ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 17, 2022

JUMLA YA VIJANA 300 KUNUFAIKA NA MRADI WA IMARIKA KIJANA MKOANI IRINGA.

 

Mratibu wa mradi wa imarika kijana Gift Mafue kutoka shirika la LYRA in Afrika akiongea na vijana walikuwa wanapata mafunzo ya vitendo namna gani ya kufuga kwa vitendo.
Vijana wakiwa wanajifunza namna ya kufuga kwa tija katika Banda la Nguruwe ili kuwakomboa kiuchumi
Vijana wakiwa wanajifunza namna ya kufuga kwa tija katika Banda la Nguruwe ili kuwakomboa kiuchumi

Na Fredy Mgunda, Iringa.
Jumla ya vijana 300 kutoka vikundi 14 mkoani Iringa wamewezeshwa na Mradi wa Imarika kijana ulio chini ya Shirika lisilo la kiserikali la LYRA in Afrika kuzitambua fursa mbalimbali ufugaji kwa ajili ya kuwakomboa kimaisha na kuwasaidia kuliondoa kundi hilo kubwa kuishi maisha ya vijiweni.

Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara ya kuwatembelea wafungaji mbalimbali waliofanikiwa mratibu wa mradi wa imarika kijana,Gift Mafue alisema kuwa jitihada zaidi za kuwawezesha vijana kutambua fursa na kujiajiri zinaitajika ili kuondosha kundi kubwa la vijana kusalia vijiweni na kujihusisha na vitendo viovu.

Mafue alisema kuwa wimbi la vijana wanaojihusisha na Uhalifu limechangiwa na changamoto ya ukosefu wa ajira pamoja na ufinyu wa maarifa ya utambuzi wa fursa za kujiajiri.

Alisema kuwa shirika la Lyra in Afrika kwa kutambua changamoto hiyo wamejikita katika uwezeshaji wa vijana katika wilaya ya Iringa na kilolo mkoani Iringa kutumia fursa zinazowazunguka ambapo sasa asilimia 81 ya vijana 1900 wamejiajiri

Mratibu huyo wa mradi wa Imarika kijana kutoka shirika la Lyra in Afrika alisema hii ni awamu ya pili uwezeshwaji wa vijana hao kutoka wilaya ya kilolo na Iringa.

Mafue alisema kuwa lengo kuu la mradi huo ni kuwainua vijana na kuimarisha uchumi wao kwa ujumla

Katika awamu hii ya pili ya mradi wa imarika kijana jumla ya vikundi 14 vimenufaika na moingoni mwao wamepata fursa ya kutembelea shughuli za mfugaji wa kuku wa asili, Nguruwe na kuku wa kisasa na ufugaji wa Nyuki katika maeneo mbalimbali ya mkoani Iringa

Hashim Deus na Rosemary Sanyagi  ni vijana wanufaika katika ziara hiyo ya ujasiriamali walisema kuwa wanalishukuru shirika lisilo la kiserikali la LYRA in Afrika kwa kuwapatia fursa mbalimbali za kujifunza miradi ya ufugaji

Walisema kuwa wataitumia fursa hiyo kuhakikisha wanafuga kisasa na kufanikiwa kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa vikundi.

Naye Mwenyeji katika ziara hiyo,Hosea Mtewele ambaye ameeleza namna alivyoanza ufyugaji akiwa na kuku watano nah ii leo tunapozungumza akiwa na kuku zaidi ya efu tatu huku uzalishaji na biashara ikiwenelea kushika kasi na kuchoche kipato chake

Mtewele alisema kuwa analipongeza shirika la lyra in afrika katika kusaidia vijana kuwa ni hatua kubwa itakayochochea kasi ya maendeleo vijijini kwa kuwa vina vijana wengi watatambua fursa zilizopo katika maeneo yao na kuanzisha miradi itakayosisimua uchumi binafsi na wa kijiji kwa ujumla.

