ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 19, 2013

YANGA 3 BLACK LEOPARDS YA AFRIKA KUSINI 2.


5
Mchezaji wa timu ya Yanga Kabange Twite akimiliki mpira mbele ya Nkosiabo  Xakane mchezaji wa Black Leopards ya Afrika Kusini  .katika mchezo wa kirafiki uliokutanisha timu hizo kwenye uwanja wa Taifa jioni hii, timu ya Yanga imeshinda magoli 3-2 dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.
Goli la Yanga limefungwa na mchezaji Jerrison Tegete kwa penati katika kipindi cha kwanza baada ya Mchezaji Haruna Niyonzima kuangushwa katika eneo la hatari na mchezaji wa timu ya Black Leopards na kuongeza goli la tatu katika kipindi cha pili , Huku mchezaji Didier Kavumbagu akapachika goli la pili katika kipindi katika kipindi hichohicho cha pili cha mchezo.
Timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini imefanikiwa kupata magoli mawili katika kipindi cha pili na kufanya matokeo kuwa Yanga 3 na timu ya Black Leopards 2 mpaka mwisho wa mchezao huo.
7
Wachrezaji wa timu ya Yanga wakishangilia mara baada ya kufunga goli la kwanza katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.
1
Mashabiki wa Yanga wakishangilia wakati timu yao ikicheza kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.


2Kikosi cha timu ya Yanga kikiwa katika picha ya pamoja.
3Kikosi cha timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini kikiwa katika picha ya pamoja.
PICHA/HABARI NA FULL SHANGWE BLOG

BONDIA RAMADHANI SHAURI KUZIPIGA KESHO


Mratibu wa pambano akiwanyanyua juu mikono ya bondia Ramadhani shauri (R) na Said Njechele (L) kuonesha wapo tayari kwa kupambana hiyoo kesho.
Bondia wa ngumi za kulipwa na bingwa wa IBF  INTERCONTINETAL Ramadhani shauri anategemea kupanda ulingoni kesho kuzipiga na Said njechele wa iringa katika pambano la kirafiki la raundi nane katika ukumbi wa  D.I.D Hall uliopo mabibo mwasho.
Mratibu  wa pambano hilo Charles Christopher mzazi  ameeleza kuwa maaandalizi ya pambano yapo kamili na mabondia wote wapo katika hali nzuri ya ushindani  na wamepima wapo sawa kabisa kwa kuzipiga. Ambapo pia kutakuwepo na mapambano mengi ya utangulizi na mabondia watakaosindikiza  pia wamepima chini ya usimamizi wa katibu mkuu wa TPBO bw Ibrahim kamwe na docta john wapo sawa kwa kupambana.
Mabondia watakaocheza utangulizi ni kama ifuatavyo HAMIS MOHAMED na  HARUNA MNYALUKOLO, PENDEZA SHOMARI atazipiga na MARTIN RICHARD, MBARUKU NASORO na KARIMU RESPECT, DOTO MUSTAFA atakabiliana na SHOMARI MIURUNDI, huku ISSA OMAR akizipiga na  JUMA J KASHNDE.
Katibu mkuu wa ngumi za kulipwa nchini Ibrahim Kamwe  ama bigright amethibisha kuwa kanuni na taratibu za ngumi za kulipwa zimefuatwa  na mabondia wapo katika hali nzuri ya kupigana hiyo siku ya jumapili katika ukumbi wa DID HALL mabibo mwisho kati ya bingwa wa IBF INTERCONTINENTAL RAMADHANI SHAURI na  SAID  NJECHELE

SIKILIZA GUMZO LA JAHAZI: KUHUSU RAIA WA CHINA ALIYETAKA KUMHONGA MKUU WA WILAYA

HABARI ILIYOKUWA GUMZO 
JANA KATIKA JAHAZI.
Mahakama ya wilayani Bunda mkoani Mara mnamo tarehe 17 jan 2013 ilimuhukumu kwenda jela miaka 3 raia wa china Mark Wang Wei (30) baada ya kukiri kosa la kutaka kutoa rushwa ya shilingi laki 5 kwa Mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe.
Watangazaji wa kipindi cha Jahazi 
ndani ya Clouds Fm Ephrahim Kibonde (L) 
na Wasiwasi Mwabulambo (R)
bOFYA kusikiliza...

Mwanasheria wa Taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa (TAKUKURU) Mwema Mella aliiambia mahakama kuwa Wei alitenda kosa hilo jan 16 mwaka huu saa saba mchana katika ofisi ya mkuu huyo wa wilaya.

Mella alisema mshatakiwa ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Panda Internatinal Company LTD ya mjini Shinyanga, inayojihusisha na usambazaji wa pembejeo za kilimo, aliamua kufanya hivyo ili kumshawishi mkuu huyo wa ili ampitishe katika zabuni ya usambazaji wa pembejeo aliyokuwa ameiomba wilayani humo.

