ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 10, 2022

SERIKALI YAJA NA HII KALI KULIKO ZOTE 'NUNUA KIWANJA LEO, PATA HATI LEO LEO'

 NA ALBERT G. SENGO

MWANZA. Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi Mhe. Angeline Mabula amesema mpaka sasa jumla ya watu 2,700 kati ya 3500 tayari wameshapata viwanja vyao, huku baadhi yao wakiwa na hati walizopata papo hapo na wengine wakisubiri kukamilisha malipo ili wapewe hati zao. Ndani ya viwanja vya Rock City Mall jijini Mwanza watumishi wa vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Ardhi wilaya ya Ilemela wameweka kambi hapa kutoa huduma zote katika eneo moja. HUDUMA ZINAZOTOLEWA 1. Kwa uuzaji wa viwanja vilivyotangazwa, mnunuzi atakwenda kwenye ramani na kuchagua kiwanja, atapewa bei kupitia mtandao, atalipa na kupewa hati ya kumiliki papo hapo. 2. Kwa wanaotaka kulipa kodi ya ardhi hakuna riba kwa msamaha wa Rais Samia. 3. Huduma zote zinazotolewa na ofisi ya ardhi zinapatikana hapa kwani hii ni One Stop Centre.

Thursday, September 8, 2022

MALKIA ELIZABETH ALAZWA KWA MATIBABU.

 


Kasri la Buckingham nchini Uingereza limetangaza kuwa kiongozi mkuu wa kimila wa nchi hiyo, Malkia Elizabeth yupo chini ya uangalizi maalumu wa matibabu kwenye kasri la Balmoral nje ya jiji la London kutokana na maradhi ambayo hayakuwekwa wazi.


Taarifa hiyo iliyotolewa leo Septemba 8, imesema madaktari wa Malkia wamependekeza abaki chini ya uangalizi wa matibabu.


“Malkia anaendelea vizuri na yuko Balmoral kwa matibabu na mapumziko," imesema sehemu ya taarifa hiyo.


Hali hiyo imemtokea malkia huyo mwenye umri wa miaka 96 ikiwa ni siku chache tangu akutane na Waziri Mkuu anayeondoka madarakani Boris Johnson kabla ya kumteua waziri mkuu mpya, Liz Truss.


Pia, kutokana na mwenendo wa afya yake malkia Elizabeth alilazamika kuahirisha kikao chake na Baraza la Mawaziri kilichotakiwa kifanyike siku ya jana, Septemba 7, 2022 baada ya kushauriwa na madaktari wake kupumzika.


Nchi hiyo inaongozwa kwa mfumo wa serikali ya kifalme huku makao makuu yake yakiwa kwenye kasri kuu la Buckingham lililopo kwenye jiji la London, hata hivyo kasri lingine ambalo malkia amepelekwa kupumzika lipo Balmoral eneo la Aberdeenshire huko Scotland.   


VIDEO TFS WAJA NA MASHINDANO YA MAGARI

 Wa kwanza kwenye video ni Mhifadhi mkuu wa shamba la miti la Sao Hill Mufindi Lucas Sabida anayefuata ni mwenyekiti wa Rally Iringa anaitwa Amjad khan



Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kupitia shamba la miti la Sao Hill mkoani Iringa wameanzisha utalii wa michezo ya magari katika shamba hill kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kutangaza utalii wa ndani kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyofanya kwenye filamu ya Royal Tour.

Akizungumza wakati wa kutangaza kwa mashindano ya magari katika shamba la miti la Sao Hill, Mhifadhi mkuu wa shamba hilo Lucas Sabida alisema kuwa wamejipanga kuanzisha utalii katika shamba hilo ambao utaongeza kipato kwa wananchi na shamba hilo.

Sabida amesema kuwa kwa sasa wameanzisha utalii wa mchezo wa magari ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 11/09/2022 katika shamba la miti la Sao Hill na wananchi wote wanakaribishwa kwenda kutazama mchezo huo.