Friday, December 16, 2022

UKEREWE HAIJAWAHI KUWA NA HOSPITALI YENYE ICU

 NA ALBERT G. SENGO/UKEREWE

Halmashauri ya wilaya ya ukerewe mkoani mwanza imefanikiwa kuokoa shilingi millioni 74 kwenye mradi wa ujenzi wa Jengo la wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum(ICU)katika Hospitali ya BWISYA iliyopo kwenye kisiwa cha Ukara wilayani humo. Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo DOKTA ALEX SIBONA amesema kuwa fedha hizo ni kati ya shilingi millioni 251 zilizotolewa na serikali kuu kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa mradi huo. Ujenzi wa mradi wa ICU katika hospitali ya BWISYA umefikia hatua za mwisho kukamilika ambapo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya ukerewe EMMANUEL SHELEMBI amewaasa wananchi kuendelea kuunga mkono Jitihada za serikali ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Wilaya ya ukerewe kwa sasa haina huduma ya ICU na Hospitali ya BWISYA inatarajiwa kuwa ya kwanza kutoa huduma hiyo.

MKENYA AISHIYE MAREKANI AKUTWA AMEFARIKI CHUMBANI KWAKE.


 Usiku wa Jumamosi ya Desemba 10, Kevin Odero alikuwa nyumbani kwa wazazi wake huko Connecticut, Marekani, na dada yake mdogo alipokata roho ghafla. Kulingana na dadake, mwili wa Kevin tayari ulikuwa umebadilika na kuwa rangi ya zambarau polisi walipofika. 

Wakati huo babake kijana huyo mwenye umri wa miaka 20 alikuwa amesafiri hadi Kenya na kuwaacha, bila kujua kwamba mauti yangelimfika mwanawe mpendwa. 

Dadake Kevin Elizabeth Odero alimwambia Hillary Lisimba wa TUKO.co.ke kwmaba dada yao aligundua mwili wa kaka yao ingawaje kwa kuchelewa. 

Kwa mujibu wake, mwili wa kijana huyo ulikuwa tayari umegeuka zambarau na juhudi za kupigia simu ya 911 ya huduma za dharura kuja kumkimbiza hospitalini hazikuzaa matunda. 

 “Walijaribu kumuamsha lakini maafisa wa afya walithibitisha kuwa tayari alikuwa amefarik dunia, ndiposa polisi walipochukua maiti ili kufanya uchunguzi,” alieleza. 

Elizabeth alifichua kuwa marehemu alikuwa na umri wa miaka 20, alizaliwa na kukulia Nairobi lakini alijiunga na familia yake Marekani mnamo 2020. 

Wakati wa kifo chake, alikuwa amemaliza tu diploma yake ya shule ya upili na alikuwa akifanya kazi ya muda huko Amazon. 

Mojawapo ya mipango ya Kevin kwa mwaka ujao ilikuwa kujiunga na chuo cha ufundi mwezi Januari na kuendelea na kozi ya ufundi wa mabomba. 

"Mwili wake ulichukuliwa na polisi jana na kwa sasa umelazwa katika makafani moja huko Massachusetts," alisema Elizabeth. 

Familia yake kwa sasa inajaribu kuchangisha dola 18,000 (KSh 2.2 milioni) ili kuwezesha mwili wake kurejeshwa nchini Kenya kwa mazishi. 

 Katika michakato mtandaoni iliyolenga kusaidia kuchangisha fedha, Kevin alisifiwa kama "mwana mpendwa wa Joseph Odero na kaka wa Virginia wa New Haven Connecticut na Adrian Amani."

 "Tafadhali mkumbuke Joseph na binti yake katika maombi na ujisikie huru kuwaambia marafiki wengine na kuwaongeza kwenye kikundi," sehemu ya chapisho hilo ilisema. 

Elizabeth alifichua kwamba familia hiyo itaandaa misa ya wafu Desemba 23 kisha mwili utasafirishwa hadi nchini Kenya kwa mazishi. 

