ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 30, 2015

"WAKATI UCHAGUZI MKUU UKIKARIBIA MAISHA YA WATU WENYE ALBINISIM YAKO HATARINI NCHINI TANZANIA" ASEMA PETER ASH

"Nina ndoto kwamba siku moja nchini Tanzania, watu wenye ulemavu wa ngozi watachukua nafasi yao inayostahiki. Na kwamba siku za ubaguzi dhidi ya watu wenye albinism zitakuwa kumbukumbu iliyofifia" amesema Peter Ash, Muasisi wa Under the SAME SUN (kulia).
Vicky Mtetema (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza na kulia ni Muasisi wa UNDER THE SAME SUN Peter Ash akionesha moja kati ya vipeperushi vya elimu kwa umma kuhusu suala la albinism.
TUKIZUNGUMZIA ukatili kwa watu wenye Albinism duiani, ni matukio mengi yametukia nchini Tanzania tangu mwezi Mei 2013 ikiwa ni pamoja na mauaji na watu kukatwa viungo hadi tukio  la mwisho lililosisimua wengi na kuwabakiza njia panda, lililotokea mnamo tarehe 27 Dec 2014 ambapo mtoto Pendo Emanuel alitekwanyara na watu ambao hawajajulikana hadi leo katika kijiji cha Ndame wilayani Kwimba mkoani Mwanza.


Kwa mujibu wa tafsiri aliyokuwa akiitoa Vick Mtetema kuwasilisha taarifa ya Muasisi wa Shirika la Under The Same Sun ambalo limekuwa likijibidiisha katika kuibua yale yaliyofichika yanayohusu changamoto, manyanyaso na ukatili kwa watu wenye albinism, Bw. Peter Ash, baada ya kufanya ziara kwenye kijiji cha Ndame wilayani humo (Kwimba) na kukutana na mama yake Pendo aitwaye Sofia Juma, amepokea malalamiko toka kwa mama huyo ambaye amelelemika kuwa tangu apate tatizo hakuna kiongozi yeyote wa Kisiasa aliyethubutu kumtembelea kujua hali yake au kutafuta ufumbuzi akiwemo yule wa jimbo lake aliyempigia kura.


Wanahabari kusanyikoni.
"Kwanini hata yule mbunge niliyempigia kura hajawahi kuja kunitembelea kunisikiliza na kujua jinsi mtoto wangu alivyotekwa nyara?"

Hiyo ni hali ambayo imekuwa ikijirudia, Peter Ash akikutana na malalamiko kama hayo pindi anapozitembelea baadhi ya familia zinazokumbana  na masahibu kama hayo yanayohusisha watu wenye ulemavu wa ngozi (wenye albinism).
"Hata familia ya mtoto Karim Kasimu (4) anayeishi na wazazi wake Nyakato jijini Mwanza ambaye pia alinusurika kutekwa nyara tarehe 6 Januari 2015 akiwa karibu na nyumbani kwao, ile familia haijaona kiongozi yoyote wa kisiasa aliyethubutu kutembelea kuona jinsi gani anaweza kuisaidia kushiriki kwa namna moja au nyingine kuwalinda watu wenye albinism" KUMSIKILIZA BOFYA PLAY


Wanahabari kikazi zaidi.
Katika nchini nyingi zenye imani potofu barani Afrika ikiwemo Tanzania inaaminika kuwa magonjwa sugu na hata yale ya kuambukiza kusafishwa kwa kumbaka mtu aliye na ulemavu wa ngozi (albinism). Moja kati ya matukio yaliyotokea ni lile lililotokea mkoani Shinyanga ambapo bintimmoja mwenye alibakwa na watu watano wenye maradhi wadai kujisafisha maradhi. BOFYA PLAY KUSIKILIZA 

AMRI BILA VITENDO NI KAZI BURE.
Hoja imewasilishwa kwa njia ya swali:- Hivi hiyo amri ya kupiga marufuku upigaji ramli iliyotolewa na Waziri wa mambo ya ndani inatofautiana nini na amri iliyotolewa na Waziri Mkuu mnamo Januari 2009,amri ambayo hata hivyo ilikuja kufutwa tarehe 30 September 2010 mwezi mmoja kabla ya UCHAGUZI MKUU?