Alisema hata hivyo baada ya kubaini kuwepo kwa mazingira ya rusha katika mazungumzo kati yake na wei, Mirumbe aliamua kuwaita maofisa wa TAKUKURU waliofika mara moja na kuweka mtego uliofanikisha kumnasa mzabuni huyo na kufikishwa mahakamani.

Katika kujitetea kwake Wei aliyekuwa akitumia lugha ya kiingereza kwa taabu kwa kuwa haijui vizuri na mahakama haina mkalimani wa lugha ya kichina alisema hakujua kuwa kufanya hivyo kwa umpendaye ni makosa hapa nchini.

Alisema hilo ni tofauti na kwao ambako wanaliona tendo hilo kama la kawaida na kuiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu.

Hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama hiyo Safina Semfukwe aliyeonekana kuguswa na maneno ya Wei, alisema kisheria kutokujua sheria hakumuondoi mtu yeyote hatiani hivyo alimhukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi laki 7.

Hata hivyo wei alilipa faini hiyo hivyo kujiepusha na kifungo hicho.

PALE VIJANA WAWILI WALIO VIONGOZI KAMBI TOFAUTI WANAPOTOA SOMO LA KUELEWEKA KWA WANANCHI

MEYA wa Jiji la Mwanza(Nyamagana) Bw.Stanislaus Mabula ambaye ni diwani wa kata ya Mkolani (CCM) amewataka Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata kushirikiana na Madiwani wao katika kupanga mikakati ya maendeleo na kuitekeleza kwa vitendo huku wakiwahamasisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo inayotoa huduma za kijamii badala ya kukalia malumbano yasiyokuwa na tija kwa wananchi kutokana na kuendeleza itikadi zao za vyama vya kisiasa zilizopo.

Wananchi wa Kata ya Igoma kusanyikoni.

Bw.Mabula alisema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Igoma wakati alipofanya mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya soko la wazi kwa lengo la kupatiwa taarifa za maendeleo za Kata hiyo pamoja na kukagua miradi ya kijamii iliyopo kwenye Kata hiyo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji, serikali kuu na wananchi kuchangia alisema kwamba wananchi wanao wawakilishi kuanzia ngazi ya Mitaa na Kata ili kero zao zitafutiwe ufumbuzi kwa kuwashirikisha wataalamu.
“Ni vyema wenyeviti, madiwani, watendaji na wataalamu kuwapatia taarifa za vikao vya WDC juu ya uamuzi wao na kuwaeleza wananchi jinsi ufumbuzi wa kero zinazowasumbua kwenye maeneo yao zilivyowasilishwa kwa Diwani ili kuhakikisha zinafikishwa kwenye Kamati za kudumu na Baraza la Madiwani kuzitafutia ufumbuzi wa haraka ikiwemo kuwaelekeza wataalamu kuzishughulikia kulingana na ilivyoamuliwa na kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza”alisema
Jeshi la Polisi wilaya ya Nyamagana nao walipata nafasi fupi ya kutoa somo kwa wananchi juu ya utii wa sheria, kujikinga, kukabiliana na uhalifu, jinsi ya kushughulikia kesi ndogondogo za majirani na jinsi ya kuzuia machafuko mitaani na majumbani. 
Awali diwani wa kata hiyo ya Igoma, Mhe. Adam Chagulani aliwataka wenyeviti kupeleka kwenye kikao cha WDC kero ambazo zimekuwa zikikwamisha utekelezwaji wa miradi ya maendeleo na ukwamishaji wa kukamilika kwake kwa kuweka kado ubinasifi na itikadi za vyama vya siasa wanavyotoka bali kwa kuzingatia masilahi ya wananchi waliowachagua kuwepo kwenye nafasi hizo.

Mkutano ulipomalizika Meya wa Jiji la Mwanza(Nyamagana) Bw.Stanislaus Mabula akibebwa na wananchi wa kata ya Igoma wakimuunga mkono kwa kuwa ni kijana mwenzao sambamba na kuonyesha ukomavu wa siasa.

