ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 1, 2018

RAIS WA ZAMANI MAREKANI AFARIKI DUNIA.



George H.W. Bush

Rais wa zamani wa Marekani George H.W. Bush amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 94 huko mjini Houston, msemaji wake Jim McGrath amethibitisha kifo chake.

Rais huyo wa zamani wa Marekani aliongoza kwa awamu moja tu akiingia madarakani mwaka 1989 na kuondoka 1993 hivyo kubaki kama Rais pekee aliyeiongoza Marekani kwa awamu moja.

Enzi za uhai wake marehemu George H. W. Bush (kulia) akiwa na mwanae George Bush Jr ambaye pia alikuwa Rais wa taifa hilo wa 43.
"Jeb, Neil, Marvin, Doro, and I are saddened to announce that after 94 remarkable years, our dear Dad has died," his son George Bush Jr, who went on to serve as the 43rd US president, said in a statement.
"[He] was a man of the highest character and the best dad a son or daughter could ask for."
HISTORIA YAKE KWA UFUPI.

AIBU NYINGINE KWA ZITTO ASHUKIWA NA KUAMBIWA AACHE UONGO


Sehemu ya Mataluma ya Reli yaliyoppo katik autekelezaji w amradi wa ujenzi wa Reli sgr Katika eneo la Soga Mkoani Pwani
Na. HABIB MCHANGE

Ninamfahamu vema sana Zitto Kabwe,  nina hakika kabisa hoja yake aliyoitoa leo kuhusu ujenzi wa reli ni ama hajui anachokisema au anaendelea na utaratibu wake ule ule wa kujifanya anajua kila kitu kuliko mtu yeyote hapa nchini

Kwa muda sasa Zitto amekuwa akipambana kuuaminisha umma kuwa ni yeye tu ndio Mtanzania mwenye akili kuliko mtu yeyote,  mwenye kujua kila kitu kuliko mtu yeyote,  mjanja kuliko kila mtu na ndie mwanasiasa mwenye kujua kuliko mwanasiasa yeyote kiasi cha kuwaona wenzake wote vilaza

Sisi tunaomfahamu Zitto na wenzake hatupati shida kuhangaika kumjibu anaporopoka maneno yake na data zake za kuunga unga

Zitto leo amesema serikali inakwamisha mradi liganga na mchuchuma kwa madai ya kitoto kabisa

Ama Zitto amesahau kuwa amekuwa kiongozi msimamizi wa Rasilimali mwenyekiti wa PAC kwa miaka mingi kuliko Mtanzania yeyote ikiwemo hiyo liganga na mchuchuma na wala hakuna cha maana alichoifanyia migodi hiyo mpaka leo

Pengine pia hajui kuwa serikali hainunui reli, hainunui taruma wala hainunui kitu chochote katika mradi wowote unaoendelea na badala yake manunuzi hufanywa na mkandarasi aliyeshinda zabuni na hivyo ni wajibu wake kuamua anunue nini wapi na kwanini huku serikali kazi yake ikiwa ni kuhakikisha inapatiwa huduma kwa kadri ilivyo kwenye mkataba

Leo Zitto hajui haya au porojo tu kama jana na juzi?.... anataka watanzania tushiriki kugombea tender zinazogombewa na makampuni ya kusambaza na kuuza chuma kweli?

Tumpuuzeni tu aisee na tuendelee kumuunga Mkono Rais Magufuli kwa kazi hii iliyotukuka anayoifanya

Nina hakika Zitto hana ufahamu wa kinachoendelea Site kuhusiana na mradi huu wa SGR.

Nimepita bahati ya kutembelea maendeleo ya mradi mkubwa na wa kihistoria wa ujenzi wa Reli yetu ya kisasa tena ya umeme wa Standard Gauge uliopangwa kujengwa kutoka DAR mpaka Mwanza na baadae kigoma na maeneo mengine ya nchi mradi ambao umewekwa kutekelezwa kwa awamu kadhaa huku awamu ya kwanza ikiwa ni DAR mpaka Morogoro KM 205 za njia kuu ya reli na zaidi KM 95 za mapishano na shughuli nyingine muhimu

Naomba nikiri hadharani,  kabla sijaenda kujionea kinachoendelea Site akili na mtazamo wangu juu ya mradi huu yalikuwa kama Zitto na wengine wanavyowaza.

