ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 11, 2023

KOKA AFANYA KWELI AZINDUA KWA KISHINDO ZAHANATI YA SAENI KATA YA MISUGUSUGU

 


Na Victor Masangu,Kibaha 


Wananchi wa mitaa mitatu ya Saeni,Zogowale na Jonung"ha iliyopo kata ya Misugusugu ambao walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya kufuata huduma ya afya kwa umbari mrefu wameondokana na adha hiyo baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa zahanati.

Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka wakati wa halfa ya uzinduzi wa zahanati ya Saeni ambayo imehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali,viongozi waCcm,Dini,pamoja na wananchi kutoka maeneo mbali mbali.


Koka alibainisha kwamba kumalizika wa mradi wa ujenzi huo kutaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kutaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuwaboreshea zaidi wananchi kupata huduma ya matibabu kwa urahisi zaidi.

Aidha alisema kwamba hapo awali wananchi wa kata ya misugusugu walikuwa wanapata shida ya kutembea umbari mrefu hivyo akaamua kushirikiana na wananchi kwa pamoja ili kuwaunga mkono.


Koka aliongeza kuwa kabla ya kuanza mradi huo alichangia kiasi cha shilingi milioni 6.5 kwa ajili ya kununua mifuko ya saruji kwa ajili ya kuweza kuanza ujenzi huo wa ujenzi wa zahanati.

"Mara ya kwanza nilitoa milioni tano lakini awamu ya nilichangia tena kiasi cha shilingi milioni 1.5 lengo ikiwa ni kuanza mradi huo wa ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Koka alibainisha lengo lake kubwa ni kuwatumikia wananchi wake hivyo atahakikisha kuwa ataendelea kuboresha zaidi huduma ya afya ili wananchi waweze kuondokana na kero ambazo wamekuwa wakizipata.


Kwa upande wake mganga mfawidhi wa halmashauri ya mji Kibaha Peter Nsanya alibainisha kuwa ujenzi huo mpaka kukamilika umegharimu kiasi cha shilingi milioni 181.

Alibainisha kuwa mradi wa ujenzi huo utaweza kusaidia zaidi hasa kwa Upande kwa huduma za mama na mtoto ambao walikuwa wanapata shida ya kwenda Hadi eneo la mlandizi.


Naye Diwani wa kata ya Misugusugu Upendo Ngonyani amemshjkuru Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kwa kutekeleza ilani kwa vitendo kwa kuchangia fedha ambazo zilisaidia katika mradi wa ujenzi huo wa zahanati.

DC TANGA AWATAKA WALIMU KUITUMIA BENKI YA NMB ILI KUWEZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

 

MKUU wa wilaya ya Tanga James Kaji akizungumza wakati alipomwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema  katika kongamano la siku ya  Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo.
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji,ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji,ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyemaha
sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema

sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema


 Na Oscar Assenga, TANGA.


MKUU wa wilaya ya Tanga James Kaji amewataka walimu mkoani humo kuhakikisha wanaitumia benki ya NMB kutokana na bidhaa zao wanazotoa za mikopo ambazo zimeweza kuwainua kimapato na hatimaye kuwakwamua kiuchumi badala ya kujiingiza kwenye mikopo kandamizi.

Kaji aliyasema hayo wakati alipomwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema  katika kongamano la siku ya  Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo.

Ambapo alisema kwamba hilo ni kutokana na kwamba benki hiyo kusheheni huduma mbalimbali ambazo wanaweza kuzitumia katikaa kujikwamua kiuchumi na kuondokana na mikopo kandamizi.

“Niwapongeza NMB kwa kuandaa Kongamano hili kwa walimu ni ya kipekee kwani nimetoa msisitizo kwa kutumia nguvu nyingi kuwezesha walimu kwenye shule za Msingi na Sekondari kwani wamekuwa wakiishi kwenye mazingira magumu  kutokana na kujiuingiza kwenye mikopo umiza”Alisema

Aidha alisema mikopo hiyo imekuwa ikiwaumiza na hivyo kupelekea kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kuweza kufundisha kutokana na kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kuirejesha.

