ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 10, 2018

TIZAMA WALICHOKIFANYA WATOTO HAWA.

NA.ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGO TV

Wakati biashara haramu ya ukahaba ikishamiri katika baadhi ya maeneo nchini kutokana na ukatili dhidi ya mtoto wa kike na umaskini wa kipato, mashirika mbalimbali yametakiwa kubuni mbinu za kuwakomboa watoto wa kike, ili kutokomeza vitendo hivyo kutokana na changamoto hiyo, Dorocella Reuben kupitia Shirika la Foundatio Dart Tanzania, ameamua kutatua kilio hicho.

Jiji la Mwanza ni moja kati ya Majiji yanayokuwa kwa kasi kubwa hapa nchini, kutokana na ongezeko la idadi ya watu, lakini changamoto kubwa iliyopo ni biashara haramu ya ukahaba inayofanyika hasa nyakati za usiku katika baadhi ya kumbi za starehe kutokana na biashara hiyo zikiwemo sababu za umaskini wa kipato cha familia, ndoto za watoto wengi wa kike hupotea ambapo kwa kutambua thamani yao, Shirika la Foundation Dart limeamua kuanzisha elimu ya ujasiriamali na kuwasomesha, ili kuwakomboa watoto wa kike.

Miriam Nzogi ni mmoja kati ya watoto walioto kakatika familia duni, leo anaelezea mafanikio yake, baada ya kuchukuliwa na shirika hilo na kisha kusomeshwa, Dorocella Reuben ni mkurugenzi wa Shirikala Foundation Dart Tanzania, lililopo kata ya Bwiru wilayani Ilemela Jijini Mwanza na Rotalinda Mhagama ni mwanafunzi wa kitivo cha sharia, katika chuo kikuu cha mtakatifu Agustino (SAUT).

Akimwakilisha kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Jonathan Shana, wakati wa hafla ya kuwatunuku vyeti watoto hao vya kuhitimu elimu ya ujasiriamali, mkuu wa Polisi wilaya ya Ilemela Ndagile Makubi, amesema Jeshi hilo halifumbia macho vitendo vya mmomonyoko wa maadili.

Mbali na kuwatukunuku vyeti watoto hao vilevile wamepatiwa medali mbalimbali, baada ya kudhihirisha vipaji vyao katika elimu wanazopatiwa na shirika hilo, zinazohusiana na stadi za maisha.




6 WAFARIKI DUNIA KWENYE AJALI MOROGORO YUMO MSANII.



Watu sita wamefariki dunia kwa ajali ya gari mkoani Morogoro, ambapo miongoni mwa waliofariki ni msanii maarufu wa muziki wa mchiriku na singeli kutoka kundi la 'Jagwa', Jack Simela.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Msamvu mkoani Morogoro, baada ya gari lao dogo lililokuwa likitokea kwenye mazishi mkoani humo kugongana uso kwa uso na lori aina ya Scania.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Dkt. Simon Tarimo, amethibitisha kupokea miili sita na majeruhi wawili, na kusema kwamba hali za majeruhi zinaendelea vizuri hospitalini hapo.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijawekwa wazi, baada ya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro kugong mwamba.

Jack Simela alikuwa ni muimbaji kiongozi wa kundi la Jagwa Music ambalo ni maarufu kwa muziki aina ya mchiriku, muziki ambao umekuwa ukipendwa na mataifa ya nje ikiwemo Ujerumani, ambako ndiko mara nyingi yeye na kundi lake walikuwa wakienda kufanya matamasha

WAZIRI KAKUNDA ATOA MAAGIZO MAZITO MTWARA.

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda, akisisitiza jambo kwa wawakilishi wa vikundi vya wabanguaji wadogo wa korosho (hawapo pichani). Kwenye kikao hicho Waziri Kakunda ameziagiza taasisi mbalimbali za serikali kuhakikisha zinafanya kazi pamoja kuwawezesha wabanguaji wadogo kushiriki zoezi la kubangua korosho zilizonunuliwa na serikali.
 Mwakilishi wa Mandawa AMCOS kutoka Wilaya ya Ruangwa, Selemani Mwigambe, akiwasilisha hoja wakati wa kikao cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji na wawakilishi wa vikundi vidogo vya ubanguaji wa korosho kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi. Kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kilikuwa na lengo la kutambua changamoto za vikundi hivyo ili kuviwezesha kushiriki zoezi la kubangua korosho iliyonunuliwa na serikali.
Baadhi ya wawakilishi wa vikundi vya wabanguaji wadogo wa korosho kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi wakifuatilia kwa makini maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda(hayupo pichani) kwenye kikao chake na wawakilishi hao leo mjini Mtwara.

GSENGOtV

Waziri Kakunda Atoa Maagizo Mazito MtwaraWaziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda ameziagiza taasisimbalimbali   za serikali   zihakikishe  zinashirikiana kwa   pamoja   ili   kutimiza   azma   yaserikali   kuona   wabanguaji   wadogowadogo   wa   korosho  wanashiriki   kwenye  zoezi   lakubangua korosho iliyonunuliwa na serikali. 

