ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 19, 2012

DIMPOZzz KUZINDUA HII..(KESHO)

BAADA ya kutamba na wimbo wake wa Nai Nai Msanii anaekuja juu kwa kasi na mshindi wa Tuzo mbili za Kili Music Award 2012, Omy Dimpoz anataraji kuzindua Single yake mpya ya Baadae katika ukumbi wa Club Bilcanas jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao huu wa Kijamii, Meneja wa Msanii huyo, Mbaruku Issa ‘Mubenga’ alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika na show itakuwa ya uhakika nay a kuvutia.

Mubenga amesema Ommy Dimpozy anataraji kuzindua wimbo huo aliofanyiwa kazi na Mwandaaji wa muziki Man Water huku spoting ya wimbo huo ikifanywa na mwanadada Angel.

Aidha Mubenga amesema Dimpoz atasindikizwa na wakali wa Bongo Fleva, Diamond, Ben Pol pamoja na msanii Alawi Jr pamoja na Ma DJ wakali wa Bongo kutoka kundi la Super Deejayz.

Tayari Dimpoz ameshaanza kuwasikilizisha wimbo huo baadi ya mashabiki wake wa mikoa ya Mwanza na Moshi wakati wa Ziara ya Wakali wa Kili Music Awartd 2012 inayoendelea ambapo leo atakuwa Mbeya chini ya Bia ya Kilimanjaro. “Wimbo ni mkali na mashabiki wanaukubali vilivyo na tunaomba mashabiki wa Bongo Fleva make tayari kwa singo hiyo mpya itakayoanza sasa kuchezwa katika vituo vya redio na kumbi za burudani nchini kote baada ya uzinduzi huo,” alisema Mubenga.

Mungenga amewakata wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambao ni mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya kujitokeza kwa wingi kumpa support Dimpoz katika uzinduzi huo wa aina yake katika Club ya Bilcanaz katikati ya jiji la Dar es Salaam jumapili.

Friday, May 18, 2012

MBONI SHOW KUANZA KURUKA NDANI YA EATV MEI 31, 2012

Mtangazaji wa Kipindi Kipya Mboni Show, Bi. Mboni Masimba kinachotarajiwa kuruka hivi karibuni katika sresheni ya EATV akiongea na waandishi wa habari juu ya kuanza kwa kipindi chake. Pembeni yake ni msimamizi wa kipindi hicho Bw. George Tyson na msimamizi wa vipindi vya EATV. Kipindi hichi cha Mboni Show dhima yake ni kuburudisha, kuelimisha, kufundisha, uonya, uadhibu na kuelekeza jamii ya Watanzania inayokabiliwa na changamoto nyingi katika maisha ya kila siku. Na pia kipindi kinakusudia kuleta mapinduzi makubwa katika muendelezo wa vipindi vya mahojiano.

Msimamizi wa kipindi cha Mboni Show Bw. George Tyson akielezea ubora wa kipindi hicho.

Meneja wa Vipindi kutoka EATV akizungumza katika uzinduzi huo wa kipindi cha Mboni Show kinachotarajiwa kuanza kuruka Mei 31 ndani ya EATV.

Waaandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.

Mtangazaji wa Kipindi Kipya Mboni Show, Bi. Mboni Masimba akiteta jambo na msimamizi wa Vipindi wa EATV. Lakini pia anapenda muziki, mitindo na ni mjasiliamali anayemiliki kampuni yake binafsi iitwayo 'CHOCLATE PRINCES' ambayo inaendesha duka la mavazi, vipondozi na viatu vya kike lakini pia ndiyo waandaaji wa kipindi kipya cha luninga 'THE MBONI SHOW'. Picha zote na www.kajunason.blogspot.com

VIJANA WAPO TAYARI KWA MASUMBWI KINONDONI

Katika picha ni baadhia ya mabondia chipukizi wa bigright boxing na mwalimu wao IBRAHIM KAMWE wakimalizia mazoezi yao ya mwishomwisho kwa ajili ya mpambano wa ngumi unaotegemewa kufanyika jumapili20/05/2012 katika ukumbi wa Vijana Hall kinondoni wakisindikiza pambano la ubingwa wa taifa wa Bantam weight chini ya usimamizi wa TPBO kati ya RAMADHAN KUMBELE na JAMES MOKIWA mchezo wa raundi kumi.

