ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 19, 2019

HESABU KALI ZATUMIKA KWA SERIKALI KUMALIMALIZA 'SHESHE' LA WACHIMBAJI WADOGO MISUNGWI


Hatimaye Serikali imeruhusu shughuli za uchimbaji dhahabu kuendelea katika machimbo ya Shilalo yalilopo katika wilayani Misungwi mkoani Mwanza Baada ya kusitishwa kwa muda kutokana na mvutano uliokuwepo.

October 07mwaka huu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella alisitisha uchimbaji wa dhahabu katika maduara38 kati ya57 ili kutafuta muafaka mara baada ya kuzuka mzozo mkubwa bkati ya mmiliki wa ardhi eneo la mgodi, wachimbaji wadogo pamoja na mtu anayedaiwa kuwa mwekezaji mpya aliyefika kwenye eneo hilo akidai kuwa wampishe kwani ndiye mwenye leseni.

 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye mkutano baina ya Waziri wa Madini na wachimbaji wadogo wa dhahabu Shilalo wilayani Misungwi.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Charles Kitwanga akitoa salamu zake kwenye mkutano huo.
 Baadhi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu wakifuatilia mkutano huo.
 Baadhi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu wakifuatilia mkutano huo.
 Waakiwa na bango lao ni baadhi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu wakifuatilia mkutano huo.


Machimbo ya Shilalo yanakadiriwa kuajiri zaidi ya wananchi elfu 6 wanaotegemea mgodi huo kuendesha maisha yao ya kila siku

Friday, October 18, 2019

ZAIDI YA WATOTO LAKI 6 KUPATA CHANJO YA SURUA NA LUBELLA MKOANI MWANZA


TAREHE 17 october 2019 katika kituo cha afya Buzuruga uzinduzi wa kimkoa wa kampeni shirikishi ya chanjo ya surua-rubella, umefanyika ukishuhudiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Dr. Zainabu Chaula aliyeambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa huo John Mongella.

Zoezi la chanjo hufanyika kila baada ya miaka mitatu tokea kampeni iliyopita. Kampeni ya mwisho ilifanyika nchini mwaka 2014 ambapo ufanisi katika mkoa wa Mwanza ulikuwa ni asilimia 97.

Katika Kampeni ya mwaka huu zitatolewa chanjo za Surua na Rubella pamoja na chanjo ya Polio. walengwa wa chanjo Chanjo ya Surua na Rubella ni watoto wote wenye umri kati ya miezi 9 hadi miaka mitano kamili.

Kwa Chanjo ya Polio walengwa ni watoto wote wenye umri kati ya mwaka mmoja na nusu na miaka mitatu na nusu.

Mkoa wa Mwanza unataraji kuchanja jumla ya watoto 637,579 dhidi ya Surua-Rubella na watoto 266,140 dhidi ya ugonjwa wa Polio. Chanjo hizi ni salama zimethibitishwa ba Shirika la Afya Ulimwenguni na DSerikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Dawa Tanzania.

Mkoa wa Mwanza una Jumla ya Vituo 608 vya kutolea chanjo hizi. Vituo hivi viko kwenye vituo vya huduma za Afya ama shule ama eneo lolote lililo karibu na makazi ya wananchi.

TAKUKURU MWANZA YAOKOA NA KUDHIBITI UPOTEVU WA ZAIDI YA SH. MILIONI 50

 Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Emmanuel Stenga, akitoa taarifa ya utendaji kazi wa taasisi hiyo kwa waandishi wa habari jana, katika kipindi cha Julai-Septemba mwaka huu. Picha na Baltazar Mashaka
Waandishi wa habari baadhi wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Emmanuel Stenga (mwenye tai nyekundu) wakiwemo watumishi wa taasisi hiyo jana.Picha na Baltazar Mashaka

NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
TAASISI ya Kupamba na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza imeokoa na kudhibiti upotevu wa fedha zaidi ya sh. milioni 50 mkoani humu huku kati ya fedha sh. milioni 30 zikirejeshwa kwenye akaunti maalumu ya serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Mkuu wa TAKUKURU mkoani humu Emmanuel Stenga alisema kuwa uokoaji na udhibiti wa upotevu wa fedha hizo ulifanyika katika kipindi cha Julai-Septemba mwaka huu. 

