ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 19, 2025

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU NLD YABADILISHA NEMBO NA BENDERA YA CHAMA YAELEZA NI HATUA KUBWA YA KIHISTORIA KWAO

 

 TAARIFA RASMI KUTOKA CHAMA CHA NLD

APRILI 18, 2025,

MABADILIKO YA NEMBO NA BENDERA YA CHAMA, NI HATUA YA KIHISTORIA KWA NLD.

Chama cha National League for Democracy (NLD) kinapenda kuwataarifu wanachama, wafuasi na wananchi kwa ujumla kuwa, kufuatia Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika tarehe 10 Aprili 2025, wajumbe wa mkutano huo kwa kauli moja waliridhia mapendekezo ya kubadilisha bendera na nembo ya chama.

Mabadiliko haya ni ya heshima na kihistoria, yakilenga kusawiri kwa undani zaidi maono, dira, na mwelekeo mpya wa chama chetu kuelekea kujenga taifa lenye demokrasia imara, usawa wa kijamii, Uzalendo Haki na Maendeleo.
Kupitia uongozi imara wa Mwenyekiti wa Taifa Mhe. Khamis Mfaume na Katibu Mkuu Doyo Hassan Doyo, Sekretarieti ya chama imekamilisha maboresho ya nembo na bendera mpya, ambazo sasa zinakwenda kutambulika rasmi kitaifa na kimataifa kama utambulisho wa chama.

RANGI YA BENDERA MPYA YA NLD NA MAANA YAKE.

Njano, Inaashiria maliasili, misitu na madini.

Nyeusi, Ni alama ya utu wetu, asili yetu na uafrika wetu.

Bluu, Inawakilisha rasilimali za maji, bahari, mito na maziwa (Blue Economy).

Nyekundu, Inawakilisha harakati za mapambano ya demokrasia katika nchi yetu.


NEMBO MPYA YA NLD.

Mkono mmoja wa ushindi (Victoria), unaashiria matumaini, nguvu na mafanikio.

Nyota tatu, zinawakilisha dira isiyo na kikomo ya chama chetu.


Kwa niaba ya uongozi wa chama, tunawapongeza sana wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kwa uamuzi huu wa busara na kizalendo. Mabadiliko haya yanadhihirisha kukua kwa chama na dhamira ya chama kusimamia misingi ya demokrasia, utawala bora na mshikamano wa kitaifa.

#NLD #MageuziYaKihistoria #DemokrasiaKwaVitendo #BenderaMpyaNLD #NemboMpyaNLD

NLD: Ukombozi wa Umma.
NLD: Mtetezi wa Umma.
NLD: Moto Moto Motooo!

Imetolewa na: Idara ya Habari na Mawasiliano
Chama cha NLD
Tandika, Temeke Jijini Dar es salaam, Tanzania
Tarehe: 18 Aprili 2025

Friday, April 18, 2025

JUMUIYA YA WAZAZI WILAYA YA BAGAMOYO YAFANYA BALAAA ZITO KATA YA ZINGA

 


VICTOR MASANGU,BAGAMOYO

Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo imetumia wiki ya maadhimisho ya wazazi kwa kufanya ziara ya kwenda kutoa msaada wa matofali elfu moja na mifuko ya saruji kwa ajili ya kusapoti  mradi wa ujenzi wa zahanati ya Kondo  iliyopo katika kata ya Zinga pamoja na mifuko ya saruji kwa lengo la kuweza kuwasogezea huduma wananchi kuondokana na  adha na kero ya kutembea umbari mrefu.
 

Pia Jumuiya hiyo wa wazazi imeweza kutumia wiki ya maadhimisho hayo kwenda kuzindua mradi wa duka la jumla na rejareja ambalo litakuwa  likiuza bidhaa mbali mbali ikiwemo nguzo za chama,pamoja na vifaa vingine ikiwemo pamoja na kwenda kufungua shina la wakereketwa la kibulu la wafugaji.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo Abubakari Mlawa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maaadhimisho hayo ameweza kuambatana na viongozi mbali mbali wa jumuiya mbali mbali ikiwemo wenyeji ambao ni  jumuiya ya wazazi na kufanya ziara kwa ajili ya kutembelea miradi hiyo ya kitega uchumi.

Mwenyekiti Mlawa ameipongeza kwa dhati jumuiya ya wazazi kata ya Zinga kwa kuweza kutekeleza ilani kwa vitendo ikiwemo kuweka mikakati madhubuti ya kuweza kuanzisha vitega uchumi vyao ambavyo vitaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa  kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondokana na wimbi la umasikni na kuondokana na kuwa tegemezi.