“Warsha hii imekuja wakati muafaka na niipongeza NMB nitoa wito kwa walimu kuweza kutumia NMB kutokana na bidhaa zao wanazotoa za mikopo ambapo lakini tumeshuhudia jinsi benki ilivyoweza kuwainua kimapato na kuweza kuboresha maisha yao hali inayoongeza uwezo kwenye utumishi wa kazi zao za kila siku”Alisema

Awali akizungumza Mkuu wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe alisema kwamba wamezindua mpango maalumu kwa ajili ya walimu ambao waliuita “Specho” na wamekuja Tanga kutoa elimu zaidi na kusisitiza juu ya huo mpango unaomwezesha mwalimu kupata mikopo yenye riba nafuu ikiwemo ya kujiendeleza kielimu wao na watoto wao.

Alisema pia wanatoa mikipo ya biashara ndogo ndogo ,ujenzi,vyombo vya moto kama bodaboda na pikipiki za miguu mitatu ikiwemo kupata mkopo wa bima yaani Insurance Premium Finance (IPF) ambayo inawezesha walimu kulipa bima kujikinga na majanga mbalimbali.

“Lakini pia tunatoa mikopo ya pembejeo na mashine za kilimo fursa za kushiriki promosheni na kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo elimu ya kifedha kwa walimu na kadhalika”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Tafiti zinaonyesha kati ya watanzania milioni 60,ni asilimia 22 tu ndio wenye akaunti za benki pia zaidi ya asilimia 70 ya watanzania wanaamiliki simu za mkononi na wana uwezo wa kufanya malipo na miamala kupitia simu zao za mkononi.

“Kwa kulitambua hilo benki yenu ya NMB imeendelea kuja na masuhulisho mbalimbali yanayohusu makundi tofauti tofauti kama hili la walimu kama njia mojawapo ya kuleta watanzania zaidi kwenye mifumo rasmi ya kifedha na kuipatia Serikali mapato kupitia masuluhisho hayo pia benki imeweza kufikishja asilimia 94 ya miamala yake kupitia simu za mkononi”Alisema

Hata hivyo alisema hivi karibuni wamezindua huduma kubwa tatu ambazo zinaendelea kuleta mapinduzi makubwa katika sekta hya kibenki Tanzania ambazo ni mikopo kidigitali (MshikoFasta),NMB Pesa Wakala na NMB Lipa Mkononi.

Alisemna kupitia mifumo hiyo wameweza kuwafikia watanzania wengi zaidi na hivyo kuchangia kuongeza idadi ya watanzania wanaotumia huduma za kibenki na pia hata kuwasaidia walimu ambao wanaweza wakawa mbali na matawi ya benki.

Naye kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka alisema siku ya mwalimu kwa benki ya  NMB ilianzia mkoa wa Tanga miaka ya nyuma wilaya ya Korogwe kwa zaidi ya miaka 7 iliyopita na wameendelea kuboresha huduma zao.

Alisema  kwa sababu walimu wameendelea nao wafanye nini na niwashukuru walimu mmekuwa wateja wote wa thamani sana kutokana na walimu kuwa chachu kubwa kwao kubioresha huduma zao wanazotoa kwa mikopo na hudumaza bidhaa mbalimbali na mwaka 2005 walikuwa wanaliopa mishaha kupitia madirisha yaliyokuwa halmshauri na baada kupitia benki .

SELINA KOKA AWEZESHA VITENDEA KAZI OFISI ZA KATA JUMUIYA YA WAZAZI KIHABA MJI

 


Na Victor Masangu,Kibaha


Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Selina Koka katika Kuhakikisha anaweka misingi imara ya kukiimarisha chama cha mapinduzi (CCM)  amegawa vitendea kazi mbali mbali kwa kata zote 14  kwa ajili ya matumizi ya ofisi za jumuiya ya umoja wa wazazi katika Wilaya ya Kibaha mjini.


Selina ambaye pia ni mlezi wa jumuiya ya umoja wa wazazi Kibaha mji alisema kwamba ameamua kutoa vifaa hivyo vya steshenari kwa lengo la kuwarahisishia wenyeviti na makatibu kufanya kazi za chama kwa lengo la kuwasaidia wanachama wao.


Hayo yamebainishwa katika mafunzo ya jumuiya ya  umoja  wazazi ngazi ya kata ambayo yamefanyika katika ukumbi wa halmashauri ya mji kibaha na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa chama pamoja na mumeo Silvestry  Koka ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini.


