ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 24, 2023

WAKAZI WA MJI WA MOSHI WAOMBWA KUTUNZA HIFADHI YA MSITU RAU.

 

Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akizungumza na wakazi wa mji wa Moshi waliojitokeza katika uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU Forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).
Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho akisoma risala kwa Mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU Forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).
Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu akitoa shukrani wa wakazi wa Moshi na viunga vyake waliohudhuria katika uzinduzi katika kampeni ya kutangaza vivutio vilivyopo katika hifadhi ya msitu Rau.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori (wa pili toka kushoto) akiwa ameongozana na viongozi wengine wakipata maelezo toka kwa Afisa Uhifadhi wa msitu Rau wakati wakitembelea vivutio vilivyopo katika msitu huo.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG

...KAMPENI YA KUTANGAZA UTALII 'TWENDE TUKACHARU RAU' YAWA KIVUTIO KWA WAKAZI WA MOSHI, KILIMANJARO

Mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori ametoa rai wa Wananchi kuendelea kutunza hifadhi ya msitu wa Rau na kuacha tabia kutupa taka taka ndani ya hifadhi.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Amesema kuwa hifadhi ya Msitu Rau ni mapafu wa mji wa Moshi kwa vile husaidia kufyonza hewa chafu hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha unaendelea kutunzwa na kuacha mara tabia ya baadhi ya watu wanaovamia na kufanya shughuli za kibinadamu.

"Hakikisheni msitu huu unatunzwa, acheni kufanya shughuli za kilimo ndani hifadhi, acheni kuingiza mifungo ndani hifadhi," amesema.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akipitishwa katika mashamba ya mpunga.
Safari ya kutembelea vivutia vya hifadhi ya msitu wa Rau.
Utalii ukiendelea ndani ya hifadhi ya msitu Rau.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akiwa na wageni wengine wakitazama moja ya chemchem za maji zilizo katika msitu huo.
---
Pia ametoa rai kwa TFS na makapuni za watalii kuendelea kuwahamasisha watalii kutembelea vivutuo vilivyopo ndani msitu huo, kwani hifadhi hiyo ipo mita chache kutoka mji wa Moshi na inafikika kirahisi.

Amesema rais Dkt Samia Suluhu amefungua fursa za Utalii kupitia filamu yake 'Royal Tour', hivyo ni vyema kuendelea kuunga mkono juhudi zake ili kuweza kuongeza idadi ya watalii nchini na ndiyo maana Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi wakishirikiana na Ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS) Moshi wamezindua Kampeni ya Kutangaza Utalii ikolojia ndani ya Hifadhi ya Misitu wa Rau ili kuongeza idadi ya watalii.

Aliongeza kuwa mpaka sasa hivi hafurahishwi na idadi ndogo ya watalii wanaofika kutembelea msitu huo, lija ya ukaribu uliopo ambapo ni watalii 1,200 tu kwa mwaka hutembelea msitu huo.

Awali akisoma taarifa kwa niaba Mkuu wa hifadhi ya msitu Rau, Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho, amesema  ndani msitu huo kuna chemchem 20 ambazo zinapeleka kuwepo mito mikubwa 3 inayotiririsha maji kipindi chote cha mwaka.

Aidha amesema mito hiyo ni chanzo cha maji inayotumika katika kilimo cha umwagiliaji cha mpunga ambapo hekta takriban 3,000  hutegemea maji kutoka msitu huu.

"Msitu una vivutio vingi ikiwemo mimea pamoja na miti ya asili ambayo haipatikana katika maeneo mengine, ikiwemo Mti wa Mvule ambayo unazaidi ya miaka 200 ni mrefu kuliko yote barani Afrika," amesema.

Aliongeza kuwa utalii mkubwa unaofanyika katika msitu huo ni Utalii wa baiskeli, ibada,  tafiti na masomo, picha, nyuki na kuangalia madhari ya misitu ndege na wanyama wanaopatikana ndani ya hifadhi.

