ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 24, 2011

AMINI USIAMINI KITU KIPYA CHENYE HADHI YA KITALII NA BEI NAFUU NDANI YA MAGU MWANZA

Ni kiota kipya kabisa kimefunguliwa ndani ya wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza eneo linaitwa Cadillac hotel.

Mazingira mazuri ndani na nje huku ukipatiwa huduma safi toka kwa wahudumu waliobobea.

Korido za kuelekea vyumbani.

Cadillac mazingira.

Flamingo ni Moja ya vyumba classic hotelini hapa.

Usingizi mwananaZZZzzzz!!!

Suitabo bediZZZzz!!

Ukumbi wa kisasa wa mikutano unapatikana hapa.

Bustani bar iliyosheheni mashamsham ya pekee.

Hii ni bar yenye kila aina ya vinywaji inayopatikana ndani ya bustani tuliiivu Cadillac Magu Mwanza.

Kwa mawasiliano zaidi piga
simu +255282530300
mobile +255786777618

BENKI YA FBME MWANZA YASABABISHA TABASAMU KWA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU

Ili kuleta furaha na tabasamu kwa watoto waioshio kwenye mazingira magumu Benki ya FBME kupitia tawi lake la Mwanza jana imekabidhi msaada wa vyakula kama vile mchele, maharagwe, mafuta ya kujipaka, mafuta ya kula na sabuni kwa kituo cha kulea watoto yatima cha Amani Girls Home.Wafanyakazi wa benki ya FBME tawi la Mwanza Joan Chovenyi (L) na Anna Lupemba (R) wakikabidhi msaada huo kwa Agripina John ambaye ni meneja wa kituo.

Joseph Gwalugano Branch manager wa benki ya FBME tawi la Mwanza akikabidhi msaada kituo cha kulelea watoto waishio mazingira magumu.

Mwenyekiti wa bodi kituo cha kulea watoto yatima jinsi ya kike cha Amani Girls (L) bw. Fabian Marugu akipokea msaada wa mafuta toka kwa mfanyakazi wa FBME Bank tawi la Mwanza Peter Nkenguye.

Shukurani na kupeana moyo kwani jukumu la malezi ni letu sote..

Picha ya pamoja wadau wa benki ya FBME, Uongozi wa Kituo cha Amani Girls na watoto walio wawakilisha wenzao toka kituoni hapo.

"Hivi ndivyo inavyotupasa kurejesha sehemu ya faida kwa jamii" says Wafanyakazi FBME Bank Mwanza.

MIAKA 50 YA UHURU HESABU ZIMETUSHINDA KABISA

Eti viongozi wanatuhamasisha kuchangia elimu, huku wakikandia kuhusu jinsi tunavyochangia maharusi mamilioni... Ulikuwa Hujui sanaa imeanzia juu....!!

Chekshia hivi majuzi tumesheherekea miaka 50 ya UHURU kwa bilioni 4 safi sanaaa, wakati zingeenda kwenye madawati na ujenzi wa madarasa suala la wanafunzi kukaaa chini mashuleni lingekuwa ndoto. Lakini mmh tuna muda mrefu sana labda tukisheherekea tena miaka 200 ya uhuru kwa maumivu.

Friday, December 23, 2011

SBL YAZINDUA KITU KIPYA KANDA YA ZIWA

Ni kitu kipya katika soko kinatambulishwa kwenu na kampuni ya Serengeti Breweries Limited ndani ya jiji la Mwanza, Kitu kinaitwa Senatar Extra Lager Bia ina alkohol 6 mwanawane.

Bia mpya Senator Wau!!!!!

Wadau mbalimbali walihudhuria kusanyiko hilo la kibiashara lenye mlengo wa kutambulisha kitu kipya sokoni fahari ya wafanyikazi na wakulima wenye nia na malengo ya kuinua uchumi wa taifa letu.

Umakini ulitawala pale mzigo mpya ukitambulishwa sokoni...

Bia hii inatengenezwa kwa shairi na ngano nayo itasambazwa kanda ya ziwa kuwanufaisha wadau muhimu fahari ya taifa letu.

Itauzwa sh 1300 kwa watumiaji wa rejareja nao uzinduzi kufanyika rasmi january 2012.

Wadau hawa si wengine jamani ni wakulima, wavuvi na wafanyakazi wavuja jasho walio fahari ya taifa letu.

Hivyo tunawakaribisha wawe karibu nasi kuifaidi ladha halisi iliyo ndani ya bia nzuri Senetar......

Meneja Masoko Efraim Mafuru akimalizia jambo kupitia maelezo elekezi.

talk time SBL team.

Thursday, December 22, 2011

LINGOJE KWA HAMU TAMASHA LA MUZIKI WA INJILI X-MASS BOXING DAY 26DEC 2011 MWANZA

Tamasha kubwa la muziki wa Injili linalotambulika kwa jina la ‘Gospel Festival’, limepangwa kufanyika siku ya Boxing Day (Desemba 26/2011) kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Mwanza, Mkurugenzi Mtendaji wa F&G Promotions, Fabian Fanuel, alisema kuwa, Tamasha hilo la msisimko na laaina yake litahusisha kwaya, bendi na waimbaji binafsi kutoka maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa na nje ya kanda ya ziwa.

