Saturday, December 25, 2010
BENKI YA FBME TAWI LA MWANZA YATOA ZAWADI YA X-MASS KWA KITUO CHA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU MWANZA.
Friday, December 24, 2010
POULSEN SAFARINI, KOCHA MSAIDIZI SLYVESTER MASH ATANGAZA KIKOSI KIPYA STARS KITAKACHO KIPIGA MICHUANO YA NILE.
KOCHA msaidizi wa timu ya taifa ya Tanzania (taifa stars) Silvester Marsh kwaniaba ya kocha mkuu wa timu hiyo Jan poulsen (aliye mapumzikoni kwao Norway) amekitaja kikosi cha wachezaji 23 wa timu hiyo kitakachoshiriki michuano ya kombe la Nile basin mashindano yanayotaraji kuanza kutimua vumbi rasmi tarehe 5 january 2011 nchini Misri.
Tofauti na wengi tulivyozoea, Tukio hilo limefanyika leo katika eneo la wazi la uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza ambapo kocha huyo msaidizi yuko ziarani kwa ajili ya shughuli maalum huku likishuhudiwa na Viongozi mbalimbali wa soka waandishi wa habari na wapenzi wa soka wa jiji la miamba.
KIKOSI KAMILI NI KAMA IFUATAVYO
GOALKEEPERS:-
1.JUMA KASEJA - SIMBA SC
2.SHAHBAN KADO -MTIBWA FC
3.SAID MOHAMED - MAJIMAJI SC
DEFENDERS:-
4.SHADRACK NSAJIGWA - YOUNG AFRICAN
5.MWASIKA STEPHANO - YOUNG AFRICAN
6.AGREY MORRIS - AZAM FC
7.KELVIN YONDANI - SIMBA SC
8.JUMA NYOSSO - SIMBA SC
9.NADIR HAROUB - YOUNG AFRICAN
MIDFIELDELS:-
10.IDRISSA RAJABU - SOFAPAKA
11.NURDIN BAKARI - YOUNG AFRICAN
12.SHAHBAN NDITI - MTIBWA FC
13.HANRY JOSEPH - NORWAY
14.JABIR AZIZ - AZAM
15.ABDI KASSIM - YOUNG AFRICAN
FOWARD PLAYERS
16.SALUM MACHAKU - MTIBWA FC
17.MRISHO NGASA - AZAM
18.NIZAR KHALFAN - CANADA
19.GODFREY TAITA - KAGERA SUGAR
20.ATHUMAN MACHUPPA - SWEDEN
21.JERRY TEGETE - YOUNG AFRICAN
22.SAID MAULID - ANGOLA
23.ALI AHMED SHIBOLI - SIMBA SC
Kocha huyo msaidizi amesema kuwa mazoezi ya Stars yataanza rasmi siku ya jumatatu ambapo kambi itakuwa uwanja wa karume jijini dar na tarehe 3jan 2011 wataanza safari kuelekea Misri. Tarehe 5jan2011 Stars kufungua na wenyeji. Wachezaji kama Erasto Nyoni, Mohamed Banka na Haruna Shamte hawajaachwa kutokana na viwango vyao kushuka bali ni kutokana na kuwa majeruhi. Kuhusu suala la kuwarejesha kikosini Machupa na Said Maulid Kocha Marsh amesema kuwa uamuzi huo umekuja kutokana na wachezaji hao kujaa uwezo kwa michezo ngazi za kimataifa.
Kocha Marsh Anauhakika na kikosi hicho alichokitaja kuwa cha ushindi akiwa na imani kubwa kuwa kila mchezaji atacheza kwa bidii na hatimaye kulipandisha soka la Tanzania katika viwango vya soka duniani.
