Saturday, February 26, 2011
CHUNGUZA MJOMBA UTABAINI....!
Friday, February 25, 2011
WASHIRIKI 45 WA MISS UTALII HAWA HAPA.....

ANG'ATWA SIKIO NA MHUDUMU WA BAR KISA TOOTHPICKS!!

Mteja :: Utaniambia nini wewe si k..a tu!
Muhudumu :: Wewe Ms..e unasemaje?
Haikuchukuwa raundi kwa mhudumu kuimiliki shingo ya mteja kwa kumpiga roba (kabali), nyonga-nyonga, niga-niga....!!...!!
Mteja :: 'aaagh NIACHIE'
Mhudumu :: 'SIKUACHII'. Hamadi sikio hili hapa mhudumu akapata 'aNaZa aIdIa' akaling'ata akilisigina kwa meno hadi likakatika 'nkwachu' kisha akalitema ppTuU!!
KUFUATIA KASH-KASH ZINAZOMZONGA GADDAFI, SASA AMLAUMU OSAMA
Friday, February 25, 2011
No comments
Kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi amekiambia kituo cha televisheni cha taifa kuwa Osama Bin Laden na wafuasi wake, ndio wa kulaumiwa kwa maandamano yanayotikisa nchi yake.
Katika hutuba aliyotoa kupitia simu, mahsusi kwa ajili ya wakazi wa mji wa al-Zawiya, Kanali Gaddafi amesema vijana wanadanganywa kwa kupewa dawa za kulevya na pombe ili washiriki katika "uharibifu na hujuma".
Kanali Ghaddafi anajitahidi kurejesha udhibiti wa mji mkuu Tripoli na maeneo ya magharibi ile hali Waandamanaji nao wamekuwa wakipata nguvu katika miji ya mashariki.
Mmoja wa waandamanaji akichoma picha ya Gaddafi
Wanasiasa wa upinzani na viongozi wa kikabila wamefanya mkutano muhimu katika mji wa mashariki wa al-Badya, kuonesha umoja dhidi ya Kanali Gaddafi. Hotuba hiyo ililenga mji wa al-Zawiya uliopo kilomita 50 magharibi mwa mji mkuu, ambapo kumekuwa na ripoti za milio ya risasi mitaani.
Osama bin Laden
Kanali Ghaddafi amesema waandamanaji hawana madai yenye msingi, na walikuwa wakiongozwa na kiongozi wa al-Qaeda. "Bin Laden.... huyu ndio adui anayewadanganya watu. Msidanganywe na Bin Laden," amesema.
"Ni wazi kuwa sasa jambo hili linaongozwa na al-Qaeda. Vijana wenye silaha, watoto wetu, wanachochewa na watu ambao wanatafutwa na Marekani na nchi za Magharibi. "Wale wanaochochea ni wachache, na hatuna budi kuwakamata." Amesema vijana hao waandamanaji "wanafurahia kupiga risasi hasa wakiwa wamelewa".
Amesema Libya sio kama Misri na Tunisia, ambazo zimeshuhudia viongozi wao wakiondolewa madarakani, kwa sababu watu wa Libya wana uwezo wa kubadili maisha yao kwa kupitia kamati.
Kwa hisani ya bbc swahili.

Kanali Ghaddafi anajitahidi kurejesha udhibiti wa mji mkuu Tripoli na maeneo ya magharibi ile hali Waandamanaji nao wamekuwa wakipata nguvu katika miji ya mashariki.

Wanasiasa wa upinzani na viongozi wa kikabila wamefanya mkutano muhimu katika mji wa mashariki wa al-Badya, kuonesha umoja dhidi ya Kanali Gaddafi. Hotuba hiyo ililenga mji wa al-Zawiya uliopo kilomita 50 magharibi mwa mji mkuu, ambapo kumekuwa na ripoti za milio ya risasi mitaani.

Kanali Ghaddafi amesema waandamanaji hawana madai yenye msingi, na walikuwa wakiongozwa na kiongozi wa al-Qaeda. "Bin Laden.... huyu ndio adui anayewadanganya watu. Msidanganywe na Bin Laden," amesema.
"Ni wazi kuwa sasa jambo hili linaongozwa na al-Qaeda. Vijana wenye silaha, watoto wetu, wanachochewa na watu ambao wanatafutwa na Marekani na nchi za Magharibi. "Wale wanaochochea ni wachache, na hatuna budi kuwakamata." Amesema vijana hao waandamanaji "wanafurahia kupiga risasi hasa wakiwa wamelewa".
Amesema Libya sio kama Misri na Tunisia, ambazo zimeshuhudia viongozi wao wakiondolewa madarakani, kwa sababu watu wa Libya wana uwezo wa kubadili maisha yao kwa kupitia kamati.
Kwa hisani ya bbc swahili.
LIVERPOOL YASONGA MBELE ULAYA.
Goli la kichwa katika dakika za lala salama limeipeleka Liverpool katika ngazi ya timu 16 katika michuano ya Kombe la Europa dhidi ya Sparta Prague.
Bao hilo limefungwa na Dirk Kuyt katika dakika ya 86, kufuatia mpira wa kona uliopigwa na Raul Meireles. Katika mchezo wa mwanzo timu hizo mbili zilitoka sare. Huu ni Ushindi wa kwanza Ulaya kwa kocha Daglish.
Rangers nayo ya Scotland ilisonga mbele kwa goli la ugenini baada ya kutoka sare ya 3-3 na Sporting. Katika mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka sare ya 2-2 kwenye uwanja wa Rangers.

