ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 9, 2018

JEH SOKO NA SHULE TUANZE NA KIPI? MKUU WA WILAYA YA SENGEREMA UZINDUZI WA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WILAYANI SENGEREMA LEO


MKUU WA WILAYA SENGEREMA MH;EMMANUEL KIPOLE LEO SAA MBILI ASUBUHI,  AMEZINDUA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WILAYANI HUMO KATIKA KATA YA IBISABAGENI ZOEZI LILILOUZULIWA NA BAADHI YA VIONGOZI NA WANANCHI KATIKA KATA HIYO AMBAPO ZAIDI YA MITI 132 

JEH SOKO NA SHULE TUANZE NA KIPI? bila shaka utakuwa unajiuliza shwali hili linaingiaje? Basi fuatilia kile kinachosimuliwa kwenye video.

Akizungumza na wananchi wa kata hiyo mh EMMANUEL  KIPOLE  Amewataka  kuendelea na utuzaji wa mazingira na kuahidi kutatua changamoto ya ujenzi wa soko iliyodumu zaidi ya miaka 32 sanjali na hayo ametoa  lai kwa wananchi kushirika katika shughuli za maendeleo yakiwemo madawati.

Kwaupande  wake mwenyekiti wa mtaa wa IBISABAGENI amesema kuwa miti hiyo imenunuliwa kwa michango ya wananchi waliojitolea kwa hiyali bila kulazimishwa ikiwa na garama ya shilingi 40,000/=

Wakitoa maonyao baadhi ya wananchi walioshiriki katika zoezi hilo wao wamesema kuwa miti hiyo itawasaidia kuboresha mazingira na kuahidi kuitunza na kuilinda kwakuwa ni kwa faida yao wenyewe

MKUU WA GEREZA LA UKONGA ASTAAFU UTUMISHI WA JESHI AKIHIMIZA KUENDELEZWA VIWANDA VYA MAGEREZA


Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kushoto), akikwagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake wakati wa hafla ya kumuaga akistaafu utumishi wa jeshi hilo, Hafla hiyo imefanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila , akipunga mkono wa kwaheri  wakati wa hafla ya kumuaga akistaafu utumishi wa jeshi hilo. Hafla hiyo imefanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Gwaride la heshima likipita mbele ya Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila, wakati wa hafla ya kumuaga kamishna msaidizi huyo iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kulia),akipongezwa na maafisa wa jeshi hilo baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo katika hafla iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila, akipongezwa na mkewe Yunisi Mwaisabila (kulia), baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo Cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kushoto) akipongezwa na mjukuu wake baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo Cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI- WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

BULYANHULU YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI MILIONI 75,649,524 KWA HALMASHAURI YA NYANG’HWALE

Meneja Mkuu wa Migodi wa  Bulyanhulu Benedict Busunzu akikabidhi hundi ya milioni 75,649,524  kwa Mkuu wa wilaya ya   Nyangh’hwale  Hamim Gweyama  kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya wilaya ya hiyo katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2017.

Meneja Mkuu wa Migodi  wa Bulyanhulu Benedict Busunzu akizungumza na madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale  ambapo alisema Acacia itaendelea kushirikiana na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi .

Meneja Mkuu wa Migodi wa Bulyanhulu Benedict Busunzu akifurahia pamoja na wafanyakazi wa Bulyanhulu baada ya kukabidhi hundi kwa halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale.


Na,Joel Maduka ,Nyang'hwale

Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu Acacia kupitia mgodi  wake  wa Bulyanhulu imekabidhi hundi ya shilingi milioni  75,649,524 kwa halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha Mwezi Julai hadi Disemba mwaka 2017.

Akikabidhi mfano wa hundi hiyo  mbele ya madiwani wa halmashauri hiyo Meneja  wa  Mgodi  huo,  Benedict  Busunzu,  alisema  kawaida  mgodi  huo hutoa  ushuru  kwa  Wilaya  mbili  ya   Msalala  na  Nyangh’hwale  kwa  ajili  ya  miradi  ya  maendeleo.