Bw.Stanislaus Mabula alibebwa hadi eneo la biashara ndogondogo za akinamama sokoni hapo ambapo alifanya maongezi ya mtu mmoja mmoja kisha akaondoka eneo la kusanyiko

Friday, January 18, 2013

UFUNGUZI WA VISIMA 30 KATIKA MAENEO YA WILAYA 6 KAME TANZANIA VILIVYOCHIMBWA KWA MSAADA WA SERIKALI YA MISRI WAFANYIKA WILAYANI MASWA.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Profesa Jumanne Maghembe (katikati) akishirikiana na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Serikali ya Misri Prof. Dr. Mohamed Bahaa El-Din Ahmed (kulia) kukata utepe kuashiria ufunguzi wa visima 30 katika maeneo ya wilaya sita kame, Tanzania vilivyochimbwa kwa msaada wa serikali ya Misri uliofanyika jana katika kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu. Kushoto kabisa ni Mhe. Pascal Mabiti ambaye ni mkuu wa mkoa wa Simiyu.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Serikali ya Misri Prof. Dr. Mohamed Bahaa El-Din Ahmed akionja ladha ya maji toka kwenye bomba kuu la chanzo cha maji yanayoelekezwa kwenye bomba la utekaji maji kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu ikiwa ni moja kati ya hatua za serikali ya Tanzania kusaidia wananchi wake kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa maji salama.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Serikali ya Tanzania Jumanne Maghembe naye akionja ladha ya maji toka kwenye bomba kuu la chanzo cha maji yanayoelekezwa kwenye bomba la utekaji maji kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu ikiwa ni moja kati ya hatua za serikali ya Tanzania kusaidia wananchi wake kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa maji salama.

Mbunge wa jimbo la Busega mkoani Simiyu  Titus Kamani naye akionja ladha ya maji toka kwenye bomba kuu la chanzo cha maji yanayoelekezwa kwenye bomba la utekaji maji kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu ikiwa ni moja kati ya hatua za serikali ya Tanzania kusaidia wananchi wake kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa maji salama.

Mama Maria akiondoka kwenye eneo la bomba kuu la kutekea maji mara baada ya kutwishwa ndoo na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Serikali ya Misri Prof. Dr. Mohamed Bahaa El-Din Ahmed huku wananchi wengine wakipiga makofi kuashiria kufurahia tukio hilo lililofanyika katika kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu. .

Jiwe la Msingi.

Ni burudani ya ngoma ya kabila la wasukuma na wala si mchezo wa vita.

Meza kuu ikifurahia yanayojiri ya kiburudani katika kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu kwenye ufunguzi wa visima 30 katika maeneo ya wilaya sita kame, Tanzania vilivyochimbwa kwa msaada wa serikali ya Misri .

 Kwa upande wake waziri wa Maji na Umwagiliaji Nchini Prof. Jumanne Magembe amesema kuwa Serikali imejipanga vyema kuhakikisha inapunguza kama si kuondoa kabisa tatizo la uhaba wa maji nchini Tanzania.
Bofya Play usikilize ..

Takwimu za upatikanaji wa maji katika Wilaya zilizochaguliwa kwenye mradi huo hadi mwezi Disemba 2011 katika wilaya zilizomo kwenye miradi zinaonyesha kuwa na hali ni ya mvua zisizoridhisha, hivyo kipaumbele katika mradi huu ni kusaidia kwanza maeneo yaliyo upande wa mvua kidogo ambapo matarajio ya serikali kwa miradi yote ikikamilika hali ya upatikanaji wa maji katika vijiji vyote itakuwa bora, suala ambalo linawezekana.

Nae Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Serikali ya Misri Prof. Dr. Mohamed Bahaa El-Din Ahmed amesema kuwa serikali yake inajivunia msaada iliyoutoa wa kiasi cha fedha Dola milioni moja za Kimarekani kusaidia kukamilika kwa miradi ya maji nchini Tanzania kwani Misri inaamini kuwa hiyo ni moja kati ya njia ya kudumisha na kuendeleza ushirikiano uliopo.  


Msaada huo wa Misri si suala geni hapa nchini kwani tangu enzi za hayati Baba wa Taifa Mwl. Nyerere, Tanzania na Misri zimekuwa zikishirikiana katika Nyanja za siasa, maji, kilimo cha umwagiliaji, na Tanzania imekuwa ikipokea madaktari wakujitolea ambao wamekuwa wakifanya kazi kwenye hospitali za mikoa na kila mwaka Tanzania imekuwa ikipeleka wataalamu wake nchini Misri kupata mafunzo kujinoa katika taaluma hiyo.

Wananchi wa kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu wakisikiliza hotuba za viongozi kwenye ufunguzi wa visima 30 katika maeneo ya wilaya sita kame, Tanzania vilivyochimbwa kwa msaada wa serikali ya Misri 
Pamoja na mradi huu, huduma ya maji imeendelea kuboreshwa kote nchini kupitia Program ya maendeleo ya Sekta ya Maji ambayo ilianza kutekelezwa tangu mwaka 2006, kwa kushirikisha juhudi za wananchi wenyewe na washirika wengine wa maendeleo. Miradi inayoendelea kutekelezwa kwa fedha za programu wilayani Maswa ni ; Miradi ya maji ya bomba ya vijiji vya Sayusayu, malampaka na Mwasayi; Miradi mipya inayokaribia kuanza kutekelezwa ni ya vijiji vya Njiapanda na Jija.