MREMBO HUYU ANASIKITIKA KUKOSA MPENZI WA KUMUOA.

 


Kisura ambaye ni mama wa mtoto mmoja, Ayishatu Adams ametangaza mitandaoni kwamba anatafuta mume wa kumuoa. 

Katika video ya kusikitisha kwenye TikTok, mwanafunzi anayesomea uuguzi alifichua kuwa atakuwa na umri wa miaka 35 mnamo 2023 na bado hana mchumba. 

Ayishatu alilalamika kwamba wanaume wanaomrushia ndoano huhepa baadaye kwani hawataki kuchukua majukumu ya kumlea mtoto wake. 

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 34 alifichua kwamba jambo hilo linamtia huzuni. 

"Nitakuwa na umri wa miaka 35 mwakani na bado sijaolewa kwa sababu nina mtoto. Mwanaume yeyote anayekuja kwangu anasema hawezi kujukumikia kisicho chake." 

Haya ni baadhi ya maoni ya watu kuhusiana na kilio cha kidosho huyo; 

Abbati SK alisema: "Hao wanaume kamwe hakupendi wala kukuthamini ndiyo maana wanakuhepa. Mtu sahihi atakuja na atakuthamini."

 Abubakari Rahinat683 alisema: ''Mwanamume sahihi na mcha-Mungu atakupata na hakuna haraka maishani. Mwenyezi Mungu anapanga zawadi maalum kwa ajili yako." 

korkor_1992 alisema: ''Zingatia sana kumlea mtoto wako kwani yeye ndiye mtu pekee ambaye atakuwepo kwa ajili yako kila wakati." zee-money alisema: "Usifadhaike wanaume wote unaokutana nao sio wako Mungu atakutendea haki." 

BENKI YA CRDB, IFC ZAKUBALIANA MAENEO SITA YA USHIRIKIANO.

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dk Ally Laay (watatu kulia), Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kulia), na Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wanne kulia) wakiwa katika kikao na Mkurugenzi wa IFC anayesimamia ushirikiano na Taasisi za Fedha Duniani, Tomasz Telma (wapili kushoto), na Mwakilishi Mkazi wa IFC nchini Tanzania, Frank Ajilore (wakwanza kushoto) walipokutana kujadili ushirikiano baina ya taasisi hizo jijini Washington Marekani jana 14 Desemba 2022. Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (watatu kushoto), na Mkuu wa Kitengo cha Hazina Benki ya CRDB, Joseph Maji.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kushoto), na Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa IFC anayesimamia ushirikiano na Taasisi za Fedha Duniani, Tomasz Telma (wapili kulia), na Mwakilishi Mkazi wa IFC nchini Tanzania, Frank Ajilore (wakwanza kushoto) walipokutana kujadili ushirikiano baina ya taasisi hizo jijini Washington Marekani jana 14 Desemba 2022.
---
Washington, Marekani 15 Desemba 2022 - Benki ya CRDB na Shirika la Kimataifa la Fedha la Benki ya Dunia (IFC) wamekubaliana maeneo sita mahususi ya ushirikiano katika juhudi zao za pamoja za kukuza ujumuishi wa kifedha nchini Tanzania na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yamefikiwa na ndio watendaji wakuu wa taasisi hizo mbili wakati wa mkutano wao huko Washington uluofanyika sambamba na Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika na Marekani.

Katika mkutano huo, ujumbe wa Benki ya CRDB uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk Ally Laay, Makamu mwenyekiti, Prof Neema Mori, na Mkurugenzi Mtendaji wa Group, Abdulmajid Nsekela, huku IFC ikiwakilishwa na Mkurugenzi anayesimamia ushirikiano na Taasisi za Fedha Duniani, Tomasz Telma.