Vijana hao wameahidi kuonesha mchezo mzuri wa ushindi 'kama ilivyo kawaida yetu ushindi kwetu ibada'
Mabondia hao wanaotegemea kupima uzito jumamosi19 katika ukumbi wa STEREO club-kinondoni na Heavy weight Anord'biggie'120kg v/s Karim'big paquiao118kgs raundi sita, feather weight-Doi miyeyusho v/s Jumanne Mtengela, Light weight Jafar Majia v/s Daudi Muhunzi, Fly weight-Sadat miyeyusho v/s swed hassan, Martin Richard v/s Yohana Thobias na mapambano mengi mengineyo yakiwemo ya watoto na Burudani toka kwa KARAPINA, MAKHIRIKHIRI WA KIBONGO NA TID.

Mapambano haya yote yameratibiwa na Tasenga na BigRight Promotion kwa lengo la mfululizo wa mapambano ya kuinua vipaji vya mabondia wa Tanzaniana kutafuta mabingwa wa taifa kabla ya kimataifa.

MWILI WA MAFISANGO WAAGWA NA WATANZANIA

Wachezaji wa timu ya Taifa la Tanzania iliyoteuliwa hivi karibuni, mbele ni Juma Nyoso (L) na John Boko (R) wakiwa wamebeba jeneza la mwili wa aliyekuwa mchezaji wa timu ya Simba marehemu Patrick Mafisango, kwaajili ya kuagwa katika viwanja vya  TTC Chang'ombe jijini Dar es salaam nchini Tanzania.

Mwili wa marehemu ukiwasili viwanjani hapo kwaajili ya wadau mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho, mbele wanaonekana Juma Nyoso na John Boko na kwa nyuma ni Shahbani Nditi.
Kombe la Ubingwa Tanzania Bara likiwa limewekwa juu ya jeneza la marehemu Patrick Mutesa Mafisango aliyezaliwa mwezi March mnamo mwaka 1980 na kufariki dunia tarehe 17 May 2012.
Sehemu ya wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania wakiwa na majonzi wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa mchezaji wa Simba aliyefariki dunia Patrick mafisango.

Golikipa wa Simba na Taifa Stars Juma Kaseja alishindwa kujizuia kulia hali iliyosababisha kupatiwa msaada toka kwa marafiki waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu Patrick Mafisango.

Mafisango, alikuwa amechaguliwa kuchezea kikosi cha kitakachowania kufuzu kwa michuano ya kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya Algeria alifariki katika ajali ya barabarani asubuhi ya kuamkia jana mjini Dar es Salaam Tanzania katika ajali iliyohusisha pikipiki na gari wakati gari alilokuwa akiliendesha lilipoteza mwelekeo na kuanguka kwenye mtaro..

Thursday, May 17, 2012

KATIBU w' CHADEMA ANAYEDAIWA KUMNG'OA SIKIO MWANANCHI AMPA SIKU 14 MKUU WA MKOA WA MWANZA KUMTAKASA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kijana Lazaro Nolbert siku alipotinga ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikiro (anayemchunguza) na pembeni ni mama wa kijana huyo.
Katibu wa Chama cha demokrasia na maendeleo wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza Abel Mwesa amempa siku 14 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikiro kumwomba radhi kupitia vyombo vya habari kwa madai ya kumdhalilisha kwa kusema kuwa ndiye aliyemng'ata na kumwondosha sikio la kulia mkazi wa jijini Mwanza Lazaro Nolbert.

Abel mwesa amesema iwapo mkuu wa mkoa hatofanya hivyo kwa muda uliotajwa atamfungulia mashitaka ya udhalilishaji. Tarehe 14 kijana Lazaro Robert alifika katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Mwanza kutoa taarifa za kung'atwa na kiongozi huyo wa CHADEMA akililaumu jeshi la polisi kushindwa kumtia nguvuni mtuhumiwa. Kutokana na madai hayo mkuu wa mkoa wa Mwanza alitoa agizo kwa polisi kumkamata mtuhumiwa wa tukio hilo ambaye aliwekwa rumande kwa siku 2
Kijana Lazaro Nolbert siku akihojiwa na waandishi wa habari.
Nae Lazaro Norbet amesisitiza kufanyiwa kitendo hicho na katibu huyo wa CHADEMA wilaya ya Ilemela akisema kuwa maelezo yake ya awali yalitofautianana na kumtaja mtu mwingine kutokana na mikwara aliyopigwa kwamba iwapo atamtaja katibu huyo kuhusika basi chamoto atakiona.

Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi CCM mkoa wa Mwanza Saimon Mangelepaa
Katika hatua nyingine akizungumza na vyombo vya habari jana katika ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Mwanza Katibu wa siasa Itikadi na Uenezi Bw. Saimon Mangelepaa amesema kuwa CCM imesikitishwa na kitendo cha kiongozi wa juu (KATIBU) wa Wilaya ya Ilemela cha kujichukulia sheria mkononi na kumfanyia kitendo cha unyama kijana Nolbert kitendo ambacho hakina budi kulaaniwa na wananchi bila kujali tofauti za kisiasa zilizopo kwa vile ni kitendo cha kinyama kwa jamii na kimeonyesha kiongozi huyo hatambui wajibu wake kwa kuvunja sheria na kujichukulia uamuzi wake binafisi ambao umemsababishia kijana huyu ulemavu wa kudumu.

WACHEZAJI SIMBA WAMLILIA PATRICK MAFISANGO

Mkurugenzi wa mtandao wa Fullshangweblog Bw. John Bukuku kulia akimsikiliza Katibu Mkuu wa timu ya Simba Bw. Evodius Mtawala wakati alipokuwa akielezea mipango ya kuuhifadhi na kuusafirisha mwili wa mchezaji wao marehemu Patrck Mafisango Mutesa aliyeafiki alfajiri ya usiku wa kuamkia leo maeneo ya Chang'ombe Veta jijini Dar es salaam, wakati akirejea nyumbani kwake na kusababisha watu wengine aliokuwa nao kupata majeraha.

Bw. Mtawala amesema hayo katika hospitali ya taifa ya Muhimbili na kueleza kwamba kwa sasa wanawasiliana na Ubalozi wa Rwanda na mashirika ya ndege ili kukamilisha utaratibu wa vibali mbalimbali tayari kwa kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda nchini Rwanda kwa mazishi na taarifa kamili ya lini utasafirishwa itatolewa kesho mara baada ya kukamilika kwa taratibu zote, katika picha kushoto ni Bw. Mwakitalima mmoja wa mashabiki wa Simba aliyefika muhimbili kushuhudia kilichotokea.
Wachezaji Haruna Niyonzima wa Yanga kushoto na Uhuru Selemani wa Simba wakisikitika wasijue la kufanya baada ya kushuhudia mwili wa mchezaji mwenzao marehemu Patrick Mafisango katika chumba cha kuhifadhia maiti muhimbili leo.

Haruna Moshi akitoka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti huku akilia kwa uchungu baada ya kuhakikisha kweli mwenzao Patrick Mafisango amefariki.

Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na Mchezaji haruna Niyonzima wa Yanga, Pawasa amesema jana walikuwa naye kwenye muziki katika klabu ya Maisha Oysterbay wakati bendi ya Akudo Impact ikifanya onyesho klabuni hapo na marehemu alimuaga kwamba anaenda nyumbani baadae akapigiwa simu kwa simu ya marehemu akiambiwa mwenye simu hii amefariki dunia kwa ajali.

Uhuru Selemani akisalimiana na wanamuziki wa bendi ya Akudo Impact ambao pia wameelezaea masikitiko yao kwani wamesema marehemu walikuwa naye usiku wa kuamkia leo katika klabu ya Maisha ambako walikuwa wakifanya onyesho lao.

Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili leo asubuhi.
Picha na Full Shangwe.

TOWN STARS MABINGWA WA ESTER BULAYA CUP

Michuano ya Mbunge wa Viti maalum kupitia Umoja wa vijana CCM mkoani mara ESTHER BULAYA CUP imemalizika juzi ambapo michuano hiyo ilidumu kwa wiki mbili katika wilaya Bunda mkoani Mara, Katika michuano hiyo Mshindi alikuwa ni Town Star baada ya kuifunga timu ya Amani FC mabao 4-2 kwa mikwaju ya Penalti huku mshindi wa tatu Ikiwa Timu ya Polisi Fc.
Mbunge wa viti maalum kupitia Umoja wa vijana CCM mkoani Mara Ester Bulaya akikagua timu mabingwa Town Star kabla ya mchezo.

Mbunge wa viti maalum kupitia Umoja wa vijana CCM mkoani Mara Ester Bulaya akikagua timu mshindi wa pili Amani FC kabla ya mchezo.

Mashabiki wakisutumuka...

Mashabiki wa timu mabingwa wakimbeba shujaa wao.

Huyu ndiye kipa aliyekuwa mwiba katika fainali.

