ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 11, 2022

MIGOGORO YA NDOA CHANZO KWA BAADHI YA MADEREVA KUSHINDWA KUSHIRIKI SENSA WAKIWA MAJUMBANI MWAO

LEO TARHE 11/06/2022 Mkuu wa Wlaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amezindua Mkutano maalum wa maandalizi ya Sensa inayotarajia kufanyika kuanzia usiku wa Tarehe 23 mwezi wa 8 mwaka huu. Baada ya kusanyiko hilo kumalizika Jembe Fm imepata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wawakilishi wa makundi mbalimbali katika jamii ambao walihudhuria kusanyiko hilo na kubaini haya.




Friday, June 10, 2022

MNEC SALIM ASAS AKERWA NA WATU WENYE NIA OVU NA CCM IRINGA

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Salim Asas  akipokea zawadi kutoka wa jumuiya ya wanawake UWT Wilaya ya Iringa wakati wa baraza la jumuiya hiyo.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Salim Asas akiteta jambo na uongozi wa jumuiya ya wanawake UWT Wilaya ya Iringa wakati wa baraza la jumuiya hiyo.
Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Bi Lena Hongole akipokea mchango wa fedha kutoka kwa Mbunge wa jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga akitoa mchango wa  Sh Milioni moja kwa jumuiya hiyo na kuahidi kuwa ataendelea kuchangia jumuiya hiyo.

 
Na Fredy Mgunda,Iringa.

 

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Salim Asas ameshauri miaka mitano ijayo ya chama hicho iwe ya ‘Siasa na Uchumi,’ kauli mbiu itakayoinua hali kwa wanachama wake kufanya siasa sambamba na kujijenga kiuchumi. 

Asas aliyasema hayo wakati akifunga Baraza la Wanawake Tanzania (UWT) la chama hicho Iringa Vijijini lililofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo, mjini Iringa. 

“Siasa ndiyo maisha yetu, kwa vyovyote huwezi kukwepa siasa kwenye maisha yako hata kama utaamua kutojihusisha na siasa. Sasa kwa kuwa siasa ni maisha, tuangalie namna bora ya kuwafanya wanachama wetu wawe na hali ya kujiinua kiuchumi,” alisema. 

Alishauri uanzishishwaji wa vyama vya ushirika wa kuweka na kukopa akisema vinaweza kusaidia kufufua fursa za kiuchumi kwa jamii na hususani wanawake na hivyo kuwafanya wafaidike na misaada mbalimbali. 

“Tanzania ina mipango mbalimbali ya kuwajengea uwezo wa kiuchumi wanawake na makundi mengine ya kijamii ili kuchochea usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana,” alisema. 

Katika hatua nyingine, Asas amewapongeza viongozi wa UWT Iringa Vijijini wanaokaribia kumaliza muda wao akisema CCM itawakumbuka kwa kazi kubwa ya kukiimarisha chama hicho waliyoifanya kwa miaka mitano iliyopita. 

Kutokana na mchango wao huo, ameahidi kuchangia ujenzi wa nyumba ya Katibu wa UWT wa wilaya hiyo akisema mpango huo unaolenga kuwaondoa watendaji wa chama na jumuiya zake kutoka katika nyumba za kupanga na kuishi katika nyumba za chama nchi nzima. 

Ahadi ya Asas ya ujenzi huo iliungwa mkono na Mbunge wa Kalenga Jackson Kiswaga aliyeahidi kutoa mchango wa awali wa Sh Milioni moja huku akiwahakikishia wanawake hao kwamba atachanga zaidi. 

Katika taarifa yake ya utekelezaji  Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Bi Lena Hongole  ametaja mafanikio yaliyopatikana kuwa ni  kuundwa kwa Vikundi 1500  kutoka vikundi 82 vya awali, ambapo pia vikundi 80 vinapata mkopo. Pia ametaja kuanzishwa kwa  viwanda 68 vinavyomilikiwa na wanawake sambamba na kufufua  shamba la jumuiya  na viwanja vitatu vimenunuliwa kwa ajili ya uwekezaji.

