ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 20, 2019

KITUO CHA AFYA BWISYA UKEREWE SASA KUFIKIRIWA KUWA HOSPITALI.


Hii ni ziara ya kwanza ya kufanywa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kisiwa cha Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza. Ambapo awali baada ya Makamu wa Rais kuhani eneo la makaburi ilimolala miili ya baadhi marehemu kati ya mamia waliofariki kwenye ajali ya Meli ya MV Nyerere iliyotokea Septemba 19 mwaka 2018, na kuweka shada la maua pia aliweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya Bwisya Ukara.

ALICHOKIFANYA BARAKA MAGUFULI MBELE YA RAIS MAGUFULI IMEBAKI HISTORIA



Ni yule mkali wa kuigiza sauti ya Mhe. Rais .....safari hii kakutana naye uso kwa uso kwenye uzinduzi wa ndege mpya uliofanyika Airport jijini Mwanza

PICHA ZA MAPOLOMOKO YA LIYOSABABISHWA NA MLIPUKO WA ARDHI NA MUA YA UPEPO MKALI RORYA

MBUNGE wa Jimbo la Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM) akipewa maelezo na Emmanuel Odworu mmoja wa athirika wa mapolomoko yaliyosababishwa mlipuko na mvua ya upepo mkali katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara.
MBUNGE wa Jimbo la Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM) akipewa maelezo na wananchi wathiriwa na mapolomoko ya urefu wa km 2 yaliyosababishwa mlipuko na mvua ya upepo mkali iliyoharibu ekari 20 za mashamba ya mazao mchanganyiko katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara.
MBUNGE wa Jimbo la Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM) akipewa maelezo na Emmanuel Odworu mmoja wa athirika wa mapolomoko yaliyosababishwa mlipuko na mvua ya upepo mkali katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara.
Sehemu ya mashamba yaliyoharibiwa ekari 20 kusombwa vibaya na mapolomoko ya mawe na aedhi zaidi ya km 2 yaliyosababishwa na mlipuko na mvua ya upepo mkali katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara. 
MBUNGE wa Jimbo la Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM) akipewa maelezo na wananchi wathiriwa na mapolomoko ya urefu wa km 2 yaliyosababishwa mlipuko na mvua ya upepo mkali iliyoharibu ekari 20 za mashamba ya mazao mchanganyiko katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara.
MBUNGE wa Jimbo la Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, Lameck Airo (CCM) akikabidhi kiasi cha Sh milioni 2.3 Kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Tatwe Julius Ochwachi ili kusaidia waathiriwa wa Kaya kumi kufatia mapolomoko ya mawe na aedhi zaidi ya km 2 yaliyosababishwa na mlipuko na mvua ya upepo mkali katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara. 
 Sehemu ya mashamba yaliyoharibiwa ekari 20 kusombwa vibaya na mapolomoko ya mawe na aedhi zaidi ya km 2 yaliyosababishwa na mlipuko na mvua ya upepo mkali katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara
PICHA ZOTE NA PETER FABIAN.

Na MWANDISHI WETU RORYA MKOA WA MARA.


MVUA ya upepo mkali yasababisha mlipuko na mapolomoko ya mawe na mmomonyoko mkubwa wa ardhi yaliyotokea Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilayani Rorya Mkubwa wa Mara yaliyosababishwa na mvua kubwa ya iliyoambatana na upepo mkali umesababisha watu 93 kuathiriwa huku kaya kumi zikiathirika zaidi.

Mbunge wa Jimbo la Rorya Lameck Airo (CCM) alitembelea eneo hilo akiambatana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Charles Ochele na viongozi wengine wa Kata na Vijiji jirani kufika katika eneo la tukio kujionea uhalibifu mkubwa wa ardhi uliopelekea mto na bonde kubwa huku za zaidi ekari 20 za mazao ya wananchi kusombwa na maji na kuharibiwa na mamia ya mawe yaliyoporomoka yenye urefu wa km 2 kutoka eneo la tukio hadi mto Chirya.

