ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 21, 2010

SAFARI YA MWISHO YA AFISA AFYA WA JIJI LA MWANZA PASTORY SHILEWA.

Tarehe 14 mwezi Dec 2010 hakika ilikuwa siku ya huzuni si tu kwa familia ya Shilewa bali hata jiji la Mwanza kwa ujumla, Huzuni ilikuja mara baada ya kuondokewa na Afisa afya wake Pastory Shilewa al-maarufu kwa jina la 'MR. CHAKULA' aliyefariki dunia kwa maradhi ya figo yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.MAREHEMU PASTORY SHILEWA.
Ni jamaa aliyehusika na kushiriki kikamilifu kuhakikisha jiji la mwanza linakuwa na utamaduni wa usafi kaya kwa kaya, mtaa kwa mtaa, kitongoji kwa kitongoji hali iliyopelekea jiji kutunukiwa mfululizo TUZO mbalimbali za usafi kitaifa na kwa Afrika Mashariki.

Mama wa Shilewa akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Pastory ambaye ndiye alikuwa mtoto wake wa kwanza.

Mke wa marehemu Teopista William Dodoma akiweka shada la maua kwenye kaburi la mumewe.

Dada wa marehemu Pastory Shilewa wakiweka shada la maua katika kukamilisha mazishi yaliyofanyika kijiji cha mtakuja Wilayani Sengerema, ijumaa ya tarehe 17.december.2010

Wawakilishi kutoka ofisi ya jiji aliyokuwa akifanya kazi marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Pastory Shilewa.

Katika picha ya pamoja, kutoka kushoto ni Monika Shilewa (dada wa marehemu), Grace Shilewa (dada wa marehemu), Mama Shilewa na ndugu wengine.

Wakifarijiana kwa kuondokewa na kipenzi chao, pichani kutoka kulia ni Mama Shilewa (mama wa marehemu), kwa ukaribu na Teopista William Dodoma ambaye ni mke wa marehemu na mwisho ni dada yake mke wa marehemu.

Baadhi ya watoto wa marehemu katika picha ya kumbukumbu pamoja na shangazi yao Monica (wa 3kulia). Marehemu Pastory alizaliwa mnamo tarehe 5 agust 1961 ameacha watoto 8 na mjane.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.