Kwa sasa hivi tunaelekea kwenye UCHAGUZI MKUU mwingine, nayo amriimetolewa. Jeh hii amri itakuwa na uzito, itafanya kazi, itatimiza malengo yaliyokusudiwa? BOFYA PLAY KUSIKILIZA.

Mwanahabari Albert G. Sengo akitafakari mara baada ya kutoka chumba cha mkutano na wadau wa Under the same sun uliofanyika katika ukumbi wa Hotel Ryans Bay wilayani Nyamagana jijini Mwanza.
UMOJA WA MATAIFA WAAMUA KUHUSU WATU WENYE ALBINISM
Zaidi ya matukio 152 ya mauaji yametokea ndani ya kipindi cha miaka 14 nchini Tanzania lakini ni asilimia 5 tu ya kesi zake zimefikishwa mahakamani.

Umoja wa Mataifa umetambua Umuhimu wa kuliangalia hili suala la watu wenye albinism, hali yao na ukatili unaofanywa dhidi yao na sasa umeitenga kuanzia mwaka huu tarehe 13 mwezi JUNI ya kila mwaka kuwa 'SIKU YA ALBINISM DUNIANI'
BOFYA PLAY SIKILIZA

AIRTEL YATANGAZA TANO BORA YA SHINDANO LA AIRTEL TRACE MUSIC STARS

Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari wakati wa kutangaza majina ya washiriki walioingia 5 bora katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars , akishuhudia Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga
Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga akiongea na waandishi wa habari wakati wa kutangaza majina ya washiriki walioingia 5 bora katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars akishuhudia
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki waliongia 5 bora katika mashindano ya kuvumbua vipaji vya mziki ya Airtel Trace Music Strars . finali za mshindano hayo zinategeme kufanyika mwanzoni mwa mwezi wa pili kulis ni  Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga
  Press Release
 Airtel yatangaza tano bora ya shindano la Airtel Trace Music Stars * Mshindi wa Airtel Trace Music kupatikana katika Finali itakayofanyika tarehe 7 februari Kampuni ya simu ya mkononi leo imetangaza washiriki walioingia tano bora katika shindano la Airtel Trace Music star shindano lenye lengo la kusaka na kuibua vibaji kwa wanamuziki chipukizi.

Shindano hilo lililozinduliwa rasmi mwaka jana Oktaba limefika katika hatua za fainali ambapo mshindi wa Airtel Trace Tanzania atapatikana katika finali inayotegemea kufanyika mwanzoni mwa mwenzi wa pili mwaka huu ambapo mshindi huyu ataenda kushiriki mashindano ya Airtel Trace Music Stars Afrika yatakayoshirikisha washiriki wengine kutoka nchi 13 barani Afrika

Akiongea na waandishi wa habari Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga alisema" leo tunayofuraha kubwa kutangaza majina ya washiriki waliofanya vizuri katika mashindano haya na kupata nafasi ya kuingia katika tano bora na kuweza kumpata mmoja kati yao atakaeibuka na ushindi wa kuiwakilisha nchi yetu katika mashindano ya Airtel Trace Afrika".

 Akiendelea kufafanua Aneth alisema "Washiriki hawa watano ni kati ya wengi waliothubutu kuonyesha uwezo wao wa kushiriki kwa kupiga simu, kuimba na kutuma nyimbo zao na hatimae majaji wamesikiliza vipaji vyao kama walivyoimba na kuwachagua kuingia tano bora (top 5), sasa kura nyingi toka kwa watanzania ndio itakayomuwezesha mmoja wao kupata uhindi wa kwanza wa Airtel Trace Tanzania.

Mashindano haya yanalengo la kuinua vibaji vya musiki kwa vijana wetu kuzifikia ndoto zao na kuwawezesha kuonyesha vipaji vyao ndani na nje ya nchi. Airtel tunajisikia furaha kuwa sehemu ya mafanikio yao na sehemu ya kuinua vipaji vya wanamuziki chipukizi kwa kupitia mashindano haya ya Airtel Trace Music Stars.

