ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 27, 2024

RAIS SAMIA KUTUA MWANZA KUGAWA BOTI NA VIZIMBA VYA SAMAKI

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amebainisha Ujio wa Rais Samia Suluhu Hassan Mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya Siku mbili kuanzia Jumatatu 29-30, 2024 ambapo atazindua Ugawaji wa Boti na Vizimba vya Samaki. Makalla amesema hayo mapema leo januari 26, 2024 wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa ukimhusisha pia Ujumbe wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kufuatia Ugeni huo Makalla amewakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani kufika kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza siku ya jumatatu kwa ajili ya kumpokea na kumlaki pamoja na siku ya jumanne kwenye uwanja wa Nyamagana. "Tarehe 30 januari, 2024 Mhe. Rais atazindua Ugawaji wa zana za Uvuvi za Kisasa kwa ajili ya Uvuvi endelevu vikiwemo Boti na Vizimba pamoja na kuzungumza na wananchi wa kanda ya Ziwa kwenye viwanja vya Nyamagana, hivyo basi nawaalika wananchi wote wa Mkoa wa Mwanza." CPA Makalla. Aidha, amefafanua kuwa Rais Samia baada ya kuwasili Mwanza siku ya Jumatatu atatumia barabara kuu ya kuelekea mjini hivyo wananchi wanaalikwa kumlaki barabarani kuanzia Sabasaba, Pasiansi, Bwiru na Kwenye Mzunguko wa Ziro ili kumshangilia na kumlaki.

Friday, January 26, 2024

RC SENDIGA AKABIDHI PIKIPIKI 42 KWA JUMUIYA ZA MAJI RUWASA

 

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amekabidhi pikipiki 42 kwa jumuiya za watoa huduma za maji katika wilaya zote za Mkoa wa Manyara ili kurahisisha utendaji kazi kwa watumiaji hao.

Pikipiki hizo zimetolewa na Wakala wa Maji Safi na Salama na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Manyara.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo Mhe. Sendiga amesema ni vyema kwa watumishi hao kuzitunza kwani ni mali ya serikali.

"Niwasihi tukahakikishe pikipiki hizi zinaenda kutumika kama ilivyokusudiwa na kuhakikisha skimu za maji zinakuwa endelevu na Wananchi wanapata huduma ya maji muda wote kwani ni haki yao ya msingi", amesema Mhe. Sendiga.

Aidha, Mhe. Sendiga amewataka wakuu wa taasisi mbali mbali kukusanya fedha za Umma kwa uadilifu kwa kuzingatia taratibu, kanuni na sheria zilizopo na kusitokee chombo chochote kukiuka kwa sababu yoyote huku akiwasihi wakuu wa wilaya wote kuendelea kusimamia vyema uhai wa miradi iliyojengwa.

"Serikali imewekeza fedha nyingi sana kujenga miradi hii ya maji, fedha hizi ni zenu kupitia kodi na tozo mbalimbali, tunajukumu kubwa la kuitunza miradi ili kuhakikisha kusudi la Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan la kumtua mama ndoo kichwani linafikiwa", amesema Mhe. Sendiga.

Akitoa shukrani zake kwa RUWASA Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange amesema kuwa atasimamia na kufuatilia kwa Ukaribu kama watumisji waliokabidhiwa pikipiki hizo wanazifanyi kazi kama ambavyo kusudio la Serikali ilivyowaagiza.
Kwa upande wake Meneja wa RUWASA mkoa wa Manyara Injinia Wolter Kilter amesema lengo la kuwapa pikipiki hizo kwa watumiaji hao ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma za maji kwa uharaha zaidi.

Amesema kuwa Mkoa wa Manyara unajumla ya Vyombo hivi 88 vinavyosimamia Skimu za maji 346 na kuhudumia wananchi 1,268,239 ambapo mpaka Septemba 30, 2023 zilikusanywa jumla ya Tshs 2,113,232,529", amesema Injinia Kilter.