Airo akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Tatwe alitoa pole kwa wananchi na kusikitisha na tukio hilo ambalo limeacha maswali mengi na kuwashitua wananchi zaidi 93 kuharibiwa mazao katika mashamba yao yenye urefu wa ekari 20 huku kaya kumi zikipata athari kubwa ikiwemo kupata nyufa kutoka na mlipuko huo.

"Tukio hili limetokea majira ya saa 11:00 jioni Desemba 12 na limeacha janga na hali ya wasiwasi baada ya kupolomoka wa shehena kubwa ya mawe na mmomonyoka mkubwa wa ardhi amapo eneo hilo limekuwa na mto mkubwa ambao unatililisha maji hadi mto Chirya haya ni maajabu lakini tushukuru hayakulenga makazi ya wananchi tungeshuhudia mamia kupoteza maisha," alisema.

Airo aliwaeleza wananchi hao kusikitishwa na tangu kutokea kwa tukio hilo ambapo Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Saimon Chacha na Kamati ya Ulinzi na Usalama na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kushindwa kufika katika eneo la tukio na kujionea athari kubwa ya mapolomoko na uharibifu wa ardhi na mazao ya wananchi kusombwa na kufunikwa na mchanga jamb ambalo amesikitishwa na kuwaomba wananchi kuwa watulivu kwa kipindi hiki ambacho tukisubilia utaratibu wa serikali baada ya kufika kujionea eneo hilo.

"Nimepokea taarifa za tukio hili kwa mshituko na nilimtaalifu Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ochele na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Samwel Kiboye ambapo hapa nimekuja na viongozi hawa wa Wilaya wa Chama na tunatoa pole ya Sh milioni 2.3 kwa Kaya tatu zilizoathiriwa na kujihifadhi kwa na jirani huku kaya saba ambazo jumla yake kuzifanya kuwa Kaya kumi kuanza kupata huduma za chakula na malazi wakati tukisubiri wataalamu wa Halmashauri kufanya tathimini ya athari ya tukio hili,

Akikabidhi kiasi cha fedha hizo kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Tatwe, Julius Ochwachi, Mbunge Airo alifafanua kuwa yeye binafsi ametoa kiasi cha Sh milioni moja, Mwenyekiti wa CCM Wilaya hiyo, Ochele ametoa Sh 300,000/- na Mdau wa maendeleo kutoka Wilaya hiyo aliyefahamika kwa jina Orwero aliyechangia Sh milioni moja pia.

Wakizungumzia katika eneo la tukio hilo baadhi ya wathirika wa tukio hilo, Kevin Chacha, Emmanuel Odworu, Rosemary Joseph walieleza kwa nyakati tofauti kuwa siku hiyo ilianza mvua majira ya saa 5:00 asubuhi ikanyesha kisha ikakata badae majira saa 11:00 jioni ikarejea mvua kubwa na kisha kusikika mliyo wa mlipuko mkubwa na kusikika kishindo cha mapolomoko ya maji, mawe na mchanga huku mvua ikiambatana na upepo mkali.

" Mvua hii iliwahi kutokea miaka 1996 lakini haikuwa na madhala kama hii leo tumeshuhudia maafa na mazao kusombwa na mawe na mchanga na tumeshuhudia nyumba mbili zikianguka na ng'ommbe wawili wakisombwa ni jambo ambalo limetuweka katika wasiwasi mkubwa na kuhofia maisha yetu hivyo tunaomba wataalam waje kufanya utafiti kutambua kilichotokea ama kilichosababisha, Alisema Rosemary Joseph

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Ochele alisema kwamba tukio hilo limewapa funzo na kuwa Wilaya hiyo ina viongozi wa Serikali wa aina gani kwa kushindwa kufika kujionea athari na uharibifu kwa wakati jambo ambalo watalikemea na kulisema kwa wahusika na kama Chama hawakufurahishwa na hali hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Tatwe, Julius Ochwachi aliwashukuru Mbunge Airo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Ochele kwa kufika na kutembelea eneo la tukio huku wakiguswa na kutoa msaada kwa waathirika kumi waliopoteza nyumba na mifugo yao huku wananchi wengine 83 wakiwa wameshuhudiwa wakipoteza mazao ya mahindi, mtama, ulezi, mihogo, viazi vitamu, mpunga na maharage katika maeneo mashamba yao zaidi ya ekari 20 huku mapolomoko hayo yakiwa na urefu wa km 2 kutoka eneo la tukio hadi mto Chirya.