Aidha  alitaja  moja  ya miradi  mingine  ambayo  mgodi  huo  umesaidia  Wilayani  humo  ni  pamoja  na  mradi  wa  mkubwa  wa  kusambaza   maji kwa  wakazi  150,000 wilayani  humo,   wenye  gharama  ya  Shilingi  Bilioni 4.5  ambao  unatarajiwa  kukamilika  mwishoni  mwa  mwaka  huu.

Aidha kwa upande wake Katibu tawala wa Mkoa wa Geita, Celestine Gesimba amewataka madiwani    na watendaji  wa  halmashauri ya hiyo    kuepuka   kutumia  fedha  zinazotolewa  na wadau  mbali mbali    kwa ajili  ya  miradi ya maendeleo  kwa  kulipana  posho  za  vikao,   badala  yake  zote  zitumike  katika miradi  kwa  manufaa  ya  ustawi  wa wakazi  wa Wilaya  hiyo.

“Ninapenda  kuwaonya  viongozi  na watendaji    ambao mpo hapa Nyangh’wale  kuwa  tusitumie hizi  fedha  kwa  ajili  ya kulipana  posho  za  vikao  badala  yake  zote  zietumike  katika  miradi  ya  maendeleo  kwa  jinsi  mtakavyoainisha,”alisema Gesimba.

  Aidha Mkurugenzi  wa  Wilaya  ya  hiyo,  Carlos  Gwamagobe,  pamoja na kushukuru mgodi  mgodi  huo  kwa kuwapatia  fedha  hizo alisema ushuru wa huduma ambayo walikuwa wakipata hapo awali  umeshuka kwani kwa  kiasi kikubwa kwani walikuwa wakipokea milioni mia nne kwa miezi sita .

“Tuna  imani  kuwa  mgodi  huu ukianza  shughuli  zake  kama  ilivyokuwa  awali   hata  ushuru  wa  huduma  utaongezeka  kwani awali  tulikuwa  tukipatiwa  kiasi  cha  Shilingi  Milioni  225   lakini  tangu  kuibuka  kwa  sakata  la  Makinikia,  ushuru  nao  umepungua  mara  mbili  ya  zile  za  awali,”alisema Gwamagobe.

SIDO YATANGAZA VITA NA WADAIWA WAKE SUGU

Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akitoa uamuzi wa wao kuwaweka kampuni ya udalali ya Yono Auction kwa ajili ya kwenda kukamata wadaiwa sugu wote.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela akitoa tamko la siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni.
Meneja wa SIDO mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akiongoza wafanyakazi na viongozi wa Yono kupita mlango kwa mlango wakati wakizundua kampeni ya kudai madeni "LIPA DENI LAKO SIDO, KUWA MZALENDO'.
 Wakiingia katika moja ya ofisi za mdaiwa wa SIDO.
Nae Mwenyekiti wa Kuatamia mawazo ya wabunifu, Joseph Mlay ameiunga mkono SIDO kwa hatua waliyochukua ya kuingia mlango kwa mlango katika kudai madeni yao. 

 Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam imetangaza vita kwa wale wadaiwa sugu kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada. 

 Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga wakati akizindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wateja wao. 

 "Leo tunazindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wadaiwa sugu wote wa SIDO hatutakuwa na huruma juu ya hili maana hawa ndiyo wanarudisha maendeleo ya shirika nyuma, kuna waliokopa, walipanga kama haujalipa deni lako ujue tunakupa siku 14 tu baada ya hapo sheria itachukua mkondo wake," amesema Mkurugenzi Maganga. 

 Meneja Macdonald Maganga amesema wadaiwa ni wale waliopewa maeneo maalumu ya viwanda kwa ajili ya kufanyia kazi zao na waliopatiwa huduma ya fedha kwa mkopo na kushindwa kurejesha kwa wakati. “Kuna ambao wamekaa miaka mingi au miezi mingi bila kurejesha fedha kwetu kama shirika inatuathiri kwa sababu hatuwezi kuwahudumia wengine,” amesema Maganga. 