“TAKUKURU Mkoa wa Mwanza katika mapambano ya rushwa, udhibiti wa ubadhirifu wa fedha za umma kwa kipindi cha Julai hadi Septemba, 2019 imefanikiwa kuokoa sh.42,529,840 na kudhibiti upotevu wa sh.8,294,560.Kati ya fedha hizo sh.30,206,840 zemerejeshwa BOT kwenye akaunti maalumu ya serikali,’alisema Stenga.

Alisema kiasi kingine cha sh.11,413,000 zilizobainika kufanyiwa ubadhirifu kwenye mradi wa ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Salongwe wilayani Magu pia kimerejeshwa kwenye akaunti ya serikali ya kijiji hicho.

Pia Stenga alisema, sh. 640,000 zimerejeshwa baada ya ukaguzi wa taasisi hiyo kufanyika kwenye mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Kakerege wilayani Ukerewe baada ya kubainika kuwa madirisha yaliyowekwa kwenye vyoo vya shule hiyo kutolingana na thamani ya fedha iliyolipwa.

Aidha, taasisi hiyo ilikagua miradi nane ya maendeleo katika sekta za elimu, maji na afya yenye thamani ya sh.2,152,600,000 ili kuona fedha za serikali zinatumika kwa usahihi na miradi inatekelezwa kwa kiwango kinachotakiwa kulingana na thamani ya fedha.

Stenga alifafanua kuwa kati ya miradi iliyokaguliwa sita ni yelimu yenye thamani ya sh. milioni 806.6, maji mradi mmoja wenye thamani ya milioni 986 na afya wenye thamani ya sh. milioni 360 na walifuatilia na kukagua fedha za ruzuku zinazotolewa na serikali kwa shule za msingi ambapo 70 zilikaguliwa katika halmashauri  zote za Mkoa wa Mwanza.

“Lengo kuu la ufuatiliaji huu kwenye miradi inayotekelezwa, ni kuzuia mianya ya rushwa na upotevu wa rasilimali ama kudhibiti fedha za serikali inapobidi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ili itekelezwe kwa kiwango kinachotakiwa na thamani ya fedha ionekane,”alisema Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani humu.ssss

DAR ES SALAAM YAONGOZA TENA KWA WALIOJIANDIKISHA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA.



Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, TAMISEMI, Selemani Jafo amewapongeza viongozi na wananchi wa Mkoa wa Dar es saalam kwa kuitikia kikamilifu zoezi la uandikishaji katika orodha ya wapiga kura na kuongoza kwa zoezi hilo katika orodha ya mkoa.

Waziri Jafo ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya uandikishaji katika daftari la orodha ya wapiga kura mara baada ya kufikia hitimisho siku ya Jana Octoba 17.

Amesema Mkoa wa Dar es saalam mwanzo ulianza kwa kusuasua lakini  baada ya kuanza kupeana hamasa wameweza kufanya vizuri, amesema viongozi wa kazi zote na wananchi kwa ujumla hatimaye kufanikiwa kwa kuandikisha kwa asilimia 108.

"Niwapongeze Mkoa wa Dar es saalam wakati natangaza kwa mara ya kwanza Mkoa ulikuwa na hali mbaya lakini viongozi wa ngazi zote wamehamasishana halikadhalika wananchi kwa kiwango kikubwa hadi kuongoza niwapongeze sana" amesema Waziri Jafo.

Aidha amesema kwa mujibu wa Ofisi ya Takwimu wananchi wenye sifa ya kupiga kura ni 26,960,485, lakini walijiwekea lengo la kuandikisha wapiga kura milioni 22,916,412 ambao ni sawa na asilimia 85, ya wananchi wenye sifa ya kupiga kura (wanaume 10,924,479) na wanawake 11,991,933.

Amesema baadhi ya maeneo yalikumbwa na changamoto mbalimbali ikiwamo mvua na baadhi ya vituo kuwa mbali na makazi ya watu, hivyo baada ya siku ya mwisho waliamua kuongeza siku tatu kwa ajili ya kuhakikisha kila mtu anapata fulsa ya kujiandikisha.