Alimesema kuwa lengo kubwa ni kuanzisha mashindano makubwa ya mbio za magari Africa kwa kuwa wanabarabara ambazo zinahimili hilo na zina urefu wa kilomete 15000


Sabida amesema kuwa SAO HILL MISITU AUTO CROSS  ni zao jipya la Utalii ndani ya Shamba la Miti SaoHill Mafinga   TFS wanasema utalii wa aina hii ni mara ya kwanza kufanyika ndani ya Shamba la Miti SaoHill

TFS WAJA NA MASHINDANO YA MAGARI "TUNATANGAZA UTALII WA MISITU"

Mhifadhi mkuu wa hamba la miti la Sao Hill Lucas Sabida akiongea na waandishi wa habari juu ya utalii huo mpya wa mchezo wa mbio za magari katika msitu wa shamba hilo.
Mhifadhi mkuu wa hamba la miti la Sao Hill Lucas Sabida akiongea na waandishi wa habari juu ya utalii huo mpya wa mchezo wa mbio za magari katika msitu wa shamba hilo.
Mhifadhi mkuu wa hamba la miti la Sao Hill Lucas Sabida akiongea na waandishi wa habari juu ya utalii huo mpya wa mchezo wa mbio za magari katika msitu wa shamba hilo.


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kupitia shamba la miti la Sao Hill mkoani Iringa wameanzisha utalii wa michezo ya magari katika shamba hill kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kutangaza utalii wa ndani kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyofanya kwenye filamu ya Royal Tour.


Akizungumza wakati wa kutangaza kwa mashindano ya magari katika shamba la miti la Sao Hill, Mhifadhi mkuu wa shamba hilo Lucas Sabida alisema kuwa wamejipanga kuanzisha utalii katika shamba hilo ambao utaongeza kipato kwa wananchi na shamba hilo.


Sabida amesema kuwa kwa sasa wameanzisha utalii wa mchezo wa magari ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 11/09/2022 katika shamba la miti la Sao Hill na wananchi wote wanakaribishwa kwenda kutazama mchezo huo.


Alisema  kuwa  wao kama Shamba mbali na kujihusisha na shughuli za mazao ya isitu lakini pia wanafanya shughuli za utalii  wa michezo ambapo kwa mara ya kwanza wameanza na utalii wa Mbio za Magari ambayo yatafanyika September 11 Mwaka huu.


"Leo tumekutana kwa lengo la kujiridhisha na kuangalia maandalizi hatua ambayo tumefikia hadi sasa sanjari na kukagua njia zote ambazo zitatumika kwa ajili ya mchezo huo kwa sababu ni zoezi ambalo halijawahi kufanyika katika historia ya shamba letu hivyo ni kitu kipya." Amesema Sabida


Sabida alisema kuwa katika Shamba hilo kuna barabara ambazo wamekuwa wakidhihifadhi  ambazo zinaurefu wa kilometer 1500 hivyo ni fursa ya kipekee ya kutumiwa kwa utalii wa michezo ambayo ni  mchezo mpya


kwa upande wake  Mwenyekiti wa Mbio za Magari kwa Mkoa wa Iringa Amjad Khan amesema kuwa  Sao hill na wao kwa pamoja wameshirikiana kuandaa  Mashindano hayo madogo ya magari ambayo huitwa sprint kwa ajili ya kujifunza kuhusu Shamba hilo


" Hadi sasa tumejipanga vizuri na maandalizi yamefikia asilimia 99 kwa sababu tulijipanga vizuri  ili kuhakikisha Mashindano hayo yanafanikiwa  kwa sababu tulianza kujiandaa mwezi mmoja na nusu kabla ya siku hii ambayo tunazungumza na waandishi ikiwa  kila kitu kimekamilika." Amesema Khan


Amesema kuwa Mashindano hayo ni fursa nzuri kwao ya kushirikiana na Serikali kuweza kutangaza msitu huo ili watu waweze kuelewa zaidi pamoja na kuunga mkono juhudi za Serikali kutangaza masuala ya utili ikiwa utalii wa michezo.


"Malengo ya Mashindano hayo ya magari ni kutangaza msitu wa sao hill hivyo Iringa motorsports Club  tumepata fursa hii hivyo .. Sisi kama club tumefurahi sana... Kwa bahati ambayo tunaipata na tumeipokea kwa mikono miwili  na tunajisikia furaha sana." Amesema Khan


Naye  Mchezeshaji wa mchezo huo wa magari  John Makeo alisema asilimia kubwa wamepata ushirikiano mkubwa kutoka kwa shamba kwakuwa ni mara ya kwanza kushiriki michezo huo katika Shamba hilo.