 Maganga amesema wanadai jumla ya sh. milioni 350 kutoka kwa wadaiwa zaidi ya 77. Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela amewashukuru SIDO kwa kuweza kuwapa kazi hiyo ya kuwakusanyia madeni na kuongeza kuwa hawata muonea huruma mdaiwa yeyote. 

 "Yono Auction Mart tunatoa siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni,". amesema Mama Kevela.

 “Kwa wadaiwa wote wa SIDO, wanaoishi kwenye viwanda na nyumba za SIDO bila kulipa pango, waliochukua mikopo na hawataki kurejesha kwa sababu wanazozijua wao, mkono wa Yono uko kazini ni vyema wakachukua hatua wakalipa ili kuondosha usumbufu,” amesema Kevela.

Mdaiwa Masoud amedai hawafanyi makusudi kutolipa madeni ni kutokana na kodi kupanda kila mwaka huku hali ya biashara ikiwa mbaya. “Ukizingitia soko la ushidani na hali ya bidhaa unashindwa kuuza kwa wakati kwa hiyo tunalipa lakini hatulipi kwa wakati,” amesema.

Amedai wamepangishwa kwa zaidi ya miaka 40 wakifanya shughuli zao na kama wangekuwa hawalipi kwa kipindi chote wangefukuzwa hivyo ameiomba serikali kutodhani kuwa wanapuuza kulipa madeni.

VIDEO:- VIPUTE NCHINI HISPANIA.



Real Madrid vs Real Sociedad 3-1 All Goals & Highlights 2018 (Last Match) HD

Valencia vs Barcelona 0-2 - All Goals & Extended Highlights - CDR 08/02/2018 HD

AU YAKANUSHA MADAI KUWA CHINA INAFANYA UJASUSI DHIDI YA AFRIKA.

AU yakanusha madai kuwa China inafanya ujasusi dhidi ya Afrika
Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika amesema kuwa madai kwamba China inafanya ujasusi katika makao makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa ni uongo mtupu unaotolewa kwa shabaha ya kuvuruga ushirikiano wa pande hizo mbili.


Moussa Faki Mahamat ambaye yuko safarini nchini China amesema kuwa, ripoti iliyotolewa na magazeti ya Ufaransa kuhusu madai ya kile kilichoitwa 'ujasusi wa China' katika makao makuu ya Umoja wa Afrika, ni uongo mtupu.
Moussa Faki amesema hajui vipi ujenzi uliofanywa na China wa kituo cha mikutano cha makao makuu ya Umoja wa Afrika na kutolewa kwake zawadi kwa umoja huo kunavyoweza kuinufaisha China kijasusi. 
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi amesema katika mazungumzo yake na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwamba, kituo cha mikutano cha umoja huo mjini Addis Ababa ni nembo ya urafiki wa Beijing na Afrika na kwamba, ripoti ya magazeti ya Ufaransa ni njama za kutaka kuvuruga uhusiano huo mzuri.



Moussa Faki na Yi, Beijing

Hivi karibuni gazeti la Le Monde la Ufaransa liliaandika kuwa, wakati wa ujenzi wa makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa mwaka 2012, China iliweka vyombo vya ujasusi katika jengo hilo na kwamba, wataalamu wamegundua ujasusi huo hivi karibuni. 
CHANZO: PARSTODAY SWAHILI

RC MNYETI AAGIZA VIGOGO 5 UCHIMBAJI MADINI KUKAMATWA.


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ameagiza vigogo watano wachimbaji na wanunuzi wa madini ya Tanzanite katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro na jijini Arusha, kukamatwa na  polisi wakidaiwa kufadhili uchimbaji haramu wa madini hayo.

Leo Februari 8, 2018 kamanda wa polisi Mkoa wa Manyara, Augostino Senga amesema vigogo hao wamekamatwa jana jioni na kulazwa Kituo cha Polisi Mirerani.