 

Changamoto iliyotajwa katika taarifa hiyo ni ukosefu wa mabweni kwa wasichana mbunge wa jimbo hilo Mhe. Jackson Kiswaga amesema utekelezaji wa ujenzi wa mabweni kwenye jimbo hilo unaendelea.

Kuhusu mikopo kwa wanawake mbunge anasema miongoni mwa sifa za wanawake wanaostahili kupatiwa mikopo kupitia mfuko wa jimbo ni vikundi  vya maendeleo visivyo vya kisiasa

 

Katika kipindi hiki ambacho chama hicho kinaendelea na uchaguzi wake wa ndani wa ngazi mbalimbali, Asas alitoa mwito kwa wana CCM kuwaogopa wajasiriamali hao kama ukoma ili kukinusuru kisipate viongozi wa ovyo, wasio na uwezo na dhamira ya dhati ya kukitumikia kwa kujitolea.

 

 “Tuwe waangalifu sana katika uchaguzi huu, tusichague viongozi kwa Sh 5,000 au Sh 10,000. Tujiepushe na aina yoyote ya rushwa katika uchaguzi huu, vinginevyo tutapata viongozi watakaotugharimu kwa miaka mitano ijayo,” alisema.

RC SENDIGA AAGIZA KUKAMILIKA KWA UJENZI WA BWENI SHULE YA IPOGOLO NDANI YA MIEZI MINNE

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe Queen Sendiga na wataalam mbalimbali wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa bweni katika shule ya msingi Ipogolo Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa sambamba na Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe Queen Sendiga na wataalam mbalimbali wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa bweni katika shule ya msingi Ipogolo 

 

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe Queen Sendiga ameagiza uendelezaji wa mradi wa shule ya msingi maalum ya ipogolo ifikapo Augost mwaka huu.

 

Amesema mkwamo wa jengo la bweni la watoto wenye ulemavu katika shule hiyo unatakiwa kukamilika ndani ya miezi minne na kuitaka Halmashauri ya Manispaa Iringa kuweka mkakati wa kukamilisha mradi huo sambamba na ujenzi wa uzio.

 

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alipokea msaada wa vitanda na magodoro 35 yenye thamani ya shilingi M.4 kwa ajili ya kusaidia watoto wenye uhitaji maalum katika shule hiyo na kuahidi ukamilishaji wa miundo mbinu ya mabweni hayo ili watoto waweze kuhamia katika mabweni Jambo litakalosaidia wazazi kuendeleza shughuli za kiuchumi na hasa ukizingatia kuwa baadhi yao wametelekezwa na waume zao.

 

Bi. Elizabeth mmoja wa wazazi wa mtoto anayeosoma katika shule hiyo amesema kutokana na changamoto zinaziwakabili ukiwemo. usafiri na miundombinu mibovu kwa watoto majumbani na mazingira yasiyo salama yanasobabishwa na wao kuwaacha watoto wao walemavu

 

majumbani pindi wanapokwenda kutafuta mahitaji yao ndiko kunakosababisha shauku yao ya kuiomba Serikali kukamilisha ujenzi huo ili kuwanusuru watoto wao ambao hata huko nyumbani watoto wengine wanalala chini.

 

Kitengo hicho cha watoto wenye ulemavu wa akili shule ya msingi maalum Ipogolo kilianzishwa Mwaka 2001 ukiwa ni mpango wa Serikali kuwezesha watoto wenye ulemavu wa akili kupata Elimu ambapo kwa Sasa kuna Jumla ya wanafunzi 90, wavulana 66 na wasichana 24 ambapo kati ya hao wengine wako katika elimu jumuishi.

 

Hata hivyo Afisa Elimu msingi Manispaa Ndugu Charles Mwakalila amesema kwa bajeti inayo anza Julai Mwaka huu zimetengwa milioni 30 kwa ajili ya ukamilishaji wa mabweni na uzio na kwa sasa wadau mbalimbali wameandikiwa barua kuomba kuchangia ujenzi wa jiko na bwalo.