"Watu wengi wa Mafinga walikuwa wanakuja  Iringa kwa ajili ya kuangalia Mashindano hayo lakini September 11 yatafanyika katika Msitu wa shamba la Sao hill ambapo wataweza kujionea fursa zilizopo na kuzitangaza ikiwemo utalii wa nyuki pamoja na gundi zipo katika msitu hii" Amesema Makeo


Hata hivyo katika Mashindano hayo jumla ya madereva  zaidi ya 20 wanatarajiwa kushiriki katika mchezo huo ambapo hadi sasa wanajumla ya washiri 14 ambao wamekubali kushiri kwenye mchezo huo watazungumza mizunguko minne ambayo Sawa na kilometer 6.


Sabida amesema kuwa SAO HILL MISITU AUTO CROSS ni zao jipya la Utalii ndani ya Shamba la Miti SaoHill Mafinga   TFS wanasema utalii wa aina hii ni mara ya kwanza kufanyika ndani ya Shamba la Miti SaoHill

Wednesday, September 7, 2022

UONGOZI WA AZIMIO WAMWIDHINISHA KALONZO KUWANIA USPIKA WA SENETI KENYA.

Kalonzo Musyoka. 

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka mnamo Jumatano, Septemba 7, alijitosa kwenye kinyang'anyiro cha spika wa Seneti baada ya kujiondoa katika kile cha spika wa Bunge la Kitaifa. Kalonzo Musyoka akizungumza na wanahabari hapo awali.

 Kalonzo alipewa msukumo na Muungano wa Azimio One Kenya unaoongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga na Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta. 

Katika kinyang'anyiro hicho, kinara wa Wiper anatazamiwa kumenyana na aliyekuwa Gavana wa Kilifi Amason Kingi ambaye anaungwa mkono na mrengo wa Kenya Kwanza.

 "Ufafanuzi katika mkutano wa Azimio Parliamentary Group (PG) kuhusu nani atawania Uspika katika Bunge la Kitaifa na seneti. 


 Kenneth Marende.

"Mhe. Kenneth Marende atawania spika wa Bunge la Kitaifa na Mhe Kalonzo Musyoka kuwa spika wa Seneti," Philip Etale, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa ODM, alitangaza. 

Hapo awali, Kalonzo alikuwa kwenye kinyang'anyiro cha spika wa Bunge la Kitaifa lakini akaamua kujiondoa kwa kuhofia kudhalilishwa kwenye uchaguzi uliopangwa kuandaliwa Alhamisi, Septemba 8. 

Aliyekuwa Makamu wa Rais chini ya Muungano wa Azimio La Umoja alikuwa amejitupa katika kinyang'anyiro cha kumkabili Moses Wetangula kutoka Muungano wa Kenya Kwanza kuwania kiti cha spika. 

Wakati akitoa uamuzi wake, Baraza Kuu la Kitaifa la Chama cha Wiper lilimtaka kiongozi wake kuanza kujenga chapa yake baada ya mgombea urais anayempendelea, Raila Odinga, kukosa kunyakua kiti hicho. 

Kalonzo, mnamo Jumatatu, Septemba 5, aliripotiwa kuchagua karatasi za uteuzi katika Bunge la Kitaifa na Seneti, akitaka kuwashawishi wanachama waliochaguliwa kuunga mkono azma yake katika mabunge yote mawili. 

Uamuzi wa kujiondoa ulijiri baada ya makubaliano ndani ya Azimio kutaka kinyang'anyiro cha spika wa Bunge la Kitaifa kushikiliwa na aliyekuwa Spika Kenneth Marende. 

Marende pia alikuwa amechagua karatasi zote mbili za uteuzi kwa Bunge la Kitaifa na Seneti. Mbunge mteule wa eneo bunge la Dadaab Farah Maalim alichaguliwa kuwa naibu wa Marende katika bunge la kitaifa baada ya mwenzake wa Rarieda kuamua kujiondoa.

"NITASTAAFU LAKINI KIONGOZI WANGU NI BABA" RAIS UHURU ASEMA.

 


Rais Uhuru Kenyatta amesema yuko tayari kumkabidhi naibu wake William Ruto mamlaka baada yake kuibuka mshindi wa uchaguzi wa urais. 

 Akiongea katika kikao na wabunge wa muungano wa Azimio katika mkahawa wa Maasai Lodge, Uhuru amesema ni wajibu wake kikatiba kufanya hivyo. 

