ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 20, 2016

RIDHIWANI AWAPIGA TAFU WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA SKONDARI BAGAMOYO.

NA VICTOR MASANGU, BAGAMAYO PWANI.
KATIKA kuunga mkono  juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu hapa nchini Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kwa kushirikiana na shirika lisilokuwa la kiserikali la KULEA Child Care Villages wametoa msaada wa vitabu 3468 vya kujifunzia masomo ya sayansi na hisabati katika shule za msingi na sekondari vyenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni 70.
Akikabidhi  msaada huo wa vitabu kwa Mwalimu mkuu shule ya sekondari Mdaula , Melkisedek Komba ambaye aliyepokea vitabu hivyo kwa niaba ya wakuu wa shule nyingine Ridhiwani amesema kwamba vitabu hivyo vitaweza kuleta mabadiiko makubwa katika Nyanja ya elimu hususan katika masomo ya sayansi na ufaulu utaweza kuongezeka.
MSIKILIZE MHE. RIDHIWANI KIKWETE

Aidha Ridhiwani amesema vitabu hivyo vitagawanywa katika tarafa tano zilizopo kwenye halmashauri ya Mji wa Chalinze ambapo tarafa ya Chalinze imepatiwa vitabu 998 na tarafa nne za Msoga, Miono, Msata na Kwaruhombo zitapata vitabu 610 kwa kila tarafa na kuwataka wanafunzi na walimu kuwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao mashuleni.
MSIKILIZE MBUNGE  



Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Mdaula Melkisedek Komba amesema msaada huo wa vitabu utaweza kuleta mabadiliko chanya kwa kuongeza kiwango cha ufaulu kwa  wanafunzi hasa katika masomo ya sayansi kwani hapo awali walikuwa wanakabiliwa na  uhaba wa vitabu vya kufundishia.
MSIKILIZE MWALIMU MKUU

Mariam Bofi ni mmoja wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari Mdaula kidato cha tatu akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake ametoa shukrani kwa Mbunge pamoja na Shirika hilo na kusema kuwa vitabu hivyo vitaweza kuwasaidia zaidi kujisomea katika masomo ya sayansi kwani hapo awali walikuwa na changamoto ya uhaba wa vitabu.
MSIKILIZE MWANAFUNZI

SHULE za msingi na sekondari katika Jimbo la Chalinze kwa sasa bado zinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa vitabu vya kufundishia masomo ya sayansi hivyo kutolewa kwa msaada huo utakuwa ni mkombozi mkubwa wa kuleta mabadiliko na kuongeza kiwango cha  ufaulu zaidi kwa wanafunzi katika masomo  hayo ya sayansi.

MBARAKA YUSUPH AOKOA JAHAZI CCM KIRUMBA LEO, TOTO AFRICANS IKITOKA SARE YA BAO 1-1 DHIDI KAGERA SUGAR.

Na Faustine Ruta, Mwanza
TIMU za Toto Africans na Kagera Sugar zimetoka sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, ambapo Toto Africans ilitangulia kufunga bao dakika ya 24 mfungaji akiwa Japhary Vedastus. 

Mfungaji alimalizia kazi nzuri ya Miraji Athumani kabla ya Kagera kusawazisha dakika ya 66 mfungaji akiwa Mbaraka Yusuph. 

BOFYA PLAY KUSIKIA TAARIFA YA JEMBE FM.Kikosi kilichoanza cha Timu ya Toto Africans cha Jijini Mwanza dhidi ya Kagera Sugar
Kikosi kilichoanza cha Kagera SugarTayari kipute kuanzishwa
Baadhi ya Viongozi wa Timu ya Toto Africans

