ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 4, 2014

VIJANA WA NYAMONGO WILAYANI TARIME MKOANI MARA WAIKUBALI SEMINA YA FURSA.

Muelimishaji wa Semina ya Fursa mhitimu wa Chuo Kikuu ambaye pia ni msanii wa Muziki wa Hip hop nchini kutoka kundi la Weusi akizungumza na vijana wa kata ya Ingwe, Nyamongo wilayani Tarime mkoani Mara jinsi ya kuzibaini na kuzifanyia kazi fursa zilizopo katika mazingira yao. 
Kaimu Meneja Mahusiano wa North Mara Gold Mine Bwana Zakayo Kabelo aliwaasa washiriki hao wa Semina ya Fursa kusikiliza kwa makini yale yote yatakayo jadiliwa, kuyazingatia kwaajili ya kwenda kuyafanyia kazi. "Furaha yetu kama mgodi pamoja na Radio Clouds itatimia pale tutakapotoka hapa na baadaye kukutana na vijana waliotoka humu wakiwa katika maisha ya ustawi tofauti na walivyokuwa siku za nyuma"
Muelimishaji wa Semina ya Fursa mhitimu wa Chuo Kikuu ambaye pia ni msanii wa Muziki wa Hip hop nchini kutoka kundi la Weusi akizungumza na vijana wa kijiji cha Ingwe, Nyamongo wilayani Tarime mkoani Mara jinsi ya kuzibaini na kuzifanyia kazi fursa zilizopo katika mazingira yao. 
Muelimishaji wa Semina ya Fursa mhitimu wa Chuo Kikuu ambaye pia ni msanii wa Muziki wa Hip hop nchini kutoka kundi la Weusi, akiweka mkazo katika moja ya mada zilizo wasilishwa ambapo mada ya kwanza ilikuwa ni
1. Maana ya Fursa na Utazitambuaje Fursa na utawezaje kuzitumia ili upate tija katika maendeleo.
2.Utawezaje kujenga tabia ya kufanikiwa na kupata maendeleo.
3.Nidhamu ya matumizi ya fedha.
4.Ujasiliamali wenye tija. (kuna wajasiliamali wengi lakini hakuna tija watu wanafanya shughuli zao za uwekezaji kwa kubahatisha bila malengo wala mpango mkakati, ubunifu na kadhalika)
5.Ushiriki mzuri katika jamii (Unawezaje kuwa kaka bora, mama bora na baba bora)
Afisa Ushirikishwaji (ABG) Nicodemus Keraryo akizungumza na wanasemina.
Kikundi cha sanaa kata ya Ingwe, Nyamongo, ambacho kimejikita katika kutoa elimu kupitia burudani kikitoa burudani kwa washiriki wa semina ya Fursa.
Mmoja kati ya akinamama ambao ni washiriki wa Semina ya Fursa katika kijiji cha Nyamongo wilayani Tarime akishiriki katikakuuliza maswali.
Vijana nao walikuwa mstari wa mbele.
Akina dada na akina mama wameitikia wito kushiriki Fursa.
Uwasilishaji wa mawazo pamoja na maswali muhimu ndani ya Semina ya Fursa.
Kwa umakiiiiini Seminani.
Akinamama nao wamo! Walilitumia vyema jukwaa la Fursa kuelezea vikwazo vinavywakabili ndani ya jamii zao hali inayosababisha wao kushindwa kupata kufaidi Fursa zinazo wazunguka.
Muelimishaji wa Semina ya Fursa Bi. Rehema yeye alizungumzia Umuhimu wa kufanya kazi  huku ukiwa na Afya bora na jinsi ya kuboresha Afya likiwemo suala la kuzingatia Tiba bora na sahihi.
Washiriki seminani.
"Afya ikiwa mgogoro jamii itazorota kimaendeleo, uzalishaji utapugua, na jamii itarudi nyuma kwani hata akiba yote itaelekezwa kwenye matibabu badala ya kuelekezwa kwenye masuala ya maendeleo likiwemo suala la kulipia  ada za shule kwa watoto, kununua pembejeo na zana muhimu za kilimo na mambo kadha muhimu" alisema Rehema.
Diwani wa viti maalum kata ya Kemambu, Tarafa ya Ingwe, Nyamongo wilayani Tarime Mh. Mwajuma Issa Chacha akichangia ndani ya Semina ya Fursa.
Elimu na daftari...
Wazee walijichanganya na vijana kuipata Elimu ya Fursa.
1. Unawezaje kujua kuwa wewe ni mzuri wa kitu fulani na unakimudu?
2. Je umewahi kujiuliza watu wa jamii yako wanakutizamaje na wanakupa thamani gani?
3. Vipi uwezo na mapungufu yako? Ukichukuwa muda wa kutafakari majibu ya yote haya utagundua kuwa wewe unamapugufu gani na una sifa gani, mwisho wa siku utakacho baini basi kifanyie kazi.
Semina ya siku ya kwanza ilimalizika.