Ameongeza kuwa "hadi kufikia Octoba 17 jumla ya wapiga kura 19,681,259 walikuwa wamejiandikisha katika orodha ya daftari la wapiga kura kwa mwaka 2019, Kati ya hao wanaume 9,529,992 na wanawake10,151,267, sawa na asilimia 86, ya lengo la wapiga kura 22,916,412, na huu ndio uandikishaji wenye mafanikio zaidi ukilinganisha na mwaka 2014" amesema.

Licha ya kila Mkoa kuvuka lengo lakuandikisha kwa asilimia 50,  Mkoa mitano iliyoongoza ni Dar es saalam 108%, Pwani 96%, Mwanza 95%, Tanga 90% na Singida 90% na wote wamezawadiwa kikombe maalamu.

Huku Mikoa mitano ya mwisho licha ya kuvuka lengo lakini imeshika nafasi tano za mwisho, wa mwisho kabisa ni Kigoma 65%, Njombe 75%, Simiyu na Shinyanga 76%, ambayo jumla ya Mkoa yote ni 86%.

"Kwa upande wa halmashauri zilizofanya vizuri ni Mlele 152%, Ngorongoro 129%, Kibiti 126%, Temeke 122% na Monduli 122% ,na halmashauri zenye wapigakura wengi zaidi ya laki tisa 90,000 iliyoongoza ni Temeke MC 122%, Ilala MC111%, Mwanza CC 105%, Ubungo MC 103% na Kinondoni MC 96%" amesema.

Aidha amewapongeza wananchi wote waliojitokeza, na viongozi wa ngazi zote kuanzia mikoa na vitongoji kwa kuhamasisha katika kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya wapiga kura la uchaguzi wa serikali za mitaa.

HABARI ZILIZOTIKISA: SUDAN 1-2 TANZANIA (KUFUZU CHAN 2020 - 18/10/2019)


#BreakingNews Tanzania yafuzu fainali za CHAN mwaka 2020 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009. Ni baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Sudan na kufuzu kwa faida ya goli la ugenini.


Kikosi cha Taifa Stars kilichoshuka dimbani leo kwenye mchezo wa Marudiano kufuzu CHAN dhidi ya Sudan.

Thursday, October 17, 2019

BONDIA AFARIKI BAADA YA KICHAPO KIKALI.


Bondia Mmarekani Patrick Day amefariki dunia jana Jumatano zikiwa zimepita siku nne tangu atolewe na machela ulingoni baada ya kupigwa na mpinzani wake Charles Conwell katika raundi ya 10 ya pambano lao.

Pambano hilo la Super welterweight lililopigwa Wintrust Arena,Chicago lilikuwa ni la utangulizi kuelekea pambano kuu la uzito wa juu kati ya Oleksandr Usyk na Chazz Witherspoon.

Patrick,27, alipoteza fahamu baada ya kupata majeraha ya ubongo na hivyo kukimbizwa Hospitali huko nchini Marekani ambapo alilazwa mpaka mauti yalipomkuta.

Taarifa iliyotolewa na Promota wake Lou DiBella inasema kuwa, Patrick alifariki akiwa amezungukwa na familia yake, marafiki zake wa karibu na watu wa timu yake ya ngumi.

Wakati Patrick alipokuwa mahututi hospitali, mpinzani wake Mmarekani Charles Conwell,21, aliandika barua ya masikitiko, akisema hakutaka kitu hicho kimtokee Patrick na kueleza kuwa tukio hilo limemfanya afikirie kuachana na mchezo wa ngumi, na pambano hilo linamjia mara kwa mara kichwani kwake na kujiuliza kwa nini tukio hilo limetokea kwani hakuna anayestahili limtokee.


MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA MWENYEKITI WA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA CDF, GENERAL VENANCE SALVATORY MABEYO AMEONGOZA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA TAIFA KUKAGUA VIPENYO SALAMA NA VISIVYO SALAMA KATIKA MPAKA WA TANZANIA NA MSUMBIJI.