Sikuwa nikijua kuwa mradi huu umeenda kuzalisha maelfu ya ajira za moja kwa moja kwa vijana na watu wa rika nyingine hapa nchini.

Sikuwa nikijua kuwa mradi huu umeongeza kwa kiasi kikubwa sana mnyororo wa kiuchumi

Nimeshuhudia kwa macho yangu tena zaidi ya mara moja namna vijana wa kitanzania wakitengeneza Mataruma yanayotumika kujengea reli hii muhimu ya kihistoria

Nimeona kwa macho yangu vijana wa kitanzania wakipata ujuzi wa kukunja nondo kitaalam zinazotumika katika maeneo mbalimbali ya ujenzi

Nimeona kwa macho yangu namna ambavyo mradi huu umeongeza kwa kiasi kikubwa sana uhaba wa saruji hapa nchini kutokana na uhitaji mkubwa wa bidhaa hiyo katika ujenzi wa mataruma,  madaraja, nguzo na  majengo mengine.

Mradi huu umenionyesha kwa sababu gani Nondo zimepanda bei mtaani kutokana na uhitaji wake mkubwa kwenye ujenzi wa mradi,

Kwa kifupi kabisa,kama Mtanzania nimefurahi sana kuona mradi unatumia malighafi na bidhaa zilizotengenezwa ndani kwa zaidi ya asilimia 50 ya mahitaji yake

Zaidi nimefurahi kuona Mataruma yanayotandikwa katika reli hii yanatengenezwa Tanzania katika kiwanda cha mataruma kilichopo Soga na baadae kiwanda kingine kitakamilika katika site ya Kilosa

Kifupi tu niseme,  kama kuna kitu Magufuli amewahi kukifanya na ataendelea kukumbukwa leo akiwa hai na kesho asipokuwepo basi ni uamuzi huu wa kiume wa ujenzi wa reli hii ya kisasa.

Magufuli ameendelea kutupa heshima sio tu watanzani lakini waafrika kwa ujumla wake kwa uthabiti na ushujaa huu.

Achana na habari ya mafanikio yake ya kihistoria katika sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo Afya, Elimu Bure, mapambano dhidi ya Rushwa, Ujenzi wa Miundombinu, ununuzi wa ndege na kadharika,  Hii ya Standard Gauge ni Heshima itakayodumu vizazi na vizazi.

Tumesoma shule ya msingi na baadae sekondari kuwa reli maarufu nchini inayoanzia Dar mpaka Kigoma ikipita pia mwanza kutokea Tabora (Reli ya Kati) ilianza kujengwa na wakoloni wa kijerumani  kati ya miaka 1905 na kuendelea.

Leo JPM ameamua kufuta historia hiyo ya wakoloni na kuandika historia mpya.  Naam historia mpya hii inaandikwa kwa kutumia fedha za ndani tena bila hofu wala wasiwasi wowote

Magufuli ametufanya tutembee kifua mbele.

Ukianza safari pale stesheni ukaona jinsi watu wanavyopiga kazi,  vyuma vikigongana,  magari yaliyobeba materials yakiwajibika utaelewa nini ninachokisema

Ukisogea shauri moyo ilala ukashuhudia ujenzi wa daraja la juu la zaidi ya Kilomita mbili na nusu litakalobadilisha pia mwonekano wa jiji la DAR,

Ukaambaa ambaa na reli ukafika Pugu na kushuhudia ujenzi wa stesheni ya kisasa ya eneo hilo lililo kilomita 20 kutoka stesheni hakika utasema Magufuli ANATENDA

Akitoka pugu akaambaa ambaa na njia ya mkandarasi inayojenga reli hiyo kuelekea soga,  njiani utajionea mwenyewe namna miamba ilivyopasuliwa, milima imechongwa tuta limewekwa kwa ustadi nakuhakikishia hautatamani kuacha kumpongeza JPM

ukifika Soga ukaona kambi ya ujenzi wa reli hiyo,  ukaona namna mataruma yanavyotengenezwa, ukaona reli iliyotandazwa juu ya tuta na ukasogea pembeni ukaona nyasi za kisasa zilizooteshwa kudhibiti uharibifu wa mazingira hauwezi kuelewa wala kusikiliza POROJO ZA ZITTO na wenzake

Ukisogea mbele ya soga kuelekea Ruvu,  ukakutana na Daraja kubwa la upana wa mita 11 na upana wa zaidi ya mita 6 linalotenganisha barabara na treni huku treni ikipita juu barabara chini,  nakuambia Zitto na wenzake wote wa aina yake lazima uwapuuze kama sio kuwadharau kabisa