Kipute kikiendelea ....patashika kwenye Lango la Timu ya Toto baada ya kupigwa kona leo kwenye mchezo wao a Ligi Kuu Vodacom ambapo wameumaliza kwa sare ya bao 1-1.Baadhi ya Mashabiki walioingi CCM Kirumba leo
Kipindi cha kwanza Baadhi ya Wachezaji wa Timu ya Kagera Sugar wakiwa vichwa chini baada ya kupigwa bao 1-0 na Toto ya hapa Jijini Mwanza
Wachezaji wa Kagera wakiwa hoi na huku wakijiuliza jinsi gani waweze kuikomesha Timu ya Toto kwenye Uwanja wao.Kocha wa Kagera Sugar Mohamed Richard maarufu kwa jina la Adolph akiwa kwenye wasiwasi baada ya Timu yake kuwa nyuma ya bao 1-0 katika kipindi cha kwanza bao lililofungwa dakika ya 24. Picha na Faustine RutaWachezaji wa Toto wakipongezana kwa baoKipindi cha pili Kocha aliwapa somo na wakaweza kutumia nafasi na kusawazisha bao hilo

Wachezaji wa Kagera Sugar walifanya mikakati na kuongeza bidii katika kipindi cha pili na kuweza kusawazisha bao.

Chupuchupu!!
Mbaraka Yusuph akipongezwa kwa bao la kusawazisha
Shangwe za kusawazisha bao!
Mbaraka Yusuph akipongezwa kwa bao la kusawazisha na wenzakeMchezaji wa Kagera Sugar akishangilia bao ambalo muda mchache lilikataliwa na Mwamuzi na kama si kukataliwa lingelikuwa la pili kwa Kagera.
Mh. Nassoro Amduni kutoka Kigoma(kushoto) ndie aliyekuwa Kamisaa wa Mtanange wa leona kulia ni Bw. Malick Tibabimale Katibu wa chama cha Soka Wilaya ya Bukoba nae alikuwepo Uwanjani hapo kushuhudia kipute.
Waandishi wa Habari wakifanya mahojiano na Kocha Mkuu wa Timu ya Kagera Sugar mara baada ya mechi kumalizika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba. Picha na Faustine RutaWaandishi wa Habari wakifanya mahojiano na Kiongozi wa Timu ya Toto Africans mara baada ya mechi kumalizika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI TBC.

Rais Magufuli afanya uteuzi wa mwenyekiti mpya wa bodi ya shirika la utangazaji nchini TBC:  

YANGA ‘WAJIHALALISHIA’ SIMBA SC, WAICHAPA 2-0 TAIFA, HII HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU 1999

Msimu wa 1999, wakati huo Ligi Kuu inadhaminiwa na bia ya Safari Lager inayotengenezwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Yanga iliichapa Simba 3-1 Mei 1, 1999 mabao ya Idd Moshi, Kali Ongala na Salvatory Edward la wapinzani likifungwa na Juma Amir Maftah, wakati marudiano wana Jangwani wakashinda 2-0 Agosti 29, 1999 mabao ya Bakari Malima ‘Jembe Ulaya’ na Mohamed Hussein 'Mmachinga'.


Katika mchezo wa leo, Simba SC ilipata pigo mapema tu dakika ya 24, baada ya beki wake wa kati, Abdi Banda kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na refa Jonesia Rukyaa wa Kagera kwa kumchezea rafu Ngoma.
Mshambuliaji wa Zimbabwe, Ngoma akaifungia Yanga SC bao la kwanza dakika ya 39, akitumia makosa ya beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Kessy aliyemrudishia pasi fupi kipa wake Vincent Angban raia wa Ivory Coast.

Ngoma aliye katika msimu wake wa kwanza Yanga SC, baada ya kusajiliwa kutoka Platinum FC ya kwao, aliiwahi pasi ya Kessy kabla haijamfikia Angban na kumlamba chenga kipa kisha kufunga.

Simba SC walitulia baada ya bao hilo na kucheza kwa tahadhari, wakiendelea kushambulia langoni mwa Yanga SC na kupata kona mfululizo, ambazo hawakuweza kuzitumia kupata bao.

Kipindi cha pili, mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mganda, Jackson Mayanja kumtoa kiungo Mwinyi Kazimoto na kumuingiza beki Nova Lufunga, yaliidhoofisha safu ya kiungo ya timu hiyo na kuwafanya Yanga waanze kutawala mchezo.

Krosi maridadi ya winga Godfrey Mwashiuya kutoka upande wa kushoto iliunganishwa nyavuni kwa guu la kulia na Mrundi Tambwe dakika ya 72 kuipatia Yanga SC bao la pili.