Ameongeza kuwa RUWASA inaendelea kuvipatia mafunzo jumuiya za watumiaji Maji kama jinsi ya kuandaa mpango wa biashara na ufungaji wa hesabu, vyombo 32 vimeshapatiwa mafunzo hayo mpaka Julai 23, 2023.

KATIBU MKUU WA CCM TAIFA AFUNGUKA JINSI WATAKAVYOSHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

 

VICTOR MASANGU KIBAHA


KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa  Dkt. Emmanuel Nchimbi amewahakikishia wana chama kuwa ana  uhakika mkubwa  chama chake kitaibuka na ushindi mkubwa wa zaidi ya asilimia 100  kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa. 

Nchimbi ameyasema hayo wakati  alipokuwa akizungumza katika kikao cha Makatibu wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika kilichofanyika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kwamfipa kilichopo Wilayani  Kibaha Kibaha mkoani Pwani.
"Nchi ya Afrika Kusini na Namibia watakuwa wakifanya uchaguzi wao mkuu, wakati Tanzania, mwaka huu na sisi tutakuwa  tukifanya  uchaguzi wa serikali za mitaa, na mwaka ujao, tutakuwa na uchaguzi mkuu niwahakikishie CCM utKATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk.Emmanuel Nchimbi amesema ana uhakika chama chake kitafanya vizuri kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa zaidi ya asilimia 100.

Ameyasema hayo jana alipokuwa akizungumza katika kikao cha Makatibu wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika kilichofanyika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kwamfipa Kibaha.

"Afrika Kusini na Namibia watakuwa wakifanya uchaguzi wao mkuu, wakati Tanzania, mwaka huu tutafanya uchaguzi wa serikali za mitaa na mwaka ujao, tutakuwa na uchaguzi mkuu niwahakikishie CCM itashinda kwa kishindo kikubwa " alisema Dkt Nchimbi.

Akizungumzia kuhusiana na mkutano huo na uwepo wa ujumbe wa chama Cha Kikomunist Cha nchini China (CPC) alisema, ni muendelezo wa mikutano iliyopita ya kujadili mambo mbalimbali ya vyama vyao. 

Pia alieleza kwamba CPC imekuwa rafiki mzuri na mshirika anayestahili wa vyama hivyo vya Ukombozi  tangu wakati wa mapambano ya ukombozi ya kisasa.

Kwa upande wa shule hiyo ya Uongozi Dkt Nchimbi alisema, kuwepo kwake ni miongoni mwa urithi ambao unazungumza mengi kuhusu muda na misimu yote ya mshikamano wa kindugu huku wakitazamia usaidizi unaoendelea, kwa mustakabali bora kwa manufaa ya pande zote za vyama hivyo.

Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere ni zao la azma ya muda mrefu la vyama vyetu kuwa na taasisi ambayo itatoa mafunzo ya uongozi na itikadi, hasa kwa vijana ambao ni kizazi kijacho kuchukua uongozi wa kuendelea na mapambano, ya kuwakomboa na kuwawezesha watu wetu kiuchumi na maisha bora.

"Nimpongeze mkuu wa shule, Prof. Marcelina Chijoriga, ambaye amekuwa akifanya kazi ya kupongezwa ili kuweka shule kwenye mstari, bila kuathiri maono na dhamira ya shule,"alisema.

Katika hatua nyingine aliwapongeza wafuasi wa Zanu-PF, wanachama, viongozi na watu wa Zimbabwe kwa kufanya uchaguzi mkuu wa kidemokrasia wenye amani, huru na wa haki, ambapo kiongozi kutoka chama hicho Emerson Mnangagwa alichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo.


Akizungumzia kuhusiana na mkutano huo na uwepo wa ujumbe wa chama Cha Kikomunist Cha nchini China (CPC) alisema, ni muendelezo wa mikutano iliyopita ya kujadili mambo mbalimbali ya vyama vyao. 

Kadhalika alieleza kwamba CPC imekuwa rafiki mzuri na mshirika anayestahili wa vyama hivyo vya Ukombozi  tangu wakati wa mapambano ya ukombozi ya kisasa.

