ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 7, 2012

RAMASTAR NDIYE MKALI SERENGETI FIESTA MC SHUJAA MWANZA

Pichani kulia ni mmoja wa waratibu wa tamasha la Serengeti Mc Shujaaa-Mwanza, Adam Mchomvu akimtangaza mshindi wa shindano la Serengeti Mc Shujaaa, aitwaye Ramastar pichani shoto ndani ya jijini la Mwanza.Shindano hilo limefanyika jioni ya leo kwenye kiota cha maraha cha Clup Lips, Isamilo jijini humo.
Katika mchakato wa shindano hilo kulikuwepo na msisimko mkubwa kwa vijana wengi kujitokeza na kushiriki kikamilifu na kuwa ushindani mkubwa,aidha walijitokeza vijana wapatao 56, kisha 15 na hatimaye kupatikana mshindi mmoja ambaye atakwenda Dar kushindana na wengine kutoka mikoa mbalimbali kwenye kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2012 lililopangwa kufanyika katika viwanja vya Lidaz Club, Kinondoni.
Nikuchanana tu kama sehemu ya misingi husika ya game ya Hip-hop ndani ya Lips Club.
Mashabiki na chata zao za wakali waliotamba katika hip-hop hawakukosekana ulingoni. 
Top four ikiwa na Clouds Crew. Baba Jonii (L) na Ncha kali (R)
Hakuna kinyang'anyiro kilichokuwa 'tite' kama hiki cha Ramstar anayemchana Pusha.
Mashabiki walijipanga... ile kisawasawa...
Ni Ramstar(L) na Ramside(R) katika fainali.
Pichani kulia ni mmoja wa majaji wa shindano la Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012,Prodyuza Duke akizungumza machache kabla ya shindano halijaanza,shoto kwake ni jaji mwingine na pia ni mmoja wa waratibu wa shindano hilo Reuben Ndege a.k.a Ncha Kali akisikiliza kwa makini.
Mc Baba Jonii akirusha shiringi kutafuata nani aanze katika fainali ya Mc Shujaa Mwanza kati ya Ramside kushoto na Ramstar aliyesimama kulia huku kamera ya Clouds Tv ikinasa kinacho endelea..

USIKU WA MTU MZIMA DAWA WAFANA NDANI YA VILLA

Mmoja wa wasanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akijiachia jukwaani na mmoja wa mashabiki waliyejitokeza kucheza  nae,kwenye shoo ya Usiku wa Mtu mzima Dawa uliofanyika kwenye kiota cha maraha cha Villa park usiku wa kuamkia leo,jijini Mwanza.Aidha katika makamuzi hayo washabiki wapenzi wa muziki wa kizazi kipya walijaa ile mbaya na palikuwa hapatoshi hata kidogo.
Wacheza shoo wa Ommy Dimpoz wakiwajibika jukwaani.
wasanii wa kundi la Wanaume TMK wakiongozwa na Chege na Temba wakilishambulia jukwaa vilivyo,ama kwa hakika ilikuwa ni shangwe tu kwenye makamuzi ya shoo ya Usiku wa Mtu mzima dawa.
Wasanii Chege na Ydash wote kutoka Wanaume TMK wakiwarusha wakazi wa Mwanza ni kibao chao cha Dar mpaka Moro.
Wanaumeeee...eeeeeh..! Wanauuumeeeee.....halafu mashabiki wanaitikia kwa nguvu kabisa eeeehhhh..!

"Sijui nimtawanyee.....aah huwezi wewe mtu mzima dawa."! Mh Temba akikamua vilivyo na Bibi Cheka jukwaai saafi kabisa huku shangwe zikiwa zinasikika kila kona,kwani Bibi Cheka alionesha uwezo wake mkubwa wa kukamua jukwaa,hata ile mitindo huru nini na niniii yuko swafi mbaya..aaah mbona palinoga Villa Park usiku wa kuamkia leo.
Ommy Dimpoz akikamu mbele ya umati mkubwa ndani ya kiota cha maraha cha Villa Park usiku wa kuamkia leo.
Watu kibao walifurika ndani ya ukumbi wa Villa Park kushuhudia Usiku wa mtu mzima dawa.