Napenda kuwapongeza na kuwatia hamasa wale wote walioshiriki na pia hawa waliofanya vizuri na kufika katika hatua hii muhimu ya mashindano haya. Akitangaza majina ya walioibuka kwenye tano bora Meneja Uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando alisema " tunawashukuru watanzania na wanamuziki chipukizi kwa kushiriki katika shindano hili na mpaka sasa tunaovijana wengi waliojaribu kuonyesha uwezo wao wa kuimba, lakini kama mnavyofahamu haya ni mashindao hivyo napenda kuwaleta kwenu wale waliofanya vizuri zaidi na kuingia katika hatua hii ya mchuano mkali .

Waliobahatika kuingia tano bora ni pamoja na Nalimi Mayunga mwenye namba ya ushiriki (YUN), Christopher Kihwele (TOJ), Tracy Eminence (MHR), Beautus Henry (BOB) na Rose Mbuya (ROS) Natoa wito kwa watanzania , wadau mbalimbali na wapenzi wa muziki kuwapigia kura washiriki hawa kwa kupiga kutuma sms yenye jina la fumbo la mshiriki kwenda kwenye namba 15594

Hii ni nafasi ya pekee kwa watanzania kuonyesha uwezo na vipaji vyao katika anga za Afrika hivyo ni matumaini yetu kuwa washiriki hawa watajifua vyema ili kufanya vizuri katika mashindano ya Afrika pindi mshindi atakapo patikana.

Akiongea mara baada ya kutangaza kuwa moja ya tano bora Christopher Kiwhele alisema" najisikia furaha sana kupata nafasi hii ya kuwa moja ya tano bora, kwakweli kwangu ni kama ndoto, siamini kama nimeweza kufudhu ma kufika katika hatua hii kubwa, na amini ntaendelea kufanya vizuri kwani naendelea kujiandaa vyema, nimetamani sana kuwa mwimbaji nyota na mwimbaji anayenivutia zaidi ni Ed sheeran naamini kupitia mashindano haya ntafika mbali na kutumiza ndoto zangu.

Nawaomba watanzania watuunge mkono na kutupigia kura ili kuendelea kufanya vizuri na hatimae kuwakilisha nchi yetu vyema katika mashindano ya Afrika. Washiriki tano bora wa Airtel Trace music Star sasa wako kambini ambapo wanapata mafunzo yatakayoendelea hadi fainali inayotegeme kufanyika tarehe 7 mwenzi wa pili 2015 jijini Dar es saalam.

MRBA YAZIBA NAFASI 4 ZA JUU ZILIZOKUWA WAZI NA KUUNDA UONGOZI WA MUDA

Chama cha mpira wa kikapu mkoa wa mwanza (MRBA) kupitia kamati ya michezo mkoa wa Mwanza kimetangaza majina ya viongozi wa muda ambao utakuwa madarakani kwa muda wa miezi mitatu kuanzia tarehe 01.02.2015.

Lengo kuu la kutangazwa viongozi hawa pamoja na kuziba nafasi za viongozi waliokuwepo awali, ni kuwataka viongozi hawa kufanya uchaguzi mkuu sambamba na kuzielekeza klabu mbalimbali kufanya uchaguzi wa viongozi katika klabu ili waweze kushiriki uchaguzi ngazi ya mkoa.

Viongozi hawa wanaziba nafasi za viongozi waliokuwepo awali ambao kwa sasa hawapo kutokana na sababu mbalimbali.