RAS SENEDA AFUNGUA MAFUNZO YA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MAFINGA

 

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa  Happiness Seneda akiongea na watumishi ambao walikuwa wanapata mafunzo ya mfumo wa usimamizi wa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii Baadhi ya viongozi wanaosimamia mafunzo ya mfumo wa usimamizi wa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii

 

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa  Happiness Seneda amefungua mafunzo ya mfumo wa usimamizi wa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii  wa Halmashauri ya Mji Mafinga.

Alisema mfumo utaanza rasmi kutumika tarehe 1/7/2022 ambapo utarahisisha vikundi vyote kuingizwa kwenye mfumo huo, usimamizi wa marejesho, utoaji w mikopo utakuwa wa haki na hakuna mtu atakopa kwenye vikundi viwili kwa kufanya udanganyifu kwani mfumo utamkataa.

Seneda ameongeza kuwa lengo la serikali ni kuona wananchi wanaondokana na umaskini na wanaweza kusimamia uchumi wao, hivyo anatarajia mafunzo hayo  yalete matokeo chanya na kuondokana na changamoto zilizokuwepo hapo nyuma katika ukopeshwaji, urejeshaji na usimamizi wa mikopo hiyo ya makundi ya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu.

Aidha Kuhusu zoezi la Kitaifa la SENSA ya watu na makazi, Katibu Tawala amesema Elimu iendelee kutolewa kwa wananchi ili waweze kushiriki zoezi hilo kikamilifu tarehe 23 Agosti kwani litasaidia kupanga mipango ya Serikali kwa sekta zote.

Mafunzo hayo, yametolewa na wawezeshaji ngazi ya mkoa wa Iringa na kuhudhuriwa na baadhi ya Wakuu wa Idara  pamoja na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Mji Mafinga Ndugu, Charles Tuyi Afisa Mazingira

MKURUGENZI MNDOLWA AWAASA WAKULIMA MVOMERO KUTUNZA VYANZO VYA MAJI.

 

KuliaBw. Raymond Mndolwa, akionesha sehemu ya daraja la mto Mvomero, halipo katika picha, lililoharibiwa vibaya na athari zitokanazo na mabadiliko ya Tabia nchi pamoja na shughuli za kibinadamu. wengine katika pichani watumishi kutoka Halmashauri ya wilaya ya Mvomero na Ofisi za Tume ya taifa ya Umwagiliaji Mkoani Morogoro.
Picha ikionesha sehemu za kingo za mto Mvomero zilivyoharibiwa vibaya na shughuli za binadamu.
Picha ikimuonesha Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akiwa na wataalam katika kikao cha pamoja, kilichofanyika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mvomero kabla ya kwenda kutembelea Skimu ya Kilimo cha Umwagiliaji Msufini.

·       KUNUSURU MIUNDOMBINU YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI.


Na; Mwandishiwetu -Mvomero

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa, amewaasa wakulima nchini kutunza vyanzo vya maji kwa kutokufanya shughuli za kibinadamu hususani za kilimondaniyamitasitini (60) ilikunusuru kuharibika kwa kingo za mito unaopelekea uharibifu wa Miundombinu ya kilimo cha Umwagiliaji.

Bw.Mndolwa ameyasema hayo mapema alipokuwa akizungumza na wakulima wa skimu ya Umwagiliaji Msufini iliyopo Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro, inayotumia maji kutoka mto Mvomero kama chanzo cha maji ya kilimo cha Umwagiliaji, ambapo ameshuhudia uharibifu mkubwa uliofanyika kutokana na shughuli za kilimo zisizorasmi.

Aliwashauri viongozi wa S erikali yakijiji kushirikiana kulinda vyanzo hivyo vya maji kwa manufaa ya kila mwananchi na aliendelea kusema “Hatulindi vyanzo vya maji yakunywatuu, hata vya kilimo na kuzuia uharibifu unaofanywa na binadamu wenzetu, asili inaharibiwa na binadamu.”Alisisitiza

Bw. Mndolwa aliagiza wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji nawataalam kutoka Halmashauri kufanya mapitio ya mto na chanzo nakuona athari iliyotokana na mafuriko yaliyopita katika mto huu. 

