ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 14, 2020

KAMISHNA WA JESHI LA POLISI, CP SABAS AMEPOKEA MSAADA WA PIKIPIKI 10 KUTOKA KAMPUNI YA KINGLION ZITAKAZOTUMIKA KATIKA SHUGHULI MBALIMBALI ZA POLISI.


 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas, akisalimiana  na mwakilishi wa Kampuni ya utengenezaji wa pikipiki aina ya Kinglion baada ya kuwasili Makao Makuu ya Polisi Jijini Dar Es Salaam walizozitoa kwaajili yakusaidia shughuli mbalimbali za Jeshi la Polisi ikiwemo Doria. (Picha na Jeshi la Polisi)
 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas, akiwa amepanda pikipiki moja kati ya 10 zilizotolewa  na Kampuni ya Kinglion ndani ya Jeshi la Polisi kwaajili ya shughuli mbalimbali za Jeshi. (Picha na Jeshi la Polisi)
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas, wa saba kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Jeshi la Polisi Makao Makuu pamoja na wawakilishi kutoka kampuni ya Kinglion baada ya kukamilika zoezi zima la makabidhiano ya kupokea  pikipiki 10 aina ya Kinglion zitakazotumia Mkoani Dodoma kwaajili ya shughuli za Jeshi la Polisi (Picha na Jeshi la Polisi)

WAFNDISHENI UELEDI WAPELELEZI - MASAUNI.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(kulia),akiangalia moja ya darasa linalotumika kufundishia wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi,wapili kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akikagua dawati katika  moja ya darasa linalotumika kufundishia wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi,wapili kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Salum Hamduni(kulia) baada ya kukagua moja ya chumba vinavyotumika kutoa huduma ya malazi kwa   wanafunzi katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Polisi baada ya kuwasili  katika Shule ya Polisi Tanzania wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo chuoni lengo kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma zinazotolewa na Jeshi la Polisi.
Na Mwandishi Wetu
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni ameutaka uongozi wa Shule ya Polisi Tanzania kuwafundisha ueledi wapelelezi ili kuweza kupunguza msongamano wa mahabusu na kesi ambazo zinasababishwa na upelelezi usio na kiwango.
Masauni ameyasema hayo mkoani Kilimanjaro wakati wa ziara ya kutembelea Shule ya Polisi Tanzania lengo ikiwa kusisitiza ufundishaji makini ili jamii iweze kufaidika na huduma za Jeshi la Polisi.
“Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli alipokua akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria aligusia suala la wapelelezi kuwa chanzo cha mlundikano wa mahabusu katika magereza yetu na mimi hii leo nimetoka gereza la Arusha nimeongea na wafungwa na mahabusu nao wanalalamikia upelelezi wa kesi zao kupindishwa na mbaya zaidi wengine wamehukumiwa vifungo kwa ajili ya upelelezi usio makini.Ni tatizo kubwa haiwezekani Rais huyu alalamike kila siku sasa maagizo ya serikali kwa chuo hiki jitahidini kupika vizuri wapelelezi wenu vizuri,tumpumzishe Rais wetu ana mambo mengi,timizeni tu wajibu wenu”amesema Masauni
Akizungumza katika ziara hiyo Kaimu Kamandanti Kamishna Msaidizi Omar Khamis Omar amesema wamechukua maelekezo ya serikali na wanaahidi kuyafanyia kazi ili yaweze kuleta tija huku akitaja idadi ya wanafunzi waliopo shuleni hapo wakisomea fani mbalimbali.
“Shule yetu kwa sasa ina wanafunzi 856 kati yao wanaume 725 na wanawake ni 131 ambao wako katika mafunzo mbalimbali na wote wanaendelea vizuri na masomo” amesema Kamishna Msaidizi Omar
Katika ziara hiyo Naibu Waziri Masauni alipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya shule hiyo ikiwemo sehemu za kulala,madarasa,uwanja wa paredi,vyumba vya komputa na ukarabati bwalo la chakula.

Thursday, February 13, 2020

NI HUZUNI KUU NA VILIO MOTO WATEKETEZA MITAJI YA MACHINGA MAKOROBOI


Moto uliozuka saa 9 alfajiri ya Jumatano Februari 12, 2020 katika soko la Makoroboi mkoani Mwanza umeacha simanzi kwa wafanyabiashara kutokana na bidhaa zao kuteketea. Moto huo uliowaka kwa dakika takribani 45  ulizimwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na wananchi, hakuna bidhaa zilizookolewa. Baadhi ya wafanyabiashara wamekiri kuwa biashara walizokuwa wakifanya katika eneo hilo zilikuwa msingi wa kuendesha maisha yao, huku Timoth Clemence akisema kuwa taarifa za kuzuka kwa moto huo alizipata baada ya kupigiwa simu na kusababisha apate mshtuko bila kujua la kufanya. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana,  Dk Philis Nyimbi amethibitisha amewataka wafanyabiashara kuwa watulivu wakati vyombo vya dola vinaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo. Naye Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Jumanne Muliro amezungumza. Bidhaa za wafanyabiashara wadogo 159 zimeteketea huku mabanda 65 nayo yakiteketea. #JembeFm #JembeHabari #KAZINANGOMA #DriveMix @jembefm

Wednesday, February 12, 2020

"RATIBA YA UCHAGUZI BADO" YASEMA NEC


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa, haijatoa wala kutangaza ratiba yoyote ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2020.