Fanuel alizitaja baadhi ya Kwaya shiriki kuwa ni pamoja na Kwaya ya EAGT Msumbiji, Nyakato Moravian za Mwanza, Kwaya ya Mapambano kutoka Geita, AIC Ushirombo kutoka Ushirombo, Chipukizi ya Baptist Misungwi, T.A.G Vijana choir Geita, Ufunuo P.A.G choir, A.I.C Nyakato choir, Vijana Choir Nyakato, Tumaini Anglikan Igoma, Jerusalem choir, C.A.G Unguja, Imani Baptist choir Buhongwa, Revival Mission Band, Grace Wagana, Christina G. Vitta kuoka Kwimba, Tumaini KKKT Igoma choir, AIC Muungano choir, Mtakatifu Mkwasa RC choir Nyakato na Mwanza Gospel.

“Washiriki wengine ni Jerusalem Band na Glory Band zote kutoka Mwanza, pamoja na Kwaya nyingine kadha wa kadha kutoka katika madhehebu mbalimbali hapa Kanda ya Ziwa ambao watapewa tafu na waimbaji maarufu kama Tumsifu Rufutu aliyeimba 'Mwambie Farao', Danie Safari wote kutoka Dar es salaam” alisema Fanuel ambaye pia ni mtangazaji wa kituo cha radio Living Water FM, Mwanza.

Fanuel alisema kuwa Tamasha hilo litafanyika sambamba na uzinduzi wa Kampuni hiyo F&G Promotions iliyojikita zaidi kwenye uandaaji wa matamasha ya aina mbalimbali kama vile maigizo, vichekesho pamoja na muziki wa aina mbalimbali kama vile, Muziki wa Injili, Muziki wa kizazi kipya, na Muziki wa Dansi.

Aidha, Fanuel aliwaomba wakazi wote wa Kanda ya Ziwa kujitokeza kwa wingi ili kushuhudia vipaji vya uimbaji kutoka ukanda wao, ambapo pia siku hiyo kampuni hiyo sambamba na kutambulisha wadau wake itatoa vyeti maalum kutambua mchango wa waimbaji, Redio mbalimbali pamoja na watumishi wa Mungu.

Tamasha la ‘Gospel Festival’ litakalokuwa likifanyika mara moja kwa mwaka, limelenga 'Kuamsha ari ya kiroho kwa watanzania kufanya kazi kwa imani na kutokata tamaa'

MIZENGO PINDA AZUNGUMZA KUHUSU KATIBA MPYA

MH Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mizengo Pinda Akiongea kuhusu mchakato wa kutafuta katiba na Baraka Baraka kutoka Urban Pulse Creative.

Wednesday, December 21, 2011

WATAALAMU WAGUNDUA MAHUSIANO YA USINGIZI NA JENI

Wanasayansi wanasema mahitaji ya usingizi kwa watu yana uhusiano na jeni zao yaani genes. Usingizi
Wamegundua kuwa watu wenye aina ya jeni iitwayo ABCC9 wanahitaji takriban dakika thelathini za ziada za usingizi kila usiku kuliko wale wasiokuwa nayo. Utafiti uliofanywa ulilenga bara la Ulaya na kugundua kuwa humusi ya watu wana aina hiyo ya jeni.

Wanasayansi hao wa Ujerumani na Uingereza wamesema matokeo hayo ni muhimu kwasababu ukosefu wa usingizi unahusishwa na matatizo mengi ya kiafya, kama vile maradhi ya unene na moyo.

Viongozi wa kisiasa, kuanzia mtawala wa zamani wa Ufaransa Napoleon hadi aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher walikuwa na sifa ya kuweza kufanya kazi zao bila matatizo licha ya kulala muda wa saa nne au tano tu kila usiku.
Lakini kwa wengine akiwemo mwanafizikia Albert Einstein hata muda wa saa 10 wa usingizi haukumtosha.

Sasa wanasayansi wanasema tofauti hizi katika mahitaji yetu ya usingizi yanaweza kuelezeka kwa kutazama muundo wa jeni zetu.

Walichambua chembe chembe za asidi nasaba DNA kutoka watu 10,000 kote barani Ulaya- na kuzilinganisha na mitindo yao ya kulala.

Walifikia kauli kwamba watu walio na aina ya jeni iitwayo ABCC9 wanahitaji muda wa nusu saa zaidi usingizini ikilinganishwa na wale wasio na aina hiyo ya jeni. Mtu mmoja kati ya kila watu watano barani Ulaya wanaaminika kuwa na jeni hiyo ya usingizi mwingi.

MVUA DAR ZALETA MAAFA NA KUUA SITA!

JIJI la Dar es Salaam na vitongaji vyake, limekumbwa na maafa ya vifo vya watu sita mpaka sasa akiwamo mmoja aliyepigwa na radi, uharibifu wa miundombinu huku mamia ya watu wakikosa makazi, kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia jana.Wakazi wa eneo la Tandale wakitaabika.
Mvua hizo zilisababisha tatizo kubwa la usafiri kutokana na barabara kujaa maji, kuezua nyumba na kuua watu sita na kuacha maelfu ya wakazi wa jiji hilo bila makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa mapaa.

