ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 5, 2025

MANISPAA YA KIBAHA YAJA NA MPANGO WA KUSAIDIA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI

 

NA VICTOR MASANGU, KIBAHA 

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani imeweka mipango madhubuti na kujipanga vilivyo ambayo itaweza kusaidia kwa kiwangon kikubwa  katika kuhakikishwa kwamba  maambukizi mapya ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi (VVU) hususan kwa upande wa  maambukizi ya  kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto  yanapungua kwa kiwango kikubwa.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa huduma za ukimwi katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr. Mariam Nganja kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji Dr. Rogers Shemwelekwa  wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani ambayo yamefanyika katika viwanja vya mwendapole na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, wakuu wa idara  watumishi wa  afya pamoja na wananchi  kutoka maeneo mbali mbali.
Mratibu huyo amesema kwamba katika kutekeleza mipango hiyo ya kupunguza maambukizi ya VVU amewahimiza wananchi wote kujenga tabia ya kwenda kupima afya zao mara kwa mara ili kuweza kufahamua hali ya afya zao ikiwemo kufahamu na kujua utambuzi kama wameambukizwa lengo ikiwa ni kuanza kupatiwa dozi ya matibabu kwa haraka.


Aidha amebainidha kwamba kwa sasa hali  ya maambukizi wa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha bado yapo juu hivyo kunahitajika juhudi za makusudi ikiwemo kukemea vikali vitendo vya ubakaji,ilawiti,ukatili wa kijinsia pamoja na baadhi ya tabia ambazo zinapelekea tabia ya maambukizi ya ugonjwa wa VVU.

 Kwa upande wake Afisa utumishi wa Halmashaurii ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela ambaye ndiyr aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amewataka wananchi wote kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja katika kutokomeza maambukizi mapya  ya  ugonjwa wa virusi vya ukimwi.

Pia amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutenga fedha nyingi katika Halmashaurinya Kibaha amabazo zimeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza miradi mbali mbali ya kimaendeleo amabzo zimeweweza kugusa katika sekta tofauti tofauti ikiwemo suala la kuboresha afya.

Pia amebainisha kwamba Rais katika kuhakikisha anaboresha huduma ya afya kwa wananchi ameweza kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Liulanzi ikiwa sambamba na kununua vifaa tiba amabvyo vimeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kuwasogezea huduma ya upapatikanaji wa huduma.

Naye Kaimu mganga mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr.Abdulkadri Sultan ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuimarisha miundomibu katika  vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali ikiwemo suala la upatikanaji wa vifaa tiba pamoja na madawa kwa ajili ya wananchi.

Maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani katika Halamshauri ya Manispaa ya Kibaha yamefanyika katika viwanja vya mwendapole ambapo Kauli mbiu ya mwaka huu  inasema kwamba shinda vikwazo imarisha mwitikio tokomeza ukimwi kwa mwaka 2025.

CCM PWANI HAWANA DOGO WAMPA MAUWA YAKE RAIS DKT.SAMIA KWA HOTUBA YAKE YENYE TIJA KWA TAIFA

 


Na Victor Masangu,Kibaha


Katibu  wa Siasa ,Uenezi  na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Dkt. David  Mramba   amesema ameipongeza kwa dhati hotuba ya Mhe.Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan  aliyoitoa tarehe Disemba  2 mwaka huu alipozungumza  na wazee wa Jiji la Dar es Salaam na kubainisha kuwa  imegusa masuala  muhimu  yanayohusu Taifa  na kutoa dira na  matumaini  makubwa  kwa maslahi ya kuleta maendeleo  kwa  wananchi wa Tanzania.

  Dkt.Mramba amesema hayo leo tarehe 5 Desemba 2025  katika mkutano na Waandishi  wa Habari uliofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya CCM  wa.  Pwani.

" Chama Cha Mapinduzi  Mkoa wa Pwani  kinaunga mkono  kwa kauli moja kama ifuatavyo;kuimarisha  amani ya Muungano, tunaunga  mkono  msisitizo wa Mhe. Rais  juu ya kulinda amani, utulivu na mshikamano wa Taifa letu kwani amani ndiyo  msingi  wa maendeleo  na hotuba yake imeonesha  dhamira  ya dhati  ya kuendeleza maridhiano,umoja na kudumisha  muungano wetu.