Rangers nayo ya Scotland ilisonga mbele kwa goli la ugenini baada ya kutoka sare ya 3-3 na Sporting. Katika mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka sare ya 2-2 kwenye uwanja wa Rangers.
Thursday, February 24, 2011
CHADEMA YAANGUSHA GHARIKA MWANZA SAUTI ZA WANYONGE ZARINDIMA...UUUuuuu!! MAANDAMANO YAMALIZIKA KWA AMANI TELE.
Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa pamoja na mawaziri wake vivuli, leo wameliteka Jiji la Mwanza na viunga vyake kwa kupata mapokezi makubwa.
@ MBOWE-"Tutawaunganisha watu wote wawe kitu kimoja tudai ukombozi wa pili wa kweli ulio halali kwa nchi hii"
Dr. SLAA
Maandamano yalianzia Kata ya Nyakato, Buzuruga na kupita barabara za Nyerere, Pamba, Kenyatta, Makongoro na hatimaye kuhitimishwa katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza kwa mkutano.
Mh. Sugu pale kati pembeni mwa diwani wa Mwaloni 'MBISHI'(sifa) Novat Manoko. Takribani wabunge 48 wanao wakilisha Chadema toka mikoa na wilaya mbalimbali hapa nchini wamehudhuria maandamano hayo na mkutano wake Mwanza.
Lengo la maandamano hayo ni kupinga serikali kulipa fidia kampuni ya Dowans, Kupanda kwa gharama za nishati na mfumuko wa bei ambao unapanda kila kukicha.
Nae mbunge wa Ilemela Higness Kiwia amewataka wananchi wa mkoa wa Mwanza kuondoa wasiwasi katika suala la ardhi kwani amekwishaongea na waziri wa ardhi na ameahidi kushughulikia tatizo hilo may mwaka huu.
Mbowe ambaye alionekana akizungumza kwa umakini mkubwa na kwa msisitizo, amesema yeye na timu yake wamekuja Mwanza kuwasha moto wa maandamano makubwa ya amani kwa muda wa siku tatu, leo katika wilaya za Nyamagana na Ilemela, kisha kuanzia kesho Ukerewe, Misungwi, Geita na Sengerema.
Aidha FREEMAN MBOWE amelipa shavu jeshi la polisi mkoa wa Mwanza kwa ushirikiano ulioonyeshwa kwa kusimamia mkutano huo na hatimaye kumalizika kwa amani.
Mbunge wa jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje amehoji kama mikoa ya kanda ya ziwa ndiyo inayoongoza kwa raslimali na utajiri mkubwa kwanini wananchi wake wapigike kimaisha, amewataka wananchi kuanza mapambano ya kuhakikisha wanauaga umasikini kwa kushirikiana na viongozi wa chama hicho.
Sanaa nayo haikuachwa nyuma kuhusishwa katika kunakshi sherehe.
Chadema imempa Kikwete siku tisa kutoa tamko kuhusu ufisadi, Dowans na hali ngumu ya Maisha.
CHADEMA wamesema kuwa Moto kama huu wataendelea kuuwasha katika mikoa ya Mara, Shinyanga, Mkoa mpya wa Simiyu na hatimaye Mkoa wa Kagera.
Mwisho wa siku wananchi haoooo...warejea makwao kwa amani na utulivu hakuna aliyeumia wala kupigwa kwenzi licha ya umati kufurika katika maandaamano na uwanjani Furahisha.
Maandamano yalianzia Kata ya Nyakato, Buzuruga na kupita barabara za Nyerere, Pamba, Kenyatta, Makongoro na hatimaye kuhitimishwa katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza kwa mkutano.
MAANDAMANO YA CHADEMA YANAYOENDELEA SASA JIJINI MWANZA NI NOMA..
YALIYONENWA NA MAGUFULI YAMEANZA KUTIMIA........
Wakati waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, akiendelea kusisitiza msimamo wake wa kuvunja majengo na kuondoa mabango yaliyo kwenye hifadhi ya barabara bila kulipa fidia, jijini Mwanza shughuli imeanza ....
Katika utekelezaji wa hilo, tayari mabango kadhaa jijini Mwanza yameanza kupigwa x ikiwa ni utekelezaji wa sheria iliyopo tangu mwaka 1938, kabla ya mabango.
Kwenye kikao cha Kamati ya Miundombinu kilichowashirikisha wadau wa usafirishaji mjini Dar es Salaam. Waziri alisikika akisema “Wakati nakabidhiwa wadhifa huu niliapa kusimamia sheria, nikaongeza na neno ‘Mungu nisaidie’ hivyo kulipa fidia watu waliovunja sheria ni kukiuka sheria ambayo ilikuwepo kabla yao. “Majengo yaliyojengwa kwenye hifadhi ya barabara yapo mengi, yakiwemo ya TANESCO na Wizara ya Maji, eneo la Ubungo. Yote yatavunjwa bila kulipwa fidia, ndiyo maana nikamwambia Meneja wa TANROADS mkoa wa Dar es Salaam aanze kubomoa ofisi zake ili asimamie vizuri kazi hiyo,”
Hata kama kuna kampuni inayotaka kuweka mabango, iingie mkataba na Mfuko wa Barabara na si vinginevyo ili fedha ziingie kwenye mfuko na zitumike kujenga barabara nyingine. Waziri Dk. Magufuli alisema halmashauri zinakusanya fedha na kwenda kuzitumia kulipana posho kwenye vikao vya madiwani, na si kujenga barabara kwa maendeleo ya wananchi.
Kwa mujibu wa Dk. Magufuli, kuyaacha mabango na majengo ndani ya hifadhi ya barabara ni kutowatendea haki Watanzania, ambao kodi zao zilitumika kutengeneza barabara kwa gharama kubwa.
Alisema endapo halmashauri zinataka kuingia mikataba ya kuweka mabango, zifanye hivyo katika barabara zinazozisimamia na si zinazosimamiwa na TANROADS.
Magufuli tayari ameziwekea ‘mgumu’ Halmashauri za Jiji na manispaa nchini akisema, “mabango yote yaliyomo kwenye barabara zetu tutayang’oa. Haiwezekani nyumba ajenge mwingine halafu aje mtu apangishe bila kukuarifu.”