IFC ni mshirika wa muda mrefu na wa kimkakati wa Benki ya CRDB na imekuwa na jukumu muhimu katika kusaidia mkakati wa benki tangu 2014.

“IFC imekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya Benki ya CRDB katika kipindi cha miaka minane iliyopita na katika kufanikisha utekelezaji wa mkakati wetu wa miaka mitano ambao unamalizika mwaka huu,” alisema Nsekela katika taarifa yake iliyowasilishwa kwa vyombo vya habari jijini siku ya Jumatano.

Alisema mkutano wa Washington ulilenga kuwaleta pamoja viongozi wakuu wa taasisi hizo mbili ili kujadili maeneo ya ushirikiano na uungaji mkono.

“Tumekubaliana kushirikiana katika masuala yanayohusu ufadhili wa shughuli za wanawake na vijana; ufadhili wa miundombinu nchini Tanzania, Burundi na DRC, pamoja na kusaidia upanuzi wa huduma za Benki yetu katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini,” Bw Nsekela alisema.

Taasisi hizo mbili, alisema pia zilikubaliana kushirikiana katika ufadhili wa miradi ya mazingira, kilimo biashara, pamoja na kuijengea uwezo Benki ya CRDB katika kubuni na kusimamia miradi ya ufadhili kiuchumi.

Katika maelezo yake wakati wa mkutano huo, Telma alielezea kwa kina uzoefu wa IFC katika kufadhili miradi nchini Tanzania na akabainisha kuwa nchi ina fursa nyingi za kiuchumi, huku akipongeza jitihada zinazofanywa na serikali katika kufungua uchumi.

Alieleza kwa kina uhusiano wa IFC na Benki ya CRDB, na kuipongeza benki hiyo kwa utendaji mzuri kulinganisha na taasisi nyengine za kifedha.

Telma alisema kwa kuwa IFC na Benki ya CRDB wamekuwa wakifanya kazi pamoja kwa miaka mingi, ana matumaini kuwa majadiliano hayo yatafungua fursa mpya za ushirikiano zaidi kati ya taasisi hizo mbili.

Katika mada yake katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alieleza kuwa Benki ya CRDB ina mizania ya Sh10.9 trilioni na mtaji wa Sh1.4 trilioni. Benkin hiyo hiyo pia inajivunia kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za kifedha kupitia njia mbadala na kuchochea ukuaji wa kiuchumi.

Ikiwa na CRDB Wakala zaidi ya 25,000, na huduma mdadala za kidijitali ikiwamo SimBanking, SimAccount, pamoja na ATM za kubadilisha fedha, asilimia 93 ya miamala ya Benki ya CRDB inafanyika nje ya tawi.

Kutokana na ufanisi huo, mwaka 2021 faida halisi ya Benki ya CRDB ilipanda hadi Sh268 bilioni kutoka Sh36 bilioni pekee mwaka 2017 huku faida ya jumla ya miezi tisa ya kwanza ya mwaka huu 2022 wa ikifika Sh257 bilioni.

Benki hiyo imerekodi amana za Sh7.672 trilioni hadi robo ya tatu ya 2022, kutoka Sh4.326 trilioni zilizosajiliwa mwishoni mwa 2017. Vile vile, Benki ya CRDB ilikuwa imefanya uwezeshaji wa mikopo ya jumla ya Sh6.244 hadi kufikia Septemba 30, 2022, kutoka Sh2.894 trilioni mwishoni mwa 2017.
Aidha, Mapato ya Mtaji yameimarika kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, benki pia imeweza kudhibiti viwango vya Mikopo Chechefu, Uwiano wa Gharama kwa Mapato kufikia viwango vinavyohitajika na Benki Kuu ya Tanzania.

Wakati matayarisho ya utekelezaji wa mkakati wa miaka mitano ijayo (2023 hadi 2027) yakiendelea, Nsekela amesema matarajio ya benki hiyo ni kwamba miaka mitano ijayo itashuhudia kipindi kingine cha ukuaji katika viashiria vyote muhimu vya utendaji.