Uongozi wa awali ulikuwa ni kama ifuatavyo:

11.      Sadoti Mazigo (Mwenyekiti) – alihama mwanza.
22.      Adam Nyoni (Makamu Mwenyekiti) – alihama mwanza.
33.      Chikoko (Katibu Mkuu) – alihama mwanza.
44.      Victor Maleko – Katibu msaidizi
55.      Flora Kavavila – Mweka hazina (Alifariki)
66.      Amri Mohamed – Kamishna wa Makocha.
77.      Twalib Puzo – Kamishna wa Waamuzi.
88.      Diana Deodatus – Kamishna wa wanawake.
99.      Haidary Abdul – Kamishna wa ufundi na uendeshaji mashindano.
110.  Kizito Bahati – Kamishna wa watoto na maendeleo ya mashule.
111.  Vincent Shinda – Mchezaji mwakilishi.

Nafasi zilizozibwa ni wahusika ni wafuatao.
11.      Juvenile Kaiza ­– Kaimu Mwenyekiti. 
22.      Benson Nyasebwa – Kaimu Makamu Mwenyekiti.
33.      Shomali Almasi – Kaimu Katibu Mkuu.
44.      Vitalis Ndanu – Kaimu M/Hazina

Viongozi hawa watashirikiana na waliopo katika kuendeleza mpira wa kikapu mkoa wa mwanza.
Imetolewa na:

Kizito Sosho Bahati
Kaimu Katibu Mkuu
MRBA

'PATA MPANGO MZIMA WA RATIBA YA HARAKATI ZA VALENTINE NDANI YA VILLA PARK'

Mpango mzima wa 'Harakati za Valentine ndani ya Villa Park Mwanza, utakao anza rasmi Alhamisi ya tarehe 12/02/2015 ambapo Mfalme Mzee Yusufu na Bendi yake ya Jahazi Mordrn Taarab kuhusika, kiingilio nishilingi 10,000/=

Kisha Jumamosi ya tarehe 14/02/2015 Valentines Day bendi ya Super Kamanyola kutambulisha safu ya waimbaji wake wapya, Kiingilio Sebuleni Tshs 5,000/= na Tshs10,000/= utazama hadi Disco ambako kutakuwa na mpambano wa Ma-Dj NANI MKALI KATI YA DJ TASS (MAGIC FM) V/s DJ EDDY (RFA)
Moja kati ya ma-dancer wa Super Kamanyola anaitwa Cathy Butamu. 
Crew ya bendi yako Super Kamanyola yenye maskani yake Villa Park Kirumba jijini Mwanza.
Kutoka kushoto ni Cathy Butamu, Alan Mwepu, Husna Bongo na Erick Ramadhan.
Kutoka kushoto ni Cathy Butamu, Rais wa bendi Shushu Di Cando, Husna Bongo na Erick Ramadhan.
Kutoka kushoto ni Erick Ramadhan, Cathy Butamu, Kadjo Litungu, na Husna Bongo.
Kutoka kushoto ni Erick Ramadhan, Cathy Butamu, Husna Bongo na mpiga drums mpya ambaye atakwenda kutambulishwa Sele Cardance.
Kutoka kushoto ni Cathy Butamu, Erick Ramadhan, Husna Bongo na mpiga rhythm Bevance.
Mji wa mawe....Mwanza kando kando ya ziwa Victoria na Wana-Super Kamanyola.
Style mpya za uchezaji kutambulishwa katika usiku wa Valentine 14/02/2015.
Ze angle.
'VIMBA' ni moja kati ya style ya uchezaji.
Super Kamanyola.
Kutoka kushoto waliokaa mbele ni Karmodee (mpiga bass), Husna Bongo (dancer), Joshua Ephaem (solo guitar), Alan Mwepu (solo guitar), Rashid Mwenzingo (mwimbaji), Cathy Butamu (dancer) na Sele Cardance (mpiga drums)

Kutoka kushoto juu ni Bevance (rhythm guitar), Erick Ramadhan (dancer), Shushu Di Cando (rais wa bendi ambaye ni mwimbaji) na Kadjo Litungu (mwimbaji) .