Pamoja na kupotea kiaina kwenye gemu ya muziki wa Bongofleva,Ferouz bado nyota yake inaonekana kuwa angavu,alifanya vyema ndani ya ukumbi wa Villa Park,kiasa kwamba shangwe kila wakati zilikuwa za kutosha.
Mkubwaa na wanaweee....na yeyeee yumooo.. ! Mkubwa Fella nae akitafuta kimwana wa kunogesha jukwaa safi kabisa.
Msanii mahiri wa hip hop hapa nchini,Mwana FA akikamua kitu cha laiti na shabiki wake jukwaani kama picha ionekavyo.
Mkali mwingine wa mitindo huru,Mwana FA a.k.a Binadamu akikamua vilivyo ndani ya ukumbi wa Villa Park usiku wa kuamkia leo,kwenye shoo ya usiku wa mkubwa dawa ambao ulifana kwa kiasi kikubwa. Picha zote na  Michuzijr.Blogspot.com

SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA KURINDIMA KESHO MWANZA

Gazeti la kila mwisho wa wiki (Mzawa) kutoka Mwanza limeandika kwenye kurasa zake za michezo.

MPANGO MZIMA NA MAMBO YA WEEKEND

Akaanga chips juu ya kichwa cha mtu ni kwenye tamasha la Coca cola viwanja vya CCM Kirumba.

Hapa afande hapa mie katika usiku wa Safari Lager Shooters Pub Mwanza...

Kushoto ni Jitah Man, Afande Sele na mwana kutoka Watu Pori.

Ni mwendo kushow love Mr. Rock Marrow wa TBL Mwanza (kushoto) akiwa na mdau wa Safari Lager .

Share the fun tuiwa na mzee mzima John Tegete (pale kati).
Meza ya wadau wa Watu Pori.

Friday, July 6, 2012

KIMENUKA CCM WILAYA YA MISUNGWI: NI JUU YA WIZI WA ZAIDI YA SH. BILIONI 4 ZA RIPOTI YA CAG

KAMATI ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza iliyoketi leo imetoa tamko lake juu ya viongozi wa chama hicho Wilayani Misungwi kubainika kuhusika katika sakata la ubadhilifu wa fedha za Umma zilioripotiwa kupote katika Halmashauri ya Wilaya hiyo.
Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa huo Saimon Mangelepaa


Akiamplyfy Exclusive jioni ya leo kwenye majira ya saa 12 hivi.. Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa huo Saimon Mangelepaa amesema kuwa kufatia ripoti ya Mkaguzi Mkuu na Mudhibiti wa Hesabu za serikali nchini CAG iliyotolewa Bungeni ya mwaka 2009/2012 ambapo baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo walituhumiwa kuhusika na wizi wa zaidi ya shilingi bilioni 4.

bofya hapa kumsikiliza

Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza kimekaa na kufatilia kwa umakini na kubaini baadhi ya viongozi wake kuhusika kwa ukaribu katika ubadhilifu huo akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Benard Polykap ambaye naye anatuhumiwa kuhusika katika Wizi wa fedha za umma zilizotolewa na serikali kuu kwa ajili ya maendeleo katika wilaya hiyo
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Clement Mabina (kushoto) akiwa na Katibu wa CCM mkoa Bi. Joyce Masunga wakati wa kikao cha kamati ya siasa kilichotoa tamko juu ya baadhi ya viongozi wake wilaya ya Misungwi wanao husika kwenye sakata la Ubadhilifu wa fedha uliolipotiwa na CAG.
Halmashauri ya Misungwi ni moja ya Halmashauri ambazo zimetajwa katika taarifa ya CAG kuhusika na upotevu wa fedha za Umma zaidi ya bilioni 4 ambapo pia mkurugenzi wake na baadhi ya watumishi wa Idara wamesimamishwa na uchunguzi ungali ukiendelea kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.
Wajumbe Kikaoni ndani ukumbi wa CCM mkoa wa Mwanza
Hivi karibuni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Ludovick Utouh aliwaonya mawaziri wapya na watendaji serikalini kwamba ripoti zake hivi sasa zina nguvu za kusimamia uwajibikaji hivyo, wanapaswa kusimamia vyema wizara zao kuzuia ubadhirifu wa fedha za umma.

KONGAMANO LA KUWEZESHANA NA KUONGEZA UELEWA JUU YA MCHAKATO WA MASUALA YA KATIBA KWA WATU WENYE ULEMAVU ULIOANDALIWA NA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

 Bwana Gideon Mandesi kutoka taasisi ya Dolasedi akiongea na waandishi wa habari juu ya mpango wa kuwakilisha mapendekezo ya pamoja ya watu wenye ulemavu kwa kamati ya kukusanya maoni ya katiba.
 Makalimani akiwaelezea washiriki wenye ulemavu wa kusikia majadiliano yalikuwa yanaendelea kwenye kongamano hilo.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba nchini, Bwana Deus Kibamba akiwajengea uwezo jamii ya wenye ulemavu nchini namna watakavyoshiriki kikamilifu katika mchakato wa katiba unaoendelea nchini.
Watu wenye ulemavu wakiwa katika kongamano la kuwajengea uwezo namna watakavyoshiriki katika mchakato wa kukusanya maoni ya katiba.