Katika michuano hiyo Mchezaji bora alikuwa Ramadhani Kifundu kutoka Aman Fc aliyepata zawadi ya shilingi ya shilingi 50,000/=

Katika michuano hiyo mabingwa Town Stars walipata zawadi ya shilingi 500,000/= na kombe.

Aman Fc wakaondoka na kitita cha shilingi 250,000/= Polisi Fc 150,000/= Mfungaji bora kutoka timu ya Balili fc 50,000/= Timu yenye nidhamu Mwembeni FC 50,000/=

BREAKING NEWS:PATRICK MAFISANGO WA SIMBA SC AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI

Marehemu Patrick Mafisango (kwenye kiduara) katika picha ya pamoja na kikosi cha Simba enzi za uhai wake.
Mchezaji wa Simba na timu ya Taifa ya Rwanda kiungo mkabaji Patrick Mafisango amefariki dunia kwa ajali ya gari leo alfajiri katika eneo la Tazara jijini Dar es salaam.
Hili ndilo Gari alilopatanalo ajali marehemu Patrick Mafisango maeneo ya TAZARA jijini Dar.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Simba bwana Aden Rage amesema kuwa taarifa za awali juu ya chanzo cha kifo cha mchezaji huyo zinasema kuwa mchezaji huyo amekutwa na mauti akiwa anaendesha gari na kujaribu kumkwepa mwendesha pikipiki.

Msiba huu unakuja wakati kocha wa timu ya Taifa ya Rwanda Milutin Sredovic 'Micho' akiwa amemteuwa kepteni wa zamani wa timu hiyo Hamada Ndikumana a.k.a 'Katauti' na Patrick Mafisango kujiunga na timu ya taifa hilo (AMAVUBI) kwaajili ya maandalizi ya nchi zitakazofuzu kwenda Brazil kwenye michuano ya Kombe la dunia 2014.

Kabla ya  kuichezea Simba mchezaji huyo alitokea Azam Fc ya jijini Dar es salaam.
Patrick Mafisango is dead.
Mwenyezi Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya marehemu Patrick Mafisango.

Wednesday, May 16, 2012

RC MWANZA AWATAKA MA DC KUPAMBANA NA UFISADI WA FEDHA ZA UMMA KWENYE HALMASHAURI ZAO

Mkuu mpya wa wilaya ya Magu Jaqueline Liana akila kiapo mbele ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo leo katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa wilaya wa Kwimba Selemani Mzee Selemani akila kiapo cha utumishi mbele ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza huku akishuhudiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza akila kiapo cha utumishi kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo huku akishuhudiwa na Katibu Tawala mkoa Doroth Mwanyika.

Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akila kiapo cha utumishi mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza katika hafla fupi ya kuwaapisha wakuu wapya saba wa wilaya za mkoa wa Mwanza uliofanyika leo.

Mkuu wa wilaya ya Misungwi wa zamani Mariam Lugaila akila kiapo mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza baada ya kuteuliwa tena kuwa mkuu wa wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Mary Tesha akila kiapo mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema Karen Yunus akila kiapo cha utumishi wa umma.

Wanahabari nao hawakuwa nyuma kuwajibika katika tukio zima la kuapishwa wakuu wapya wa wilaya saba za mkoa wa Mwanza walioteuliwa hivi karibuni ambapo leo wameapishwa rasmi.
Picha ya pamoja ya wakuu wa wapya wilaya walioapishwa na viongozi waalikwa.

MISS ILEMELA KUFANYIKA GOLD CREST HOTEL MWANZA TAREHE 25/05/212

Baadhi ya warembo watakao shiriki kinyang'anyiro cha miss Ilemela kinachotarajiwa kufanyika tarehe 26/05/2012 kwa mara ya kwanza katika ukumbi mkubwa wa GOLD CREST HOTEL jijini Mwanza.

Ni warembo wenye sifa zote stahiki.

Flash ya warembo Kinyang'anyiro cha Miss Ilemela 2012.
Mkao binafsi kwenye flash..

Pamoja na kuwa na kipaji cha shughuli za ulimbwende pia mrembo huyu yu mtangazaji wa kituo cha Tv Barmedas jijini Mwanza.

W0w...!

Kuna TATIZO...!!?

Nice & Cool..

Fresh...

Crazy..

Chain..
Hapa ndipo mahala mrembo wa Miss Ilemela atapatikana ... Some body ameuliza kuhusu burudani jibu ni kwamba Rais wa Masharobaro Bob Junior atakisanukisha usiku huo ile mmmmmwaaa!!!