"Kwa kweli mimi nimefarijika sana kuungana na jumuiya ya wazazi katika kuadhimisha wiki yao na mimi nimeungana nao na kwa kweli nawapongeza sana kwa kuweza kuwa wabunifu kwa kuanzisha miradi ya kwa ajili  ya vitega uchumi ikiwemo kufungua duka kubwa la nguo na vifaa mbali mbali vya ccm kwa hiyo nina imani na kata nyingine zitaweza kuiga mfano huo kama walivyofanya kata ya Zinga.

Aidha Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa katika Wilaya ya Bagamoyo wameweza kujipanga kwa ajili ya kujiandaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ambapo wamemejipanga vya kutosha kumsapoti na kumpa kura nyingi za  kishindo  cha zaidi ya asilimia 96 Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kadhalika Mwenyekiti huyo katika kuhakikisha kwamba anaiboresha jumuiya hiyo na kuiimarisha ameamua kuchangia  mabati 72 kwa ajili ya mradi wa  ujenzi wa nyumba ya katibu ya jumuiya ya wazazi ambayo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kwa mtendaji huyo kutekeleza majukumu yao ipasavyo ambapo pia ameahidi kuwasaidia kuwapa sapoti ya kuwaongezea mtaji wa bidhaa katika duka hilo.  

Kwa upande wake Katibu wa umojawa jumuiya ya wazazi Wilaya ya Bagamoyo Halima Dosa  amebainisha kwamba lengo lao kubwa la jumuiya hiyo ni kuhakikisha kwamba kila kata inakuwa na vitega uchumi mbali mbali ili kuweza kuondokana na kuwa tegemezi na kuondokana wimbi la umasikini.

Alisema kwamba ameridhishwa na viongozi wa jumuiya ya wazazzi Kata ya Zinga kwa kuamua kusaidia jamiii ikiwemo kutoa matofali elfu moja kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Zahanati ikiwa pamoja na kuzindua mradi mwingine wa duka ambalo litakuwa linauza bidhaa mbali mbali pamoja na nguo za chama.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Kata ya Zinga Hassan  Kashingo amebaisha kwamba katika Kata ya Zinga wamejipanga  na kuweka mikakati madhubuti ikiwemo kuwa ni mradi mbali mbali ya kitega uchumi amabyo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo na kukuza uchumi kwa jumuiya ya wazazi.

Maadhimisho ya wiki ya  wiki ya jumuiya ya wazazi  katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo yamefanyika katika eneo la viwanja vya Mnada wa mbuzi,na ng'ombe lililopoKata ya Zinga na kuhudhuria na viongozi mbali mbali wa chama pamoja na jumjiya zake ikiwemo viongozi wa serikali pamoja na wananchi kutoka kata zote 11.

Benki ya CRDB, COSTECH wasaini mkataba wa shilingi bilioni 2.3 kuwezesha biashara za vijana

 


Dar es Salaam. Tarehe 17 Aprili 2025: Katika kuimarisha ubunifu na ujasiriamali miongoni mwa vijana nchini, Benki ya CRDB kupitia taasisi yake ya CRDB Bank Foundation na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) wamesaini mkataba wa shilingi bilioni 2.3 kwa ajili ya kuziwezesha biashara changa za vijana.

Makubaliano hayo yaliyoshuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda, ni sehemu ya Programu ya IMBEJU kupitia dirisha lake la IMBEJU BUNI yakilenga kuwasaidia vijana wabunifu nchini kupata elimu ya fedha na mitaji nafuu ya kukuza biashara zao.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini, Waziri Mkenda amesema: “Hii ni hatua ya kupongezwa inayochochea ukuaji wa uchumi wa ubunifu. Ushirikiano huu ni jibu la changamoto ya kukosekana kwa ufadhili kwa vijana wabunifu na ni kielelezo cha juhudi za serikali kujenga uchumi shindani wa viwanda wenye ubunifu.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa ameeleza kuwa ushirikiano huu una akisi dhamira ya Benki ya CRDB kushiriki kujenga uchumi jumuishi.

“Tangu kuanzishwa kwa Programu ya IMBEJU Machi 2023, tulilenga kuwafikia vijana na wanawake waliopo pembezoni na kuwapa fursa za kifedha. Kupitia mkataba huu, tunatarajia kuwafikia vijana zaidi ya 1,000 na kuwapa mitaji wezeshi, mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha ili waweze kuendesha biashara endelevu kwa mfumo rasmi hivyo kuwa rahisi kwao kukua zaidi,” amesema Tully.