Kwa upande wa shule hiyo ya Uongozi Dkt.Nchimbi alisema, kuwepo kwake ni miongoni mwa urithi ambao unazungumza mengi kuhusu muda na misimu yote ya mshikamano wa kindugu huku wakitazamia usaidizi unaoendelea, kwa mustakabali bora kwa manufaa ya pande zote za vyama hivyo.

Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere ni zao la azma ya muda mrefu la vyama vyetu kuwa na taasisi ambayo itatoa mafunzo ya uongozi na itikadi, hasa kwa vijana ambao ni kizazi kijacho kuchukua uongozi wa kuendelea na mapambano, ya kuwakomboa na kuwawezesha watu wetu kiuchumi na maisha bora.

"Nimpongeze mkuu wa shule, Prof. Marcelina Chijoriga, ambaye amekuwa akifanya kazi ya kupongezwa ili kuweka shule kwenye mstari, bila kuathiri maono na dhamira ya shule,"alisema.
Katika hatua nyingine aliwapongeza wafuasi wa Zanu-PF, wanachama, viongozi na watu wa Zimbabwe kwa kufanya uchaguzi mkuu wa kidemokrasia wenye amani, huru na wa haki, ambapo kiongozi kutoka chama hicho Emerson Mnangagwa alichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo.

Dkt. Nchimbi  ameshiriki kikao na  cha siku tatu na Makatibu kutoka vyama vya Ukombozi  Kusini mwa Afrika ambavyo ni ANC cha Afrika kusini, SWAPO cha nchini Namibia, FRELIMO cha Msumbiji, MPLA cha Angola, ZANU - PF cha Zimbabwe na CPC Chama Cha kikomunisty cha nchini China.

WAZIRI AWESO AWASHA MOTO HUDUMA KUBORESHWA MAMLAKA YA MAJI ARUSHA,ATOA SIKU 30


 Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso(MB) amewasili jijini Arusha kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali za upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama ikiwa ni siku moja tu baada ya maelekezo ya Chama Cha Mapinduzi kutoka kwa Katibu wa NEC Itikati, Uenezi na Mafunzo CCM Ndg.Paul Makonda.

Akiwa jijini Arusha ameianza kazi kwa kufanya vikao vya ndani na Serikali  ya Mkoa na Wilaya ya Arusha pamoja na kuketi na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Arusha.

Katika hatua nyingine Waziri Aweso amefanya ziara ya aina yake kwa kushtukiza katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Arusha kujionea hali halisi ya  utoaji huduma na upatikanaji wa maji na kupata fursa ya kuwasikiliza wananchi.

Aidha, Akizungumza baada ya kuzungukia mitaa mbalimbali Aweso amekemea vikali changamoto zilizobainika na kutoa siku 30 kwa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa mazingira Arusha (AUWSA) kuhakikisha wanaboresha matatizo yote.
Changamoyo zilizoonekana kwa haraka ni pamoja na maunganisho mapya ya huduma ya maji kwa wateja eneo lenye malalamiko kwa muda mrefu, Huduma kwa wateja isioridhisha, upotevu wa maji na mambo mengine.
Waziri Aweso kwa hisia akizungumza kwa hisia kali, amesisitiza suala la ushirikishwaji wa wananchi katika kupata taarifa na kutowabambikia bili za maji na kutanabaisha kuwa ni muda muafaka sasa wa Serikali kuanza matumizi ya Mita za Lipa kabla (Pre-paid meter).

Akihitimisha amemtaka Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Arusha AUWSA Mhandisi Rujomba kufanya mabadiliko ya vitengo mbalimbali na kuondoa watu wazembe ikiwa ni pamoja na kutengeneza mpango kazi mpya.

RC KUNENGE AMPA KONGOLE RAIS SAMIA KWA KUTOA MATREKA MATATU KWA AJILI YA KILIMO

 

NA VICTOR MASANGU PWANI 

Serikali Mkoani Pwani katika kumuunga mkono Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweka mikakati kabambe ya kutenga maeneo  kwa ajili ya kilimo cha kisasa na chenye tija  ambacho kitajumuisha mazao ya kibiashara kwa lengo la kukuza uchumi.