Kwenye   kikao   chake   na   wawakilishi   wa   vikundi   mbalimbali   vya   kubangua   koroshokutoka mikoa ya Lindi na Mtwara, Waziri Kakunda amewaagiza Makatibu Wakuu wawizara yake na ile ya Kilimo kwa kushirikiana na Makatibu Tawala  wa   mikoa   hiyomiwili,   wanahakikisha   wabanguaji   wadogo   wanapewa   ushirikiano   kwa   kupatiwakorosho za kubangua kutoka kwenye maeneo yao.

Kuhakikisha ubora wa korosho itakayobanguliwa na vikundi vya wabanguaji wadogoinakidhi viwango vya soko, mheshimiwa Kakunda amelitaka  Shirika la  Mendeleo  yaViwanda Vidogo (SIDO) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele kwa pamoja wafanyeziara za kutembelea vikundi hivyo ili kujua changamoto zinazowakabili. “Jipangenikuwatembelea   kwenye   maeneo   yao   mjiridhishe   na   kuona   teknolojia   wanazotumiamuwasaidie inapobidi ili ubora wa korosho itakayobanguliwa ulindwe na uwe mzuri”amesisitiza Waziri Kakunda. 

Waziri Kakunda pia ameitaka SIDO ihakikishe inavisaidia vikundi hivyo vya ubanguajimikopo  ya   mashine   itakapothibitika  kikundi kina   uwezo  kufanya  kazi  lakini  hakinavitendea kazi.Kuhusu kilio cha wakulima kudhulimiwa korosho wakati wa kupima, Waziri Kakundaameagiza   Wakala   wa   Vipimo   (WMA)   ianze   mara   moja   zoezi   la   kuhakiki   mizanizinazotumiwa   kwenye   maeneo   ya   kukusanya   na   kupima   korosho.   

Waziri   Kakundaamesema,   “Wakala   wa   vipimo   nchini   watembelee   maeneo   yote   yanayofanyaukusanyaji na upimaji wa korosho kwenye mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma na Pwaniwajiridhishe kama vipimo vinavyotumika vinakidhi matakwa ya kisheria”.

Aidha amewataka Makatibu Tawala wa mikoa wahakikishe wanasimamia utekelezajiwa Sheria ya Ardhi namba 4 na 5 ya mwaka 1999 ambayo inazitaka serikali za mitaangazi ya halmashauri kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi kila kijiji. 

Sheriahizo mbili zimetenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kijamii, kidini nakiuchumi. Utekelezaji wa sheria hizo utawanufaisha wabanguaji wadogo kwa kutengamaeneo watakayo kuwa wanafanya kazi zao bila bughudha. 

Kwa upande wao wabanguaji wadogo wamepongeza hatua iliyochokuliwa na serikaliya   kununua   na   kuhakikisha   korosho   zote   zinabanguliwa   nchini.   “Uamuzi   wakushirikisha wabanguaji wadogo ni jambo la kupongezwa sana, hakika Rais Magufuli nikiongozi   wa   wanyonge”   amesema   Bi.   Daria   Erasto,   Mtendaji   Mkuu   wa   Umoja   waWabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT). 

10 WAFANYIWA UPASUAJI WA KICHWA + MGONGO KWA MAFANIKIO BUGANDO


GSENGOtV
Wagonjwa 10 wenye tatizo katika ubongo na mishipa ya fahamu na mgongo wamefanyiwa upasuaji na kukamilika salama katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando jijini Mwanza.

Upasuaji huo unafanywa na daktari bingwa wa mifupa kutoka Marekani kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa hospitali hiyo.
Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati upasuaji huo ukiendelea hospitalini hapo, Daktari bingwa wa upasuaji Isidory Ngayomela, amesema hatua hiyo inalenga kutatua changamoto za upasuaji.
Ameongeza kuwa mpaka hapo walipofika wamefanikiwa kufanya upasuaji kwa watu 10 wale waliopata ajali na kuumia kichwani pamoja na mgongo kupinda kutokana na uzee.
Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji kutoka Saint Francis Hospital and Medical Centre ya Hartford nchini Marekani, Dr. Christopher Comey (kulia katika picha juu akiwa na mwanahabari Albert G. Sengo wa Jembe Fm Mwanza) amesema tangu awasili Bugando ikiwa ni wiki moja sasa, wameshafanya upasuaji kwa wagonjwa 10 zikiwemo oparesheni mbili za ubongo.
"Mara kwa mara nimekuwa nakuja nchini Tanzania, kwaajili ya kutoa huduma ya kujitolea lakini safari hii nimeamua kutoa na mafunzo kupitia ujuzi niliona kwa madaktari wa hapa ili huduma ziendelee na hata kama sipo watu wasiendelee kutaabika"
Comey amewasifia madaktari wa Bugando akisema "Pamoja na changamoto ya uhaba wa vifaa na miundombinu mingine nafurahi kuona  madaktari wa Bugando wakichapa kazi kwa bidii maarifa na weredi wa hali ya juu huku wakizingatia kile ninachowafundisha" 

Sunday, December 9, 2018

Mo Salah refuses to accept MOTM award and gifts it to James Milner



Hat-trick hero Mohamed Salah was awarded the MOTM trophy after Liverpool’s impressive win against Bournemouth but refused to accept it, instead handing it to his teammate James Milner on his 500th Premier League appearance.