Bhudagala ni jina lililo maarufu katika zama za sasa ndani ya kabila la watu wa Sukuma, ukipata nafasi kuingia ndani ya wilaya na vijiji mbalimbali kanda ya ziwa utapata majibu ya hiki ninachokujuza hapa.
Nimewahi kuhudhuria sherehe mbalimbali za wadau kanda ya ziwa ikiwa ni pamoja na matamasha na kupata fursa ya kuzisikia na kushuhudia watu wakizicheza nyimbo za jamaa huyu tena zikiombwa na kurudiwa rudiwa.
Jamaa anajaza show zaidi ya vile unavyodhani tena bila ya promo ya redio wala mitandao.
KISA NA MKASA
Ujumbe unaowasilishwa unaigusa jamii ukielezea maisha halisi ya watu wa kijijini wa hali ya chini na changamoto zao umekuwa kichocheo cha yote hayo, na haiishii hapo lugha nayo imekuwa sababu ya kuusababisha muziki wa jamaa huyu kuvuma sana kwani wengi hasa vijiji vya ndani usukumani hawaijui vyema legha ya kiswahili hivyo kwa mwanamuziki huyu kuimba akitumia lugha mama ya kabila lake imekuwa kichocheo cha kukubalika.
Lakini kingine kikubwa ni uwezo pia katika kuimba na kucheza.
Polisi waendelea kuwabana wanavunja Sheria, Wananchi waomba operesheni 3D
iendele.
-
Na Abel Paul, Jeshi la Polisi-Arusha.
Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Kimeendelea na operesheni ya
kutoa elimu na kuwakamata wale wote wanaoe...
59 minutes ago