Katika kipindi hiki cha ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na COSTECH, zaidi ya vijana 700 wabunifu wamefikiwa na kuwezeshwa kupitia dirisha la IMBEJU Buni ambalo ni mahsusi kwa ajili ya wabunifu wenye biashara changa kwa kuwapa mafunzo na mitaji wezeshi yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 5.

Katika utekelezaji wa mkataba uliosainiwa, kutakuwa na kamati ya pamoja ya usimamizi (Steering Committee) kati ya Benki ya CRDB, CRDB Bank Foundation na Tume ya Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya kufanya tathmini, ufuatiliaji, na usimamizi madhubuti wa utekelezaji ili kuhakikisha kunakuwa na uwazi wa kutosha kulifikia lengo lililowekwa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu amesema, “Tunaendelea kujenga mazingira wezeshi kwa vijana kubuni na kustawi kibiashara. Ushirikiano huu na CRDB Bank Foundation ni muendelezo wa safari tuliyoianza mwaka 2023, na sasa tunaongeza msukumo zaidi kufanikisha ndoto za vijana wengi.”

Tangu kuanzishwa kwake, Programu ya IMBEJU imekuwa mfano wa kuigwa katika uwezeshaji jumuishi. Katika kipindi cha mwaka mmoja tu, programu hii imewezesha zaidi ya vijana na wanawake milioni moja na kutoa mitaji wezeshi zaidi ya TZS bilioni 20 katika sekta mbalimbali.

Kupitia madirisha yake ya IMBEJU BUNI, IMBEJU NG'ARA ambalo ni mahsusi kwa ajili ya wanawake, IMBEJU KILIMO kwa ajili ya wakulima wadogo wadogo na IMBEJU UBIA kwa ajili ya kukuza ushirika wa kimkakati ili kutekeleza kwa ufanisi program mbalimbali za uwezeshaji kwa vijana na wanawake, CRDB Bank Foundation imefanikiwa kutoa uwezeshaji muhimu kwa ajili ya kukuza biashara changa za vijana na wanawake wajasiriamali kote nchini.
















IBADA YA IJUMAA KUU,18.04.2025.

 Karibu nyote nyumbani mwa Bwana tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.

Toa sadaka yako kupitia MBEZI BEACH LUTHERAN HUDUMA". MAENDELEO BANK 014154966021, CRDB 0150080095503, M-PESA+255769217618.

Wednesday, April 16, 2025

SERIKALI YAZINDUA MRADI WA MAJI KIJIJI CHA TUNGAMAA PANGANI, WANANCHI ZAIDI YA 2500 KUNUFAIKA

 

 


Na Oscar Assenga,Pangani

ZAIDI ya Wananchi 2500 wa Kijiji cha Tungamaa wilayani Pangani mkoani Tanga watanufaika na mradi wa Maji baada ya Serikali kutekeleza mradi katika eneo hilo uliogharimu kiasi cha Milioni 500 kupitia Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA)

Akizungumza wakati akizindua mradi huo ambao umetekelezwa kwa muda mfupi kwa kutumia Force Akaunti, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt,Balozi Batilda Burian,Mkuu wa wilaya ya Pangani Gift Msuya alisema utakuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi.

Alisema matarajio yao kutokana na utekelezaji wa mradi huo na mengine mikubwa ya maji katika kata za nne za wilaya hiyo na maeneo mengine wana uhakika ifikapo Desemba mwaka huu upatikanaji wa maji utafikia asilimia 90.2.

Alisema hilo linatokana na miradi mikubwa inayotekelezwa, Mkwaja, Sange, Madanga na Bushiri na maeneo maengine wana uhakika kufikia kiwango hicho cha upatikanaji wa maji na kwa upande wa mijini wana miradi miwili ya inayotekelezwa wa hati fungani.

Ambapo alisema mradi huo wa hatifungani ni kuboresha miundombinu ya usambazaji wa maji mjini kwa kuiondosha ya zamani chakavu na kuweka mipya na mradi wa mji 28 ambao uliwekwa jiwe la msingi na Rais Dkt Samia Suluhu alipofanya ziara Tanga.

Alisema kwamba na mradi huo utafanyika kwenye kata kata ya Madanga,Ubangaa na Pangani Mashariki na Magharibu ambapo mpaka sasa upatikanaji wa maji Mijini ni asilimia 76 na mradi utakapokamilika Desemba watakiwa wamefikia upatikanaji wa maji asilimia 100 na kuvuka lengo la utekelezaji wa ilani asilimia 95 kwa upatikani wa maji mijini kwa wilaya ya Pangani.