 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akiongea na wananchi wa kijiji cha Kitaya baada ya kutoka kutembelea eneo la kumbukizi ya shujaa UD 5826 L/CPL Ahamad Mzee, alipoangushia Ndege mbili za Ureno april 1972, katika Msafara huo umeongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mwenyekiti wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama CDF, General Venance Salvatory Mabeyo. (PICHA NA JESHI LA POLISI)
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mwenyekiti wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama CDF, General Venance Salvatory Mabeyo amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano katika Vyombo vya Ulinzi na Usalama, ameyasema hayo leo alipokuwa katika kijiji cha Kitaya baada ya kutoka kutembelea eneo la kumbukizi ya shujaa UD 5826 L/CPL Ahamad Mzee, alipoangushia Ndege mbili za Ureno april 1972 .( PICHA NA JESHI LA POLISI)
 Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mwenyekiti wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama CDF, General Venance Salvatory Mabeyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro pamoja na Mkuu wa Usalama wa Taifa, Kamishna Diwani Athuman wakiwa katika eneo Kitaya mkoani Mtwara katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji ilipo  kumbukizi ya shujaa UD 5826 L/CPL Ahamad Mzee, alipoangushia Ndege mbili za Ureno april 1972, . (PICHA NA JESHI LA POLISI)
Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mwenyekiti wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama CDF, General Venance Salvatory Mabeyo, katikati ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro pamoja na Mkuu wa Usalama wa Taifa, Kamishna Diwani Athuman alie mkono wa kushoto wa IGP Sirro wakiwa katika hifadhi ya bandari ya Ghuba ya Mnazi na maingilio ya mto Ruvuma baada ya kukagua kipenyo cha Kilambo kinachotumiwa na wahalifu kutoka nchi jirani ya Msumbiji. (PICHA NA JESHI LA POLISI)

BITEKO AAHIDI 500,000/= KWA KILA MWANAFUNZI ATAKAYEPATA DARAJA LA KWANZA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2019

 Mgeni Rasmi, Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini akiwasili Mahafali ya 15 ya Shule ya Sekondari Busangi iliyopo Halmashauri ya Msalala, Wilaya Kahama mkoani Shinyanga, Oktoba 16, 2019.

Akizungmza kwenye Mahafali hayo, Biteko alitoa ahadi ya mifuko 300 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa shuleni hapo huku akiungwa mkono na viongozi wa Serikali na taasisi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala aliyeahidi kupeleka Tsh. 25,000,000 (milioni 25) kwa ajili ya ujenzi huo.

Aidha Biteko aliahidi kutoa Tsh. 500,000 (laki tano) kwa kila mwanafunzi atakayefaulu kwa daraja la kwanza katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne katika Shule hiyo ya Sekondari Busangi.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko akipungia wananchi mkono alipokuwa akiwasili kwenye Mahafali hayo.
 Kijana wa Skauti akimvisha Skafu Mgeni Rasmi, Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko.
 Wahitimu wa Shule ya Sekondari Busangi wakiimba wimbo wa kuwaaga wenzao kwenye Mahafali hayo.
 Viongozi mbalimbali meza kuu.
 Mgeni Rasmi, Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko akizungumza kwenye Mahafali hayo.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Busangi akisoma taarifa ya Shule hiyo.
 Katibu Tawala Mkoa Shinyanga akitoa salamu za Serikali kwenye Mahafali hayo.
 Wahitimu.
 Mgeni Rasmi, Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko akikabidhi vyeti kwa wahitimu pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo taaluma.
Tazama Video hapa chini

WAASWA KULINDA AMANI, MASHEIKHE 20 WAKIHUDHURIA MAULIDI YA MTUME MUHAMMAD S.A.W ....

 Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Hasani Kabeke (mwenye kanzu nyeupe), akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu Maalumu wa BAKWATA wa kupokea taarifa ya maandalizi ya sherehe za Maulidi ya Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza Novemba 9, mwaka huu.
 Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Hasani Kabeke (katikati),akizungumza kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa BAKWATA wa kupokea taarifa ya maandalizi ya sherehe za Maulidi ya Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza Novemba 9, mwaka huu.

 Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W. Sadiki Mshola akitoa taarifa fupi ya fedha za maandalizi kutoka vyanzo mbalimbali.
4.Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Miundombinu na  Mapambo, Musa Mkumbi, akitoa taarifa kwenye mkutano Mkuu Maalum wa BAKWATA mikoa ya Kanda ya Ziwa kuhusu hatua iliyofikiwa pamoja na bajeti inayohitajika.
 Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Hasani Kabeke akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa BAKWATA mikoa ya Kanda ya Ziwa baada ya kupokea taarifa ya maandalizi ya Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W. yanayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini humu Novemba 4-9, mwaka huu.
 NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

WAUMINI wa Dini ya Kiislamu Jiji la Mwanza wameaswa kulinda amani, utulivu na usalama wa nchi pamoja na wageni wakati wote wa sherehe za Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W, kwani amani ikivunjika wote watahusika.

