




Katika mchezo huo wa pili Taqwa waliondoka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Buswelu (pichani).
Kwenye mchezo wa awali leo nayo Nsumba Sekondari imeibamiza timu yenye majigambo mengi vijana wa mjini Mwanza Sekondari 1-0
Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano hayo mkoa wa Mwanza Job Mushumba amesema kuwa michezo ya ligi hiyo katika hatua inayofuata itachezwa kwa njia ya mtoano yaani Fist looser kucheza na Second looser kupata mshindi wa tatu na First winner kucheza na Second winner kumpata bingwa wa kituo cha Mwanza,
Michezo yote hiyo inataraji kuchezwa jumamosi ya wiki hii kiwanja nitakwambia papahapa.
Chini ya ulinzi: Kulia ni mfanyakazi wa meli hiyo
Mchezo huo mchafu ulistukiwa na mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza bwana Kitana, ambaye pia ana miliki vyombo vya usafirishaji na uvuvi ziwani Victoria, mara baada ya kuona mazingira yasiyoeleweka alito taarifa kwa wamiliki wa meli ya Mv. Allez ambao kwa haraka walipanga mchakato wa mtego na siku iliyofuata walifanikiwa kushuhudia wizi huo mwanzo mwisho live bila chenga jinsi unavyochezwa.
Watuhumiwa hao katika mahojiano wamesema kuwa wamekuwa wakijihusisha na mchezo huo kwa kipindi kirefu wakishirikiana na wafanyakazi wa meli hiyo nao hufanya zoezi hilo nyakati za usiku pindi meli zinapotoka safari, kwa kufyonza mafuta yaliyosalia mara baada ya meli kutoka safarini na hili hufanyika kabla meli haijaandikiwa mafuta kwa safari inayofuata.
Wezi hao wakiwa na boti yao maarufu yenye jina la upako ‘ASANTE MUNGU’ waliokutwa wakifyonza mafuta hayo kiulaini, huku jumla ya madumu 140 yakinaswa mengine yakiwa tayari yameshibishwa mafuta huku mengine yakiwa kwenye foleni.