ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 15, 2024

MAFIA BOXING PROMOTION WAUNGA MKONO KAMPENI YA RAIS DKT SAMIA SULUHU YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

 

  

Na Oscar Assenga,TANGA

KAMPUNI ya Mafia Promotion Boxing imetoa msaada wa majiko ya Gesi kwa wanawake wanaojishughuli na uuzaji wa vyakula katika masoko ya Mgandini, Makorora na Mlango wa Chuma yaliyoko jijini Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu ya matumizi ya Nishati Safi ya kupikia.

Licha ya kugawa mitungi hiyo ya gesi lakini wametoa msaada mwengine wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulea watoto yatimacha Green Cresent Ophanege Foundation cha Jijini humo .

Hatua ya kampuni hiyo kuunga mkono juhudi hizo inatokana na ushindi walioupata mabondia mbalimbali wanaodhaminiwa na kampuni hiyo ambao walipata ushindi katika mapambano yao walipopanda hivi mwanzoni mwa mwezi 0ctoba mwaka huu Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Mkurugenzi wa Matangazo na Uzalishaji kutoka Kampuni ya Mafia Promotion Omari Clayton alisema pambano hilo lilichagizwa na Technical Knock Out ‘KO’ ya Rais Dkt. Samia Suluhu.

Alisema baada ya ushindi huo wapewa fedha taslimu kama zawadi kwa mabondia hao ambayo imewatia hamasa kuhakikisha wanazidi kuijengea heshima Tanzania kupitia mchezo wa ngumi.

Alisema kwamba jambo ambalo wameifanya kwa kugawa majiko hayo ya gesi ni kama sehemu ya kurudisha kwa jamii ikiwa ni utaraibu wao na wanaungana na watanzania kupitia Kampeni ya Rais Dkt. Samia ya kuhamasisha juu ya matumizi ya nishati safi na kuachana na matumizi ya mkaa na kuni katika kupikia na shughuli nyingine hali ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi na uzalishaji wa hewa ukaa.
Alisema kwamba kampuni hiyo ya Mafia wanaunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kupambana na kuhamasisha watanzania kuhama kutoka kwenye matumizi ya mkaa na kuni kupikia na kwenda kwenye matumizi ya nishati safi.

“ Ndio maana leo tumegawa majiko ya gesi kwa mama zetu wanapika vyakula katika masoko yaliyopo katika jiji la Tanga” Alisema Clayton.
“Tumehamasika na tunampongeza sana Rais wetu Dkt. Samia kuja na ‘KO ya Mama’ na kuwazawadia mabodia wetu ambao walipambana kuhakikisha wanabakisha mikanda hapa Tanzania na walifanikiwa na tunamuahidi kwamba mama kupitia Mafia Boxing tutazidi kuiheshimisha Tanzania”Alisema .

Akizungumza kwa niaba ya mabondi wenzanke Ibrahim Mafia alisema kwamba haikuwa rahisi kupamba ulingoni kutokana na mpinzani wake kuwa imara lakini kupitia maombi ya watanzania alipambana kuhakikisha anawapa furaha kwa kupata ushindi .

“Ule ushindi ni ushindi ni ushindi wetu lakini pia ni ushindi wa watanzania walikuwa wakituombea tumepokea zawadi kutoka kwa Rais wetu mama Samia tukaona hatuwezi kuitumia peke yetu bali tushirikiane kile ambacho tumepata kwa kuwapa majiko ya gesi na kutoa msaada kwa kituo cha watoto yatima tunaomba mzidi kutuombea dua ili wakati mwingine tuweze kutoa kikubwa zaidi. Alisema Mafia”

Bondia Ibrahim Mafia alipanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake Enoch Tettey raia wa Ghana kuwania mkanda wa dunia ‘World Boxing Council Bantamweight’ wenye uzito wa Kg 53 katika ukumbi wa City Center Hall Magomeni Sokoni na hatimaye kufanikiwa kubwaga chini mpinzani wake kwa KO.
Hata hivyo wakina mama mntilie ambao walipata majiko hayo waliwapongeza mabondia wote kwa ushindi walioupata pamoja na kuishukuru Kampuni ya Mafia Boxing Promotion kwa kuwapatia mitungi ya gesi ambayo itawasaidia katika shughuli zao.
Tunawashukuru kwa zawadi zenu na sisi tunaendelea kuwaombea kwa Mungu hakika atawalipa tulikuwa na changamoto ya kupata mkaa kwa ajili ya kupikia lakini sasa kupitia majiko haya yatatusaidia kurahisisha shughuli zetu za kupika kila siku .

Monday, October 14, 2024

RAIS SAMIA APOKEA MWENGE WA UHURU KWENYE KILELE CHA MAADHIMISHO MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wakati akihitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge ambazo kitaifa zimefanyika Jijini Mwanza katika Uwanja wa CCM Kirumba tarehe 14 Oktoba, 2024.

