AFISA Mdhibiti mkuu Ubora wa shule Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Asha Kiliza amesema wazazi wanatakiwa kuhakikisha watoto wao wanaohitimu elimu ya awali wanaandikishwa mapema kuanza masomo ya darasa la kwanza kwa mwaka 2026.
“ Tumetoka mbali, zamani familia iliyokuwa maarufu na kuheshimika kijijini ni ile iliyokuwa na taa ya chemli na watu walijipanga kuangalia namna inavyofaidi mwanga, Dunia imebadilika kwa kiwango ambacho leo hii kila nyumba ina umeme na watu wanaona umeme kama hitaji la lazima kwenye maisha yao, Nataka niwaombe walimu wote nchini endeleeni kuishi kwa dunia inayobadilika, fikirini upya kila siku. Viongozi mnatakiwa kuwafikia walimu wote, kuwasikiliza na kuwahudumia ili wapate sababu ya kuwapenda ”. amesema Dkt. Biteko
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema hayo Oktoba 16, 2025 katika Manispaa ya Musoma, Mkoani Mara wakati akifungua Semina ya Viongozi wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kanda ya Ziwa na kanda ya Magharibi iliyoshirikisha viongozi kutoka mikoa minane.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Safia Jongo, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, akibainisha kuwa mauaji hayo yalifanyika usiku wa Oktoba 11, 2025, majira ya saa 3:00, na kugundulika Oktoba 16, 2025, majira ya saa 7:00 mchana.
Kwa mujibu wa Kamanda Jongo, uchunguzi wa awali umebaini kuwa mama huyo alimjeruhi mumewe kwa kitu chenye ncha kali baada ya kutokea ugomvi baina yao. Baada ya tukio hilo, watoto wa familia hiyo walianza kumtafuta baba yao bila mafanikio, hali iliyozua mashaka miongoni mwa majirani na hatimaye kufanikisha kugundulika kwa tukio hilo.
Kamanda Jongo ametoa wito kwa jamii kuepuka tabia ya kujichukulia sheria mkononi wanapokumbana na changamoto au migogoro ya kifamilia. Pia, amesisitiza umuhimu wa kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama pale mtu anapopotea au kunapotokea tukio linalotia shaka.
“Wakati mwingine matukio ya watu kupotea huchangiwa na watu wa karibu kabisa, hivyo jamii inapaswa kuwa makini na kutoa taarifa mapema,” alisema Kamanda Jongo.
Gsengo Blog inatoa pongezi za dhati kwa Bwana Kadama Malunde, Mkurugenzi, mmiliki na muasisi wa blogu hiyo, pamoja na timu nzima ya waandishi wanaofanikisha kazi hii kwa bidii na ubunifu.
Tuzo hii ni uthibitisho kwamba kazi nzuri, uaminifu na weledi hulipa.
Hongereni sana Malunde 1 Blog — endeleeni kung’ara na kuweka historia!
NA ALBERT G. SENGO/MWANZA
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka bodi mpya ya Bonde la ziwa Victoria kusimamia menejimenti ya bonde la ziwa hilo ili iwajibike ipasavyo katika kulinda rasilimali maji kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Mhe. Mtanda ametoa rai hiyo jana tarehe 15 Oktoba, 2025 wakati akizindua bodi ya nane ya bonde hilo pamoja na vitendea kazi (Magari) kwa ajili ya matumizi ya bodi hiyo hafla iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya bonde hilo jijini Mwanza. Mhe. Mtanda amesema katika kutekeleza majukumu yao wana wajibu wa kutoa elimu kwa jamii juu ya taratibu na sheria za matumizi ya rasilimali maji na sio kusubiri mwananchi akosee ndipo wamchukulie hatua hususani wanaochimba visima vya maji. Aidha, Mhe. Mtanda ameishukuru Serikali kwa kutoa Tshs.Bilioni 264.8 mkoani humo katika sekta ya maji ambazo zimetumika kuongeza upatikanaji wa maji mjini vijijini kutoka 58% hadi 85% na kutoka 53% hadi 77% kwa mjini huku akibainisha uwepo wa miradi kadhaa vijijini na mijini.Winnie alifichua kuwa baba yake aliendelea kuwa na nguvu hadi dakika za mwisho.
Alikuwa amezoea kufanya mazoezi kila asubuhi. Katika siku hiyo ya maafa, Winnie alisema kuwa babake alitembea kwa raundi tano, na Wakenya wanapaswa kujivunia kwamba alikufa kama mwanajeshi.
"Leo tunaposherehekea maisha yake, nilichagua sio tu kukumbuka kiongozi ambaye kila mtu alijua, lakini baba ambaye nilimpenda kwa kila utu wangu. Sehemu kubwa zaidi ya mimi nilikufa mnamo Oktoba 15. Roho ya simba inanguruma milele.
Nilikuwa naye India wakati alivuta pumzi yake ya mwisho. Alikufa mikononi mwangu, lakini hakufa kama watu wamekuwa wakisema kwenye mitandao ya kijamii. Kila siku angeamka asubuhi na kutembea kila siku. alisukuma hadi raundi tano alikufa kwa nguvu na kwa heshima na kiburi na lazima ujivunie kwa hilo.
Winnie pia aligusia kujifunza kuhusu matakwa ya mwisho ya baba yake.
"Sijui nitamkosa nani zaidi baba yangu au shujaa wangu. Nilikuwa msichana mwenye bahati zaidi duniani kwa sababu ulikuwa baba yangu. Baba, ulikuwa mwepesi, thabiti, mnyenyekevu, na mwanadamu. Ulipokuwa mdogo walikuita Aluo, wakaanza kukuita mtoto wa Jaramogi. Kwangu mimi, ulikuwa baba tu, mtu ambaye uwepo wake ulikuwa wa kawaida."