Rai hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Masheikhe wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Haruna Kichwabuta, kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa BAKWATA kwa niaba na masheikhe hao wakati wa kupokea taarifa ya maandalizi ya maulidi uliofanyika,kwenye Ukumbi wa Sheikhe Salum Ferej.

Sheikhe huyo wa Mkoa wa Kagera, alisema suala la amani na utulivu ni muhimu, lakini ikivunjika waislamu wote watahusika,hivyo lazima wajichunguze na kuwachunguza wengine wenye nia ovu wanaoweza kujipenyeza ili kuvuruga amani, utulivu ili kuharibu jina la Uislamu na Maulidi yenyewe.

 “Waislamu tuhakikishe tunakuwa macho na watu wenye nia ovu wanaoweza kujipenyeza miongoni mwetu wakati wa Maulidi ili kuchafua Uislamu.Tunahitaji watu watakaokuja hapa watusaidie kulinda amani na utulivu wa nchi yetu na kuhakikisha usalama unakuwepo.Pia tutakuwa na wageni , tuwaangalie na kusimamia usalama wao licha ya kuwepo kwa vyombo vya ulinzi na usalama,”alisema Sheikhe Kichwabuta.

Alisisitiza kwa vile waislamu wanayo dhamana kubwa ya kulinda amani na utulivu wahakikishe sherehe hizo za kihistoria za maulidi ya Mtume S.A.W. yanafanyika kwa amani, usalama, mshikamano na upendo miongoni mwa waumini Kiislamu na jamii ya Watanzania.

Sheikhe Kichwabuta pia ahimiza waumini kushiriki na masheikhe kuendelea kusema na kukutangaza jambo hilo la heri kwenye mimbari (msikitini) na kushughulika na watu wanaoyahitaji maulidi,waachane na wasiyoyataka ili mwisho wa siku yafanyike kulingana na hadhi ya Jiji la Mwanza.

Aidha, Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza alhaji Hasani Kabeke alisema Kitendo cha Mufti Abubakar Zuberi kuipa BAKWATA mkoani humu jukumu la kuandaa Maulidi ya Mtume S.A.W. Kitaifa baada ya miaka 29 ni mtihani, ili kuufaulu ni kuyafanikisha.

Alisema kwa sababu Watanzania waislamu na wasio waislamu wanashirikiana kwa mambo mbalimbali ya kijamii, washirikiane kwa wenye uwezo,wajitoe hali na mali, wenye magari ama nyumba za wageni wasaidie kuwahifadhi wageni hao wa Mtume S.A.W. na kuwasafirisha.
 
Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Hasani Kabeke akifunga mkutanoMkuu Maalumu wa BAKWATA mikoa ya Kanda ya Ziwa baada ya kupokea taarifa ya maandalizi ya Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W. yanayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini humu Novemba 4-9, mwaka huu.


Tunashirikiana na waislamu na wasio waislamu, hivyo wasio waislamu hawajaweewa pazia (mipaka), wanayo haki ya kuchangia Maulidi.Wajitokeze na watusaidie kuwahudumia wageni wa Mtume Muhammad S.A.W. na si BAKWATA.Watakachotoa ni kwa ajili ya wageni hao wa mtume,”alisema.

Kwa mujibu wa Sheikhe Kabeke jumla ya watu 10,000 wanaratajiwa kuhudhuria kwenye sherehe hizo wakiwemo masheikhe 20 kutoka nchi za Burundi, Kenya, Uganda na Rwanda, kuanzia Novemba 4 hadi 9, mwaka huu  huku shilingi milioni 171 zihitajika kwa shughuli hiyo.

Wednesday, October 16, 2019

LIONEL MESSI AKABIDHIWA TUZO YAKE YA KIATU CHA DHAHABU.

Lionel Messi La Purga tayari kashakabiziwa tuzo ya Golden Boot iliyotokana na kuwa mfungaji bora wa ligi za Ulaya msimu wa 2018-19.

Hii inakuwa tuzo yake ya sita (6) ya Golden Boot akitwaa katika nyakati tofauti.