Hayo  yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge wakati wa halfa fupi ya kukabidhi matreka matatu kwa uongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Kibaha vijijini.
Kunenge alisema kwamba matreka hayo matatu ambayo wamepatiwa na Rais Samia yatakwenda kuwa msaada mkubwa na kuleta mapinduzi katika kilimo cha kisasa.

"Sisi kama Mkoa wa Pwani kwa sasa tumejipanga kuhakikisha kwamba tunajikita zaidi katika kuboresha sekta ya kilimo na kwa sasa tumepokea matreka haya kwa ajili ya halmashauri ya Wilaya ya Kibaha vijijini kwa hivyo hatuna budi kumshukuru Rais wetu kwa hatua hii ya kutupatia matreka haya,"alisema Kunenge.
Aidha Kunenge alibainisha kwamba kwa sasa wameshaanza kujikita katika kilimo cha mazao ya biashara ikiwemo zao la Pamba,ufuta kilimo pamba.mchikichi,korosho mihogo  pamoja na mazao mengine ambayo yataweza kuleta mabadiliko katika kukuza shughuli  mbali mbali za  kiuchumi.

Aidha aliongeza kwamba Mkoa wa Pwani wanataka kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo hivyo ana imani kubwa mabadiliko hayo yatakwenda katika halmashauri zote tisa zilizopo katika Mkoa wa Pwani.
Pia kunenge aliwaomba viongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha kwamba wanayatunza vizuri matrekta hayo ili yaweze kudumu kwa kipindi kirefu ili kuweza kuwasaidia wakulima katika kilimo cha biashara.


Aidha pamoja na hayo aliongeza kwamba katika kuendana na kasi ya mabadiliko katika Wilaya ya Rufiji tayari kumeshafanyika uzinduzi wa zao la pamba na kwamba kutajengwa kiwanda kikubwa kwa ajili ya kuchakata zao hilo.

Kunenge amempongeza kwa dhati Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za  hali na mali katika kukuza sekta   ya kilimo cha kuwezesha matreka hayo.

 Aidha Kunenge katika hatua nyingine aliwawahimiza wakulima wa Mkoa wa pwani kuendana na mabadiliko na kuwataka wakulima wajikite zaidi katika kilimo cha mazao ya biashara.
Sambamba na hayo alisema wapo katika mikakati ya kujenga skimu kubwa za umwagiliaji ambazo zitaweza kuwasaidia wakulima katika kuendesha shughuli zao za kilimo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimon amesema kwamba wameshakubaliana matrekta hayo yatakwenda katika halmashauri ya Wilaya ya kibaha ili kuboresha kilimo cha kisasa.

Aidha alibainisha kwamba katika mpango wao wamekubaliana mambo matatu ikiwemo kuunganisha kilimo pamoja na viwanda,rasirimali watu pamoja na teknolojia lengo ikiwa ni kuwasaidia wakulima kulima kilimo cha kisasa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha vijijini Erasto Makala  lengo lao kubwa ni kutoka katika kilimo cha chakula na kujikita katika biashara.
Mkoa wa Pwani kwa sasa umejipanga kuunganisha kilimo pamoja na viwanda lengo ikiwa ni kutimiza azma ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hasssan kulisha dunia nzima kupitia sekta ya kilimo.

Wednesday, January 24, 2024

'MALIZIENI MIRADI KWA WAKATI' - RC SENDIGA

 

Na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/MMG, Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga mapema leo Januari 23, 2024 amefanya ziara ya kukagua baadhi ya miradi inayoendelea katika mkoa wake wilayani Babati.

Ziara hiyo ilianzia katika Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharula (EMD) katika Hospitali ya Mji wa Babati, ambapo amewataka wasimamizi wa mradi huo akiwemo mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange kujitahidi ujenzi wa jengo hilo unakamilika kwa haraka.