Pamoja na kuwa nyuma kwa 2-0, Simba SC waliendelea kufikisha mipira kwenye eneo la hatari la Yanga, lakini hata hivyo leo safu yake ya ulinzi iliyoongozwa na Vincent Bossou na Mbuyu Twite ilikuwa makini.

Vikosi vilikuwa;
Yanga SC: Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Mwinyi Hajji Mngwali, Pato Ngonyani, Deus Kaseke/Godfrey Mwashiuya dk64, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Haruna Niyonzima/Simon Msuva dk52.

Simba SC: Vincent Angban, Hassan Kessy, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murushid, Abdi Banda, Justice Majabvi, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto/Novat Lufunga dk46, Hamisi Kiiza/Danny Lyanga dk59,Ibrahim Hajib/Brian Majwega dk80 na Said Ndemla.
MWANZA
Kipute cha dimba la CCM Kirumba Mwanza ni Toto Vs Kagera Sugar 1-1.
Kocha wa timu ya Kagera Sugar Adolf Richard akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza mara baada ya mchezo baina ya timu yake dhidi ya Toto Africans ambapo timu hizo  zimetoka sare ya kufungana 1-1
Kocha wa timu ya Toto Africans ya jijini Mwanza John Tegete akizungumza na waaandishi wa habari baada ya mchezo.
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo, Toto Africans imelazimishwa sare ya 1-1 na Kagera Sugar Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. ZAIDI KILICHOJIRI BOFYA PLAY


Azam FC imeichapa Mbeya City maabo 3-0 Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, mabao ya Kipre Herman Tchetche, John Raphael Bocco na Farid Mussa.

Azam FC inafikisha pointi 45 kwa ushindi huo, baada ya kucheza mechi 18 na kupanda hadi nafasi ya pili, ikiizidi Simba kwa wastani wa mabao. 

Mechi nyingine; Mgambo JKT imetoa sare ya 1-1 na Prisons Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Stand United imetoka 1-1 na JKT Ruvu Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na 

"TRANSCATHETER " NJIA SALAMA ZAIDI KWA TATIZO LA TUNDU LA MOYO KWA WATOTO




DK. C.S Muthukumaran, mtaalamu wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka hospitali za Apollo.

Na Mwandishi Wetu,

Watoto wachanga wanaozaliwa na tatizo la tundu kwenye moyo, linalosababishia kudumaa katika ukuaji wao na hata kuwa na matatizo ya moyo wanashauriwa kupata matibabu ya kuziba tundu hilo kwa njia ya mrija bila kufanyiwa upasuaji. Hayo yamesemwa na DK. C.S Muthukumaran, mtaalamu wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka hospitali za Apollo.

(VSD) ni tundu katika ukuta unaotenganisha ventriko ya upande wa kulia na kushoto katika moyo. Ni tatizo linalotokea mara nyingi wakati wa kuzaliwa kwa mtoto na linaweza tokea lenyewe au kama ugonjwa.
Ni kawaida kwa watoto wote kuzaliwa na tundu dogo katikati ya atria mbili na mara nyingi tundu hilo huziba ndani ya wiki chache. Mara nyingi hakuna tundu kati ya ventiko hizo mbili, ila baadhi ya vichanga huzaliwa na tundu hilo ambalo linakuwa ni chanzo cha magonjwa ya moyo na ndio sababu kubwa  ya watoto wachanga wengi kuonana na wataalamu wa magonjwa ya moyo.

Imezoeleka mara zote kuziba tundu hili kwa upasuaji wa moyo (operesheni), ambao unahusisha kupasua kifua, kupitisha mashine na kuziba tundu hilo. Kwa mujibu wa DK. Muthukumaran kwa miaka 10 iliyopita kumekuwa na maendeleo makubwa ya kutibu tatizo hili ambapo hospitali za Apollo wamegundua njia ya kuziba tundu hilo kwa kutumia njia ya “pini kwenye tundu” (angiogram) bila kovu lolote kifuani. Licha baadhi ya aina za tundu hilo kwenye moyo kama lile lililopo chini ya valvu za moyo ni lazima lizibwe kwa upasuaji. Makala hii inaonyesha jinsi gani tundu hilo katika moyo linaweza kuzibwa bila upasuaji au wowote.

