ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 16, 2024

UANDIKISHAJI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WAFIKIA 45% NCHINI - WAZIRI MCHENGERWA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka wananchi kuendelea kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili waweze kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27, 2024.

Amesema hayo wakati akizungumza na  waandishi wa habari jana Oktoba 15, 2024  katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza kwa lengo la kufikisha elimu na hamasa kwa Wananchi  juu ya umuhimu wa kujiandikisha.


Mhe. Mchengerwa amewataka wananchi wenye sifa na wanaokidhi vigezo vya kugombea wajitokeze kuchukua fomu kuanzia Oktoba 26, 2024 mpaka Novemba 1, 2024 ili waweze kugombea  nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali za Mitaa na Vijiji.

Vilele Waziri Mchengerwa  amewataka wasimamizi wa uchaguzi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, kanuni, miongozo pamoja na maelekezo ya usimamizi wa uchaguzi.

"Maelekezo yangu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuzingatia kanuni viapo na kutekeleza majukumu kwa mujibu wa viapo vyao". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa.

Aidha Mhe. Mchengerwa amewataka Viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa kutoa elimu kwa wanachama wao juu ya kujiandikisha na kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Zoezi la kujiandikisha katika daftari la makazi limeanza rasmi  Oktoba 11, 2024 mpaka Oktoba 20, 2024 ambapo kila Mwananchi mwenye sifa na vigezo anatakiwa kujiandikisha katika eneo analoishi ili aweze kushiriki zoezi la Uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.