Akitoa taarifa Mganga Mkuu wa Mji Daktari Kyabaroti Kyabaroti amesema kuwa jengo hilo lilitengewa Mil. 300 ambapo mpaka sasa lipo katika hatua za umaliziaji na ifikapo mwanzoni mwa mwezi wa Februari litaanza kutumika.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga akiteta jambo na Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange mara baada ya kutembelea ujenzi wa jengo la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara ililopo eneo la Maisaka Katani kata ya Maisaka, Babati Mjini.
Pia, Mhe. Queen Sendiga alipata wasaa wa kutembelea ujenzi wa jengo la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara ililopo eneo la Maisaka Katani kata ya Maisaka, Babati Mjini ulioanza Oktoba 25, 2023.

Mhe. Sendiga amejionea ujenzi huo huku akiwataka wataalamu hao kumaliza kwa wakati bila kutoa visingizio vyovyote vitavyosababisha ukwamishaji wa ujenzi huo.

Ujenzi huo unaogharimu shilingi Mil. 600 ambapo awamu ya kwanza wamepewa zaidi ya mil. 285 kwa ajili ya ukamilishaji wa Boma, msingi mpaka gorofa ya kwanza na sasa ujenzi umefikia asilimia 21.4.

Aidha Jeshi la Zimamoto Walimemshukuru Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuendelea kuwezesha majeshi ya Tanzania katika kukabiliana na majanga mbali mbali huku wakimshukuru Mhe. Sendiga na ofisi yake kwa ujumla kuweza kuwawezesha katika miongozo mbali mbali.
Mradi wa ujenzi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara linalojengwa eneo la mkoani wilayani Babati. 
Baadae Mhe. Queen Sendiga alifika katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara linalojengwa eneo la mkoani wilayani Babati. Mradi ulibuliwa baada ya Serikali kuanzisha mkoa wa Manyara mwaka 2002 na ndipo uhitaji wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa ulipotokea.

Jengo hilo la ghorafa nne ambapo likikamilika litakuwa na jumla ya vyumba vya ofisi 33 kati ya hivyo 06 ni vyumba vya ofisi za maafisa wakuu ngazi ya mkoa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, ACP George Katabazi amesema utekelezaji unaoendelea ni awamu ya Kwanza ambayo ilianza baada ya Serikali kutoa fedha mnamo mwezi Aprili 2023 jumla ya shilingi milioni mia nane tu (TShs.800,000,000.00) ambazo zilipokelewa Polisi Mkoa Manyara.

Amesema kazi zilizofanyika ni ujenzi wa msingi, nguzo na sakafu za ghorofa zote nne huku wakifanya maandalizi ya ujenzi wa kuta za pamoja na kuezeka na ujenzi wa chumba cha mitambo ya lifti ambapo wanatarajia ujenzi huo ukamilike mwishoni mwa mwezi Februari.

Nae Mhe. Sendiga amewapongeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara kwa kutekeleza mradi kwa vitendo huku akizitaka taasisi nyingine zenye miradi mkoani humo kuiga Jeshi la Polisi.

Aidha Mhe. Sendiga amemtaka mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange kuhakikisha anasimamia kwa ufasaha ujenzi wa jengo la ofisi ya yake linakamilika kwa wakati maana ujenzi wake umekuwa ukisua sua jambo linaloleta ukakasi kila anapotembelea.

Jengo la ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Babati ambapo ujenzi wake umekuwa ukisua sua. (Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/MMG, Manyara)

TAWIRI NA MUENDELEZO WA TAFITI UGONJWA WA TWIGA ULIOATHIRI ASILIMIA 62 YA TWIGA KATIKA HIFADHI YA TAIFA RUAHA.

 


Taasisi ya Utafiti wa  Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) inaendelea kufanya  tafiti zaidi juu ya madhara na matibabu ya ugonjwa wa ngozi wa Twiga ambao  matokeo ya awali yameonyesha maeneo yanayoathirika ya viungio kwenye miguu (magoti) hususan miguu ya mbele, kuna vimelea vya bakteria, virusi na fangasi.


