Friday, September 19, 2025
KATIBU MKUU UWT TAIFA KUCHELE AWAPA SOMO WANAWAKE WA KILOLO UMUHIMU WA KUPIGA KURA ZA KISHINDO
NA MWANDISHI WETU,KILOLO.
MABAKI YA DAWA MAJUMBANI JANGA KWA UHAI NA MAZINGIRA.
KATIKA sehemu mbili zilizotangulia za ripoti hii maalum, tulieleza namna mabaki ya dawa na vifaa tiba majumbani yanavyoendelea kuwa chanzo hatarishi cha uchafuzi wa mazingira, kuongeza usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa na kuathiri moja kwa moja afya ya wananchi.
Pamoja na juhudi za kisheria na kisera zilizowekwa kudhibiti changamoto hiyo, utekelezaji wake bado ni wa kusuasua, huku wananchi wengi wakiwa hawana uelewa wa kutosha kuhusu namna salama ya kushughulikia taka hizo.
Sehemu hii ya mwisho inaleta majibu, mapendekezo na mustakabali wa taifa katika kupambana na bomu hili la kimyamya ambalo kila kaya inaweza kuwa linachangia maradhi, pasipo kujua. Endelea
SERA IPO, LAKINI...
Sera ya Afya ya mwaka 2007, ambayo pia inahusisha usimamizi wa taka za huduma za afya, imeweka bayana dhamira ya kulinda afya ya jamii na mazingira kupitia udhibiti wa taka kuanzia zinapozalishwa hadi zinapoteketezwa. Sera hiyo inaelekeza kuwapo miundombinu salama, elimu kwa jamii na mfumo wa ufuatiliaji unaosimamiwa kikamilifu.
Hata hivyo, hali halisi katika maeneo mengi, hasa vituo vya afya vya mtaani na majumbani, inapingana kabisa na misingi ya sera hiyo. Dk. Peter Maziku, Mhadhiri kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dar es Salaam, anasema changamoto kubwa ipo kwenye utekelezaji.
“Vituo vingi vya afya vya mtaani havina vifaa maalumu vya kuteketeza taka hatarishi. Badala yake, taka hizo huunguzwa kwenye mashimo ya wazi, zikiambatana na taka nyingine. Hii ni hatari kubwa kwa afya ya jamii na mazingira,” anasema. Kwa mujibu wa Dk. Maziku, udhibiti wa taka hizi hauwezi kufanikiwa pasipo ufuatiliaji wa mara kwa mara na uwajibikaji kutoka kwa mamlaka husika.
Anaongeza kuwa vitendo vya kuchoma taka ovyo vimekuwa vya kawaida hata katika baadhi ya vituo vya afya binafsi, kutokana na ukosefu wa rasilimali au uelewa wa kina.
Dk. Stanley Mwita, mtafiti wa masuala ya afya, katika utafiti wake wa mwaka 2021, alibaini kuwa gharama kubwa na taratibu nyingi zinazohitajika ili kupata kibali cha kuteketeza taka za dawa ni miongoni mwa sababu zinazochangiautupaji holela wa dawa na vifaa tiba. “
Wamiliki wa baadhi ya vituo binafsi hulazimika kutafuta njia mbadala, ambazo isivyo bahati si salama kwa mazingira kama vile kutupa kwenye mashimo au kwenye madampo kama taka za kawaida,” anasema Dk. Stanley.
Ni hoja inayoungwa mkono na matukio mengi ya vitendo vya kiholela vya utupaji dawa maeneo ya makazi, ambako wananchi huzifukia dawa au kuzitupa katika mapipa ya taka, bila kujua athari zake kwa udongo, vyanzo vya maji na viumbe hai.
UTARATIBU SAHIHI
Benedict Brash, Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Kati, anafafanua kuwa kuna utaratibu rasmi unaopaswa kufuatwa na vituo vya afya vya umma na binafsi katika uteketezaji dawa na vifaa tiba vilivyopitwa na muda.
“Wamiliki wa vituo wanapaswa kuwasilisha ombi rasmi kwa TMDA likiwa na barua ya maombi, aina ya dawa, na thamani ya bidhaa hizo. Baada ya hapo, kibali hutolewa na uteketezaji hufanyika kwa njia salama kwa kutumia vifaa maalum,” anasema Brash.