Hebu sogea Ruvu basi kidogo,  nenda kajionee namna maji yalivyofinyangwa finyangwa kuweka njia ili mitambo ipite wewe,  Zitto huwezi muamini tena

Sogea basi Kwala pale,  ujionee eneo kubwa linalojengwa Marshalling Yard eneo ambalo zaidi ya treni yenye urefu wa kilomita mbili zinaunganishwa na kupishana huku pembeni kidogo pakiwa na bandari kavu, halafu Zitto na wenzake wanaleta hadithi za Arifu lela olela?

Toka Kwala sasa sogea mpaka Ngerengere uone shughuli nyingine zinazoendelea, njoo mpaka Moro mjini ujionee mitambo inavyofanya kazi halafu usikilize takataka za kina zitto hizi, utatamani kutema mate chini.

Toka Moro elekea Dodoma kupitia Kilosa na GULWE, angalia namna ambavyo wanaume wanachoronga milima ya kilosa ili kupitisha Treni mita 90 Ardhini,  halafu wahuni wachache wanasemaje?

Njoo mpwapwa uone namna vijana wanavyopiga kazi mchana na usiku kuelekea Ihumwa.  Weweeee? Acheni tu jamani

Hapo sijakueleza kuhusu idadi ya  ajira zilizozalishwa, unaambiwa zaidi ya watanzania 5900 wameajiriwa kufanya ujenzi wa mradi huu utakaodumu na kudumu katika akili za watanzania

Sijakwambia kuhusu madaraja, njia za juu, njia za chini, vivuko,  majengo ya stesheni na mambo mengine.

Sijakwambia pia juu ya namna elimu inavyopandikizwa kwa wazawa wanaoshuhudia ujenzi wa mambo mbalimbali kutoka kwa wataalam wa kimataifa.

Kuendelea kuwasikiliza wapotoshaji wa aina ya Zitto ambao wao kila kitu wanataka kufanya siasa ama kiki ni kujipotezea muda tu. Standard Gauge inajengwa kwa kasi ya ajabu na mwaka 2020 Zitto na wenzake watasafiri na reli hiyo hiyo wanayoionea donge