Akizungumza wakati wa ufuatiliaji wa matibabu ya ugonjwa huo katika hifadhi ya Taifa Ruaha, Dkt. Julius Keyyu ambaye ni  Mkurugenzi wa Utafiti  TAWIRI,  amesema ugonjwa wa ngozi wa Twiga uliogundulika katika hifadhi  ya Taifa  Ruaha mwaka 2000 ni tofauti na ugonjwa wa ngozi wa Twiga katika nchi nyingine duniani 

" tumefuatilia ugonjwa huu kwa nchi nyingine duniani na kubaini upo tofauti na hapa nchini" amebainisha  Dkt. Keyyu


Dkt.Keyyu amesema asilimia  62% ya Twiga waliopo hifadhi ya  Taifa Ruaha wana ugonjwa wa ngozi ambao pia, umeonekana kwa kiwango kidogo katika hifadhi za Taifa za Tarangire na Serengeti, na tafiti za awali zimeonesha madhara ya ugonjwa huo ni pamoja na Twiga wenye ugonjwa kutembea kwa  kuchechemea, hivyo kushindwa kukimbia wanapofukuzwa na wanyama wawindao pia hutembea umbali mdogo kwa siku, kwa wiki na kwa mwezi ukilinganisha na Twiga wasio na ugonjwa. 


Dkt. Keyyu amesema kwa sasa TAWIRI inaendelea na ufuatiliaji wa matibabu ya ugonjwa huo ili kubaini kisababishi asili cha ugonjwa (_primary agent_) na kupata matokeo ya kushauri nini kifanyike ili kudhibiti ugonjwa huu wa ngozi wa Twiga na kuhakikisha mnyama huyu ambaye ni nembo ya taifa anazidi kuwepo.


Ikumbukwe  utafiti  wa  ugonjwa  huu wa ngozi  wa  twiga  unatekelezwa chini ya Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) uliopo chini  ya  Wizara  ya  Maliasili  na  Utalii  na jukumuu la TAWIRI  ni kufanya  tafiti .


Tuesday, January 23, 2024

SERIKALI YAIPONGEZA BARRICK KWA KUENDELEA KUKUZA UCHUMI WA TANZANIA KUPITIA UWEKEZAJI WAKE KATIKA SEKTA YA MADINI.

 

Naibu Waziri wa Madini, Dk. Steven Kiruswa, akikabidhi mfano wa hundi ya kiasi cha dola za kimarekani 10000 kwa Wawakilishi wa Kikundi cha Tujikomboe cha mkoani Geita, Maria Mihayo (kushoto) na Chausi Kasura cha akina mama wa ponda kokoto iliyotolewa na taasisi ya NVeP inayofadhiliwa na Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick,Mark Bristow, katika hafla iliyofanyika katika Mgodi wa Bulyanhulu mkoani Shinyanga . Kulia ni Rais na Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, Mkuu wa Mkoa wa shinyanga Christina Mndeme na Mkuu wa mkoa Geita, Martin Shigella(kushoto).
Naibu Waziri wa Madini, Dk. Steven Kiruswa akiongea katika mkutano huo
Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow akiongea na waandishi wa habari kushoto kwake ni Meneja wa Barrick nchini,Melkiory Ngido
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigella akiongea katika mkutano huo
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christine Mndeme akiongea katika mkutano huo
Mkuu wa wilaya ya Kahama.Mboni Mhita akitambulisha viongozi wa mkoa
---
Naibu Waziri wa Madini, Dk. Steven Kiruswa, ameipongeza kampuni ya Dhahabu ya Barrick, ambayo inaendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals Corporation kwa kufanya uwekezaji wenye ufanii ambao umeanza kuleta mabadiliko chanya kwa kuchangia pato la Taifa sambamba na kufanikisha miradi mbalimbali ya kijamii na kuongeza wigo wa ajira kwa watanzania.

Dk. Kiruswa alitoa pongezi hizo wakati wa mkutano uliondaliwa na Barrick kwa ajili ya kutoa taarifa za utendaji wa kampuni katika kipindi cha robo mwaka uliopita kwa waandshi wa habari na wadau mbalimbali uluofanyika katika mgodi wa Barrick Bulyanhulu ambao pia ulijumuisha viongozi wa Serikali mkoani Shinyanga.