Katika kile huenda kikazua hisia mseto, Rais alisema atafanya hivyo lakini kiongozi wake atasalia kuwa aliyekuwa mgombea wa urais kwa Azimio. "… nitapeana mamlaka nikiwa natabasamu kwa sababu ni wajibu wangu kikatiba kufanya hivyo, lakini mimi kiongozi wangu ni Baba Raila Odinga," Uhuru amesema. 

 Rais amewakosoa Wakenya kwa kumchagua Ruto akisema wamekataa nafasi ya kuleta umoja nchini. "Mmekataa nafasi ya kuleta umoja humu nchini. 

Si Raila mmenyima nafasi," alisema Rais wakati wa kikao hicho Amewataka viongozi wa Azimio la Umoja kusalia ngangari huku akiwashtumu wale ambao wanaungana na Kenya Kwanza. "Jameni msiwekwe mfuko," alisema akiashiria viongozi ambao wameamua kufanya kazi na muungano wa Ruto. 

Rais alikuwa akiunga mkono Raila kuwa rais wa tano wa kitaifa baada yake kukosana na naibu wake. Wakati wa kikao hicho, alipigia debe Kalonzo Musyoka kuwa Spika wa Seneti akisema wakifaulu kufanya hivyo watakuwa na nafasi ya kuendeleza ajenda za Azimio. 

Sasa Kalonzo watamenyana na aliyekuwa gavana wa Kilifi Amason Kingi ambaye anaungwa mkono na Kenya Kwanza. Katika bunge, Kenneth Marende naye amependekezwa na Azimio huku Kenya Kwanza nao wakiunga mkono Seneta Moses Wetangula. 

Ruto aliibuka mshindi wa uchaguzi wa urais baada ya kujizolea kura 7.1M dhidi ya Raila aliyepata 6.9M.

RC Pwani aziagiza halmashauri kubuni vyanzo vipya vya mapato

 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge akizungumza na wajumbe mbali mbali wa kikao hicho cha kazi.

 Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho cha kazi wakisikiliza mada mbali mbali zilizokuwa zikitolewa. 

Na Victor Masangu,Pwani 


MKUU wa Mkoa wa Pwani,alhaj Abubakari Kunenge , ameziagiza halmashauri zote kuhakikisha kwamba wanajikita zaidi katika kukabiliana na kumaliza migogoro ya ardhi kwa lengo la kuwapa fursa wawekezaji kuja kwa wingi katika kuwekeza viwanda.


Kunenge ametoa Kauli hiyo Wilayani Kibaha ,wakati wa  kikao kazi cha Viongozi wa Mkoa huo kilichohusu  Tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2021/2022, Tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe na ukusanyaji wa mapato.

Katika kikao hicho ambacho kilihudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali wakiwemo wakurugenzi,wakuu wa Wilaya,wakuu wa idara,wakuu wa taasisi mbali mbali za umma pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Pwani lengo ikiwa ni kujadili na kuweka mipango ya kusaidia ukusanyaji wa mapato.

Aidha Kunenge alisema kwamba ni lazima kila kiongozi wa halmashauri husika anapaswa kuona jinsi ya kuwavutia wawekezaji katika maeneo yao ambao wataweza kuleta mabadiliko chanya katika ongezeko la ukusanyaji wa mapato kupitia viwanda vitakavyojengwa.

"Hapa nataka kusisitiza sana kwa halmashauri zote kuondoa kabisa changamoto ya kuwepo kwa migogoro hii ya ardhi kwani nina Imani ikitafutiwa ufumbuzi na maeneo yakawa hayana shida lazima kutawavutia wawekezaji kutoka sehemu tofauti,"alifafanua Kunenge


Mkuu huyo aliwataka wakurugenzi wa halmashauri kuweka mikakati ya kubuni vyanzo vingine vipya vya mapato ambavyo vitasaidia katika kuongeza kasi ya ongezeko la mapato na sio kutegemea chanzo kimoja.


"Ni vema kwa Sasa tukabadilika katika halmashauri zetu kwa kuangalia vyanzo vingine vipya vya matapo ndio serikali yetu inavyotaka kupanga bajeti yake  vizuri ili kuweza kuwahudumia wananchi wake ikiwemo kuwapatia miradi ya maendeleo,"alisema Kuenge.