"Leo nimefurahi sana kushiriki katika mafunzo haya ya jumuiya ya wazazi lakini pamoja na hayo niliahidi kuboresha vitendea kazi katika ofisi zote 14 zilizopo ndani ya jimbo la Kibaha kwa hiyo nina imani kubwa vifaa hivi vya steshenari vitawasaidia viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao,"alisema Selina.

Aidha Selina aliahidi kuendelea kuwasaidia wanawake kiuchumi kwa kuwapatia mitaji pamoja na mafunzo mbali mbali ili kuweza kuondokana na wimbi la umasikini lengo ikiwa ni kuwaletea maendeleo wanawake.

Aidha aliongeza kuwa viongozi wanapswa kumpa ushirikiano Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan,pamoja na Mbunge wa jimbo la Kibaha mjini kuendelea kuwapa muda katika kipindi chote cha utekelezaji wa majukumu yao bila kusumbuliwa kwa maslahi ya wananchi.

Kwa Upande wake mmoja ya wakufunzi wa mafunzo hayo Abdalah Zaidi  amewataka viongozi hao kuhakikisha wanasimamia malezi kwa watoto wao ili kuepukana na changamoto ya kuwepo kwa  mmomonyoko wa maadili.

"Mafunzo haya yataweza kuwasaidia zaidi viongozi wa kata zote 14 za jimbo la Kibaha mjini kwa hiyo kikubwa ninachoomba ni kusimamia maadili hasa kwa watoto wetu ikiwemo mambo ya ushoga,"alisena Zaidi.


Pia mkufunzi huyo ambaye ni kada wa CCM kutoka Wilaya ya bagamoyo aliwakunbusha viongozi hao kuachana na tabia ya kutoa siri za chama na badala yake wabadilike na kuweka mikakati ya kukiimarisha chama pamoja na kukilinda.


 "Ni wajibu wa kila kamati ambazo zitaundwa katika jumuiya ni kulinda Siri za chama katika ngazi mbali mbali kuanzia matawi,mashina na kuendelea na kufanya hivyo kutaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kulinda maadili ya wanachama wote,"alisena mkufunzi huyo.

Katika hatua nyingine alimpongeza Mbunge wa jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kwa kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo na kuwataka baadhi ya watu kuachana na vitendo vya kuwaingilia viongozi waliopo madarakani na badala yake wawape ushirikiano wa kutosha mpaka wamalize muda wao.

Jumuiya ya umoja wa wazazi Wilaya ya Kibaha mji imeamua kuwapatia mafunzo mbali mbali viongozi wa ngazi za kata zote 14 kwa lengo la kuwakumbusha mambo mbali mbali ikiwemo maadili,itifaki,majukumu na wajibu wa viongozi pamoja na  mambo mengine.


Wednesday, August 9, 2023

Wakulima waimwagia sifa Benki ya CRDB mbele ya Rais Samia

 

Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara wa Benki ya CRDB, Ndugu Maregesi Shaaban alipotembelea Banda la Benki ya CRDB katika kilele cha maadhimisho ya Nanenane yaliyofanyika kitaifa Jijini Mbeya. Wakishuhudia ni Spika wa Mbunge Mh. Dkt. Tulia Ackson na Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Ndungu Fredrick Nshekanabo.
BAADHI ya wakukima mkoani Mbeya wameishukuru Benki ya CRDB mbele ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa imewasaidia kupata mikopo ya fedha na nyenzo ikiwemo trekta aina ya Power Tiller, kuwa vitawasaidia kuinua kilimo na kupata kipato.

Mmoja wa wakulima hao kutoka Wilaya ya Mbalali mkoani Mbeya Halima Ally, ametoa ushuhuda huo leo mbele ya Rais Dkt. Samia alipotembelea Banda la Benki ya CRDB kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nane Nane) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

"Sisi wakulima wa Mbarali tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kutuwezesha kupata mikopo ya fedha na zana za kufanyia kazi kama ilivyotukopesha Power Tiller. Kwa kupata Power Tiller hii itaniwezesha kuendeleza kilimo changu cha mpunga na mahindi" alisema Ally.
Wakulima zaidi ya 600 kutoka Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wanatarajiwa kukopeshwa na Benki ya CRDB trekta, power tiller, zana za kuvunia, fEdha za mikopo ya kulimia na pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu, mbolea na madawa, na mikopo ya Stakabadhi Ghalani.