Amesema wanawashikilia baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kupata taarifa kuwa, vigogo hao wanashiriki kuwadhamini vijana wanaoingia kwa wizi kwenye migodi ya kampuni ya TanzaniteOne yenye ubia wa asilimia 50 kwa 50 na Shirika la Madini la Taifa (Stamico).

Amesema wanachunguza suala hilo na iwapo vigogo hao ambao majina yao tunayo utakamilika, watafikishwa mahakamani.

AIRTEL YAWAZAWADIA WASHINDI WA SHINDA NA SMATIKA INTANETI - DROO 1

 Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiongea na mmoja kati ya washidi  wakati Airtel Ilipochezesha droo ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti ambapo washindi 2000 kila mmoja alijishindia 1GB. Kushoto ni ni Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Abdallah Hemedy na Afisa Masoko Airtel Nassoro Abubakar
Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando akionyesha moja namba ya washindi wakati wakuchezesha droo ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti ambapo washindi 2000 kila mmoja alijishindia 1GB za SMATIKA Yatosha Intaneti. Kushoto ni ni Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Abdallah Hemedy na Afisa Masoko Airtel Nassoro Abubakar

Airtel yawazawadia washindi 2,000 wa promosheni ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti
Kampuni ya simu za mkokoni Airtel Tanzania leo imewazadia washindi 2,000 wa kwanza wa promosheni yaSHINDA NA SMATIKA Intaneti kwenye droo ambayo imechezesha jijini Dar es Salaam.

Promosheni ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti ilizunduliwa mapema wiki hii ambapo kuna washindi 1,000 wakila siku ambao wanajishindia bando ya 1GB pamoja na zawadi nyingine zikiwepo wakishinda simu za kisasa za smatiphone na moden.

Akiongea baada ya droo hiyo, Meneja Uhusiani Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema wateja wa Airtel 2000 wameweza kujishindia bando ya 1GB.

Kama mnvyoona hapa leo droo ya promosheni yetu ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti inafanyika kwa uwazi kabisa na washindi. Ni ya promosheni hii ni kutoa shukrani kwa wateja wa Airtel kwa kuonyesha uaminifu wao kwa kuendelea kutumia mtandao bora kabisa hapa nchini, alisema Mmbando.

Ni muhimu kufahamu kuwa mteja haitaji kujisajili kwa ajili ya promosheni ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti. Kile anachotakiwa kufanya ni kupiga *149*99# halafu changua namba 5 Yatosha SMATIKA Intaneti, hapo atanunua bando aidha ya siku, wiki au mwezi na kuwa mmoja wa washindi wa zawadi zetu kambambe, alisema  Mmbando.

Mmbando aliongeza kuwa promosheni ya Shinda na Yatosha SMATIKA intaneti ilizinduliwa mwanzo mwa wiki na itakuwa ni ya siku 30 huku kukiwa na droo 3 kila wiki – Jumatatu, Jumatano na Ijumaa. Kwa droo za kila siku, wateja 1000 watajishindia bando ya intaneti yenye 1GB kila mmoja wakati kwenye droo kubwa kutakuwa na washindi 10 huku watano wakishinda simu za smatiphone na  5 wakijishindia moden.

HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA YABOMOA NYUMBA YA SERIKALI

Muonekano wa Nyumba  yenye namba 1103/5 ambayo ipo katika eneo la Mafiat Jijini Mbeya , ilifunguliwa kesi namba 63 ya mwaka 2007 katika mahakama ya Wilaya Mbeya.

Na EmanuelMadafa,Mbeya 
HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya, imetoa siku saba kwa mkandarasi anayejenga nyumba ya serikali iliyoamuliwa na mahakama kuu kujengwa, kuibomoa baada ya kubainika kujengwa chini ya kiwango.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake , Afisa habari wa halmashauri hiyo, John Kilua, amesema ofisi kupitia idara ya majengo ilitembelea eneo la nyumba hiyo inayojengwa kwa amri ya mahakama kuu na kubaini changamoto mbalimbali za ujenzi.

Amesema, kutokana na changamoto hizo wahusika wanaojenga nyumba hiyo wametakiwa kuibomoa na kuanza upya kwa kufuata kanuni za ujenzi na kwamba zoezi la kubomolewa kwa jengo hilo la nyumb linatakiwa kufanyika ndani ya siku saba.