KIKOSI cha Yanga kimewasili salama Jijini Lilongwe, Malawi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Silver Strikers Jumamosi.
Msafara wa Yanga ulioondoka Saa 1:40 mapema asubuhi ya leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam ulifika Lilongwe Saa 4:44 tayari kwa mchezo huo es Oktoba 18 Uwanja wa Taifa wa Bingu Jijini Lilongwe.
Kocha mpya Msaidizi wa Yanga — Mmalawi Patrick Mabedi ni miongoni mwa waliosafiri na timu wiki moja tangu ajiunge na kikosi cha Wananchi kuliongezea nguvu benchi la Ufundi chini ya Kocha Mkuu, Mfaransa Romain Folz.

KIKOSI cha Simba SC kimeondoka bila kipa wake namba moja, Mousa ‘Pin Pin’ Camara raia wa Guinea kwenda Eswatini kwa ajili mchezo wa kwanza za Raundi ya Pili Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Nsingizini Hotspurs.
Kuelekea mchezo huo wa Jumapili ya Oktoba 19 Uwanja wa Taifa wa Somhlolo mjini Lobamba — Simba imeondoka na makipa wawili, Yakoub Suleiman na Hussein Abel.
Timu hizo zitarudiana Jumapili nyingine ya Oktoba 26 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam na mshindi wa jumla ataingia hatua ya makundi inayohusisha timu 16.
NA ALBERT G.SENGO/MWANZA
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezindua Mradi wa Dunia wa kukabiliana na magonjwa ya Mlipuko nchini na kuzitaka wizara zote tawala za mikoa na serikali za mitaa pamoja na taasisi kutekeleza shughuli za kipaumbele katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko na dharura za kiafya. Dkt. Biteko ametoa agizo hilo Oktoba 15, 2025 jijini Mwanza na kusema mradi huo wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 38.7 unalenga kuboresha huduma za afya kwa watanzania na kuchochea maendeleo ya nchi. Amesisitiza kuwa wizara, taasisi na washirika wa maendeleo wanatakiwa kusimamia utekelezaji katika uwekezaji huo na kuhakikisha yanapatikana matokeo chanya kama ilivyokusudiwa.📌 Dkt. Biteko ataka utekelezaji wa kuleta matokeo chanya
📌 Mradi kugharimu Dola za Kimarekani milioni 38.7
📌 WHO, FAO, UNICEF na Pandemic Fund zaipongeza Tanzania
Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezindua Mradi wa Dunia wa kukabiliana na magonjwa ya Mlipuko nchini na kuzitaka wizara zote tawala za mikoa na serikali za mitaa pamoja na taasisi kutekeleza shughuli za kipaumbele katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko na dharura za kiafya.
Dkt. Biteko ametoa agizo hilo Oktoba 15, 2025 jijini Mwanza na kusema mradi huo wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 38.7 unalenga kuboresha huduma za afya kwa watanzania na kuchochea maendeleo ya nchi.
Amesisitiza kuwa wizara, taasisi na washirika wa maendeleo wanatakiwa kusimamia utekelezaji katika uwekezaji huo na kuhakikisha yanapatikana matokeo chanya kama ilivyokusudiwa.
“Wizara zote, Tawala za mikoa na Taasisi , tekelezeni shughuli zote za kipaumbele katika kukabiliana na magonjwa haya ya mlipuko na dharura nyingine za afya kulingana na maeneo yenu na hakikisha kwamba hakuna hata shilingi moja inayopotea au kuchepushwa kando ya malengo yaliyokusudiwa,” amesema Dkt. Biteko.