Katika zoezi hilo wataalam watatakiwa kuja na mapendekezo yanini kifanyike ili kurekebisha athari za mafuriko hali itakayopelekea skimu ya Msufini kuanza kufanya kazi.

Aliongeza kuwa, kitachofanyika kwa sasa nikutengeneza chanzo kinachopeleka maji katika skimu hiyo matengenezo ambayo yataridhisha pande zote ikiwa ni pamoja na serikali na watumiaji wa skimu hiyo.

“siwezi ruhusu mkandarasi aliyefanya kazi kwa kiwango cha chini upande mwingine aje tena hapa,sababu kuna mahali kaharibu na nitamfukuza, kama kaharibu kwingine na hapa ataharibu.”Alibainisha Mndolwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Miundo mbinu kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Mhandisi Ntonda Kimasa alisema, kuwa mradi huo umetengewa fedha kwa mwaka wafedha 2022/2023 kwa ajili yakuboresha miundombinu yake, hivyo mara baada ya kukamilika mapendekezo ya timu kazi ya ukarabatiwa miundombinu itaanza mara moja.

Awali, Bw. Mndolwa aliwakumbusha wakulima swala zima za kulipa Tozo na ada za matunzo ya skimu za Umwagiliaji baada ya kujengewa na kukarabatiwa kwa miundombinu hiyo.

Kwa upande mwingine aliwashauri wadau husika akitolea mfano wadau wa  barabara, kilimo na  wadau wengine wakae kwa pamoja ili yafanyike maamuzi sahihi na kuona namna ya kuunusuru mto mvomero kutokuacha njia yake ya asili na kupelekea kuvamia makazi ya watu.

Skimu ya kilimo cha Umwagiliaji Msufini, iliyopo Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro pamoja na kuathiriwa na athari zitokanazo na mabadiliko ya Tabia nchi,imeharibiwa vibaya nashughuli za kibinadamu zinazofanyika ndani ya mita sitini, bila kuzingatia sheria.

Thursday, June 9, 2022

KUNA WANAUME WENGINE MIZIGO - IGP SIRRO

Na Albert G.Sengo Kufuatia kukithiri kwa mikasa ya mauaji na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake , akiwa kama mzazi, mlezi na kiongozi IGP Simon Sirro anaamua kuzama mtaani ambapo hapa anateta na baadhi ya madereva wa bodaboda wanao wakilisha kundi la wanaume katika jamii. #JembeHabari #JeshiLaPolisiTanzania #MauajiTanzania #TokomezaUkatili #HabariZilizoTufikia

TANGA UWASA YATUMIA ZAIDI YA MILIONI 150 KUAGIZA MITA MALIPO KABLA NCHINI UFARANSA

 

KAIMU Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga-Uwasa) Mhandisi Rashid Shaban akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani
kuhusiana na tuzo walizopata katika maonyesho ya 9 ya Biashara yaliyofanyika Jijini hapa

KAIMU Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga-Uwasa) Mhandisi Rashid Shaban katikati akiwa amebeba Kombe la Ushindi na tuzo ikiwa chini akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka hiyo kwenye Banda lao mara baada ya kukabidhiwa
KAIMU Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga-Uwasa) Mhandisi Rashid Shaban katikati akiwa amebeba Kombe la Ushindi na tuzo ikiwa chini akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka hiyo kwenye Banda lao mara baada ya kukabidhiwa

NA OSCAR ASSENGA,TANGA.


KAIMU Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga-Uwasa) Mhandisi Rashid Shaban amesema mamlaka hiyo imetumia zaidi ya Shs Milioni 150 kwa ajili ya kuagiza mita za malipo ya kabla (pre-paid)toka Nchini Ufaransa.


Mhandisi Shabani aliyasema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tuzo walizopata katika maonyesho ya 9 ya Biashara yaliyofanyika Jijini hapa.

Mhandisi Shabani alisema kumekuwepo na malalamiko kwa wateja yanayohusu madai ya kuongezewa gharama za malipo(bili) ambapo mita hizo ndio zitakuwa muarobaini wa malalamiko hayo.