Nyumba hiyo yenye namba 1103/5 ambayo ipo katika eneo la Mafiat Jijini hapa, ilifunguliwa kesi namba 63 ya mwaka 2007 katika mahakama ya Wilaya ambayo pia ilivunja ndoa ya Mhandisi Simbonea Kileo na mkewe Gladness Kimaro na kuamuru mali za ndoa hiyo zigawanywe.

Amesema katika uamuzi huo,kileo alipeleka ombi mahakamani na kuomba nyumba hiyo isiingie kwenye mgawanyo kwa sababu aliuziwa kwa makataba maaalumu na Serikali na kwamba katika kipindi cha miaka 25 hatakiwi kuifanyia matengenezo yoyote yale ikiwamo kuiuza.

Hata hivyo aliyekuwa mke wa Kileo, mtalaka Gladness Kimaro alikata rufaa mahakama kuu kupinga ombi la mumewe ,kwa madai hakupeleka vielelezo kutoka kwa wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) kuonyesha kuwa nyumba hiyo ina mkataba maalumu na haitakiwi kuendelezwa kwa miaka 25.

Baada ya Jaji Samweli Kalua kupitia rufaa hiyo mwaka 2013, alitoa uamuzi kuwa kesi hiyo irejeshwe kwenye mahakama ya wilaya na isikilizwe na hakimu mwingine na jambo lolote lisifanyike katika nyumba hiyo.

Inadaiwa kuwa wakati Kileo akisubiri kuitwa na mahakama ya wilaya kutokana na maamuzi ya mahakama kuu, ghafla  mwaka 2015 aliondolewa kwa nguvu kwenye nyumba na mtalaka wake lakini alikata rufaa.


Februari 8, 2017 Jaji Atuganile Ngwala aliagiza kesi hiyo irejeshwe mahakama ya wilaya na ipangiwe hakimu mwingine na kwamba kabla ya kesi ya msingi kusikilizwa walalamikiwa akiwemo mfanyabiashara ambaye pia ni Mbunge S.H Amoni na mtalaka wa  mhandisi kileo, Gladness na madalali wawili wa mahakama kuirejesha na kuijenga upya nyumba hiyo.

Mwisho

Wednesday, February 7, 2018

KATIBU WA UWT JUDITH LAIZER KUTATUA TATIZO LA VYOO KATIKA SHULE YA YA MSINGI ILULA NA ISOLIWAYA ZILIZOPO KILOLO

Katibu wa umoja wa wanawake wa Ccm (UWT) wilaya ya Kilolo Judith Laizer akiongea na baadhi ya viongozi ,walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Isoliwaya wakatika wa kukabidhi msaada huo kwa ajili ya kujengea vyoo ya walimu wa shule hiyo
 Katibu wa umoja wa wanawake wa Ccm (UWT) wilaya ya Kilolo Judith Laizer akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa chama hicho Leah Moto na Nancy Nyalusi walikuwa kwenye ziara ya kusherekea miaka 41 ya chama cha mapinduzi 
 Hili ni moja ya jengo lashule ya msingi Ilula iliyopo katika tarafa ya mazombe wilayani kilolo mkoani Iringa 
 Baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi wilaya ya kilolo wakiwa katika kusherekea miaka 41 ya kuzaliwa chama chao kwa kufanya shughuli za kijamiii


Na Fredy Mgunda,Iringa. 

WALIMU wa shule ya msingi Ilula na Isoliwaya zilizoko katika kata ya Ilula Wilaya ya Kilolo wanakabiriwa na magonjwa ya Mlipuko kwa kukabiliwa na changomoto ya choo.
 
Shule hizo zilizotenganishwa baada idadi kubwa ya wanafunzi, walimu 49 wanalazimika kutumia choo Chenye matundu mawili hali inayohatarisha usalama wa afya zao.