MAANDALIZI YA TAMASHA LA MIAKA 10 YA THT Escape 1 MIKOCHENI YAKAMILIKA (2)

Maadhimisho ya miaka kumi ya THT Jumamosi hii Escape 1, Mikocheni

·        Ben Paul, Grace Matata waongezeka kwenye burudani, Mrisho Mpoto na Weusi kusindikiza

·        Viingilio shilingi elfu 15 kwenye vituo na elfu 20 mlangoni

Tamasha la miaka kumi ya THT litakalofanyika jumamosi hii katika viwanja vya Escape 1 Mikocheni, limekamilisha maandalizi yake na hivyo kuwataka wadau na wapenzi wake wajitokeze kwa wingi kushuhudia burudani kubwa ya mziki hapa nchini.

THT, ambayo inasifika kwa kuzalisha wasanii mahiri nchini kama Linah, Barnaba, Mwasiti, Ditto, Mataluma, Vumi, Beka, Recho, Marlaw, Msami, Makomando na wengine wengi, imejipanga kutoa burudani kubwa ya mziki kwa mashabiki wake.

Akizungumza kuhusu maandalizi hayo, Meneja Mkuu wa THT, Mwita Mwaikenda alisema maandalizi yanaenda vema na mashabiki wahudhurie kwa wingi kujionea namna kituo hicho kilivyoweza kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya muziki.

‘Mpaka sasa wasanii wa THT watakaotoa burudani wako tayari, na kama mnavyojua THT utamaduni wake ni kupiga muziki kwa kutumia bendi lakini pia wasanii watakaotusindikiza ni kama Ben Paul, Mrisho Mpoto na Weusi’ alisema Mwita.

Akizungumzia wadhamini waliojitokeza kwenye shughuli hiyo, Mwita aliwashukuru Mr. Price waliowavisha wasanii wote, Mziiki.Com ya Spice Afrika walionunua tiketi 500 za tamasha kwa ajili ya wateja wao, SanMoto Pikipiki waliotoa pikipiki, Tanzania Fashion and Design Limited, Darling Hair ambao wametoa nywele kwa waimbaji wote wa kike na Clouds Media Group.

‘Tunatoa shukrani za dhati kwa wadhamini wetu, kwa kutuunga mkono katika kuadhimisha miaka kumi ya kuleta mapinduzi katika burudani’ alisema Mwita.

Tiketi za tamasha zinapatikana maduka ya Robby One Fashion Kinondoni na Sinza, Yahya Boutique Kinondoni, Born 2 Shine Mwenge, Ofisi za Clouds, Moca City Samora Avenue, City Sports Lounge, Mr Price na THT Kinondoni.

Kiingilio ni 15,000/-  kwenye vituo hivyo na kwa wale wanaotaka za VIP ni 50,000/- na zinapatikana THT pekee yake.


Siku ya onesho pale Escape One, mlangoni kiingilio kitakuwa ni Shs 20,000/=.

Thursday, January 29, 2015

ALI KIBA AMTAMBULISHWA RASMI SAUTI ZA BUSARA

Mwenyekiti wa Bodi wa Busara Promotions, wandaaji wa tamasha la Sauti za Busara, Simai Mohammed (katikati) akiongea na wandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa mkutano wa wanahabari Jijini Dar es Salaam, juu ya tamasha la 12 la Sauti za Busara, litakalofanyika, Februari 12 hadi 15, mwaka huu, Ngome Kongwe, Zanzibar. Wengine (kushoto) ni Meneja wa tamasha hilo, Journey Ramadhani. na upande wa kulia ni Mkurugenzi wa tamasha hilo, Yusuf Mahmoud 'Dj Yusuf, akifuatiwa na msanii wa bongo fleva nchini, Ali Kiba (kulia).
Simai, Dj Yusuf na Kiba wakiwa wameunganisha mikono kwa kusalimiana ikiwa ni ishara ya Umoja na Amani, kama Kauli mbiu ya mwaka huu ya tamasha hilo inavyohimiza amani.
Ali Kiba katika 'Selfie' na Mwenyekiti wa Bodi ya Busara Promotions, Simai Mohammed, muda mfupi baada ya utambulisho wa msanii huyo juu ya kupiga shoo kwenye tamasha la 12 la Sauti za Busara, litakalofanyika Februari 12 hadi 15, Zanzibar.