Kwa upande wa vifaa tiba kama sindano, Brash anasema huwa vinawekwa katika incinerator mashine maalum ya kuchoma taka kwa joto la juu ambalo huharibu kemikali na vimelea vyote hatarishi. Brash anasema TMDA pia inaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya kuhifadhi au kutupa dawa ovyo.
Lakini, changamoto kubwa inaonekana zaidi kwa wagonjwa wanaopatiwa huduma nyumbani. Hawana mwongozo maalum wa namna ya kushughulikia dawa zilizobaki, jambo linalosababisha wengi kuzihifadhi majumbani au kuzitupa kiholela, kwa dhana ya kuwa ni mali yao binafsi.
ELIMU KWA JAMII
Dk. Christina Kifunda, Mhadhiri wa masuala ya mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), anasisitiza kuwa elimu kwa jamii ndiyo silaha muhimu zaidi katika mapambano dhidi ya utupaji ovyo wa mabaki ya dawa.
“Wananchi wengi hawajui kwamba dawa zilizobaki zinaweza kuwa sumu kubwa. Tunahitaji kuwa na vituo rasmi vya ukusanyaji dawa hizo katika kila kata au mtaa,” anasema Dk. Kifunda.
Anaongeza kuwa sekta ya afya inapaswa kutoa mwongozo wa moja kwa moja kwa wagonjwa kuhusu nini cha kufanya iwapo dawa walizopewa zitakuwa zimebaki.
“Watoa huduma wa afya wawaeleze wagonjwa ‘dawa hizi ni kwa siku tano, ukibakiwa nazo, peleka sehemu maalum’. Mwongozo huo uwe wazi na utekelezwe,” anashauri Dk. Kifunda.
JICHO LA CAG
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2022/23 ilifichua udhibiti hafifu katika vituo binafsi vya afya nchini.
Mojawapo ya upungufu ulioonekana ni kutokuwa na maeneo maalum ya kuhifadhi dawa zilizopitwa na muda au vifaa tiba visivyotumika tena.
CAG aliitaka serikali kuweka mfumo madhubuti wa kufuatilia uendeshaji vituo hivyo, hasa ikizingatiwa kuwa huduma za afya binafsi zimeongezeka kwa kasi, lakini uwezo wa kusimamia taka zao bado ni mdogo sana.
Vilevile, kama mwanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tanzania ina wajibu wa kuzingatia miongozo ya kimataifa kuhusu usimamizi wa taka za afya.
WHO inapendekeza matumizi ya incinerators zilizoidhinishwa, ambazo zina uwezo wa kuchoma taka kwa joto la juu na kupunguza uchafuzi wa hewa unaotokana na gesi zenye sumu.
Aidha, WHO inasisitiza kuwapo utaratibu wa kuzuia dawa zisizohitajika kuingia katika mzunguko wa matumizi, hasa katika mazingira ya dharura au vituo vya afya vyenye uhaba wa vifaa.
OSHA YAKABIDHI VIFAA CHUO CHA UFUNDI MIRONGO JIJINI MWANZA
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi, akiwasilisha hotuba yake wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR BONANZA 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo Jijini Mwanza akiwa ni Mgeni Rasmi wa Bonanza hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda wakimkabidhi Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Mirongo vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na OSHA kukiwezesha chuo hicho. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na kompyuta, makoti ya usalama na vifaa vya michezo.
Na Fredy Mgunda,Mwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mheshimiwa Amina Makilagi, amewataka waajiri na wafanyakazi kote nchini kuitekeleza kikamilifu Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Na. 5 ya mwaka 2003 ili kupunguza au kuondoa kabisa ajali na magonjwa yanayotokana na mazingira duni ya kazi.
Mheshimiwa Makilagi alitoa wito huo jana wakati wa Bonanza la OSHA la Huduma kwa Jamii (OSHA CSR Bonanza 2025) lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyakabungo, Wilaya ya Nyamagana, Jijini Mwanza. Bonanza hilo lilihusisha shughuli mbalimbali za kijamii na michezo kwa lengo la kuimarisha mshikamano kati ya OSHA na jamii inayohudumiwa, pamoja na kutoa msaada kwa wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Mirongo, wakiwemo wenye ulemavu.