KIKOSI KAMILI NI KAMA IFUATAVYO
GOALKEEPERS:-
1.JUMA KASEJA - SIMBA SC
2.SHAHBAN KADO -MTIBWA FC
3.SAID MOHAMED - MAJIMAJI SC
DEFENDERS:-
4.SHADRACK NSAJIGWA - YOUNG AFRICAN
5.MWASIKA STEPHANO - YOUNG AFRICAN
6.AGREY MORRIS - AZAM FC
7.KELVIN YONDANI - SIMBA SC
8.JUMA NYOSSO - SIMBA SC
9.NADIR HAROUB - YOUNG AFRICAN
MIDFIELDELS:-
10.IDRISSA RAJABU - SOFAPAKA
11.NURDIN BAKARI - YOUNG AFRICAN
12.SHAHBAN NDITI - MTIBWA FC
13.HANRY JOSEPH - NORWAY
14.JABIR AZIZ - AZAM
15.ABDI KASSIM - YOUNG AFRICAN
FOWARD PLAYERS
16.SALUM MACHAKU - MTIBWA FC
17.MRISHO NGASA - AZAM
18.NIZAR KHALFAN - CANADA
19.GODFREY TAITA - KAGERA SUGAR
20.ATHUMAN MACHUPPA - SWEDEN
21.JERRY TEGETE - YOUNG AFRICAN
22.SAID MAULID - ANGOLA
23.ALI AHMED SHIBOLI - SIMBA SC
Kocha huyo msaidizi amesema kuwa mazoezi ya Stars yataanza rasmi siku ya jumatatu ambapo kambi itakuwa uwanja wa karume jijini dar na tarehe 3jan 2011 wataanza safari kuelekea Misri. Tarehe 5jan2011 Stars kufungua na wenyeji. Wachezaji kama Erasto Nyoni, Mohamed Banka na Haruna Shamte hawajaachwa kutokana na viwango vyao kushuka bali ni kutokana na kuwa majeruhi. Kuhusu suala la kuwarejesha kikosini Machupa na Said Maulid Kocha Marsh amesema kuwa uamuzi huo umekuja kutokana na wachezaji hao kujaa uwezo kwa michezo ngazi za kimataifa.
Kocha Marsh Anauhakika na kikosi hicho alichokitaja kuwa cha ushindi akiwa na imani kubwa kuwa kila mchezaji atacheza kwa bidii na hatimaye kulipandisha soka la Tanzania katika viwango vya soka duniani.
TANZANIA TENA GIZANI.
TANESCO YATANGAZA MGAO WA UMEME NCHI NZIMA.
SHIRIKA la Umeme (Tanesco) juzi lilitangaza mgawo mpya na mkubwa wa nishati hiyo ambao utavifanya viwanda, maduka, ofisi na makazi kukosa umeme kwa kati ya masaa sita hadi 12 kwa muda wa mwezi mzima.Tangazo hilo la mgawo ambalo limekuja katika kipindi ambacho mjadala wa jenereta za kampuni ya Dowans ukiwa umeibuka tena, linatarajiwa kuongeza gharama za maisha kutokana na ukweli kuwa viwanda vingi vitalazimika kutumia jenereta katika uzalishaji licha ya Tanesco kutangaza kuwa vitapewa umeme nyakati za mchana. Tangazo la Tanesco limetolewa wakati kukiwa na ahadi kemkem za kumaliza kabisa tatizo la mgawo wa umeme, huku Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ikiwa imeliruhusu shirika hilo la umma kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 18.5. "Mgawo utahusisha mikoa yote iliyounganishwa kwenye gridi ya taifa isipokuwa mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Lindi na Mtwara." Kwa mujibu wa Badra Masoud, mgawo wa sasa umetokana na upungufu wa umeme uliojitokeza baada ya moja ya visima vinavyozalisha gesi vya kampuni ya Pan African Energy, kuzimwa. Alisema kisima hicho kinachotoa gesi kimezimwa kwa ajili ya kukifanyia matengenezo ya kawaida, hivyo kusababisha upungufu wa megawati 40 za umeme zinazokwenda katika gridi ya taifa. Pan African Energy ni kampuni ambayo inachimba gesi hiyo eneo la Songo Songo, Kilwa na baadaye husafishwa na kusafirishwa na kampuni ya Songas ambayo huzalisha umeme wa megawati 180 eneo la Ubungo na kuiuzia Tanesco. Kwa mujibu wa makubaliano, Songas hutakiwa kuzalisha umeme kwa kiwango kilicho kwenye mkataba na ni jukumu la Tanesco kuutumia umeme huo wa gesi kulingana na mahitaji yake au kutoutumia. Tanesco huilipa Songas hata pale inapokuwa haitumii umeme wa kampuni hiyo.Badra alisema kuwa kiwango hicho cha upungufu wa umeme kinaweza kuongezeka hadi kufikia megawati 120 jambo alilosema likitokea, shirikma hilo litazidisha mgawo.
Alieleza kuwa mgawo huo utaanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni katika baadhi ya maeneo huku maeneo yaliyopata umeme katika muda huo yakiukosa kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 5:00 usiku mara tatu kwa wiki. Kwa mujibu wa Badra, ratiba ya mgawo huo zitatangazwa katika magazeti na vyombo vingine vya habari. Hata hivyo, alisema baadhi ya maeneo hayatakumbwa na mgawo huo akitaja baadhi kuwa ni hospitali, pampu za maji, migodi na viwandani ambako alisema vitakosa umeme usiku ili mchana viendelee kuzalisha. Alisema kuwa maeneo yanayopata umeme kutoka transoma ya Kipawa hawatakumbwa na mgawo huo, kutokana na kukamilika kwa matengenezo yake. Akizungumzia siku kuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, Badra alisema Tanesco itajitahidi kuhakikisha wananchi wanasherehekea siku hizo bila kukosa umeme huku akiwaomba radhi kwa mgawo huo.