“Ndugu zangu niwaambie kwamba hakuna mbadala wa maji ndio sababu hakuna maendeleo yanaweza kuja bila kuwepo kwa maji kwa sababu wananchi wakikosa maji hakutakuwa na utulivu wa kiasiasa wala uchumi hivyo uchumi unaonekana kwa sababu huduma za maji zinapatikana na niwapongeze Ruwasa kwa kazi nzuri na juhudi mnazozionyesha kuwapatia wananchi huduma safi ya maji salama na kutosheleza “Alisema

Awali akizungumza kuhusu mradi huo ,Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Omari Lugongo alisema kwamba mradi huo ulizinduliwa mwaka jana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian na mwaka huu ameuzindua mradi huo wa maji ambao miuondombinu yake inaruhusu kuteka maji sio kwenye vilula tu na inaruhusu kuunganisha maji majumbani.

“Kwenye mji huu ambao mradi umezinduliwa kuna kaya zaidi ya 600 na mpaka sasa kaya 20 zimeunganishwa maji kwenye nyumba zao kwa hiyo tunaendelea kuwahamasisha wananchi kuunganisha nyumba kwenye nyumba zao”Alisema

Aidha alisema kwa Mkoa wa Tanga tayari wilaya ya Pangani wamekwisha kutekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 100 ambapo hali ya upatikanaji wa maji mpaka sasa ni asilimia 86 lakini kimkoa ni asilimia 75 .

Hata hivyo alisema kwa hiyo wilaya hiyo ilani imetekeleza kwa asilimia 100 na wilaya nyengine wanaendelea na wanatategemea ifikapo Desemba 2025 zaidi ya asilimia 90 wananchi wa Pangani watapata maji safi na salama kwa eneo la Vijijini na Mijini.


Tuesday, April 15, 2025

HALMASHAURI YA WILAYA YA BAGAMOYO YATEKELEZA AGIZO LA RAIS YAPANDA MITI 500 ENEO LA ZINGA KUBORESHA MAZINGIRA

NA VICTOR MASANGU/PWANI. IMESOMWA NA ALBERT G.SENGO Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani katika kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hasana la kutunza na kuhifadhi mazingira ambapo imefanikiwa kupanda miti zaidi ya mia 500 katika eneo la mnada wa mbuzi na ng'ombe uliopo katika Kata ya Zinga kwa mtoro lengo ikiwa ni kuweza kurudisha uoto wa halisi uliopotea pamoja na kupambana na wimbi la na ukataji wa miti ovyo ambao unasabisha hali ya ukame.

AZIZ KI WA MOTO, CHAMA AMEWAKA YANGA YAITANDIKA STAND UNITED 8-1 MWENGE

MABINGWA watetezi, Yanga SC wamefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 8-1 dhidi ya Stand United jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.

Nyota wa mchezo wa leo ni kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Burkina Faso aliyehusika kwenye mabao saba kwa kusaidia upatikanaji mabao matatu na yeye mwenyewe kufunga manne.

Alifunga mabao yake dakika za 10,48, 58 na 61 huku pia akiwasetia beki Nickson Kibabage kufunga dakika ya 20 na kiungo Mzambia, Clatous Chama mawili, dakika ya 32 na 40.

Bao la nane la Yanga liliparikana kwa ushirika wa wachezaji waliotokea benchi, mshambuliaji Mzambia - Kennedy Musonda akifunga kwa kumalizia krosi ya kiungo Farid Mussa, huku bao pekee la Stand United likifungwa na Msenda Senda dakika ya 48.

Yanga sasa itakutana na JKT Tanzania ambayo jana iliitoa Pamba Jiji FC ya Mwanza kwa kuichapa mabao 3-1 Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam.

Nusu Fainali itazikutanisha Simba SC  iliyoitoa Mbeya City kwa kuichapa mabao 3-1  juzi hapo hapo Uwanja wa KMC na Singida Black Stars iliyoitoa Kagera Sugar kwa kuifunga mabao 2-0 Uwanja wa CCM LITI mjini Singida jana.

CCM TANGA WAMSHUKURU MBUNGE UMMY MWALIMU KWA KUWEKEZA KWA VIJANA KUPITIA MICHEZO

 

Na Oscar Assenga,Tanga. 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tanga, Shabani Hamisi, amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa kuandaa mashindano ya Oddo Ummy Cup kwa kushirikiana na chama cha mpira mkoa wa Tanga (TRFA) akisema kuwa ni hatua muhimu katika kukuza vipaji vya vijana jijini humo.