Ndimi tena
Habib Mchange
0762178678
Morogoro, Tanzania

UNAIDS KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUPAMBANA NA UKIMWI


 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde (wa pili kushoto) akiwasili kwenye viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Bi .Mwanahamisi Mukunda (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng (kulia) wakielekea kutembelea kijiji cha Vijana wakati wa hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yayonafanyika Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa kiufundi-FP wa shirika la JHPIEGO, Bi. Lena Mfalila (kushoto) kuhusu shughuli zinazoendeshwa na Shirika hilo kupitia mradi wa Tupange Pamoja (TCI)  ambayo ni huduma rafiki ya vijana katika afya ya uzazi kwa vijana wakati walipotembelea kijiji cha Vijana kwenye hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yayonafanyika Jijini Dodoma. Wengine katika picha ni Mtaalamu wa kiufundi-AYSRH wa shirika la JHPIEGO kupitia mradi wa Tupange Pamoja (TCI), Bw. Waziri Njau (katikati) pamoja na ‘Coacher’ -SRH wa shirika la JHPIEGO kupitia mradi wa Tupange Pamoja (TCI),Bi Rehema Mzungu.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akipata maelezo kutoka kwa Mratibu wa Uzazi Salama mkoa wa Dodoma wa Shirika la PSI Tazania, Bi. Sophia Jamal (kushoto) kuhusu elimu ya afya ya uzazi wanayotoa kwa mabinti kuanzia miaka 13-19 yenye kauli mbiu ya Binti “Dhamiria kutimiza ndoto yako-“Simama Imara” “Vaa Taji”, “Kua Mzuri” wakati alipotembelea kijiji cha Vijana kwenye hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yanayofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Bi .Mwanahamisi Mukunda aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na  Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko wakipata maelezo kutoka kwa Bi. Debora Frank (kushoto) ambaye ni Afisa Miradi wa Huduma za Vijana  wa shirika la EGPAF ambao wanaotekeleza mradi wa USAID wa Boresha Afya kwa kushirikiana na ENGENDER Health kuimarisha afya za watanzania wote na kuongeza upatikanaji wa huduma za afya timilifu za kiwango cha juu na jumuishi wakati alipotembelea kijiji cha Vijana kwenye hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yanayofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma. Mradi unaolenga kuboresha huduma za kinga na matibabu ya VVU/UKIMWI, uzazi wa mpango, Kifua Kikuu na kutoa huduma mahususi wa kuyafikia makundi  maalum kwa watoto na vijana.
 Pichani ni Hawa Musa (20) mmoja kati ya vijana zaidi ya 2000 wanaonufaika na mafunzo ya ujasiriamali yaliyofadhiliwa na Shirika la EGPAF ambapo mafunzo hayo yamewasiaida kutengeneza bidhaa mbalimbali  ikiwemo vikoi, mikoba ya shanga, Ubuyu, sabuni za maji na miche ambazo zinawasaidia kupata fedha za matumizi mbalimbali akishiriki kuonyesha kazi zake katika mabanda ya kijiji cha Vijana wakati wa hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yanayofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akipata maelezo kutoka kwa Meneja masoko wa Shirika lisilo la kiserikali la T-MARC Tanzania, Bi. Sophia Komba kuhusu shirika hilo linalotoa elimu kuhusu matumizi ya Kondomu ili kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya ngono ikiwa pamoja na UKIMWI katika mabanda ya kijiji cha Vijana wakati wa hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma. T-MARC Tanzania wanafanya kazi kwa kushirkiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto katika kuboresha afya ya jamii ya watanzania ambapo pia ni wasambazaji wa bidhaa za afya ambazo ni Kondomu ya kiume- Dume, Kondomu ya kike Lady Pepeta na vidonge vya uzazi wa mpango-Flexi P. Wa pili kushoto ni Outreach Educator wa T-MARC Tanzania, Dotto Iddy.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde, Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko,  Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Bi .Mwanahamisi Mukunda pamoja na Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng wakipata maelezo kutoka kwa Mshauri mwandamizi wa masuala ya afya ya uzazi kwa vijana kutoka mradi wa Sauti unaratibiwa na Shirika la JHPIEGO, Esther Majani (wa kwanza kushoto) kuhusu shughuli wanazofanya za kutoa elimu ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa makundi hatarishi ikiwemo mabinti walio nje ya shule wa miaka 15-24 wakati walipotembelea kijiji cha Vijana kwenye hafla ya kuhitimisha wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi yaliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
 Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Bi .Mwanahamisi Mukunda akizungumza jambo kwa niaba ya Mkuu mpya wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Bilinith Mahenge wakati akimkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akihutubia wananchi wa Dodoma wakiwemo vijana wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
 Balozi wa Vijana ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mh. Jokate Mwegelo akizungumza na hadhira ya vijana (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Madawa ya Kulevya na Ukimwi ambaye pia ni Mbunge wa Biharamulo, Mhe. Oscar Mukasa akitoa salamu za kamati yake wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko akitoa neno kwa mgeni rasmi Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Balozi wa Vijana ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mh. Jokate Mwegelo akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Msanii wa Bongo Flava Maua Sama akitoa burudani kwa wakazi wa Dodoma wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Mchekeshaji maarufu nchini Stan Bakora akitoa burudani ya kuhamasisha upimaji wa UKIMWI kwa njia ya vichekesho wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Afisa Maendeleo Vijana wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Tumsifu Mwasambale (kushoto) akionyesha moja ya picha iliyoshinda wakati wa wiki ya shughuli za kijiji cha vijana iliyochorwa kijana Edward Malongo na kupigwa mnada ambapo zaidi shilingi 2.7 zilipatikana ambapo nusu zilienda kwa mchoraji na nyingine kwenye mfuko wa udhibiti wa Ukimwi (ATF) wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akikabidhi zawadi ya kombe ya mshindi wa kwanza kwa kapteni wa timu ya mpira ya vijana walio nje ya shule ya Panama, Bw. Dunia Salumu wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mh. Antony Mavunde akikabidhi zawadi ya kombe ya mshindi wa kwanza kwa kapteni wa timu ya mpira wa pete ya Vijana Queens, Ngesa Selemani wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
 Pichani ni baadhi ya kazi za mshindi wa kwanza katika eneo la uchoraji Edward Malongo (tisheti nyeupe)  wa picha zinatoa ujumbe wa kuhamasisha kampeni ya kutokomeza VVU zikionyeshwa kwa wageni wa meza kuu wakati wa hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.