SHIRIKA la Umeme (Tanesco) juzi lilitangaza mgawo mpya na mkubwa wa nishati hiyo ambao utavifanya viwanda, maduka, ofisi na makazi kukosa umeme kwa kati ya masaa sita hadi 12 kwa muda wa mwezi mzima.Tangazo hilo la mgawo ambalo limekuja katika kipindi ambacho mjadala wa jenereta za kampuni ya Dowans ukiwa umeibuka tena, linatarajiwa kuongeza gharama za maisha kutokana na ukweli kuwa viwanda vingi vitalazimika kutumia jenereta katika uzalishaji licha ya Tanesco kutangaza kuwa vitapewa umeme nyakati za mchana. Tangazo la Tanesco limetolewa wakati kukiwa na ahadi kemkem za kumaliza kabisa tatizo la mgawo wa umeme, huku Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ikiwa imeliruhusu shirika hilo la umma kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 18.5. "Mgawo utahusisha mikoa yote iliyounganishwa kwenye gridi ya taifa isipokuwa mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Lindi na Mtwara." Kwa mujibu wa Badra Masoud, mgawo wa sasa umetokana na upungufu wa umeme uliojitokeza baada ya moja ya visima vinavyozalisha gesi vya kampuni ya Pan African Energy, kuzimwa. Alisema kisima hicho kinachotoa gesi kimezimwa kwa ajili ya kukifanyia matengenezo ya kawaida, hivyo kusababisha upungufu wa megawati 40 za umeme zinazokwenda katika gridi ya taifa. Pan African Energy ni kampuni ambayo inachimba gesi hiyo eneo la Songo Songo, Kilwa na baadaye husafishwa na kusafirishwa na kampuni ya Songas ambayo huzalisha umeme wa megawati 180 eneo la Ubungo na kuiuzia Tanesco. Kwa mujibu wa makubaliano, Songas hutakiwa kuzalisha umeme kwa kiwango kilicho kwenye mkataba na ni jukumu la Tanesco kuutumia umeme huo wa gesi kulingana na mahitaji yake au kutoutumia. Tanesco huilipa Songas hata pale inapokuwa haitumii umeme wa kampuni hiyo.Badra alisema kuwa kiwango hicho cha upungufu wa umeme kinaweza kuongezeka hadi kufikia megawati 120 jambo alilosema likitokea, shirikma hilo litazidisha mgawo.
Alieleza kuwa mgawo huo utaanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni katika baadhi ya maeneo huku maeneo yaliyopata umeme katika muda huo yakiukosa kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 5:00 usiku mara tatu kwa wiki. Kwa mujibu wa Badra, ratiba ya mgawo huo zitatangazwa katika magazeti na vyombo vingine vya habari. Hata hivyo, alisema baadhi ya maeneo hayatakumbwa na mgawo huo akitaja baadhi kuwa ni hospitali, pampu za maji, migodi na viwandani ambako alisema vitakosa umeme usiku ili mchana viendelee kuzalisha. Alisema kuwa maeneo yanayopata umeme kutoka transoma ya Kipawa hawatakumbwa na mgawo huo, kutokana na kukamilika kwa matengenezo yake. Akizungumzia siku kuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, Badra alisema Tanesco itajitahidi kuhakikisha wananchi wanasherehekea siku hizo bila kukosa umeme huku akiwaomba radhi kwa mgawo huo.
Thursday, December 23, 2010
"JEMA NI MALI KULIKO..........."
NIMEKUTANA NA BANGO HILI ASUBUHI YA LEO NIKAKUMBUKA MPANGO MWEMA UNAOENDELEA SASA WA CLOUDS FM JUU YA KUWAJALI WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU + X.MASS ZAWADI.
AT THE SAME TIME - NIKAMKUMBUKA NDUGU YANGU fadhilimshairi.blogspot.com
NA KATIKA MOJA YA MASHAIRI YAKE (TENDA WEMA) ALIANDIKA.
Kuna wengi walimwengu, kujaa dunia nzima,
Muumba ni yeye Mungu, kila moja na karama,
Wenye maisha machungu, huhitaji tendwa mema,
Tenda wema nenda zako.