Katika tukio hilo, OSHA ilikabidhi vifaa mbalimbali kwa Chuo cha Ufundi Mirongo, vikiwemo kompyuta, vifaa kinga vya usalama kazini, pamoja na vifaa vya michezo kama mipira na jezi za michezo.
Akizungumza kama Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Makilagi aliipongeza OSHA kwa juhudi zake za kuhakikisha mazingira salama na yenye afya sehemu za kazi na kuonesha moyo wa huruma kwa makundi maalum katika jamii.
“Nitoe rai kwa waajiri na wafanyakazi nchini kuisoma na kuitekeleza Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Sheria hii ikitekelezwa ipasavyo, maeneo ya kazi yatakuwa salama, bila ajali wala magonjwa, hivyo kuongeza tija kazini,” alisema Mkuu wa Wilaya Makilagi.
Aidha, aliihakikishia OSHA ushirikiano wa Halmashauri na Ofisi yake katika kusimamia usajili na ukaguzi wa maeneo ya kazi, sambamba na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya maboresho ya mazingira ya kazi.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, alisema Bonanza hilo ni sehemu ya mpango wa taasisi hiyo wa kurudisha kwa jamii (Corporate Social Responsibility) na kwamba msaada uliotolewa kwa Chuo cha Mirongo umetokana na tathmini iliyofanywa na wataalam wa OSHA baada ya kutembelea chuo hicho.
“Tunaamini kuwa kwa kusaidia vyuo vya ufundi kama Mirongo, tunachangia kwa kiasi kikubwa maandalizi ya wataalamu wa baadaye katika fani muhimu za kiufundi na kazi,” alisema Bi. Mwenda.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mirongo, Bi. Herieth Richard, pamoja na mwanafunzi wa fani ya ushonaji, Bi. Aneth Augustino, waliishukuru OSHA kwa msaada huo ambao wamesema umeongeza ari ya kujifunza na kushiriki katika shughuli za kijamii.
Bonanza hilo lilihusisha michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha, na michezo ya jadi kama kukimbia kwenye magunia, kukimbia na ndimu kwenye kijiko, rede na kukamata kuku. Washiriki walitoka OSHA na vyuo vya Ufundi vya Mirongo, Nyakato na Kisesa.
Chuo cha Ufundi Mirongo kinamilikiwa na Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), na hutoa mafunzo ya umeme, useremala, ushonaji na uchomeleaji kwa vijana wakiwemo wenye mahitaji maalum.
KOKA AOMBA RIDHAA YA KUCHAGULIWA NA WANANCHI KATA YA VISIGA ILI KUWALETEA CHACHU YA MAENDELEO
NA VICTOR MASANGU,KIBAHA
Thursday, September 18, 2025
ORODHA YA WACHEZAJI WA SIMBA SC WALIOPO BOTSWANA

SIMBA SC baada ya kupoteza Ngao ya Jamii, Septemba 16 2025 mbele ya Yanga SC msafara ulikwea pipa na umefika salama Botswana kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya awali dhidi ya Gaborone United.
Hii hapa orodha ya wachezaji wa Simba SC waliopo Botswana watakuwa na kazi Jumamosi ya Septemba 20 2025:-
Makipa
Moussa Camara, Yakoub Suleiman na Alexender Erasto.
Mabeki
Shomari Kapombe, Anthony Mligo. Rushine De Reuck, Wilson Nangu, Naby Camara.
Viungo
Yusuph Kagoma, Allasane Kante, Kibu Dennis, Ellie Mpanzu. Ladack Chasambi, Mzamiru Yassin, Neo Maema. Joshua Mutale, Jean Ahoua, Daud Semfuko Morice Abraham.
Washambuliaji
Steven Mukwala, Seleman Mwalimu, Jonathan Sowah.
SUBIRA MGALU KUWAKOMBOA WANANCHI BAGAMOYO FURSA ZA AJIRA NA BARABARA ZA LAMI
NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO
MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI WODI YA MAMA NA MTOTO MWAMI NTALE
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, ameweka jiwe la msingi katika wodi ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Mwami N’tale, kilichopo kata ya Heru, Halmashauri ya Mji Kasulu.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Ussi amesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao kwa amani, utulivu, na kuchagua viongozi wanaowataka. Amesema kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu inahimiza amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.
