Matokeo ya hiki ukionacho ni kutoka katika Tukio lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika bar moja maarufu kwa kuuza 'mdudu' jijini mwanza maeneo ya Kilimahewa iitwayo 'AR Pub', ambapo kaka mwenye sikio lake zimaaa!.. aling'atwa akiwa nje ya bar katika harakati za kutafuta usafiri wa pikipiki kuelekea anakokujua ikiwa ni mara baada ya kupata huduma ya chakula akipendacho ndani ya bar hiyo na kisha kulipa vizuri tu. Sheshe lilikuja mara baada ya wawili hao kuzama katika majibizano yaliyo jaa kejeli yaliyotokana na mteja huyo mwenye sikiong'atwa hapo juu kunyimwa kwa maksudi njiti hizo za kusafishia meno aka 'tuthi piki'.
Mteja :: Utaniambia nini wewe si k..a tu!
Muhudumu :: Wewe Ms..e unasemaje?
Haikuchukuwa raundi kwa mhudumu kuimiliki shingo ya mteja kwa kumpiga roba (kabali), nyonga-nyonga, niga-niga....!!...!!
Mteja :: 'aaagh NIACHIE'
Mhudumu :: 'SIKUACHII'. Hamadi sikio hili hapa mhudumu akapata 'aNaZa aIdIa' akaling'ata akilisigina kwa meno hadi likakatika 'nkwachu' kisha akalitema ppTuU!!
KOICA Yajenga Maabara ya Kisasa ya 3D ATC
-
Na Woinde Shizza, Arusha
Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya
Kimataifa la Korea (KOICA), kimezindua rasmi maabara...
Simba SC inafahamu la kufanya ili 'kupindua meza'
-
Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids amesema wachezaji na jopo la ufundi
wanafahamu fika wanachopaswa kukifanya katika mchezo wa marejeano wa
fainali ya Ko...
Duh! ni hatari kwenda kwenye hiyo bar kama mambo yanyewe ndo hivyo. Pole kwa kungátwa na sikio....
ReplyDeleteUkitaka kula nenda mgahawani, Bar kuna mengiii. Pole sana.
ReplyDelete