Ali Kiba ahidi makubwa Sauti za Busara Februari 12
Ali Kiba atamba kufanya kweli Sauti za Busara mwaka huu
Ali Kiba kupiga shoo ya 'live' Sauti za Busara Feb 12

Na Andrew Chale
Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba ametamba kukonga nyoyo watu mbalimbali watakaojitokeza kwenye tamasha la 12 la Sauti za Busara linalotarajia kufanyika, Februari 12 hadi 15, Ngome Kongwe, Zanzubar.

Ali Kiba alieleza hayo leo Alhamisi, Januari 29. wakati wa mkutano wa ulioandaliwa na Busara Promotions, wandaaji wa tamasha hilo kubwa la Kimataifa linalofanya muziki wa 'Live',  ambapo kwa mwaka huu zaidi ya wanamuziki na vikundi 37, watatoa burudani kwenye tamasha hilo kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja, Zanzibar.

Akizungumza mbele ya wandishi wa habari, Ali Kiba alisema kwa sasa amejiandaa kutoa burudani ya aina na ambayo itakonga nyoyo kwa watu wote watakaojitokeza kushuhudia tamasha hilo.

"Hii itakuwa ni zawadi kwa watanzania wote kunishuhudia nikiimba 'live' bila kutumia 'cd' kama wafanyavyo wengine. Mimi ni mwanamuziki na nimesoma muziki hivyo nitapiga muziki wa nguvu jukwaani" alisema Ali Kiba.

Na kuongeza kuwa, kwa sasa yupo kwenye mazoezi ya muda mrefu wa kujifua na bendi maalum  kwa ajili ya shoo hiyo huku akitamba kuwa, yeye ni msanii kwani muziki aliusomea na kujifunza huko nyuma alipokuwa  katika Nyumba ya kuibua vipaji THT, ambapo alijifunza vitu vingi ikiwemo kuimba muziki wa bendi na 'live'.

Aidha, aliwaomba wapenzi na wadau wa muziki kujitokeza kwa wingi 

kushuhudia tamasha hilo kwani wasanii mbalimbali wa ndani na nje watatoa burudani ya kipekee.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi ya Busara Promotion, wandaaji wa tamasha hilo, Simai Mohammed, alisema tamasha limeweza kuongeza ajira na uchumi wa Zanzibar kwani pia limeongeza fursa za utalii.

Kwa upande wake, Meneja wa tamasha  hilo, Journey Ramadhani, alisema tamasha hilo limeweza kuongeza fursa kila mwaka ikiwemo kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania kwa asilimia 90, ambapo kwa mwaka huu wanatarajia kuwa na watendaji kazi na wa kujitolewa watakolipwa katika kusaidia tamasha hilo, zaidi ya watu 150.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa tamasha hilo, Yusuf Mahmoud 'Dj Yusuf' alisema tamasha hilo limeweza kuibua wasanii mbalimbali ikiwemo kujitangaza kimataifa.

Aidha, Dj Yusuf alieleza kuwa, tamasha la mwaka huu litaendana na kauli mbiu ya kuimiza Amani, pia wameandaa tuzo maalum na zawadi maalum kwa wasanii wa Tanzania watakaoshinda katika kutunga nyimbo za amani.

Mbali na Ali Kiba, Wasanii wengine Isabel Novella kutoka  Msumbiji, Ihhashi Elimhlophe (Afrika Kusini),   Tcheka (Cape Verde),   Diabel Cissokho (Senegal),  Culture Musical Club (Zanzibar),  Msafiri Zawose (Tanzania),   Aline Frazão (Angola),   Tsiliva (Madagascar),   Leo Mkanyia and the Swahili Blues Band (Tanzania),   Mohamed Ilyas & Nyota Zameremeta (Zanzibar),   Thaïs Diarra (Senegal / Mali / Uswisi),   Liza Kamikazi and band (Rwanda),   Erik Aliana (Cameroon),  Mpamanga (Madagascar),   Mgodro Group (Zanzibar),   Rico Single & Swahili Vibes (Zanzibar),   Zee Town Sojaz (Zanzibar),   Ifa Band (Tanzania) na wengine wengi. Maelezo zaidi yanapatikana katika www.busaramusic.org