Hata kama kuna kampuni inayotaka kuweka mabango, iingie mkataba na Mfuko wa Barabara na si vinginevyo ili fedha ziingie kwenye mfuko na zitumike kujenga barabara nyingine. Waziri Dk. Magufuli alisema halmashauri zinakusanya fedha na kwenda kuzitumia kulipana posho kwenye vikao vya madiwani, na si kujenga barabara kwa maendeleo ya wananchi.
Wednesday, February 23, 2011
DJ SUMMER DEE AZIKWA JIONI YA LEO JIJINI MWANZA.
Hatimaye Marehemu Issa Hassan Mohamed al-maarufu kama Dj Summer Dee amezikwa leo majira ya saa 10:30 katika makaburi ya Mlango Mmoja wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.
Mwili wa marehemu ukitoka msikitini mara baada ya ibada ya alasili..
Mwili wa marehemu ukishuka kaburini eneo la makaburi ya mlango mmoja..
Maswahiba wakiwa katika kutafakari eneo la makaburi kwenye mazishi ya Summer Dee Kutoka kushoto ni Mr Mdau Mwanza, Iddi Baka Pandisha na kwambali Ally Coco na Eddy Grand...
Sala ya mwisho mbele ya kaburi la marehemu Issa Hassan Mohamed (Summer Dee) leo katika makaburi ya mlango mmoja jijini Mwanza.
Wakiwa nyumbani kwa kaka wa marehemu, Hawa ni baadhi ya marafiki wakuu wa marehemu kutoka kushoto Dj George, Ommy, Dj Curter, Prince Baina Kamukulu, Jacob Usungu na Frank Pangani.
Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya marehemu.
Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya marehemu.
TAARIFA ZA MSIBA DJ SUMMER DEE AFARIKI DUNIA

Mazishi yatafanyika leo saa kumi jioni jijini Mwanza.
TUJIANDAE NA CHANGA LA MACHO JINGINE.......



Mpango mkakati wa kumnasa Al Adawi, ulipangwa na kufanikishwa kwa pamoja na duru huru za habari kutoka kwa raia wema ambao, awali walidokeza kuwa bosi huyo wa Dowans angefanya ziara kukagua mitambo ya kampuni hiyo mapema asubuhi. Swali ni kwamba nini kitafuata baada ya hili....
Habari kamili tembelea mwananchi.co.tz
Tuesday, February 22, 2011
CLOUDS TV UTAMU UNAENDELEA KUMWAGWA ......
Picha zote zimepigwa mbele ya screen ya luninga.
Subscribe to:
Posts (Atom)