Aidha alisema Mamlaka hiyo imefanya tafiti za kutosha na kubaini kwamba wananchi wengi hawajatambua tatizo la ongezeko la bili ya maji hivyo kuanza kutafuta mbinu mbadala ya kumaliza tatizo hilo.

Alisema lengo ni kukidhi hitaji la Serikali la kutaka wananchi waweze kupata huduma ya maji katika maeneo yote kwa Mijini na Vijijini.

“Tumeanza kufanya tathmini kama tulivyoagizwa na Wizara kuhusiana na mita hizi za malipo ya kabla(pre-paid) na tathmini yetu iko vizuri na matarajio yetu tutafanikiwa”Alisema Mhandisi Shaaban.

Alisema matarajio kuanza na mita 500 ambapo Mamlaka hiyo imepanga kuzifunga kwa baadhi ya wateja kama sehemu ya majaribio na mafanikio yake ndio yatakayopelekea kufungwa kwa mita hizo Mkoa Mzima.

“tumeshaanza majaribio ya mita hizo na zinaonekana kuwa na tija lengo letu sasa ni kuhakikisha tunazisambaza Mkoani kote ”Alisema Mhandisi Shaaban.

Mhandisi Shabani alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi Mkoani Tanga kupokea huduma hiyo na watakuwa na uwezo wa kununua maji kutokana na uwezo wa mteja kama inavyofanyika katika huduma nyingine za kijamii.

Hata hivyo alisema Mamlaka hiyo imepokea tuzo ya watoa huduma bora dhidi ya Mamlaka za Serikali zilizokuwepo kwenye maonyesho hayo kwa kupatiwa cheti na ngao na ile ya ushindi wa Jumla.

FAMILIA YAGOMA KUONDOA KABURI KATIKATI YA BARABARA BARIADI..MKUU WA MKOA DAVID KAFULILA AINGILIA KATI

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu David Kafulila (aliyeshika kiuno) akimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Bariadi Lupakisyo Kapange (mwenye kofia) akimwelezea namna changamoto ya kaburi kuwa katikati ya barabara kijiji cha Nkindwabiye.

Na Constantine Mathias, Bariadi.

Familia ya Saguda Madako katika kijiji cha Nkindwabiye Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, imegoma kuhamisha kaburi linalodaiwa kuzikwa mama yao mzazi ambalo lipo katikati ya Barabara katika kijiji hicho kwa madai hadi walipwe kiasi cha Shilingi Milioni 30 na serikali.


Kaburi hilo limejengwa katikati ya Barabara kuu ya Nkololo-Byuna- Nkindwabiye–Halawa, ambapo familia hiyo imedai mama yao mzazi alizikwa eneo hilo tangu mwaka 1974, na kujengelewa mwaka 2006.


Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa huo David Kafulila wakati akikagua ujenzi wa Barabara hiyo, Meneja Tarura Wilaya, Mhandisi Mathias Mgolozi amemweleza Mkuu huyo wa Mkoa kuwa licha ya kukaa na familia hiyo mara kwa mara kwa ajili ya kuhamisha kaburi hilo lakini imeshindikana.


Mgolozi amesema mara ya kwanza familia hiyo ilitaka Milioni 30 ili kaburi hilo lihamishe, baadaye wakataka Milioni 20, na mara ya mwisho walipunguza na sasa wanahitaji Milioni 1.5.


“Baada ya madai hayo, tulimweleza kwa mujibu wa sheria kuhamisha kaburi familia inapewa kiasi cha Sh. 500,000 na serikali itasaidia kuhamisha kaburi hilo, lakini mpaka sasa familia imegoma,” amesema Mhandisi Mgolozi.



Baada ya hali hiyo Mkuu wa Mkoa, aliagiza kuhamishwa kwa kaburi hilo bila ya kusikiliza uamuzi wa familia kama inataka au hapana na familia ipewe kiasi hicho cha pesa kama sheria inavyotaka.


“Kama sheria inasema hivyo basi naagiza kaburi hili liondolewa mara moja, endapo ujenzi wa Barabara hii utaaanza kaburi liondolewa familia ikubali isikubali kaburi liondolewe na ujenzi wa barabara ufanyike,” amesema Kafulila.