Akizungumza mbele ya Katibu wa umoja wa wanawake wa Ccm (UWT) wilaya ya Kilolo Judith Laizer, mwalimu Msaidizi wa shule ya Msingi Isoliwaya, Huruma Mbena alisema hali hiyo inahatarisha afya za walimu kutokana na changamoto hiyo.

Mbena alisema kuwa baada ya shule hizo kutenganishwa vyoo vya walimu vilibaki kwa shule ya Ilula hivyo kutokana na idadi kubwa ya walimu wanalazimika kutumia vyoo hivyo licha ya kutotosheleza kutokana na idadi kubwa ya walimu.

Aidha alisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya nyumba za walimu ambao hadi sasa walimu 21 wanaishi katika nyumba za kupanga hali inayowaletea ugumu wa maisha zaidi.

Alisema kuwa changamoto nyingine wanayokabiliana nayo ni ukosefu wa ofisi za walimu na ofisi ya mwalimu mkuu na kulazimika kutumia moja ya darasa kama ofisi na kupunguza idadi ya madarasa.

Akijibia hoja zilizopo kwenye risala Katibu wa umoja wa wanawake wa Ccm (UWT) wilaya ya Kilolo Judith Laizer alisema kuwa umoja huo umewaleta mifuko ya saruji kumi na tano (15) na bati saba kwa ajili ya kusaidia kujenga vyoo vya walimu ili kupunguza adhabu wanayoipata.

“Kweli ukikosa huduma ya choo bora walimu hawezi kuwa huru kufundisha wanafunzi maana anaenda chooni huku akijua kuwa wanafunzi wake wanamtazama kwa mtazamo tofauti na ukizingatia maisha ambayo wanaishi majumbani kwao” alisema Laizer

Laizer alisema kuwa changamoto nyingine kama ukosefu wa nyumba za walimu,upungufu wa vyumba nane vya madarasa na ukosefu wa ofisi ya walimu atazifikisha kwa viongozi wa wilaya na kwa mbunge wa jimbo hilo Vennace Mwamoto.

“Hizi changamoto zenu zinatatulika kwa kuzingatia kuwa vingozi wa wilaya hii ni wachapakazi na waadilifu kuwatumikia wananchi nauhakika kuwa watakuja hapa na kuzitafutia ufumbuzi hizi changamoto kwa kuwa nitazifikisha kama nilivyozichukua hapa” akisema Laizer

Lakini Laizer aliwataka viongozi wa bodi ya shule hilyo kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa ukaribu na wazazi wa shule hiyo kwa kuhakikisha wanaanza ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na kujenga vyumba vya madarasa na mwishoni mbunge na halmshauri watamalizia sehemu iliyobaki.

“Naombeni nyie viongozi kufanya kazi kwa ukaribu na viongozi hao bila kuwashirikisha walimu kwa kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kama alivyoagiza kuwa elimu bure bila malipo” alisema Laizer

Laizer aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa kufanya kazi kubwa ya kufaulisha kwa wastani unaolidhisha na kuwaomba kuongeza bidii kufundisha huku wakibuni mbinu mpya za ufundishaji.

MAMA MITINDO AELEZA UKWELI KUHUSU KUSTAAFU KUANDAA LADY IN RED!


Baada ya tetesi kuvuma zilizo jaa ukweli kuhusiana na Mama wanamitindo maarufu hapa Tanzania, Asya Idarous Khamsin kustaafu kuandaa jukwaa la ‘Lady In Red, sasa leo  6/Feb/2018 Asya amedhibitisha  tetesi hizo kama ifuatavyo.

 Akizungumza na wandishi wa habari katika ukumbi wa King Solomon Asya amesema kuwa Jukwaa la Lady in Red mpaka sasa limedumu kwa muda wa miaka 15 likiwa chini yake.  Pia alifafanua  dhamira ya jukwaa la Lady in Red ambapo alisema jukwaa hilo lilianzishwa kwa lengo la kukuza vipaji vipya kwenye Tasnia ya Mitindo hapa Tanzania, ndio maana jukwaa asilimia kubwa huwa linapandisha upcoming Designers maana ndio jukwaa lao la kujidaia.