Wale walio shidani, kamwe sije watupa,
Waondoe majonzini, usijaribu wakwepa,
Wafanye was'ende chini, maisha wakaogopa,
Tenda wema nenda zako.
Wale walio na njaa, usisite kuwalisha,
Waso nguo za kuvaa, ukapate kuwavisha,
Waliokata tamaa, imani kuwahuisha,
Tenda wema nenda zako.
NA KATIKA MOJA YA MASHAIRI YAKE (TENDA WEMA) ALIANDIKA.
Kuna wengi walimwengu, kujaa dunia nzima,
Muumba ni yeye Mungu, kila moja na karama,
Wenye maisha machungu, huhitaji tendwa mema,
Tenda wema nenda zako.
Wale walio shidani, kamwe sije watupa,
Waondoe majonzini, usijaribu wakwepa,
Wafanye was'ende chini, maisha wakaogopa,
Tenda wema nenda zako.
Wale walio na njaa, usisite kuwalisha,
Waso nguo za kuvaa, ukapate kuwavisha,
Waliokata tamaa, imani kuwahuisha,
Tenda wema nenda zako.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.
Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.
Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
22 Desemba, 2010
Wednesday, December 22, 2010
PILIKAPILIKA MAANDALIZI YA SIKUKUU ZA X MASS & MWAKA MPYA KWETU HOME 'ROCK CITY'
UTALII MWANZA NA TANAPA.

Zana hizi za ndani zilizotengenezwa kwa miti huku zikiwa namvuto wakipekee zinapatikana katika ofisi za Tanapa barabara ya kuelekea Hotel Tilapia na Yatch Club Mwanza.
Kukamilika kwa mchakato huo, kumeiwezesha hifadhi hii kuwa ya kipekee hapa nchini kwa kuvuta idadi kubwa ya watalii wa ndani ambao hadi sasa wanazidi wale wa nje kwa asilimia 90, kwani kila siku hasa za jumapili wabongo wamekuwa wakidondoka katika eneo husika.
MORE PIX.....
Tuesday, December 21, 2010
SAFARI YA MWISHO YA AFISA AFYA WA JIJI LA MWANZA PASTORY SHILEWA.
Tarehe 14 mwezi Dec 2010 hakika ilikuwa siku ya huzuni si tu kwa familia ya Shilewa bali hata jiji la Mwanza kwa ujumla, Huzuni ilikuja mara baada ya kuondokewa na Afisa afya wake Pastory Shilewa al-maarufu kwa jina la 'MR. CHAKULA' aliyefariki dunia kwa maradhi ya figo yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.
MAREHEMU PASTORY SHILEWA.
Ni jamaa aliyehusika na kushiriki kikamilifu kuhakikisha jiji la mwanza linakuwa na utamaduni wa usafi kaya kwa kaya, mtaa kwa mtaa, kitongoji kwa kitongoji hali iliyopelekea jiji kutunukiwa mfululizo TUZO mbalimbali za usafi kitaifa na kwa Afrika Mashariki.
Mama wa Shilewa akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Pastory ambaye ndiye alikuwa mtoto wake wa kwanza.
Mke wa marehemu Teopista William Dodoma akiweka shada la maua kwenye kaburi la mumewe.
Dada wa marehemu Pastory Shilewa wakiweka shada la maua katika kukamilisha mazishi yaliyofanyika kijiji cha mtakuja Wilayani Sengerema, ijumaa ya tarehe 17.december.2010
Wawakilishi kutoka ofisi ya jiji aliyokuwa akifanya kazi marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Pastory Shilewa.
Katika picha ya pamoja, kutoka kushoto ni Monika Shilewa (dada wa marehemu), Grace Shilewa (dada wa marehemu), Mama Shilewa na ndugu wengine.
Wakifarijiana kwa kuondokewa na kipenzi chao, pichani kutoka kulia ni Mama Shilewa (mama wa marehemu), kwa ukaribu na Teopista William Dodoma ambaye ni mke wa marehemu na mwisho ni dada yake mke wa marehemu.
Baadhi ya watoto wa marehemu katika picha ya kumbukumbu pamoja na shangazi yao Monica (wa 3kulia). Marehemu Pastory alizaliwa mnamo tarehe 5 agust 1961 ameacha watoto 8 na mjane.
Ni jamaa aliyehusika na kushiriki kikamilifu kuhakikisha jiji la mwanza linakuwa na utamaduni wa usafi kaya kwa kaya, mtaa kwa mtaa, kitongoji kwa kitongoji hali iliyopelekea jiji kutunukiwa mfululizo TUZO mbalimbali za usafi kitaifa na kwa Afrika Mashariki.