Katika hatua nyingine aliwasisitiza viongozi wote wa Mkoa huo kuorodhesha makampuni ambayo yamewekeza biashara zao katika Mkoa wa Pwani ili aweze kufuatilia jinsi ya utaratibu mzima inatumika katika kulipa Kodi ya serikali.


Nao baadhi ya viongozi waliohudhulia katika kikao hicho walisema kumekuwepo na wimbi la makampuni kwenda mkoani humo kuchimba madini ya mchanga lakini wamekuwa wakikwepa kulipa kodi hivyo kusababisha kupotea kwa fedha za serikali.

Aidha mmoja wa wadau hao ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo Kasilda Mgeni ameeleza kuwa bado kuna tatizo la ulipaji wa baadhi ya magari yanayotekea Dar es Salaam kwenda kuchukua madini ya kokoto na badala yake hawalipi mapato katika eneo husika hivyo akaiomba serikali kuingilia Kati.


BENKI YA CRDB YAZINDUA ATM YA KUWEKA PESA HADI MILIONI 100

 


Afisa Mkuu wa Uwendeshaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile (wapili kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mashine mpya na ya kisasa ya kuweka pesa ( Deposit ATM) katika hafla fupi iliyofanyika kwenye tawi ya Benki ya CRDB, Mlimani city jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Mkuu wa Kitengo cha Uwakala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Erick Willy (wapili kushoto), Kaimu Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, George Yateta (kulia) pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City, Zaituni Manoro.
---
Wateja wa Benki ya CRDB sasa kupata huduma ya kuweka fedha masaa 24 kupitia ATM za kisasa za kuweka pesa. Hayo yameelezwa leo na Afisa Mkuu Uendeshaji wa Benki hiyo, Bruce Mwile wakati akizindua huduma hiyo katika tawi la Benki ya CRDB Mlimani City.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mwile alisema mashine hiyo inatumia teknolojia ya kisasa ambayo inawawezesha wateja kuweka pesa wenyewe bila usaidizi kwa urahisi, usalama, na unafuu. Mwile alisema mashine hizo zinauwezo wa kupokea hadi shilingi milioni 100 kwa mara moja.

“Tunatambua zipo biashara ambazo zinaendeshwa nje ya muda wa kazi wa kawaida ambapo matawi ya Benki na hata CRDB Wakala wanakuwa wamefunga, mashine hii inakwenda kutatua changamoto hii kwani huduma ya kuweka pesa sasa itapatikana masaa 24 kwa urahisi na usalama zaidi,” alisisitiza.

Pamoja na msisitizo wa mifumo ya kidijitali, ukweli ni kuwa matumizi ya fedha taslimu ‘noti na sarafu’ bado ni makubwa. Hii inaifanya huduma ya kuweka pesa “deposit” kuwa moja ya huduma muhimu za kibenki. Mashine hii ya kisasa ya kuweka pesa iliyozinduliwa na Benki ya CRDB inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa ya kihuduma.

Akieleza namna ya kutumia mashine hiyo Mwile alisema: “Mteja atatakiwa kuchagua lugha anayopenda kati ya kiswahili na kingereza, kisha ataweka TemboCard yake na kuingiza namba ya siri. Mteja ataweka pesa hadi noti 200 na kisha kubonyeza kitufe cha ‘Weka Pesa’, kisha utapokea taarifa kupitia ujumbe mfupi.”

Mwile aliongezea kuwa pamoja na kuzindua mashine hiyo katika tawi la Mlimani City, Benki ya CRDB pia inatarajia hadi ifikapo mwishoni mwa mwezi Oktoba itazindua mashine nyengine za kisasa zaidi katika miji na sehemu zote zenye biashara kubwa kote nchini ikiwemo Mwanza, Arusha, Dodoma.

Benki ya CRDB inatajwa kuwa Benki kiongozi nchini ikiongoza katika ubunifu wa huduma na bidhaa zinazokidhi mahitaji halisi ya wateja. Benki ya CRDB inaongoza kwa kuwa na mtandao mpana zaidi wa utoaji huduma kupitia matawi zaidi ya 260, CRDB Wakala zaidi ya 22,000, ATMs zaidi ya 550, na vifaa vya manunuzi (PoS) zaidi ya 2,500.