Alisema ubia wa Serikali na kampuni ya Barrick umekuwa ukiendelea kupata mafanikio siku hadi siku na mchango wa faida inayotokana na ubia huu kuingia katika mfuko wa Serikali na huduma za kijamii kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka migodi ya Barrick kupata huduma bora kupitia miradi inayotekelezwa kwa fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR).

”Serikali tunajivunia uwekezaji huu ambao ni mfano wa kuigwa pia natoa wito kwa makampuni ya wawekezaji kuwa na programu za kukutana na viongozi wa Serikali katika maeneo yao na kutoa ripoti za utendaji,hii mbali na kudumisha uwazi inachangia kupata maoni ya wadau kutoka pande zote mbili”.alisisitiza Dk.Kiruswa.

Kwa upande wake, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow,Alisema kuwa migodi ya dhahabu ya Barrick ya North Mara na Bulyanhulu imeendelea kudumisha rekodi yake ya utendaji mzuri na kufikia mwongozo wa uzalishaji kwa mwaka 2023.

alisema mageuzi ya migodi miwili iliyokuwa imetelekezwa kuwa mkusanyiko wa maeneo ya uchimbaji wenye hadhi ya kimataifa ambayo kwa pamoja inazaliha dhahabu katika kiwango cha daraja la kwanza,yanaonyeha mafanikio yanayoweza kufikiwa pale kampuni za uchimbaji madini na Serikali wenyeji zinaposhirikiana katika kuwapatia wadau wao thamani halisi.

“Ubia wa Twiga sio tu kwamba umeleta mageuzi katika tasnia ya uchimbaji wa dhahabu nchini Tanzania bali pia umeiweka nchi,inayojulikana kama kivutio cha utalii barani Afrika,katika nafasi ya kivutio kikuu cha uwekezaji ambacho kina utajiri mkubwa wa raslimali za chuma na madini,”alisema Bristow.

Uchimbaji wa kupekecha katika migodi yote miwili unaonyesha mafanikio katika hifadhi zake za dhahabu zilizokuwa zimeihiwa au kupungukiwa dhahabu.Katika mgodi wa North Mara, uwezekano wa kuwa na hughuli nyingine za uchimbaji chini ya ardhi unachunguzwa huku uborehaji wa mpango wake wa mgodi wa wazi unatarajiwa kuongeza miaka zaidi katika uhai wake, katika mgodi wa Bulyanhulu, kuna fursa karibu na uso wa ardhi wa ardhi na uwezekano wa kuongeza uzalishaji na kunyumbuka kwa uchimbaji.

Bristow, alisema tangu Barrick ichukue migodi ya Tanzania mwaka 2019 imekua na kuwa mchangiaji mkubwa wa mapato ya Serikali, kupitia kodi, ajira, malipo kwa wazabuni wa ndani, miradi ya jamii na gawio kwa wanahisa.Uwekezaji wake katika uchumi hadi sasa una jumla ya zaidi ya dola bilioni 3.4 (kwa msingi wa 100%), ambapo kutokana na mafanikio haya migodi yake katika kipindi cha mwaka jana imetunukiwa tuzo mbalimbali za utendaji kazi kwa ufanisi mkubwa.

Awamu ya kwanza ya mpango wa Twiga wa kusongesha Mbele mustakabali wa Elimu ( Twiga Future Forward Education Initiative) wenye thamani ya Dola milioni 30 inakaribia ukingoni.Mpango huu utaborehwa kwa kiasi kikubwa miundombinu ya elimu ya Tanzania kwa kutoa vyumba vya madarasa,mabweni na vyoo kwa wanafunzi zaidi wapatao 49.000.

Kwa upande wao Mkuu wa Mkoa wa shinyanga Christina Mdeme na Mkuu wa mkoa Geita, Martin Shigella wakiongea kwa nyakati tofauti katika mkutano huo walipongeza kampuni ya Barrick kwa kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika mikoa yao husuani kupitia miradi inayotekelezwa na fedha za uwajibikaji kwa jamii ambayo imeboreha sekta mbalimbali hususani afya ,elimu ,maji safi na miundombinu ya barabara.