Mtoto wa kike wa umri wa miaka 12 amekuwa na tatizo la moyo. Aligundulika akiwa na tundu katika moyo akiwa na umri wa miaka miwili. Madaktari walishauri afanyiwe upasuaji kwa sababu tundu lilikuwa karibu sana na valvu hivyo ingeweza kuharibu valvu ya moyo. Wazazi wake waliogopa suala la binti yao kufanyiwa upasuaji huo ambao ungeweza kusababisha apoteze maisha lakini pia kuwa na kovu kubwa kifuani. Waliahirisha upasuaji huo mpaka pale binti alipofikisha umri wa miaka 14. Kwa umri huo tayari lile tundu lilikuwa limeshaanza kuharibu ile valvu iliyokuwa karibu nalo.

Wazazi walikwenda hospitali ya watoto Apollo kwa ajili ya ushauri mwezi Septemba  2014. Baada ya utafiti wa kwanza madkatari walisema wanashauri tundu lile lizibwe kwa njia ya “pini” bila kufanya upasuaji. Baada ya wazazi kuelewa, walimchukua mtoto kwa ajili ya maandalizi. Hatua za maandalizi zilifanywa mtoto akiwa katika nusu kaputi (local anaesthesia). Hatua hizo zilichukua nusu saa tu. Tundu hilo lilizibwa kwa mafanikio makubwa kwa njia ya pini na katheta na mgonjwa aliruhusiwa kutoka hospitalini siku iliyofuata. Familia ilifurahi sana, kwa jinsi walivyotua mzigo mkubwa wa tatizo hilo la binti yao wa miaka 14.

Wakati wa ufuatiliaji wa maendeleo kwa muda wa mwaka mmoja, binti alikuwa akiendelea vizuri, hakukuwa na uvujaji wowote wala tatizo katika aortic na valvu za upumuaji. Tiba hii ya siku moja imemwezesha binti huyu kuepuka upasuaji katika mfumo wake wa upumuaji, kovu kubwa la maisha yake kifuani na siku 5-6 za kulala hospitali kwa ajili ya upasuaji.

Uzibaji wa tundu katika moyo umekuwa ukifanywa kwa mafanikio kwa muda wa miongo miwili. Ufuatiliaji wa maendeleo  kwa muda mrefu umeonyesha kuwa uzibaji wa tundu katika moyo kwa njia hii mpya ijulikanayo kitaalamu kama ‘Transcatheter’ ni mbadala bora wa kuepuka upasuaji. Kwa kipindi kirefu upasuaji umekua njia pekee ya kuziba tundu katika moyo. Ila ina kuwa hatarishi mara kadhaa hasa moyo kuziba kabisa, baada ya kufanyiwa upasuaji zaidi ya mara moja na hata vifo. Zaidi ya yote, matatizo ya maambukizi, mfumo wa fahamu na mapigo ya moyo kwenda kasi zaidi (tachyarrhythmia). Baada ya kufanyiwa upasuaji, kovu litadumu maisha yote. Hivyo kwa njia ya hii mpya ya kuziba tundu ni bora na salama kwa afya ya baadae.

Dk. C.S Muthukumaran ametoa maoni yake kwamba, kurithi ni moja kati ya sababu kubwa za kusababisha tundu katika moyo. Kwa mfano, mzazi mwenye tatizo la tundu kwenye moyo ana nafasi kubwa ya kupata mtoto mwenye hali hiyo zaidi ya mazazi asiye na tatizo hilo. Watoto wenye maradhi ya kurithi kama utindio wa ubongo mara nyingi huwa na tundu katika moyo. Uvutaji sigara kipindi cha ujauzito kwa mama kumehusishwa pia kama chanzo cha matatizo haya ya tundu katika moyo wa mtoto.