Benki ya CRDB pia inaongoza kwa ubunifu wa mifumo ya kidijitali ya utoaji huduma ikiwamo SimBanking, SimAccount, Internet Banking, na TemboCard. Mtandao wa Benki hiyo umevuka mipaka hadi Burundi ambapo ina kampuni tanzu, na hivi karibuni inatarajia kuingia katika nchi ya Jamhuru ya Kidemokrasia ya Congo.

Mkuu wa Kitengo cha Uwakala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Erick Willy (wapili kulia) akiweka taarifa zake katika mashine ya kuweka pesa ( Deposit ATM) wakati wa hafla ya uzinduzi wake uliofanyika kwenye tawi ya Benki ya CRDB, Mlimani city jijini Dar es salaam.

Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City, Zaituni Manoro akizungumza katika hafla fupi ya uzinduzi wa mashine mpya na ya kisasa ya kuweka pesa ( Deposit ATM) iliyofanyika kwenye tawi ya Benki ya CRDB, Mlimani city jijini Dar es salaam.




MAMA KOKA KULETA MAGEUZI YA KIUCHUMI KWA WANAWAKE WA UWT KIBAHA MJI.

Baadhi ya viongozi wa uwt Wilaya ya Kibaha mji wakiwa katika picha ya pamoja  

Na Victor Masangu,Kibaha


Mlezi wa umoja wa wanawake wa Chama Cha mapinduzi Wilaya ya Kibaha mjini (UWT) Selina Koka ameahidi kushirikiana bega kwa bega na wanawake wenzake kwa lengo la kuweza kuleta chachu ya maendeleo na kukuza uchumi.

Selina ambaye ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ameyasema hayo Leo wakati wa baraza la la UWT lililoandaliwa kwa lengo la kutoa mafunzo ya uongozi kwa wanawake hao kutoka kata mbali mbali.

Alisema kwamba nia na dhamira yake ni  kuhakikisha anaweka mipango madhubuti ikiwemo kuanzisha Saccos ambayo itaweza kuwasaidia wanawake wa Jimbo la Kibaha mjini kujikwamua  kiuchumi na kuondokana na wimbi la umasikini.


"Kitu kikubwa ninachotaka kuwaambia Mimi Sina upendeleo na mwanamke yoyote yule lakini ninachotaka kusema kikubwa wakinama wasiniangushe lengo ni kujipanga kuanzia ngazi za kata ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi,"alisema Mama Koka.

Pia aliongeza kuwa katika kuwawezesha kiuchumi atatembelea katika kata mbali mbali na kupeleka wakufunzi kwa ajili ya kuwapa mafunzo ya ujasiriamali pamoja na Mambo mengine yanayohusiana na maendeleo.

Aidha aliwataka wanawake wa UWT kuwa na vitega uchumi na kwamba atakuwa mstari wa mbele katika kusaidia juhudi zao na atajitahidi kwa hali na mali  kufufua miradi ambayo imekwama katika ngazi ya kata.

"Kitu kikubwa wanawake wa UWT mnapaswa kuwa na mipango ya maendeleo ikiwemo Jambo la kuwa na vitega uchumi na hili jambo kwa upande wangu nitasaidiana na wenzangu katika Jambo hili,"alisema Selina.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Mariam Mugasha alimpomgeza kwa dhati mlezi wao kwa juhudi zake na ushirikiano ambao anautoa kwa wanawake hao.

Monday, September 5, 2022

TBS YAWANOA MAAFISA BIASHARA NA AFYA PWANI

 Na Victor Masangu,Pwani 

Serikali mkoani Pwani imewataka watumishi wa halmashauri hususan maafisa afya na biashara kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo katika kudhibiti ubora wa bidhaa zinazozalishwa ziwe na viwango vinavyotakiwa kwa mujibu wa Sheria na taratibu.


Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Zuwena Jiri wakati kufungua mafunzo ya siku moja kwa watendaji wa halmashauri tisa za Mkoa wa Pwani juu ya kujifunza mwongozo wa utekelezaji wa majukumu ya ushirikiano wa na Shirika la viwango wa Tanzania (TBS)

Katibu huyo aliongeza kuwa watumishi hao wanapaswa kuyatumia vema mafunzo hayo waliyoyapata katika kuwahudumia wananchi wote ambao wapo katika halmashauri zao na kwamba katika suala zima la kuhakiki ubora wa bidhaa.

