawezesha kulipwa fidia kwa kila mwananchi aliyeguswa, pia rai yangu kwa wananchi ni kuhakikisha wanaondoka badala ya kuchukua fidia kisha kusubili kuondolewa kwa nguvu jambo ambalo si vyema likajitokeza.

BAADA YA OMAN, SKYLIGHT BAND KUNOGESHA VALENTINE’S DAY NDANI YA THAI VILLAGE JUMAMOSI HII USIKOSE

IMG-20150210-WA0115

DSC_0002
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 (wa pili kulia) akiongoza vijana wake kutoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar. Kutoka kushoto ni mwimbaji Baby, Ashura Kitenge pamoja na Sam Mapenzi.
Ijumaa hii Skylight Band hawatopiga Thai Village watakua njiani wakitokea nchini Oman, wanaomba radhi kwa usumubufu wowote utakaojitokeza kwa wateja wao.

Ila siku ya Jumamosi siku ya wapendanao (Valentine's Day) Skylight Band wataporomosha burudani ya nguvu na ya aina yake kwa mashabiki wao ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar huku mashabiki wakipata fursa ya kuchagua nyimbo wazipendazo zinazoendana na siku hiyo maalum pamoja na kugawa zawadi kwa "couples" itakayonoga na kutokelezea.
DSC_0011
I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I, Love You, (Aiyayaaaaa)...I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I Love You,.....(Aiyayaaaaa)...Mmm Take Me,....Nitembee Nawe,.....Baby Take Me, Nitembee Nawe....Aneth Kushaba AK47 akipiga kolabo na Sam Mapenzi.
DSC_0029
Kikosi kazi cha Skylight Band wakisakata lisebene.
DSC_0035
Moja ya zawadi ndani ya usiku maalum wa Valentine's ni hii Membership card aliyoshika mdau Francis Machibya, ambayo inakupa nafasi ya kuhudhuria show zote za Skylight Band zinazofanyika Thai Village bure kwa mwaka mzima.
DSC_0134
Mashabiki wa Skylight Band wakicheza moja ya style inayofahamika kama "Yachuma chuma".
DSC_0177
Sehemu ya umati wa mashabiki wa Skylight Band wakisebeneka.
DSC_0168
Ni mwendo kusebeneka.
DSC_0042
Ashura Kitenge akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) huku akipewa sapoti na Aneth Kushaba AK47 pamoja na Baby.
DSC_0023
Wadau wakinywa na ku-enjoy muziki mzuri wa Skylight Band.
DSC_0069
Sam Mapenzi akikonga nyoyo za mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita huku akipewa sapoti na John Music pamoja na Sony Masamba....Usikikose Jumamosi hii Valentine's day Thai Village watakinukisha.
DSC_0147
Sam Mapenzi akiongoza mashabiki wa Skylight Band kwa style ya aina yake.
DSC_0149
Hapooooo...
DSC_0151
Sony Masamba akijimwaga na shabiki wake kwenye dancing floor.
DSC_0295
Mpaka chini...
DSC_0171
Katika kupika mziki mzuri wa Skylight Band ukanoga basi huyu jamaa James Kibosho, anahusika sana na hivi sasa ametua Skylight Band.
DSC_0175
Kiungo kingine chenye vipaji lukuki si mwingine ni Danny Kinanda akifanya yake.
DSC_0083
Burudani ikiendelea.
DSC_0191
Burudani ikiendelea.
DSC_0194
Pale mzuka wa mashabiki unapopanda.
DSC_0205
Kwa matukio mengi zaidi ingia hapa

MABONDIA MCHUMIATUMBO NA IDI BONGE WAPIMA UZITO KUPIGANA FEB 14 P.T.A SABASABA

Bondia Iddi Bonge kushoto akitunishiana misuli na Alphonce mchumiatumbo baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika feb 14 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Dar es salaam siku ya jumamosi.
Bondia Vicent Mbilinyi.
Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana masuli na Halidi Manjee baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika feb 14 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Dar es salaam.

Bondia Iddi Bonge kushoto akitunishiana misuli na Alphonce mchumiatumbo baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika feb 14 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Dar es salaam siku ya jumamosi.
Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana masuli na Halidi Manjee baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika feb 14 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Dar es salaam picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu
MABONDIA wa uzito wa juu wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa taifa mabondia hawo ni Iddi Bonge na Alphonce mchumiatumba ambao watapanda uringoni siku ya feb 14 katika ukumbi wa P.T.A sabasaba kwa ajili ya kumaliza ubishi
ambao umetanda mitaani ni nani bingwa wa uzito wa juu nchini ambapo kwa mda mrefu akuna bingwa wa uzito huo katika upimaji wa uziti zilizogubikwa na tambo mbalimbali za mashabiki waliojazana kushidia upimaji wa uzito 

mpambano huo wa raundi kumi utakuwa ni wa aina yake kwa kuwa kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi ambapo bondia Iddi Mnyeke atapambana na Yonas Sego nae Alidi manjee atakabiliana na bondia chipkizi anaekuja kwa kasi katika ulimwengu wa masumbwi Vicent Mbilinyi wakati Shabani Kaoneka atamkabili Saidi Mbelwa, na Deo Samweli akipambana na Adam Ngange Juma fundi atakabiliana na Bakari Ostadhi na Amani Bariki 'Manny Chuga' atapambana na Mohamed Kashinde 
 

Manyoka aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha ndani na nje ya ukumbi huo ambapo amesha wasiliana na walinzi mbalimbali
siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali

Na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

PRODUCER WA MO-MUSIC NA BARAKA DA PRINCE AACHIA NGOMA YAKE MPYA.