“Maendeleo tunayoyaona leo ni matokeo ya utulivu na amani inayotamalaki nchini. Hivyo ni wajibu wetu kuilinda na kuithamini hali hii,” alisema Ussi.
Mradi wa ujenzi wa kituo hicho umegharimu kiasi cha Tsh milioni 300, na tayari umekamilika kwa asilimia 100. Utaanza kutoa huduma za afya kwa kina mama na watoto katika eneo la Heru na maeneo jirani.
Kituo hiki kinatarajiwa kupunguza kwa kiwango kikubwa vifo vya mama na mtoto kwa kutoa huduma bora, za karibu, na za uhakika kwa wananchi.
Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo muhimu katika kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji, na uzalendo miongoni mwa Watanzania.
KATIBU MKUU UWT AUNGURUMA KWA WANAWAKE IRINGA AWAFUNDA JUU UMOJA KIPINDI CHA UCHAGUZI MKUU
NA MWANDISHI WETU,IRINGA
SIMBA SC WAKWEA PIPA KUELEKEA BOTSWANA KUWAVAA GABORONE UTD JUMAMOSI LIGI YA MABINGWA

KIKOSI cha Simba SC kimeondoka JANA mchana kutoka Jijini Dar es Salaam kwenda Botswana kwa ajili ya mchezo wa kwanza Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Gaborone United Jumamosi kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa Taifa wa Botswana Jijini Gaborone.
Timu hizo zitarudiana Jumapili ya Septemba 28 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla kati ya Simba Bhora ya Zimbabwe na Nsingizini Hotspurs ya Eswatini.




FOLZ 'AZIMA' SHEREHE ZA WACHEZA YANGA DHIDI YA SIMBA.
KOCHA wa Yanga, Romain Folz, amewataka wachezaji wa timu hiyo kusahau ushindi wao wa bao 1-0 dhidi ya Simba na kugeukia mechi yao ya hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete de Benguela ya Angola.
Mara baada ya mchezo wa juzi wa Ngao ya Jamii kumalizika huku wachezaji wa timu hiyo wakiwa na furaha, Folz aliitisha kikao cha dharura na kuwataka wachezaji hao kusahahu ushindi huo na kuelekeza mawazo na nguvu zao kwenye mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mchezaji mmoja wa timu hiyo ameliambia gazeti hili kuwa furaha yao ya kuifunga Simba ilikatishwa ghafla na Kocha Folz, alipowakumbusha kuwa wana mechi ngumu dhidi ya Wiliete na waache kushangilia mechi hiyo ya Ngao ya Jamii.
"Baada ya kuifunga Simba tulirudi vyumbani tukiwa na furaha kubwa, wenyewe tunashangilia, kocha Folz, alipoingia alikuta tunashangilia sana, akatuamuru tukae chini haraka, akatuambia ile ilikuwa mechi ya 'bonanza', tujiandae na mechi kamili ni dhidi ya Wiliete wikiendi hii, basi ikabidi tukae kimya wote," alisema mchezaji huyo.
Alisema kocha huyo amewataka kuweka mkazo kenye mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa na kusahau ushindi wa Ngao ya Jamii.
Kikosi cha Yanga tayari kimetua nchini Angola tayari kwa mchezo huo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga itacheza mchezo huo kesho kwenye uwanja wa 11 de Novembro, jijini Luanda saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na baadaye kurudiana jijini Dar es Salaam Septemba 27.
Wakati Simba na Yanga zikiwa zimeondoka nchini, Azam ilikuwa ya kwanza, Ijumaa iliyopita kwenda Juba, nchini Sudan Kusini kwa ajili ya mchezo wa awali wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya El Merrikh Bentiu, unaotarajiwa kuchezwa, Jumamosi, Uwanja wa Juba, nchini humo, saa 11:00 jioni kwa sasa za Tanzania.
SAMIA: UKIPIGA KURA KATULIE NYUMBANI KUDUMISHA AMANI.

Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Samia Suluhu Hassan amesema atahakikisha amani na utulivu vinatawala katika msimu wote wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Katika kauli yake hiyo, amewasihi wananchi kufuata utaratibu uliowekwa wa kupiga kura na kurudi nyumbani, kwa kuwa uchaguzi ni tendo la kidemokrasia na sio vita.