“Tumetumia miaka 5 iliyopita kuboresha mifumo yetu ya utendaji na utuaji huduma kwa wateja, lakini pia tumejenga msingi sahihi wa kukuza biashara na kuongeza thamani kwa wadau wetu. Mkakati huu mpya unasisitiza katika kuijenga Benki bora zaidi kiutendaji na kuwekeza katika ubunifu wa huduma na bidhaa tukilenga kuboresha maisha ya watu na uchumi kwa ujumla,” alisema.

Tuesday, December 13, 2022

BIBI HARUSI ASHANGAZA KUVALIA GAUNI JEUSI KWENYE HARUSI YAKE.

Bibi harusi kutoka Nigeria kwa sasa anavuma kwenye mitandao ya kijamii baada ya picha zake za harusi kusambaa mtandaoni.


Dasplang Rinset Lisa aliamua kubadilisha tamaduni ya kuvalia gauni jeupe kwenye harusi na kuvaa gauni jeusi.


 Katika picha hizo, bibi harusi huyo aliyetambulika kwa jina la Dasplang Rinset Lisa, aliamua kubadilisha tamaduni ya kuvalia gauni jeupe kwenye harusi na kuvaa gauni jeusi na alionekana kupendeza ndani yake.


Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Lisa alifichua kwamba watu wengi walimuuliza maswali mengi kuhusu kwa nini aliamua kuvaa nguo nyeusi siku ya harusi yake.

 

“Nilipata maswali mengi kuhusu kwa nini nilichagua kuvaa gauni jeusi kwenye harusi yangu.

Sawa nina majibu mengi ya maswali, hili nitaandika baadaye, lakini kwa sasa kuna mtu yeyote anaweza kuniambia kwa nini atapendelea gauni jeupe na kwa nini asipende rangi nyingine yoyote ya mavazi?” alimaka.

TALIA: WANAWAKE WATATU WAUAWA KWA RISASI KATIKA MGAHAWA


Inadaiwa kuwa mtuhumiwa wa mauaji hayo aliingia katika mgahawa uliopo Jijini Rome na kufyatua risasi ambazo pia zilijeruhi wengine wanne huku mmoja akiwa kwenye hali mbaya kiafya


Mtuhumiwa ambaye ana umri wa miaka 57, amekamatwa baada ya kuzidiwa nguvu na raia waliopambana kumdhibiti


Mmoja kati ya waliouawa ni Nicoletta Golisano, huyu ni rafiki wa Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni.

Monday, December 12, 2022

TMDA YAWAPIGA MSASA WAKAGUZI WA DAWA NA VIFAA TIBA MKONI IRINGA.

 

Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kanda ya kati Sonia Mkumbwa akitoa mafunzo kwa wakaguzi wa Dawa na vifaa tiba mkoani Iringa
Viongozi mbalimbali wa mkoa wa Iringa wakiongozwa na mganga mkuu pamoja na kaimu katibu tawala mkoa wa Iringa,Elias luvanda wakati wa kufungua mafunzo kwa wakaguzi wa dawa na vifaa tiba mkoani Iringa
Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kanda ya kati Sonia Mkumbwa akitoa mafunzo kwa wakaguzi wa Dawa na vifaa tiba mkoani Iringa


Na Fredy Mgunda,Iringa.


MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kuwajengea uwezo wataalamu wa ukaguzi wa dawa na vifaa tiba katika Halmashauri zote za Mkoa wa Iringa kwa lengo la kuboresha ufanisi wa kazi wawapo kazini ili kulinda afya za watumiaji wad awa na vifaa tiba.


Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo kaimu katibu tawala mkoa wa Iringa,Elias luvanda alisema kuwa ni kielelezo tosha kuwa wakaguzi ngazi ya Halmashauri mnathamini mchango wa TMDA katika kuwapa elimu kuhusu namna bora ya kutekeleza majukumu na  kulinda Afya za wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa letu la Tanzania.