Akizungumza kama mgeni rasmi kwenye fainali ya mashindano hayo, Hamisi alisema kuwa michezo ni ajira kwa vijana kama zilivyo ajira nyingine, na ni njia mojawapo ya kuimarisha mahusiano na kuwaepusha na vitendo viovu.
"Kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge, nipo hapa kama mgeni rasmi kuhakikisha kuwa mashindano haya yanakuwa chachu kwa vijana katika kujikwamua kiuchumi. Michezo ni ajira, na pia ni njia bora ya kujenga nidhamu na mahusiano bora katika jamii," alisema.
Aidha Alisema kuwa Ummy Mwalimu amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha vijana wa Tanga wanashiriki katika michezo mbalimbali na kutumia fursa zinazojitokeza. Alisisitiza kuwa mbunge huyo yuko tayari kushirikiana na vijana katika nyanja tofauti ili kuwawezesha kufikia ndoto zao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Tanga (TRFA), Martin Kibua, aliwataka wachezaji na makocha kuzingatia sheria za mchezo, huku akipiga marufuku wachezaji kuhama hama katika timu bila kufuata utaratibu rasmi.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Hassan Nyelo, alieleza kuwa ligi ya mwaka huu imekuwa ya kihistoria kutokana na udhamini mkubwa uliotolewa na Mbunge huyo, ikiwa ni mara ya kwanza kwa ligi ya wilaya kupata udhamini wa asilimia 100, ikijumuisha michezo 98 na zawadi zote.
"Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hasa katika sekta ya michezo. Ameahidi kuendeleza juhudi hizi kwa michezo mingine zaidi baada ya mpira wa miguu," aliongeza.
Nyelo alihitimisha kwa kuwaomba vijana na wakazi wa Tanga kuendelea kumuunga mkono Mhe. Oddo Mwalimu kwa juhudi zake za kukuza maendeleo ya vijana kupitia michezo.




HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAUNGA JUHUDI ZA RAIS SAMIA KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YAPANDA MITI 500 ZINGA

 


VICTOR MASANGU, BAGAMOYO

Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani  katika kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hasana  la  kutunza na kuhifadhi  mazingira ambapo imefanikiwa kupanda miti   zaidi ya mia 500  katika eneo la mnada wa mbuzi na ng'ombe uliopo katika Kata ya Zinga kwa mtoro lengo ikiwa ni kuweza kurudisha uoto wa halisi uliopotea  pamoja na  kupambana na wimbi la  na ukataji wa miti ovyo ambao unasabisha hali ya ukame.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo Stellah Msofe wakati wa maadhimisho ya siku ya upandaji wa miti ngazi ya Wilaya ambayo yamefanyika katika eneo la Zinga kwa mtoro ambapo amewataka wakuu wa idara, watendaji,zikiwemo taasisi binafsi kuweka mikakati ya kuhimiza suala la upandaji wa miti ili kutimiza agizo la serikali la kupanda miti milioni 1.5 kwa kila mwaka.

Alisema kwamba serikali imeamua kwenda kupanda miti katika eneo hilo la mnada wa Zinga kutokana na kubaini kwamba mazingira yake yameathirika kwa kiasi  kutokana na kuwepo kwa shughuli mbali mbali za kibinadamu ikiwemo suala la uchimbaji wa mchanga hivyo wakaona kun aumuhimu mkubwa sana katika kuhakikisha anapanda miti mingi ambayo itasaidia kurejesha hali yake ya kawaida.


Naye Mkuu wa kitengo cha maliasili na mazingira katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoto Dkt. Obed Mwinuka amebainisha kwamba lengo lao  kubwa ni kutekeleza kampeni ya  kitaifa katika kuboresha mazingira ambapo wamefanikiwa kupanda miti ipatayo 500 katika eneo hilo la mnada wa mbuzi na ng'ombe lililopo kata ya Zinga.
 
Pia alisema kwamba lengo kubwa la Halmashauri ni kuhakikisha kwamba wanapanda miti mingi ambayo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na changamoto ya ukame ambao umekuwepo katika baadhi ya maeneo na kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha utunzaji wa mazingira .

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo amebainisha kwamba hadi sasa wameshafanikiwa kupanda miti zaidi ya laki saba na kwamba lengo na mikakati waliyojiwekea ni kufikia lengo la  serikali la kupanda miti  milioni 1.5 ambayo itakuwa ni mkombozi mkubwa katika kurudisha hali nzuri ya uoto wa hasiri.

Mmoja wa wawekezaji katika mnada huo wa Zinga kwa mtoro  Hassan  Kashingo  akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara wenzake ameahidi kushirikiana bega kw abegaa naa serikali ikiwa pamoja na kuitunza miti hiyo 500 ambayo imepandwa katika eneo hilo la mnada.