AIRTEL YATOA MSAADA WA VITABU SHULE YA SECONDARY NANJ MONDULI ARUSHA

Meneja Mauzo wa Airtel Kanda ya Kaskazini Brighthon Majwala akikabithi vitabu kwa Afisa Elimu wa shule za sekondari halimashauri ya Monduli Bwana Shaban Kasim Mgunya kwaajili ya shule ya sekondari Nanja iliyoko Monduli mkoani Arusha. wakishuhudia ni baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Nanja.
Meneja Mauzo wa Airtel Kanda ya Kaskazini Brighthon Majwala akikabithi vitabu kwa Afisa Elimu wa shule za sekondari halimashauri ya Monduli Bwana Shaban Kasim Mgunya kwaajili ya shule ya sekondari Nanja iliyoko Monduli mkoani Arusha wakishuhudia kulia ni Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde  na kushoto ni mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Nanja Yona Lukas
Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde  akipitia kitabu na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Nanja mara baada ya Airtel kukabithi msaada wa vitabu vya sayansi kwa shule hiyo chini ya mpango wake wa Airtel shule yetu.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Nanja wakionyesha vitabu vyao mara baada ya Airtel kukabithi msaada wa vitabu vya sayansi kwa shule hiyo chini ya mpango wake wa Airtel shule yetu.

Airtel yatoa msaada wa Vitabu shule ya Secondary Nanj Monduli Arusha
·         Chini ya mpango wake wa shule yetu, shule za sekondari manyara, Moshi na Tanga kupokea msaada huo mwenzi huu
WANAFUNZI na walimu wa shule ya Sekondari Nanja wamepokea msaada wa vitabu kutoka Airtel, Msaada utakaoweza kuchangia katika kutatua tatizo la uhaba wa vitabu shule ni hapo.

Akitoa taarifa ya shule , Mkuu wa shule ya sekondari ya Nanja Bwana Yona luka alisema” shule yetu ina jumla ya wanafunzi 549 na walimu 32,  matokeo ya shule ya kidato cha nne yanakuwa kila mwaka ufaulu wa asilimia 71% pamoja na kukua kwa kiwango cha ufaulu bado shule inachangamoto nyingi ikiwemo uhaba wa vitabu na walimu.

Kwa sasa uwiano  wa vitabu vya sayansi ni kitabu 1 kwa wanafunzi 5 wakati kwa vitabu vya sayansi ya jamii uwiano ni kitabu 1 wanafunzi 30. Tunafurahi sana kupokea vitabu hivi toka Airtel kwani msaada huu umekuja kwa wakati muafaka”

Akiongea wakati halfa hiyo fupi ya kukabithi vitabu , Afisa Elimu wa shule za sekondari halimashauri ya Monduli Bwana Shaban Kasim Mgunya alisema” napenda kuwashukuru sana Airtel kwa kufikisha msaada huu wa vitabu kwa sekondari hii ya Naja , vitabu hivi vya sayansi havitachangia kuongeza kiwango cha ufaulu tu bali vitawahamasisha wanafunzi wengi kujiunga na masomo ya sayansi. Natoa wito kwa walimu kuwapatia wanafunzi vitabu hivi wavisoma ili kuwajengea wanafunzi hawa tabia ya kusoma vitabu. 

Nawahasa wanafunzi kuvitunza vitabu ili viweze kutumika na wanafunzi wengi zaidi shuleni hapa Aliongeza kwa kusema” shule imeweza kujenga maktaba lakini tunayochangamoto ya uhaba wa vifaa vya maktaba , nachukua fulsa hii kuwaomba Airtel waendelee kutusaidia kwa kuchangia vifaa vya mahabara na kuwezesha masomo ya sayansi ya vitendo”

Akiongea kwa niaba ya Airtel Meneja wa kanda ya kaskazini Brighton Majwala alisema”wote tunatambua tatizo la uhaba wa vitabu katika shule za sekondari ambapo hali halisi haiendani namahitaji, uwiano wa kitabu 1 ni kwa wanafunzi 10. Kwa kuliona hilo Airtel tumejikita na kushirikiana na serikali katika kuhakikisha tunatutua changamoto hii na kuongeza kiwango cha ubora wa elimu nchini.  