Taarifa iliyotolewa na NEC kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa, utaratibu wa Tume ni kupanga ratiba ya uchaguzi mara baada ya kuvunjwa kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tukio ambalo bado muda wake haujafika.

Ufafanuzi huo wa NEC umetolewa kufuatia kuwepo kwa taarifa katika mitandao mbalimbali ya kijamii zinazopotosha taarifa ya tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo.

NEC imewaomba Wananchi kupuuza taarifa kuhusu tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi zinazosambazwa katika mitandao hiyo ya kijamii kwa kuwa si rasmi, na kwamba kitendo hicho kinafanyika kwa nia ovu.

Kwa mujibu wa NEC, ratiba ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu itatolewa muda utakapowadia kulingana na matakwa ya kisheria.

MASAUNI AWASILI JIJINI ARUSHA KWA ZIARA YA KIKAZI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (kulia), kwa ziara ya kikazi itayohusu taasisi zilizopo chini ya wizara.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akizungumza kuhusu masuala ya Ulinzi na Usalama na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo(kulia), baada ya kuwasili jijini Arusha kwa ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiwa katika picha ya pamoja na  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo(kulia),baada ya kumaliza mazungumzo yaliyohusu Ulinzi na Usalama. Naibu Waziri yuko  jijini Arusha kwa ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Tuesday, February 11, 2020

JEH MBEYA CITY HII LEO KUITIA MCHANGA KEKI YA YANGA?


Klabu ya soka ya yanga leo inasheherekea miaka 85 huku siku yao hii muimu itakuwa kibaruani na timu ya mbeya City mchezo utakaochezwa uwanja wa taifa saa 1:00 usiku.

ALIYECHANA QURAN TUKUFU AFUKUZWE KAZI MOJA KWA MOJA.

Rais  wa muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  amemuagiza waziri  Suleimani Jafo kumfukuza kazi moja kwa moja mtumishi aliyechana Quran tukufu kilosa mkoani Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa leo akiwa,Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam wakati akizindua jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni na Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni.


“Juzi nilkuwa namsikiliza Waziri Jafo yupo Mtumishi alichana Quran nafurahi umemsimamisha kazi, lakini naagiza afukuzwe moja kwa moja, ashinde kesi asishinde ila aondoke, muandikie barua ya kumfukuza, akitoka huko atajua mwenyewe atakakoyatafuta Maisha”- JPM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 11, Febuari, 2020 anazindua Jengo la Manispaa ya Kigamboni na Jengo la Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni katika Eneo la Gezaulole Kigamboni Jijini Dsm.

Huduma ya Fahari Kilimo ni mkombozi kwa wakulima wa Pamba- RC Mtaka

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza kwenye Kongamano la Wadau wa Sekta ya Kilimo lililoandaliwa na Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Shirika la Uwezeshaji Sekta ya Kilimo (PASS).
Mkurugenzi wa Mikopo Benki ya CRDB, Xavery Makwi akizungumza kwenye kongamano hilo.
Meneja wa Kanda ya Ziwa Benki ya CRDB, Lusingi Sitta akielezea fursa mbalimbali zinazotolewa na Benki ya CRDB ikiwemo mikopo yenye riba nafuu kwa wakulima wa Pamba.
Mmoja wa wadau wa zao la Pamba akichangia mada wakati wa Kongamano hilo.
Mmoja wa wadau wa zao la Pamba akichangia mada wakati wa Kongamano hilo. 
Mkurugenzi wa kampuni ya uchenjuaji Pamba Nsagali Ltd, Gungu Silanga akielezea namna ambavyo kampuni hiyo imenufaika na mikopo ya uwezeshaji kwa viwanda inayotolewa na Benki ya CRDB. 
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima akitoa salamu zake wakati wa kongamano hilo.
Afisa Kilimo wa Wilaya ya Bariadi, Golang'a Ally akitoa taarifa kuhusu kilimo cha Pamba katika wilaya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga akichangia hoja wakati wa kongamano hilo.
Wakulima wa zao la Pamba wakiendelea na zoezi la kujaza fomu kwa ajili ya kufungua akaunti CRDB.
Wakulima wakijisajili ili kumiliki akaunti CRDB.
Washiriki wakifuatilia kongamano hilo.
Wadau wa kilimo wakifuatilia kongamano hilo. 
Na Mwandishi Wetu, Simiyu
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amesema akaunti ya Fahari Kilimo kupitia Benki ya CRDB imekuwa mkombozi mkubwa kwa wakulima wa Pamba kanda ya ziwa. Mtaka amesema huduma zinazoambatana na akaunti ya Fahari Kilimo ikiwemo mikopo ya pembejeo na zana za kilimo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza tija kwa wakulima pamoja na kuboresha mnyororo wa thamani wa kilimo nchini. 