Wednesday, June 8, 2022

MABORESHO YA MAPANGO YA AMBONI KUIUNGANISHA TANGA NA ZANZIBAR KIUTALII

 

Mkuu wa Kanda wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Mecksadeck Mwambungu akizungumza wakati wa Semina kwa waandishi wa habari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kushoto ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga (TPC) Lulu George akifuatiwa na Kaimu Meneja  Uhusiano wa Umma NCAA Joyce Mgaya
Kaimu Meneja Uhusiano wa Umma wa  Mamlaka  NCAA Joyce Mgaya akizungumza wakati wa semina hiyo kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga (TPC) Lulu George na Mkuu wa Kanda wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Mecksadeck Mwambungu
Kaimu Meneja Uhusiano wa Umma (NCAA) Joyce Mgaya akizungumza wakati wa semina hiyo kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga (TPC) Lulu George na Mkuu wa Kanda wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Mecksadeck Mwambungu
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga (TPC) Lulu George akitoa neno wakati wa semina hiyo kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa Umma wa NCAA Joyce Mgaya kulia ni Mkuu wa Kanda wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Mecksadeck Mwambungu
Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga Burhan Yakub akiuliza jambo wakati wa semina hiyo
Mwandishi wa habari wa Kituo cha ITV na Radio One Mkoa wa Tanga Wiliam Mngazija akiuliza swali katika semina hiyo
Sehemu ya washiriki kwenye semina hiyo
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia matukio mbalimbali
Sehemu ya washiriki kwenye semina hiyo

NA OSCAR ASSENGA, TANGA.

MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorogoro (NCAA) imeanza mkakati kabambe kwa kuleta Mapinduzi Makubwa ya kiutalii katika Mkoa wa Tanga kupitia Mapango ya Amboni baada ya kueleza dhamira yao ya kutaka kuunganisha utalii unaofanyika kwenye mapango ya Amboni na Visiwani Zanzibar.

Mkakati huo ulitangazwa na Mkuu wa Kanda wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Mecksadeck Mwambungu wakati wa Semina kwa waandishi wa habari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.

 

Mwambunhu ambaye pia ni Afisa Malikale Amboni kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro alisema mkakati huo unakwenda sambamba na kuhakikisha wanafanikisha upatikanaji wa boti ya watalii wanaotoka zanzibar iliwaweze kukaa amboni kwa muda kidogo.

“Kwa kweli mkakati wetu ni kuhakikisha tunaunganisha utalii unaofanywa mapango hayo na Visiwani Zanzibar na tunakusudia kuhakikisha tunafanikisha upatikanaji wa boti kwa lengo la kuwawezesha wakija kwenye mapango hayo wanakaa muda mrefu”Alisema

 

Bw. Mwambungu ameongeza kuwa NCAA wanamkakati wa kuanzisha utalii wa Boarder(mpakani) kwani kuna watu wanatamani kufika Kenya na hawajui watafikaje na kutoka Horohoro mpaka Amboni ni Kilomita 60 hivyo  wanataka kuweka mpango wa kuweka utaratibu mzuri wa kuwawezesha kufika na kufurahia utalii.

 

“Lakini tatu tunataka kuangalia vivutio vya vilivyopo jirani na Tanga tuweze kuviinua vikiwemo Marine Park na eneo la Maji Moto tunaamini tukiviinu vizuri vitaleta tija kubwa”Alisema  

 

Hata hivyo alisema suala lingine ambalo wanalifikiria ni kutaka kuhakikisha kwamba wanaongeza idadi ya watalii kwenye eneo la Mapango ya Amboni na wanaamini kutokana na mikakati walioweka utafanikiwa.

 

“Kwa sasa tunapokea watalii karibia 1000 mpaka 2000 wengi ni wenyeji na wageni ni wachache sana hivyo tunaamini kutokana na maboresho yaliyofanyika ya miundombinu itakuwa ni fursa nzuri kwao kuweza kuongeza idadi hiyo “Alisema

 

Hata hivyo alisema kwamba mpango wao waliokuwa nao kwa sasa ni kuanzisha ulipaji kwa njia ya mtandao na mahitaji muhimu kwa watalii ambapo wanaamini utakuwa na manufaa makubwa.