Pichani juu na chini ni sehemu ya wakazi wa Dodoma walioshiriki hafla ya kufunga wiki ya shughuli za vijana kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.

UNAIDS kuendelea kushirikiana na serikali kupambana na UKIMWI
Na Mwandishi wetu
Mkurugenzi Mkazi na Mwakilishi wa Shirika la Kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa (UNAIDS) nchini, Dk. Leo Zekeng amesema kuwa kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano dhidi ya Ugonjwa huo.

Akizungumza jana Jijini Dodoma wakati wa kilele cha shughuli za vijana kuelekea maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani, Dk Zekeng alisema kwamba kuna haja kubwa ya kuhakikisha kwamba taifa linapambana na maambukizi mapya kwa kuhakikisha kwamba kunatolewa huduma rafiki miongoni mwa vijana ambao ndio kundi kubwa linalohitaji msaada kwa sasa ni jukumu la kila mwanajamii na kuomba ushirikiano wadau wote katika mapambano hayo.

Alisema wakati taifa nusu yake ni vijana wenye umri kati ya miaka 15-24 na huku takwimu zikionesha kwamba kundi hilo linaathirika sana ipo kila sababu ya kutengeneza mkakati na kuweka mazingira rafiki ili kuokoa kizazi hicho.

Alisema kwa sasa vijana wanahitaji kusaidiwa kwa kuwaweka katika mazingira rafiki ya kuhitaji huduma zinazotolewa katika kampeni ya kukabiliana na maambukzi ya VVU.

Alisema kwa sasa huduma hizo si rafiki ziko chache na hivyo kuwafanya vijana wasishiriki kwa sababu ya hofu ya kunyanyapaliwa na pia kukosekana kwa elimu hitajika.

Aliongeza ili taifa lifikie uchumi wa kati unaotakiwa mwaka 2025 na kufikia agenda 2030 ni lazima liwe ni taifa lenye vijana wanaojitambua na wenye afya bora.

“iko haja ya kushawishi vijana ambao ndio kundi kubwa kujitambua na katika package nzima wajue namna ya kujikinga, na kuishi kwa afya hata kama wana virusi” alisema Dk Zekeng  na kusisitiza kwamba shirika lake litaendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha kwamba vijana wanapatiwa elimu ya kutosha na mahitaji mengine katika vita dhidi ya UKIMWI.

Alibanisha kuwa takribani watu milioni 37 Duniani wanaishi na Virusi vya UKIMWI na sehemu kubwa wakiwa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Siku ya UKIMWI Duniani huadhimishwa kila ifikapo Disemba Mosi kila mwaka ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema Pima Jitambue, Ishi ambapo mwaka huu yanafanyika Jijini Dodoma na Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Warizi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa.

JAMII YAASWA KUACHA FIKIRA POTOFU JUU YA UGONJWA WA KIFAFA

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwasilisha utafiti wake juu ya Ugojwa wa Kifafa katika muhadhara  wa Kiprofesa uliofanyika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS). Profesa Matuja alifanya utafiti wa Ugonjwa wa Kifafa kwa muda wa miaka minne katika Wilaya ya Mahenge, Morogoro. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mwenyekiti wa Muhadhara huo, Prof. Gadi Kilonzo akifungua majadiliano ya kuulizana maswali juu somo la ugonjwa wa kifafa alilolitoa Profesa William Matuja (kushoto).
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwasilisha utafiti wake juu ya Ugojwa wa Kifafa katika muhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS). Profesa Matuja alifanya utafiti wa Ugonjwa wa Kifafa kwa miaka minne katika Wilaya ya Mahenge, Morogoro.
Wageni waalikwa wakifuatilia muhadhara huo.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kushoto) akikabidhiwa zawadi ya cheti shukrani na Mhadhiri mwandamizi idara. Dkt. Tumaini Nagu mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa. Katikati ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani Dkt. Patricia Munseri.
  Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kulia) akikabidhiwa zawadi na Mhadhiri mwandamizi idara ya Magonjwa ya Ndani Dkt. Tumaini Nagu mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa.
 Dkt Pilly Chillo akikabidhi zawadi ya ua.
  Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kulia) akikabidhiwa zawadi na Kaimu Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani Dr. Patricia Munseri  mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa.
 Afisa Uhusiano wa MUHAS, Hellen Mtui akitoa shukrani kwa wageni waliofika katika muhadhara huo.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na wanafamilia.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na wafanyakazi wa kitengo chake.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Imani potofu ndiyo inayopelekea kuongezeka wa Ugonjwa wa Kifafa katika maeneo mbali mbali ya nchi ya Tanzania hasa Wilaya ya Mahenge, Morogoro.