Kama tatizo hilo la tundu katika moyo lisipopatiwa matibabu huwa linaweza kusababisha matatizo ya moyo, anasema Dk. Muthukumaran. Ukuaji wa tundu hilo katika moyo inaweza kusababisha moyo kushindwa kuendelea kusukuma damu, au kuwa na mapigo yasiyo sahihi, kudumaa kwa mwili hasa kwa watoto wachanga. Mtoto anashindwa kula sawa sawa na hivyo kuathiri ukuaji wake. Na matokeao yake mtoto anapungua uzito au asikue kabisa.
Katika hospitali ya watoto ya Apollo uzibaji wa tundu katika moyo kwa njia ya Transcatheter  umefanywa kwa zaidi ya watoto 300 kwa miaka 5 iliyopita kwa kutokuwa na matatizo yoyote makubwa. Zaidi ya 50% ya matatizo ya tundu la saizi ndogo mpaka yale ya wastani yamezibwa kwa njia hiyo kuingiza katheta. Ujuzi mkubwa wa madaktari, uchaguzi sahihi wa wagonjwa, mipango sawia ndio ufunguo wa mafanikio katika njia hii ya kisasa.



Kuhusu Hospitali ya Apollo

Hospitali za Apollo ni za kwanza katika eneo Asia Pacific kutoa huduma za upasuaji kwa kutumia mfumo huu wa Robot, ambayo ni aina ya upasuaji isiyokuwa na madhara. Taasisi ya upasuaji kutumia Robot iliyopo hospitalini hapo wamejitoa kipekee katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa. Taasisi ina wataalamu waliobobea kwenye mafunzo ya upasuaji, upendo katika utoaji wa huduma vifaa vya matibabu vya kisasa vinavyolenga kutoa uzoefu bora kwa mgonjwa. Vifaa hivyo ni pamoja na vifaa Robot ya Da Vinci inayotumika katika upasuaji.
Mfumo huu wa upasuaji hutumika katika teknolojia ya upasuaji wa magonjwa yanayohusiana na mfumo wa mkojo (Urology), magonjwa ya wanawake (Gynaecology), moyo, utumbo, na magonjwa ya watoto na matatizo ya uti wa mgongo

BENKI YA POSTA TANZANIA YAJENGA VYOO VYENYE THAMANI YA SH. MILIONI 4.7 KATIKA SHULE YA MSINGI MAKAMBI ILIYOPO MANISPAA YA SONGEA MKOANI RUVUMA

 Wanafunzi wa shule ya msingi ya Makambi iliyopo Kata ya Ndilima Litembo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wakifurahia vyoo vya kisasa vilivyojengwa na Benki ya Posta Tanzania.
 Meneja Mwandamizi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Benki ya Posta, Noves Moses akiongea kwenye mkutano katika shule hiyo muda mfupi kabla ya kuzindua vyoo hivyo. 
 Meneja Mwandamizi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Benki ya Posta, Noves Moses akikata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua vyoo vyenye matundu 14, vitakavyohudumia wanafunzi 850 katika shule ya Msingi ya Makambi, Songea Mkoa wa Ruvuma, ujenzi huo umegharimu shilingi milioni 4.7 kulia ni Meneja wa Oparesheni wa tawi la Songea, Simon Mlelwa.
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Benki ya Posta, Noves Moses akiwa kwenye picha ya pamoja na walimu wa shule hiyo pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya mtaa.

Na Mwandishi Wetu

MENEJA mahusiano na mawasiliano wa Benki Posta Tanzania, Noves Moses amelitaka suala la elimu bure liendane na mazingira mazuri ya kimiundo mbinu kwa wanafunzi pamoja na walimu wao ili kuifanya elimu hiyo kuwa bora zaidi.

Rai hiyo aliitoa jana wakati akizindua vyoo vya kisasa vya Shule ya Msingi ya Makambi iliyopo Kata ya Ndilima Litembo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, ambavyo vimejengwa na Benki hiyo kwa thamani ya shilingi Milioni 4.7 ikiwa ni sehemu ya mchango kwa jamii katika kuboresha mazingira ya elimu.

Akizindua matumizi ya vyoo hivyo vyenye matundu 14, Noves alisema kuwa jamii na taasisi mbalimbali zinatakiwa zitambue kuwa suala la elimu bure linatakiwa liendane na uboreshwaji wa mazingira ya wanafunzi na walimu wawapo shuleni hapo.