Amesema kuwa Serikali kwa upande wake itaendelea kushirikiana na wadau wote wa ndani na nje ya nchi kuimairsha mradi huo ili uweze kuleta matokeo chanya katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ambayo yamekuwa tishio kwa maisha ya watu na kurudisha nyuma maendeleo.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga amesema uzinduzi wa mradi huo, ni muhimu katika jitihaza za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko.Amesema mradi huo unatekelezwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia sehemu ya Afya moja pamoja na wadau wa maendeleo likiwemo Shirika la Afya Duniani(WHO), Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) na Pandemic Fund.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya ambaye ni Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe amesema mradi huo utaboresha mwitikio wa mifumo ya afya katika kukabiliana na magonjwa kama Ebola, MPOX, Marburg, ZIKA na magonjwa mengine yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi.Dkt. Magembe amefafanua kuwa utekelezaji madhubuti utawezesha upatikanaji wa taarifa za haraka kuhusu uwepo au uvumi kuhusu magonjwa ya mlipuko na hivyo kuzifanyia kazi taarifa hizo.
Amesema upatikanaji wa fedha hizo utawezesha pia maboresho ya maabara ya taifa na kikanda ikiwa ni njia ya kupata taarifa za haraka kwa usahihi kutoka kwa wananchi.
Akizungumzia utekelezaji wa mpango huo, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Salim Nassor Slim amewashukuru viongozi wa Kitaifa kwa hatua za kuboresha afya za wananchi ili kuwa na afya bora.Naye Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNICEF, Dkt. Patricia Safi ameipongeza Tanzania kwa ushirikiano ulipo kati yake na mashirika ya kimataifa na kuongeza kuwa Shirika hilo litahakikisha linaendeleza mashirikiano katika kutatua changamoto za kijamii.
Amesema UNICEF itahakikisha mchango wake unajikita katika maendeleo ya mtoto na kufanya jitihada za kuwezesha watoto wote wanapata huduma kwa mujibu wa mipango iliyopo.
Wafungaji wa Iran ni washambuliaji Amirhossein Hosseinzadeh dakika ya 17 kwa njia ya penati baada ya beki wa Stars Ibrahim Baka kufanya madhambi ndani ya 18, na Mohhamad Mehdi Mohebi katika dakika ya 28 aliyepokea pande kutoka kwa K. Taheri.

NA ALBERT G. SENGO/ MWANZA
Takribani shilingi Bilioni 245 zahitajika kutekeleza Mpango wa Usimamizi wa Maji – BONDE LA ZIWA VICTORIA. Robert Sunday, ni Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali za Maji, akizungumza kwenye Jukwaa la Wadau wa Sekta Mtambuka lililofanyika jijini Mwanza, anasema fedha hizo zinahitajika kwa ajili ya kutekeleza Mpango wa Usimamizi wa Rasilimali za Maji katika Bonde la Maji la Ziwa Victoria, ikiwa ni pamoja na utoaji elimu ya utunzaji mazingira. Sunday amesema mpango huo unalenga kuboresha matumizi endelevu ya maji, uhifadhi wa vyanzo vya maji, pamoja na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na shughuli za usafi wa mazingira kwa jamii zinazozunguka bonde hilo. Aidha, amewataka wadau kushirikiana kwa karibu na serikali katika utekelezaji wa mikakati hiyo ili kuhakikisha upatikanaji wa maji salama, usalama wa mazingira na maendeleo ya kijamii na kiuchumi vinaimarika. Tathmini ya Umoja wa Afrika ikishirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika na Shirika la Global Worker Partnership imeonyesha kuwa ili bara la Afrika lifikie malengo endelevu ya kimataifa ifikapo mwaka 2030, zinahitajika dola za Marekani milioni 30 kwa mwaka kwa ajili ya sekta ya maji.

.


! Andrew ana mambo nyie.