Mramba  amesema kuwa katika kuchochea  uchumi na fursa  za maendeleo Chama Cha Màpinduzi  Mkoa wa Pwani  wanapongeza kwa moyo wote  maelekezo  ya Mhe. Rais  kuhusu  kuendeleza  mageuzi  ya kiuchumi ,kukuza utekelezaji, kuimarisha  miundombinu  na kutengeneza ajira kwa wanawake.

"Katika hotuba ya Mhe.Rais  ameweka wazi  kuwa Serikali  inaendelea  kujenga  mazingira  rafiki ya biashara  na kuhakikisha  matunda  ya uchumi  yanawafikia  wananchi wake" amesema Dkt. Mramba.

Aidha Dkt. Mramba amesema kuwa  Mhe.Rais amesema kuwa  atahakikisha anasimamia  utawala bora  na mapambano  dhidi ya rushwa pia  kwamba CCM  Mkoa wa Pwani  wanaunga  mkono kauli ya Mh.Rais ya kuendeleza  vita dhidi ya  rushwa ,ubadhirifu na matumizi mabaya  ya madaraka kauli yake imedhihirisha kuwa Tanzania  inaongozwa  kwa misingi  ya  haki  uwajibikaji na uwazi.

" Chama Cha Mapinduzi  Mkoa wa Pwani  tunapongeza dhamira  njema  ya Serikali  katika  maeneo yafuatayo:
kuimarisha  sekta  ya afya, kuboresha elimu,kutoa wigo mpana  wa upatikanaji wa maji safi, kuhakikisha huduma bora  za kijamii kwa wazee,vijana  na makundi zinapatikana  kwa wakati ,katika kipengele pia ikumbukwe kuwa  hotuba  ya Mhe.Rais  Inaonesha Uongozi  shirikishi  unaoweka mbele utu na ustawi wa Watanzania" amesisitiza  Dkt. Mramba.

Kuhusu ushirikiano  wa ushirikishwaji wa wazee  amesema ,"CCM  Mkoa wa  Pwani tunaunga  mkono kwa  dhati  utayari wa Mhe. Rais  kusikiliza ushauri wa wazee ,kuthamini mchango wao na kutambua  kama nguzo muhimu ya hekima na utulivu  wa taifa letu".

Dkt. Mramba amehitimisha kwa kusemakuwa  CCM Mkoa wa Pwani  wanaunga mkono hotuba ya Mhe. Rais Samia  kwa sababu kuu nne ikiwa ni pamoja na kuweka  mwelekeo  sahihi wa taifa ,inajenga
matumaini  kwa watanzania ,inasisisitiza mshikamano na inaweka  msingi  wa maendeleo  endelevu  kwa vizazi  vya sasa  na vijavyo.

" Sambamba na  na hayo yote ,Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa wa Pwani  tunampongeza  Mhe.Rais Dkt Samia  Suluhu  Hassan  kwa  uongozi wake  mahiri , wenye hekima  na wa kijasiri kwa kuonesha  uzalendo wa kweli  katika  kulipigania  Taifa. 
CCM  Mkoa wa Pwani kwa umoja wetu, tunaahidi, kushirikiana  na  serikali katika  kutekeleza maelekezo  yote  yaliyotolewa  kwa  manufaa na maslahi ya Taifa.

Tuesday, December 2, 2025

DC KIBAHA AKABIDHI GARI LITAKALOTUMIKA KUBORESHA HUDUMA KATIKA DIVISHENI YA ARDHI

 

NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon,(Hapo Juu Pichani Kushoto) amekabidhi rasmi gari jipya kwa Divisheni ya Ardhi na Mipango Miji, lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kuwafikia wananchi kwa haraka zaidi katika utatuzi wa changamoto za ardhi.

Makabidhiano hayo yamefanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Akizungumza wakati wa kukabidhi gari hilo, Mhe. Simon alisema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameweka kipaumbele katika utatuzi wa migogoro ya ardhi na upatikanaji wa maeneo ya viwanda na uwekezaji.

“Hili gari limeletwa ili muweze kuwafikia wananchi kwa haraka na kuhakikisha changamoto za ardhi zinatatuliwa kwa wakati. Nawaomba mlitunze na mlitumie kwa kazi iliyokusudiwa,” alisema Mhe. Simon, huku akimpongeza Mkurugenzi wa Manispaa, Dkt. Rogers Shemwelekwa, kwa kutekeleza maagizo kwa ufanisi.