Rais Dkt. Samia, aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuweza kukopesha wakulima kwa riba ya asilimia tisa, huku akiitaka benki hiyo kuendelea kufuatilia l zana za kilimo wanazowakopeaha wakulima ili ziendelee kufanya kazi, na ikibidi kuwasaidia kutengeneza pindi zinapoharibika, kwani baadhi yao zana hizo zikiharibika, wanazitelekeza.

"Nawapongeza CRDB kwa kuweza kutoa mikopo ya riba ya asilimia tisa. Itawasaidia wakulima kuweza kukopa kwa wingi na kulima kwa tija.

"Na mikopo ya Power Tiller mnayotoa kwa wakulima muweze kuifuatlia na muwasaidie au kuweza kuwasaidiia waweze kutengeneza. Wakati mwingine power tiller linaharibika na kulitelekeza hivyo kushindwa kuleta tija" alisema Rais Dkt. Samia.

Awali, Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara wa Benki ya CRDB Maregesi Shaaban alisema Benki ya CRDB imeendelea kutoa mikopo inayofikia sh. trilioni 3.9 kwa misimu mitano iliyopita hadi kufikia Julai, 2023, sawa na asilimia 43 ya mikopo yote itolewayo na mabenki kwenye Sekta ya Kilimo na Mifugo hapa nchini.

"Tunatoa mafunzo kwenye vituo atamizi chini ya mpango maalum wa BBT kupitia Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Tunaendelea kutoa elimu ya fedha na usimamizi wa miradi kwenye vituo vilivyoko kote nchini. Uwezeshaji vijana na wanawake kwenye kilimo, uvuvi, mifugo, viwanda na biashara Bara na Visiwani.

"Benki ya CRDB kupitia kampuni yetu tanzu ya CRDB Bank Foundation, inawekeza kwa vijana na wanawake ili waweze kutimiza ndoto zao ikiwa ni pamoja na kuwapa mafunzo na kuwapatia mitaji kwa ajili ya uanzishaji wa miradi mipya (startup capital). 

Mitaji hii hutolewa kwa vijana na wanawake wenye mawazo bunifu kibiashara, na Benki ya CRDB inatoa mitaji ya awali ikiwa ni mbegu itakayoleta matunda na kuwafungulia kesho yao yenye tija zaidi kiuchumi, chini ya program ya kipekee ijulikanayo kama IMBEJU".alisema Shaaban.

Shaaban alisema Benki ya CRDB imefanikiwa kufufua matumaini ya wana ushirika kwa kuongezea mtaji inayofikia sh. bilioni 10.2, ambapo sh. bilioni 3.2 kwa TACOBA na sh. bilioni 7.0 kwa KCBL. Taasisi hizo zilikuwa zikijiendesha kwa hasara na baada ya kupata mtaji na usimamizi madhubuti kutoka Benki ya CRDB, zimeanza kujiendesha kwa faida kubwa na kutokana na mikakati madhubuti ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia, wanaendelea kutekeleza ndoto nzuri ya kiuchumi ya uanzishwaji wa Benki ya Ushirika ya Taifa. 

Shaaban alisema, Benki ya CRDB ikishirikiana na wauzaji wa vifaa madhubuti vya kilimo (Agricom), imeweza kuwakabidhi baadhi ya wanufaika waliopata mikopo ya kununua Power Tillers kwa ajili ya kilimo cha mpunga mkoani Mbeya.

"Benki ya CRDB itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuendeleza fursa za uwekezaji zilizopo Bara na Visiwani.

Tunawakaribisha wadau wote walipo ndani na nje ya nchi yetu ya Tanzania wafike kwenye matawi yetu yaliyoko kote nchini na kwenye nchi jirani za Burundi na Congo DRC ili tuweze kuwahudumia.

"Tunatoa Shukran za dhati kwa Business Units zote za CRDB na uongozi wa Benki yetu pendwa ya CRDB (kipekee tunatoa Shukran kwa our MD&Group CEO, CCO, COO, CFO, DCA, DCB, DRB, DC, DCA, MD-CRDB BANK FOUNDATION & the entire CRDB MARKETING TEAM) kwa kutuwezesha vilivyo hadi kufikia kilele cha maadhimisho haya ya Maonesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Mbeya kwa mafanikio makubwa" alisema Shaaban. 