"Azma ya serikali ni kwa ajili ya kushughulikia mambo mbali mbali ya udhibiti wa bidhaa ambazo zinazalishwa ikiwemo bidhaa vipodozi pamoja na chakula pamoja na biashara kuwa na viwango vya hali ya juu,"alisema Katibu huyo.

Pia maafisa wa afya pamoja na maafisa biashara inatakiwa wawe na sifa na kuzingatia maadili na miongozi yote katika kukabiliana na udhibiti wa bidhaa mbali mbali hivyo serikali itaendelea kushirikiana na Tbs ili kutoa elimu zaidi kwa watumishi.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la viwango Tanzania (TBS) Dkt. Ngenya Yusuph amebainisha kuwa lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu kwa  watumishi ili waweze kupata fursa ya kuwahudumia wananchi katika suala la udhibiti ubora wa bidhaa.


Aidha alifafanua mafunzo hayo yataweza kuwajengea uwezo zaidi watumishi wa halmashauri hizo za Mkoa wa Pwani katika suala zima la kueaelimisha wananchi wa ngazi za chini kuhusiana na udhibiti wa ubora wa bidhaa zao.

"Leo tupo hapa Wilayani Kibaha na sisi Kama tbs kwa kushirikiana na serikali tumeona Kuna umuhimu mkubwa wa kuwakutanisha maafisa wa  afya na biashara katika kuwapatia elimu juu ya udhibiti ubora wa bidhaa katika vipodozi na masuala ya chakula,"alisema Mkurugenzi huyo.


Nao baadhi wa washiriki wa mafunzo hayo wameahidi kuyatumia vema mafunzo hayo ambayo wamedai yataweza kuwaongezea ufanisi mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yao.



Mafunzo hayo ya siku moja ambayo yamewashirikisha maafisa biashara na maafisa afya kutoka halmashauri zote Tisa za Mkoa wa Pwani yameandaliwa na Shirika la viwango Tanzania (TBS).

RUTO ASHINDA KESI YA UCHAGUZI, NDIYE RAIS ANAYESUBIRI KUAPISHWA.

Philomena Mwilu (kushoto) na Martha Koome wakati wa moja ya mikutano ya kusikilizwa kwa kesi ya urais.

 Jaji Mkuu wa Mahakama ya Upeo Martha Koome hatimaye ametangaza kuafiki uamuzi wa ushindi wa Rais Mteule William Ruto, kwenye kesi iliyowasilishwa na muungano wa Azimio la Umoja. 

Akitoa uamuzi huo siku ya Jumatatu, Koome alisema kwamba makamishna wanne waliojitenga na kutangazwa kwa matokeo ya mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati hawakuwa na ushahidi kwamba uchaguzi wa Agosti 9 ulitiwa doa. 

Vile vile Jaji Mkuu alidokeza kuwa ushahidi wa John Githingo haukuafikia viwango vinavyotakikana. 

Wakati huo huo mgombea urais wa Azimio Raila Odinga ameposti picha akifuatilia mwenendo wa kesi hiyo ya uchaguzi kwa njia ya television.

 

Raila alikuwa amesema kuahirishwa kwa chaguzi hizo ulikuwa ni njama ya mahasimu wake kwa ushirikiano na mwenyekiti, kusababisha watu wasijitokeze kumpigia kura katika maeneo hayo ambayo ni ngome yake.

Tayari shamrashamra zimeanza kulipuka, huku baadhi ya television zikionesha matukio mbalimbali toka viunga tofauti tofauti kwa wananchi wa taifa hilo wakishangilia ushindi wa bwana Ruto.

KISINDA APIGWA STOP USAJILI YANGA.


 

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)


MAKOSA YA UONGOZI WA YANGA AU TFF? CHANZO:- JUMA AYO

✍kama yanga walikuwa wameshakamilisha idadi ya wachezaji 12 wa kimataifa alafu ghafla wakamuongeza Kisinda jumla wanakuwa na wachezaji 13 kama walikuwa na option ya kumtoa mchezaji mmoja ii kisinda achukue nafasi lazima wavunje mkataba wa huyo mchezaji au wamuuze kwenda timu A au wamtoe kwa mkopo ili usajili wake ufutwe kwenye orodha.

✍Lakini kama yanga walikuwa wanatoa jina tu la mmoja ili kisinda aingie kwenye system na huyo mchezaji anakuwa hajafutwa kwenye mipangi ya klabu bado wanakuwa na wachezaji 13 kinyume na kanuni.
Huu ndio utaratibu ninavyojua mimi.