Awali akizungumza wakati wa semina hiyo Kaimu Meneja  Uhusiano wa Umma wa NCAA, Joyce Mgaya alisema eneo la Mapango ya Amboni limekuwa na simulizi nzuri na ya kuvutia kutokana na kwamba ndani ya mapango kuna eneo ambalo watu wanafanya ibada wa imani tatu tofauti kwa wakati mmoja na wanaweza kuabudu na kuamini sawa kwamba wakienda hapo wanafanya ibada na kuaminiana

“Hivi sasa kuna utandazawazi mkubwa baadhi tunapoteza hamasa ya kupenda simulizi zetu au kupenda vya kwetu na badala yake tunathamini simulizi za nje ..nadhani kwenye mapango kuna mtu anasafiri kutoka nje ya nchi anakuja kufanya tambiko na kuondoka”Alisema


Hata hivyo alisema kwamba wanafikiria kuweka kitanda kwenye mapango ili watu wanaokwenda kutalii eneo hilo waweze kupata eneo la kupumzika usiku na kuweza kusikilizia usiku kunakuwaje.

TANZANIA NA MAREKANI ZAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MICHEZO NA SANAA

 

Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa wakiambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi wamekutana na Balozi wa Marekani hapa nchini leo Juni 8, 2022 wamekutana jijini Dar es salaam na kujadili masuala mbali mbali ya sekta za ikiwa ni pa moja na ujio wa msanii mashuhuri wa uchoraji ,Ashley Collins hapa nchini.


Wakizungumza katika  kikao hicho ambacho Mhe. Balozi  wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Donald Wright ameambatana na Afisa Uhusiano wa Ubalozi huo, James Rodriguez wamejadili pia ujio wa Timu ya wachezaji nguli wanawake ya mchezo wa kikapu wa ligi  ya NBA nchini Marekani  hapa nchini ambao watakuja Tanzania kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wachezaji wanawake wa mchezo huo hapa nchini. 


Mhe. Mchengerwa amesema viongozi hao wamekubaliana  kuendeleza  malengo ya Royal Tour kwa kushirikiana zaidi  kwenye kuendeleza sekta  za sanaa na michezo ikiwemo kuendeleza  filamu za hapa nchini za “Swahiliwood” ili ziwe  katika  kiwango cha kimataifa kama zile za nchini Marekani kwa kupata walaam ambao watasaidia katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa miswada (script)


Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na maeneo ya kipekee ya kuchezea  filamu ambazo zingeweza  kuwa bora na kusisitiza kuwa ni azma ya serikali kujenga mazingira  wezeshi ikiwa ni pamoja na kuangalia kodi mbalimbali ili kuwavutia wageni kuja  kurekodia  hapa nchini.


Aidha amesema eneo jingine ambalo limejadiliwa ni pamoja na kutoa mafunzo maalum katika eneo la haki miliki na hakishiriki kwa kazi mbalimbali za wasanii ikiwa ni pamoja na tuzo za muziki na Kwa upande mwingine amesema wamejadili namna ya kushirikisha wataalam kwenye program maalum ya kuibua vipaji vya wasanii na wanamichezo ya mtaa kwa mtaa.

Sunday, June 5, 2022

Picha : RC ROBERT GABRIEL AONGOZA SHEREHE MAALUMU ZA 'USIKU WA WAANDISHI NA WADAU WA HABARI KANDA YA ZIWA

 


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel amewaongoza Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC).

Sherehe hizo zenye lengo la kuwaleta pamoja wadau wa habari ili waweze kueleza tathmini yao ya mwaka mmoja wa utekelezaji wa mipango yao ya mwaka ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan zimefanyika Usiku wa Ijumaa Juni 3,2022 katika ukumbi wa Rock City Mall Jijini Mwanza na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa Habari kutoka Kanda ya Ziwa.