Mtaka aliyasema hayo Februari 10, 2020 wakati wa kongamano la wadau wa sekta ya kilimo lilioandaliwa na Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Shirika la Uwezeshaji Sekta ya Kilimo (PASS). Akitoa hotuba yake katika kongamano hilo ambalo lilihusisha mikoa ya Simiyu, Mwanza na Mara, Mtaka aliipongeza Benki ya CRDB kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kuboresha kilimo cha Pamba. 

"Sote tunafahamu changamoto ambayo tuliipata katika zao la Pamba mwaka jana, lakini Benki ya CRDB ilionyesha uzalendo wa hali ya juu kwa kushirikiana na Serikali kutoa mikopo kwa wanunuzi wa Pamba lakini pia kutafuta masoko ndani na nje ya nchi, hili ni jambo la kupongezwa sana" alisema Mtaka. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uendelezaji zao lao la Pamba, Adam Malima alisema Serikali inaridhishwa na jitihada kubwa zinazofanywa na Benki hii ya CRDB katika kuboresha sekta ya kilimo nchini. Malima alisema Serikali ya Awamu ya Tano imejidhatiti katika kuhakikisha zao la Pamba linaongezeka thamani ili kuboresha maisha ya wakulima wa Pamba.

"Niwaombe wakulima wetu wa Pamba tuendelee kutumia fursa hizi zinazotolewa na Benki yetu ya CRDB, tukifanya hivyo tutaweza kuongeza uzalishaji na kuongeza thamani ya kilimo chetu. Serikali ipo tayari kufanya kazi bega kwa bega na Benki ya CRDB kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea" alisema Mtaka. 

Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi alisema akaunti ya Fahari Kilimo ni sehemu ya mkakati mpana wa benki kuwahudumia wakulima kwa ukaribu zaidi kwa kuzingatia mahitaji yao. Makwi alisema mpaka sasa wakulima zaidi ya 30,000 tayari wameshajiunga na akaunti ya FahariKilimo na hivyo kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Benki ya CRDB. 

"Akaunti hii ya FahariKilimo hufunguliwa bure kabisa na hakuna gharama zozote za uendeshaji wa akaunti kwa mkulima, tukilenga kumpa mkulima unafuu wa kupokea malipo yake pindi anapopokea malipo baada ya kuuza mazao" alisema Makwi. 

Makwi alisema wakulima ambao wamejiunga na Fahari Kilimo wameweza kunufaika na mikopo ya pembejeo, mikopo ya zana za kilimo, mikopo ya ujenzi wa maghala, pamoja na uunganishwaji na masoko. "Uwezeshaji huu tunaufanya pia katika uwekezaji katika viwanda vya uchenjuaji Pamba" alisema Makwi.

Makwi alisema baadhi ya viwanda vilivyonufaika na uwezeshaji huu unaofanywa na Benki ya CRDB ni pamoja na Gaki Investment Company Ltd, Fresho Investment Company Ltd, Aham Investment Company Ltd, Nsagali Company Ltd na Birchand Oil Mill Limited. 

Naye Meneja wa PASS Kanda ya Ziwa, Langelika Kalebi alisema shirik a hilo litaendelea kushirikiana na Benki ya CRDB kuwawezesha wakulima na vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) wa Pamba hususani katika kuandaa mpango wa kilimo na uongezaji wa thamani wa dhamana ikiwa ni vitu muhimu vinavyohitajika wakati wa uombaji wa mikopo ya pembejeo, zana za kilimo na maghala. 

Akizungumza kwa niaba ya wakulima wa Pamba, Medard Marko ambaye ni mkulima wa Pamba kutoka Bariadi vijijini aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mkombozi kwa wakulima kupitia akaunti ya Fahari Kilimo. "Kupitia akaunti hii tumekuwa tukipata mafunzo ya mara kwa mara juu ya uboreshwaji wa kilimo chetu, lakini pia tumekuwa tukiunganishwa na huduma za mikopo ya pembejeo, zana za kilimo kama matrekta na ujenzi wa maghala kupitia AMCOS" alisema Marko. 

Takwimu zinaonyesha Mkoa wa Simiyu unaongoza nchini kwa uzalishaji wa zao la Pamba, akizungumza katika kongamano hilo Afisa Kilimo wa Wilaya ya Bariadi, Golong’a Ally alisema mwaka jana Mkoa huo ulizalisha zaidi ya kilo milioni 160 za Pamba. 

Monday, February 10, 2020

Rais mstaafu Mwai Kibaki afika kumpa heshima zake hayati Moi


Na wakenya walipokuwa wakitiririka katika majengo ya bunge kumtazama na kumpa buriani rais wa pili wa taifa hili, rais mstaafu mwai kibaki alifika kumuomboleza mtangulizi wake. Enock sikolia anaeleza uhusiano wa kisiasa kati marais hao wastaafu.