✍Maswali ya msingi
Je yanga walipokuwa wanaomba mabadiliko ya wachezaji walianisha kama wanamtaka mchezaji fulani acheze kimataifa au waliomba mchezaji abadilishwe kwasababu Kuna mmoja ana majeraha??

✍Kanuni ya wachezaji wa kigeni ndani ya nchi ni 12 tu na hakuna klabu inapswa kuvuka idadi hii....yanga wanayo room ya kwenda kwenye kamati lakini hakuna usajili wa mchezaji 13 inapswa kutolewa pia tukumbuke kabla dirisha kufungwa kuna dirisha la CAF ambayo klabu zote zilishatuma idadi ya wachezaji wake ambao ni 12 na tff ndio wanatuma majina hayo CAF mapema.

LIVE: SUPREME COURT JUDGMENT ON PRESIDENTIAL ELECTION PETITION


 

"Hukumu katika ombi hili itatolewa leo Jumatatu, tarehe 5 Septemba, 2022, saa 6 mchana katika Mahakama ya Juu ya Kenya ya Milimani," taarifa kutoka kwa msajili mkuu wa mahakama ya juu ilisoma.

Mahakama hiyo inatarajiwa kushikilia au kubatilisha ushindi wa Rais Mteule William Ruto katika chaguzi za Agosti 9.

Azimio pia walidai kuwa IEBC haiwezi kuhesabu kura 250,000, bila kujumuisha kura zilizopigwa.

Raila na mgombea mwenza waliitaka mahakama kuu kuwatangaza rais mteule na naibu rais mteule mtawalia.

Raila pia alitaka ukaguzi wa kina na wa kitaalamu wa vifaa na teknolojia zote zilizotumiwa na tume ya uchaguzi katika uchaguzi wa urais.

MWENGE WA UHURU UMEZINDUA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA SH.BILIONI 1.6 IRINGA

 

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akikabidhiwa mwenge wa Uhuru na Mkuu wa wilaya ya Mufindi Saad Mtambule kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa wilayani humo

Wakimbiza mwenge wa Uhuru kitaifa wakiendelea kukimbiza Mwenge wa Uhuru kwenye miradi ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa
Moja ya mradi ambao mwenge wa Uhuru uliukagua wakati ulipokuwa kaka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa


Na Fredy Mgunda, Iringa.


Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo amesema Mwenge wa Uhuru umezindua miaradi ya bilioni moja na Milioni mia tisa(1,600,000,000) katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Akizungumza mara baada ya miradi yote kuzinduliwa mkuu wa wilaya ya Iringa Moyo alisema kuwa miradi ambayo imezinduliwa ni madarasa mawili ya shule ya sekondari Tangamenda ya mradi wa 5441TC RP, Isakalilo sekondari kwa kuweka jiwe la msingi,kuweka jiwe la msingi hospital ya Frelimo, kuzindua barabara ya mtwivila darajani Ikonongo kwa kiwango cha lami kilometa 1.4 na miradi ya huduma ya jamii na kiichumi kwa maendeleo ya wananchi wa kikundi cha Ebenezer.

Moyo alisema kuwa kuwa anawashukuru wakimbiza mwenge wa Uhuru kwa kuikubali miradi yote kwa ubora ambao unatakiwa kutekelezwa kulingana na thamani ya fedha.


Alisema kuwa anawapongeza wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa kujitokeza kwa wingi kuulaki mwenge wa Uhuru ulipokuwa unakimbizwa kwenye Halmashauri hiyo.

Lakini pia mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na viongozi wakimbiza mwenge wa Uhuru kitaifa kwa ajili ya kuimarisha ubora ya miradi na utumishi wa UMMA.

Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa,Sahili Nyanzabara Geraruma alisema kuwa viongozi Manispaa ya Iringa wamejitahidi kusimamia miradi ambayo inatekelezwa kwa fedha za serikali kuu na serikali za mitaa kwa lengo la kuleta maendeleo ya wananchi.

Geraruma alisema kuwa viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na mkuu wa wilaya ya Iringa wanatakiwa kuwa makini kuangalia namna ambavyo miradi yote inayotekelezwa ili kukidhi vigezo kulingana na thamani ya fedha ilayotolewa na serikali.