Natoa wito kwa wanafunzi wa Nyala kuzitumia vitabu hivi vizuri na kuboresha kiwango cha ufaulu.

Kwa upande wa wanafunzi wameishukuru Airtel kwa kuboresha elimu na kusema vitabu hivi vitawasaidia kuongeza ujuzi katika masomo ya sayansi na kufanya vizuri zaidi.

Halfa ya kukabithi vitabu katika shule ya sekondari Nanja ilimalizika kwa zoezi la kupanda miti ambapo walimu, wanafunzi na Airtel walishiriki katika kuboresha mazingira ya shule.

Airtel chini ya mpango wake wa Airtel Shule yetu mpaka sasa imezifikia shule zaidi ya 1300 nchini, shule nyingine katika kanda ya kaskazini zitakazofaidika na vitabu hivi ni pamoja na  Manyara, Moshi na Tanga na shule nyingine katika maeneo mbalimbali ya nchi nazo zitaendelea kupata msaada huu wa vitabu

MSHINDI WA PILI "MTOKO WA MBUGANI" AKIVINJARI NDANI YA HIFADHI YA SERENGETI

Mshindi wa pili wa shindano la “Tutoke na Serengeti” Bw.Deogratias Peter Mbogole (kushoto) akiwa na rafiki yake Goodluck Shirima(kulia) ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti kukamilisha mtoko wao wa siku mbili ndani ya hifadhi hiyo...Hapa ni Tarangire river view waliposimama kujionea kundi kubwa la tembo wakivuka barabara. Deo aliibuka mshindi mara baada ya kushiriki kwenye shindano linaloendelea la “Tutoke na Serengeti” linaloendeshwa na SBL kwa ushirikino na BPESA
Mshindi wa mtoko wa mbugani Bw. Deogratias Peter Mbogole akiangalia kundi la simba ndani ya hifadhi hiyo waliposimama “Small Serengeti plains”  ambapo wanyama hao wanaonekana kwa wingi. Safari hii inadhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti. Deo aliibuka mshindi mara baada ya kushiriki kwenye shindano linaloendelea la “Tutoke na Serengeti” linaloendeshwa na SBL kwa ushirikino na BPESA
Mshindi wa mtoko wa mbugani Bw. Deogratias Peter Mbogole (kushoto) akiwa na rafiki yake Goodluck Shirima(kulia) wakitumia darubini kuangalia makundi makubwa ya viboko ndani ya “Hippo pool view”-Manyara ambapo wanyama hao wanaonekana vizuri na kwa wingi. Deo aliibuka mshindi mara baada ya kushiriki kwenye shindano linaloendelea la “Tutoke na Serengeti” linaloendeshwa na SBL kwa ushirikino na BPESA.
Mshindi wa mtoko wa mbugani Bw. Deogratias Peter Mbogole(kushoto) akiwa na rafiki yake Goodluck Shirima(kulia) walipoanza safari yao ya utalii wa siku 2 ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti. Deo aliibuka mshindi mara baada ya kushiriki kwenye shindano linaloendelea la “Tutoke na Serengeti” linaloendeshwa na SBL kwa ushirikino na BPESA.
Mshindi wa mtoko wa mbugani Bw. Deogratias Peter Mbogole(kulia) na rafiki yake Goodluck Shirima (kushoto) wakiangalia tembo wanaovuka barabara kwa ukaribu zaidi ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti walipoanza mtoko wao wa siku mbili ndani ya mbuga hiyo. Deo aliibuka mshindi mara baada ya kushiriki kwenye shindano linaloendelea la “Tutoke na Serengeti” linaloendeshwa na SBL kwa ushirikino na BPESA
“Tutoke na Serengeti”
“Tutoke na Serengeti”