Lengo la Programu ya Maji ni kuwa kufikia mwaka 2015,huduma ya maji vijijini iwe wastani wa asilimia 65.
Wananchi wa kijiji cha Mwanang'ombe wilayani Maswa mkoani Simiyu wakisikiliza hotuba za viongozi kwenye ufunguzi wa visima 30 katika maeneo ya wilaya sita kame, Tanzania vilivyochimbwa kwa msaada wa serikali ya Misri 

Wito umetolewa kwa wananchi wa kijiji hicho na maeneo yote ya miradi nchini kuwa walinzi wa miundombinu ya maji. kutokomeza tatizo la miundombinu ya maji na vifaa vya maji kuhujumiwa na watu wabaya ambao huing'oa na kuuza kama chuma chakavu hivyo kila mwananchi awe mlinzi wa miundombinu hiyo kwa faida ya taifa na kwa kuzingatia maslahi ya walio wengi (kuwaepusha mama zetu na adha ya kusafiri umbali mrefu kusaka maji salama).

WAWEKEZAJI SERENGETI BALLON WAWANYASWA WATANZANIA

 Na Shomari Binda
          Serengeti,


WAFANYAKAZI Watanzania wa Kampuni ya Serengeti Balloon Safaris inayofanya shughuli za Kitalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wamelalamikia Uongozi wa Kampuni hiyo kwa kuwafanyisha kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila kuwapa mikataba inayotambulika Kisheria licha ya kufatilia suala hilo katika ngazi zinazohusika.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari Mjini Mugumu,Wafanyakazi hao  walisema wanashangaa kuona Wawekezaji wa Kampuni hiyo kutoka Nchini Uingereza ambayo Meneja anayesimamia shughuli zao ni mzawa kushindwa kuwatimizia masharti ya kazi huku wakiwatolea lugha zisizo za kiungwana wanapofatilia mikataba yao.

Walisema licha ya kufatilia kwa muda mrefu suala la kutengenezewa mikataba ya Kisheria kwa Meneja wa Kampuni hiyo waliyemtaja kwa jina la Maria Straus licha ya kuwa ni Mtanzania mwenzao ameshindwa kuwasaidia na kila anapoitwa katika vikao vya kulizumzia suala la mikataba amekuwa akishindwa kufika bila kutoa sababu zozote.

"Tunashangaa kuoa Mtanzania mwenzetu kushindwa kua karibu na suala hili huku akijua ni muda mrefu tunafanya kazi bila kuwa na mikataba ya Kisheria ambayo itaweza kutulinda katika shughuli hizi za Utalii ambazo tunazifanya katika mazingira ambayo pia ni hatari kwa maisha yetu. 

"Kabla ya kuja hapa kwenye Kampuni ya Balloon alikuwa ni Meneja wa Kampuni nyingine ya Utalii ya Abercombie and Kent (A & K) nako amekuwa na matatizo kama haya ya kutokuwathamini Watanzania wenzake na kupelekea kufutwa kazi baada ya kukataliwa na Wafanyakazi,walisema wafanyakazi hao.

Walidai kuwa wamepanga kufanya mgomo ndani ya mwezi huu wa kutofanya kazi kwa muda usiojulikana katika vituo vyote vya Seronera,Ndutu,Kirawira na Sasakwa kitu ambacho kitakuwa ni aibu kwa Taifa na wageni wanaofanya Utalii wa Balloon kutokana na Mtalii mmoja kutoa Dolla 499 kwa safari moja.

Madai ya Wafanyakazi hao licha ya kutaka mikataba ya Kisheria pia wanalalamikia nyongeza ya mishahara kutokana na mishahara inayotolewa na kampuni kutokukidhi mahitaji kutokana na kutolewa mshahara wa shilingi laki moja na themanini 180,000 kwa kima cha chini kiwango ambacho walidai ni kidogo kuliko ya kile walichokuwa wakilipwa mwanzoni.

Wafanyakazi hao walidai kuwa baada ya kuona Meneja wao anashindwa kulifatilia suala lao waliamua kulifikisha katika Ofisi za Chama cha Wafanyakazi wa Mahotelini (CHODAWU) Mkoa wa Mara tangu mwezi wa 8 mwaka jana kwa ajili ya ufatiliaji zaidi na kuamua kuwabana wawekezaji na kuwataka kuandaa mikataba ya Kisheria.

"Tumefika (CHODAWU) na wao walikaa na Wawekezaji kupitia Mwanasheria wao katika kuandaa mikataba na tulipoletewa tuliona bado inamapungufu kutokana na vipengele mbalimbali na kushindwa kuijaza na wao tumesikia wamepeleka CHODAWU tena kwa kweli suala hili bado linatusumbua kutokana na kulifatilia kwa muda mrefu,"walisema.

Akizungumzia suala hilo Katibu wa (CHODAWU) Mkoa wa Mara Daudi Mapuga alidai kulipokea suala hilo katika Ofisi yake na wanalishughulikia ili yale yanayodaiwa na Wafanyakazi hao yaweze kushughulikiwa kwa mujibu wa kanuni za kazi na mikataba ya Kisheria inavyoeleza.

"Ni kweli nimepokea suala la wafanyakazi wa Serengeti Ballon Safaris wakitaka mikataba ya Kisheria kutoka kwa waajili,tumekaa na waajili pamoja na Mwanasheria wao na tumekubaliana vipengele mbalimbali naamini baaadaya kuvikamilisha tutaenda kukutana na Wafanyakazi kwa ajili ya kuisaini kwa mujibu wa Sheria,"alisema Mapuga.

Akizungumzia suala la Wafanyakazi hao,Mbunge wa Jimbo la Serengeti Stiven Kebwe alisema hakuna Sheria yoyote inayotaka Wawekezaji kuwanyanyasa Watanzania katika shughuli yoyote na kuwataka waajili wa Baloon kuhakikisha wanalifanyia kazi suala la kuandaa mikataba sahihi ya Kisheria ambayo inakidhi mahitaji na hali halisi.

Kebwe alisema Sheria ya mikataba lazima izingatiwe na mamlaka zinazohusika lazima zifanye ufatiliaji kwa kuwa ameshapokea malalamiko mengi kutoka katika kampuni mbalimbali za Utalii katika Hifadhi ya Serengeti ambayo pia ni sehemu ya Jimbo lake analo liongoza.  

"Haiwezekani kuendelea kuangalia na kulikalia kimya suala la Watanzania kuendelea kunyanyaswa na Wawekezaji kutokana na maslahi na kufanya kazi bila mikataba sababu si busara Mtalii kuruka na Balloon mara moja  na kutoa Dolla 499 huku mfanyakazi mzawa anayefanya anayefanya kazi kubwa akilipwa shilingi laki moja na themanini,"alisema Kebwe.

PRECISION AIR YAZINDUA SAFARI ZA MBEYA

Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri wa Wizara ya Uchukuzi, Peter Lupatu, akikata utepe kuzindua Safari za Ndege za Shirika la Precision Air za Mbeya kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Precision Air, Michael Shirima. 
Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri kutoka Wizara ya Uchukuzi, Peter Lupatu, akishuka kutoka katika ndege ya shirika la Precision Air wakati wa uzinduzi wa Safari za Mbeya – Dar kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe kabla ya kukata utepe kuzindua safari hizo. Nyuma yake ni Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Michael Shirima. 
  
Mwenyekiti wa Bodi ya Precision Air (PW), Michael Shirima, (Kushoto) akiteta jambo na abiria wa kwanza kununua tiketi ya safari ya Mbeya wakati wa uzinduzi wa Precision Air wa  njia ya Mbeya – Dar, Bw. Alfred Mwambeleko Jumatano hii. 
  
Mzee akisaidiwa kupanda ndege, ambaye ni mkazi wa mkoani Mbeya wakati wa uzinduzi wa Safari za Ndege za Shirika la Precision Air za Mbeya – Dar uliofanyika Jumatano hii kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe uliofanyiwa marekebisho kutumika kwa safari za kimataifa.


=========  ===============  =========

Shirika la ndege la Precision Air yazindua safari za Mbeya

SHIRIKA la ndege la Precision Air (PW) jana lilizindua safari zake za mkoani Mbeya, kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe ambao umekamilika kukarabatiwa hivi karibuni na kuuwezesha utumike katika safari za kimataifa.

Huu ni ujio mpya wa safari za shirika hilo ambapo walikuwa wanaruka kuenda mkoani Mbeya kati ya miaka ya 1997 hadi 2000 wakitua kastika uwanja mdogo uliopo katikati wa mji wa Mbeya.

Uzinduzi ambao ulifanywa na Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi, Peter Lupatu kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya usafiri wa anga ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Songwe, ambapo wakazi wa Mbeya walielezea furaha yao juu ya uzinduzi huo.

Shirika hilo lilitumia ndege yake aina ya ATR-72 yenye uwezo wa kubeba abiria 70, katika kuzindua njia hiyo mpya, kwa kuanza na ratiba ya kuruka Mbeya mara nne katika wiki (Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili) kwa nauli ya shilingi 249,000/= kwa tiketi ya kwenda na kurudi na shilingi 165,000 /= kwa tiketi ya njia moja, zikijumuisha kodi na gharama nyinginezo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Lupatu alisema kuwa hatua iliyochukuliwa na Precision Air itauwezesha mkoa wa Mbeya na majirani zake kuwa na fursa nyingi za kibiashara na maendeleo kwa upatikanaji wa usafiri wa anga katika eneo hilo.