DHAMIRA YETU NI KUKIDHI MAHITAJI YA WATEJA YA KIBENKI NA YA KIFEDHA.

Pichani ni  Meneja wa Tawi lililopo ndani ya  maonyesho ya biashara ya Kimataifa ya 38 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwal.Julius Nyerere jijini Dar,Bi. Upendo Tendewa akifafanua zaidi huduma zitolewazo na benki hiyo.Bi.Upendo amesema kuwa dhamira yao kubwa ni kukidhi mahitaji ya wateja ya kibenki na ya kifedha kwa kuhakikisha upatikanaji wa bidha na huduma bora kabisa katika soko  kwa bei inayowezekana kulipa na viwango  vyenye manufaa yanayolingana na gharama na faida ya kurudhisha kwa mwanahisa.

Amesma benki hiyo inatumia kadi yako iitwayo Twiga ExpressCard ambayo mteja anaweza kuitumia kupata huduma za kibenki katika ATM yoyote iliyounganishwa na mtandano wa UMOJA SWITCH,ambapo zaidi ya ATM 180 na mabenki ishirini nna nne nchini yameunganishwa.
 Afisa Masoko wa Benki ya Twiga Bancorp Bwa.Adalbert Alchard akizungumza na Wanahabari nje ya banda lao kuhusiana na huduma mbalimbali zitolewazo na benki hiyo kwa wateja wao, kwenye maonyesho ya biashara ya Kimataifa ya 38 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwal.Julius Nyerere jijini Dar.Pichani kushoto ni  Afisa wa Benki hiyo,Bi Tuddy Lutengan.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, ABDULRAHMAN KINANA NA RAIS MSTAAFU, ALI HASSAN MWINYI WATEMBELEA GYM YA MAZOEZI YA TIMU YA AZAM FC, CHAMAZI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakijaribu kufanya mazoezi katika mashine zilizo ndani ya Gym ya mazoezi ya timu ya Azam Fc, wakati walipotembelea Gym hiyo kujionea leo baada ya hafla ya uzinduzi wa Msikiti wa ‘Masjidil Huda’, kwenye Uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam, leo Julai 4, 2014.
Mkurugenzi wa Makampuni ya SSB, Said Mohamed, (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa viongozi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa Makampuni ya SSB, Said Salim Bakhresa, wakati walipokuwa wakitembelea kujionea Uwanja wa Azam Complex, unaomilikiwa na timu ya Azam Fc, leo Chamazi.
Wakitembelea Uwanja wa Chamazi, kujionea maendeleo ya timu ya Azam Fc , leo.
Mkurugenzi wa Makampuni ya SSB, Said Mohamed, (kulia) akitoa maelezo kwa viongozi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi,  wakati walipokuwa wakitembelea kujionea Uwanja Gym ya mazoezi ya timu ya Azam Fc iliyopo kwenye Uwanja wa Azam Complex, unaomilikiwa na timu ya hiyo, leo Chamazi.
Mkurugenzi wa Makampuni ya SSB, Said Mohamed, (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa viongozi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi,  wakati walipokuwa wakitembelea kujionea Uwanja Gym ya mazoezi ya timu ya Azam Fc iliyopo kwenye Uwanja wa Azam Complex, unaomilikiwa na timu ya hiyo, leo Chamazi
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akijaribu kufanya zoezi katika moja ya mashine zilizo ndani ya Gym ya mazoezi ya timu ya Aazam Fc, kwenye Uwanja wa Chamazi Complex, wakati walipotembelea Gym hiyo leo. Picha na OMR

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI AZINDUA MSIKITI WA MASJIDIL HUDA CHAMAZI MBAGALA JIJINI DAR LEO.

Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, akikata utepe kuzindua rasmi Msikiti wa ‘Masjidil Huda’ uliojengwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Said Salim Bakhresa  katika eneo la Uwanja wa Chamazi, Mbagala jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti huyo wa Makampuni ya SSB, Said Salim Bakhresa, ambapo pia uzinduzi huo uliofanyika leo Julai 4, 2014, ulihudhuriwa na baadhi ya Viongozi wa Kiserikali akiwemo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na wengineo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokelewa na Mwenyeji wake Mwenyekiti wa Makampuni ya SSB, Said Salim Bakhresa, wakati alipowasili Msikiti wa ‘Masjidil Huda’ uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa msikiti huo uliofanyika leo Julai 4, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa tatu kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi (wa pili kushoto) Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana ( wa pili kuli) Mwenyekiti wa Makampuni ya SSB, Said Salim Bakhresa (katikati) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kushoto) wakijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mkititi wa ‘Masjidil Huda’ na Swala ya Ijumaa uliofanyika leo Julai 4, 2014, Chamaz jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na wenyeji wake wakati alipowasili Msikiti wa ‘Masjidil Huda’ uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa msikiti huo uliofanyika leo Julai 4, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati alipowasili Msikiti wa ‘Masjidil Huda’ uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa msikiti huo uliofanyika leo Julai 4, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na wenyeji wake wakati alipowasili Msikiti wa ‘Masjidil Huda’ uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa msikiti huo uliofanyika leo Julai 4, 2014. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa tatu kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi (wa pili kushoto) Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana ( wa pili kuli) Mwenyekiti wa Makampuni ya SSB, Said Salim Bakhresa (katikati) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kushoto) wakijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mkititi wa ‘Masjidil Huda’ na Swala ya Ijumaa uliofanyika leo Julai 4, 2014, Chamaz jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