Luvanda alisema kuwa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Afya, yenye jukumu la kudhibiti ubora, usalama na ufanisi wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi na Taasisi hiyo imeundwa chini ya sheria ya Dawa na Vifaa Tiba sura 219.

Alisema kuwa majukumu yanayofanywa na TMDA na yale yaliyokasimishwa kwenu, lengo lake ni lilelile la kulinda afya ya jamii kwa kuzuia athari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi. 

 

“Kwa kutambua jukumu zito la TMDA, Serikali iliona ni vema kukasimu baadhi ya madaraka na majukumu yao kwa Halmashauri kwa lengo la kusogeza karibu na wananchi huduma za udhibiti wa ubora na usalama wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi”alisema Luvanda


Luvanda aliwataka watendaji wote kufanya kazi kwa kutoa taarifa zilizo sahihi kwa wakati unatakiwa ili kurahisisha utendaji wa taasisi hiyo hivyo Mwongozo wa Kukasimu Madaraka na Majukumu umebainisha wazi kuwa taarifa za utendaji kazi za robo mwaka na taarifa za ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa kazi za udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa zinazodhibitiwa katika soko zinatakiwa kuandaliwa na kutumwa TMDA kupitia viongozi wa ngazi ya Halmashauri.


“Ni mategemeo yangu kwamba mafunzo haya yatatoa maelekezo ya namna ya kuboresha utendaji kazi wenu, na kuondoa changamoto zinazojitokeza mara kwa mara kuwa, wakaguzi wa Halmashauri wanatumia nguvu nyingi nyakati za kaguzi ambazo husababishwa na kutokutoa elimu kwa wateja (wafanyabiashara) Hivyo kukinzana na utaratibu wa ukaguzi wa TMDA ambao umejikita zaidi katika kuelimisha na kuwezesha” alisema Luvanda.


Alimalizia kwa kusema kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itafanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa maagizo na makubaliano yatakayowekwa ili kuhakikisha wananchi wanahakikishiwa upatikanaji wa bidhaa bora na salama.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kanda ya kati Sonia Mkumbwa alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwaongezea ujuzi wakaguzi ili waweze kufanya kazi ya ukaguzi kwa kuzingatia sheria.

Mkubwa alisema kuwa wakaguzi watatekeleza kazi zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo kama zilivyotolewa na TMDA kama vile Kufanya ukaguzi wa maeneo yanayohusika na utunzaji, uuzaji na usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi, Kufanya ufuatiliaji na kutoa taarifa za ubora na usalama wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi katika soko.


Aliongeza kuwa wakaguzi watatakiwa kuchukua sampuli za bidhaa zinazodhibitiwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara pale inapohitajika na kufanya ufuatiliaji wa madhara/matukio yanayohisiwa kusababishwa na matumizi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi.


 Mkumbwa alisema kuwa wakaguzi wanatakiwa kufanya uhakiki wa bidhaa zisizofaa kwa matumizi kabla ya uteketezaji kwa kujaza fomu ya uhakiki (Kiambatisho Na.7) baada ya mawasiliano na Ofisi ya Kanda ya TMDA na kusimamia zoezi la kuteketeza bidhaa ambazo hazifai kwa matumizi baada ya uhakiki na kisha kujaza fomu ya uteketezaji (Kiambatisho Na. 8) na kuiwasilisha ofisi ya Kanda ya TMDA kwa ajili ya kuandaa cheti cha uteketezaji.


Alimazia kwa kuwasema kuwa kila Halmashauri itaandaa na kuwasilisha taarifa za utendaji kazi kwenye Ofisi za TMDA za Kanda  na kuwasilisha nakala kwa Katibu Tawala wa Mkoa ambazo ni taarifa ya utendaji ya robo mwaka na taarifa ya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa kazi za udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa katika soko.