Sunday, December 15, 2019

MBUNGE TWEVE NA KOMBA WAIPA HESHIMA TANZANIA

Mbunge Rose Tweve akishangiliwa na wabunge wenzake 
Mbunge Rose Tweve  na Yosepher Komba kulia wakijiandaa kwa kuanza riadha 
Mbunge Rose Tweve kulia akiwakimbiza wakenya 
Wabunge wanaume wanamichezo toka Tanzania wakimshangilia mbunge Tweve
 Wabunge wanawake Rose Tweve na Yosepher Komba wameendelea kuing'aza nyota ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuibuka na medali za dhahabu katika mbio za mita Mia moja (100m) na mita elfu moja na Mia tano (1500m).

Wakati Rose Tweve kutoka Mkoa wa Iringa akiwaburuza wabunge wa nchi za Kenya, Uganda, Burundi na wale wa Bunge la Afrika Mashariki EALA,  Yosepher Komba kutoka Viti Maalum Mkoa wa Tanga aliwagaragaza wapinzani wake katika mbio za mita 1500.

Wabunge Hao Vijana sasa mwaka wa Pili mfululizo wanaendelea kuipeperusha vema Bendera ya Tanzania katika mchezo wa riadha Naendelea wanatarajia kuendelea tena hapo jumapili katika mbio za kupokezana Vijiji.

Kwa upande mwengine mwanamama Anatropia Teonest alimaliza nafasi ya Pili katika mbio za mita 400, huku wanaume kupokezana Vijiji Tanzania ilishika nafasi ya tatu.

Michezo hiyo inaendelea Kesho katika mchezo wa Wavu wanaume na wanawake wakati Bunge la Tanzania watajitupa uwanjani kuvaana na Bunge la Afrika Mashariki

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA KITUO CHA AFYA UKARA



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, akiweka Shada la Maua kwenye Mnara wa kumbukumbu  Eneo waklipoozikwa Wahanga wa Ajali ya Kivuko cha MV Nyerere Kisiwani  Ukara Wilayani Ukerewe  Disemba 14,2019 wakati malipotembekea Eneo hilo.
Picha ya Wananchi wa Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, akikata utepe kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe  Disemba 14,2019.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, akimpa pole Mtoto Femia Sabato (3)mkazi wa Bwisya Ukara aliyelazwa katika  Kituo cha Afya  Bwisya Ukara kwa matibabu mara baada  kuzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Wilayani Ukerewe  Disemba 14,2019. kushoto ni Bibi wa Mtoto huyo Silimagi Manyeji.




Picha ya Wananchi wa Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza.  
Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Ngoma ya Matoigaa Charoo cha Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza Goabth Bwere akionesha Umahiri  wake katika uwanja wa Bwisye Ukara wakati wa Hafla ya  kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe Disemba 14,2019.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, akihutubia Wananchi wa wa Bwisye Ukara Wilayani Ukerewe baada ya kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe Disemba 14,2019. .
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, katikati akiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Ngoma ya Matoigaa Charoo cha Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza Goabth Bwere katika uwanja wa Bwisye Baada ya Makamu wa Rais  kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe Disemba 14,2019.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, katikati akiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Ngoma ya Matoigaa Charoo cha Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza Goabth Bwere katika uwanja wa Bwisye Baada ya Makamu wa Rais  kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe Disemba 14,2019.
Picha ya Wananchi wa Ukara Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza.




.Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Suluhu Hassan, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela alipowasili Uwanja wa ndege wa Mwanza  akitokea Kisiwani ukara wilayani Ukerewe  Baada ya kuweka Jiwe la Uzinduzi wa Majengo mapya ya Kituo cha Afya  Bwisya Ukara Ukerewe Disemba 14,2019.