Hayo ameyasema Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja wakati akiwasilisha ufatifi wake katika muhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ili kuweza kutoa mapendekezo yake njia za kuweza kusaidia jamii.

Profesa Matuja amesema Jamii inahitaji kuondokana na imani potofu maana watu wengi wamekuwa wakijua kuwa ugonjwa unasambabishwa na ushirikina.

Ameongeza kuwa jamii ni bora kujitokeza kupima mara kwa mara ili kuweza kupatiwa tiba mahususi ili kuweza kuondokana na tatizo hilo.

"Nimefanya utafiti katika wilaya ya Mahenge, Morogoro ila tulichogundua mwanzo ni jamii haikuwa na ueleza zaidi kuhusiana na ugonjwa wa kifafa na hivyo kupelekea watu wengi sana kuugua ugonjwa huo, lakini wengi wao wanafikiria imani potofu hasa haya mambo ya ushirikina," ameongeza Prof Matuja.

Aidha ameongeza kuwa ni vyema serikali na wadau wote wa afya kujitokeza kuipa elimu ya kutosha jamii ili kuweza kutambua jinsi ugonjwa wa kifafa unavyopatikana na tiba yake.

Profesa Matuja amesema kwa sasa kuna aina mpya ya kifafa ambayo ni Kifafa cha Kichwa kuanguka kifuani (Nodding Syndrome) ambao ulionekana kwa mara ya kwanza 1960 katika wilaya ya Mahenge na kwa nchi nyingine Kifafa hichi kimeonekana miaka ya 1980 Liberia, Cameroon, Sudan Kusini na Uganda Magharibi miaka ya 2000.

Amesema njia kuu za kujikinga na kifafa Tanzania ni:-
1. Kujikinga na visababishi vinavyozuilika kama kumjali mama mjamzito kipindi cha ujauzito kwa kumshauri kuhudhuria kliniki pamoja na kumpatia vipimo mara  kwa mara, ugunduzi na matibabu ya haraka kwa watoto wanaopata homa, matumizi ya choo, kunawa mikono na kula nyama ya nguruwe iliyoiva vizuri.

2. Kuwepo na muendelezo wa kutoa elimu vjijini ili kutonyanyapaa na kuwabagua kwa makundi kutokana na matatizo yao; mfano mashuleni kwa ngazi zote ikiwemo walimu.

3. Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa afya juu ya chanzo, jinsi ya kujikinga na matibabu sahihi kwa watu wenye kifafa.

4. Kutoa elimu maalum inayohitajika kwa watoto wenye kifafa na uwezo wa kusoma.
5. Serikali ihakikishe kuwepo na utoaji wdawa za kutosha.

SIKIA KAULI KUHUSU WASAFI FESTIVAL MWANZA KUTOKA KWA MKURUGENZI WA JEMBE MEDIA LTD



GSENGOtV

Tarehe 15 Mwezi Disemba 2018 Wasafi Festival inafanyika Mwanza, hii itakuwa mara baada ya kuzunguka mikoa takribani mitano.

Jana ijumaa katika kipindi cha Hit Zone kinachoruka kupitia Jembe Fm, Mkurugenzi wa kituo hicho Dr. Sebastian Ndege ametoa kauli ambayo imewastua wengi. 

Ukurasa wa Twitter wake Diamond Platnumz unamaneno haya kwenye picha hapo juu.

ZEE LATIA MIMBA MWANAFUNZI 'LAKIONA CHA MTEMA KUNI'



GSENGOtV

Katika siku ya 4 mara baada ya mafunzo kwa vitendo  ya jinsi ya kumkwamua mtoto wa kike toka kwenye wingu la ukatili na mbinu ya jinsi ya kuvidhibiti, viongozi wa kada mbalimbali washiriki wanatinga katika mtaa wa KanyaMwanza kata ya Mwabaluhi wilayani Sengerema, na kulianzisha tena.

IGIZO
Zee la miaka yake latongoza binti wa shule hata kumpatia mimba, laswekwa gerezani na adhabu kali, nini jamii inasema kuhusu mikasa kama hiyo?

 Fuatilia kuona nini sababu.