Dk Samia ametoa kauli hiyo Jumatano Septemba 17, 2025 alipozungumza na wananchi wa Makunduchi visiwani Zanzibar, wakati wa mkutano wake wa kampeni za urais, alioufanyia katika Uwanja wa Kajengwa.
“Uchaguzi ni tendo la kidemokrasia, ni watu kwenda kwa utaratibu uliowekwa, kuweka kura zetu rudi nyumbani katulie ili nchi ibaki salama,” amesema.
Amewataka wananchi visiwani humo, kuhakikisha katika uchaguzi wanadumisha amani na utulivu, kwani tukio hilo sio tendo la vita.
Dk Samia amesema baada ya kuapishwa kuwa Rais, alikutana na wazee wa Pemba, pamoja na mambo mengine walimwelekeza kuhakikisha anadumisha amani na utulivu, jambo ambalo ameapa kuhakikisha linatimia.
“Si muda wote kushika silaha kunaleta suluhisho, muda wote kushika silaha yoyote, iwe ya moto au ya kimila hakuleti suluhisho la maana. Niwaombe sana wote wanaotusikiliza, amani na utulivu wa nchi yetu ni jambo la muhimu zaidi kuliko mengine yote hasa wakati huu wa uchaguzi,” amesema.
Amesema vyombo vya ulinzi na usalama vya Tanzania, vimejipanga vema kulinda nchi.
“Sasa hutaki kishindo kapige kura rudi nyumbani tulia, tumejipanga vema. Kwa hiyo nisisitize suala la amani na utulivu,” amesema Dk Samia.
Kauli hiyo ya Dk Samia, imesisitizwa pia na Mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM, Dk Hussein Ali Mwinyi aliyesema amani, umoja, mshikamano na maridhiano nchini Tanzania kwa kuwa ndicho kipaumbele cha chama hicho.
MASHAHIDI 100 KUWASILISHA USHAHIDI KESI YA KUPOROMOKA JENGO KARIAKOO

Zaidi ya mashahidi 100 wanatarajiwa kuwasilisha ushahidi katika kesi ya mauaji bila kukusudia inayowakabili wafanyabiashara sita, kufuatia kuporomoka kwa jengo la ghorofa mnamo Novemba 16, 2024, katika Mtaa wa Mchikichi na Kongo, Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Kesi hiyo iliwasilishwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kusomwa maelezo ya mashahidi na vielelezo kwa washitakiwa. Hata hivyo, hatua hiyo haikufanyika kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha maandalizi.
Wakili wa Serikali, Clemence Kato, aliieleza mahakama kuwa kesi hiyo inatarajiwa kuwa na mashahidi zaidi ya 100, lakini hadi sasa ni nusu pekee ya mashahidi ambao maelezo yao yamekwishachapwa.
“Waheshimiwa, tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kusoma maelezo ya mashahidi na vielelezo kwa washitakiwa, kwa kuwa bado hatujakamilisha maandalizi,” alisema Wakili Kato mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Geofrey Mhini.
Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mhini alikubaliana na ombi la upande wa mashtaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 9, 2025.
Washitakiwa:-
Wafanyabiashara wanaokabiliwa na kesi hiyo ni:
- Lendela Mdete, mkazi wa Mbezi
- Zenabu Islam maarufu kama Zaibanu, mkazi wa Kariakoo
- Ashour Ashour, mkazi wa Ilala
- Soster Nziku na Stephen Nziku, wakazi wa Mbezi Beach
- Aloyce Sangawe, mkazi wa Sinza Wanadaiwa kusababisha vifo kwa uzembe baada ya jengo walilohusishwa nalo kuporomoka na kuua wakazi na wafanyakazi waliokuwemo.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, jalada hilo bado halijakamilika na linasubiri kuwasilishwa katika Mahakama Kuu, kutokana na uzito wa kosa linalowakabili washitakiwa.
MGOMBEA UDIWANI KATA YA KIBAMBA ATEMA CHECHE AAHIDI NEEMA YA MAJI NA BARABARA KWA WANANCHI
NA VICTOR MASANGU,KIBAMBA
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)










.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)