Mvua ilianza kunyesha mnamo saa 9:00 alfajiri ikiambatana na radi na ngurumo nzito na kusababisha kukatika mara kwa mara kwa umeme katika baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es salaal.

Nyumba zikiwa zimezingirwa na maji kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jijini Dar es Salaam jana.

Mmoja ya wakazi akipima maji ili kuona uwezekano wa kwenda kuwasaidia watu waliozingirwa na maji.

Baadhi ya wakazi wakiwa sintofahamu baada ya kushuhudia mafuriko yaliochokuwa maisha ya wapendwa watatu.

Baadhi ya waokoaji wakiwa na vifaa vya kazi tayari kuokoa maisha ya wakazi wa mabondeni.
Picha na Michuzi JR.

TEMBO ANAPOGEUKA KUWA TRAFIKI

'STOP' Hakuna njia.

Akijilaza tu.. Twafa!

Picha kwa hisani ya PGS ISAAC

ROMA, BELLE 9 KUSINDIKIZA UZINDUZI HILL WAY BAND X. MASS HII NDANI YA GOLD CREST MWANZA

nI kWa mARa yA kWANzA mWANZA kUPENdEzA USIKOSE!!!!

Tuesday, December 20, 2011

WENJE AIWEZESHA SEKTA YA ELIMU NYAMAGANA

"Pamoja na Taifa Letu kuwa na uri mkubwa (miaka 50 ya Uhuru) sambamba na rasilimali tulizonazo, nchi hii inashika nafasi ya tatu kuwa ombaomba duniani, nchi ya kwanza ni Iraq ya pili ni Afriganstan nchi hizo zikiongoza kwasababu ya vita nchi ya tatu ni Tanzania"

Kama unakunywa kila siku pombe za shilingi elfu kumi na mtoto wako hana dawati anakaa chini shuleni basi juwa kuwa unafanya dhambi.

Madawati Mchango wa mbunge Ezekiel Wenje yatakayo zinufaisha shule mbalimbali za wilaya yake.

Madawati mchango wa mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje yakitinga kusanyikoni.

"Kila baba mwema anapenda mtoto wake asome mahali pazuri, kama kungekuwa na shule mbinguni basi kila mwanaume angehangaika mwanae apate nafasi huko, lakini kwanini tusianze kuwatengenezea mazingira mazuri kuanzia hapa kwa kidogo tulichonacho?"

Umma uliofurika kumsikiliza mbunge Wenje

Wenje akipiga sahihi katika kadi za wanachama wapya walonunua kadi kwenye mkutano huo ambapo maelfu ya wanachama wapya walipatikana.

WENJE AKANA ONGEZEKO LA 'SITINGI ALAWANSI' asema tangu itajwe hajaiona kwenye akaunti yake. "Mimi Wenje sijalipwa na wala sijaiona posho iliyoongezeka inayoitwa sitting alowance, kimsingi kwa dhana tu ya kawaida ile posho ni siting alawansi, so hebu tujiulize utalipwaje kama haupo Dodoma, na Makinda alisema kama mnakumbuka maisha yamepanda Dodoma, sasa utalipwaje posho ukiwa Mwanza? na ile posho inatakiwa ukiwa pale bungeni ndiyo ulipwe, sasa mimi niliye huku jimboni mwangu Nyamagana nilipwe sitting alowance ya nini kwa lipi? Kama wanalipwa basi wanalipana wao kwa wao wanajuana"

SAKATA LA MAFUTA MSITUFANYIE KIHIVYO.

Hivi Serikali imelala usingizi gani huo mzito hadi wamiliki wa vituo vya mafuta wanapata kiburi kugoma kutoa huduma hiyo?

Kwa migomo kama hii ya mara kwa mara inawezekana Serikali yetu Tz imewekwa mfukoni na Atajiri wachache wa Mafuta?....!!!

Rais Jakaya Halfani Mrisho Kikwete, Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda mbona hatuoni makali yenu? Ngeleja Upo wapi hadi uji wa mgonjwa unamwagiwa mchanga…..?!!!!...!!!

TAFAKARI CHUKUWA HATUA KABLA KENGELE HAIJA LIA….Konng….kONNg’’’!!!!!

Monday, December 19, 2011

BODABODA TIGO RUSHA YAZINDULIWA J.MOSI ARUSHA

Mwendesha Pikipiki boda boda, John Lembele akimuhuzia mda wa maongezi Peter Shebobo wakati wa udhinduzi wa Boda boda tigo rusha iliyofanyika jumamosi.

Mwanadada wa tigo akikabidhi 'Kiziba tope'.

Waendesha pikipiki wawekezaji.

Penye Shangwe pana jambo zuri.

Waendesha pikupiki (boda boda) wakiwa katika picha ya pamoja leo wakati wa uzinduzi wa Tigo Rusha Bodaboda.(Picha na Mpigapicha Wetu)