--

Monday, August 7, 2023

DKT SIMEO: MICHEZO NI NGUZO MUHIMU YA UTULIVU NA USALAMA KWENYE NCHI

 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akizungumza wakati alipozindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime

 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akizungumza wakati alipozindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime
Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Tanga Edgar Mdime akizungumza kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo
MKUU wa Idara ya Maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Sinde Mtobu akieleza umuhimu wa uchangiaji damu
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime

Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime akichangia damu


Na Oscar Assenga, TANGA.

MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Japhet Simeo leo amezindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga huku akieleza kwamba michezo ni moja ya nguzo muhimu katika utulivu na usalama kwenye nchi.

Simeo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba kwenye uzinduzi huo alisema kwamba michezo ina tija sana katika maisha ya binadamu ikiwemo kuwaunganisha jamii na kutengeneza undugu.

Alisema kwamba uchangiaji wa damu ni muhimu ili kuokoa maisha ya wagojwa wahitaji wa damu wakiwemo waluopata ajali, wakina mama wajawazito na watoto waliopo katika hospital mbalimbali mkoani Tanga.

Mganga Mkuu huyo aliwapongeza wanachama hao kwa utayari wao wa kuona umuhimu wa kuchangia damu ambayo itakwenda kusaidia jamii yenye uhitaji huku akizitaka Taasisi, Vikundi na watu binafsi kuendelea kuwa na utamaduni huo ili kuweza kuokoa maisha ya watu wanaofika hospital kupata huduma hiyo.

"Nawapongeza mashabiki wa timu ya Simba SC kwa utayari wenu kuja kuchangia damu mimi nawaambia hii ni sadaka na thawabu kubwa sana mliyoitoa kwa wenzenu wenye uhitaji wa damu " Alisema Simeo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Matawi ya Klabu ya Simba SC Edgar Mdime alisema kwamba zoezi la uchangiaji wa damu imekuwa ni utaratibu waliojiwekea kila mwaka lengo likiwa kuhakikisha wanakuwa sehemu ya kuokoa maisha ya wahitaji.

Alisema bado wanasukumwa kuchangia damu katika hospitali wakitambua kuwa uhitaji wa damu ni mkubwa kwa wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu hivyo licha ya kushiriki siku hiyo adhimu kwao bado wanaendelea kuhamasishana kujitoa kwa pamoja katika zoezi hilo.

Aidha alisema walianza na zoezi la usafi kubwa zaidi ilikuwa ni kuchangia damu na hamasa kubwa sana ambayo imetokea kwa mkoa huo kwa wana Simba na matawi yote wameungana kwa pamoja kwa ajili ya zoezi hili la kuchangia damu

Hata hivyo alisema kwamba wanajua damu ni muhimu sana kwa kila mmoja hasa ukizingatia wapo wakina mama wanaojifungua katika hospitali ikiwemo ajali zinatokea watu wanahitaji kuwekewa damu kwa hiyo wao wamehamasika kama wanajamii ukiachana na suala la michezo.

Tambo 

Mwenyekiti huyo alisema kwamba dhamira yao kubwa msimu huu lazima timu yao ichukue Ubingwa kutokana na uwepo wa kikosi kipana kulingana na usajili mkubwa uliofanyika wakiamini lazima timu hiyo ifanye makubwa katika mashindano ya ndani na hata kimataifa pia.

Katika hatua nyengine, Mdime alituma salamu kwa watani zao timu ya wananchi Yanga kuelekea mechi za Ngao ya jamii zitakazo chezwa Mkwakwani Tanga ambapo ametamba kwa kusema kuwa hawatakuwa tayari ngao hiyo aichukue tena mtani mbele yao.

Mchezo huo unatarajiwa kucheza Agosti 9 mwaka huu katika uwanja wa CCM Mkwakwani Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa Ngao ya jamii watakutana na matajiri wa Chamanzi Azam FC huku Simba SC wao wakiminyana na Singida Fountain Gate katika hatua ya nusu fainali timu zote zikitafuta nafasi ya kuanza vyema msimu 2023/2024 .