ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 15, 2025

HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAUNGA JUHUDI ZA RAIS SAMIA KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YAPANDA MITI 500 ZINGA

 


VICTOR MASANGU, BAGAMOYO

Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani  katika kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hasana  la  kutunza na kuhifadhi  mazingira ambapo imefanikiwa kupanda miti   zaidi ya mia 500  katika eneo la mnada wa mbuzi na ng'ombe uliopo katika Kata ya Zinga kwa mtoro lengo ikiwa ni kuweza kurudisha uoto wa halisi uliopotea  pamoja na  kupambana na wimbi la  na ukataji wa miti ovyo ambao unasabisha hali ya ukame.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo Stellah Msofe wakati wa maadhimisho ya siku ya upandaji wa miti ngazi ya Wilaya ambayo yamefanyika katika eneo la Zinga kwa mtoro ambapo amewataka wakuu wa idara, watendaji,zikiwemo taasisi binafsi kuweka mikakati ya kuhimiza suala la upandaji wa miti ili kutimiza agizo la serikali la kupanda miti milioni 1.5 kwa kila mwaka.

Alisema kwamba serikali imeamua kwenda kupanda miti katika eneo hilo la mnada wa Zinga kutokana na kubaini kwamba mazingira yake yameathirika kwa kiasi  kutokana na kuwepo kwa shughuli mbali mbali za kibinadamu ikiwemo suala la uchimbaji wa mchanga hivyo wakaona kun aumuhimu mkubwa sana katika kuhakikisha anapanda miti mingi ambayo itasaidia kurejesha hali yake ya kawaida.


Naye Mkuu wa kitengo cha maliasili na mazingira katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoto Dkt. Obed Mwinuka amebainisha kwamba lengo lao  kubwa ni kutekeleza kampeni ya  kitaifa katika kuboresha mazingira ambapo wamefanikiwa kupanda miti ipatayo 500 katika eneo hilo la mnada wa mbuzi na ng'ombe lililopo kata ya Zinga.
 
Pia alisema kwamba lengo kubwa la Halmashauri ni kuhakikisha kwamba wanapanda miti mingi ambayo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na changamoto ya ukame ambao umekuwepo katika baadhi ya maeneo na kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha utunzaji wa mazingira .

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo amebainisha kwamba hadi sasa wameshafanikiwa kupanda miti zaidi ya laki saba na kwamba lengo na mikakati waliyojiwekea ni kufikia lengo la  serikali la kupanda miti  milioni 1.5 ambayo itakuwa ni mkombozi mkubwa katika kurudisha hali nzuri ya uoto wa hasiri.

Mmoja wa wawekezaji katika mnada huo wa Zinga kwa mtoro  Hassan  Kashingo  akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara wenzake ameahidi kushirikiana bega kw abegaa naa serikali ikiwa pamoja na kuitunza miti hiyo 500 ambayo imepandwa katika eneo hilo la mnada.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.