Thursday, July 3, 2014

MCHOMVU NA B12 WAZICHAPA LIVE HEWANI,WAPIGWA RED CARD.

MCHOMVU.                                             B12.                                                DJ FETTY.

WATANGAZAJI wa kipindi Double XXL cha Radio Clouds fm 88.5 Dar, Adam Mchomvu, Dj Fetty na B12 ni ubishani wa 'KIUTANI' ulioanza hatimaye wakazichapa wakiwa LIVE On Air.

Linapokuja suala la 'Talk Talk za Mastori', Mchomvu dizaini ni kama ana utata utata siku zote uliojaa 'MASIHARA' lakini jana alim challenge 'SIRIAZ' Fetty kuhusu deal ya kurelease Compilation Album ambayo anaifukuzia. 

Wakati huo huo b12 akawachallenge kuwa wamechelewa sana coz yeye tayari ameshaiandaa China na soon inakuja, wakati huo huo Adam hakupenda hicho kitu, akasema ilikuwa ni AIDIA yake na ataitoa yeye ndipo Fetty na b12 wakamchana alishindwa kutoa Album tangu mwaka jana kipindi cha Fiesta hii ataiwezea wapi...!!!? Ndipo Adam akaja juu kwa jibu la Fetty (akiwa amepanik dizain) na kutaka kumchapa makofi Fetty.

B12 katikati akijaribu kurescue situation, ni.aibu coz yote yalikua on Air na b12 mara kwa mara alijaribu kuzima mic kabla ya ugomvi na wenzake wakazidi kumuona kuwa anabana na mbona ni suala la ufafanuzi kama mara zote wanavyofanya (UWAZI NA UKWELI) lakini haikuwa salama na ilikuwa sahihi. 

KILICHOFUATA:-
Kilichofuata ni sokomoko la ndondi hali iliyo sababisha hali ya studio kuchafuka huku baadhi ya vitendea kazi muhimu vikivunjwa na kusababisha kipindi kilichokuwa kikifuata cha jahazi kuanza kwakusuasua kikikosa baadhi ya viashiria kutokana na Kompyuta ya matirio muhimu kuvunjwa....

HEKA HEKA:-
Mara baada ya kusumbuliwa na SMS nyingi za wasikilizaji kuwa 'mara zote Clouds fm inazungumza habari za watu wengine leo tunataka hekaheka zenu' hivyo leo kupitia kipindi cha LEO TENA kinachoendeshwa na Da-Hu katika segment ya Hekaheka Geha Habibu amelazimika kuwatafuta kwa njia ya simu Ma-prizenta hao ambao inasemekana wamepigwa barua nzito huku wakitakiwa kuandika barua za kujieleza kwa uongozi. SIKILIZA KWA KUBOFYA PLAY.

KIKUNDI CHA RUGU CHANYAKUWA UBINGWA BALIMI NGOMA FESTIVAL 2014.

Baadhi ya wacheza ngoma wa kikundi cha Rugu kutoka Karagwe mkoani Kagera wakishangilia na kitita cha Shilingi 600,000/=mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Balimi Ngoma Mkoa wa Kagera yaliyofanyika katika Uwanja wa Kaitaba Bukoba mjini.
Baadhi ya washiriki na mashabiki wa Balimi Ngoma wakishuhudia fainali za mashindano ya Ngoma mkoa wa Kagera yaliyofanyika  katika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mjini.
Kikundi cha Ngoma cha Rugu- Karagwe chatwaa ubingwa wa Mkoa Balimi Ngoma Kagera.

FAINALI za mashindano ya Ngoma za Asili ngazi ya mikoa zijulikanazo kama “Balimi Ngoma Festival 2014” Mkoani Kagera kikundi cha Rugu chenye makazi yake Karagwe kimefanikiwa kuwa au bingwa wa Mkoa wa Kagera na kuzawadiwa fedha taslimu Shingi 600,00/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa wa Kagera katika fainali za Kanda zinazotarajiwa kufanyika Augusti 16,2014 Mkoani Mwanza.