Messi katika picha ya pamoja na mkewe Antonella Roccuzzo na watoto wao Thiago na Mateo baada ya kuipokea tuzo hiyo jijini Barcelona

SIMBA VS AIGLE NOIR NGOMA DRAW.

Mchezo wa kirafiki leo uliochezwa mkoani Kigoma kati ya Simba na wageni wao Aigle Noir kutoka Burundi umekamilika kwa sare ya bila kufungana.

Mchezo huo umechezwa kwenye uwanja wa Lake Tanganyika jioni ya leo umeshuhudia mlinda mlango Beno Kakolanya akiendelea kuwa imara kwa kutoruhusu bao kupenya kwenye ngome yake tena.

Huu unakuwa mchezo wa pili sawa na dakika 180 kwa Kakolanya kukaa langoni kwenye mechi za kirafiki bila kuruhusu bao baada ya ule wa kwanza mbele ya Bandari kuokoa michomo minne ya moto.

Mpaka sasa Simba imecheza michezo mitatu na imeshinda miwili na imetoa sare mchezo mmoja leo mkoani Kigoma

VIONGOZI WA DINI ARUMERU WAWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA



 Viongozi wa dini katika wilaya ya Arumeru wamewataka wananchi kujitokeza kuandikisha majina katika daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za vijiji na vitongoji unaotarajiwa kufanyika Tarehe 24/11/2019

Hatua ya viongozi hao wa dini kuwataka wananchi kujitokeza imekuja kufuatia hatua aliyofanya  mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro kuzunguka mitaani kuhamasisha wananchi kujitokeza na kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa vijiji na vitongoji 

Wakizungumzia mwenendo wa zoezi la uandikisha linavyokwenda askofu mkuu wa makanisa ya AMEC TANZANIA Askofu Baltazar Kaaya na sheikh mkuu wa wilaya ya Arumeru Sheikh Alli issa Ibrahim mbali na kupongeza jitihada zinazofanywa na serikali ya wilaya ya Arumeru katika kuwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha wamesema kazi hiyo siyo ya serikali peke yake na inapaswa kuungwa mkono na wadau wote wanaopenda maendeleo na amani katika wilaya ya Arumeru ambapo pia wamemuhakikisha Mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa watasimama na serikali katika kuhakikisha wanahamasisha waumini wao kwenda kujiandikisha .

Tazama picha na video za kikao.

*Imetolewa na ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arumeru *
14/10/2019

KATIBU CCM AJIVUNIA MAFANIKIO SHULE ZA KATA NA BALTAZAR MASHAKA,ILEMELA

 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kilimani,Gaudensia Bagoka akizungumza kwenye mahafali ya tano ya kidato cha nne cha shule hiyo jana.
 Wahitimu wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kilimani, Ilemela Irene Magesa na Ally Mohamed wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi , Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli, jana.
 Wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ye Kilimani Sekondari iliyopo Ilemela wakiigiza kama maarusi wakati wa mahafali yao iliyofanyika jana shuleni hapo.
 Wahitimu wa kike wa Shule ya Kilimani Sekondari, wakionyesha ubunifu wao wa mavazi ya asili wakati wa mahafali yao iliyofanyika jana.
 Mkuu wa Shule ye Kilimani, Gerana Majaliwa, akitoa taarifa fupi ya mafanikio ya shule hiyo jana kwenye mahafali ya kidato cha nne mwaka huu.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kilimani,Gaudensia Bagoka akisoma risala ya shule hiyo akielezea changamoto na mafanikio kwa mgeni rasmi, wakati wa mahafali ya tano ya kidato cha nne cha shule hiyo jana.
 Mgeni rasmi kwenye mahafali ya kidato cha nne cha Shule ya Kilimani Sekondari, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli akizungumza na wazazi, walimu, wahitimu na wanafunzi jana.
 Stumai Hamis, mhitimu wa kidato cha nne wa shule ya sekondari Kilimani akipokea cheti kutoka kwa mgeni rasmi,baada ya kuonyesha nidhamu ya hali ya juu shuleni hapo.
 Mhitimu wa kidato cha nne wa Shule wa Sekondari Kilimani, Deogratius Kadomole, akipokea moja ya vyeti kutoka kwa mgeni rasmi, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli wakati wa mahafali ya shule hiyo jana.Kadomole alifanya vizuri kwenye masomo ya Baiolojia, Kemia,English na Fizikia pamoja na kwenye usafi na michezo.
Mgeni rasmi wa mahafali ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kilimani, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu waliofanya vizuri kwenye masomo yao baada ya kuwanutunu vyeti wakati wa mahafali ya shule hiyo jana.Picha zote na Baltazar Mashaka

KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza Salum Kalli, amesema maendeleo ya nchi yanategemea vijana wasomi walioelimika na kutumia elimu yao kwa manufaa ya wengi na kuonya jamii isikubali watoto wa kike wakatishwe masomo.
Pia amewataka wazazi kufuatilia maendeleo ya elimu kwa watoto wao na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za sekta ya elimu ili kukuza taaluma shuleni.

 Kalli ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya tano ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kilimani,iliyopo  Manispaa ya Ilemela alitoa kauli hiyo jana.

Alisema dhamira ya serikali kutoa elimu bure kuanzia shule za awali hadi kidato cha nne inalenga kuzalisha watalaamu wasomi wa fani mbalimbali,weledi watakaotumia elimu yao kwa maslahi ya wengi na maendeleo ya nchi, hivyo wazazi na jamii wasikubali watoto hasa wa kike kukatishwa masomo kwa namna yoyote.

Pia dhamira hiyo ya serikali ya awamu ya tano inalenga kuwahudumia na kuwanufaisha watoto wa masikini na kuhakikisha wanapata elimu itakayowakomboa kwenye maisha yao.

“Nimefurahi kuona elimu inayotolewa kwenye shule hii ya kata na zingine licha ya kubezwa, imewawezesha wahitimu kuelezea changamoto na mafanikio ya shule kwa lugha ya Kiingereza.Inaonyesha jinsi walimu wanavyounga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kutoa elimu bure na wanafunzi wanafanya vizuri.Rai yangu wazazi na jamii msikubali watoto wakatishwe masomo,”alisema.

Katibu huyo wa CCM Mkoa wa Mwanza alieleza kuwa Serikali ya awamu ya nne ilijenga shule za kata ili watoto wapate elimu wakiwa karibu na mazingira ya nyumbani na kuwapunguzia baadhi ya changamoto ambapo awamu ya tano imeboresha kwa kuondoa changamoto  na kero nyingi kwa kutoa elimu bure.

Aidha, Kalli alitoa sh. milioni Moja kwa ajili ya kusaidia ukamilishaji wa ujenzi wa ofisi ya walimu inayohitaji sh. milioni 3.5 pamoja na kompyuta moja itakayotumika kuandaaa kanzi data,uchapaji wa nyaraka za shule na shughuli za kitaaluma.

Awali katika risala za wahitimu hao na shule zilizosomwa na Irene Magesa na Ally Mohamed pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Gaudensia Bagoka zilielezea changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa, ukosefu wa ofisi na nyumba za walimu, mabweni ya wasichana, maktaba, kompyuta tatu, upungufu wa samani kwa ajili ya wanafunzi na walimu, huduma ya maji safi na salama.

Walisema changamoto hizo ni kikwazo cha ukuaji wa taaluma shuleni hapo na kuomba wasaidiwe ikizingatiwa ni moja ya shule bora mkoani Mwanza ambapo kwenye matokeo ya mitihani wa taifa kidato cha nne mwaka 2016, ilishika nafasi 115 kati  ya shule 218 kimkoa.

Mwaka 2017 kwa mujibu wa makamu mwenyekiti wa bodi ilishika nafasi ya 138 kati ya 220 kimkoa, mwaka 2018 ilishika nafasi ya 70 kimkoa kayo ya shule 241,mafanikio ambayo ni ya kujivunia baada ya kutunukiwa cheti na ngao kutokana na kuimarika kitaaluma.

Aidha, katika hatua nyingine Kalli alisema kutokana na mafanikio ya shule hiyo, wazazi hawana budi kwenda kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura kuchagua viongozi wa serikali ya mtaa kupitia CCM wenye dhamira ya kuwaletea maendeleo.
Alisema watafanya makosa kuchagua watu wasioumizwa na maendeleo ya wananchi ambao siku zote wamebaki kulalamika huku wakiichonganisha wananchi na serikali yao kwa kubeza mafanikio yaliyopatikana. ssss