Alisema kuwa kumekuwepo na baadhi ya wadau wa elimu kulichukulia suala la elimu bure kama kigezo cha kutokuchangia sekta hiyo na baadala yake wanadai ni kazi ya serikali pekee jambo ambalo siyo sahihi katika uboreshaji elimu.

“Suala la elimu bure lisiwe kigezo cha wadau kushindwa kuichangia sekta hiyo kwani kufanya hivyo kunapelekea baadhi ya shule kushindwa kuwa na mazingira mazuri ya watoto kujisomea pamoja na walimu wao kutokuwa na morali ya kufundisha” alisema Meneja mahusiano .

Noves alisema kuwa Benki ya Posta Tanzania inafanya kazi kwa kiwango kikubwa na serikali hivyo imetoa misaada mbalimbali ya kijamii hasa kwa upande wa afya na elimu huku katika upande wa elimu wamechangia madawati na ujenzi wa vyoo bora vya kisasa kwenye shule mbalimbali hapa nchini .

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule hiyo, Kanisius Ngongi awali akitoa taarifa ya shule hiyo kabla ya kukabidhiwa vyoo hivyo alisema kuwa shule hiyo ina wanafunzi 850 na matundu ya vyoo yapo 14 na kuwa vyoo vyote vina maji ya kutosha.

Ngongi aliipongeza benki hiyo alisema kuwa shule hiyo kwa sasa imeshabadilika, mazingira yamekuwa bora kwa upande wa vyoo vya wanafunzi ambavyo kwa sasa hakuna shule ndani ya Manispaa hiyo yenye vyoo kama hivyo.

Mwalimu Ngongi alisema kuwa licha ya vyoo vya wanafunzi kuwa bora lakini bado kuna changamoto ya vyoo vya walimu maana vyoo walivyokuwa wakivitumia vimeshapoteza ubora wake na kuwafanya walimu hao kupata shida mahala pa kujisitili hivyo amewaomba wadau mbalimbali waweze kuchangia kama Benki ya Posta inavyojitolea.

UONGOZI WA BANDARI YA TANGA WAPEWA SIKU 16 KUTOA TAARIFA JUU YA UNUNUZI WA MATISHARI.

Waziri mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa ametoa masaa 16 kwa uongozi wa mamlaka ya usimamizi wa bandari tawi la Tanga kumpa taarifa kamili iliyosababisha kununua matishari manne yenye thamani ya zaidi dola milioni 10.1 kutoka nchini China wakati mahitaji ni matishari mawili.
Akizungumza baada ya ukaguzi wa matishari na vitendea kazi vingine katika bandari hiyo, waziri mkuu amesema serikali ilikuwa na lengo la kupunguza usumbufu na gharama kwa wateja wa bandari hiyo ambapo alimtaka mhandisi wa bandari Bwana Felix Mtui kutoa majibu ya papo kwa papo ili kuleta uwiano wa kile atakachoulizwa na majibu yake.
Hata hivyo waziri mkuu alipombana kaimu meneja wa bandari tawi la Tanga Bwana Henry Arika kuelezea utaratibu wa kuchukua mafundi kutoka nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya kurekebisha miundo mbinu ya matishari hayo na gharama zake zikoje meneja huyo alikwepa na kudai kuwa yeye ni mgeni na amekuja miezi kadhaa kukaimu nafasi hiyo.
Katika ukaguzi huo waziri mkuu aliwaagiza maofisa wa mamlaka ya mapato nchini tawi la Tanga, uongozi wa mamlaka ya bandari kwa kushirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha wanadhibiti uingizaji wa sukari kutoka Brazil ambayo imekuwa ikiingizwa nchini kinyume cha sheria bila kulipiwa ushuru na kufanyiwa ukaguzi na mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA hatua ambayo imekuwa ikiathiri soko la ndani.

Friday, February 19, 2016

WASEMAVYO MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA MWANZA KUELEKEA MCHEZO WA WATANI HAO WA JADI 20 FEB 2016.

Simba Sports Club.
Yanga Africans.