Mpango wa kuielimisha jamii kwa kutumia maigizo kupitia watu maarufu na wanaotambulika katika nyadhifa mbalimbali kwenye jamii na ngazi mbalimbali serikalini, umekuja kama mbinu mpya kukabiliana na yale yanayochangia vitendo vya ukatili dhidi ya watoto hususani mtoto wa kike.

Badala ya kutumia vikundi vya sanaa, Wakuu wa wilaya, Wakurugenzi, Mabwana na Mabibi afya, Wachungaji, Mashekhe, Viongozi jumuiya ya wazazi, Makatibu Tawala, Wenyeviti na Makatibu Watendaji wa vijiji na vitongoji ndiyo wamekuwa wasanii.

Ni katika mradi wa mwaka mzima uliochini ya FAWE Tanzania, ukiratibiwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Korea (KOICA)

WAFUNGWA 113 WATOROKA GEREZANI.




Wafungwa 113 wametoroka gerezani katika jimbo la Aceh nchini Indonesia.

Kwa mujiu wa taarifa zilizotolewa na gazeti la Kompas,Katika  gereza lililopo  Banda Aceh lililokuwa na wafungwa 726 kulitokea vurugu jana jioni na hatima yake wafungwa 113 walitoroka.

Baada ya tukio hilo wafungwa 20 miongoni mwa waliotoroka walikamatwa maeneo mbalimbali na kurudishwa gerezani. Msako bado unaendelea kutafuta waliosalia.

Mpaka sasa iliyopelekea vurugu hizo hazijajulikana, uchunnguzi kuhusiana na tukio hilo umeanza kufanywa.

Friday, November 30, 2018

MRADI WA MAJITAKA MWANZA WAIBUKA KINARA

 Moja ya eneo lililonufaika na mfumo wa majitaka ujulikanao kama ‘Simplified Sewerage’. Pichani ni Mtaa wa Unguja, Kata ya Mabatini Jijini Mwanza ambao ni miongoni mwa maeneo yaliyonufaika na mradi wa majitaka wa simplified sewerage kupitia ufadhili wa African Infrastructure Trust Fund (EU-AITF).
 Moja ya eneo lililonufaika na mfumo wa majitaka ujulikanao kama ‘Simplified Sewerage’. Pichani ni Mtaa wa Unguja, Kata ya Mabatini Jijini Mwanza ambao ni miongoni mwa maeneo yaliyonufaika na mradi wa majitaka wa simplified sewerage kupitia ufadhili wa African Infrastructure Trust Fund (EU-AITF).
  Moja ya eneo lililonufaika na mfumo wa majitaka ujulikanao kama ‘Simplified Sewerage’. Pichani ni Mtaa wa Unguja, Kata ya Mabatini Jijini Mwanza ambao ni miongoni mwa maeneo yaliyonufaika na mradi wa majitaka wa simplified sewerage kupitia ufadhili wa African Infrastructure Trust Fund (EU-AITF).
  Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa (Mb) akikagua ubunifu uliotumika katika ujenzi wa mradi wa majitaka, Mabatini mtaa wa Unguja wilaya ya Nyamagana. Mradi huo umejengwa kwenye maeneo ya miinuko na umesaidia kuondosha uchavuzi wa mazingira na magonjwa ikiwamo Kipindupindu.
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Anthony Sanga (mbele) akiwaongoza wajumbe wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Maji Mjini Moshi (MUWSA) eneo la Mabatini Jijini Mwanza walipotembelea kujifunza mfumo wa majitaka Oktoba, 2018. Ni mradi wa kipekee kuwahi kutekelezwa nchini.