"Natoa wito kwa wakazi wa Mbeya na majirani zake kutumia fursa hii kikamilifu iliyotolewa na Precision Air baada ya kuanzisha safari zake za kibiashara katika mkoa huu. Hii ni hatua kubwa kwa mkoa na sekta ya usafiri wa anga nchini.

"Uwepo wa usafiri wa uhakika wa ndege tunaouanzisha leo hii unaonyesha kwamba Mbeya na mikoa ya jirani sasa itapata fursa kubwa za kibiashara pamoja na kuunganishwa na miji mikubwa ya kibiashara na miji mingine duniani.

"Kuanzishwa kwa njia hii mpya itakuwa ni chachu ya ukuaji mkubwa wa shughuli mbalimbali za kiuchumi katika mkoa huu ambazo ni pamoja na kilimo cha mbogamboga na maua, kwa kuwa sasa wakulima wanauhakika wakusafirisha mazao yao kwa wakati katika masoko yanayostahili," alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Precision Air, Michael Shirima, aliiomba serikali kutafuta mwekezaji ambaye atawekeza katika uuzaji wa mafuta ya ndege katika uwanja wa ndege wa Songwe ili kuwasaidia wawekezaji katika sekta ya usafiri wa anga kupunguza gharama za uendeshaji.

"Ombi langu kwa serikali ni kuhakikisha kuwa kunakuwepo na upatikanaji wa mafuta  ya ndege ya kutosha katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe. Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za uendeshaji kwa mashirika ya ndege. Kwa sasa, tunalazimika kubeba mafuta ya akiba ambayo huongeza mzigo katika ndege, hivyo inatulazimu kubeba abiria wachache na kuacha nafasi kwa ajili ya mafuta ya akiba, "alisema Bw Shirima.

Muasisi huyo wa PW pia aliiomba serikali kuhakikisha kuwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe unakuwa na vifaa bora vya kuongozea ndege kutokana na eneo lilikojengwa ili kulinda usalama wa ndege na abiria wake. Pia aliiasa serikali kufunga rada katika uwanja huo wa ndege, kama ilivyo katika viwanja vingine vya kimataifa.

Aliwahakikishia wakazi wa Mbeya kwamba shirika katika siku za usoni litaongeza idadi ya safari zake za Sogwe endapo abiria wa kwenda na marudio itaongezeka.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Norman Sigala akizungumza wakati wa kuwakaribisha wageni alisema kuwa anafuraha na uamuzi wa Precision Air wa kufika mkoani Mbeya kwa kuwa jitihada hizo zitapunguza changamoto za usafiri kwa wakazi wa mkoa huo za usafiri hususani usafiri wa Dar es Salaam na kuungana na miji mingine duniani.

"Uzinduzi tunaoushuhudia leo ni wa baraka kubwa kwa Mkoa wa Mbeya na majirani zake. Napenda kuwahakikishia wakazi wa Mbeya kuwa Mbeya ya leo haifanani na Mbeya ya jana na ya siku zijazo. Kwa kuwa Precision Air imezindua safari zake kwa mkoa huu, utaona mashirika mengi ya ndege yakileta ndege zao hapa. Uwepo kwa usafiri wa anga sasa kutafanya ndoto zetu za kuendeleza kilimo cha mbogamboga na matunda katika mkoa wetu kufanikiwa. Shughuli zaidi za kiuchumi sasa zitafanyika katika mkoa na hivyo kuwainua watu wetu kiuchumi," alisema. 

2nd ANNIVERSARY, LETS CELEBRATE TOGETHER

  


CALL US NOW  0715376136

WASANII WA FILAMU BONGO KUPELEKWA NIGERIA

Mkurugenzi wa Mad Mad Entertainment, Yasmin Razak (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu kampuni yake kuingia mikataba na wasanii wa filamu wa Tanzania watakaokwenda Nigeria na Jmahuri  ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kutengeza filamu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior, Issack Kasanga na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba. 

Msanii wa filamu, Steve Nyerere (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano hupo.Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior, Issack Kasanga na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba. 

DAR ES SALAAM, Tanzania

KAMPUNI ya Mad Mad Entertainment iliyopo jijini London nchini Uingereza, imeanzisha program maalum ya kupeleka wasanii wa filamu za bongo nje ya nchi kwa lengo la kukuza sanaa hiyo hapa nchini.
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Yasmin Razak alisema ameamua kufanya kazi na wasanii  hao ili kuleta mabadiliko na kuwakwamua kiuchumi wasanii wa filamu hapa nchini.