Aidha aliongeza kuwa kustaafu kuandaa jukwaa la Lady in Red haimaanishi kwamba ataachana na mambo ya ubunifu, “siwezi kuacha maana ndio kazi inayo niweka mjini” alisisitiza Asya.  “Kilicho kikubwa nimeamua kutoa fursa kwa wanamitindo ambao wamekulia kwenye jukwaa hilo”.

Kumbuka Lady in Red 2018 itafanyika 9/Feb/2018 katika ukumbi wa King Solomon uliopo Dar es salaam- Namanga. Siku hiyo ndipo Asya atakapo jivua kuandaa na kukabidhi Designers wengine jukwaa hilo usikose. Kwako mdau wa mitindo endelea kuisambaza kwa walimwengu wote asante.


UCHAGUZI KINONDONI FEB 06, 2018: MZOZO, POLISI NA WAFUASI WA CHADEMA BAADA YA KAMPENI


Wanachama wa Chama cha demokrasia na Maendeloa CHADEMA, wamezuiwa kwa dakika kadhaa na polisi waliokuwa wakisimamia amani katika kampeni za uchaguzi, Kinondoni.

RAIS MAGUFULI AZINDUA KITUO CHA MAFUNZO MAALUM YA KIJESHI BAGAMOYO-PWANI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 06 Februari, 2018 amezindua Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi (Comprehensive Training Center – CTC) kilichopo Mapinga katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.
Kituo hicho kimejengwa kwa msaada kutoka Jeshi la Ukombozi la Watu wa China kwa gharama ya Shilingi Bilioni 67.87 na kitatumika kutoa mafunzo ya kijeshi ya kisasa yatakayowawezesha askari kukabiliana na vitisho vya kisasa vya kiusalama.Mhe. Rais Magufuli amelishukuru Jeshi la Ukombozi la Watu wa China na Serikali ya China kwa kutoa msaada wa kujengwa kwa kituo hicho na amesema Serikali ya Awamu ya Tano inathamini na kutambua mchango wa China katika Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania.
Mhe. Rais Magufuli amesema China imeendelea kudhihirisha urafiki na udugu wake na Tanzania kwani licha ya kujenga kituo hicho pia imetoa msaada wa kujenga kituo cha mafunzo ya kijeshi ya anga cha Ngerengere Mkoani Morogoro na miradi mingine ya maendeleo ya jamii na hivyo amemuomba Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke kufikisha shukrani zake kwa Rais wa China Mhe. Xi Jinping.

Tuesday, February 6, 2018

YANGA 4-0 NJOMBE MJI (MAGOLI YOTE, CHIRWA AKIPIGA HAT-TRICK) - VPL 06/02/2018


Ni mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara (VPL) uliopigwa katika dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam ambapo Obrey Chirwa ameandika Hat-trick yake ya pili.

YANGA SC imerudi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Njombe Mji FC jioni ya leo Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam.

Pongezi ziende kwa mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa aliyefunga mabao matatu peke yake, huku bao lingine likifungwa na mzawa, winga Emmanuel Martin.


Kwa ushindi huo, timu ya kocha Mzambia, George Lwandamina inafikisha pointi 34 baada ya kucheza mechi 17 sasa ikizidiwa pointi nne tu na vinara Simba SC, ambao kesho watacheza mechi yao ya 17 dhidi ya Azam FC, iliyo nafasi ya tatu kwa pointi zake 33.

HILI HAPA SONGI JIPYA LA HIP HOP:- Dj Hiplus - Jisaidie Mwenyewe.



Wimbo mpya toka kwa Dj Hiplus ft selementaly,Mtafya,Miss Geezy & Zill Vega - Jisaidie Mwenyewe (Prod by Gachi) beat chorus habari za wakati huu leo ikiwa ni siku yangu yakuzaliwa napenda kuleta mbele yako project yangu yakwanza inayokwenda kwa jina la jisaidie mwenyewe Dj Hiplus ft Selementaly, Mtafya, Miss Geezy & Zill Vega - Jisaidie Mwenyewe (Prod by Gachi) beat chorus

KATIBU WA CCM ELIREHEMA NASSAR NITAWASHUGHULIKIA WATENDAJI WA SERIKALI WANAKWAMISHA JUHUDI ZA RAIS

Katibu wa wilaya wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Elirehema Nassar akiwa kwenye ziara ya kusherekea miaka 41 ya chama hicho kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii

Na Fredy Mgunda,Mufindi.