MTAYARISHAJI wa muziki  na mtunzi wa nyimbo kutoka studio za K-Records za jijini Mwanza Goodluck Gozbert aka 'Lollypop' ambaye ndiye mwandishi wa wimbo wa Mo Music Basi Nenda  na ule wa mpya wa Baraka Da Prince unaoitwa 'Siachani nawe' na nyingine nyingi, hatimaye ameamua kuchomoka kivyake kuonyesha umma kipaji alichonacho cha uimbaji kwa kufyatua mpini wenye hisia unaoitwa 'Acha waambiane'.

Akizungumza na GSengo Blog Lollypop amesema kuwa hii siyo track yake ya kwanza kuitoa hewani kwani muziki ndiyo chachu kwake kuwa  Mtayarishaji hii leo, akianzia kama mwimbaji wa muziki wa Injili kupitia kwaya kanisani, kundi na mwimbaji solo hatimaye hii leo Mtayarishaji mkubwa wa muziki tena wa kuaminika.

"Wimbo 'Acha waambiane' umebeba ujumbe wa kufariji wale wote wanaokutana na changamoto mbalimbali za maisha iwe ni kufukuzwa kazi, kukosa mtoto, changamoto za elimu, maradhi na kadhalika kiufupi wimbo unagusa kiroho zaidi" alisema Lollypop

Lollypop anawashukuru watanzania kwa kumpokea vyema katika Utayarishaji muziki kupitia nyimbo kadhaa zilizokubalika kitaifa na kimataifa zika-Hit zikiwemo zile alizo andika na hata kuwatayarishia wasanii wakali kama Baraka Da Prince na Mo Music, kwani zimempa kujiamini na changamoto zaidi ya kufanya makubwa katika fani.

BOFYA PLAY KUSIKILIZA SINGLE YAKE MPYA.

Thursday, February 12, 2015

AIRTEL YATANGAZA KUFANYA DROO YA WIKI YA PILI YA PROMOSHENI YA 'Airtel Yatosha Zaidi'

Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akiongea na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa kuitambulisha promosheni ya Airtel yatosha zaidi kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma,  uliofanyika katika Dodoma Hoteli. pichani ni Afisa Masoko wa Airtel Bi Rebecca Mauma.
Afisa Masoko wa Airtel Bi Rebecca Mauma na waandishi wa habari wakati wa kuitambulisha promosheni ya Airtel yatosha Zaidi kwa wakazi wa Dodoma, akishuhudia ni Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde.
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akijadili na waandishi wa habari kuhusu promosheni ya Airtel yatosha zaidi wakati wa mkutano wa kuitambulisha promosheni hiyo kwa wakazi wa mkoa wa Dodoma
Airtel Yatangaza kufanya droo ya wiki ya pili ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kufanya droo ya wiki ya pili ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi siku ya kesho Ijumaa tarahe 13 februari 2015 ambapo washindi 7 wa  gari aina ya Toyota IST watapatikana na kutangazwa
Akiongea na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa kuitambulisha promosheni ya Airtel yatosha zaidi kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma,  uliofanyika Dodoma Hoteli, Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde alisema” kama ilivyo kawaida tunazunguka katika mikoa mbalimbali kutoa elimu juu ya huduma na bidhaa zetu  pamoja na kuitambulisha promosheni hii ya Airtel Yatosha Zaidi tuliyoizindua hivi karibuni inayo wapa wateja wetu na watumiaji wa vifurushi vya Airtel yatosha nafasi ya kujishindia gari aina ya Toyota  IST kila siku
Mpaka sasa tunao washindi watatu waliopatikana na Tayari wawili wamekabithiwa magari yao akiwemo Mwajuma Churian Mkazi wa Dar es saalam aliyekabithiwa gari lake siku ya Jumanne na leo Alhamisi tunakabithi gari kwa mwalimu mstaafu mkazi wa Mtwara Bwana Namtapika Kilumba . Mshindi wa tatu aliyetangazwa ni Bwana Ramadhani Dilunga ambaye ni Mkulima anatokea  mkoa wa Pwani.
Nachukua fulsa hii kuwajulisha watanzania kuwa droo ya wiki ya pili ya promosheni hii inategemea kufanyika kesho siku ya Ijumaa ambapo washindi saba watapatikana na kutangazwa, tunaomba wateja wakae karibu na simu zao  na watapigiwa simu za kutangiziwa ushindi huo toka namba 0684291105 ambapo Watanzania na wateja wetu 7 kesho wataondoka na Toyota IST.”
Napenda kutoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na vifurushi hivi vya Airtel yatosha kufanya hivyo kwa kupiga *149*99# , au kununua vocha za Airtel yatosha au kununua vifurushi hivi kupitia huduma ya Airtel Money sasa.  Kila mtanzania na mtumiaji wa huduma ya Airtel yatosha ataingia kwenye droo na kupata nafasi ya kujishindia hivyo ni wakati kwa wakazi wa Dodoma na mikoa mingine ya Tanzania kuchangamkia fulsa hii. Aliongeza Matinde
Airtel Yatosha Zaidi ni promosheni iliyozinduliwa na kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel mwanzoni mwa mwezi wa pili mpaka sasa watanzania wameendelea kubahatika kwa kujishindia magari aina yaToyota IST, promosheni hii itadumu kwa muda wa miezi miwili.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA BALOZI WA SAUDI ARABIA ANAYEMALIZA MUDA WAKE NCHINI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Balozi wa Saudi Arabia, Hani Abdullah Mominah, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo Feb 12, 2015 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia, Hani Abdullah Mominah, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo Feb 12, 2015 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na  Balozi wa Saudi Arabia, Hani Abdullah Mominah, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika wakati  Ofisini kwa Makamu Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo Feb 12, 2015 wakati Balozi huyo alipofika kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini. Picha na OMR