 “Kwa muda mrefu niliokaa London sioni kama sanaa hii ina maendeleo, nikafikiria kitu gani nifanye ili  kukuza tasnia hii, katika mkataba na kampuni msanii atakayetengeneza filamu na wasanii wa nje atalipwa kiasi cha sh 50 milioni pamoja na malipo mengine yatakayokuwepo kwenye mkataba, ikiwa ni pamoja na asilimia fulani kwa kila kazi itakayouzwa hapa nchini.

“Nimekuwa nikifanya kazi hiyo na wasanii wengi kutoka Nigeria wakiwemo kina Omotola, Two Face na wengineo na pia Ghana, Congo na hata Uingereza, hivyo nimeonelea kuwa itakuwa vema Tanzania nao kuingia katika mchakato huo,”alisema Razak.

Razak ambaye amewahi kufanya kazi ya filamu na Fally Ipupa,  alitaja vigezo vya msanii atakayechaguliwa ikiwa ni pamoja na umaarufu,  kuijua lugha ya kiingereza, uwezo wa kuigiza na kuuvaa uhusika wowote pamoja na mavazi.

Naye rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba aliwataka wasanii hao kujipanga katika kuhakikisha wanaingia kwenye ushindani huo na kuwataka wale watakaochaguliwa kujituma na kuonyesha nidhamu ya uhakika.

“Hapa kuna kuinua vipaji, soko la kimataifa na mengineyo, hivyo ni vema kufanya kazi kikamilifu kwa wale watakaochaguliwa na si kujisahau, wanatakiwa wasanii watatu na tupo katika hatua za awali za mchujo,” alisema
Mwakifamba.

Naye muigizaji Issa Musa maarufu kama Cloud, alisema kuwa lugha itakuwa ni tatizo kubwa kwa wasanii walio wengi, hivyo kuitaka kampuni hiyo iangalienamna ya kuweza kuwasaidia wasanii hao.


Rajabu Mhamila 'Super D'
Photojournalist at Majira, Business Times

Thursday, January 17, 2013

WILAYA YA MASWA NA VIVUTIO VYAKE KATIKATI YA MJI.

Sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere iliyoko katika kipita shoto cha katikati ya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu kama nilivyokinasa hii leo.

Mikoa mingi hapa nchini imeshindwa kujenga sanamu ya Baba wa Taifa na kubakia kujenga sanamu za malighafi zizalishwazo mikoani humo (samaki (Mwanza), ndizi (Bukoba), tembo na Mmasai (Arusha na kadha wa kadha)) pamoja na rasilimali nyingine kisa mikoa hiyo ikiogopa kupata aibu kama ile iliyolikumba jiji la Mwanza kwa sanamu ya Baba wa Taifa katikati ya kipita shoto cha jiji hilo la miamba kushushuliwa kuwa na utofauti na taswira halisi ya JK na hatimaye sanamu hilo lililogharimu pesa nyingi kupotea kusikojulikana mpaka leo...
 Swali ni Jeh Maswa wameweza?

Muonekano full wa Sanamu hiyo..

Kipitashoto kikuu wilayani Maswa.

Naam inakukumbusha historia...


Waijua TANU weye?

Na bustani yake...

"MOMBASA RAHA AU KARAHA???"

Long time sijasafiria mabasi haya nataka mnipe tathinini... Hivi tule 'tupipi' na 'tujojo' tulizokuwa tukigawiwa bado tupopo?


Humo ndani ni 'levo siti' au 'kajamba nani dizaini'?

CHAMA CHA ADC CHAFANYA UCHAGUZI WILAYANI RORYA

 Na Shomari Binda
       Rorya,


CHAMA kipya cha Upinzani Nchini Tanzania cha Alliance For Democtratic Change (ADC) kilichopata usajil wa kudumui mwaka jana kimeendelea kujiimalisha katika Wilaya za Mkoa wa Mara baada ya kufanya uchaguzi na kuunda safu nzima ya uongozi katika Wilaya ya Rorya ikiwa ni Wilaya ya pili kufanya hivyo katika Mkoa huo.

Katika Uchaguzi huo uliofanyika katika Kata ya Nyathorogo ulihudhuliwa na Wanachama zaidi ya mia moja wa Chama hicho pamoja na Wananchi na Viongozi wa Vyama vingine vya Siasa Wilayani Rorya ulishuhudia Erinesti Ojunga akichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Chama hicho Wilayani Rorya kwa kupigiwa kura zote 107 za ndiyo baada ya kukosa mpinzani katika nafasi hiyo.