Mradi wa Majitaka unaotekelezwa kwenye maeneo ya miinuko Jijini Mwanza unaofahamika kama "Simplified Sewerage" umekuwa miongoni mwa miradi miwili bora zaidi kuwahi kutekelezwa Barani Afrika chini ya ufadhili wa African Infrastructure Trust Fund (EU-AITF).
Hayo yameelezwa mwishoni mwa Mwezi Novemba, 2018 wakati wa Mkutano wa kujadili miradi inayofadhiliwa na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) kupitia mfuko huo wa EU-AITF.
Katika mkutano huo ilielezwa kwamba tangu mfuko huo uanzishwe mnamo mwaka 2007 ni miradi miwili pekee ambayo imefuzu na kuwa miradi bora zaidi kuwahi kutekelezwa ambayo ni Mradi wa Majitaka wa Simplified Sewerage wa Jijini Mwanza, nchini Tanzania na mwingine ni mradi wa Nishati ya Umeme wa Benin & Togo.
Akizungumzia mradi wa Majitaka wa Jijini Mwanza, Mshauri wa masuala ya Kiufundi wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya, Raoul Pedrazzani alielezea hali ilivyokuwa hapo awali kabla ya kujengwa kwa mradi mpya wa majitaka kwenye maeneo ya milimani jijini humo.
Pedrazzani alisema kuwa kijiografia maeneo mengi ya Jiji la Mwanza ni milima/miinuko na kabla ya mradi huo wa majitaka wakaazi wa maeneo ya milimani hawakuwa na mfumo mzuri wa uondoaji wa majitaka hali ambayo iliwasababishia adha mbalimbali ikiwemo uchafuzi wa mazingira na maradhi.
Alisema suluhisho ilikuwa ni kubuni mradi ambao utarahisisha utoaji wa majitaka kutoka kwenye makazi hayo kwenda yanakostahili.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Anthony Sanga alithibitisha kupokea ujumbe wa pongezi juu ya ushindi huo.
Mhandisi Sanga aliipongeza Bodi ya Wakurugenzi ya MWAUWASA kwa usimamizi mahiri wa shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka na pia aliwapongeza watumishi wote wa MWAUWASA kwa utekelezaji na usimamizi mzuri wa miradi husika. “Mungu ni Mwema, tunamuomba Aendelee kutusaidia. Hakika kwa pamoja tunaweza,” alisema Mhandisi Sanga.
Aliongeza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha huduma ya majitaka inapanuka zaidi ili wananchi walio wengi waweze kufikiwa.
Maeneo ya miinuko ambayo tayari yamefikiwa na mfumo huo wa Simplified Sewerage ni Kilimahewa, Mabatini na Igogo na huku lengo likiwa ni kupanua wigo na kufikia maeneo mengi zaidi.

RAIS WA ZANZIBAR AZUNGUMZA NA UJUMBE WA WASHIRIKA WA MAENDELEO SEKTA YA KILIMO TANZANIA.

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Meneja Mkaazi wa Growing Africa’s Agriculture (AGRA) wakati wa mazungumzo na Ujumbe wa Washirika wa Sekta ya Kilimo Tanzania, ukiongozwa na Mwakilishi wa FAO Tanzania na Mwenyekiti wa Washirika wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania  Mr. Fred  Kafeero, ulipofika Ikulu leo 30/11/2018 kwa mazungumzo.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwakilishi  wa FAO Nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Washirika wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania Mr. Fred Kafeero, alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo na kungozana na Ujumbe wake .(Picha na Ikulu) 30/11/2018.
 Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Ujumbe wa Washiriki wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania kushoto Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania pia ni Mwenyekiti wa Washiriki wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania Mr, Fred Kafeero akiwa na Mwakilishi wa UNIDO Tanzania,Mauritius na EAC.Mr. Stephen Bainous Kargbo, 30/11/2018.(Picha na IKulu)
 Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Ujumbe wa Washiriki wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania kushoto Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania pia ni Mwenyekiti wa Washiriki wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania Mr, Fred Kafeero akiwa na Mwakilishi wa UNIDO Tanzania,Mauritius na EAC.Mr. Stephen Bainous Kargbo, 30/11/2018.(Picha na IKulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania Mr.Fed Kafeero, alipofika Ikulu Zanzibar na Ujumbe wake wa Washirika wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Tanzania, kwa mazungumzo leo 30/11/2018.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiongozana na mgeni wake Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania pia ni Mwenyekiti wa Washirika wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania Mr. Fed Kafeero, wakitoka katika ukumbi wa mkutano  baada ya kumaliza mazungumzo yao  yaliofanyika Ikulu Zanzibar leo 30/11/2018.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania Mr. Fred Kafeero kushoto na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Ujumbe wa Washirika wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Tanzania, baada ya mazungumzo yao yaliofanyika Ikulu Zanzibar.30/11/2018,(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiagana na mgeni wake Mwakilishi wa FAO Nchini Tanzania Mr. Fred Kafeero, alipofika Ikulu Zanzibar na Ujumbe wake wa Washirika wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Tanzania, kwa mazungumzo na Rais wa Zanzibar. (Picha na Ikulu)