Monday, December 20, 2010
HAPA NA KULEee!...! 'PEPESA MACHO NDUGU'
HAFLA YA MAKABIDHIANO YA MAJUKUMU KUTOKA BARAZA LA HABARI TANZANIA KWENDA UTPC, YAFANYIKA LEO NYUMBANI HOTEL MWANZA.
Umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC) leo umekabidhiwa rasmi majukumu ya kuendesha mradi wa klabu za Waandishi wa habari ambao awali ulikuwa ukiendeshwa na baraza la Habari Tanzania (MCT).
KULIA NI RAIS WA UTPC KENNETH SIMBAYA AKIPOKEA VITENDEA KAZI TOKA KWA KATIBU MTENDAJI WA MCT BW. KAJUBI MUKANGA.
Makabidhiano hayo ambayo yamefanyika leo katika ukumbi wa Nyumbani Hotel mjini Mwanza yalianza kwa maelezo mafupi kutoka kwa meneja mpango wa baraza la Habari Tanzania Bi. Pili Mtambalike ambaye aligusia matatizo yaliyochangia kukwamisha harakati kadhaa za maendeleo ya chama kwa kipindi kilichopita.
PILI MTAMBALIKE MENEJA PROGRAM WA MCT.
Meneja huyo ameyataja matatizo hayo kuwa ni tatizo la fedha kwa wanachama kutolipa ada kwa muda muafaka, waandishi kukosa weledi wa majukumu yao na migongano ya kiuongozi kati ya waandishi na waandishi.
RAIS WA UTPC KENNETH SIMBAYA AKIONESHA NYENZO ALIZO KABIDHIWA.
Rais wa Umoja wa klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC) Bwana. Keneth Simbaya amesema kuwa jukumu kubwa walilonalo wanachama ni kujenga umoja endelevu kwa waandishi wa habari nchini kwa kila wanachama kufanya kazi kwa ufanisi na kiwango cha hali ya juu hivyo kuleta taswira ambayo jamii inahitaji kufikia kimaendeleo
Naye katibu mtendaji wa MCT Kajubi Mukajanga ameyataja mambo yanayodhamiriwa kufanyika ndani ya mpango huo wa makabidhiano kuwa ni kuweka misingi ya kidemokrasia katk utawala, kuweka mifumo ya menejimenti ya bodi, vilevile kuweka kanuni za utendaji wa bodi ili kutoa fursa kwa kila mwanachama aweze kutenda kazi kwa mujibu wa kanuni.
WANACHAMA WA UTPC MKUTANONI.Kulia ni mwenyekiti chama cha waandishi wa habari mkoa wa Ruvuma bw. Juma Nyumayo ambaye vilevile ni Mwenyekiti wa kamati ya maadili UTPC akiwa bize' mkutanoni.
KUTOKA KUSHOTO WALIOKETI NI;John Nguya (meneja wa fedha MCT), Zilipa Joseph (makamu wa rais), Pili Mtambalike (meneja programu), kajubi Mukanga (katibu mtendaji MCT), Kenneth Simbaya (rais UTPC)na Jackob Kambili (kaimu mkurugenzi mtendaji wa UTPC-MWANZA). Waliosimama ni bodi ya UTPC.
Katika miaka sita ya uongozi wake kwa waandishi, Baraza la habari Tanzania (MCT) linajivunia kuwa na uwakilishi wa vyama vya waandishi wa habari kwa kila mkoa nchini, vyama vyenye kuweza kuweza kujiendesha vyenyewe na hatimaye leo Baraza hilo linakabidhi mradi kwa klabu za waandishi wenyewe.
Makabidhiano hayo ambayo yamefanyika leo katika ukumbi wa Nyumbani Hotel mjini Mwanza yalianza kwa maelezo mafupi kutoka kwa meneja mpango wa baraza la Habari Tanzania Bi. Pili Mtambalike ambaye aligusia matatizo yaliyochangia kukwamisha harakati kadhaa za maendeleo ya chama kwa kipindi kilichopita.
Meneja huyo ameyataja matatizo hayo kuwa ni tatizo la fedha kwa wanachama kutolipa ada kwa muda muafaka, waandishi kukosa weledi wa majukumu yao na migongano ya kiuongozi kati ya waandishi na waandishi.
Rais wa Umoja wa klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC) Bwana. Keneth Simbaya amesema kuwa jukumu kubwa walilonalo wanachama ni kujenga umoja endelevu kwa waandishi wa habari nchini kwa kila wanachama kufanya kazi kwa ufanisi na kiwango cha hali ya juu hivyo kuleta taswira ambayo jamii inahitaji kufikia kimaendeleo
Subscribe to:
Posts (Atom)