Wakati Yanga na Simba zikikutana kesho kwenye mchezo wa Ligi Kuu unaoitwa wa kisasi, siyo timu hizo tu zimeupania mchezo huo bali hata mashabiki wa timu hizo kubwa hapa nchini Tanzania.
Kutoka Mwanza hivi ndivyo mashabiki wanavyoronga pindi walipozungumza na SPORTS RIPOTI ya JEMBE FM.
Simba inayocheza mchezo wa 20 kesho, inaongoza ligi ikiwa na pointi 45, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 43 na mechi moja kiporo, Azam pointi 42 na mechi mbili za kiporo.

COOL CHARTER AJA NA PAN ME.

Kutoka kipindi cha RIDDIM ZONE kinachoruka kila Jumamosi saa 7 hadi 10 moja ya maprizenta wa pale Cool Charter tayari kesha liweka pishi lake meza ya mikito ....Nenda ukajisevie.

MSICHANA KUTOKA CHINA GUMZO MTIHANI WA TAIFA TANZANIA.

Msichana kutoka China ameibuka wa pili kwa ubora katika matokeo ya mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kushoto akiwa na mama yake.
Congcong Wang, 16, alifanyia mtihani wake shule ya upili ya wasichana ya Feza iliyoko eneo la Kinondoni, Dar es Salaam.
Bi Congcong, aliyepata alama B katika Kiswahili, anatoka jiji la Changchun katika mkoa wa Jilin nchini Uchina.
Ameambia wanahabari kwamba ameshangazwa sana na matokeo hayo.
"Sijawahi kudhani ningekuwa mmoja wa wanaoongoza. Nimekuwa nikitia bidii masomoni lakini sikutarajia hili,” amenukuliwa na gazeti la The Citizen.
Alijiunga na shule za Feza mwaka 2006 akitokea China na akalazimika kujifunza Kiswahili na Kiingereza.
Mwanafunzi bora kitaifa alikuwa Butogwa Shija, 17, kutoka shule ya wasichana ya Canosa, Dar es Salaam.
Jumla ya wanafunzi 240,996 walifanya mtihani huo wa kitaifa Novemba mwaka jana.

BONDIA FRANSIC CHEKA ATAMBA KUMDUNDA MSERBIA GEARD AJETOVIC


Bondia Fransic Cheka 'katikati' akiwa katika picha ya pozi na meneja wake, Juma Ndambile wa Kampuni ya Advanced Security Limited baada ya kuzunumzia mpambano wake na Mserbia Geard Ajetovic utakaofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 kushoto ni meneja msaidizi Nassoro Said 'mzee wa mbele.
Msanii wa bendi ya muziki wa dansi African Stars 'twanga pepeta' Luiza Mbutu kulia akizungumza na waandisho wa habari awapo pichani wakati wakitangaza mpambano wa bondia Fransic Cheka na Mserbia Geard Ajetovic utakaofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 katikati ni msanii Ally Choki na kushoto ni promta Jay Msangi.
Meneja wa Cheka ambaye pia ni Mkurugenzi wa Advance Security, Juma Ndambile kushoto akizungumza na waandishi wa habari awapo pichani juu ya mpambano wa bondia Fransic Cheka katikati kulia ni promota Jay Msangi mpambano wa Cheka na Mserbia Geard Ajetovic utakaofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27.
Bondia Fransic Cheka  kushoto akizungumza na waandishi wa habari juu ya mpambano wake na  Mserbia Geard Ajetovic utakaofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Februari 27 katikati ni meneja wake Mkurugenzi wa Advance Security, Juma Ndambile  na promota Jay Msangi.


SUPER D KUSHOTO NA FRANSIC CHEKA

Na Mwandishi Wetu

BONDIA maarufu nchini  Francis Cheka na Mserbia, Geard Ajetovic.watazipiga katika
Pambano  la raundi 12 la kuwania ubingwa wa mabara wa WBF la uzani wa super middle limepangwa kufanyika kwenye viwanja vya Leaders Dar es Salaam ambapo bendi ya Twanga Pepeta itatoa burudani.

Meneja wa Cheka ambaye pia ni Mkurugenzi wa Advance Security, Juma Ndambile alisema Jana kuwa maandalizi yote yamekamilika na Waziri Nape ameridhia kuwa mgeni rasmi siku hiyo.