Airtel yakabidhi zawadi kwa washindi wa droo ya kila siku wa Airtel Money Sabasaba

 Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde (kushoto) akimkabithi bwn Bernard Chezue modem baada ya kuibuka kuwa mshindi wa droo ya kila siku inayowawezesha wateja wa Airtel waliofanya malipo ya bidhaa katika viwanja vya sabasaba kuweza kujishindia zawadi mbalimbali kila siku. Akishuhudia ni mfanyakazi wa huduma kwa wateja wa Airtel bi Monica Mgalwa

 Mshindi wa droo ya kila siku ya Airtel money bwana Frank Joakim Mgumba akijaribu kutumia simu yake mara baada ya kuibuka kuwa mshindi katika droo inayohusisha wateja wa Airtel walionunua bidhaa kwa kupitia Airtel money katika maonyesho ya Sabasaba. Pichani Katikati ni Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde pamoja na wafanyakazi wa Airtel huduma kwa wateja wa viwanja vya sabasaba.

 Mfanyakazi wa huduma kwa wateja wa Airtel bi Monica Mgalwa akichezesha droo ya kuchagua mshindi wakati wa kuchezesha droo ya kila siku iliyofanyika jana katika viwanja vya sabasaba ambapo wateja watano walionunua bidhaa kwa kupitia huduma ya Airtel money walijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo simu, modem na muda wa maongezi. Wakishuhudia pichani ni wafanyakazi wa Airtel

 Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde (kushoto) akimkabithi mshindi wa droo ya kila siku Bw Rucha Selemani modem baada ya kuibuka kuwa moja kati ya washindi wa siku , droo hiyo inahusisha wateja waliofanya malipo ya bidhaa kupitia Airtel money katika viwanja vya Sabasaba kuweza kujishindia zawadi mbalimbali kila siku. Akishuhudia ni mfanyakazi wa huduma kwa wateja wa Airtel bi Heleni Kimati

 Wanafunzi wa shule ya msingi ya Neema Academy iliyoko jijini Dar es salaam wakipata maelekezo kuhusu huduma na bidhaa mbalimbali kutoka kwa watoa huduma wa Airtel mara baada ya kutembelea banda la Airtel lililopo katika viwanja vya maonyesho ya Sabasaba

 Wanafunzi wa shule ya msingi ya Neema Academy iliko jiji Dar es salaam wakipata maelekezo kuhusu huduma ya internet ya 3.75G kutoka kwa mfanyakazi wa kitengo cha huduma kwa wateja baada ya kutembelea banda la Airtel lililopo katika viwanja vya maonyesho ya Sabasaba

Wanafunzi wa shule ya msingi ya Neema Academy iliko jiji Dar es salaam wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutembelea banda la Airtel lililoko katika maonyesho ya Sabasaba kilwa Road Dar es Saalam.

OMMY DIMPOZ NA DJ ALLY WASHIRIKI PARTY YA KUZINDUA STONE CLUB MPYaaaaaaaa.......!!!!!

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Ommy Dimpoz usiku wa kuamkia leo (nikimaanisha jana alhamisi) ameshiriki vyema kwenye party ya kuzindua Stone Club ambayo imekuja kivingine, na sevis mpya na wahudumu wapya  mara baada ya ukarabati wa muda mrefu. 
Party hiyo iliyokuwa ya kimya kimya ilinogeshwa na dance la nguvu lililomwagwa na Ommy Dimpoz akishirikiana na densaz wake mahiri.
Dance likiendelea katika stage ndani ya party hilo ambapo usiku huo pia ulitumika kama usiku wa kwanza mara baada ya wanavyuo kumaliza pepa.
On the one and Two alisimama Dj Ally ' mzee wa kitu juu ya kitu' toka A- town ambaye alifanya makamuzi ya hatari uspime ndani ya Stone Club Mpyaaa iliyofungwa sound full kiwango ..... Dj Ally amesaini 'kontrakti'  ya muda wa kutosha hivyo ataendelea kukisanukisha hapa.
Ommy Dimpoz kwa poz akicheza na shabiki wake mara baada ya mzuka kumpanda...