Awali akifungua Mkutano Mkuu Maalumu wa Uchaguzi huo,Msimamizi wa Uchaguzu huo ambaye pia ni Kamishina wa Chama cha ADC Mkoa wa Mara Jumanne Magafu aliwataka Wanachama wa Chama hicho kuwa makini katika kuchagua viongozi ambao watafikisha malengo ya Chama katika kuwafikia Wananchi kama Katiba inavyoeleza. 

Alisema lengo la kuanzinshwa kwa Chama hicho ni kuwa Viongozi kuwashilikisha Wananchi katika shughuli zote zikiwemo za kiuchumi,Kijamii,Elimu na na masuala yote ya Shughuli za Kimaendeleo na Uwajibikaji kwa Viongozi kwa Wananchi. 

Magafu alidai katika Imani ya Chama cha ADC kifungu cha 1.1 (a) hadi (n) kinaelezea masuala mazima ya Uwajibikaji wa Kiongozi na Ushilikishwaji wa Wananchi katika masula mbalimbali ya Kijamii bila kumtenga mtu yoyote lakini pia Imani ya Chama hicho inamtambua Mwenyezi Mungu ikiwa ni kumtaka kiongozi na Mwanachama yeyote kufanya kazi za Chama kwa kumheshimu Mungu.

Katika muundo wa Uongozi wa Katiba ya Chama cha ADC Katibu wa Wilaya ya Rorya wa Chama hicho Aboum Thomas hakupigiwa kura katika Mkutano huo bali aliteuliwa na Uongozi wa Taifa huku pia Mkutano huo ukichagua safu nyingine za Uongozi ikiwemo Bodi ya Uongozi kwa mujibu wa Katiba.  

Wajumbe wa Bodi ya Uongozi wa Chama hicho iliyochaguliwa katika Mkutano huo ni pamoja na Dominikus Ong'ong'a,Abouk Odiero,Jenifa Kanar,Joyce Dede,Joshua Kanar,Rajabu Samson,Ayoo Ayoma, Deus Akoto,Frola Kura pamoja na Owe seda.

Katika Uchaguzi huo wa Chama cha ADC Wilaya ya Rorya pia ilichaguliwa Kamati ya Utendaji ya Wilaya ambao pia ni Wakuu wa Idara ya Chama hicho ambapo katika Idara ya Ulinzi na Usalama alichaguliwa Ayoo Ayoma,Mipango na Uchaguzi Joshua Kanar,Siasa na Uenezi Deus Akoto,Fedha na Utawala Frola Kura huku Haki za Binadamu Akichaguliwa Owe Seda.

Kamati ya Usuruhishi ya Wilaya,Richard Jaoko alichaguliwa kama Mwenyekiti na Ernest Nyakani Katibu huku Wajumbe wa Mkutano huo  wakiwa ni Edward George,Benard Onene,Eliva Paulo pamoja Abrosi Onono.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kanda waliochaguliwa katika Uchaguzi huo ni Joseph James,Paulo Aduongo,Janeth Kanar pamoja Frola Kura ambao wataiwakilisha Wilaya ya Rorya katika Mkutano Mkuu wa Kanda.

Mara baada ya Uchaguzi huo kukamilika na kuundwa kwa safu nzima ya Uongozi wa ADC katika Wilaya ya Rorya,Wajumbe pamoja na VIongozi wa Chama hicho waliomba Uongozi wa Chama hicho ngazi ya Taifa kufanya jitihada ya kuwatafutia usafiri ambao utawasaidia kukiimalisha na kufanya shughuli za Chama katika maeneo mbalimbali ya Vijiji vya Wilaya hiyo.

Nao baadhi ya Wanachi na Viongozi wa Vyama vingine vya Kisiasa walioalikwa katika Mkutano huo wa Uchaguzi wa Chama cha ADC walisema Katiba ya Chama hicho kama ilivyoelezwa na Kamishina wa Chama hicho Mkoa iwapo viongozi wataifata kitakuwa ni Chama cha mfano wa kuigwa katika Taifa hasa katika ukomo wa Uongozi.

"Kwa kweli nimeipenda Katiba ya ADC japo mimi nimealikwa ni Mwanachama wa (CCM) nimeisoma na iwapo Viongozi waliochaguliwa wataifuata Chama hiki kitaimalika sana hasa katika Wilaya hii ya Rorya ambayo baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa wanafanya kazi kwa masrahi yao binafsi badala ya Wanachi,"alisema Otieno Opiyo aliyejitambulisha kama Mwanachama wa CCM.

Tayari Chama cha ADC kimeshafanya uchaguzi katika Wilaya ya Tarime na hivi sasa Chama hicho kinajipanga kuendelea na ratiba za kufanya Uchaguzi katika Wilaya mbalimbali za Mkoa wa Mara na baada ya Rorya kitaelekea katika Wilaya za Butiama,Musoma Mjini,Serengeti na baadae Wilaya ya Bunda.