Awali, akiwasilisha taarifa fupi, Dkt. Shemwelekwa alibainisha kuwa gari hilo linathamani ya shilingi milioni 170, na litakuwa nyenzo muhimu katika kuongeza kasi ya utoaji huduma bora hususan katika Divisheni ya Ardhi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Divisheni ya Ardhi, Denis Kahumba, amesema changamoto ya usafiri ambayo ilikua ikikwamisha utendaji sasa imepatiwa ufumbuzi.

“Ahadi yangu ni kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi. Tunashukuru kwa vitendea kazi na mazingira mazuri ya kazi ambayo yameongeza morali kwa watumishi,” alisema Kahumba.

Naye, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Pwani, Rugambwa Banyikila, ametoa pongezi kwa uongozi wa Manispaa ya Kibaha kwa kutatua changamoto zilizokuwa zikikabili ofisi ya ardhi na kuwataka watumishi kuongeza bidii na uwajibikaji.

Makabidhiano haya yanatarajiwa kuongeza kasi ya usimamizi wa ardhi, kutatua migogoro, na kuimarisha huduma kwa wananchi wa Kibaha, huku yakiendana na dira ya Serikali ya kujenga mazingira bora ya uwekezaji na maendeleo.

DR. NICAS KUNOGILE AKWEA PIPA NAFASI YA UMEYA HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA

 


Na Victor Masangu,Kibaha 


Diwani mteule wa Kata ya Tumbi  Dkt. Nicas Mawazo amechaguliwa kuwa Meya mteule wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha baada ya kupata kura 15 kati ya kura halali zipatazo  19 ambazo zimepigwa na madiwani  wateule wa chama cha mapinduzi (CCM)  huku Aziza Mruma akichaguliwa kuwa katika nafasi ya Naibu meya kwa kupata kura 10 .

  Akitangaza matokeo hayo ya uchaguzi wa ndani wa chama Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Issack Mawazo amebainisha kwamba zoezi zima uchaguzi huo umemalizika  salama na kwamba viongozi  hao wateule wanatarajiwa kuapisha Disemba 4 mwaka huu  

Katibu huyo amefafanua kuwa zoezi hilo la uchaguzi limekwenda vizuri na kwamba  wagombea wote wameridhishwa na matokeo hayo na kuwahimiza viongozi hao kuvunja makundi na badala yake wawatumikie wananchi.


Kwa upande wake Meya mteule kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM ) Dr,Nicas Mawazo  amesema kwamba uchaguzi huo umeendeshwa kwa haki na uhuru na kwamba matarajio yake makubwa ni kushirikiana na madiwani wenzake katika kuwaletea chachu ya maendeleo ikiwa pamoja na kuwapambania wananchi walio wanyonge.

 Naye Naibu Meya mteule  waa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Aziza Mruma amesema kuwa lengo lake kubwa ni kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo.

Viongozi hao waliochaguliwa katika nafasi za Meya na Naibu Meya   Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha wanatarajiwa kuapishwa rasmi  Disemba 4 mwaka huu.

Monday, December 1, 2025

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI JUU YA KAMPENI YA KUWAPELEKA WATOTO SHULE

MWANDISHI:- VICTOR MASANGU, PWANI MTANGAZAJI:- ALBERT G.SENGO Naibu waziri Ofisi ya Waziri mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Reuben Kwagilwa anayeshugulikia masuala ya elimu amewaagiza wakurugenzi wote nchi nzima kufanya kampeni kwa ajili ya kuwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka na kuwaandikisha watoto wao shule za awali na msingi pindi ifikapo Januari mwaka 2026, Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja ambapo ameweza kugagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambayo imejengwa katika eneo la Disunyara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani na kumwagiza mkandarasi kumaliza mradi huo kwa muda uliopangwa.

Sunday, November 30, 2025

STANBIC BANK MWANZA YAFANYA KWELI SEKTA YA AFYA MWANZA

 NA. ALBERT G.SENGO/MWANZA

Benki ya Stanbic imeonesha tena dhamira yake ya kusaidia jamii kwa vitendo, baada ya kukabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 19 kwa uongozi wa Mkoa wa Mwanza. Vifaa hivyo ambavyo ni pamoja na vitanda vya wagonjwa, mashuka na viti mwendo, vitapelekwa katika Hospitali za Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, ili kusaidia katika utoaji wa huduma bora za afya. Kutoka kwa mwanahabari wetu Albert G. Sengo., anashuka na taarifa kamili