Kwa mujibu wa Ndambile, mpinzani wa Cheka atawasili Jumatano hii sanjari na wawakilishi kutoka Shirikisho la ngumi la dunia (WBF) wakiongozwa na Rais wake, Goldberg Haward ambao watawasili Alhamisi hii.

"Maandalizi yote yamekamilika, Serikali Yetu imetusapoti kwa namna ya pekee na Waziri wa Michezo ameridhia kuwa mgeni rasmi siku hiyo.

"Kabla ya Cheka kupanda ulingoni, kutakuwa na burudani ya bendi ya Twanga Pepeta na pambano rasmi litaanza saa moja Jioni ," alisema.

Akizungumzia pambano hilo, Cheka alisema yuko fiti na kusisitiza  hajawahi kuwaangusha Watanzani hivyo wajitokeze kumpa sapoti.

"Nimefarijika kuona Waziri wa Michezo anakuja kunisapoti, nimuombe pia hata Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) aje alishuhudie na waahidi Watanzania sitawaangusha," alisema Cheka.

Cheka na Ajetovic watazichapa kwa Mara ya pili jijini Dar es Salaam baada ya Mara ya kwanza nchini England mwaka 2008 na Cheka kupigwa kwa pointi.
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile

Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi 
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

AIRTEL YACHEZESHA DROO YA MWISHO PROMOSHENI YA AIRTEL MKWANJIKA

Haya mmoja wa washiriki huyooooo....
Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde akimkabithi mshindi wa  Airtel Mkwanjika Diana Samwel na mkazi wa Dar es Saalam pesa taslimu mara baada ya kujinyakulia shilingi 480,000 kupitia boksi la Airtel Mkwanjika. 
Airtel yachezesha droo ya mwisho ya promosheni ya Airtel Mkwanjika
·         Zaidi ya wateja 212 wajishindia pesa taslimi
Dar es Salaam, Alhmasi 18th February 2016,  Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imechezesha droo ya mwisho ya promosheni ya Airtel Mkwanjika nakupata washindi 40 ambapo kila mmoja atajishindia pesa taslimu hadi shilingi milioni 1 kupitia boksi la Airtel Mkwanjika.

Promosheni ya Airtel Mkwanjika ilizinduliwa mwishoni mwa mwezi Disemba na kuwazawadia wateja wanne watakaojiunga na vifurushi vya yatosha au kuongeza  muda wa maongezi kupitia vocha au Airtel Money kila siku. Jumla ya washindi 28 walipatikana kupitia droo kila wiki na kuzawadiwa pesa taslimu.

Akiongea wakati wa kuchezesha droo ya mwisho, Afisa Uhusiano wa Airtel, Bi Jane Matinde alisema”  Leo tumefikia mwisho wa promosheni yetu ya Airtel Mkwanjika , promosheni ambayo imeweza kuwazawadia wateja zaidi ya 212.

nchi nzima.  Tunajisikia furaha kuona mwitikio mkubwa  kutoka kwa wateja wetu na tunapenda kuwahakikishia kuwa Airtel itaendelea kutoa huduma bora za kibunifu  zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu yanayoendelea kubadilika na kukua kila siku na  huku tukiendelea kuwazawadia kupitia promosheni kama hii ya Airtel Mkwanjika”

“Tunaamini kupitia Airtel Mkwanjika tumetoa zawadi ambazo zimewawezesha wateja wetu kukabiliana na changamoto walizonazo na kuwasaidia  kuongeza mitaji ya biashara zao na  kuongeza ufanisi katika  shughuli zao mbalimbali za kiuchumi na za kijamii. Tunaamini washindi wetu watakuwa ni ushuhuda tosha wa namna gani Airtel kupitia promosheni hii imeweza kubadili maisha yao na ya jamii zao kwa ujumla. Aliongeza Matinde


Promosheni ya Airtel Mkwanjika imefikia mwisho, Airtel bado itaendelea kuwawezesha washindi kutoka katika mikoa mbalimbali nchini  ambao bado hawajaingia kwenye  boksi la Airtel Mkwanjika kupata nafasi ya kufanya hivyo ili kuweza kujiokotea pesa na kukabithiwa zawadi zao