CHAMA cha mapinduzi wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kimewataka viongozi wa halmashauri ya mji wa mafinga kufanyakazi kwa weledi unaotakiwa kuwatumikia wananchi katika kutatua changamoto zinazozuia kuleta maendeleo.

Hayo yamesemwa na katibu wa wilaya wa chama hicho Elirehema Nassar wakati wa kusikiliza kero za wananchi walipokuwa wanasherekea miaka 41 ya chama cha mapinduzi katika wilaya hiyo.

Nassar alisema kuwa mmezisikia kero za wananchi lakini hapa mnajibu kisiasa na sio kitaalamu,sasa naomba nipatiwe majibu ya kutosha na yenye ukweli na sio uongo mnaotudanya hapa.

“Hapa mnaleta siasa kwenye kero za wananchi sitaki kusikia siasa kwenu watendaji mnaulizwa maswali ya msingi ambayo ni kero za wananchi harafu mnajibu majibu mepesi hivyo haiwezekani” alisema Nassar

Nassar aliwataka viongozi wa serikali ya halmashauri ya mji wa Mafinga kuacha kukaa maofisini na badala yake wanatakiwa kwenda kutatua kero za wananchi waliokiweka madarakani chama cha mapinduzi hivyo achene kufanya kazi kimazoea

“Wiki nzima unamkuta mfanyakazi wa serikali yeye ni kupiga soga tu ofisi huku wananchi wanateseka na kero mbalimbali ambazo muda mwingine hazina tija hivyo nikibaini hili nitalala mbele na huyo mtumishi” alisema Nassar

Aidha Nassar amewataka wafanyakazi kubuni viradi iliyofanyiwa utafiti na iwe inatija kwa wananchi kwa ajili ya kuleta maendeleo ambayo yatadumu kwa miaka mingi.

“Mnaanzisha miradi ambayo haina tija mfano hapa mmeanzia mradi wa soko la kuchoma nyama lakini hakuna mwananchi au mfanyabiashara anajua jinsi gani ya kufanya biashara hiyo hivyo ni marufuku kufanya miradi ambayo sio shirikishi kwa wananchi” alisema Nassar.

Pia Katibu huyo aliwataka watumishi hao wa serikali kuhakikisha wanaenda kuwaelimisha wananchi kuhusu kodi wanazozita zilipwe kuliko kumwambia mwananchi alipe kodi ambayo hajui inatokana na nini na kwa nini analipa,lakini kukuwa na elimu ya kutosha hakutakuwa na migongano.

Sambamba na kuwaasa watumishi wa serikali Katibu Nassar aliwaambia wananchi na mafinga na wanachama wa CCM wa Wilaya ya Mufindi kuacha kujenga nyumba bila ya vibali vya serikali na mwisho wa siku mwananchi anakuja kupata hasara pale anapoambia abomoe kwani ikon je ya mipango miji.

Nao wananchi na Wanaccm wa Wilaya walitoa kero zao mbalimbli kwa watendaji wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga,ambapo walizitaka kero hizo kama uchafu wa Mazingira kwa baadhi ya maeneo,huduma mbovu katika Hospitali ya Wilaya baadhi ya mitaa na kata moja kutokuwa na watendaji wa kabisa.

Nyingine ni baadhi ya shule za mshingi kukosa miundo mbinu kama matundu vyoo sanjali na upungufu wa vyumba vya madarasa, na tatizo la upatikanaji wa mbolea za kilimo sambamba na dawa ya kuulia wadudu waharibifu wanaokula mazao, na kuwataka  watendaji hao kushugulikia kero hizo haraka.