Mazoezi ya viungo nayo yalikuwepo katika ya kuingia msituni.
Waendesha baskeli nao walinyoosha viungo.
Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho akiwakaribisha wageni.
Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu akiwasalimia wageni.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori (kushoto) akiwa pamoja na Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu (kulia) wakizindua utalii wa baskeli.
Utalii wa baskeli nao ulifanyika.
Kwa upande wake Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu amefurahishwa na ubunifu wa kuandaa kampeni ili kutangaza vivutio vilivyopo katika hifadhi ya msitu Rau.

"Nawaomba waandaaji kuendelea kuandaa matamasha mengi zaidi yatakayosaidia wananchi wengi ili waweze kutembelea msitu huo na kujifunza mambo mbali mbali," amesema Meya Kidumu.

Hifadhi ya Misitu Rau ulianzishwa ukiwa na ukubwa  hekari 3526, ambapo kwa sasa ni hekta 584 zimebaki kutokana uvamizi wa Wananchi na kuanzisha shughuli za kilimo.

NSSF YATOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KATIKA KONGAMANO LA WANAWAKE NA MANUNUZI YA UMMA

 

Meneja wa Sekta isiyo rasmi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Rehema Chuma (kushoto) akimsikiliza Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga, Theresia Makyao mara baada ya kutembelea banda la NSSF wakati wa kongamano la Wanawake na Manunuzi ya Umma, linalofanyika jijini Tanga
Meneja wa Sekta isiyo rasmi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Rehema Chuma (kushoto) akifuatilia jambo wakati wa Kongamano la Wanawake na Manunuzi ya Umma Jijini Tanga
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), umeshiriki na kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa washiriki wa kongamano la Wanawake na Manunuzi ya Umma, linaloendelea jijini Tanga. 

Akizungumza wakati wa kongamano hilo Meneja wa Sekta isiyo rasmi, Rehema Chuma ambaye  alikuwa miongoni mwa waliotoa mada katika kongamano hilo lililoanza tarehe 23 Agosti, 2023, amesema kupitia kongamano hilo NSSF imetoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi ambayo imebeba kundi kubwa.

Kundi hilo kubwa ambalo sekta isiyorasmi ni  kama vile wakulima, wafugaji, wavuvi, mama lishe, bodaboda na wajasiriamali wengine wote ili waweze kujiunga na kuchangia katika Mfuko kwa maisha yao ya sasa na baadaye.

Lengo la kongamano hilo ni kueleza fursa za biashara zinazoambatana na mradi wa bomba la mafuta Afrika Mashariki (EACOP) hivyo mradi huo ni fursa kwa NSSF kupata wanachama wapya ambao watapata ajira za moja kwa moja na wale watakaonufaika na ajira za muda pamoja na wanufaika wengine kama vile mama lishe na bodaboda ambao wataweza kujiunga na kuchangia katika Mfuko.

Katika kongamano hilo, NSSF licha ya kutoa elimu ya hifadhi ya jamii pia itaeleza fursa mbalimbali zinazopatikana zikiwemo za nyumba na viwanja ambazo zinauzwa kwa bei nafuu.

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ahudhuria Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Johannesburg nchini Afrika Kusini

  


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Wakuu wa nchi na Serikali kwenye Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 24 Agosti, 2023.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa China Mhe. Xi Jinping kando ya Mkutano wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 24 Agosti, 2023.

 

Viongozi Wakuu wa BRICS wakiwa kwenye Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 24 Agosti, 2023.

TANZIA: MKURUGENZI WA VIGIMARK HOTEL ABEL MAJIGE AFARIKI DUNIA

 

Mkurugenzi wa Vigimark Hotel Mjini Shinyanga Abel Majige amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Alhamisi Agosti 24,2023 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan Nairobi nchini Kenya.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika familia, kesho jioni mwili utawasili uwanja wa ndege Mwanza na kwenda kuhifadhiwa Hospitali ya Kanda ya Bugando, Jumatatu mwili utafuatwa Bugando na kulala nyumbani Lubaga Shinyanga. 

Jumanne Ibada katika kanisa la A.I.C.T na mwili kusafirishwa kwenda Salawe kwa ajili ya mazishi siku ya Jumatano.