 "Nimehitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru pamoja na Wiki ya Vijana hapa mkoani Mwanza. Ninawashukuru wote waliojitokeza kushiriki tukio hili la kihistoria ambapo Mbio za Mwenge wa Uhuru zimefikisha miaka 60."

"Pongezi kwa wote walioshiriki kuukimbiza kwa mwaka huu na kazi nzuri waliyofanya ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo"


"Nimepokea taarifa ya miradi yote iliyotembelewa katika mbio hizi ambayo inakwenda kunufaisha wananchi kwenye kila kona ya nchi yetu. Nimepokea mapendekezo na salamu za wananchi wa maeneo yote ulikopita Mwenge wa Uhuru, na kwa umakini na uharaka tutayafanyia kazi yale yote yaliyoainishwa kwa manufaa ya Taifa letu"

RAIS wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 14, 2024 amewaongoza Viongozi na Wananchi mbalimbali kwenye kilele cha mbio za Mwenge zilizoambatana na Wiki ya Vijana na Nyerere Day katika uwanja CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Rais Samia akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Ndugu Godfrey Eliakim Mzava kwenye Kilele cha Maadhimisho Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
Matukio mbalimbali katika kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.


TASAC YAFANYA MAZUNGUMZO NA KANALI MTAMBI KUIMARISHA USALAMA WA USAFIRI MAJINI

 





Katika jitihada zake za kuendelea kuimarisha utekelezaji wa majukumu yake, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limekutana na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi kuzungumzia masuala ya usalama wa usafiri wa majini kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa.


Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kanali Mtambi ameipongeza TASAC kwa hatua mbalimbali wanazochukua kuimarisha masuala ya usafiri wa majini na ushirikiano wanaoutoa katika Mkoa wa Mara na hususan usalama wa wasafiri katika katika Ziwa Victoria.


Kanali Mtambi ameiomba TASAC kuendelea kutoa elimu kuhusu sheria na kanuni zinazohusiana na usafiri wa majini kwa wananchi na taasisi za Serikali na binafsi ili kupunguza ajali na athari za ajali za vyombo vya usafiri wa majini.


“Sisi kama Serikali tunatakiwa kuendelea kuwahakikishia usalama watumiaji wa Ziwa Victoria ikiwemo wasafiri wanaotumia vyombo vya usafiri vya majini kuhusiana na usalama wao wanapotumia usafiri wa majini,” amesema Mhe. Kanali Mtambi.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Udhibiti, Ulinzi, Usalama na Utunzaji wa Mazingira na Usafiri wa Majini, Bi. Leticia Mutaki amesema TASAC inaendelea na jukumu lake la utoaji wa elimu ya usalama wa usafiri majini kwa wadau wa mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo taasisi na Halmashauri kuhusiana na usimamizi wa usafiri wa majini.


“Tuna mpango wa kuingia katika makubaliano ya ushirikiano na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Halmashauri zote zinazopakana na ziwa ili Halmashauri zisaidie kusimamia usafiri wa majini kwa niaba ya TASAC,” amesema Bi. Mutaki.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TASAC, Bi. Judith Kakongwe amesema Sheria na kanuni za sasa zinawabana zaidi wenye vyombo vya usafiri kuweka jaketi okozi lakini haziwabani abiria kuzivaa jambo ambalo linaleta changamoto kwa sababu wamiliki wakiweka bila kuvaliwa hazisaidii kama inatokea ajali.


“Tupo kwenye mchakato wa kubadili vipengele vya sheria na kanuni ili abiria nao wabanwe kuvaa jaketi okozi na sio tu wamiliki wa chombo kama ilivyo sasa ili kusaidia kupunguza madhara ajali zinapotokea” amesema Bi. Kakongwe.


TPA kuanza usimamizi wa mwalo wa Kirumba wilayani Ilemela

 

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) inatarajia kuanza rasmi usimamizi wa shughuli zote za kibandari katika mwalo wa Kirumba ulipo Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza kufuatia tangazo lililotolewa kwenye gazeti la Serikali.

Akitoa taarifa kwa umma Ijumaa Oktoba 11, 2024 kupitia waandishi wa habari, Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge alisema hatua hiyo ni utekelezaji wa tangazo la Serikali namba 855 la tarehe 24/12/2023 ambalo linaipa TPA mamlaka ya kusimamia mialo yote iliyo rasmi.

Lugenge aliongeza kuwa shughuli za usimamizi wa mwalo huo zitaanza kesho rasmi Jumamosi Oktoba 12, 2024 zikihusisha usimamizi wa usalama wa vyombo vya majini.

Awali mwalo huo ulikuwa ukisimamiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ukiwa ni miongoni mwa mialo 10 katika Ziwa Victoria iliyotangazwa kusimamiwa na TPA.
Na George Binagi- GB Pazzo, Mwanza
Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge akitoa taarifa kwa umma kuhusu TPA kuanza kuusimamia mwalo wa Kirumba wilayani Ilemela.
Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge akizungumza na wanahabari jijini Mwanza.
Tazama Video hapa chini