Nafasi ya pili ya mashindano hayo ilichukuliwa na Kikundi cha Rugolo ile cha mjini Bukoba ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 500,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa katika fainali za Kanda.

Nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha Abagambakamo cha Muleba ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 400,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Alute Continue ambacho kilizawadiwa fedha taslimu shilingi 300,000/=.

Nafasi ya tano mpaka ya kumi ilichukuliwa na Uviti Ruzinga, Chupukizi, Kasharu, Kabete cha Ihangilo, Jipe Moyo na Upendo Musira hivi vilizawadiwa kifuta jasho cha 150,000/= kila kikundi. Jumla ya Vikundi 11 vilijitokeza kushiriki fainali hizo za Mkoa wa Kagera ngazi ya Mkoa kwa Mwaka 2014.

Akizungumza na kwa nyakati tofauti Meneja matukio wa Kanda yaZiwa, Erick Mwayela alisema Sababu msinigi ya kuwepo kwa Mashindano ya Balimi Ngoma za Asili ni kuenzi na kulinda utamaduni wa Kitanzania.

Mwayela aliongeza pia kuwa wao Kampuni ya Bia nchini ni sehemu yao ya kurudisha fadhila kwa watumiaji wa Kinywaji cha Balimi Extra Lager pamoja na vinywaji vyote vya Kampuni ya Bia Tanzania(TBL).

Fainali za Mkoa wa Kagera zilifanyika katika Uwanja wa Mkoa wa Kaitaba na fainali za Kanda za mashindano ya Balimi Ngoma zinatarajiwa kufanyika August 16,2014 jijini Mwanza kwa kushilikisha vikundi viwili viwili kutoka Tabora, Shinyanga, Bukoba,  Musoma na Wenyeji wa mashindano Mwanza.

KUTOKA UFARANSA HADI TZ AKIONYESHA BURUDANI YA ZIADA KATIKA SOKA.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Mohn's John Ntuli (kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kumtambulisha Mwanamichezo kutoka nchini Ufaransa Sean Garnier (katikati) ambaye yuko nchini Tanzania kwa ziara maalum ya kimichezo. Pembeni ni Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Mohan’s Vijay Joshi.
Mwanamichezo kutoka nchini Ufaransa Sean Garnier (katikati) ambaye yuko nchini Tanzania kwa ziara maalum ya kimichezo akifafanua machache mbele ya waandishi wa habari mara baada ya kutambulishwa. Pembeni yake kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni ya Mohn's John Ntuli, Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Mohan’s Vijay Joshi na Msimamizi wa shughuli hiyo Sam Odera.

 Mwanamichezo kutoka nchini Ufaransa Sean Garnier akionyesha jinsi ambavyo unaweza kupiga danadana huku ukiwa unacheza mziki staili mbali mbali.
Mwanamichezo kutoka nchini Ufaransa Sean Garnier akionyesha jinsi ambavyo unaweza kupiga danadana na kupita katika tundu dogo huku ukiendelea na mchezo. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Mwanamichezo kutoka nchini Ufaransa leo anatarajiwa kuonyesha shoo ya bure ambapo ataonesha umahiri wa kucheza mpira wa mitaani, sarakasi na kucheza dansi.

Mfaransa huyo Sean Garnier ambaye yuko nchini kwa ziara maalum ya kimichezo jana usiku alianza ziara hiyo kwa kuonesha umahiri wake wa kucheza mpira wa mtaani katika viwanja vya ufukwe wa Coco (Coco Beach) jijini Dar es Salaam.

Garnier ambaye anakipaji cha kupiga danadana mpira huku akiweka mapozi mbalimbali alionekana kuwa kivutio mbele ya mkutano na waandishi wa habari ambao walikuwepo kwenye mkutano huo huku akionesha umahiri wake wa kupiga danadana na kucheza na mpira katika barabara ya Alli Hassan Mwinyi baada ya mkutano huo.

Mwenyeji wa ziara ya Garnier, Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Mohan’s Vijay Joshi alisema kwamba huyu ni mwanamichezo mwenye kushikilia taji la kipaji cha kucheza ‘Free Style’ duniani.

“Ameletwa kwa udhamini wa ‘Redbull Street Sytle’ na atakuwa nchini kwa siku tano ambapo ni kati ya Julai 2 hadi Julai 7 ataondoka.

Aidha mbali ya kumudu kucheza na mpira pia nacheza sarakasi katika mitindo mbalimbali huku akiwataka watanzania kuiga baadhi ya michezo ambayo ataionyesha akiwa atakapokuwa mtaani.

Baadhi ya mitaa atakayo pita ni Kariakoo, Mlimani City, Posta, Viwanja vua Sabasaba, Chuo Cha Biashara (CBE) na Sea Clif Jijini Dar es Salaam.