Tuesday, August 22, 2023

ZAIDI YA BILIONI 1.18 KUTATUA KERO YA MAJI TARAFA YA NAIPANGA NACHINGWEA

 

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo aliyesimama mwenye shati jeupe akimtambulisha mkandarasi wa mradi wa maji wa tarafa ya Naipanga Shaban Kimaro kutoka kampuni ya Broadway Engineering co.LTD wenye gharama ya zaidi ya bilioni 1.18 Kwa lengo la kutatua kero ya maji kwa kumtua mama ndoo kichwani
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Adinani Mpyagila akimshukuru Rais Dr Samia suluhu Hassan kwa kutatua kero ya maji katika Tarafa ya Naipanga
Meneja wa RUWASA wilaya ya Nachingwea Mhandisi Sultan Ndolwa akielezea namna ambavyo mradi huo utatekelezwa na kutatua kero ya maji kwa wananchi wa Tarafa ya Naipanga.


Na Fredy Mgunda, Nachingwea.

BAADA ya kilio cha miaka mingi cha wananchi wa Tarafa ya Naipanga wilayani Nachingwea kwa kukosa maji hatimaye serikali ya awamu sita imepeleka mradi wa zaidi ya bilioni 1.18 kutatua kero hiyo ya maji.
Akizungumza wakati wa kumtambulisha mkandarasi wa mradi huo,mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa alisikikiza kero za wananchi kuhusu tatizo la maji na wakazifanyia kazi.

Moyo alisema kuwa mradi huo utahusisha kata za Naipanga,Chiumbati,Rahaleo na Stesheni ambazo zitanufaika Moja kwa Moja na mradi utahudumia vijiji 11 na wananchi 19,110 lengo likiwa kuwatua ndoo akina mama wa Tarafa ya Naipanga.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dr Samia suluhu Hassan imekuwa sikivu kutatua kero za wananchi ndio maana hata mradi huo imekuwa rahisi kuupata.

Moyo aliwaomba wananchi kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza wakati wa mradi huo ukiwa unatekelezwa huku akiwataka kuacha tabia ya kuwaibia vifaa wakandarasi wanavyotekeleza mradi huo.

Kwa upande wa meneja wa RUWASA wilaya ya Nachingwea mhandisi Sultan Ndolwa alisema kuwa mradi utakuwa na tenki Moja lenye ujazi wa Lita za maji 300,000,uzio, vituo 40 vya kuchotea maji vyenye sehemu 2 Kila kimoja na mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilometa 32,425.

Mhandisi Ndolwa alisema kuwa mradi huo utakamilika baada ya miezi kumi na mbili Kwa mujibu wa mkataba aliosaini mkandarasi wa mradi huyo Broadway engineering Co LTD na mradi huo unajengwa chini ya mpango wa lipa Kwa matokeo na kusimamiwa na wakala wa usafi wa mazingira vijijini (RUWASA).

Naye mkurugenzi wa Broadways Engineering co. Ltd Shaban Kimaro alisema kuwa atakamikisha mradi Kwa wakati ili kuwatua ndoo kichwani wanawake kama ambavyo dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dr Samia suluhu Hassan inavyotaka.

Kimaro alisema kuwa anaomba ushirikiano na wananchi wa vijiji vyote vya Tarafa ya Naipanga katika kipindi chote ambacho mradi unatekelezwa.








Monday, August 21, 2023

TAMKO LA KAMATI YA AMANI MKOA WA MWANZA KUHUSU BANDARI

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

KAMATI ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Mwanza, inayoundwa na viongozi mbalimbali hii leo asubuhi imetoa tamko lake ikiishauri jamii kutumia busara katika kuyazungumzia masuala ya mkataba wa bandari, sanjari na kuiomba Serikali kuandaa makongamano ya elimu kwa wananchi ili kutoa maoni yao kwenye marekebisho ya vipengele vinavyoleta utata ndani ya mkataba huo tofauti na sasa ambapo kila mmoja anazungumza kivyake kwa lugha ngumu na zenye hasira mitandao bila muongozo.
Tamko hilo hilo lilitolewa mbele ya waandishi wa habari na Wenyeviti Wenza wa Kamati hiyo Askofu Dk. Charles Sekelwa na Sheikh Hasani Kabeke.