Katika sherehe hizo Maalumu za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya habari  wadau wa habari wamepata fursa ya kuonyesha bidhaa au huduma zao mbele ya vyombo vya habari   pamoja na kujenga mahusiano ya kikazi baina ya vyombo vya habari na wadau wa habari.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel pia amezindua Akaunti ya Benki kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 

Miongoni mwa Wadhamini wa Sherehe za Usiku wa Waandishi wa Habari Kanda ya Ziwa ni pamoja na Kampuni ya TBL, TCRA,NSSF, Kampuni ya Jambo, UTPC, Metro Fm, Clouds Media, TRA, TIRA, EMEDO, YUHOMA,MSCL,RFA, Cecy Toto & Gift Shop na SBC LTD.

Mwenyekiti wa MPC , Edwin Soko amesema kuwa, kwa Mwaka ujao 2023 usiku wa waandishi wa habari na wadau wa habari Kanda ya Ziwa kwa Mwaka utaadhimishwa kitaifa ili kuwaleta wadau wengi zaidi kwani kumekuwa na maombi toka kwa wadau juu ya hafla hiyo kuwa ya kitaifa.

Soko ameongeza kuwa, MPC inatambua uwepo wa wadaua na kwa mwaka 2022/ 2023 itahakikisha inaboresha mahusiano zaidi ya wadau wa habari Kanda ya Ziwa .

Usiku wa waaandishi wa habari na wadau wadau Kanda ya Ziwa ilitanguliwa na wiki ya wadau Kanda ya Ziwa iliyoanza Mei 29 na kuhitimishwa Juni 3, 2022, ambapo wadau wa habari waliweza kutembelewa na vyombo vya habari na kueleza tathimini ya utendaji kazi wao na mipango yao kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Tazama Picha hapa chini

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel akizungumza katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel akizungumza katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel akizungumza katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza, Edwin Soko akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
MC Ben na MC Gsengo (kulia) wakizungumza jambo kwwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 
Mkuu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (kushoto) akikata utepe kuzindua Akaunti ya Benki kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 
Mkuu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (kushoto) akionesha namba za akaunti baada ya kuzindua Akaunti ya Benki kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 
Mkuu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (kushoto) na Mwenyekiti wa MPC , Edwin Soko wakionesha namba za akaunti baada ya kuzindua Akaunti ya Benki kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania , Abubakar Karsan (kushoto) akichangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 
Mkurugenzi wa Shirika la EMEDO, Editrudith Lukanga (kushoto) akichangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) 
Mkuu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (kulia) akimpongeza Mwenyekiti wa MPC , Edwin Soko kwa kupata tuzo ya kutetea uhuru wa kujieleza
Meza kuu wakiwa katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mwakilishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Khalfan Isango akielezea huduma wanazotoa ikiwa kusajili watoa huduma za bima kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan akizungumza sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mwakilishi wa NSSF, Ignas Njau akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando Dkt. Fabiani Massaga akielezea huduma zinazotolewa katika hospitali kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Msimamizi wa Radio Free Africa (RFA) Beatrice Rabachi akizungumza sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mhandisi Abel Gwanafyo kutoka Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Meneja wa Metro Fm, Allex Ngusa akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa Shirika la EMEDO, Editrudith Lukanga akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa Uhuru Hospital, Dkt. Derick Nyasigwa akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa Taasisi ya Yuhoma Educational Limited , Yusuph Yuhoma akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Mkurugenzi wa Cecy Toto & Gift Shop, Cecilia Mekhior akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Leonard Paul ambaye ni Wakala wa Matangazo 'Mwana Leonard Company' akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza

Mwenyekiti wa Mabalozi wa Sensa ya watu na Makazi, Mansour Jumanne akizungumza kwenye sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
Wadau wakiwa kwenye Sherehe za Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza
MC Ben na MC Gsengo (kushoto) wakiwa katika Sherehe za Usiku wa Marafiki wa Vyombo vya Habari Kanda ya Ziwa maarufu 'Usiku wa Waandishi na Wadau wa Habari Kanda ya Ziwa' zilizoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club - MPC) Juni 3,2022. 

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog