ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 1, 2018

JAMII YAASWA KUACHA FIKIRA POTOFU JUU YA UGONJWA WA KIFAFA

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwasilisha utafiti wake juu ya Ugojwa wa Kifafa katika muhadhara  wa Kiprofesa uliofanyika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS). Profesa Matuja alifanya utafiti wa Ugonjwa wa Kifafa kwa muda wa miaka minne katika Wilaya ya Mahenge, Morogoro. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mwenyekiti wa Muhadhara huo, Prof. Gadi Kilonzo akifungua majadiliano ya kuulizana maswali juu somo la ugonjwa wa kifafa alilolitoa Profesa William Matuja (kushoto).
Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwasilisha utafiti wake juu ya Ugojwa wa Kifafa katika muhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS). Profesa Matuja alifanya utafiti wa Ugonjwa wa Kifafa kwa miaka minne katika Wilaya ya Mahenge, Morogoro.
Wageni waalikwa wakifuatilia muhadhara huo.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kushoto) akikabidhiwa zawadi ya cheti shukrani na Mhadhiri mwandamizi idara. Dkt. Tumaini Nagu mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa. Katikati ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani Dkt. Patricia Munseri.
  Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kulia) akikabidhiwa zawadi na Mhadhiri mwandamizi idara ya Magonjwa ya Ndani Dkt. Tumaini Nagu mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa.
 Dkt Pilly Chillo akikabidhi zawadi ya ua.
  Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja (kulia) akikabidhiwa zawadi na Kaimu Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani Dr. Patricia Munseri  mara baada ya kumaliza kuwasilisha utafiti wake juu ya ugonjwa wa kifafa.
 Afisa Uhusiano wa MUHAS, Hellen Mtui akitoa shukrani kwa wageni waliofika katika muhadhara huo.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na wanafamilia.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja akiwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na wafanyakazi wa kitengo chake.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Imani potofu ndiyo inayopelekea kuongezeka wa Ugonjwa wa Kifafa katika maeneo mbali mbali ya nchi ya Tanzania hasa Wilaya ya Mahenge, Morogoro.

Hayo ameyasema Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Ndani wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja wakati akiwasilisha ufatifi wake katika muhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ili kuweza kutoa mapendekezo yake njia za kuweza kusaidia jamii.

Profesa Matuja amesema Jamii inahitaji kuondokana na imani potofu maana watu wengi wamekuwa wakijua kuwa ugonjwa unasambabishwa na ushirikina.

Ameongeza kuwa jamii ni bora kujitokeza kupima mara kwa mara ili kuweza kupatiwa tiba mahususi ili kuweza kuondokana na tatizo hilo.

"Nimefanya utafiti katika wilaya ya Mahenge, Morogoro ila tulichogundua mwanzo ni jamii haikuwa na ueleza zaidi kuhusiana na ugonjwa wa kifafa na hivyo kupelekea watu wengi sana kuugua ugonjwa huo, lakini wengi wao wanafikiria imani potofu hasa haya mambo ya ushirikina," ameongeza Prof Matuja.

Aidha ameongeza kuwa ni vyema serikali na wadau wote wa afya kujitokeza kuipa elimu ya kutosha jamii ili kuweza kutambua jinsi ugonjwa wa kifafa unavyopatikana na tiba yake.

Profesa Matuja amesema kwa sasa kuna aina mpya ya kifafa ambayo ni Kifafa cha Kichwa kuanguka kifuani (Nodding Syndrome) ambao ulionekana kwa mara ya kwanza 1960 katika wilaya ya Mahenge na kwa nchi nyingine Kifafa hichi kimeonekana miaka ya 1980 Liberia, Cameroon, Sudan Kusini na Uganda Magharibi miaka ya 2000.

Amesema njia kuu za kujikinga na kifafa Tanzania ni:-
1. Kujikinga na visababishi vinavyozuilika kama kumjali mama mjamzito kipindi cha ujauzito kwa kumshauri kuhudhuria kliniki pamoja na kumpatia vipimo mara  kwa mara, ugunduzi na matibabu ya haraka kwa watoto wanaopata homa, matumizi ya choo, kunawa mikono na kula nyama ya nguruwe iliyoiva vizuri.

2. Kuwepo na muendelezo wa kutoa elimu vjijini ili kutonyanyapaa na kuwabagua kwa makundi kutokana na matatizo yao; mfano mashuleni kwa ngazi zote ikiwemo walimu.

3. Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa afya juu ya chanzo, jinsi ya kujikinga na matibabu sahihi kwa watu wenye kifafa.

4. Kutoa elimu maalum inayohitajika kwa watoto wenye kifafa na uwezo wa kusoma.
5. Serikali ihakikishe kuwepo na utoaji wdawa za kutosha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.