ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 16, 2022

MREMBO HUYU ANASIKITIKA KUKOSA MPENZI WA KUMUOA.

 


Kisura ambaye ni mama wa mtoto mmoja, Ayishatu Adams ametangaza mitandaoni kwamba anatafuta mume wa kumuoa. 

Katika video ya kusikitisha kwenye TikTok, mwanafunzi anayesomea uuguzi alifichua kuwa atakuwa na umri wa miaka 35 mnamo 2023 na bado hana mchumba. 

Ayishatu alilalamika kwamba wanaume wanaomrushia ndoano huhepa baadaye kwani hawataki kuchukua majukumu ya kumlea mtoto wake. 

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 34 alifichua kwamba jambo hilo linamtia huzuni. 

"Nitakuwa na umri wa miaka 35 mwakani na bado sijaolewa kwa sababu nina mtoto. Mwanaume yeyote anayekuja kwangu anasema hawezi kujukumikia kisicho chake." 

Haya ni baadhi ya maoni ya watu kuhusiana na kilio cha kidosho huyo; 

Abbati SK alisema: "Hao wanaume kamwe hakupendi wala kukuthamini ndiyo maana wanakuhepa. Mtu sahihi atakuja na atakuthamini."

 Abubakari Rahinat683 alisema: ''Mwanamume sahihi na mcha-Mungu atakupata na hakuna haraka maishani. Mwenyezi Mungu anapanga zawadi maalum kwa ajili yako." 

korkor_1992 alisema: ''Zingatia sana kumlea mtoto wako kwani yeye ndiye mtu pekee ambaye atakuwepo kwa ajili yako kila wakati." zee-money alisema: "Usifadhaike wanaume wote unaokutana nao sio wako Mungu atakutendea haki." 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.